Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

RIWAYA : SALA YA SARAH.

.
MTUNZI : ALEX KILEO.


SEHEMU YA SITA.

ILIPOISHIA.

Siku iliyofuata ambayo ilikuwa ni jumapili, Mark alienda kanisani huku akiambatana na Sarah, uzuri ni kuwa siku hiyo hata Taita na wenzake walikuwa wamehudhuria kanisani hapo.
Wakati misa ikiwa mwishoni, ni kawaida kwa kanisa hilo itoe nafasi kwa mzee mmoja, kijana mmoja na mtoto mmoja kwa ajili ya kwenda mbele na kusali kwa niaba ya wenzake.
Alianza Mzee akaomba, akafuata kijana na nafasi ya mwisho ilimuangukia Sarah, Sarah alienda mbele ya kanisa na kuwekewa kipaza sauti mdomoni, kisha akawaomba waumini wafumbe macho, kisha kwa hisia na sauti ya kawaida kabisa, Sarah alisema,
"Mungu naomba niwe mkubwa, na niwe nawaka kama moto" Sarah alipomaliza kusema hivyo alirudisha kipaza sauti na kuacha waumini wakishangaa na wengine walicheka kabisa, ila Taita peke yake aliyekaa kiti cha mbele ndiyo alionekana ameguswa na hiyo sala ya Sarah..........

***********ENDELEA************

Taita aliinuka katika kiti hata kabla misa haijsisha na kuelekea nje, alipofika aliingia katika gari lake na kuchukua simu na kumpigia Trigger,

" uko upande gani?" Taita aliuliza baada ya simu kupokelewa,

"Niko nje ya uzio wa kanisa" Trigger alijibu,

"Njoo kwenye gari yangu" Taita aliongea kisha akakata simu.

Baada ya dakika Trigger alikuwa ndani ya gari ya Taita,

"Aisee yule Mzee wa kizungu yupo kanisani na Sarah, sasa itabidi umfuatiliea na ujue anapokaa" Taita aliongea,

"Yupo na Sarah kivipi wakati ulisema jana mlikubaliana Sarah abaki kwa babu yake?" Trigger aliuliza,

"Hilo limenishangaza, wewe fanya nilichokuagiza na mimi nitalifuatilia hilo" Taita aliongea na wakati huo na waumini wengine walianza kutoka ibadani ikiwa na maana misa imekwisha.

Taita aliweza kumshuhudia Mark akitoka ndani ya kabisa huku akiwa amemshika mkono Sarah na kuelekea kwenye gari la kifahari lilikuwa limeegeshwa eneo husika na kisha lile gari likatoka taratibu huku Taita akiliangalia,

"Imekuaje yule Mzungu yupo na Sarah?" Harry aliuliza huku akiingia ndani ya gari,

"Wamenigeuka wale wazee wapuuzi sana, ebu twende uko" Taita aliongea kisha akawasha gari na safari ilipangwa iishie kwa baba isack.

Iliwachukua takribani dakika kumi kufika nyumbani kwa Baba Isack, na bahati nzuri waliweza kuikuta na gari ya Mark ikiwa imeegeshwa nje ya ile nyumba.

"Nisubiri, nakuja" Taita aliongea na kutelemka katika gari kisha akaelekea ndani huku akionekana mwenye hasira.

Aliingia moja kwa moja sebuleni na kuwakuta baadhi ya ndugu wa marehemu Isack wakiwa wamekaa, Taita akawasalimia na kisha akakaa kwenye kochi,

"Sasa Mzee wangu imekuwaje huyu Mzungu amchukue Sarah? jana tulikubaliana nini au mmenigeuka?" Taita aliuliza maswali mfululizo huku akimtazama Baba Isack,

"Mwanangu bora umuache mtoto aende kusoma uko, kwa maana huyu bwana Mark amekuja na mikataba aliyoingia na baba Sarah kuhusu huyo mtoto na pia gharama alizotumia ni kubwa katika kushughulikia hiyo safari na shule atakayoenda kusoma uko" Baba Isack aliongea kwa upole,

"Kwa hiyo mmeuza mtoto?" Taita aliuliza,

"Hapana hajauzwa, ila baada ya masomo atarudi na utakaa nae kama unavyotaka" Mark alijibu,

"Kwani gharama ulizotumia ni shilingi ngapi?" Taita aliuliza huku akimuangalia Mark,

"Milioni mia hamsini tu" Mark alijibu,

"Nitazilipa" Taita alijibu,

"Sioni sababu ya kuingia hasara kuzilipa, muache akasome tu" Baba Isack alijibu,

"Kwa hiyo mpo upande wa huyu Mzungu?" Taita alihoji,

"Tupo upande wa mtoto, tunataka awe na maisha mazuri" Baba Isack alijibu,

"K wangu hatokuwa na maisha mazuri?" Taita aliuliza,

"Sijamaanisha hivyo, ila mimi kama babu nimependekeza mtoto akasome uko uingereza" Baba Isack aliongea na kufanya Taita ainuke na kuondoka kwa hasira na kuwaacha watu wakimshangaa.

Taita alitoka mpaka katika gari yake na kumkuta Trigger akiwa na Harry,

"Mtoto anatakiwa aende uingereza, tena safari ni kesho" Taita aliongea baada ya kuingia katika gari,

"Na wewe umekubali?" Harry aliuliza,

"Nimepinga ila watu wote ndani wanataka mtoto aende akasome uko" Taita alijibu kinyonge,

"Huyu Mzee wa kizungu anatakiwa afe leo, yeye na Sarah" Harry aliongea,

"Wanakufaje sasa?" Taita aliuliza,

"Trigger hakikisha unamfuatilia huyu Mzungu kila hatua leo mpaka upajue kwake na kisha usiku utaenda kummaliza, ni lazima atakuwa na Sarah tu" Harry aliongea,

"Hilo jambo ni zuri, ebu Trigger fanya hivyo" Taita aliongea,

"Sawa bosi" Trigger alijibu,

"Sasa sisi acha tuondoke, wewe endelea kumfuatilia huyu mzungu" Taita aliongea kisha akawasha gari na kuondoka.

Trigger aliendelea kuwepo maeneo yale, alisubiri kwa muda saa nzima na ndipo alipoweza kumuona Mark akitoka ndani huku akiwa na Sarah, walipotoka walielekea moja kwa moja katika gari na kuingia kisha wakaondoka.

Trigger akasubiri sekunde kadhaa kisha nae akaingia katika gari yake na kuanza kushika uelekeo ule ule ilipoelekea gari ya Mark.

Kwa mbali aliweza kuiona gari ya Mark. Trigger akapunguza mwendo na kuanza kuifuatilia kwa mbali ile gari ya Mark. Walitembea hivyo kwa dakika nyingi mpaka ile gari ya mark ilipoenda kuingia katika nyumba moja ndogo ila ya kisasa.

Trigger akasimamisha gari kwa mbali na kuanza kuangalia lile geti la nyumba ile na pia alikuwa anajaribu kuona kama atajua idadi ya watu wa mule ndani, kwa maana mpaka hapo alikuwa ameshajua idadi ya watu watatu ambao ni Mark, Sarah na mlinzi wa getini.

Trigger akiwa bado yupo pale akisoma mazingira, aliweza kuna gari jingine dogo la rangi nyeusi likiingia ndani ya ile nyumba, Trigger ikaendelea kusubiri, alipanga kujua kila kitu kwa muda huo ili usiku akija aje huku akiwa anajua pa kuanzia na pa kumalizia.

Baada ya masaa mawili Trigger aliweza kuna geti la ile nyumba likifunguliwa na akaiona ile gari ndogo nyeusi ikitoka na kusimama nje ya geti kisha Mark akatoka ndani ya geti na kuongea kidogo na yule dereva wa gari ambaye alikuwa ni kijana wa kizungu kisha wakaagana na ile gari ikaondoka na Mark akabaki peke yake kisha akarudi ndani na kurudishia geti.

Trigger ikaendelea kukaa pale mpaka giza lilipoanza kuingia na yeye akawa amepata kitu akitakacho, akawasha gari na kuondoka huku akijiaminisha kuwa ndani ya nyumba ile wapo watu watatu tu, ambao ni mlinzi, Mark na Sarah.

Trigger alirudi mpaka nyumbani kwa Taita na kuwakuta Taita na harry wamekaa katika bustani huku wakinywa kahawa,

"Umefanikisha?" Taita alimuuliza Trigger,

"Nimefanikisha kujua anapokaa na nimeweza kuangalia mazingira ya pale na nimeona panaingilika kirahisi tu" Trigger alijibu,

"Hakuna mlinzi hapo anapokaa?" Harry aliuliza,

"Yupo security guard mmoja tu pale getini, najua jinsi kumuingilia" Trigger alijibu,

"Inabidi hii mission ifanyike usiku wa leo" Taita aliongea,

"Tena naenda saa mbili tu" Trigger aliongea,

"Saa mbili mbona mapema?" Taita aliuliza,
.

"Ukienda usiku sana unaweza kufanya mlinzi aingie wasiwasi, inabidi niwahi ili niingie kama mgeni" Trigger alijibu,

"Utaenda peke yako au nikupe vijana wa kukuongezea nguvu?" Taita aliuliza,

"Mwenyewe tu, watu watatu hawawezi kunishinda" Trigger alijibu huku akitabasamu,

"Basi sawa, nenda kajiandae na hakikisha gari ni nzima na ina mafuta ya kutosha" Taita aliongea,

"Sawa" Trigger aliongea na kisha akaondoka zake na kuwaacha Taita na Harry wakimuangalia,

"Hili Jamaa ni jembe sana, mchezo ya kuua linaiweza sana" Harry aliongea wakati Trigger akiondoka,

"Sijui kama atafanikiwa leo, maana huyu mtoto kumuua imekuwa ngumu" Taita aliongea kivivu huku akijikuna kitambi chake.

********************

Mishale ya saa mbili usiku ilimkuta Trigger akiwa anajongea kwenye nyumba ya mark, alipofika aligonga geti na mlinzi akafungua,

"Habari yako bwana" Trigger alitoa salamu,

"Safi, nikusaidie nini?" Mlinzi aliuliza huku akimuangalia Trigger,

"Nataka nionane na boss" Trigger aliongea kwa upole,

"Una mihadi nae?" Mlinzi aliuliza,

"Ndio" Trigger alijibu huku akitabasamu,

"Ngoja nikamuulize. Unaitwa nani kwanza?" Mlinzi aliuliza,

"Mr Danny" Trigger alijibu na mlinzi akawa anaelekea ndani, ila kosa alilofanya mlinzi ni kuacha mlango wa geti ukiwa wazi,

Baada ya sekunde chache mlinzi alirudi getini na kukuta hamna mtu, akatoka nje ya geti ili kuangalia, na ndipo hapo hapo Trigger akatoka haraka kwenye kibanda cha mlinzi na kuingia sebeleni kwa Mark, akamkuta Mark akitazama runinga, Trigger akafunga mlango kwa ndani na kuchomoa bastola na kumuelekezea Mark, na muda huo huo vikasikika vishindo vya mtu akija katika mlango wa mbele,

"Boss" Sauti ya mlinzi ilisikika ikiita na Trigger akampa ishara Mark akimtaka aitike,

"Sema" Mark aliitika,

"Mtu mwenye ameondoka" Sauti ya mlinzi iliongea,

"Sawa, kuwa makini getini hapo, usiruhusu mtu kuingia" Mark alijibu,

'Sawa boss" Mlinzi alijibu na vikasikika vishindo vyake akielekea getini.

"Boss nimekuja kwa jambo moja tu, namtaka Sarah" Trigger aliongea huku akiwa amemkazia macho Mark,

"Mmewaua wazazi wake na bado mnaitaka roho yake" Mark aliongea huku akimtazama Trigger,

"Sijaja kujadiliana hapa" Trigger aliongea kwa jeuri,

"Mimi najua kila kitu, Sarah ameniambia yote" Mark aliongea kwa lengo la kumuogopesha Trigger,

"Unajua kila kitu eee? Kama nini unachokijua?" Trigger aliuliza huku akitabasamu,

"Wewe ni kibaraka tu wa Taita, nyie ndiyo mlimchoma Isack na familia yake ndani na mkamuiba mtoto wake mdogo wa kiume, Sarah anajua vyote na msidhani ni mdogo kiasi kwamba ashindwe kuwajua" Mark aliongea huku akimtupia jicho Trigger,

"Kweli unajua kila kitu, nimeridhika" Trigger aliongea na kutabasamu,

"Hakuna cha kuficha, najua kila kitu, siri zenu zote" Mark aliongea,

"Sawa unajua kila kitu, ila hujui kitu kimoja tu" Trigger aliongea na kuacha kutabasamu,

"Nini nisichokijua?" Mark aliuliza,

"Hujui kifo" Trigger aliongea na kukaza macho,

"Unamaanisha nini?" Mark alihoji huku hofu ikimshika, lakini Trigger wala hakuongea kitu, akairuhusu risasi utoke katika bastola yake na kwenda kumpiga Mark katika kichwa, Mark akafa pale pale,

"Hiyo ndiyo maana yangu" Trigger alijibu na wakati huo huo huko nje vilisikika vishindo vya mlinzi akija mbio baada ya kusikia mlio wa bunduki, kwa mawazo ya Trigger alijua mlinzi hawezi kuingia ndani kwa kuwa mlango umefungwa.

Trigger akaiweka bastola kiunoni na alikuwa anataka sasa kuanza kupekua ile nyumba amtafute Sarah, lakini ghafla alishtuka mlango umefunguliwa na mlinzi alikuwa amesimama mbele ya Trigger huku akiwa amemuelekezea bunduki,

"Weka Mikono juu muuaji wewe" Mlinzi alimwambiaTrigger huku akimuangalia boss wake Mark aliyekuwa amekaa juu ya kochi huku mwili ukiwa bila roho........

**********ITAENDELEA***********


the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

.
MTUNZI : ALEX KILEO.


SEHEMU YA SABA

ILIPOISHIA.

Trigger akaiweka bastola kiunoni na alikuwa anataka sasa kuanza kupekua ile nyumba amtafute Sarah, lakini ghafla alishtuka mlango umefunguliwa na mlinzi alikuwa amesimama mbele ya Trigger huku akiwa amemuelekezea bunduki,

"Weka Mikono juu muuaji wewe" Mlinzi alimwambiaTrigger huku akimuangalia boss wake Mark aliyekuwa amekaa juu ya kochi huku mwili ukiwa bila roho........

********ENDELEA********

."Mpuuzi wewe, nyie ndio majambazi mnaotafutwa na serikali, tupa silaha chini na uweke mikono juu" Mlinzi aliongea huku kamnyooshea Trigger bunduki, Trigger akatupa bastola pembeni na kuweka mikono juu huku akitabasamu,

"Hiyo bunduki yako ni nzito sana, ina kilo sita na hujaibeba vizuri" Trigger alimwambia mlinzi huku akitabasamu,

"Muuaji wewe, yaani unatabasamu huku umeua?" Mlinzi aliongea kwa hasira,

"Bosi wako hajafa huyo, hii bastola yangu haiui, inaleta tu usingizi" Trigger aliongea huku akitabasamu na kufanya mlinzi asogee jirani na mark ambaye alikuwa hatua mbili tu toka alipokuwa amesimama Trigger, ilo lilikuwa kosa kubwa sana.

Mlinzi akamtingisha Mark ila Mark hakuonekana ana uhai tena,

"Umeua wewe" Mlinzi aliongea,

"Mgeuze kisogoni uone kama ana damu, maana ukimpiga risasi lazima utoboe mpaka kisogo" Trigger aliendelea kuongea na tabasamu halikumdondoka. Mlinzi akamgeuza na kumuangalia Mark kisogoni, Trigger akatumia mwanya huo wa na kuipiga teke ile bunduki ya mlinzi na ikadondoka, kisha hakapiga hatua moja na kurusha teke Kali lililompata shingoni yule mlinzi na kuanguka chini, na kwa haraka sana Trigger akaokota bastola yake,

"Zamu yangu sasa kukuuliza, mtoto Sarah yupo wapi?" Trigger aliuliza huku bastola ikimuelekea mlinzi,

"Sarah hayupo, alichukuliwa jioni na ndugu yake Mark" Mlinzi alijibu huku akitetemeka,

"Huyo ndugu yake Mark anakaa wapi?"Trigger alihoji,

"Sijui kwa kweli?" Mlinzi alijibu,

"Kwanini hujui wakati wewe ni mlinzi wa hapa?" Trigger aliuliza,

"Sijui kitu boss wangu" Mlinzi aliongea,

"Sawa, je humu ndani wanaishi watu wangapi?" Trigger aliuliza,

"Anaishi Mark peke yake" Mlinzi alijibu kwa hofu,

"Unaogopa nini sasa, au hii bastola niliyoishika?" Trigger aliuliza kisha akaitupa ile bastola mbele ya mlinzi, alafu akaokota bunduki ya mlinzi na kisha akawa anaelekea sehemu vilipo vyumba.

Mlinzi akaona hiyo ni nafasi yake, kwa kitendo cha haraka sana mlinzi aliiokota ile bastola na kumuelekezea Trigger ambaye alikuwa akielekea sehemu vyumba vilipo,

"Simama hapo ulipo na tupa silaha chini" Mlinzi aliongea kwa mamlaka na kufanya Trigger asimame, kisha akageuka taratibu,

"Mimi nilivyokushikia silaha sikukuua, nilikupa nafasi ya kuishi" Trigger aliongea huku akitabasamu,

"Acha kelele, nitakufumua miguu hiyo" Mlinzi aliongea kwa hasira,

"Sawa nifumue, ila ukishindwa nitakufumua mimi" Trigger aliongea kwa kujiamini na kumnyooshea bunduki mlinzi, Mlinzi akafyatua risasi ila hazikutoka, akajaribu tena na hali ikawa vile vile,

"Sikuwa mjinga kukutupia bastola, niliitoa risasi" Trigger aliongea huku akitabasamu na kisha akamuelekezea bunduki yule mlinzi, na hakuwa na cha kupoteza, akamfyatulia risasi zilipiga bega la mlinzi na kisha mlinzi akatupwa na kutua chini kama mzigo, akalala na kutulia kimya,

"Pumzika hapo, nikitoka ndio nitakuua" Trigger aliongea na yule mlinzi aliyekuwa amelala pale chini huku akiwa hana fahamu.

Trigger akaelekea upande wa vyumbani na kuanza kumtafuta Sarah kila chumba, lakini hakufanikiwa kumpata, akaanza kupekua pekua makaratasi ili apate chochote kitakachoweza kumpa uelekeo wa wapi Sarah alipo lakini alikosa.

Trigger akatoka vyumbani kwa hasira na kurudi sebuleni ambapo alimkuta Mlinzi akiwa bado amelala bila fahamu, Trigger akaikota bastola yake na kuipachika mahali husika, kisha akamuangalia yule mlinzi kwa sekunde kadhaa huku bunduki ikiwa mkononi, mwisho akaamua aitupe chini ile bunduki ya mlinzi na kisha akatoka zake nje huku akitembea kwa hatua za haraka haraka, alitembea kwa mwendo huo mpaka alipofika sehemu alipoegesha gari yake, akapanda na kuondoa gari lake kwa mwendo wa taratibu utasema hajatoka kuua vile.

Aliendesha gari mpaka nyumbani kwa Taita na kufunguliwa geti kisha akaingiza gari ndani,

"Bosi yupo?" Trigger alimuuliza mlinzi wa geti,

"Yupo ndani" Mlinzi alijibu na Taita akashika uelekeo wa kuingia ndani.

Alipofika sebuleni alimkuta Taita akiwa amekaa na yule mtoto mdogo wa kiume ambaye ni mdogo wake Sarah,

"Vipi umefanikisha?" Taita aliuliza hata kabla Trigger hajakaa,

"Mark amekufa" Trigger alijibu huku akikaa,

"Sarah je?" Taita aliuliza kwa umakini,

"Sarah sijamkuta, kwa maelezo ya mlinzi nimegundua kuwa Sarah aliondolewa eneo lile jioni, na haijulikani alipo" Trigger alijibu kinyonge,

"Huyu mtoto ana nini? kila siku tunamkosa tu, au atakuwa kwa babu yake?" Taita alihoji kwa hasira,

"Sijui kwa kweli" Trigger alijibu,

"Ila ulivyoondoka kwa Mark umeacha hali Salama, hakuna jirani aliyegundua kitu?" Taita aliuliza,

"Kupo Salama, kuna mlinzi tu nimemuacha amepoteza fahamu" Trigger alijibu,

"Hawezi kuleta shida kama Sarah?" Taita aliuliza,

"Hawezi, kwanza ni ngumu sana kuniona" Trigger alijibu,

"Sawa, basi wewe nenda kapumzike tu, masuala mengine tutaongea siku inayofuata" Taita aliongea,

"Sawa" Trigger alijibu na kuanza kuelekea nje, alitembea mpaka kwenye gari aliyokuja nayo na kufungua mlango kisha akaiwasha, baada ya hapo akaiondoa taratibu.

*******************

Mishale ya saa kumi na mbili asubuhi ilimkuta Sarah akiwa uwanja wa ndege huku akiwa ameambatana na msichana mmoja aliyekuwa anatabasamu kila wakati.

Baada ya kukaguliwa mizigo ya Sarah, Sarah aliingia ndani ya ndege na yule mwanamke alikwenda kukaa eneo la wageni pale kiwanja cha ndege, lengo lake likiwa ni kuhakikisha Sarah ameondoka na yeye ndio atoke pale uwanja wa ndege.

Baada ya nusu saa ndege ile kubwa iliyokuwa ina maandishi ubavuni yaliyosomeka "BRITISH AIRLINE" ilipaa na kuiacha ardhi ya Tanzania na ikawa angani, yule mwanamke aliyekuja na Sarah akatabasamu baada ya ile ndege kumpotea machoni mwake, kisha akaelekea nje alipoegesha gari lake na kuingia, akatoa simu yake na kutafuta namba anayoitaka na kubonyeza kitufe cha kupigia simu, baada ya sekunde kadhaa simu aliyoipiga ikapokelewa,

"Hey Mark habari?" Mwanamke aliongea kwa bashasha,

"Samahani huongei na Mark unaongea na polisi, Mark amepata matatizo" Sauti ya upande wa pili alijibu na kumfanya mwanamke ashtuke,

"Matatizo gani?, yeye yupo wapi?" Mwanamke aliuliza maswali mfululizo,

"Njoo polisi hapa, kituo cha kati utapata taharifa zote" Sauti alijibu na kisha yule mwanamke akakata simu na kuwasha gari kisha akaiondoa kwa kasi, alikuwa kama amechanganyikiwa mwanamke huyu wa kizungu.

Aliendesha gari mpaka nje ya kituo cha polisi na kushuka, kwa mwendo wa haraka akaenda mpaka pale kaunta na kusimama,

"Namuulizia Mark, Mzee wa kizungu" Mwanamke aliongea kwa pupa,

"Wewe ndio ulipiga simu yake muda mchache uliopita?" Polisi aliyekuwepo kaunta aliuliza,

"Ndio mimi" Mwanamke alijibu,

"Panda ngazi hapo, kaingie ofisi namba 13" Polisi alitoa maelekezo na yule mwanamke akafuata huku wasiwasi ukimuongezeka.

Alipofika kwenye mlango namba 13 akagonga na kukaribishwa, akaingia na kupewa ruhusa ya kukaa kwenye kiti, na mbele yake alikuwepo mwanaume wa makamo aliyekaa nyuma ya kibao kilichoandikwa "RPC" yaani Region Police Commissioner, kwa lugha yetu tunaita mkuu wa police,

"Karibu" Mkuu wa polisi aliongea huku akiwa anamuangalia,

"Namuulizia Mark" Mwanamke aliongea,

"Mark......Mark.....ndio nani?" Mkuu wa polisi aliuliza huku akionekana kutojua kitu,

"Mzee wa kizungu, nilipiga siku yake asubuhi nikaambiwa yupo hapa" Mwanamke aliongea kwa hasira baada ya kuhisi anazungushwa tu,

"Oooh, ni nani yako yule Mzee?" Mkuu wa polisi aliuliza baada ya kukumbuka,

"Ni binamu yangu" Mkuu wa polisi akachukua karatasi na kuanza kuandika,

"Unaitwa nani?" Mkuu wa polisi alimuhoji,

"Emilly David" Mwanamke alijibu,

"Sasa Emily kuna shida kubwa imetoka, Mark alivamiwa jana usiku na muda huu yupo hospitali" Mkuu wa polisi aliongea huku akijaribu kumficha kuhusu kifo cha Mark,

"Ameumizwa?" Emily aliuliza kwa hamaki,

"Nitakupa vijana wangu uongozane nao, ukamuangalie" Mkuu wa polisi aliongea,

"Sawa" Emily alijibu na kisha mkuu wa polisi akapiga simu na baada ya muda wakaingia askari watatu,

"Mpelekeni hospitali mkamuangalie yule Mzee wa kizungu aliyevamiwa jana" Mkuu wa polisi alitoa agizo na kisha Emily na wale askari wakatoka na kuelekea nje, wakapanda gari na safari ya hospital ikaanza.

Haikuwachukua muda wakawa wamefika hospitali na moja kwa moja wakaelekea monchwari, hapo ndipo Emily alichanganyikiwa kabisa.

**"*************

Asubuhi hii ndiyo ilikuwa siku ya kwenda kumfuta kumbukumbu mdogo wake Sarah, Taita na wenzake walikuwa nje ya jengo la hospital wakimsubiri Daktari waliyekubaliana nae kufanya huo mpango, wakiwa wamesimama pale walishuhudia gari la polisi likisimama jirani nao, na kisha wakatelemka askari wawili wakiwa na mtu mmoja aliyekuwa ameshika bega lake na likionekana limejaa damu, ndipo Trigger alipomuangalia yule mtu, akagundua ni yule mlinzi aliyemjeruhi siku iliyopita, na kwa bahati mbaya yule mlinzi akamtupia jicho Trigger, yule mlinzi akashtuka...............

**********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH.

.
MTUNZI : ALEX KILEO.


SEHEMU YA NANE.

ILIPOISHIA.

Asubuhi hii ndiyo ilikuwa siku ya kwenda kumfuta kumbukumbu mdogo wake Sarah, Taita na wenzake walikuwa nje ya jengo la hospital wakimsubiri Daktari waliyekubaliana nae kufanya huo mpango, wakiwa wamesimama pale walishuhudia gari la polisi likisimama jirani nao, na kisha wakatelemka askari wawili wakiwa na mtu mmoja aliyekuwa ameshika bega lake na likionekana limejaa damu, ndipo Trigger alipomuangalia yule mtu, akagundua ni yule mlinzi aliyemjeruhi siku iliyopita, na kwa bahati mbaya yule mlinzi akamtupia jicho Trigger, yule mlinzi akashtuka...............

**********ENDELEA***********

"Kaza mwendo, unashangaa nini wewe?" Askari mmoja aliongea huku akimsukuma yule mlinzi,

"Subirini basi niwaambie" Mlinzi aliongea huku akiwa bado anamtizama Trigger,

"Nenda wewe, utuambie nini sasa" Askari aliongea kisha akamsukuma tena yule mlinzi,

"Usinisukume sasa" Mlinzi aliongea kwa hamaki baada ya kuona anaonewa,

"Unabishana na serikali?" Askari aliuliza ila hakutaka kujibiwa na badala yake akampiga mtama yule mlinzi na kisha akamuinua kwa kumshika kibindoni na kumuingiza ndani ya jengo la hospitali.

Kipindi chote Trigger alikuwa makini kufuatilia lile tukio, ila hakuweza kusikia maneno waliyokuwa wakiongea kati ya wale askari na yule mlinzi, ila aliamini kuna kitu kisicho cha kawaida kilikuwa kitaendelea.

"Hapa hapafai, ngoja niwaache" Trigger aliongea kwa sauti ndogo sikioni kwa Taita,

"Kuna nini?" Taita aliuliza huku akiangaza angaza macho yake eneo lile,

"Tutaongea baadae" Trigger alijibu huku akianza kuondoka kwa kupiga hatua za haraka haraka kuelekea nje ya geti na kuwaacha Taita na harry wakimtazama tu mwenzao huyo.

***************

Mlinzi aliingizwa ndani ya hospitali juu juu na Askari huku akiwa anajitahidi kupambana na Askari wasimshike kidhalilishaji vile, ila kabla hawajaingia eneo husika, Askari waliwaona wenzao wakija eneo lile huku wakiwa wameongozana na mwanamke wa kizungu aliyekuwa anafuta machozi.

Wale Askari walipowafikia walisalimiana,

"Madam" Mlinzi aliita baada ya kunyanyua uso wake na kumuona Emily yule mwanamke wa kizungu,

"Sengu, ni nini kimetokea mpaka Mark akauawa?" Emilly aliuliza huku akionekana ana uchungu sana,

"Madame tulivamiwa jana usiku, na hapa unaponiona nimepigwa risasi ya bega" Mlinzi aliongea kwa huzuni,

"Wamechukua nini sasa baada ya kuvamia, au walikuwa wanaitaka roho ya Mark tu?" Emily aliuliza na kushindwa kujizuia kulia,

"Mvamizi alikuwa anamtaka Sarah, maana alimuulizia na alikuwa anataka kujua alipo muda ule" Mlinzi alijibu,

"Ulimtambua kwa sura huyo mvamizi? au alivaa kitu usoni?" Emily aliuliza huku akijifuta machozi,

"Ni sura ngeni, ila nimemuona hapo nje, nilipotaka kuwaambia hawa Askari badala ya kunisikiliza wananipiga" Mlinzi aliongea huku akimuangalia yule Askari aliyempiga mtama muda mchache uliopita na aligundua jinsi Askari huyo alivyotamalaki,

"Twende ukatuoneshe" Askari huyo aliongea huku akitangulia kupiga hatua na wenzake wakamfuata kwa nyuma huku wakionekana wana hamu ya kumuona huyo muuaji.

Walitoka mpaka nje na Mlinzi alielekea moja kwa moja mpaka pale aliposimama Trigger na wenzake, ila cha ajabu hawakumkuta Trigger,

"Tuambie yupo wapi hapa?" Askari aliuliza huku akimtazama mlinzi na kufanya Taita na Harry washtuke,

"Alikuwepo hapa, amesimama ni hawa" Mlinzi aliongea kwa kujiamini,

"Eti waheshimiwa huyo mtu ambaye inasemekana mlisimama nae ameenda wapi?" Askari aliuliza huku akiwatazama kwa zamu,

"Sijui, kwani huyo ni nani kwetu? mbona mnakuja kwa vitisho namna hiyo?" Taita aliuliza huku mikono ameiweka mfukoni,

"Kwa hiyo mlisimama na mtu ambaye hamumjui?" Askari aliuliza kwa hasira,

"Unauliza vitu gani wewe? unajua hapa wamesimama watu wangapi? na si kila aliesimama tunamjua, hii ni hospitali ya serikali kwa hiyo watu wengi wanakuja hapa na wanasimama popote wanapojisikia" Taita alijibu,

"Kwa hiyo huyo mtu hamumfahamu? hilo ndilo lilikuwa swali langu" Askari aliuliza,

"Hatumjui" Harry alijibu baada ya kumuona Taita amepaniki,

"Sawa tunashukuru waheshimiwa" Askari aliongea kisha akamkamata mkono mlinzi na kumpeleka ndani kupatiwa matibabu na kuwaacha Taita na Harry wakiwaangalia.

"Itakuwa ni Trigger tu, ndo maana alikimbia haraka" Harry aliongea huku akitabasamu,

"Itakuwa ni ile ishu ya kifo cha Mark, maana aliniambia kuwa hakumuua mlinzi" Taita aliongea,

"Trigger amekuwa mzembe siku hizi, au ndio amekuwa mzoefu?" Harry aliuliza,

"Kazi ya hatari inahitaji umakini, siku hizi anakurupuka tu, yaani anajiamini mpaka anataka kuharibu kazi" Taita aliongea huku akionekana kutoridhika na utendaji wa kazi wa Trigger na muda huo Daktari waliyemfuata alikuwa anafika eneo hilo,

"Nimewaweka sana ee, poleni" Daktari aliongea huku akitabasamu,

"Usijali, haya tuambie sasa" Taita aliongea,

"Mipango tayari, sasa twendeni ndani" Daktari aliongea huku akitangulia na nyuma alifuatwa na Harry na Taita ambaye alikuwa amembeba mtoto ambaye ni mdogo wake Sarah.

Waliingia mpaka katika chumba kidogo ambacho kilionekana ni cha siri ila kilijaa vifaa vyote vya vipimo na dawa tofauti,

"karibuni sana, hiki ni chumba maalum cha magendo" Daktari aliongea huku akitabasamu,

"Asante" Harry na Taita walijibu,

"Sasa hatua ya kwanza nitamchoma mtoto sindano ya usingizi, alafu nitamchoma na sindano nyingine mbili shingoni ambazo zitaharibu mfumo wa mawasiliano, alafu nitampeleka wodini, anaweza kukaa wiki nzima bila fahamu" Daktari aliongea na kumuangalia Taita,

"Akae hata mwezi, ila cha muhimu ni kumbukumbu zote zimpotee" Taita alijibu,

"Zitampotea tu, tena itakuwa rahisi maana ni mdogo sana, ana umri gani?" Daktari aliuliza,

"Miaka minne" Taita alijibu,.

"Sawa, nyie nendeni nje, ngoja nimshughulikie" Daktari aliongea huku akimchukua mtoto,

"Na malipo si tutakupa tukiwa nje?" Taita aliuliza,

"Nipeni hapa hapa, kiasi cha hawali, kilichobaki si tumekubaliana mtanipa baada ya kazi" Daktari aliongea,

"Sawa" Taita aliongea kisha akaingiza mkono ndani ya koti la suti na kutoka na kibunda cha pesa, akamkabidhi Daktari,

"Milioni tatu hizi?" Daktari aliuliza huku akitabasamu,

"Zihesabu" Taita aliongea,

"Nakuamini, hizo milioni mbili zilizobaki ndo kama tulivyokubaliana" Daktari aliongea,

"Wewe usijali kuhusu pesa, Fanya kazi tu" Harry aliongea baada ya ukimya wa muda Mrefu,

"Sawa waheshimiwa, kaningojeni nje" Daktari aliongea

"Itachukua muda gani hii hatua ya hawali?" Taita aliuliza,

"Mhmmm mhmmm nusu saa hizi, au chini ya hapo, haiwezi kuzidi dakika thelathini" Daktari alijibu huku akiitazama saa yake ya mkononi,

"Okey, kazi njema" Taita alijibu kisha wakaondoka na Harry na kumuacha Daktari akimlaza Mdogo wake Sarah katika kitanda kidogo kilichopo chumbani hapo.

********************

Mishale ya saa tatu na dakika zake usiku, ndio ndege aliyopanda Sarah ilikuwa inatua katika ardhi ya uingereza kwenye jiji la London, baada ya dakika kumi mlango wa ndege ulifunguliwa na Sarah akawa ni miongoni mwa watu wa mwanzo kutelemka, alikuwa chini ya uangalizi wa muhudumu wa kike wa ndege ambaye alikabidhiwa na Emily.

Sarah alipelekwa mpaka eneo wanalokaa watu wanaousubiri wageni wao, hapo ndipo walipomkuta kijana mmoja wa kizungu akiwa amebeba bango liliandikwa jina la Sarah, yule muhudumu akampeleka Sarah mpaka mwa kijana yule, kisha yule kijana akatoa shukrani kwa yule muhudumu na baada ya hapo yule kijana akimshika mkono Sarah na kutoka nae eneo la nje ya uwanja wa ndege, wakaelekea kwenye gari ambayo alikuja nayo yule kijana na wakaingia humo, safari ya makazi mapya ikaanza, ndani ya gari ukimya ulitawala,

"Mbona umepoa hivyo, au kwa kuwa Mark ameuawa?" Sarah aliuliza baada ya muda kidogo na kumfanya yule kijana ashtuke, kwa maana yule kijana aliambiwa mtoto huyo hajui chochote kuhusu kifo cha Mark na wala hasimpe taharifa hizo za kifo.

Sasa Sarah amejuaje?

*********ITAENDELEA**********

the Legend☆
 
Asante sana the _legend. Mwacha Sarah a some baadae alipize kisasi
 
Mkuu utapata shida sana kujua mi ni mtu wa aina gani. Watu wanaonizunguka wenyewe kuanzia mitaa nliyokaa, kote nlikowahi kupitia, mpaka sasa ofisini hamna anaejua the legend ni mtu wa aina gani exactly, sembuse huku mitandaoni

the Legend☆
Mkuu unaenda mbali...

Nitakujua kwa maandishi??
Tabu sipati maana nikujuwe ili iweje?
Inatosha sana mbona tunavyojuana humu..... ....
Afu usijidanganye eti hamna anaye kujua...kwani umetoka sayari ya mars?? au pluto??
Hii dunia ina pande mbili...
Huwezi amini kwa imani hiyo uliyonayo...
Haya tuendelee mkuu ..lakini mimi hapa nacheka sana... ... ...
Ndio hivyo yaani....
Ila mkuu hizi stori zinakolea mpaka basi...
zina vingi sana vya kuburudisha na kufunza..asante mkuu...

Usijali kabisa ...changamsha baraza tu hii... ... siko kama udhaniavyo...
Haya gazeti hiloooo...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu unaenda mbali...

Nitakujua kwa maandishi??
Tabu sipati maana nikujuwe ili iweje?
Inatosha sana mbona tunavyojuana humu..... ....
Afu usijidanganye eti hamna anaye kujua...kwani umetoka sayari ya mars?? au pluto??
Hii dunia ina pande mbili...
Huwezi amini kwa imani hiyo uliyonayo...
Haya tuendelee mkuu ..lakini mimi hapa nacheka sana... ... ...
Ndio hivyo yaani....
Ila mkuu hizi stori zinakolea mpaka basi...
zina vingi sana vya kuburudisha na kufunza..asante mkuu...

Usijali kabisa ...changamsha baraza tu hii... ... siko kama udhaniavyo...
Haya gazeti hiloooo...

Sent using Jamii Forums mobile app
soon ntazishusha episodes nyingine za sala ya Sarah, hicho ndo cha msingi, na ndo hasa lengo la huu uzi, kwa heshima ya wanaoifuatilia riwaya hii. Tuachane na hayo mengine mkuu

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom