the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,112
- Thread starter
- #41
RIWAYA : SALA YA SARAH.
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA NNE.
ILIPOISHIA.
Trigger akafuata maelekezo na kwenda moja kwa moja mpaka sehemu husika, alipofika alisukuma mlango na kumkuta Sarah akiwa amelala huku amefunikwa shuka zito mwilini.
Trigger akamsogelea kwa tahadhari na kumfikia, Sarah akafungua macho na kukutana na sura ya Trigger, uzuri ni kuwa alimkumbuka, Sarah akaanza kupiga kelele, Trigger akamuwahi na kumziba mdomo kwa mkono mmoja,
"Sssssssshiiii" Trigger aliongea huku akiwa ameweka kidole chake cha shaada kwenye midomo yake, alikuwa anatoa ishara ya kutaka Sarah ahache kelele, lakini Sarah aliendelea kukuruka pale kitandani, Trigger akajiona kama anapoteza muda, akachukua mikono yake na kuikamata shingo ya Sarah, Trigger akaongeza nguvu mikononi ili atimize lengo lake, alidhamiria kummaliza huyu malaika hasiye na hatia......
*********ENDELEA**********
"Mwachie mtoto na ugeuke taratibu bila usumbufu wowote" Sauti ilisikika na Trigger akaisikia vyema masikioni make, Trigger akamuachia Sarah na kugeuka huku akitabasamu na kukutanisha macho yake na mtu aliemuelekeza wodi muda mfupi uliopita, alikuwa ni yule mpelelezi na mkononi alikuwa na bastola, na muda huo huo mtoto Sarah alitoka kitandani na kukimbilia nyuma ya mpelelezi,
"Shida nini tena, mbona kuna amani tu" Trigger aliongea huku mikono ikiwa juu
"Unamjua huyu?" Mpelelezi alimuuliza Sarah,
"Ndio" Sarah alijibu,
"Kwanini asinijue wakati mimi ni baba yake mdogo?" Trigger aliuliza huku akitabasamu,
"Ni baba mdogo kweli?" Mpelelezi alimuuliza Sarah,
"Sio, huyu alikuja jana usiku nyumbani" Sarah alijibu na ubongo wa mpelelezi ukafanya kazi haraka, akahisi kabisa huyu huenda anahusika na tukio la moto,
"Nenda nje, mtafute dokta yoyote ukakae nae" Mpelelezi aliongea na kumfanya Sarah atoke mbio mbio ndani ya wodi,
"Unataka kufanya nini sasa?" Trigger aliuliza huku tabasamu likiwa bado limemkaa,
"Upo chini ya ulinzi, hutakiwi kufanya chochote, geuka nyuma na uweke mikono nyuma ya kichwa" Mpelelezi aliongea kwa amri,
"Chini ya ulinzi kivipi? Kwanza angalia kidole chako ulivyokiweka kwenye kifyatulio, hakiko sawa na nikiamua kukufanya lolote naweza" Trigger aliongea kwa dharau na kufanya mpelelezi atupie jicho kidole kilichokuwepo kwenye trigger, ilo ndilo lilikuwa kosa lake, Trigger alituka juu na kuipiga teke ile bastola, bastola ikaseleleka mpaka mlangoni, kisha kwa ufundi wa hali ya juu akaachia ngumi Kali iliyotua sawia kwenye mdomo wa mpelelezi, mpelelezi akaenda chini na kutema damu, Trigger akaona hiyo ndio nafasi ya kuiwahi bastola, wakati anaanza kukimbia, mpelelezi akamdaka mguu na kumvuta, Trigger akaenda chini na kisha akarusha teke lingine lililomkuta shingoni mpelelezi, mpelelezi akamuachia, Trigger haraka akasimama na kwenda kuichukua ile bastola na kumuelekezea mpelelezi,
"Nyanyuka" Trigger alimwambia, mpelelezi akatii huku mikono ikiwa juu,
"Unachofanya unadhani ni sahihi?" Mpelelezi alimuuliza Trigger huku mikono ikiwa juu,
"Usahihi wa mtu upo kulingana na akiwazacho" Trigger alijibu huku akitabasamu,
"Sawa, shusha silaha chini" Mpelelezi alimwambia Trigger,
"Daima Trigger akimnyooshea mtu silaha uwa haishushi silaha chini mpaka risasi itoke" Trigger aliongea na safari hii hakuwa na tabasamu tena,
"Unamaanisha nini?" Mpelelezi aliuliza lakini hakupewa jibu, Trigger alifyatua risasi ilienda moja kwa moja katika kichwa cha mpelelezi, mpelelezi akarushwa mpaka dirishani, dirisha likapasuka vioo na mpelelezi akatokea dirishani mpaka chini, aliporomoka umbali wa ghorofa saba.
"Maana yangu ni hiyo" Trigger aliongea kisha akaitupia chini ya kitanda ile bastola na kisha akatoka ndani huku akikimbia. Alijiunga na watu wengine waliokuwa wanakimbia baada ya kusikia mlio ule wa bastola, Trigger akajichanganya nao na kuanza kukimbia kama na yeye ni mmoja wao vile, njiani wakati akishuka ghorofani alipishana na askari kadhaa wenye silaha wakipandisha juu.
Trigger alikimbia mpaka chini na kwenda eneo lile lile alipoanguakia yule mpelelezi, watu walishalizunguka eneo lile, Trigger akajisogeza na kupangua watu wawili watatu na kufanikiwa kuweza kumuona mpelelezi yule, alikuwa sio mtu tena, ulikuwa ni mwili tu usio na nafsi, yaani tayari mpelelezi alikuwa ni marehemu, Trigger akatoa tabasamu dogo na kisha akaanza kupangua watu ili aweze kutoka, aliwapangua na kutoka kwenye lile kundi la watu, akaanza kuelekea nje ya geti, alitoka nje ya geti la hospitali na kusimamisha usafiri, akapanda na kupelekwa moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Taita.
Alimkuta Taita akiwa anajiandaa na safari ya kwenda msibani,
"Nadhani umemaliza kazi" Taita aliongea huku akifungua mlango wa gari lake,
"Misheni imefeli" Trigger aliongea kwa sauti tulivu na kufanya Taita ashtuke na asitishe mpango wa kufungua mlango wa gari,
"Kipi kilichokufanya ukashindwa?" Taita aliuliza kwa ukali,
"Wakati natekeleza mpango alitokea askari mwenye silaha, ndio alinikwamisha" Trigger alijibu,
"Oooh shit, alafu nini kikafuata mpaka umerudi Salama?" Taita aliendelea na maswali,
"Nilimdhibiti yule askari, nikamuua ndipo nikafanikiwa kukimbia" Trigger alijibu,
"Safi, je mtoto hukumuona tena?" Taita alihoji,
"Sijabahatika kumuona tena, nadhani alienda kujiweka sehemu Salama zaidi" Trigger alijibu,
"Sawa, mimi naelekea msibani, nadhani wewe unapaswa kurudi kule hospital ili ukaendelee kufuatilia nyendo za mtoto" Taita aliongea huku akiingia ndani ya gari,
"Sawa, Harry yupo wapi?" Trigger aliuliza,
"Nitamkuta mbele uko, kuna sehemu ameenda" Taita alijibu,
"Safari hii inabidi niende na gari ili niwe huru zaidi" Trigger aliongea na kufanya Taita ajisachi na kutoa ufunguo wa gari na kumkabidhi Trigger,
"Chukua ile harrier nyeusi, ipo hapo mtaa wa nyuma inaoshwa, kuna tatizo jingine?" Taita aliuliza,
"Hakuna, kama litatokea tutawasiliana" Trigger aliongea kisha Taita akawasha gari na kuliondoa taratibu na kupotea eneo hilo na kumuacha Trigger akimtazama.
Taita aliendesha gari mpaka mtaa unafuatia na kumkuta harry akimsubiri hapo, akampakia kwenye gari na kisha wakaanza safari ya kwenda msibani.
Ndani ya gari Taita alimueleza Harry kila kitu kuhusu Trigger kutofanikisha mpango wa kumuua Sarah na kisha akamueleza ni kitu gani amemuagiza akakifanye.
"Hili jambo la kummaliza linatakiwa liwe la haraka, maana yule mtoto ni mkubwa na anajua kila kitu kilichotokea kuhusu wazazi wake" Harry aliongea,
"Ila nitafanikisha tu, maana nikishamchukua na kuishi nae ndipo nitamuua kirahisi" Taita aliongea,
"Hiyo usiiwaze, anaweza kutuchoma hata kabla hujamchukua, wewe fikiria kama aliweza kumtambua Trigger anashindwa vipi kukutambua wewe?" Harry aliuliza,
"Madaktari wamesema kumbukumbu zake haziko sawa" Taita aliongea,
"Upuuzi mtupu, kama kumbukumbu zake hazipo sawa amemtambuaje Trigger, ni ujinga kuendelea kufikiria hivyo" Harry aliongea huku akionekana kutofurahishwa na mawazo ya boss wake,
"Ebu ngoja tukitoka uko msibani tutapanga vizuri" Taita aliongea kwa utulivu,
"Mmh sawa" Harry aliishia kuguna tu kisha ukimya ukatawala.
Gari lilitembea kwa mwendo mrefu na atimae lilifika eneo lenye msiba. Taita aliposhuka tu, wanawake ambao walikuwa wakifahamu uhusiano wake na magreth wakaanza kuangusha kilio upya, yaani utasema wamepokea habari hizo muda huu.
"Broo unatakiwa uingie ndani moja kwa moja" Kijana mmoja aliongea sikioni kwa Taita, inaelekea huyu kijana ni ndugu wa Isack ambaye ni baba yake Sarah.
Taita akaelekea moja kwa moja sehemu aliyotakiwa na kuingia ndani ambapo aliwakuta wazazi wa Isack na ndugu wengine, Taita akawasalimia na kuoneshwa sehemu ya kukaa,
"Mbona umechelewa mwanangu?" Baba Isack alimuuliza,
"Asubuhi niliamkia hospitali ili nikamuangalie Sarah hali yake ipoje" Taita akajitetea,
"Vizuri, anaendeleaje mjukuu wangu?"Baba Isack aliuliza,
"Mzima kabisa, kesho anaweza kuruhusiwa, nitamchukua na kuishi nae" Taita alijibu,
"Na yule mwingine mdogo yeye ndio ameteketea kabisa kawa majivu" Baba isack aliongea kwa uchungu,
"Dah, ni mipango ya Mungu" Taita alijibu,
"Sasa hapa sisi tumeshapanga maziko, tumeamua kupanga mapema baada ya kukusubiri muda mrefu na hukutokea, kwa hiyo hapa tunachongoja kutoka kwako ni kuridhia na kubariki mipango yetu" Baba Isack alizungumza na kumtupia jicho Taita,.
"Mmepanga yafanyike lini?" Taita aliuliza,
"Leo hii saa kumi" Baba Isack alijibu,
"Kwanini tusimsubiri mtoto aruhusiwe hospitali hili naye ashiriki maziko ya wazazi wake?" Taita aliuliza,
"Hata sisi tulitaka iwe hivyo, ila kwa jinsi ile miili ilivyoharibika, ni ngumu sana kuacha mpaka kesho" Baba Isack alijibu
"Sawa, mimi nimeridhia" Taita aliongea kwa upole,
"Nashukuru sana kijana wangu, nadhani cha muhimu ni kwenda tu monchwari kuisafisha miili ili mpaka saa saba iwe imefika hapa na mipango ya kuaga miili ianze" Baba Isack alizungumza na watu kadhaa wakamuunga mkono, kisha wakatoka baadhi ya ndugu wa marehemu wakiambatana na Taita na wakaelekea hospitali kwa ajili ya kuitayarisha miili ya marehemu.
*********************
Trigger alikuwa ameegesha gari lake ndani ya uzio wa hospitali huku akijaribu kuyasoma mazingira ya pale vizuri. Wakati akiwa bado anapiga hesabu zake ndipo alipomuona daktari akiwa ameongozana na Sarah na mwanaume wa makamo ambaye ni Mzungu. Trigger akayaweka macho yake umakini mkubwa, akaweza kuona daktari akitoa maelezo kwa yule Mzee wa kizungu, ila Trigger hakuweza kusikia neno lolote kwa kuwa alikuwa mbali kidogo.
Trigger aliendelea kushuhudia daktari akiongea na yule Mzee Mzungu na kisha akaona wakipeana mikono, alafu yule Mzee wa kizungu akaondoka huku akiwa ameongozana na Sarah na kuingia kwenye gari moja la kifahari, kisha ile gari ikaondoka kwa mwendo wa taratibu.
Baada ya lile gari kutoka nje ya geti, Trigger nae aliondoa gari lake na kuanza kuifuata ile gari huku akiwa anaangalia namna ya kupanga mashambulizi ya kummaliza Sarah.
Zile gari ziliendelea kufuatana huku zikiwa zimeachana umbali kidogo, walipofika eneo ambalo kulikuwa na pori kidogo, Trigger akaongeza mwendo na kuipita kabisa ile gari ya Mzee wa kizungu, tena akaiacha mbali kiasi kwamba hakuiona, alifanya hivyo makusudi baada ya kutengeneza mipango yake.
Trigger alienda na kusimamisha gari pembeni ya barabara, akashuka na kuanza kusubiri. Baada ya dakika tano ilitokea ile gari ya Mzee wa kizungu na Trigger akajifanya kama anatengeneza gari lake, yaani aliigiza gari lake limeharibika.
Gari la Mzee wa kizungu lilipomkaribia Trigger akalipiga mkono na likasimama pembeni ya barabara, Trigger akatazama kioo cha mbele kwa jicho la chini ili aone watu waliomo ndani ya gari, akamuona ni yule Mzee wa kizungu na Sarah tu, akajikuta anatabasamu na kuishusha kofia yake chini zaidi ili Sarah asimtambue.
Trigger akawa anasogea katika gari ya yule Mzee wa kizungu,
"Samahani Mzee gari yangu imeniharibikia, naomba msaada" Trigger aliongea huku akiwa amesimama katika dirisha la gari.
"Unataka msaada gani sasa?" Mzee wa kizungu aliuliza,
"Nataka maji, nahisi rejeta imeisha maji" Trigger aliongea huku mkono wake ukianza kuivuta bastola ndogo iliyopo kiunoni upande wa nyuma, Trigger mtu mbaya alidhamiria kuua, na kawaida yake ni kwamba akikunyooshea bastola uwa haishushi mpaka itoe risasi.......
*********ITAENDELEA**********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA NNE.
ILIPOISHIA.
Trigger akafuata maelekezo na kwenda moja kwa moja mpaka sehemu husika, alipofika alisukuma mlango na kumkuta Sarah akiwa amelala huku amefunikwa shuka zito mwilini.
Trigger akamsogelea kwa tahadhari na kumfikia, Sarah akafungua macho na kukutana na sura ya Trigger, uzuri ni kuwa alimkumbuka, Sarah akaanza kupiga kelele, Trigger akamuwahi na kumziba mdomo kwa mkono mmoja,
"Sssssssshiiii" Trigger aliongea huku akiwa ameweka kidole chake cha shaada kwenye midomo yake, alikuwa anatoa ishara ya kutaka Sarah ahache kelele, lakini Sarah aliendelea kukuruka pale kitandani, Trigger akajiona kama anapoteza muda, akachukua mikono yake na kuikamata shingo ya Sarah, Trigger akaongeza nguvu mikononi ili atimize lengo lake, alidhamiria kummaliza huyu malaika hasiye na hatia......
*********ENDELEA**********
"Mwachie mtoto na ugeuke taratibu bila usumbufu wowote" Sauti ilisikika na Trigger akaisikia vyema masikioni make, Trigger akamuachia Sarah na kugeuka huku akitabasamu na kukutanisha macho yake na mtu aliemuelekeza wodi muda mfupi uliopita, alikuwa ni yule mpelelezi na mkononi alikuwa na bastola, na muda huo huo mtoto Sarah alitoka kitandani na kukimbilia nyuma ya mpelelezi,
"Shida nini tena, mbona kuna amani tu" Trigger aliongea huku mikono ikiwa juu
"Unamjua huyu?" Mpelelezi alimuuliza Sarah,
"Ndio" Sarah alijibu,
"Kwanini asinijue wakati mimi ni baba yake mdogo?" Trigger aliuliza huku akitabasamu,
"Ni baba mdogo kweli?" Mpelelezi alimuuliza Sarah,
"Sio, huyu alikuja jana usiku nyumbani" Sarah alijibu na ubongo wa mpelelezi ukafanya kazi haraka, akahisi kabisa huyu huenda anahusika na tukio la moto,
"Nenda nje, mtafute dokta yoyote ukakae nae" Mpelelezi aliongea na kumfanya Sarah atoke mbio mbio ndani ya wodi,
"Unataka kufanya nini sasa?" Trigger aliuliza huku tabasamu likiwa bado limemkaa,
"Upo chini ya ulinzi, hutakiwi kufanya chochote, geuka nyuma na uweke mikono nyuma ya kichwa" Mpelelezi aliongea kwa amri,
"Chini ya ulinzi kivipi? Kwanza angalia kidole chako ulivyokiweka kwenye kifyatulio, hakiko sawa na nikiamua kukufanya lolote naweza" Trigger aliongea kwa dharau na kufanya mpelelezi atupie jicho kidole kilichokuwepo kwenye trigger, ilo ndilo lilikuwa kosa lake, Trigger alituka juu na kuipiga teke ile bastola, bastola ikaseleleka mpaka mlangoni, kisha kwa ufundi wa hali ya juu akaachia ngumi Kali iliyotua sawia kwenye mdomo wa mpelelezi, mpelelezi akaenda chini na kutema damu, Trigger akaona hiyo ndio nafasi ya kuiwahi bastola, wakati anaanza kukimbia, mpelelezi akamdaka mguu na kumvuta, Trigger akaenda chini na kisha akarusha teke lingine lililomkuta shingoni mpelelezi, mpelelezi akamuachia, Trigger haraka akasimama na kwenda kuichukua ile bastola na kumuelekezea mpelelezi,
"Nyanyuka" Trigger alimwambia, mpelelezi akatii huku mikono ikiwa juu,
"Unachofanya unadhani ni sahihi?" Mpelelezi alimuuliza Trigger huku mikono ikiwa juu,
"Usahihi wa mtu upo kulingana na akiwazacho" Trigger alijibu huku akitabasamu,
"Sawa, shusha silaha chini" Mpelelezi alimwambia Trigger,
"Daima Trigger akimnyooshea mtu silaha uwa haishushi silaha chini mpaka risasi itoke" Trigger aliongea na safari hii hakuwa na tabasamu tena,
"Unamaanisha nini?" Mpelelezi aliuliza lakini hakupewa jibu, Trigger alifyatua risasi ilienda moja kwa moja katika kichwa cha mpelelezi, mpelelezi akarushwa mpaka dirishani, dirisha likapasuka vioo na mpelelezi akatokea dirishani mpaka chini, aliporomoka umbali wa ghorofa saba.
"Maana yangu ni hiyo" Trigger aliongea kisha akaitupia chini ya kitanda ile bastola na kisha akatoka ndani huku akikimbia. Alijiunga na watu wengine waliokuwa wanakimbia baada ya kusikia mlio ule wa bastola, Trigger akajichanganya nao na kuanza kukimbia kama na yeye ni mmoja wao vile, njiani wakati akishuka ghorofani alipishana na askari kadhaa wenye silaha wakipandisha juu.
Trigger alikimbia mpaka chini na kwenda eneo lile lile alipoanguakia yule mpelelezi, watu walishalizunguka eneo lile, Trigger akajisogeza na kupangua watu wawili watatu na kufanikiwa kuweza kumuona mpelelezi yule, alikuwa sio mtu tena, ulikuwa ni mwili tu usio na nafsi, yaani tayari mpelelezi alikuwa ni marehemu, Trigger akatoa tabasamu dogo na kisha akaanza kupangua watu ili aweze kutoka, aliwapangua na kutoka kwenye lile kundi la watu, akaanza kuelekea nje ya geti, alitoka nje ya geti la hospitali na kusimamisha usafiri, akapanda na kupelekwa moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Taita.
Alimkuta Taita akiwa anajiandaa na safari ya kwenda msibani,
"Nadhani umemaliza kazi" Taita aliongea huku akifungua mlango wa gari lake,
"Misheni imefeli" Trigger aliongea kwa sauti tulivu na kufanya Taita ashtuke na asitishe mpango wa kufungua mlango wa gari,
"Kipi kilichokufanya ukashindwa?" Taita aliuliza kwa ukali,
"Wakati natekeleza mpango alitokea askari mwenye silaha, ndio alinikwamisha" Trigger alijibu,
"Oooh shit, alafu nini kikafuata mpaka umerudi Salama?" Taita aliendelea na maswali,
"Nilimdhibiti yule askari, nikamuua ndipo nikafanikiwa kukimbia" Trigger alijibu,
"Safi, je mtoto hukumuona tena?" Taita alihoji,
"Sijabahatika kumuona tena, nadhani alienda kujiweka sehemu Salama zaidi" Trigger alijibu,
"Sawa, mimi naelekea msibani, nadhani wewe unapaswa kurudi kule hospital ili ukaendelee kufuatilia nyendo za mtoto" Taita aliongea huku akiingia ndani ya gari,
"Sawa, Harry yupo wapi?" Trigger aliuliza,
"Nitamkuta mbele uko, kuna sehemu ameenda" Taita alijibu,
"Safari hii inabidi niende na gari ili niwe huru zaidi" Trigger aliongea na kufanya Taita ajisachi na kutoa ufunguo wa gari na kumkabidhi Trigger,
"Chukua ile harrier nyeusi, ipo hapo mtaa wa nyuma inaoshwa, kuna tatizo jingine?" Taita aliuliza,
"Hakuna, kama litatokea tutawasiliana" Trigger aliongea kisha Taita akawasha gari na kuliondoa taratibu na kupotea eneo hilo na kumuacha Trigger akimtazama.
Taita aliendesha gari mpaka mtaa unafuatia na kumkuta harry akimsubiri hapo, akampakia kwenye gari na kisha wakaanza safari ya kwenda msibani.
Ndani ya gari Taita alimueleza Harry kila kitu kuhusu Trigger kutofanikisha mpango wa kumuua Sarah na kisha akamueleza ni kitu gani amemuagiza akakifanye.
"Hili jambo la kummaliza linatakiwa liwe la haraka, maana yule mtoto ni mkubwa na anajua kila kitu kilichotokea kuhusu wazazi wake" Harry aliongea,
"Ila nitafanikisha tu, maana nikishamchukua na kuishi nae ndipo nitamuua kirahisi" Taita aliongea,
"Hiyo usiiwaze, anaweza kutuchoma hata kabla hujamchukua, wewe fikiria kama aliweza kumtambua Trigger anashindwa vipi kukutambua wewe?" Harry aliuliza,
"Madaktari wamesema kumbukumbu zake haziko sawa" Taita aliongea,
"Upuuzi mtupu, kama kumbukumbu zake hazipo sawa amemtambuaje Trigger, ni ujinga kuendelea kufikiria hivyo" Harry aliongea huku akionekana kutofurahishwa na mawazo ya boss wake,
"Ebu ngoja tukitoka uko msibani tutapanga vizuri" Taita aliongea kwa utulivu,
"Mmh sawa" Harry aliishia kuguna tu kisha ukimya ukatawala.
Gari lilitembea kwa mwendo mrefu na atimae lilifika eneo lenye msiba. Taita aliposhuka tu, wanawake ambao walikuwa wakifahamu uhusiano wake na magreth wakaanza kuangusha kilio upya, yaani utasema wamepokea habari hizo muda huu.
"Broo unatakiwa uingie ndani moja kwa moja" Kijana mmoja aliongea sikioni kwa Taita, inaelekea huyu kijana ni ndugu wa Isack ambaye ni baba yake Sarah.
Taita akaelekea moja kwa moja sehemu aliyotakiwa na kuingia ndani ambapo aliwakuta wazazi wa Isack na ndugu wengine, Taita akawasalimia na kuoneshwa sehemu ya kukaa,
"Mbona umechelewa mwanangu?" Baba Isack alimuuliza,
"Asubuhi niliamkia hospitali ili nikamuangalie Sarah hali yake ipoje" Taita akajitetea,
"Vizuri, anaendeleaje mjukuu wangu?"Baba Isack aliuliza,
"Mzima kabisa, kesho anaweza kuruhusiwa, nitamchukua na kuishi nae" Taita alijibu,
"Na yule mwingine mdogo yeye ndio ameteketea kabisa kawa majivu" Baba isack aliongea kwa uchungu,
"Dah, ni mipango ya Mungu" Taita alijibu,
"Sasa hapa sisi tumeshapanga maziko, tumeamua kupanga mapema baada ya kukusubiri muda mrefu na hukutokea, kwa hiyo hapa tunachongoja kutoka kwako ni kuridhia na kubariki mipango yetu" Baba Isack alizungumza na kumtupia jicho Taita,.
"Mmepanga yafanyike lini?" Taita aliuliza,
"Leo hii saa kumi" Baba Isack alijibu,
"Kwanini tusimsubiri mtoto aruhusiwe hospitali hili naye ashiriki maziko ya wazazi wake?" Taita aliuliza,
"Hata sisi tulitaka iwe hivyo, ila kwa jinsi ile miili ilivyoharibika, ni ngumu sana kuacha mpaka kesho" Baba Isack alijibu
"Sawa, mimi nimeridhia" Taita aliongea kwa upole,
"Nashukuru sana kijana wangu, nadhani cha muhimu ni kwenda tu monchwari kuisafisha miili ili mpaka saa saba iwe imefika hapa na mipango ya kuaga miili ianze" Baba Isack alizungumza na watu kadhaa wakamuunga mkono, kisha wakatoka baadhi ya ndugu wa marehemu wakiambatana na Taita na wakaelekea hospitali kwa ajili ya kuitayarisha miili ya marehemu.
*********************
Trigger alikuwa ameegesha gari lake ndani ya uzio wa hospitali huku akijaribu kuyasoma mazingira ya pale vizuri. Wakati akiwa bado anapiga hesabu zake ndipo alipomuona daktari akiwa ameongozana na Sarah na mwanaume wa makamo ambaye ni Mzungu. Trigger akayaweka macho yake umakini mkubwa, akaweza kuona daktari akitoa maelezo kwa yule Mzee wa kizungu, ila Trigger hakuweza kusikia neno lolote kwa kuwa alikuwa mbali kidogo.
Trigger aliendelea kushuhudia daktari akiongea na yule Mzee Mzungu na kisha akaona wakipeana mikono, alafu yule Mzee wa kizungu akaondoka huku akiwa ameongozana na Sarah na kuingia kwenye gari moja la kifahari, kisha ile gari ikaondoka kwa mwendo wa taratibu.
Baada ya lile gari kutoka nje ya geti, Trigger nae aliondoa gari lake na kuanza kuifuata ile gari huku akiwa anaangalia namna ya kupanga mashambulizi ya kummaliza Sarah.
Zile gari ziliendelea kufuatana huku zikiwa zimeachana umbali kidogo, walipofika eneo ambalo kulikuwa na pori kidogo, Trigger akaongeza mwendo na kuipita kabisa ile gari ya Mzee wa kizungu, tena akaiacha mbali kiasi kwamba hakuiona, alifanya hivyo makusudi baada ya kutengeneza mipango yake.
Trigger alienda na kusimamisha gari pembeni ya barabara, akashuka na kuanza kusubiri. Baada ya dakika tano ilitokea ile gari ya Mzee wa kizungu na Trigger akajifanya kama anatengeneza gari lake, yaani aliigiza gari lake limeharibika.
Gari la Mzee wa kizungu lilipomkaribia Trigger akalipiga mkono na likasimama pembeni ya barabara, Trigger akatazama kioo cha mbele kwa jicho la chini ili aone watu waliomo ndani ya gari, akamuona ni yule Mzee wa kizungu na Sarah tu, akajikuta anatabasamu na kuishusha kofia yake chini zaidi ili Sarah asimtambue.
Trigger akawa anasogea katika gari ya yule Mzee wa kizungu,
"Samahani Mzee gari yangu imeniharibikia, naomba msaada" Trigger aliongea huku akiwa amesimama katika dirisha la gari.
"Unataka msaada gani sasa?" Mzee wa kizungu aliuliza,
"Nataka maji, nahisi rejeta imeisha maji" Trigger aliongea huku mkono wake ukianza kuivuta bastola ndogo iliyopo kiunoni upande wa nyuma, Trigger mtu mbaya alidhamiria kuua, na kawaida yake ni kwamba akikunyooshea bastola uwa haishushi mpaka itoe risasi.......
*********ITAENDELEA**********
the Legend☆

