Riwaya: Sala ya Sarah

RIWAYA : SALA YA SARAH.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA TATU.

ILIPOISHIA...

Baada ya muda madaktari waliondoka na ndani akabaki daktari mmoja, mpelelezi akaingia,
"Karibu, mtoto huyu hapa amezinduka" Daktari aliongea, inaelekea wanajuana,
"Hakuna mtu aliyekuja kumuangalia?" Mpelelezi aliuliza,
"walikuja wafanyakazi wa wizara anayofanyia kazi mama yake" Daktari alijibu,
"Wamesemaje" Mpelelezi aliuliza,
"Hakuna, kwanza kipindi wanakuja bado mtoto alikuwa hajazinduka" Daktari alijibu,
"Ameongea tokea amezinduka?" Mpelelezi aliuliza,
"Hapana" Daktari alijibu na kipindi hiki ndipo Taita alikuwa anaingia wodini, alikuwa peke yake.
Alipoingia kwanza alishtuka kumuona Sarah akiwa amezinduka, akapata wasiwasi,
"Sarah unakumbuka jana nini kilitokea" Mpelelezi aliuliza na kumfanya Sarah amuangalie Taita, hapo sasa mapigo ya moyo ya Taita yakawa yanapishana bila mpangilio, yule mpelelezi akavua miwani na kumuangalia Taita kwa jicho kali.......

**********ENDELEA***********

"Unamjua huyu?" Mpelelezi alimuuliza Sarah huku akimuangalia Taita, Sarah akakataa kwa kuyumbisha kichwa kushoto na kulia,

"Hana kumbukumbu vizuri, kuna baadhi ya vitu na watu hawakumbuki, nadhani aliangukia kisogo" Daktari aliongea huku akitabasamu,

"Bosi umekuja kumuona mtoto?" Mpelelezi aliuliza huku akimtupia jicho Taita,

"Ndio, ni Mjomba wangu kabisa huyu, mama yake ni mdogo wangu" Taita aliongea huku akitabasamu,

"Wewe ndio Taita? Nilikuwa nakutafuta. Naitwa Simon Frank, ila wewe niite Sai" Mpelelezi aliongea huku akivaa miwani yake na kumpa mkono Taita,

"Nashukuru kukufahamu, je kwanini unanitafuta?" Taita aliuliza,

"Mimi ndiye niliyepewa kazi ya kupeleleza juu ya moto ulioteketeza familia ya dada yako" Sajenti Minja alijibu,

"Si ni moto tu wa kawaida, inawezekana ni itirafu ya umeme, au labda unadhani nini?" Taita aliuliza huku wasiwasi ukimrudia tena, maana hakutegemea habari kama ile,

"Kwa maelezo ya majirani, inawezekana kabisa ile nyumba ilichomwa na watu" Mpelelezi yule aliongea na kufanya Taita ashtuke wazi,

"Hao watu wamepatikana?" Taita aliuliza,

"Bado, nadhani tutaongea zaidi kwa muda mwingine, hili eneo sio rafiki na maongezi yetu" Mpelelezi aliongea,

"Sawa afisa" Taita alijibu huku akishukuru kwa hayo maongezi kusitishwa,

"Sasa muheshimiwa huyu mtoto atabaki hapa kwa siku moja zaidi ili tuangalie hali yake" Daktari aliongea huku akimuangalia Taita,

"Sawa, nitakuja kumchukua nikaishi nae kwangu" Taita alijibu,

"Sawa, ila kuna mtu nae amesema atamchukua huyu mtoto ili akaishi nae" Daktari aliongea,

"Ni nani huyo mtu? mimi ndio nitakaa nae" Taita aliongea kwa ukali kidogo,

"Usipate shida, kesho uje umchukue, kwa maana wewe ni kama mwanao huyu" Daktari aliongea huku akitabasamu,

"Gharama za Huduma uliyompatia ni shilongi ngapi?" Taita aliuliza,

"Zimeshalipwa" Daktari alijibu,

"Ni nani huyo aliyelipa?" Taita aliuliza,

"Huyo mtu ambaye amesema atamchukua huyu mtoto" Daktari alijibu,

"Sawa, mimi natoka, akija tu huyo mtu umwambie akuachie namba zake ili tuwasiliane" Taita aliongea kisha akaondoka bila hata ya kuaga.

"Huyu Jamaa anaonekana mbabe mbabe sana" Mpelelezi aliongea huku akimuangalia Daktari,

"Huyu ndivyo alivyo, ila ni tajiri sana huyu, ana pesa chafu" Daktari alimuambia Mpelelezi,

"Haya bwana, acha mimi nirudi ofisini, ila unatakiwa umbadilishe huyu mtoto, mpeleke kwenye wodi nyingine" Mpelelezi alimshauri Daktari,

"Kwanini?" Daktari aliuliza,

"Mazingira ya vifo vya familia yake inaonekana wameuawa, nina wasiwasi kuwa huenda watu waliofanya hivyo wanaweza kurudi hapa kummalizia huyu mtoto"Mpelelezi aliendelea kumshauri daktari,

"Kweli aisee, basi inabidi utoke nae na kumpeleka wodi namba 543, ipo ghorofa ya juu kabisa, mimi nakuja" Daktari aliongea na kisha Sajenti Mpelelezi akambeba Sarah na kwenda nae nje ya wodi, Kisha akaingia kwenye lift na kupanda nae juu mpaka katika wodi aliyoelekezwa na Daktari, alipofika alimshusha Sarah na kumuweka juu ya kitanda,

"Nikuletee nini to too?" Mpelelezi alimuuliza Sarah, ila Sarah alijibu kwa kutingisha kichwa kwa ishara ya kukataa,

"Nitakuletea juisi baadae, lala mtoto mzuri" Mpelelezi aliongea huku akimlaza kitandani Sarah na kumfunika shuka zito, kisha Mpelelezi yule akatoka na kwenda zake ofisini kwake.

*******************

Taita alivyotoka ndani ya wodi, alienda moja kwa moja mpaka alipoegesha gari lake na kuingia ndani ya gari ambapo alikuwa Harry na Trigger,

"Trigger nenda kamalize kazi, utatukuta nyumbani" Taita aliongea,

"Wodi namba ngapi?" Trigger aliuliza huku akiitoa bastola yake ilikuwa chini ya kiti cha gari,

"Bastola ya nini tena, yule unamvunja tu shingo, mbona anashingo laini tu, alafu nenda kwa akili kwa maana kuna askari na daktari" Taita alitoa angalizo,

"Sawa mkuu" Trigger aliongea na kushuka ndani ya gari, akaanza kuelekea wodini, ndani ya gari akabaki Taita na Harry.

"Mtoto hajanikumbuka, Daktari anadai kuwa kuna baadhi ya kumbukumbu amepoteza" Taita alimwambia Harry huku akiwasha gari lake,

"Ila zitarudi, kumbukumbu za hivyo hazipoteagi Mara moja" Harry alijibu,

"Acha Trigger akammalize" Taita aliongea,

"Alafu suala la msiba linakuaje?" Harry aliuliza,

"Huu msiba utafanyika kwa wazazi wa ndugu wa mume, walinipigia asubuhi na kuniomba wachukue miili ya watu wote wawili" Taita alijibu,

"Hawajamuulizia mtoto mdogo wa kiume?" Harry aliuliza,

"Wanajua ameteketea na moto mpaka amekuwa majivu, ila kuna askari niliyemkuta ndani ya wodi, huyo anaweza kuwa kikwazo kwetu" Taita aliongea,

"Inabidi afe" Harry aliongea,

"Itabid iwe hivyo, ngoja Tri arudi nimpe hiyo mission" Taita aliongea huku akiliingiza gari lake ndani ya uzio wa nyumba yake.

"Msibani tunaenda muda gani?" Harry aliuliza,

"Nitaenda hata usiku" Taita alijibu,

"Hapo ndipo unakosea, ujue wewe ndio ndugu wa karibu kabisa wa Dada yako, unatakiwa ufike mapema ili mawazo juu ya maziko mkapange pamoja, hata Kama usipotia neno basi uwepo wako unaweza kuleta hisia nzuri kwa watu wanaojua uhusiano wenu" Harry aliongea huku akimtazama Taita,

"Muda huu nilitaka nimpeleke mtoto akachomwe sindano ya kupoteza kumbukumbu" Taita aliongea huku akiingia ndani na Harry akamfuata kwa nyuma,

"Lakini hiyo ya mtoto haina haraka sana, tutaifanya hata baada ya kumalizika msiba" Harry aliendelea kumshauri Taita,

"Lakini haya mambo ya msiba ni kama hayanihusu" Taita aliongea kijinga huku akigeuka,

"Hapo unakosea boss, inabidi twende kule msibani, usipoenda watu wanaweza kuhisi vibaya, na kama ulivyosema kuna askari wameanza kifuatilia lile tukio, itakuwa hatari upande wetu" Harry aliongea,

"Basi nimekuelewa, sasa kitu kingine ni huyu mtoto, sitaki ahishi hapa, mke wangu naijua roho yake, anaweza kumfanya kitu kibaya" Taita aliongea,

"Hilo ni sala zuri, twende kwanza msibani alafu tukirudi tutapanga" Harry aliongea,

"Haina shida, ngoja nikabadili nguo" Taita aliongea huku akielekea chumbani kwake.

**************

Trigger aliingia ndani ya hospital na kuanza kutembea koridoni huku akisoma namba za wodi katika kila mlango. Aliendelea kutembea kwa mwendo huo mpaka alipofika kwenye wodi namba nne, alisukuma mlango na kuingia, akukuta kitandani hakuna mtu, ila alimkuta daktari akikusanya vitu vyake, nadhani alikuwa anajiandaa kuondoka,

"Habari dokta, nilikuja kumuangalia mgonjwa wangu, ni mtoto mdogo wa kike, anaitwa Sarah" Trigger aliuliza huku akimuangalia Daktari,

"Wewe ni nani yake?" Daktari alimuuliza,

"Ni mdogo wa baba yake" Trigger alijibu,

"Oooh ni baba yake mdogo? mtoto tulimuamisha, yupo wodi namba 543" Daktari alijibu,

"Ipo upande gani hiyo wodi?" Trigger aliuliza,

"Nenda ghorofa ya mwisho juu, utaulizia uko" Daktari aliongea na Trigger akatoka wodini na kuelekea kwenye lifti, akapanda mpaka katika ghorofa aliyoelekezwa. Wakati anatoka ndani ya lifti, akakutana na mpelelezi,

"Samahani mista, eti wodi namba 543 ipo upande gani?" Trigger aliuliza na kufanya mpelelezi atie shaka kidogo,

"Wewe ni mgeni humu?" Mpelelezi aliuliza,

"Hujakosea, nipo hapa kumuona mtoto wa kaka yangu" Trigger aliongea,

"Elekea na hii korido mpaka kule mwisho, ingia kushoto wodi ya pili upande wa kulia" Mpelelezi alielekeza na kuingia ndani ya lifti.

Trigger akafuata maelekezo na kwenda moja kwa moja mpaka sehemu husika, alipofika alisukuma mlango na kumkuta Sarah akiwa amelala huku amefunikwa shuka zito mwilini.

Trigger akamsogelea kwa tahadhari na kumfikia, Sarah akafungua macho na kukutana na sura ya Trigger, uzuri ni kuwa alimkumbuka, Sarah akaanza kupiga kelele, Trigger akamuwahi na kumziba mdomo kwa mkono mmoja,

"Sssssssshiiii" Trigger aliongea huku akiwa ameweka kidole chake cha shaada kwenye midomo yake, alikuwa anatoa ishara ya kutaka Sarah ahache kelele, lakini Sarah aliendelea kukuruka pale kitandani, Trigger akajiona kama anapoteza muda, akachukua mikono yake na kuikamata shingo ya Sarah, Trigger akaongeza nguvu mikononi ili atimize lengo lake, alidhamiria kummaliza huyu malaika hasiye na hatia......

***********ITAENDELEA**********

*Nini hatma ya Sarah?

*je mpelelezi atafanikisha dhamira ya kuujua undani wa kesi hii?
*fuatilia sehemu inayofuata

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom