the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,112
- Thread starter
- #101
RIWAYA : SALA YA SARAH
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA KUMI NA SITA.
ILIPOISHIA.
Dereva wa gari ndogo akashusha kioo, alikuwa ni yule dalali wa Sarah, vijana wa Taita wakamsalimia,
"Unaweza kutufungulia milango kuna mtu tunamtafuta" Kijana wa Taita aliongea huku akimuangalia Dalali,
"Hakuna mtu zaidi yangu ndani ya gari" Dalali alijibu baada ya kufikiria kwa muda, vijana wa Taita wakamtilia shaka,
"Basi fungua milango" kijana mmoja akaongea kwa hasira,
"Hakuna mtu, si nimeshawaambia" Dalali aliongea,
"Mbona mnambeleleza sana" kijana mwingine aliongea huku akimuwekea bastola usawa wa kichwa yule dereva,
"Haya fungua milango" Kijana aliongea huku akiwa hana mzaha hata kidogo, dalali akalegeza kamba, aka unlock milango yote, kisha kwa pupa vijana wa Taita wakakimbilia kufungua milango ya nyuma ya ile gari ya dalali.........
************ENDELEA**************
Baada ya kufungua milango hawakukuta mtu ndani ya gari,
"Niliwaambia nipo peke yangu, mbona mnanichelewesha? kwanza nyie ni wakina nani, mbona hamjajitambulisha?" Dalali aliuliza kwa kulalamika lakini hakujibiwa kitu, vijana wa Taita walikuwa bize na upekuzi wa gari.
Walipekua na walipojiridhisha ndipo wakamruhusu dalali aondoke, Dalali aliondoka huku akinung'unika sana, alihisi hakutendewa haki kabisa.
Vijana wa Taita wakaendelea kusimama pale huku wakiendelea na kazi ya kukagua kila chombo cha usafiri kinachoingia na kutoka eneo lile.
**********_**
Tekso akiwa na vijana wawili walifanikiwa kufika mpaka guest ile aliyokuwa anaishi Sarah, waliweza kufika kaunta na kumkuta dada wa mapokezi akisugua kucha zake,
"Karibuni kaka zangu, vyumba vipo" Dada wa mapokezi aliongea kwa uchangamfu,
"Hapana hatuna shida na vyumba, kuna dada tunamtafuta anaishi hapa" Tekso aliongea huku akimtazama Dada wa mapokezi aliyekuwa na mwili mkubwa, uswahilini tunawaita vibonge,
"Yukoje?" Dada wa mapokezi akauliza,
"Mwembamba na ana kimo cha wastani, mweupe" Tekso alitoa jibu kulingana na maelezo ya Taita,
"Ameondoka muda sio Mrefu" Dada wa mapokezi alijibu,
"Atarudi muda gani?" Tekso aliuliza,
"Yaani ameondoka moja kwa moja, amesema anaenda kuishi kwa rafiki yake kwa kuwa kuishi hapa ni gharama. Ni ndugu yenu kwani?" Dada wa mapokezi aliuliza,
"Ameondoka muda gani?" Tekso aliuliza huku akiwa amekata tamaa,
"Sasa hivi tu, yaani hana hata dakika tano" Dada wa mapokezi alijibu na kufanya Tekso awaze kwa muda,
"Ameondoka na usafiri?" Tekso aliuliza,
"Ndio, amechukuliwa na gari ndogo nyeusi" Dada wa mapokezi alijibu na kufanya Tekso akumbuke kuwa alipishana na gari ndogo nyeusi iliyokuwa na vioo vya Giza (tinted),
"Ebu wapigie simu wenzako waulize kama wameiona hiyo gari pale njiani" Tekso aliongea huku akimgeukia kijana mmoja waliyeambatana nae, yule kijana akatoa siku mfukoni na kubonyeza vitufe kadhaa kisha akaiweka simu sikioni, baada ya sekunde akaanza kuongea na upande wa pili wa siku na kisha akakata,
"Hiyo gari wameiona ila wanadai ndani alikuwepo mtu mmoja tu, mwanaume" Kijana aliyeongea na simu alimpa taarifa Tekso,
"Dah, kwa hiyo inawezekana huyo dada bado yupo mtaa huu huu?" Tekso aliwauliza wenzake,
"Kama hawajamuona basi inawezekana yupo" Kijana mmoja alijibu,
"Dada unaweza kunipeleka chumba alichokuwa anahishi?" Tekso alimuuliza Dada wa mapokezi,
"Lakini kaka yangu hamjajitambulisha" Dada wa mapokezi aliongea,
"Utatujua baadae, nipeleke katika chumba alichokuwa anaishi" Tekso aliongea na kisha Dada wa mapokezi akatoka kaunta na kuelekea moja kwa moja katika chumba alichokuwa akikaa Saraha na kukifungua mlango kisha akaingia na nyuma yake alikuwa Tekso, baada ya kuingia ndani Tekso akaanza kukichunguza kile chumba kama ataambulia chochote, ila hakubagatika kupata kitu chochote, akatoka nje huku akifuatwa na dada wa mapokezi.
Walielekea mpaka kaunta,
"Unaweza kutusaidia jina lake?" Tekso alimuuliza yule dada, na kufanya yule dada achukue daftari lake la orodha ya wageni walichukua vyumba na kuanza kupekua kutafuta jina la Sarah ila hakuliona, akarudia tena pia hakuona,
"Jina lake halionekani" Dada wa mapokezi aliongea,
"Kwani wewe hulijui jina lake?" Tekso alimuuliza,
"Silijui" Dada wa mapokezi alijibu na kufanya Tekso amuangalie tu bila kuongea kitu, kisha akawaamuru vijana wake waondoke eneo hilo.
Tekso na vijana wake wakaenda mpaka walipokuwa wenzao na gari lao, wakaongea maneno mawili matatu kisha wakaingia kwenye gari na kuondoka zao.
******************
Kipindi hicho chote Sarah alikuwa ameshafika mbali sana, kumbe hakuingia ndani ya gari la dalali, badala yake Sarah alimuuliza dalali kama kuna njia nyingine ya kuondoka eneo lile tofauti na hiyo inayotumiwa kila siku, ndipo dalali aliposema kuwa njia ipo ila ni ya watembea kwa miguu tu, vyombo vya moto haviwezi kupita kwa maana mbele kuna mto umekatiza na hakuna daraja kubwa, kuna kadaraja kadogo tu kwa ajili ya watu.
Sarah ndipo akachagua kupita njia hiyo, alifanya hivyo baada kuhisi huenda vijana wa Taita wanaweza kusambazwa njia kubwa na ikawa kazi kwake kutoka salama eneo hilo. Sarah akaamua kupita uko huku akimwambia dalali watawasiliana baada ya muda mchache.
Sarah alifanikiwa kutembea mpaka alipofika eneo lenye watu wengi, akachukua simu yake na kumpigia dalali ili amfuate, haikuchukua muda Mrefu sana dalali akafika eneo lile na kisha sarah akaingia ndani ya gari, tena siti za mbele,
"Kwanini ulipita ile njia?" Dalali alimuuliza Sarah,
"Kuna kitu nilienda kununua, maana nilielekezwa kinapatikana mitaa ile" Sarah alimdanganya dalali,
"Basi mwenzako mbele nilikutana na maaskari sijui wale, wakanisimamisha, inaelekea kuna mtu wanamtafuta" Dalali aliongea na kufanya Sarah ashtuke, ila hukuonesha mshtuko wake,
"Huenda kuna kibaka au jambazi wanamtafuta, huenda waliambiwa yupo mtaa ule" Sarah aliongea huku akiuficha mshtuko wake,
"Wasumbufu tu wale" Dalali aliongea,
"Waache wafanye kazi" Sarah aliongea na kisha yakafuata maongezi mengine ya kawaida mpaka walipofika kwenye hiyo nyumba ambayo Sarah ameenda kuiangalia.
Wakashuka na kisha Dalali akaenda kumchukua mwenye nyumba, hakuwa mbali na pale,
Kipindi dalali ameenda kumchukua mwenye nyumba, Sarah alitumia muda huo kuikagua ile nyumba kwa kuizunguka, baada ya dakika tano dalali alifika huku akiwa ameongozana na mwenye nyumba,
"Karibu binti" Mwenye nyumba aliongea huku akimpa mkono Sarah,
"Asante, shikamoo baba" Sarah alimsalimia huku akimpa mkono,
"Marahaba binti, nyumba umeiona?" Mwenye nyumba alimuuliza Sarah,
"Nimeiona kwa nje, nimeridhika ila bado sijajua kwa ndani ikoje?" Sarah alijibu,
"Twendeni ndani ili apaone" Mwenye nyumba alimwambia dalali kisha wakaanza kuelekea ndani ya nyumba, walifika mlangoni kisha mwenye nyumba akafungua mlango na wote wakaingia, Sarah akaanza kuikagua ile nyumba, alikagua kila chumba na kila kitu ndani ya ile nyumba, akaridhika nayo.
"Nimeridhika Mzee wangu, je naweza kuipata leo, yaani tukauziana na kumalizana leo leo?" Sarah alimuuliza mwenye nyumba,
"Mbona haraka hivyo?" Mwenye nyumba aliuliza kwa mshangao,
"Nahitaji leo Mzee, naomba tumalizane tu" Sarah aliongea kwa mkazo,
"Sawa, twende kwa mwenyekiti wa kijiji na pia unatakiwa na mashahidi wawili" Mwenye nyumba aliongea,
.
"Shahidi yupo mmoja, huyu dalali, sina ndugu Tanzania" Sarah aliongea na kufanya wenzie wamtolee macho,
"Wewe ni mgeni?" Mwenye nyumba aliuliza,
"Mgeni, sina ndugu wala sina rafiki" Sarah alijibu,
"Umetoka nchi gani?" Mwenye nyumba aliuliza,
"Uingereza" Sarah alijibu,
"Mbona unaongea kiswahili safi?" Dalali aliuliza,
"Nilijifunza na pia Nina kidogo hapa nchini kwenu" Sarah alijibu,
"Sawa mama nimekuelewa, sasa itabidi uwe na kila kitu ili tufanikishe kuuziana hii nyumba, hata ikishindikana kufikia makubaliano leo, basi kesho naamini tutamalizana" Mwenye nyumba aliongea,
"Itabidi iwezekane leo, maana sina pa kulala" Sarah aliongea na kufanya wenzake wacheke wakidhani utani wakati mwenzao alidhamiria.
Baada ya hapo wakatoka mpaka kwa mwenyekiti wa mtaa na kuanza hatua za kuuziana nyumba, ingawa kulikuwa na hatua nyingi na ngumu, ila baada ya masaa matatu kila kitu kilienda sawa, Sarah akachukua nyumba yake, kisha akaenda mjini na kununua samani za ndani na kuchukua vijana watano kwa ajili ya kumsaidia kufanya usafi.
Baada ya masaa mawili kila kitu kilikuwa safi, nyumba ilinoga, na ikawa ndio makazi rasmi ya Sarah.
Akawalipa vijana wale kisha wakaondoka zao, yeye akaelekea bafuni kuoga, alipomaliza akaingia chumbani kwake na kuvaa suruali nyeusi na fulana nyeusi, usoni alivaa miwani yenye kioo cheupe, hiyo ilikuwa yapata saa kumi na mbili jioni.
************************
Mishale ya saa moja jioni, Taita na jopo lake la watu muhimu walikuwa wanaingia vin hotel, moja kwa moja wakaelekea kwenye chumba kidogo cha mikutano kwa ajili ya kujadili shambulio la bomu lilimuua kijana wao mmoja.
Mwenyekiti wa kikao alikuwa Taita, ila kabla hawajafungua rasmi kikao, mlango wa kile chumba ulifunguliwa na mlangoni alisimama binti akiwa na nguo nyeusi, Taita na wenzake wakabaki wamemtolea macho...............
**********ITAENDELEA**********
the Legend☆
MTUNZI : ALEX KILEO.
SEHEMU YA KUMI NA SITA.
ILIPOISHIA.
Dereva wa gari ndogo akashusha kioo, alikuwa ni yule dalali wa Sarah, vijana wa Taita wakamsalimia,
"Unaweza kutufungulia milango kuna mtu tunamtafuta" Kijana wa Taita aliongea huku akimuangalia Dalali,
"Hakuna mtu zaidi yangu ndani ya gari" Dalali alijibu baada ya kufikiria kwa muda, vijana wa Taita wakamtilia shaka,
"Basi fungua milango" kijana mmoja akaongea kwa hasira,
"Hakuna mtu, si nimeshawaambia" Dalali aliongea,
"Mbona mnambeleleza sana" kijana mwingine aliongea huku akimuwekea bastola usawa wa kichwa yule dereva,
"Haya fungua milango" Kijana aliongea huku akiwa hana mzaha hata kidogo, dalali akalegeza kamba, aka unlock milango yote, kisha kwa pupa vijana wa Taita wakakimbilia kufungua milango ya nyuma ya ile gari ya dalali.........
************ENDELEA**************
Baada ya kufungua milango hawakukuta mtu ndani ya gari,
"Niliwaambia nipo peke yangu, mbona mnanichelewesha? kwanza nyie ni wakina nani, mbona hamjajitambulisha?" Dalali aliuliza kwa kulalamika lakini hakujibiwa kitu, vijana wa Taita walikuwa bize na upekuzi wa gari.
Walipekua na walipojiridhisha ndipo wakamruhusu dalali aondoke, Dalali aliondoka huku akinung'unika sana, alihisi hakutendewa haki kabisa.
Vijana wa Taita wakaendelea kusimama pale huku wakiendelea na kazi ya kukagua kila chombo cha usafiri kinachoingia na kutoka eneo lile.
**********_**
Tekso akiwa na vijana wawili walifanikiwa kufika mpaka guest ile aliyokuwa anaishi Sarah, waliweza kufika kaunta na kumkuta dada wa mapokezi akisugua kucha zake,
"Karibuni kaka zangu, vyumba vipo" Dada wa mapokezi aliongea kwa uchangamfu,
"Hapana hatuna shida na vyumba, kuna dada tunamtafuta anaishi hapa" Tekso aliongea huku akimtazama Dada wa mapokezi aliyekuwa na mwili mkubwa, uswahilini tunawaita vibonge,
"Yukoje?" Dada wa mapokezi akauliza,
"Mwembamba na ana kimo cha wastani, mweupe" Tekso alitoa jibu kulingana na maelezo ya Taita,
"Ameondoka muda sio Mrefu" Dada wa mapokezi alijibu,
"Atarudi muda gani?" Tekso aliuliza,
"Yaani ameondoka moja kwa moja, amesema anaenda kuishi kwa rafiki yake kwa kuwa kuishi hapa ni gharama. Ni ndugu yenu kwani?" Dada wa mapokezi aliuliza,
"Ameondoka muda gani?" Tekso aliuliza huku akiwa amekata tamaa,
"Sasa hivi tu, yaani hana hata dakika tano" Dada wa mapokezi alijibu na kufanya Tekso awaze kwa muda,
"Ameondoka na usafiri?" Tekso aliuliza,
"Ndio, amechukuliwa na gari ndogo nyeusi" Dada wa mapokezi alijibu na kufanya Tekso akumbuke kuwa alipishana na gari ndogo nyeusi iliyokuwa na vioo vya Giza (tinted),
"Ebu wapigie simu wenzako waulize kama wameiona hiyo gari pale njiani" Tekso aliongea huku akimgeukia kijana mmoja waliyeambatana nae, yule kijana akatoa siku mfukoni na kubonyeza vitufe kadhaa kisha akaiweka simu sikioni, baada ya sekunde akaanza kuongea na upande wa pili wa siku na kisha akakata,
"Hiyo gari wameiona ila wanadai ndani alikuwepo mtu mmoja tu, mwanaume" Kijana aliyeongea na simu alimpa taarifa Tekso,
"Dah, kwa hiyo inawezekana huyo dada bado yupo mtaa huu huu?" Tekso aliwauliza wenzake,
"Kama hawajamuona basi inawezekana yupo" Kijana mmoja alijibu,
"Dada unaweza kunipeleka chumba alichokuwa anahishi?" Tekso alimuuliza Dada wa mapokezi,
"Lakini kaka yangu hamjajitambulisha" Dada wa mapokezi aliongea,
"Utatujua baadae, nipeleke katika chumba alichokuwa anaishi" Tekso aliongea na kisha Dada wa mapokezi akatoka kaunta na kuelekea moja kwa moja katika chumba alichokuwa akikaa Saraha na kukifungua mlango kisha akaingia na nyuma yake alikuwa Tekso, baada ya kuingia ndani Tekso akaanza kukichunguza kile chumba kama ataambulia chochote, ila hakubagatika kupata kitu chochote, akatoka nje huku akifuatwa na dada wa mapokezi.
Walielekea mpaka kaunta,
"Unaweza kutusaidia jina lake?" Tekso alimuuliza yule dada, na kufanya yule dada achukue daftari lake la orodha ya wageni walichukua vyumba na kuanza kupekua kutafuta jina la Sarah ila hakuliona, akarudia tena pia hakuona,
"Jina lake halionekani" Dada wa mapokezi aliongea,
"Kwani wewe hulijui jina lake?" Tekso alimuuliza,
"Silijui" Dada wa mapokezi alijibu na kufanya Tekso amuangalie tu bila kuongea kitu, kisha akawaamuru vijana wake waondoke eneo hilo.
Tekso na vijana wake wakaenda mpaka walipokuwa wenzao na gari lao, wakaongea maneno mawili matatu kisha wakaingia kwenye gari na kuondoka zao.
******************
Kipindi hicho chote Sarah alikuwa ameshafika mbali sana, kumbe hakuingia ndani ya gari la dalali, badala yake Sarah alimuuliza dalali kama kuna njia nyingine ya kuondoka eneo lile tofauti na hiyo inayotumiwa kila siku, ndipo dalali aliposema kuwa njia ipo ila ni ya watembea kwa miguu tu, vyombo vya moto haviwezi kupita kwa maana mbele kuna mto umekatiza na hakuna daraja kubwa, kuna kadaraja kadogo tu kwa ajili ya watu.
Sarah ndipo akachagua kupita njia hiyo, alifanya hivyo baada kuhisi huenda vijana wa Taita wanaweza kusambazwa njia kubwa na ikawa kazi kwake kutoka salama eneo hilo. Sarah akaamua kupita uko huku akimwambia dalali watawasiliana baada ya muda mchache.
Sarah alifanikiwa kutembea mpaka alipofika eneo lenye watu wengi, akachukua simu yake na kumpigia dalali ili amfuate, haikuchukua muda Mrefu sana dalali akafika eneo lile na kisha sarah akaingia ndani ya gari, tena siti za mbele,
"Kwanini ulipita ile njia?" Dalali alimuuliza Sarah,
"Kuna kitu nilienda kununua, maana nilielekezwa kinapatikana mitaa ile" Sarah alimdanganya dalali,
"Basi mwenzako mbele nilikutana na maaskari sijui wale, wakanisimamisha, inaelekea kuna mtu wanamtafuta" Dalali aliongea na kufanya Sarah ashtuke, ila hukuonesha mshtuko wake,
"Huenda kuna kibaka au jambazi wanamtafuta, huenda waliambiwa yupo mtaa ule" Sarah aliongea huku akiuficha mshtuko wake,
"Wasumbufu tu wale" Dalali aliongea,
"Waache wafanye kazi" Sarah aliongea na kisha yakafuata maongezi mengine ya kawaida mpaka walipofika kwenye hiyo nyumba ambayo Sarah ameenda kuiangalia.
Wakashuka na kisha Dalali akaenda kumchukua mwenye nyumba, hakuwa mbali na pale,
Kipindi dalali ameenda kumchukua mwenye nyumba, Sarah alitumia muda huo kuikagua ile nyumba kwa kuizunguka, baada ya dakika tano dalali alifika huku akiwa ameongozana na mwenye nyumba,
"Karibu binti" Mwenye nyumba aliongea huku akimpa mkono Sarah,
"Asante, shikamoo baba" Sarah alimsalimia huku akimpa mkono,
"Marahaba binti, nyumba umeiona?" Mwenye nyumba alimuuliza Sarah,
"Nimeiona kwa nje, nimeridhika ila bado sijajua kwa ndani ikoje?" Sarah alijibu,
"Twendeni ndani ili apaone" Mwenye nyumba alimwambia dalali kisha wakaanza kuelekea ndani ya nyumba, walifika mlangoni kisha mwenye nyumba akafungua mlango na wote wakaingia, Sarah akaanza kuikagua ile nyumba, alikagua kila chumba na kila kitu ndani ya ile nyumba, akaridhika nayo.
"Nimeridhika Mzee wangu, je naweza kuipata leo, yaani tukauziana na kumalizana leo leo?" Sarah alimuuliza mwenye nyumba,
"Mbona haraka hivyo?" Mwenye nyumba aliuliza kwa mshangao,
"Nahitaji leo Mzee, naomba tumalizane tu" Sarah aliongea kwa mkazo,
"Sawa, twende kwa mwenyekiti wa kijiji na pia unatakiwa na mashahidi wawili" Mwenye nyumba aliongea,
.
"Shahidi yupo mmoja, huyu dalali, sina ndugu Tanzania" Sarah aliongea na kufanya wenzie wamtolee macho,
"Wewe ni mgeni?" Mwenye nyumba aliuliza,
"Mgeni, sina ndugu wala sina rafiki" Sarah alijibu,
"Umetoka nchi gani?" Mwenye nyumba aliuliza,
"Uingereza" Sarah alijibu,
"Mbona unaongea kiswahili safi?" Dalali aliuliza,
"Nilijifunza na pia Nina kidogo hapa nchini kwenu" Sarah alijibu,
"Sawa mama nimekuelewa, sasa itabidi uwe na kila kitu ili tufanikishe kuuziana hii nyumba, hata ikishindikana kufikia makubaliano leo, basi kesho naamini tutamalizana" Mwenye nyumba aliongea,
"Itabidi iwezekane leo, maana sina pa kulala" Sarah aliongea na kufanya wenzake wacheke wakidhani utani wakati mwenzao alidhamiria.
Baada ya hapo wakatoka mpaka kwa mwenyekiti wa mtaa na kuanza hatua za kuuziana nyumba, ingawa kulikuwa na hatua nyingi na ngumu, ila baada ya masaa matatu kila kitu kilienda sawa, Sarah akachukua nyumba yake, kisha akaenda mjini na kununua samani za ndani na kuchukua vijana watano kwa ajili ya kumsaidia kufanya usafi.
Baada ya masaa mawili kila kitu kilikuwa safi, nyumba ilinoga, na ikawa ndio makazi rasmi ya Sarah.
Akawalipa vijana wale kisha wakaondoka zao, yeye akaelekea bafuni kuoga, alipomaliza akaingia chumbani kwake na kuvaa suruali nyeusi na fulana nyeusi, usoni alivaa miwani yenye kioo cheupe, hiyo ilikuwa yapata saa kumi na mbili jioni.
************************
Mishale ya saa moja jioni, Taita na jopo lake la watu muhimu walikuwa wanaingia vin hotel, moja kwa moja wakaelekea kwenye chumba kidogo cha mikutano kwa ajili ya kujadili shambulio la bomu lilimuua kijana wao mmoja.
Mwenyekiti wa kikao alikuwa Taita, ila kabla hawajafungua rasmi kikao, mlango wa kile chumba ulifunguliwa na mlangoni alisimama binti akiwa na nguo nyeusi, Taita na wenzake wakabaki wamemtolea macho...............
**********ITAENDELEA**********
the Legend☆
