Riwaya: Sala ya Sarah

Riwaya: Sala ya Sarah

RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA SITINI NA SABA.

ENDELEA..................

Ila Sarah akaupiga mkono wa Trigger kwa chini na yeye akabonyea kidogo, ile risasi ya Trigger ilivyotoka iliondoka na baadhi ya nywele za Sarah, Sarah akashika kichwa huku Sajenti Minja na Aisha wakiwa hawaamini wanachokiona, kumbuka kwenye bastola ya Trigger kulikuwa na risasi moja tu, kwa hiyo baada ya kumkosa Sarah akataka aiwahi ile bastola iliyomponyoka Sarah, ila kwa wepesi wa Sarah aliinuka na kiti na kumpiga nacho Trigger kichwani, Trigger akadondoka chini, kisha Sarah akajibetua na kuokota bastola yake, kisha akamnyooshea Trigger aliyekuwa yupo chini,

"una lolote la kuongea labda?" Sarah alimuuliza Trigger huku akitabasamu, ila Trigger hakuonekana kutaka kujibu kitu, alikuwa yupo chini,

"inuka ukae kwenye kiti hapo juu" Sarah Alimwambia Trigger, ambaye alitii agizo,

"nisaidie kujibu hili swali, kulikuwa na ulazima gani kuwachoma wazazi wangu moto?" Sarah aliuliza huku akijishika kichwani eneo risasi ilipomkosa,

"maswali ya nini? Kama umeamua kuniua niue, sitojibu swali lolote kuhusu watu waliokufa" Trigger aliongea na kucheka, Sarah akaona huu muda sio wa kubembelezana, akamfyatulia risasi ya mguu na Trigger akatoa ukelele wa maumivu, kisha Sarah akatoa risasi nyingine na kuzijaza kwenye bastola yake, akampiga risasi nyingine Trigger, ila hii alimpiga kwenye mguu wa pili na kumfanya Trigger alie kama mtoto, kufikia hapo Trigger hakuwa na uwezo wa kutembea kwa maana miguu yote ilikuwa imepigwa risasi.

Sarah akainuka na kwenda sehemu alipofungwa Aisha na kumfungua,

"mfungue huyo mzee" Sarah alimwambia Aisha ambaye alifanya kama alivyoagizwa, baada ya Dokta Innocent Malle kufunguliwa akashukuru sana kwa Sarah,

"mzee ondoka, nenda nyumbani" Sarah aliongea kwa ukali,

"mama siwezi kuondoka, nimekuja na Kijana wangu hapa" Dokta Innocent Malle aliongea huku akimuangalia yule kijana wake,

"Aisha mfungue na huyo, ondokeni moja kwa moja nendeni nyumbani, msipite sehemu yoyote kutoa taharifa" Sarah aliongea kwa msisitizo,

"nifungueni na mimi" Sajenti Minja aliongea huku akiwatizama,

"huyo mfungue uondoke nae, mpeleke sehemu umfungie alafu utanitaharifu ulipo, nitakuja ngoja nimalizane na huyu mwamba" Sarah alimwambia Aisha kwa sauti ndogo ambayo Sajenti Minja hakuweza kusikia,

"mbona mnanong'ona? Mnataka kunifanya nini?" Sajenti Minja aliuliza kwa utani huku akicheka,

"ngoja tukuachie kamanda, ila ukiachiwa ondoka, sitaki ujihusishe na hii kazi hapa niliyonayo" Sarah aliongea huku akimuangalia Sajenti Minja,

"hakuna tabu" Sajenti Minja alijibu huku akiwa na wazo endapo ataachiwa atawageuzia kibao.

Aisha akaenda kwenye nguzo aliyofungiwa Sajenti Minja na kuanza kumfungua taratibu mpaka akamaliza, alipomaliza tu Sajenti Minja akatoa bastola yake,

"haya wewe jiunge na mwenzako hapo, mpo chini ya ulinzi" Sajenti Minja aliongea huku akimsukuma Aisha,

"wewe mpumbavu kweli" Aisha aliongea kisha akajizungusha na teke kali lililoipiga bastola ya Sajenti Minja na kufanya ianguke,

"tulia hivyo hivyo, Aisha mfunge kamba huyo" Sarah aliongea kwa hasira huku akimuangalia Sajenti Minja,

"nilikuwa nawadanganya tu" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu,

"hatuna utani" Aisha aliongea na kumchota mtama Sajenti Minja, kisha akamkimbilia na kumkamata mikono kwa nyuma na kumfunga kamba,

"haya tuondoke" Aisha aliongea huku akimuinua Sajenti Minja na kuanza kumkokota kuelekea nje.

Wakaelekea kwenye gari aliyokuja nayo Aisha kisha Sajenti Minja akawekwa upande wa kushoto wa dereva na Aisha akaingia upande wa dereva,

"unanipeleka wapi?" Sajenti Minja aliuliza,

"uwa unapenda mziki?" Aisha aliuliza huku akimuangalia,

"hujanijibu swali langu" Sajenti Minja aliongea tena,

"tunaenda clab, ndio maana nikauliza hupendi mziki?" Aisha alijibu huku akitabasamu, Sajenti Minja akahisi akilegea anaweza kutekwa kizembe, akamsukuma na bega Aisha, Aisha akapiga breki ya ghafla na Kumfanya Sajenti Minja akose balance kutokana na kamba alizofungwa, Sajenti Minja akakigonga kioo cha mbele cha gari kisha Aisha akamvuta kwa nguvu na kumpiga ngumi ya shingo iliyopelekea Sajenti Minja apoteze fahamu, kisha Aisha akakilaza kiti alichokalia Sajenti Minja, akakanyaga mafuta na gari ikatembea mbele.

"haka kajamaa kana mbinu za kizamani kweli, sema tu kamenikuta siku hizi nina ubinsdamu, vinginevyo asingekuwa hai huyu" Aisha aliongea kwa hasira kisha akaingiza gia.

Aisha aliendesha gari kwa muda wa dakika ishirini, kisha akaiingiza kwenye nyumba moja ndogo iliyokuwa katika uzio mkubwa, kisha akamtoa Sajenti Minja, akajaribu kumbeba akashindwa, akaamua ambulute mpaka ndani, akamuingiza katika eneo moja la wazi na kumfunga katika dirisha lililokuwa na nondo, kisha Aisha akashusha pumzi ndefu kutokana mchoko alioupata baada ya kumvuta Sajenti Minja.

"nipumzike kidogo kisha nimrudie Sarah nikamtazame kama ameshaondoka" Aisha aliongea huku akikaa sakafuni, kwa maana eneo hilo halikuwa na viti.

*******************

Taita aliendelea kukaa sebuleni huku mawazo yakionekana kumzidi, akasimama na kwenda kwenye friji akatoa maji ya baridi na kuyanywa kwa pupa, kisha akarudi kwenye kochi na kutafakari kwa muda, akatoa simu yake na kubofya namba anayoijua yeye, kisha simu akaweka sikioni na kuisikiliza kwa namna inavyoita ila simu haikupokelewa,

"huyu Trigger mpuuzi sana, yaani ni mzito sana kupokea simu" Taita alilaumu huku akikaa kwenye kochi, kisha akainuka na kwenda kwenye friji tena, akatoa pombe kali na kurudi nayo kwenye kochi, akatoa kizibo na kuigida kwa hasira, chupa ilipofika nusu akaishusha huku akiwa amekunja uso kutokana na ukali wa pombe yenyewe, akaiangalia simu yake tena na kufikiri kwa muda, kisha akaitafuta namba anayoitaka na kubonyeza, simu ikaanza kuita, iliita kwa muda na haikupokelewa, akaitupa simu kwa hasira,

"hawa watu vipi? au wameanza kunidharau?" Taita alijiuliza huku akiiangalia simu yake iliyoangukia juu ya kochi, ila akahisi mlango wa sebuleni unafunguliwa, akatupia macho mlangoni kwa haraka na kumuona Strategic akiingia,

"wewe mbona nakupigia simu hupokei?" Taita alimuuliza kwa hasira,

"sikuona sababu ya kuipokea wakati nilikuwa hapo nje, ndio maana nimekuja" Strategic alijibu huku akitabasamu,

"unatakiwa upokee na usikilize ninachosema, au ulijua nataka niseme nini?" Taita aliuliza kwa hasira,

"nisamehe mkuu" Strategic aliongea baada kuona Taita ana hasira kubwa sana,

"unapajua kwa Dokta Innocent Malle?" Taita alimuuliza Strategic na kumfanya Strategic afikirie kidogo,

"hapana, hata Dokta mwenyewe simjui" Strategic alijibu ingawa alikuwa anapajua,

"aaaaagh, nikikupa ramani si utaamka?" Taita aliuliza,

"ndio mkuu" Strategic alijibu kisha Taita akachukua karamu na karatasi na kuanza kuchora chora, aliporidhika akampatia ile karatasi Strategic,

"si utaelewa hapo?" Taita aliuliza,

"ndio mkuu" Strategic alijibu,

"nenda kamuangalie Trigger, nimemtuma uko, nampigia simu hapokei" Taita aliongea,

"endapo nitamkosa?" Strategic aliuliza,

"nipigie sure nenda kule kambini" Taita aliongea,

"sawa" Strategic alijibu,

"ukimkuta nipigie simu ili niongee naye" Taita aliongea,

"sawa" Strategic alijibu kisha akaondoka kwa haraka kuwahi kwenye gari, alipoingia kwenye gari simu yake iliita, alipoitazama aligundua ni Vin, akapokea simu haraka,

"nipo ndani hapa kwa mzee, nimesikia ukiongea nae, mimi amenifungia chumbani, je unaweza kuja kunisaidia kunifungulia mlango" Vin aliongea haraka haraka,

"upo chumba kipi?" Strategic aliuliza,

"chumba cha mzee" Vin alijibu,

"hapo siwezi kukusaidia, maana yeye yupo sebuleni na huwezi kwenda chumbani kwake bila kupitia sebule" Strategic alijibu,

"basi naomba unisaidie kitu, nenda kwa Dokta Malle na umuwahi Trigger, ameenda kufanya mauaji, nilimpigia simu Sarah ila sijajua kama amefanikisha au vipi? Kwa maana hapokei simu zangu" Vin aliongea haraka haraka,

"sawa nitawahi, sasa kwanini mzee amekufungia ndani?" Strategic aliuliza,

"tutaongea baadae, wewe nenda kwanza, mimi najua mzee atafungua tu mlango baadae" Vin aliongea,

"poa" Strategic aliongea na kukata simu, kisha akawasha gari na kuiondoa kwa kasi.

***********************

Sarah baada ya kuachwa na Aisha, alimgeukia Trigger na kumuangalia kwa hasira, Trigger alikuwa amekaa chini huku akiugulia maumivu ya kupigwa risasi za miguuni, hata kutembea hakuweza.

"unajisikiaje?" Sarah alimuuliza Trigger ila Trigger hakujibu kitu, Sarah akamfuata na kuanza kumvuta kuelekea ndani, tena alimshika mguu na kumfanya Trigger asikie maumivu maradufu.

Sarah alimvuta Trigger mpaka eneo la ndani ya nyumba ambayo ilikuwa kama sebule kwa maana kulikuwa na makochi na meza na ukutani kulikuwa na runinga bapa ya kisasa, tena yenye ukubwa wa kiwango cha juu.

Sarah akatafuta kiti cha mbao ambacho kilikuwa eneo pembeni na sebuleni, alikikuta kikiwa na viti vingine vingi vya mbao vilivyoizunguka meza moja kubwa, Sarah akatambua ile ni sehemu ya kupata chakula. Sarah akakivuta kile kiti na kurudi nacho sebuleni, kisha akamchukua Trigger na kumkalisha juu ya kile kiti, alafu akaenda kwenye chumba ambacho alishawahi kutekewa,. Akaingia katika kile chumba na kurudi na kamba, kisha akaanza kumfunga Trigger kwa kumuambatanisha na kile kiti cha mbao,

"unataka kunifanyaje?" Trigger aliuliza huku akicheka kwa dharau, Sarah hakujibu kitu, alitabasamu tu.

Baada ya Sarah kumaliza kumfunga Trigger, Sarah alitoka mpaka nje ya nyumba huku akiwa amebeba ndoo na mpira wa maji mfupi, Sarah alitoka na kwenda kwenye gari alilokuja nalo Trigger, kisha akafungua tank la mafuta na kuingiza ule mpira kwenye tank kisha upande wa pili akauingiza mdomoni kwake na kuvuta mafuta, kisha akauelekezea mpira katika ndoo aliyoenda nayo, mafuta yakawa yanatoka kwenye tank na kujaa kwenye ndoo.

Sarah aliporidhika na kiwango cha mafuta, alifunga tank na kuondoka na ndoo mpaka sehemu alipomuacha Trigger,

"Mimi nadhani tuitimishe, maana tumewindana sana na leo mwenye bahati kabahatika" Sarah aliongea huku akimuangalia Trigger,

"unataka kunichoma moto?" Trigger aliuliza huku akicheka,

"ukiishi kwa upanga utakufa kwa upanga, malipo ni hapa hapa duniani" Sarah aliongea huku akimmiminia mafuta Trigger na kisha mafuta mengine akayamwaga eneo lililomzunguka Trigger, eneo ambalo hakuweka mafuta ni mlangoni tu,

"una lolote la kunishauri au kunisifia?" Sarah aliuliza huku akitabasamu, Trigger akainua kichwa na kumtazama, macho ya Trigger yalikuwa mekundu sana,

"kama nimeshindwa kukuua mimi, Vin atakuua" Trigger aliongea kwa uchungu huku machozi yakimtoka, Sarah akatabasamu na kuamini ni maneno ya mkosaji, Sarah akanyoosha bastola yake kwenye eneo lenye mafuta, alitaka kulipua sasa, simu yake ikaita, ilikuwa ni namba ya Aisha,

"vipi?" Sarah aliongea baada ya kupokea simu,

"upo wapi?" Aisha aliuliza,

"kwani wewe upo wapi?" Sarah nae akauliza,

"nipo njiani nakufuata hapo kambini kwa Taita" Aisha aliongea,

"sipo, nimeshaondoka, nimeenda nyumbani kupumzika" Sarah alidanganya, hakutaka mtu yoyote aende eneo hilo,

"sasa huyu afande nimfanyaje?" Aisha aliuliza,

"usimuachie, nitakutafuta baadae" Sarah aliongea,

"poa" Aisha alijibu kisha akageuza gari na kurudi alipomuacha Sajenti Minja.

Sarah akakata simu, kisha akaelekeza bastola sehemu yenye mafuta na kufyatua risasi, mafuta yakashika moto na kuanza kutembea kumuelekea Trigger, Trigger akatabasamu,

"siku zangu za mwisho zimekuwa za taabu sana, wewe mtoto umekuja kuharibu kila kitu" Trigger aliongea huku akicheka na moto ulikuwa umeshamfikia ukamvaa na Trigger akaanza kupiga kelele na pia nyumba yote ikashika moto.

**************

Strategic alienda mpaka kwa Dokta Malle, akamkosa Trigger, hata Dokta mwenyewe hakumkuta.

Strategic akatoka mpaka kambini kwao, alipofika getini alishangaa kuona nyumba nzima ikiwa imeshika moto, strategic akataka atelemke, ila akili yake ikamwambia hata akishuka kwa moto ule hawezi kuokoa kitu chochote.

Strategic akachukua simu yake ili ampigie Taita na kumpa taharifa juu ya moto huo, lakini bahati mbaya simu yake ilizimika kwa maana iliisha chaji. Strategic akaondoa gari ili kwenda kutoa taharifa kwa Taita juu ya moto huo.

*************

Ndani ya nyumba, Sarah alikuwa amesimama pembeni akimuangalia Trigger namna anavyoungua na jinsi anavyojitahidi kuupigania uhai wake. Moto ukazidi kushika kasi mpaka poa la nyumba likaanza kutoa sauti kama linaachia, Sarah akaona bora aondoke, aliamini Trigger hawezi kupona kwa ule moto.



Sarah akageuka nyuma ili aondoke, ila kutokana na ule moto kumuunguza Trigger kwa kiasi kikubwa, kamba alizofungwa zilikuwa zimeungua na kuisha, sasa wakati Sarah amegeuka aondoke, Trigger akamshika Sarah mguu na kuuvuta kumzuia asiondoke ili wote waungue, Sarah akageuka ili ammalize Trigger na risasi, ila mbao moja kutoka juu ya paa ikaachia na kudondoka, ikamuangukia Sarah kichwani, Sarah akadondoka na kupoteza fahamu, na muda huo moto ulishazunguka nyumba nzima na paa zikiwa zinaanguka tu, yaani nyumba ilikuwa inajifunika.

Sarah alivyopoteza fahamu, Trigger akaanza kujivuta kwa mikono, alitambaa mpaka akafikia bastola ya Sarah, kisha Trigger akajivuta mpaka mpaka kwenye ndoo ya maji na kuibeba kisha akajimwagia maji kwa maana moto ulikuwa bado unawaka, sasa Trigger alipata ahueni baada ya moto kuzimika, akaifungua bastola na kuona ina risasi za kutosha, akaifunga na kumuelekezea Sarah kichwani, Trigger akatabasamu,

"bora tufe wote" Trigger aliongea huku akitabasamu, moto ulikuwa umemuunguza vibaya sana, mwili mzima........................

***********ITAENDELEA***********

the Legend☆
 
RIWAYA : SALA YA SARAH

MTUNZI : ALEX KILEO

SEHEMU YA SITINI NA NANE.

ENDELEA..................

Sarah alivyopoteza fahamu, Trigger akaanza kujivuta kwa mikono, alitambaa mpaka akafikia bastola ya Sarah, kisha Trigger akajivuta mpaka mpaka kwenye ndoo ya maji na kuibeba kisha akajimwagia maji kwa maana moto ulikuwa bado unawaka, sasa Trigger alipata ahueni baada ya moto kuzimika, akaifungua bastola na kuona ina risasi za kutosha, akaifunga na kumuelekezea Sarah kichwani, Trigger akatabasamu,

"bora tufe wote" Trigger aliongea huku akitabasamu, moto ulikuwa umemuunguza vibaya sana, mwili mzima, Trigger akaacha ghafla kutabasamu, machozi yakaanza kumtoka, akalia kwa uchungu, akageukia ndoo ya maji na kuibeba, akammwagia maji Sarah, Sarah akakurupuka na kumkuta Trigger akiwa ameshika ndoo ya maji na bastola. Sarah baada ya kuzinduka na kumkuta Trigger katika hali ile, akajua kabisa Trigger amemmwagia maji ili amzindue.

Trigger akawa anamuangalia Sarah huku machozi yakimtoka na pua bastola akiwa amemnyooshea Sarah, Trigger akaigeuza bastola na kumrushia Sarah,

"toka nje, hii nyumba inaanguka sasa hivi" Trigger aliongea huku akilia na kumfanya Sarah ashangae huo wema wa Trigger,

"Sarah toka nje, nenda nje ujiokoe uende ukatimize ndoto zako" Trigger aliongea huku akilia, hapo huruma ikamuingia Sarah, akasimama huku machozi yakimtoka, alimuonea huruma Trigger kwa namna moto ulivyomfanya, aliungua vibaya, hakuweza kutazamika mara mbili.

"twende nje, nitakusaidia kutoka" Sarah aliongea kwa upole huku akilia,

"hata nikitoka sitoweza kukaa muda mrefu, ni lazima nitakufa tu" Trigger aliongea kwa huruma,

"hapana usiseme hivyo, nimekusamehe kwa kila baya ulilonifanyia, nakuomba tutoke nje" Sarah aliongea,

"Sarah toka nje, hichi kifo ni haki yangu, wala sitokulaumu" Trigger aliongea kwa hasira huku akimuangalia Sarah,

"usiseme hivyo, twende nje" Sarah aliongea,

"hapana, Sarah nenda mama, leo nilikuwa na uwezo wa kukuua, ila sikutaka kufanya hivyo, nilitaka ukakamilishe matakwa yako, pia nilitaka nikuoneshe upande wangu wa pili, mimi ni mzazi na nina mtoto ambaye nampenda sana, hajui wala hawezi kukubali mimi ni mtu mbaya kutokana na jinsi ninavyoishi nae, sasa leo ule upendo nimehamishia kwako" Trigger aliongea kwa huzuni huku akilia na kumfanya Sarah azidi kulia zaidi.

"bado una nafasi ya kuishi, usikate tamaa" Sarah aliongea kwa huzuni,

"nafasi ambayo unaona ninayo, naomba niitupe, sitaki kuishi nikiwa katika hali hii" Trigger aliongea kisha akachukua ile ndoo ambayo Sarah alikuwa ameweka petrol, Trigger akajimwagia petrol kisha akaokota kipande cha mbao kilichokuwa na moto na kugusisha katika mwili wake na hapo moto ukamshika tena, Sarah akaanza kulia kwa sauti huku akimtazama Trigger aliyekuwa ametulia huku moto ukazidi kummaliza. Sarah akamnyooshea Trigger bastola na kumlenga kichwa, kisha akaruhusu risasi itoke, risasi ikatua kwenye kichwa cha Trigger na kummaliza pale pale, Sarah hakutaka Trigger ateseke zaidi, alimuonea huruma.

Na hiyo ndiyo ikawa safari ya mwisho ya Trigger, Sarah alipata hofu sana kila akiuangalia mwili wa Trigger, akakiri kifo cha moto ni kifo kibaya sana, akavuta picha namna wazazi wake walivyokuwa wanaungua, akajikuta machozi yanazidi kumtoka.

Nyumba ilizidi kuungua, Sarah akageuka nyuma na kugundua hata mlango anaotakiwa kupitia tayari wote umeshika moto, hakuna njia tena, na moto ulizidi kupamba katika kile chumba, Sarah akaiendea ndoo ya maji na kubeba, kisha akamwaga maji mlangoni na kufanya moto upungue kidogo, alafu maji mengine akajimwagia mwilini kisha kwa kasi ya ajabu alipita kwenye ule moto na kuelekea nje, alipotoka ndani ya nyumba fulana yake ilichanwa ilikuwa imeanza kushika moto, akaivua na kuitupa, sasa mtihani mwingine uliomkabili ni kutoka nje akiwa kifua wazi ilihali yeye ni binti.

"potelea mbali" Sarah aliongea kisha akawa anaelekea upande wa mbele kwenye geti, alitembea mpaka getini na kumkuta yule kijana mlinzi wa getini akiwa amelala, hakuwa na fahamu kutoka muda ule alivyopigwa na Aisha.

Sarah akamuinamia yule kijana na kumvua fulana, kisha akaivaa yeye. Sarah akataka kufungua geti ili atoke nje, ila alisikia sauti za watu zikiokea nje, na walionekana ni watu wengi, walikuwa ni majirani na wapita njia, walijaa nje ya nyumba ya kambi ya Taita wakishuhudia nyumba ikiteketea.

Sarah akaamua ahairishe mpango wa kutokea getini, akaona bora atumie njia aliyotumia kuingilia. Sarah akaenda nyuma ya nyumba na na kuukwea ukuta, kisha akaangukia upande wa nyuma ambapo kuna nyumba nyingine, lakini ilionekana hakuna mtu anayeishi katika hiyo nyumba.

Sarah akasogea karibu na bomba lililokuwepo katika nyumba hiyo na kujaribu kufungulia maji, yakatoka.

Sarah akaanza kunawa uso wake na sehemu ambazo alihisi ni chafu kutokana na moto aliopambana nao ndani, kisha akaenda mpaka kwenye geti la hiyo nyumba na kujaribu kufungua, akagundua limefungwa, Sarah akarudi nyuma kisha akalifuata lile geti kwa kasi, alipokaribia umbali wa hatua mbili, Sarah aliruka na kulikamata lile geti kwa juu, kisha akajivuta na kuangukia nje, alipotua chini akatupia macho kwenye kambi ya Taita na kuona namna watu walivyojaa wakishuhudia jinsi nyumba inavyoteketea kwa moto.

Sarah hakutaka kusogea, akaenda zake upande wa kushoto na ile nyumba ikawa ameipa mgongo. Sarah alitembea kwa mwendo wa dakika mbili akapishana na zimamoto, lilikuwa linaelekea upande ambao Sarah ametokea.

Baada ya kutembea kwa muda Sarah akatoa simu na kuangalia namba anayoitaka, kisha akapiga na simu ikaanza kuita,

"Aisha upo wapi?" Sarah aliuliza baada ya mtu wa upande wa pili kupokea simu,

"nipo sehemu moja hivi huku uswazi" Aisha alijibu,

"upo na huyo afande?" Sarah aliuliza,

"nipo nae" Aisha alijibu,

"muachie, angalia namna nzuri ya kumuachia ili asikugeuzie kibao" Sarah alimwambia Aisha,

"kwanini nimuachie? Huna mpango nae?" Aisha aliuliza,

"sina tatizo nae, nilitaka umshike ili nimalizane na Trigger kwanza" Sarah alijibu,

"kwa hiyo Trigger umemalizana nae?" Aisha aliuliza,

"tayari" Sarah alijibu,

"poa" Aisha alikata simu na kumgeukia Sajenti Minja ambaye alikuwa akiyafuatilia maongezi yao,

"vipi?" Sajenti Minja aliuliza kwa wasiwasi baada ya kuona Aisha akimuangalia sana,

"nataka nikuachie" Aisha aliongea huku akimsogelea Sajenti Minja,

"sawa, ni jambo jema" Sajenti Minja aliongea huku akifurahi,

"ila siwezi kukuachia kienyeji, nakujua wewe ni polisi, endapo nitakuachia kienyeji unaweza kunigeuka" Aisha alimtahadharisha Sajenti Minja,

"sasa unataka uniachiaje?" Sajenti Minja aliuliza kwa wasiwasi, ila Aisha hakujibu, badala yake alimpiga Sajenti Minja ngumi nyepesi iliyotua katika shingo na kumfanya Sajenti Minja apoteze fahamu, kisha Aisha akamfungua na na kuanza kumvuta kumpeleka nje, alimvuta na kumuweka kwenye gari, kisha akaondoka nae na kwenda kumtupa mahali anapopajua yeye.

**********************

Strategic alikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Taita, akaegesha gari kwa nje kisha akashuka na kuingia ndani moja kwa moja,

"mbona nakupigia siku hupatikani wewe?" Taita aliuliza kwa hasira,

"simu ilizimika" Strategic alijibu kwa uoga,

"Trigger umemkuta?" Taita aliuliza,

"kwa Dokta Malle sijamkuta Trigger, ila pia nimeenda kambini pia sijajua kama yupo" Strategic alijibu,

"sasa hujajua kama yupo kwani hukuingia ndani?" Taita aliuliza,

"sijaingia, nimekuta ile nyumba inaungua, tena moto mbaya ulikuwa unawaka" Strategic alijibu na kumfanya Taita ashtuke,

"sasa si ungeingia ili ujue ndani kuna nini?" Taita aliuliza kwa hamaki,

"kwa jinsi nyumba ilivyokuwa imeisha, ndani hakuwezi kubaki kitu, kwa hiyo sikuwa na sababu ya kuingia" Strategic alijibu,

"ebu twende" Taita aliongea huku akisimama na kuelekea nje na kumfanya Strategic amfuate kwa nyuma.

Taita alitembea na kutoka nje ya geti na kumpita mlinzi wa getini aliyekuwa amesimama kwa wasiwasi, alimuogopa sana Taita,

"usiruhusu mtu aingie humu, ila Trigger peke yake" Taita alimwambia mlinzi wa getini,

"sawa bosi" Mlinzi alijibu kwa ukakamavu na kumfanya Strategic acheke chini chini, Taita akaenda nje na sasa Strategic alikuwa amemfikia mlinzi,

"nenda kamfungulie Vin, yupo katika chumba cha mzee" Strategic aliongea kwa sauti ndogo na kumfanya mlinzi ashangae,

"Mimi siruhusiwi kutoka getini" Mlinzi alijibu Kaa sauti ndogo pia, strategic akatoa noti ya elfu kumi na kumrushia mlinzi,

"unataka miujiza kama iendelee?" Strategic alimuuliza mlinzi na mlinzi akaitikia kwa kichwa kukubsliana nae,

"kafanye nilichokwambia, hakika utashuhudia muujiza huu wa pesa ukiendelea kukutembelea" Strategic aliongea huku akiondoa na kumuacha mlinzi akiokota ile elfu kumi aliyotupiwa.

Strategic akaelekea mpaka nje na kumkuta Trigger ameshaingia kwenye gari, strategic akawasha na kuindoa kwa kasi.

Haikuwachukua muda mrefu sana kufika eneo la tukio, walikuta watu wengi wakiwa wamejaa nje ya nyumba na zaidi zimamoto walikuwa wakiendelea na kazi yao ya kuzima moto.

Trigger alitelemka kwenye gari na kutaka kuingia moja kwa moja getini, ila askari waliokuwepo walimzuia,

"mnanizuia kuingia kwenye nyumba yangu?" Taita aliuliza kwa hasira na pia baadhi ya majirani walikuwa wakiwapigia kelele polisi wakimtambulisha Taita ndiye mwenye hiyo nyumba,

"hatujakuzuia, ngoja zimamoto waruhusu, si unaona mzee bado wanaangaika kuzima?" Askari mmoja alimueleza Taita,

"wakati najenga sikupangiwa, iweje mnipangie muda wa kuingia?" Taita alihoji kwa hasira,

"muachieni apite" Sauti ya askari mmoja wa zimamoto iliongea na kufanya askari wa pale getini wamruhusu Taita aingie. Taita alipita ndani ya geti na kukuta moto umeshazimwa ila bado kuna baadhi ya sehemu kulikuwa na moshi mzito,

"hakuna mtu ndani?" Taita aliuliza,

"hatujui kwa maana bado hatujakagua, moto ukipoa tutaangalia" Askari wa zimamoto alijibu na kumfanya Taita aanze kuzunguka zunguka huku akiwa na wasiwasi.

Baada ya nzima moto ulikuwa umepoa kabisa, askari wa zimamoto kwa kushirikiana na wananchi wakaanza kutoa poa lililoangukia ndani na kuangalia kama kuna watu waliongua.

Baada ya muda mchache waliweza kuupata mwili wa Trigger, ila hakuna mtu aliyeutambua kutokana na kuharibika vibaya, hata Taita mwenyewe hakuweza kuujua.

"sasa kama wewe mwenye nyumba umeshindwa kumtambua marehemu, au kulikuwa na watu wangapi wanaishi humu?" Askari mmoja aliuliza,

"ni mlinzi tu pekee, tena mmeniambia mmemkuta getini akiwa hana fahamu. Sasa huyo mlinzi ndio anaujua ukweli" Taita aliongea kwa hasira,

"sawa, nadhani sisi tumemaliza kazi yetu" Askari wa zimamoto aliongea na kuwahimiza wenzake waondoke na kumuacha Taita akiwa amesimama akiiangalia nyumba yake.

,

"huu mwili unaweza kuwa wa Trigger kweli?, ila Trigger hawezi kufa kizembe" Taita alijiuliza huku akitoka nje, akaingia kwenye gari na kumuamuru Strategic aelekee hospitali ambayo mlinzi wa getini alipelekwa.

***********ITAENDELEA************

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom