the_legend
JF-Expert Member
- Jan 14, 2019
- 1,612
- 7,112
- Thread starter
- #701





the Legend☆





41RIWAYA : SALA YA SARAH
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA
ILIPOISHIA.................
Akiwa amekata tamaa kabisa, Sarah alifungua chumba cha mwisho, alikuta kipo giza ila alihisi kuna mtu anahema kwa nguvu sana, Sarah akapapasa ukutani ili atafute switch ya taa, hakuiona, akaamua kufuata sauti ya mihemo inapotokea, ghafla akamulikwa usoni na tochi yenye mwanga mkali, kisha taa ya chumba kile ikawashwa, alishangaa kumkuta Trigger juu ya kile kiti, yeye ndio aliutengeneza mtego ule wa kumnasa Sarah,
"karibu himayani malaya mtoto" Trigger aliongea huku amekamata bastola yake mkononi, Sarah akataka kurudi mlangoni ili akimbie, ghafla mlangoni akatokea Harry huku nyuma yake akiwa Tekso na Strategic na wote walikuwa na silaha nzito za kivita,
"jisalimishe" Harry aliongea huku akisimama na pia akitoa tabasamu la ushindi. Sarah akazungusha macho kama mtu anayefanya tathmini, ila aliona hawezi kufua dafu mbele ya wanaume wale wenye silaha nzito, Sarah akatoa silaha zake zote na kuzitupa chini, akapiga magoti na Mikono akaiweka juu, Sarah alisalimu amri ingawa hukupenda, aliamua akubaliane na matokeo bila kujua kuwa huenda mwisho wake umekaribia......................
**********ENDELEA***********
"mfunge kamba malaya huyu" Harry aliongea kisha Trigger akanyanyuka na kuchukua kamba na kumsogelea Sarah,
"weka mikono nyuma malaya wewe" Trigger aliongea huku akiivuta mikono ya Sarah kwa nyuma, kisha akamfunga kamba mikononi na kisha akamsukuma kwa mbele, Sarah akaangukia tumbo, kisha Trigger akaishika miguu ya Sarah na kuifunga kwa kamba, sasa rasmi Sarah akawa mateka wa vijana wa Taita.
"katundikeni kwenye chumba cha mateso" Harry aliamrisha kisha Trigger na Tekso wakamkamata Sarah mkono wa kushoto na Tekso alikuwa upande wa kulia wa Sarah , wakaanza kumpeleka, walifika sehemu katika eneo la sebuleni na kuondoa meza, kisha wakakuta kuna mfuniko kama wa chemba, wakauvuta na kumfanya kuuweka pembeni, kisha wakaingia kwa kutumia ngazi wakaanza kushuka chini, muda wote Sarah alikuwa akishangaa namna hiyo sehemu ilivyojificha.
Walipofika chini walikuta korido ndefu, wakaanza kuifuata mpaka katika mlango mmoja uliokuwa na kufuri nzito, Trigger akatoa funguo na kufungua ile kufuri, kisha wakamuingiza Sarah ndani, Kisha wakamfunga katikati ya chumba ambapo sehemu ya juu kulikuwa na vyuma vinaning'inia, wakaifunga mikono ya Sarah juu katika vile vyuma na miguu yake ikabaki ikining'inia, yaani haikufika chini,
"sasa leo nataka unijibu maswali yangu machache" Harry aliongea huku akivuta kiti na kukaa, ila Sarah hakuonesha kuogopa, alitabasamu tu,
"kwanini unataka kutuua?" Harry aliuliza,
"kuwaua? Kama ningetaka kuwaua basi wewe ningeshakuua zamani, bado sijataka kuwaua, bado nangoja nyie mtake kufa wenyewe" Sarah alijibu huku akitabasamu,
"lini sasa wakati wewe hapo ulipo ndio mwisho wako" Trigger aliongea kwa kejeli huku akicheka,
"hakuna anaejua mwisho wangu, na wala huu hautakuwa mwisho wangu" Sarah alijibu kijeuri,
"mpumbavu wewe upo kwetu bado unatujibu jeuri?" Trigger aliongea huku akimrushia Sarah ngumi kali iliyotua kwenye mdomo wa Sarah na kumfanya Sarah ageuze shingo na kutema damu,
"nadhani wewe ni mzuri sana kwenye matumizi ya silaha, ila kwenye matumizi ya ngumi hauna kitu, nimelithibitisha hilo, ngumi yako ni nyepesi sana, kama ya binti wa miaka kumi na mitano" Sarah aliongea huku akitoa kicheko kikubwa cha dharau,
"mpuuzi wewe, leo nitakuua, nitakuua kwa mkono wangu" Trigger aliongea na kumrushia Sarah ngumi mbili zilizomfikia usoni na nyingine ikatua kwenye pua ya Sarah, damu ikawa inamchuruzika Sarah kwenye pua yake,
"hizo ngumi zote zingekuwa ni za mwanaume aliyekamilika, nadhani ningekuwa nimepoteza fahamu au ningekuwa nimeshakufa" Sarah aliongea, ila safari hii hakua akicheka tena, alikuwa akisikitika huku akimuangalia kwa jicho la dharau,
"malaya wewe nitakuua" Trigger aliongea kwa hasira huku akijiandaa kurusha ngumi nyingine,
"tulia wewe, huyo anakupa wendawazimu tu, usiangaike kupambana nae, tutakuwa nae muda wote hapa, utampiga utakavyo na utamtafanya utakavyo, hata mkiamua kumbaka kwa zamu mnaweza" Harry aliongea huku akiwa ameushika mkono wa Trigger na kumuacha,
"Harry una akili sana, nadhani wazazi wako waliona mbali na ndio maana wakaweka dhamira mpaka ukafika chuo kikuu na ukabobea kwenye masuala ya sheria, ila ulichobobea haukitendei haki, unaonea wanyonge kwa sababu ya fedha, umegeuzwa mbwa wa mwenye fedha, unatumiwa kinyume na matarajio ya ulichokisomea, umekuwa mtumwa" Sarah aliongea huku akimtazama Harry,
"binti kuna kitu umsaahau, wazazi wangu walinisomesha kwa juhudi na bidii ili nije kuwa na fedha na niwasahidie kipindi wakizeeka, hicho ndicho ninachokifanya, nipo kwa ajili ya kupata pesa, hujakosea kusema ninatumikishwa kwa ajili ya pesa" Harry alijibu kwa umakini huku akiwa amemkazia macho Sarah,
"unatumikishwa kwa pesa, ila siku ya kifo chako itaandikwa umekufa kwa ajili ya haki" Sarah aliongea huku akitabasamu,
"sasa binti sio kila jambo jema nililolifanya napaswa kulitangaza, kuna mambo mema mengi sana nimeyafanya katika upande wa haki, so usinihukumu kwa kuwa sijawahi kufanya jema mbele yako" Harry aliongea huku nae pia akitabasamu,
"je unaweza kunisaidia kitu ili nikuhesabu kuwa ni mmoja kati ya watu wema niliowahi kukutana nao?" Sarah aliuliza,
"nikusaidie nini?" Harry aliuliza,
"naomba uwe shahidi au uwe mwanasheria wangu katika kesi nitakayoifungua dhidi ya vifo vya wazazi wangu" Sarah aliongea huku akimuangalia Harry,
"utafungua lini sasa wakati huu ndio mwisho wako?" Trigger aliuliza kwa dharau huku akicheka,
"wewe huwezi ujua mwisho wangu kama mwanzo wangu hukuwahi kuujua" Sarah alijibu kwa sauti ya utulivu,
.
"kama ukiweza kutoka hapo, nitakusaidia" Harry alijibu huku akinyanyuka na kuondoka zake, aliamini kabisa Sarah hana ujanja tena wa kutoka pale alipo, na pia aliamini katika ule mchakato wake wa kumuua Sarah ili abakie na amani.
Huku ndani Trigger aliendelea kutamba mbele ya Sarah,
"Mimi usiku nitakupiga tu mpaka nichoke, sina sababu ya kukupiga, nakupiga kufurahisha nafsi" Trigger aliongea huku akiokota mnyonyoro uliokuwa unazagaa sakafuni,
"ukiamua kunipiga, nipige mpaka nife, ukiniacha hai ama ukanivunja kila kiungo changu ila ukaniacha nikipumua, huo utakuwa muendelezo wa makosa yako dhidi yangu, kama tutakutana tena, ndio itakuwa tamati yetu, mmoja lazima afe" Sarah aliongea kwa kujiamini,
"wewe maliza maneno yote, mimi siongei tena, leo nakupiga tu, kesho ndio nitakuuliza maswali" Trigger aliongea kisha akawaruhusu Tekso na Strategic waondoke, akabaki yeye na Sarah, Trigger akamuondoa fulana Sarah na kumuacha mgongo wazi, akaanza kumtandika kwa kutumia ule mnyonyoro, alimtandika sana, Sarah alilia mpaka sauti ikamkauka, mwisho akalegea, macho yakajaa giza na baada ya hapo ubongo haukuwa na mawasiliano tena na dunia, Sarah alilegeza shingo na kufunga macho, lakini Trigger aliendelea kumpiga tu, mpaka aliporidhika, akazima taa ya kile chumba na Kutoka zake kifua mbele, leo alimkamata mwizi wake baada ya arobaini nyingi zisizo na idadi.
***************.
Asubuhi ya leo Sajenti Minja aliamkia hospitali, wakati yupo njiani akielekea hospitali, njiani habari ilikuwa ni kuibwa mgonjwa katika hospitali kubwa na yenye hadhi, magazeti yote na radio zilikuwa ni habari hizo hizo na kila mtu mtaani alikuwa anaongea lake, wapo waliolaani hicho kitendo na wapo pia walituhumu uzembe wa watu wa usalama wa hospitali na wapo wengine waliomlaumu mgonjwa.
Njia nzima Sajenti Minja mawazo yake yalikuwa ni kuwaza hilo tukio, huku akijaribu kutengeneza picha namna hao watu wakiingia hospitali na kufanya uharifu huo.
Sajenti Minja akafika eneo la hospital na kuomba kuonana na mkurugenzi wa hospitali, akaruhusiwa,
"kama nilivyojitambulisha hapo hawali, mimi ni askari na huyo mgonjwa aliyechukuliwa alikuwa na kesi ambayo nilikuwa naipeleleza mimi, kwa hiyo basi, ningependa kuona camera za matukio yote ya jana usiku" Sajenti Minja alizungumza kwa utulivu,
"hakuna shida mkuu, twende chumba cha usalama" Mkurugenzi wa hospitali aliongea huku akisimama na kutangulia kutoka nje huku Sajenti Minja akimfuata kwa nyuma. Safari yao iliishia kwenye mlango mmoja ulioandikwa "security room", mkurugenzi akagonga mlango na ukafunguliwa na kijana mmoja aliyevaa sare za rangi ya blue tupu na kiatu cheusi,
"karibu mkurugenzi" kijana aliongea huku akiwa amesimama mlangoni,
"huyu ni askari mpelelezi, ana kitu anataka kuangalia kwenye record za jana" Mkurugenzi aliongea,
"karibu, pita ndani" Kijana aliongea huku akiacha njia Sajenti Minja apite,
"sasa mimi acha nikuache, nimekufikisha sehemu husika" Mkurugenzi aliongea huku akimpa mkono Sajenti Minja,
"shukran mkurugenzi, nitakuona nikitoka hapa" Sajenti Minja aliongea huku akitabasamu, kisha akaingia ndani na kuoneshwa sehemu ya kukaa, alikaa pembeni ya yule kijana,
"jana usiku ulikuwepo?" Sajenti Minja alimuuliza yule kijana,
"nilikuwepo toka jana mchana" kijana alijibu,
"ok, ebu weka camera ya wodi namba tano kisha uirudishe mpaka Nyakati za jana usiku wakati wa tukio" Sajenti Minja alimwambia yule kijana, yule kijana akairudisha ile camera mpaka muda huo, lakini walionekana wale wageni wa hawali tu waliongia kumuona Dokta Pendo, baada ya hapo camera zikakata mawasiliano,
"huyu aliefanya hili tukio huenda ni mtaalam sana au anayajua mazingira yote ya hapa" Sajenti Minja aliongea huku akisikitika,
"na hata nilipoangalia camera za nje pia sikumuona, nazo zilikuwa zinakata kama hivyo" Kijana aliongea huku akimuwekea Sajenti Minja nae ajionee,
"nashukuru mista, nitarudi tena endapo kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo" Sajenti Minja aliongea huku akisimama na Kuondoka zake, aliweza kupishana na baadhi ya waandishi wa habari wakiwa wapo bize kuhoji wafanyakazi wa hospitali ile.
Sajenti Minja alienda mpaka kwenye gari lake na kuingia, kisha akatoa simu na kumpigia Sarah, simu haikuita, akajaribu tena kupiga namba za Dokta Pendo, pia simu haikuwa hewani, Sajenti Minja akaenda zake ofisini kuendelea na kazi zake.
************************
Dokta Pendo alifungua macho saa mbili asubuhi, hakumkuta Sarah pembeni yake, akadhani huenda yupo jikoni anapika.
Saa tatu asubuhi ikafika lakini hakuona dalili zozote za Sarah kuwepo, akahisi huenda ameenda sokoni.
Saa nne ilipofika hakuona uwepo wa Sarah, Dokta Pendo akajiuliza hata kama sokoni, hilo soko lipo umbali gani? Dokta Pendo akatoa mawazo ya Sarah kuwepo sokoni, akaweka mawazo huenda Sarah ameenda kazini na labda atarudi mchana, akawaza sasa kwanini amshindishe na njaa?
"huyu mwanamke alaaniwe, kwanini anitese hivi??? Si bora angeniacha hospitali?" Dokta Pendo aliongea peke yake huku njaa ikimtafuna, tena kwa kwa kasi ya ajabu.
Mwishowe ikafika saa kumi, Dokta Pendo akaanza kutukana matusi yote makubwa kumuelekea Sarah, kibaya zaidi Dokta Pendo alianza kunyong'onyea kutokana na njaa na pia alikuwa amemeza dawa kali zilizopo kwenye droo ya kitanda pembeni yake. Njaa iliendelea kumuuma na kunyanyuka alikuwa hawezi, akaanza kupiga kelele ili hata mtu akipita amsikie, lakini haikuwezekana kwa sababu nyumba ya Sarah ilijitenga sana, akaamua anywe maji yote yaliyokuwa kwenye chupa pembeni yake.
Saa mbili usiku ikamkuta Dokta Pendo yupo Hoi kitandani, taabani, alichokuwa anakifanya ni kumuomba Mungu huku akilaani kitendo hicho anachofanyiwa na Sarah, kitu ambacho hakukijua ni kuwa muda huo Sarah alikuwa kwenye hali hatari zaidi yake, japo Sarah alikuwa kwenye hatari na akiwa katika hali mbaya kiafya, bado alimuomba Mungu amsaidie Dokta Pendo jambo lolote baya lisimpate.
*****************
Wakati Sarah na dokta Pendo wakiwa katika hali hizo tete, Sajenti Minja mawazo yalikuwa yameaongezeka zaidi baada ya kufokewa na mkuu wake kama mtoto mdogo, alionekana ni mzembe aliyeshindwa kuifanya kazi yake kwa weledi.
Mida hii ya saa tatu usiku, Sajenti Minja alikuwa anajiona ni mtu mwenye hatia sana, aliona jambo lolote baya litalomkuta Dokta Pendo, basi yeye atahusika kwa namna moja au nyingine hata kama hatokuwa mlengwa wa moja kwa moja.
Na muda huu wa saa tatu usiku, Sajenti Minja alikuwa akielekea nyumbani kwa Sarah baada ya kupata wasiwasi kwa maana tokea asubuhi alikuwa akipiga simu na haikuita, na muda huu simu ya Sarah ikawa haipatikani kabisa, Sajenti Minja alikuwa hayupo kwenye hali nzuri kimawazo, kwanza alipanga kumfanya vibaya mtu yoyote atakayehisiwa na kupatikana na hatia juu ya matatizo ya Dokta Pendo.
Saa tatu unusu Sajenti Minja alikuwa anasimamisha gari yake nje ya nyumba ya Sarah, alikuta geti limefungwa, akataka kuondoka ila roho yake ikakataa, akapiga hesabu na kuamua aingie kwa njia isiyo sahihi, akaruka ukuta na kuingia ndani ya uzio wa nyumba, akaelekea kwenye mlango wa sebuleni, akajaribu kuusukuma mlango ukafunguka, akahisi hatari zaidi, akaingia kwa hatua za kunyata, akakuta sebuleni kuko giza, akawasha taa.
Dokta Pendo akiwa chumbani alisikia mtu akiwasha taa, akashukuru Mungu huku akiamini Sarah amerudi, akapanga kumnunia, tena mnuno wa kimataifa.
Sebuleni Sajenti Minja akakuta vitu vyote vipo kwenye utaratibu mzuri, akafungua droo na kuikuta simu ya Sarah,
"atakuwa ameenda kazini amemsahau simu" Sajenti Minja aliongea kwa sauti ya kawaida huku akiifunga droo, akazungusha macho kushoto na kulia, akazima taa akawa anaelekea mlango wa kumtoa sebuleni.
Dokta Pendo aliweza kusikia yote hayo, aliweza kuisikia mpaka sauti ya Sajenti Minja akaitambua, akaona huo ndio wakati wake wa kuwa huru na kutoka mikononi kwa Sarah, aliamua kuwa muwazi kwa Sajenti Minja.
ila kilichomtisha Dokta Pendo ni kuhisi kama Sajenti Minja anataka kuondoka, Dokta Pendo akavuta pumzi ndefu na kupiga kelele kubwa za kutaka msaada................
**********ITAENDELEA*************
the Legend☆
Kakudanganya Nani?Asante sana the legend.nitammiss Sarah Ana ni remind na peniella ila tofauti ya Sarah sio mtu wa mabwana
Ushaambiwa waliformat memory card yake utotoni so mafile ya wazazi wake ni complete deleted yani hayapo hata kwenye recyle bin!!!Vin hana akili kabisa, yaani MTU kaua wazazi wako halafu kirahisi tu...........ayaaa
Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante kunitag ila mi nishamalizana nayo jikoni!!RIWAYA : SALA YA SARAH
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA SITINI NA TANO.
ENDELEA..................
"weka silaha chini" Sajenti Minja aliongea kwa ukali huku akimuangalia Vin, Vin akaweka silaha chini huku akitabasamu, maana alikamatwa na ushahidi kabisa.
"ongoza mbele" Sajenti Minja aliongea kwa amri na kufanya Vin aanze kupiga hatua huku akiwa bado anatabasamu, tabasamu la mshangao kutokana na tukio lililotokea ghafla. Wakati Vin akitaka kuanza kupiga hatua, Daktari Aliyepigwa risasi alimshika mkono,
"kumbe hajafa?" Vin aliuliza kwa mshangao huku akimuangalia,
"majibu ya vipimo vyako yapo ndani ya ofisi yangu" Daktari aliongea kwa tabu huku akiwa anatoka damu puani na mdomoni,
"Dokta mimi ndiye niliyekupiga risasi?" Vin alimuuliza huku akiwa amemuinamia, Daktari akatingisha kichwa kwa maana ya kukataa, Sajenti Minja akampiga kikumbo Vin na kusogea karibu na Daktari,
"unamjua huyu?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuonesha picha ya Trigger, Daktari akaitikia kwa kichwa kumaanisha anamjua,
"huyu ndiye aliyekupiga risasi mwanzo?" Sajenti Minja aliuliza na Daktari alitingisha kichwa na kujibu ndio,
"ndio huyo huyo amempiga na sasa hivi" Vin aliongea kwa sauti,
.
"eti ni kweli?" Sajenti Minja aliuliza na Daktari akakubali kwa kutikisa kichwa na kumfanya Vin ashukuru Mungu kwa kumuepusha na balaa lile,
"huyo mtu alikuwepo humu?" Sajenti Minja aliuliza tena ila daktari hakujibu tena, mwili ulikakamaa na kisha akatema damu nyingi kwa mkupuo na kukilaza kichwa chake pembeni, kwa maana hiyo daktari alikuwa amekufa,
"sogeeni tutoe huduma" Dokta mwingine aliwapangua wakina Sajenti Minja na kisha akamsogelea yule daktari aliyekufa na kuanza kusikiliza mapigo yake ya moyo, hakutaka kuamini kirahisi kama mwenzake amekufa.
"wewe twende" Sajenti Minja aliongea kibabe huku akimvuta Vin,
"unanipeleka wapi sasa wakati daktari amesema mimi sijampiga risasi?" Vin aliuliza kijeuri,
"wewe twende, una kesi nyingi za kujibu ukiitoa hii ya kumshambulia daktari kwa risasi" Sajenti Minja aliongea na kumsukuma mbele Vin,
"sawa, basi ngoja nipewe majibu yangu, si umemsikia daktari amesema yapo ofisini kwake" Vin aliongea huku akimtazama Sajenti Minja,
"we dada, ebu njoo" Sajenti Minja alimuita dada wa mapokezi,
"abee" Dada wa mapokezi aliitikia baada ya kufika, alikuwa ni lydia,
"ingia kwenye ofisi ya yule daktari aliyepigwa risasi, kuna cheti cha mtu nakihitaji, wewe jina nani?" Sajenti Minja aliongea kisha akamgeukia Vin,
"Vin Denis, kama yatakuwa yapo ndani ya bahasha, basi juu ya bahasha kutakuwa kumeandikwa "DNA TEST, Vin Denis and Sarah isack" Vin aliongea,
"wewe umejuaje yameandikwa hayo yote, kama sio lenu moja kati yako na yule aliyempiga risasi daktari?" Sajenti Minja aliuliza huku akimuangalia Vin,
"mara nyingi hospitali nyingi duniani uwa zinatumia mfumo huo" Vin alijibu,
"wewe kama utayapata majibu au utayakosa uje nje unipe taharifa" Sajenti Minja alimwambia lydia,
"sawa" lydia alijibu huku akielekea ofisini kwa Dokta mkuu kwenda kumuomba ruhusa ya kuingia kwenye ofisi ya daktari aliyepigwa risasi.
Sajenti Minja akatoka na Vin mpaka nje na kumpakia kwenye gari, kisha akawa anamsubiria dada wa mapokezi.
Baada ya dakika kumi na tano dada wa mapokezi aliwafuata na kuwapatia bahasha ya kaki yenye majibu ya vipimo vya Vin, Vin akatabasamu,
"nipe, ni majibu yangu hayo na wala sio yako" Vin aliongea baada ya kumuona Sajenti Minja akiyapokea na kuyaweka pembeni yake. Sajenti Minja hakutaka kujibu kitu, aliwasha gari na kuiondoa.
Walifika mpaka kituo cha polisi, na kisha wakashuka wakawa wanaelekea ndani,
"koplo Rama anaendeleaje?" Sajenti Minja alimuuliza askari aliyekuwepo kaunta, alimuulizia yule askari aliyekanyaga bomu na kupoteza fahamu.
"imebidi apelekwe hospitali, inaonekana presha inamsumbua" Askari aliyeulizwa alijibu na kumfanya Sajenti Minja aelekee ofisini kwake huku akitabasamu.
Sajenti Minja aliingia ofisini kwake na kupanga vitu vizuri kutokana na purukushani ya Bomu feki la Aisha, baada ya hapo akakaa kwenye kiti,
"kuna maswali machache nataka unijibu kwa ufasaha zaidi ili urudi uraiani" Sajenti Minja aliongea huku akimtazama usoni Vin,
"nitajibu ninavyojua, sasa wewe ndio utajua nimejibu kwa ufasaha au lah!" Vin aliongea huku nae pia akimuangalia usoni Sajenti Minja,
"sawa, je unaweza kunionesha kibali cha umiliki wa silaha yako?" Sajenti Minja aliuliza,
"ninavyo vibali, vipo nyumbani" Vin alijibu,
"swali la pili, huyu mtu aliyempiga risasi daktari, jana tu nimemkuta upo nae kwenu, wewe na Taita, kwa maana hiyo ni lazima kuna kitu mnakijua juu ya hilo tukio alilolifanya" Sajenti Minja aliongea,
"nadhani naweza nikawa najua, ila kwa hisia tu" Vin alijibu,
"nieleze unachokijua" Sajenti Minja aliongea,
"ni hayo majibu ya hospitali, nadhani hakutaka niyapate hayo majibu ya hospitali kutokana na sababu nisizozijua" Vin aliongea,
"siku ile kwenye kifo cha familia ya Harry, mlinzi alikuona na wewe ukiingia nyumbani kwa Harry kabla familia ya Harry haijauawa, mimi napenda nikuweke hatihani kutokana na vifo hivyo" Sajenti Minja alimueleza Vin,
"ni kweli nilionekana, ila sikuua mtu" Vin aliongea,
"Sarah ni nani yako?" Sajenti Minja huku akimuangalia,
"Sarah sikuwa namjua wala sikuwahi kumjua, ila inasemekana ni ndugu yangu wa damu" Vin alijibu,
"kwanini useme humjui, alafu useme inasemekana, kwani hamjawahi kukua pamoja?" Sajenti Minja aliuliza,
"bado nasema inasemekana kwa maana inadaiwa wakati mdogo nilifutwa kumbukumbu zangu na nikaanza upya" Vin alijibu,
"hiyo haiwezekani, mtu kufutwa kumbukumbu?" Sajenti Minja alibisha huku akicheka,
"hata mimi iliniwia vigumu kuelewa hilo jambo, ila nilielewa baadae nilipokutana na Daktari aliyefanya hilo jambo" Vin alimueleza Sajenti Minja,
"hilo jambo lilifanyika katika hospitali za hapa nchini?" Sajenti Minja aliuliza,
"ndio, uzuri ni kuwa hata daktari wake bado yupo hai ingawa jambo hilo lilifanyika zamani sana" Vin alijibu
"mwaka gani?" Sajenti Minja aliuliza,
"miaka ishirini iliyopita, inasemekana baada ya nyumba yetu kuchomwa moto na wazazi kufariki" Vin alijibu, na kufanya Sajenti Minja aikumbuke ile report iliyofungwa mara baada ya askari aliyekuwa akiifuatilia ila kesi ya nyumba ya baba yake Sarah kuuawa, ile report iliandikwa miili iliyopatikana imeteketea kwa moto ni mitatu, yaani wa baba yake Sarah, mama yake Sarah na mfanyakazi wa ndani, huku mwili wa mtoto wa kike aitwae Sarah ulikutwa nje ya nyumba, na mwili mmoja wa mtoto wa kiume hakuonekana,
"wewe ni Sebastian?" Sajenti Minja aliuliza,
"Sarah uwa ananiita hivyo, ila mimi naitwa Vin" Vin alijibu na kumfanya Sajenti Minja achukue ile bahasha yenye majibu ya vipimo vya DNA na kuifungua, kisha akaanza kusoma taratibu, ilimchukua dakika tano kuisoma kisha akamtupia jicho Vin,
"ulisema daktari aliyekufuta kumbukumbu yupo, anakaa wapi?" Sajenti Minja aliuliza ila safari kwa upole zaidi na kumfanya Vin ashangae, kisha Vin akamuelekeza Sajenti Minja,
"hivi unajua ugomvi wa Sarah na Taita ni ugomvi wa kisasi baada ya wazazi wa Sarah kuuliwa na Taita?" Sajenti Minja alimuuliza Vin,
"ndio" Vin alijibu,
"utafanyaje ukigundua kuwa Taita sio baba yako ila aliwaua wazazi wako?" Sajenti Minja aliuliza,
"siwezi kufanya kitu, kwa maana siwajui wazazi wangu, Taita ndio mzazi wangu" Vin alijibu,
"sawa, nenda, ila uje kesho ukiwa na nyaraka za umiliki wa silaha uliyonayo" Sajenti Minja aliongea na kumfanya Vin ajisachi, kisha akatoa kitambulisho na kukitupa juu ya meza ya Sajenti Minja, Sajenti Minja akakiokota na kukiangalia, akashtuka,
"nitakutafuta nitapokuhitaji"Sajenti Minja aliongea huku akimrudishia kitambulisho,
"naomba na majibu yangu ya hospitali" Vin aliongea kwa upole kisha Sajenti Minja akaichukua ile bahasha na kumpatia,
"kafungulie nje, nataka kutoka" Sajenti Minja aliongea baada ya kuona Vin anataka kutoa karatasi iliyopo ndani ya bahasha.
Vin akatabasamu na kutoka nje huku Sajenti Minja nae akiwa kwa nyuma yake, Sajenti Minja alipanga kuelekea kwa Dokta Innocent Malle muda huo, alikuwa anataka kwenda kumuhoji kutokana na maelezo ya Vin.
*****************
Trigger alivyotoka hospitali alirudi nyumbani kwa Taita na kumkuta akiwa sebuleni,
"umefanikisha?" Taita alimuuliza Trigger,
"kazi imefanyika, ila Vin yupo hatarini" Trigger aliongea,
"yupo hatarini kivipi?" Taita aliuliza huku akionekana kushtuka,
"wakati nampiga daktari risasi, Vin alikuwa katika chumba cha daktari, na isitoshe polisi walikuwa eneo hilo" Trigger alijibu,
"umekosea sana, je Vin amekuona?" Taita alimuuliza,
"ameniona ndio" Trigger alijibu,
"umekosea Trigger, sasa atakufikiriaje?" Taita aliuliza kwa kulalamika,
"kama kutufikiria vibaya mbona tayari ameshatufikiria vibaya, muda wote wanaongea na Sarah, wanasaliana, unadhani wanaongea nini kama sio kutumaliza, huoni hata Sarah hatusumbuhi siku hizi? itakuwa kuna mipango wanaipanga na ikikamilika watatudhuru" Trigger aliongea,
"Vin hawezi kunifanyia hivyo" Taita aliongea kwa kujiamini,
"ulijua ipo siku hatokuamini wewe kama baba yake na akaamua kwenda kupima ili apate ukweli, usimuamini mtoto asiekuwa wako, maana anakugeuka muda wowote" Trigger aliongea na kumfanya Taita afikiri kidogo,
"basi nitamwambia arudi marekani akaendelee na mambo yake" Taita aliongea,
"mzee Vin ni wa kuuawa tu, maana ukweli ameshaanza kuujua ukweli kuhusu kifo cha wazazi wake" Trigger aliongea,
"siwezi kumuua vin" Taita alijibu huku akitabasamu,
"mzee utakurupuka kukiwa kumekucha, elewa pia jana Vin alikuwa kwa Dokta Malle" Trigger aliongea na kumfanya Taita ashtuke,
"alienda kufanya nini?" Taita aliuliza kwa hofu,
"sijui kilichoongelewa, ila wewe unadhani wataongelea nini kama sio habari zile zile za miaka ishirini iliyopita?" Trigger aliuliza,
"wewe umejuaje Vin alienda kwa Dokta Malle siku iliyopita?" Taita aliuliza,
"nilimfuatilia jana kwa kila hatua, maana hata Strategic nakosa imani nae" Trigger alijibu,
"basi nenda kwa Dokta ukamuohoji Vin alifuata nini pale?" Taita alimuagiza Trigger,
"sawa" Trigger alijibu na kuondoka huku akiwa na hasira.
******************
Sajenti Minja hakupata tabu kuipata nyumba ya Dokta Innocent Malle kwa maana Sajenti Minja aliujua mji vizuri.
Sajenti Minja alifika na kuiegesha gari yake nje ya nyumba ya Dokta Innocent Malle, kisha akabonyeza kengele, baada ya dakika moja yule kijana aliyewapokea wakina Vin siku iliyopita alienda na kufungua geti,
"habari yako? Dokta nimemkuta?" Sajenti Minja aliuliza,
"yupo, karibu" Kijana aliongea huku akiacha nafasi Sajenti Minja apite, Sajenti Minja akaingia ndani ya geti na kumkuta Dokta Innocent Malle akiwa amekaa kwenye viti vya nje akinywa kahawa, Sajenti Minja alimsalimu,
"mzee mimi ni polisi, kuna maswali kidogo naomba unisaidie kujibu" Sajenti Minja aliongea huku akiweka kitambulisho juu ya meza kisha Dokta Innocent Malle akakichukua na kukikagua na mwisho akaridhika kuwa Sajenti Minja ni polisi kweli,
"mimina Kahawa kwanza alafu ndio tuendelee kuulizana" Dokta Innocent Malle aliongea huku akitabasamu, kisha Sajenti Minja akamimina kahawa kwenye kikombe na kugida fundo moja,
"mzee naomba unisaidie kueleza tukio la mtoto aliyeletwa kwako kufutwa kumbukumbu, hilo tukio lilitokea miaka ishirini iliyopita" Sajenti Minja aliuliza na kumuangalia Dokta Innocent Malle,
"kweli mmeamua, jana tu huyo mtoto alikuja hapa kuniuliza, hama kweli ukweli haufichiki, hata uhufiche miaka Mia, ipo siku utajitokeza tu" Dokta Innocent Malle aliongea na kisha akaelezea mkasa mzima ulivyokuwa, hakuficha kitu,
"huyo kijana mweupe mwenye michoro mwilini uliyemtaja kama kijana wa kazi wa Taita, amefanana na huyu?" Sajenti Minja alimuuliza Dokta Innocent Malle huku akimuonesha picha ya Trigger iliyokuwa kwenye simu ya yake,
"ndio huyu haswa, ingawa hapa anaonekana mtu mzima kidogo" Dokta Innocent Malle aliongea huku akiiangalia ile picha,
"hii picha nimeipiga leo, nilikuwa kwa Taita nafuatilia ile kesi yake ya kutekwa na kutupwa" Sajenti Minja aliongea,
"sasa mbona juu ya hiyo picha umeandika muuaji?" Dokta Innocent Malle aliuliza,
"choo kipo wapi, nikitoka chooni nitakujibu hilo swali, hapa haja ndogo imenishika kidogo kutokana na kahawa" Sajenti Minja aliuliza na yule kijana akamuelekeza Sajenti Minja akaelekea chooni.
Kipindi Sajenti Minja akiwa chooni ndicho kipindi ambacho Trigger alikuwa anaingia kwa Dokta Innocent Malle. Trigger aliingia na kukaa kwenye kiti kile kile alichokalia Sajenti Minja, kisha akamsalimia Dokta Innocent Malle,
"bado upo imara, ni muda sana tangu tuonane" Trigger aliongea huku akitabasamu,
"siku mbili hizi mmenikumbuka, jana kaja Vin, leo wewe" Dokta Innocent Malle aliongea huku akitabasamu,
"na kilichonileta ni suala hilo hilo la Vin" Trigger aliongea,
"ebu hama kwenye hicho kiti, kuna kijana mmoja polisi ndio amekaa hapo, ameingia uwani, nae amekuja kwa masuala hayo hayo ya Vin," Dokta Innocent Malle aliongea na kumfanya Trigger ashtuke na kuitupia jicho simu ya Sajenti Minja iliyokuwepo mbele yake na kuiona picha yake ya ikiwa na maandishi " MUUAJI" Trigger akashtuka zaidi,
"yuko wapi polisi mwenyewe?" Trigger aliuliza huku akiibeba simu ya Sajenti Minja,
"ameelekea uko nyuma, chooni" Dokta Innocent Malle alijibu na wakati huo Sajenti Minja alikuwa akirejea, Sajenti Minja alipotokezea akamuona Trigger akiwa ameshika simu yake, Sajenti Minja akashtuka na kusimama, kitendo chake cha kusimama tu ghafla, Trigger akatoa bastola na kumnyooshea,
"kumbe ulivyokuwa pale kwa Taita hukumfuata yeye ila ulinifuata mimi?" Trigger aliuliza huku bastola yake ikimuangalia Sajenti Minja,
"kwanini unasema hivyo?" Sajenti Minja aliuliza huku akiwa anajua kabisa kuwa Trigger ameiona picha yake kwenye simu yake yeye Sajenti Minja, na kipindi hicho Dokta Innocent Malle na mwanaye walikuwa wamepigwa na butwaa huku wakiwa hawajui la kufanya,
"hii picha umenipiga leo maana hata nguo nilizovaa ni hizi hizi, alafu unajifanya ulimfuata Taita" Trigger aliongea huku akionesha ana hasira,
"telemsha bastola basi nikueleze vizuri" Sajenti Minja aliongea huku huku akiweka tabasamu la bandia na kumfanya Trigger pia atabasamu,
"Trigger uwa hashushi silaha mpaka itoe risasi" Trigger aliongea huku akiendelea kutabasamu na kuikoki bastola yake, Sajenti Minja akashtuka,
"una maana gani kusema hivyo?" Sajenti Minja aliuliza huku akitetemeka, ila Trigger hakujibu, akamfyatulia risasi Sajenti Minja, Sajenti Minja akatupwa chini na kunyooka kama mti mkavu, Dokta Innocent Malle na mwanae wakabaki wameshika midomo kwa mshangao,
"hiyo ndio maana yangu" Trigger aliongea huku akimuangalia Dokta Innocent Malle na pia akitabasamu............
***********ITAENDELEA*************
the Legend☆
Pamoja sana mkuuAhsante kunitag ila mi nishamalizana nayo jikoni!!
Asante sana dearTukutane tena usiku kwa episode nyingine, na hatimae kesho asubuhi kwa episodes zitakazobaki. Na hapo tutakua tumefikia mwisho wa Sala ya Sarah. Muwe na jioni njema wakuu
the Legend☆
Duuu sitaki kuamini kama Sarah kafanya hayo mapuuza, asante the LegendKaribu dear
the Legend☆
au ni mimi sijakuelewa mkuu?
the Legend☆
Duh, basi nimechanganya mafaili pale nlivyoona umequote post nliyomjibu Shunie
Duh, basi nimechanganya mafaili pale nlivyoona umequote post nliyomjibu Shunie
the Legend☆