Riwaya: Niacheni nikufuru

Riwaya: Niacheni nikufuru

RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com




SEHEMU YA KUMI NA TATU

Tulipoishia sehemu iliyopita...............

Sikiliza bibie, mume wako 'Johnson' ni muuaji, kwahiyo mimi lengo langu nataka askari polisi wakija kuwahoji kama ni kweli Johnson ana mienendo ya kiuhalifu mujibu ndio, tena wewe ndo inabidi useme kuwa umewahi kumuona mara kwa mara na wale wenzake aliowaua wakijadiliana kwa siri mipango yao kule kwenu, jieleze vizuri ili mukawe mashahidi kule mahakamani. Akishaadhibiwa tu kifungo cha maisha au kunyongwa basi nakufungulia biashara kubwa hapa mjini. Hakuna mwanamke atakayekufikia kwa utajiri Dodoma nzima" Mr. Hassan alizidi kupalilia maneno yake.

"Kama ni hivyo nipo tayari, mi siwezi kumsapoti mwanaume muuaji kama Johnson, kwanza namchukia sana", Jackline alijibu baada ya kusikia maneno matamu kutoka kwa Mr. Hassan.


Sasa tuendelee....................


"Mpango wetu ni huu; kesho kuna askari wa upelelezi watakuja kwenu kuwahoji. Munachotakiwa ninyi ni kukariri hizi sura za waliouawa. Chukueni hii picha yao, nyuma kuna majina ya kila mmoja. Huyu wa kushoto anaitwa Gideon, anayefuata anaitwa Oscar, anayefuata ni Daud na huyo wa mwisho ni Selemani. Kwahiyo ili uweze kuwakumbuka vizuri kariri neno 'GODS'. Yaani G=Gideon, O=Oscar, D=Daud na S=Selemani. Tumeelewana?", Mr. Hassan aliwapa maelekezo Idris na Jackline huku akiwapatia na picha.

"Hapa bado hatujaelewa muheshimiwa. Sisi tunatakiwa tuwaambie nini polisi?", Idris aliuliza.

"Wakija kuwahoji muwaambie kwamba huwa munamuona Johnson mara kwa mara na wale jamaa zake ingawa hamujui ni nini huwa wanajadiliana. Pia muwaelekeze kuwa hao waliouliwa huwa wanakuja hata nyumbani kwa Johnson. Shahidi muhimu hapa ni mke wake Johnson, huwa anawashuhudia kila wakifika. Hapo vipi?", Mr Hassan alitoa ufafanuzi.

"Hapo tumekupata, hakuna kitakachoharibika", Jackline alidakia.

"Kwahiyo malipo yetu yatafanyika lini?", Idris aliuliza.

"Kesi ikiisha tu na hukumu ya kifungo cha maisha au kunyongwa ikitoka basi ntawalipa chenu. Ila tukishindwa kesi sitoweza kuwalipa chochote", Mr Hassan alitoa ufafanuzi kuhusiana na makubaliano yao.

Baada ya majadiliano ya takribani nusu saa, Mr Hassan aliagana na wenyeji wake kisha akaondoka huku wakiwa wameahidiana kuwa mkataba wa makubaliano yao utasainiwa siku tatu zijazo.


SIKU 12 ZILIZOPITA (NYUMBANI KWA IDRIS)

"Umesema upo njiani unarudi Dodoma?, mbona hukunipa taarifa mapema ili nijiandae Roida", ilikuwa ni sauti ya kulalamika ya Idris akiongea na Roida kwa njia ya simu.

"Jamani Iddy, si nishakwambia kuwa nakuja tu kwa dharula?, kuna gari la mtu binafsi limetoka Iringa, ndo nimepewa tu lifti", Roida alijibu.

"Ok sio kesi. Karibu sana ila tambua kuwa Jack nae yuko hapa na ninalala nae", Idris aliongea huku akishusha pumzi.

"Hilo sio tatizo Iddy, nitalala hata sebuleni. Kuanzia kesho kutwa ndo nitatafuta chumba nikapange", Roida alijibu.

"Ok, karibu sana. Uko sehemu gani?", Idris aliuliza.

"Nakaribia kufika, kwenye saa tatu nitakuwa hapo", Roida alijibu.

"Poa karibu sana", Idris alijibu na kukata simu.

Roida aliumia sana baada ya kugundua kuwa kwa sasa hana chake tena kwa Idris. Alidhani kumfanyia mpango Idris wa kumshawishi Jackline usingeleta athari katika mahusiano yake. Ila leo anajuta. Neno ninge..........

.........................................................................................

Chumbani kwa Idris.

"Jack, nina ombi moja kipenzi changu, naomba leo na kesho Roida alale hapa. Alafu keshokutwa ataenda kujitafutia chumba akapange", Idris aliongea kwa unyenyekevu akiomba ruhusa kwa mpenzi wake huyu mpya (Mke wa Johnson).

"Kama ataondoka baada ya siku mbili haina shida, ila atalala sebuleni ama chumba cha wageni. Sitaki kumuona huku chumbani kwetu", Jack alijibu huku akimuangalia Idris kwa jicho lenye ishara za wivu.

"Hakuna tatizo malkia wangu, atalala chumba cha wageni. Hata yeye amekubali kulala chumba cha wageni", Idris alijibu huku akishika shika nywele za Jackline.

"Poa babe, mi nina wivu sana mwenzako. Sipendi mtu mwingine ale kwenye shamba langu", Jackline aliongea kwa sauti yake ya kudeka. Yani alishasahau kama yeye ni mvamizi tu, mwenye mali halali ni Roida. Ndio hivyo, kashafanya mapinduzi. Roida hana chake kwa sasa.

Majira ya saa tatu na robo usiku, Roida aliwasili nyumbani kwa Johnson. Alimkuta Jackline akiwa jikoni anapika chakula cha usiku. Walisalimiana salamu za kinafiki, kila mmoja alikuwa na chuki kwa mwenzake. Jack alichukia kumuona Roida kwenye miliki yake mpya na Roida nae alimchukia Jack kwa kuvamia miliki yake. Hawakuongeleshana tena jambo lolote zaidi ya salamu tu. Daaah, WANAWAKE BWANA.

Roida alipotoka jikoni alielekea chumbani kwa Idris ambapo alimkuta anasoma soma vitabu.Walisalimiana. Akaweka vitu vyake vizuri kisha akarudi tena sebuleni.

"Lazima nitimize malengo yangu leo na kesho, keshokutwa nirudi zangu Mkonze. Lazima nizijue namba za siri za 'shelf'. Pia siwezi kulala kwenye chumba cha wageni, lazima nilale chumbani kwa Idris ili nikamilishe mipango yangu", Roida alikuwa akiwaza peke ake pale sebuleni.

Baada ya dakika kumi, Idris alitoka chumbani na kuungana na Roida pale sebuleni na kuanza kupiga nae stori mpaka pale Jackline alipoleta chakula mezani wakaanza kula. Ilikuwa ni futari ya ndizi mbivu iliyochanganywa na nyama ya ng'ombe pamoja na maharagwe. Kilikuwa ni chakula kitamu.

"Jack, mimi na wewe ni marafiki. Sipendi tupishane maneno wala tugombane kisa Idris. Sijapenda leo namna ulivyonipokea. Mi keshokutwa tu naondoka. Nivumilie kwa siku mbili hizi", Roida alianzisha mazungumzo wakati wa kula.

"Roida, naomba tule. Hapa sio mahakamani", Jack alijibu kwa jeuri huku akibetua mdomo wake.

"Sawa mama yaishe. Ila wewe utabaki kuwa rafiki yangu, si adui yangu. Naomba tutabasamu kama zamani",Roida aliongeza.

Jack hakujibu kitu. Idris nae hakupenda kuingilia mazungumzo ya wake zake hao.

"Jack, mbona hujaleta maji ya kunywa, tunakulaje kama nyoka?", Idris aliuliza punde alipohitaji maji anywe.

"Hakuna tatizo, ngoja nikufatie", Roida aliongea na kuinuka kwenda kufata maji.

"Hii ndio nafasi niliyokuwa naihitaji, lazima nifanikishe lengo langu leo. Lazima Idris alie", Roida aliwaza punde alipoingia jikoni. Alilifuata friji na kutoa jagi la maji baridi. Akaingiza mkono kwenye sidiria yake na kutoa dawa ya unga kwenye mfuko. Aliimiminia dawa ya kutosha kwenye glasi na kukoroga yale maji. Aliporizika akabeba jagi na kurudi nalo sebuleni. KIZAA ZAA.

Idris alipokea jagi la maji, alimimina maji kwenye glasi na kuanza kunywa.

"Babe, nimiminie na mimi ninywe", Jackline aliongea kwa sauti ya kudeka ili amuumize Roida. Laiti kama angejua.........

Idris alimimina tena maji kwenye glasi na kumpatia Jack.

"Naomba uninyweshe, mikono yangu inauma", Jack alizidi kumdekea Idris na sauti yake nyororo ili amuumize Roida. Ameshasahau kama Roida ndie aliyemfanyia mpango wa yeye kuwa na Idris

"Usijali kipenzi changu, haya kunywa sasa", idris alijibu huku akimnywesha Jack maji. Roida alinyamaza tu huku akishuhudia hila za rafiki ake wa zamani. Aliamua kupotezea tu vile vituko vya Jackline kwa kuwa alijua nini amelenga kufanya, ingawa moyoni alikuwa akiumia.

NMP (NeuroMuscular Blocking pills) ni aina ya dawa ambayo hupoozesha viungo vya mwili kwa muda mfupi. Muathirika huwa hawezi kufanya jambo lolote pindi anapoinywa hii dawa na kukaa walau dakika kumi. Na hukaa mwilini kwa masaa yasiyozidi tisa.

Idris alianza kujihisi kuishiwa nguvu, mwili wote ulianza kumsaliti. Alipotaka kuzungumza jambo alijikuta hawezi hata kunyanyua mdomo. Jackline nae hali yake ilikuwa sawa na Idris, nae alikuwa amejilaza kwenye sofa huku akijitahidi kusimama pasipo mafanikio yoyote. Roida aliwaweza.

Roida alipoona wenyeji wake wameshazidiwa na ile dawa, aliinuka na kuelekea moja kwa moja chumbani kwa Idris. Alilifungua kabati la Idris na kutoa kiboksi cha chuma kilichokuwa na ukubwa sawa na dumu la mafuta la lita tano. Alijitahidi kulishusha hadi chini na kutaka kulifungua.

"Mungu wangu, namba ya siri ya kufungulia hili boksi siijui, ila sio mbaya, acha niondoke nalo", Roida alijiwazia moyoni na kuanza kulikokota lile boksi la chuma na kuteremka nalo hadi sebuleni. Aliwakuta Jack na Idris wakiwa bado hawajiwezi. Alifungua mlango wa kutoka nje na kulipakiza katika gari la Idris na kuondoka nalo.

"Hello Babe, sijafanikiwa kuchukua zile nyaraka. Ila nimefanikiwa kuchukua lile boksi ambalo alikuwa akitunzia hela zake", Roida alikuwa akiongea na simu na mpenzi wake aliepo Mkonze-nje ya mji wa Dodoma.

"Basi chukua taxi likulete hadi huku", sauti ya kiume ilijibu.

"Sawa, nakuja. Ndo nipo njiani", Roida alijibu na kukata simu.



MKONZE - DODOMA



Majira ya asubuhi, maiti ya mwanamke umri miaka 27-30 inagunduliwa ndani ya nyumba ya kulala wageni. Wapita njia wamekusanyika karibu na nyumba ya kulala wageni ya "Malaika Guest house" huku kila mmoja akizungumza lake.

"Huyu binti aliekufa mi namjua, anaishi mtaani kwetu, anaitwa Roida. Masikini ya mungu amekufa kifo kibaya sana daah", Mama mmoja wa makamo aliyejifunga ushungi wa kanga kichwani alikuwa akiwaeleza wenzake.

"Yani amepigwa nondo ya kisogoni, kichwa chote hakitamaniki. Alafu nasikia huyo mwanaume aliemuua ametoroka. Wanaume wabaya jamani", Mdada mwingine anayefahamika kwa jina la pendo alidakia.

"Maisha ya sahizi usikubali tu mtu anatokea huko anakwambia dada nakupenda, na wewe bila kujiuliza mara mbilimbili unakubali tu. Mwisho wa siku unakufa kifo kama cha Roida", mdada mwingine aliongea.

"Roida nae alikuwa mapepe, kila mwanaume wake. Ona sasa leo kauliwa kifo cha kinyama. Mungu amsamehe tu dhambi zake huko aliko", Mama anayefahamika kama 'Mama Juma' nae alizungumza lake.

Kila mmoja alizungumza aliloona linafaa. Roida ameuliwa na mwanaume alielala nae 'gesti'.

Je, ni mwanaume yupi huyo?, au ni yule mpenzi wake waliopanga njama za pamoja za kumtapeli Idris?



USIKOSE SEHEMU IJAYO.

TUKUTANE TENA KESHO.
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com




SEHEMU YA KUMI NA TATU

Tulipoishia sehemu iliyopita...............

Sikiliza bibie, mume wako 'Johnson' ni muuaji, kwahiyo mimi lengo langu nataka askari polisi wakija kuwahoji kama ni kweli Johnson ana mienendo ya kiuhalifu mujibu ndio, tena wewe ndo inabidi useme kuwa umewahi kumuona mara kwa mara na wale wenzake aliowaua wakijadiliana kwa siri mipango yao kule kwenu, jieleze vizuri ili mukawe mashahidi kule mahakamani. Akishaadhibiwa tu kifungo cha maisha au kunyongwa basi nakufungulia biashara kubwa hapa mjini. Hakuna mwanamke atakayekufikia kwa utajiri Dodoma nzima" Mr. Hassan alizidi kupalilia maneno yake.

"Kama ni hivyo nipo tayari, mi siwezi kumsapoti mwanaume muuaji kama Johnson, kwanza namchukia sana", Jackline alijibu baada ya kusikia maneno matamu kutoka kwa Mr. Hassan.


Sasa tuendelee....................


"Mpango wetu ni huu; kesho kuna askari wa upelelezi watakuja kwenu kuwahoji. Munachotakiwa ninyi ni kukariri hizi sura za waliouawa. Chukueni hii picha yao, nyuma kuna majina ya kila mmoja. Huyu wa kushoto anaitwa Gideon, anayefuata anaitwa Oscar, anayefuata ni Daud na huyo wa mwisho ni Selemani. Kwahiyo ili uweze kuwakumbuka vizuri kariri neno 'GODS'. Yaani G=Gideon, O=Oscar, D=Daud na S=Selemani. Tumeelewana?", Mr. Hassan aliwapa maelekezo Idris na Jackline huku akiwapatia na picha.

"Hapa bado hatujaelewa muheshimiwa. Sisi tunatakiwa tuwaambie nini polisi?", Idris aliuliza.

"Wakija kuwahoji muwaambie kwamba huwa munamuona Johnson mara kwa mara na wale jamaa zake ingawa hamujui ni nini huwa wanajadiliana. Pia muwaelekeze kuwa hao waliouliwa huwa wanakuja hata nyumbani kwa Johnson. Shahidi muhimu hapa ni mke wake Johnson, huwa anawashuhudia kila wakifika. Hapo vipi?", Mr Hassan alitoa ufafanuzi.

"Hapo tumekupata, hakuna kitakachoharibika", Jackline alidakia.

"Kwahiyo malipo yetu yatafanyika lini?", Idris aliuliza.

"Kesi ikiisha tu na hukumu ya kifungo cha maisha au kunyongwa ikitoka basi ntawalipa chenu. Ila tukishindwa kesi sitoweza kuwalipa chochote", Mr Hassan alitoa ufafanuzi kuhusiana na makubaliano yao.

Baada ya majadiliano ya takribani nusu saa, Mr Hassan aliagana na wenyeji wake kisha akaondoka huku wakiwa wameahidiana kuwa mkataba wa makubaliano yao utasainiwa siku tatu zijazo.


SIKU 12 ZILIZOPITA (NYUMBANI KWA IDRIS)

"Umesema upo njiani unarudi Dodoma?, mbona hukunipa taarifa mapema ili nijiandae Roida", ilikuwa ni sauti ya kulalamika ya Idris akiongea na Roida kwa njia ya simu.

"Jamani Iddy, si nishakwambia kuwa nakuja tu kwa dharula?, kuna gari la mtu binafsi limetoka Iringa, ndo nimepewa tu lifti", Roida alijibu.

"Ok sio kesi. Karibu sana ila tambua kuwa Jack nae yuko hapa na ninalala nae", Idris aliongea huku akishusha pumzi.

"Hilo sio tatizo Iddy, nitalala hata sebuleni. Kuanzia kesho kutwa ndo nitatafuta chumba nikapange", Roida alijibu.

"Ok, karibu sana. Uko sehemu gani?", Idris aliuliza.

"Nakaribia kufika, kwenye saa tatu nitakuwa hapo", Roida alijibu.

"Poa karibu sana", Idris alijibu na kukata simu.

Roida aliumia sana baada ya kugundua kuwa kwa sasa hana chake tena kwa Idris. Alidhani kumfanyia mpango Idris wa kumshawishi Jackline usingeleta athari katika mahusiano yake. Ila leo anajuta. Neno ninge..........

.........................................................................................

Chumbani kwa Idris.

"Jack, nina ombi moja kipenzi changu, naomba leo na kesho Roida alale hapa. Alafu keshokutwa ataenda kujitafutia chumba akapange", Idris aliongea kwa unyenyekevu akiomba ruhusa kwa mpenzi wake huyu mpya (Mke wa Johnson).

"Kama ataondoka baada ya siku mbili haina shida, ila atalala sebuleni ama chumba cha wageni. Sitaki kumuona huku chumbani kwetu", Jack alijibu huku akimuangalia Idris kwa jicho lenye ishara za wivu.

"Hakuna tatizo malkia wangu, atalala chumba cha wageni. Hata yeye amekubali kulala chumba cha wageni", Idris alijibu huku akishika shika nywele za Jackline.

"Poa babe, mi nina wivu sana mwenzako. Sipendi mtu mwingine ale kwenye shamba langu", Jackline aliongea kwa sauti yake ya kudeka. Yani alishasahau kama yeye ni mvamizi tu, mwenye mali halali ni Roida. Ndio hivyo, kashafanya mapinduzi. Roida hana chake kwa sasa.

Majira ya saa tatu na robo usiku, Roida aliwasili nyumbani kwa Johnson. Alimkuta Jackline akiwa jikoni anapika chakula cha usiku. Walisalimiana salamu za kinafiki, kila mmoja alikuwa na chuki kwa mwenzake. Jack alichukia kumuona Roida kwenye miliki yake mpya na Roida nae alimchukia Jack kwa kuvamia miliki yake. Hawakuongeleshana tena jambo lolote zaidi ya salamu tu. Daaah, WANAWAKE BWANA.

Roida alipotoka jikoni alielekea chumbani kwa Idris ambapo alimkuta anasoma soma vitabu.Walisalimiana. Akaweka vitu vyake vizuri kisha akarudi tena sebuleni.

"Lazima nitimize malengo yangu leo na kesho, keshokutwa nirudi zangu Mkonze. Lazima nizijue namba za siri za 'shelf'. Pia siwezi kulala kwenye chumba cha wageni, lazima nilale chumbani kwa Idris ili nikamilishe mipango yangu", Roida alikuwa akiwaza peke ake pale sebuleni.

Baada ya dakika kumi, Idris alitoka chumbani na kuungana na Roida pale sebuleni na kuanza kupiga nae stori mpaka pale Jackline alipoleta chakula mezani wakaanza kula. Ilikuwa ni futari ya ndizi mbivu iliyochanganywa na nyama ya ng'ombe pamoja na maharagwe. Kilikuwa ni chakula kitamu.

"Jack, mimi na wewe ni marafiki. Sipendi tupishane maneno wala tugombane kisa Idris. Sijapenda leo namna ulivyonipokea. Mi keshokutwa tu naondoka. Nivumilie kwa siku mbili hizi", Roida alianzisha mazungumzo wakati wa kula.

"Roida, naomba tule. Hapa sio mahakamani", Jack alijibu kwa jeuri huku akibetua mdomo wake.

"Sawa mama yaishe. Ila wewe utabaki kuwa rafiki yangu, si adui yangu. Naomba tutabasamu kama zamani",Roida aliongeza.

Jack hakujibu kitu. Idris nae hakupenda kuingilia mazungumzo ya wake zake hao.

"Jack, mbona hujaleta maji ya kunywa, tunakulaje kama nyoka?", Idris aliuliza punde alipohitaji maji anywe.

"Hakuna tatizo, ngoja nikufatie", Roida aliongea na kuinuka kwenda kufata maji.

"Hii ndio nafasi niliyokuwa naihitaji, lazima nifanikishe lengo langu leo. Lazima Idris alie", Roida aliwaza punde alipoingia jikoni. Alilifuata friji na kutoa jagi la maji baridi. Akaingiza mkono kwenye sidiria yake na kutoa dawa ya unga kwenye mfuko. Aliimiminia dawa ya kutosha kwenye glasi na kukoroga yale maji. Aliporizika akabeba jagi na kurudi nalo sebuleni. KIZAA ZAA.

Idris alipokea jagi la maji, alimimina maji kwenye glasi na kuanza kunywa.

"Babe, nimiminie na mimi ninywe", Jackline aliongea kwa sauti ya kudeka ili amuumize Roida. Laiti kama angejua.........

Idris alimimina tena maji kwenye glasi na kumpatia Jack.

"Naomba uninyweshe, mikono yangu inauma", Jack alizidi kumdekea Idris na sauti yake nyororo ili amuumize Roida. Ameshasahau kama Roida ndie aliyemfanyia mpango wa yeye kuwa na Idris

"Usijali kipenzi changu, haya kunywa sasa", idris alijibu huku akimnywesha Jack maji. Roida alinyamaza tu huku akishuhudia hila za rafiki ake wa zamani. Aliamua kupotezea tu vile vituko vya Jackline kwa kuwa alijua nini amelenga kufanya, ingawa moyoni alikuwa akiumia.

NMP (NeuroMuscular Blocking pills) ni aina ya dawa ambayo hupoozesha viungo vya mwili kwa muda mfupi. Muathirika huwa hawezi kufanya jambo lolote pindi anapoinywa hii dawa na kukaa walau dakika kumi. Na hukaa mwilini kwa masaa yasiyozidi tisa.

Idris alianza kujihisi kuishiwa nguvu, mwili wote ulianza kumsaliti. Alipotaka kuzungumza jambo alijikuta hawezi hata kunyanyua mdomo. Jackline nae hali yake ilikuwa sawa na Idris, nae alikuwa amejilaza kwenye sofa huku akijitahidi kusimama pasipo mafanikio yoyote. Roida aliwaweza.

Roida alipoona wenyeji wake wameshazidiwa na ile dawa, aliinuka na kuelekea moja kwa moja chumbani kwa Idris. Alilifungua kabati la Idris na kutoa kiboksi cha chuma kilichokuwa na ukubwa sawa na dumu la mafuta la lita tano. Alijitahidi kulishusha hadi chini na kutaka kulifungua.

"Mungu wangu, namba ya siri ya kufungulia hili boksi siijui, ila sio mbaya, acha niondoke nalo", Roida alijiwazia moyoni na kuanza kulikokota lile boksi la chuma na kuteremka nalo hadi sebuleni. Aliwakuta Jack na Idris wakiwa bado hawajiwezi. Alifungua mlango wa kutoka nje na kulipakiza katika gari la Idris na kuondoka nalo.

"Hello Babe, sijafanikiwa kuchukua zile nyaraka. Ila nimefanikiwa kuchukua lile boksi ambalo alikuwa akitunzia hela zake", Roida alikuwa akiongea na simu na mpenzi wake aliepo Mkonze-nje ya mji wa Dodoma.

"Basi chukua taxi likulete hadi huku", sauti ya kiume ilijibu.

"Sawa, nakuja. Ndo nipo njiani", Roida alijibu na kukata simu.



MKONZE - DODOMA



Majira ya asubuhi, maiti ya mwanamke umri miaka 27-30 inagunduliwa ndani ya nyumba ya kulala wageni. Wapita njia wamekusanyika karibu na nyumba ya kulala wageni ya "Malaika Guest house" huku kila mmoja akizungumza lake.

"Huyu binti aliekufa mi namjua, anaishi mtaani kwetu, anaitwa Roida. Masikini ya mungu amekufa kifo kibaya sana daah", Mama mmoja wa makamo aliyejifunga ushungi wa kanga kichwani alikuwa akiwaeleza wenzake.

"Yani amepigwa nondo ya kisogoni, kichwa chote hakitamaniki. Alafu nasikia huyo mwanaume aliemuua ametoroka. Wanaume wabaya jamani", Mdada mwingine anayefahamika kwa jina la pendo alidakia.

"Maisha ya sahizi usikubali tu mtu anatokea huko anakwambia dada nakupenda, na wewe bila kujiuliza mara mbilimbili unakubali tu. Mwisho wa siku unakufa kifo kama cha Roida", mdada mwingine aliongea.

"Roida nae alikuwa mapepe, kila mwanaume wake. Ona sasa leo kauliwa kifo cha kinyama. Mungu amsamehe tu dhambi zake huko aliko", Mama anayefahamika kama 'Mama Juma' nae alizungumza lake.

Kila mmoja alizungumza aliloona linafaa. Roida ameuliwa na mwanaume alielala nae 'gesti'.

Je, ni mwanaume yupi huyo?, au ni yule mpenzi wake waliopanga njama za pamoja za kumtapeli Idris?



USIKOSE SEHEMU IJAYO.

TUKUTANE TENA KESHO.
Nice
 
RIWAYA: NIACHENI NIKUFURU

MTUNZI: FAHAD MUSSA

EMAIL: fahadmussa55@gmail.com



SEHEMU YA KUMI NA NNE


Kata ya Makulu- DODOMA


"We chapombe, wewe chapombe wewe, Baba Betty, we Baba Betty hebu amka huko. Muone, na sahizi umetoka kuweweseka tena maneno yako ya kila siku", Mama Betty aliongea kwa hasira huku akimuamsha muwewe.

"Eeh, eeh, naam, nini", Baba Betty aliitika huku bado akiwa usingizini, aligeukia ubavu wa pili na kujifunika tena shuka.

"Si nimekwambia uamke, amka kwanza unieleze una tatizo gani. Kila siku unaweweseka na kutamka hayo mambo yako ya ajabu. Hebu amka huko", Mama Betty alizidi kufoka kwa hasira huku akimfunua shuka mumewe na kumuinua pale kitandani.

"Jamani mwanamke wewe hebu acha gubu, mi nina usingizi mwenzako. Niache nisinzie", Baba Betty alimlaumu mama Betty kwa kuukatisha usingizi wake.

"Hebu kaa vizuri huko alafu unieleze hayo maneno unayoyatamkaga usingizini yana maana gani", Mama Betty aliongea kwa hasira.

"Jamani mke wangu, mbona mi sina michepuko, nakupenda wewe tu, nitaropoka nini usingizini zaidi ya kusema nakupenda!!", Baba Betty alijitetea.

"Hujaota kuhusu michepuko, ulikuwa unasema 'sina hatia, munanionea', tena leo sio mara ya kwanza wala ya pili kuweweseka maneno hayo. Huwa una maanisha nini?, kila siku nikikuuliza unanificha", Mama Betty aliuliza kwa ukali.

"Ok, punguza jazba mke wangu. Ngoja leo nikwambie ukweli wa maisha yangu ambao unanitesa hadi sasa. Sikupenda kuusema ila leo sina budi kuusema", Baba Betty alikohoa na kujiweka vizuri pale kitandani, kisha akaendelea kuzungumza.

"Bila shaka unafahamu kuwa mimi mumeo, Alexander Florence, ni muuza mitumbo ya nguo na viatu katika soko la Saba saba. Na hiyo kazi ndio inayotuwezesha kula na kulipa kodi ya hivi vyumba viwili tulivyopanga. Ila nisamehe sana, sikuwahi kukuambia kwamba takribani miaka kumi iliyopita niliwahi kuwa Askari polisi, tena mwenye cheo kizuri tu", Baba Betty aliongea na kunyamaza kidogo ili kumpa uzingativu mkewe. Kisha akaendelea.

"Nilikuwa na cheo cha 'Mrakibu msaidizi wa polisi yaani Assistant Superintendent of Police (ASP). Niliifanya kazi yangu kwa umakini sana mpaka pale nilipoingilia maslahi ya wakubwa zangu. Hapo ndipo Nilipotengenezewa kesi ya uporaji na kujeruhi mtu. Cha ajabu huyo mtu ambae wanasema nilimpora na kumjeruhi hata sikuwahi kumtia machoni hapo kabla hadi kipindi cha kuhudhuria mahakamani ndipo nikamtia machoni. Huwezi amini, vidhibiti vyote vya mimi kutenda kosa kuanzia Silaha, alama za vidole hadi gari lililotumika kupora vilikuwa ni vya kwangu kweli. Na hata hizo mali nilizopora zilikutwa nyumbani kwangu. SIJUI ILIKUWAJE", Baba Betty aliongea kwa masikitiko.

"Kwahiyo hukumu ilikuwaje", Mama Betty akauliza.

"Nilihukumiwa kwenda Jela miaka mitano na nikafutwa kazi. Nilipotimiza kifungo changu ndipo nikaanza kujishughulisha na biashara ya mitumba mpaka pale nilipokutana na wewe, hadi leo hii tuko hapa pamoja. Kwahiyo hadi sasa bado ninaweweseka upweke. Sikutarajia kama siku moja ningefungwa kwa kusingiziwa na mwisho wa siku ningefanya kazi kama hii ninayoifanya leo." Baba Betty alimalizia simulizi yake.

"Pole sana mume wangu, kumbe ulikuwa Afisa mkubwa kabisa wa polisi, sikujua. Ila nimekusamehe kwa kunificha hilo jambo. Kuanzia leo naomba usahau yaliyopita. Pia punguza kulewa, ikiwezekana acha kabisa pombe. Mungu atatujalia tu, tutakuwa matajiri siku moja", Mama Betty alimfariji muwewe.

"Nishapoa mke wangu, na ninakuahidi, mda si mrefu nitaacha kulewa hovyo. Ni msongo wa mawazo ndio unaonifanya niipende pombe", Baba Betty alimuahidi mkewe. Wakakumbatiana na kupiga stori nyingine mpaka pale palipokucha.






Turudi nyuma (MAUAJI YA ROIDA)




"Eliza, nikufanyie nini ili uamini kuwa nakupenda?, kwanini unataka kulivuruga penzi letu?, nina kasoro gani hadi unataka kuniacha?, Pliiz, usinifanyie hivyo mama, naomba tuendelee na penzi letu", David alikuwa akim'bembeleza Eliza, mwanamke ampendae kuliko wanawake wote duniani.

"Hauna hela we mwanaume, hiyo ndo kasoro kubwa uliyonayo. Hata poda ya miatano unashindwa kuninunulia. Tafuta hela alafu ndipo tuendelee na penzi letu. Nimechoka maisha ya kimasikini, nahitaji matunzo mtoto wa kike", Eliza alijibu kwa nyodo huku akitaka kuondoka.

"Nielewe Eliza, kuna ishu naisikilizia, mambo yakitiki tu nitatimiza yote unayoyahitaji. Vuta subira mama", David alizidi kubembeleza.

"Nyie ndio wanaume ambao Chriss mauki anawaita 'WASANII', kila siku unasema kuna ishu unaisikilizia, utasikilizia hiyo ishu hadi lini?. Tafuta pesa ,alafu tuendelee", Eliza alizidi kuongea kwa nyodo huku akisimama mahala alipokaa na kuondoka.

David alibaki peke yake pale chini ya mti wa muembe, hakujua afanye nini. Mpenzi ndo huyo amemkimbia, kisa hela.

"Lazima nimsisitize Roida aufanye ule mpango wetu haraka iwezekanavyo ili nipate hela ya kula maisha na Eliza. Siwezi kumlaumu Eliza, amenivumilia sana hadi leo hii ameamua kunikimbia. Ngoja nitafute hela, nitarudi.

*****************************************************



Baada ya Roida kuiba boksi la chuma kutoka kwa Idris, aliondoka na gari la Idris hadi nje ya mji ambapo alilitelekeza lile gari na kuchukua taksii hadi Mkonze, kwa mpenzi wake 'David'.

"Babe, mi nshafika hapa stendi. Kwahiyo uko wapi?", Roida aliongea kwa simu baada ya kufika stendi ya Mkonze.

"Naomba uchukue bodaboda alafu akulete 'Malaika Guest House', utanikuta hapa, chumba namba 17. Usije na hiyo taxii, iache hukohuko. Shuka alafu upande boda hadi huku", David alimpa maelekezo Roida.

"Sawa switi, nakuja", Roida alijibu na kukata simu.

Alimlipa dereva taksi nauli, alishuka na mkoba wake ambao ndani yake kulikuwa na lile boksi. Alisimama pale hadi taksii ilipoondoka ndipo nae akazunguka mtaa wa pili na kupanda bajaji ambayo ilimpeleka hadi 'gesti' ya Malaika. Alimlipa dereva bajaji hela yake kisha akaingia ndani ya ile gesti na mzigo wake. Muda ulikuwa ni saa sita usiku.


"Waaaooooo, kipenzi changu", David alimlaki Roida kwa furaha punde alipoingia ndani. Alimkumbatia kwa nguvu huku akim'busu sehemu mbali mbali za uso wake.

"Hongera sana mpenzi kwa kazi nzito, tunaenda kuwa matajiri sahizi. Naomba tulivunje hili boksi. Nimekuja na vifaa vyote vya kulivunja hili boksi", David alimpongeza Roida huku akilitoa lile boksi kwenye mkoba na kuliweka mezani.

"Naomba basi tulivunje sahizi ili tuhakikishe kama kweli kuna hizo hela tunazozifikiria. Tunaweza jiaminisha hapa kumbe ndani kuna makaratasi tu", Roida alizungumza.

"Humu lazima kuna hela, huu uzito sio bure", David aliongea huku akianza kuligonga gonga lile boksi kwa nyundo na praizi.

Ilichukua takribani dakika 40 ndipo lile boksi lilifunguka. Hakuna aliyeamini macho yake. Ndani kulikuwa na mafungu mengi ya elfu kumi kumi. Ambayo baada ya kuhesabiwa zilipatikana jumla milioni 76. Wote kwa pamoja waliruka kwa furaha na kucheza cheza kama ishara ya kuuaga umasikini. Roida hakujua mpenzi wake 'David' ana malengo gani dhidi yake. Laiti kama angejua.............


Saa kumi na moja alfajiri, David aliamka kwa lengo la kutoroka na zile hela. Alizikusanya hela zote na kuziingiza kwenye begi lake la mgongoni. Wakati alipokuwa anataka kutoka ndipo Roida nae alikuwa anafumbua macho, aliangalia pale walipoweka hela hakuziona akamuangalia David, akamuona amebeba begi lililotuna. KIZAA ZAA.

"Devi, unataka kufanya ujinga gani?, unatoroka na hela ili iweje?, kumbe wewe ni shetani kiasi hiki?",Roida aliongea kwa tahamaki huku akinyanyuka na kwenda kumzuia David pale mlangoni.

Mambo yalishaharibika. David ilimpasa kulishusha begi chini na kutoa panga dogo. Roida alipoona David ameshika panga mkononi, alitaka kufungua mlango ili akimbie. Ila bahati haikuwa yake, David alishamfikia na kumpiga Roida panga la kisogoni. MCHEZO KWISHA.

David alibeba begi lake na kutoka nje. Alitoka nje ya gesti pasipo kuaga. Alielekea kwa mpenzi wake ampendae 'Eliza'.


NYUMBANI KWA IDRIS

Majira ya saa moja asubuhi, Idris anaamka. Anajikuta yeye na mpenzi wake 'Jackline' wapo sebuleni. Ndipo anapokumbuka kuwa usiku uliopita, yeye na Jackline walikunywa maji yaliyowekewa dawa za kulevya, zilizowafanya wakose nguvu za kufanya chochote, hatimae wakalala sebuleni.

Akainuka haraka pale sebuleni na kuelekea moja kwa moja chumbani kwake. Alilikuta kabati lake lipo wazi, ndipo alipogundua kuwa fedha zake zote zimeibiwa. Alichanganyikiwa kupita maelezo, pesa alizopanga kufungulia mradi mkubwa wa kilimo kijijini kwao zilishachukuliwa na Roida.

Akiwa bado na taharuki, simu yake ya mkononi iliita, akaipokea na kuisogeza sikioni.

"Hallo, naongea na Idris Jamal", upande wa pili wa simu ulisikika.

"Ndio, mwenzangu nani?", Idris aliuliza.

"Hapa ni kituo cha polisi Image", kuna gari yako "TOYOTA Harrier" tumelikuta limetelekezwa maeneo yetu haya. Tunakuomba hapa kituoni mara moja", Yule afande aliongea.

"Sawa afande, nakuja mda si mrefu", Idris aliitikia na kukata simu.

Alitoka chumbani na kuelekea sebuleni ambapo alimuamsha Jackline na kumueleza kila kinachoendelea. Jackline alipigwa na butwaa baada ya kukumbuka tukio la usiku uliopita
Kikubwa zaidi aliumia baada ya kusikia Roida ameiba boksi la chuma linalotumika na Idris kama benki yake. Walijiandaa na kuelekea kituo cha Image ambacho kipo Kilomita kadhaa kutoka Dodoma jiji.


TUKUTANE TENA KESHO PANAPO MAJAALIWA.
 
Ila haiingii akiĺini eti umuombe mke wa mtu mshare bwana yako theņ huyo mwanàmke hasistuke!!!
Mbona ngumu kumeza?
Roida hakuwa mke wa mtu,na wala hakufunga ndoa na Idris. Ndio maana hata alipokuwa akitumwa kwenda kumshawishi Jackline alikubali na alikuwa akilipwa. Roida na Idris walikuwa tu kama marafiki ambao machoni pa watu walionekana kama wanandoa. Ingawa walikuwa hawanyimani sex

Mwisho wa siku alikuja kupata wivu baada ya kuona Idris hamjali tena kama zamani. But kiuhalisia, she was there for money.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom