Riwaya: muuaji aliyebakia

Riwaya: muuaji aliyebakia

Sehemu ya 15

Bila kuchelewa alimpa taarifa hizo Geofrey
ambaye alichukulia jambo hilo kama la
kawaida na aliamini siku ambayo angerudi
Tanzania mambo yote yangekuwa sawa.
Magreth alikuwa amejiwekea utaratibu wa
kumtembele gerezani kila mwisho wa wiki
jambo lililompa sana faraja. Geofrey naye
tayari alianza kuingiwa na mshtuko wa moyo
juu ya Magreth kutokana na ishara za wazi
alizozipata lakini aliona jambo hilo haliku
wezekana kwa yeye kuwa na uhusiano na
mrembo huyo. Siku zote alimchukulia kama
msichana mwenye huruma na aliamini
hakuna jambo ambalo lingeweza kutokea
kuhusiana na hisia zake. Muda ulikwenda na
hatimaye Geofrey alibakiwa na wiki mbili za
kutumikia adhabu yake, hakuamini hata
kidogo kuwa angeliacha gereza hilo na kuwa
huru. Furaha yake iliongezeka zaidi kutokana
na ahadi ambayo Magreth alishampa ya
kufanikisha safari yake kurudi Tanzania.
Zilibaki siku mbili, hatimaye moja na
mwishoe siku ya Jumapili majira ya saa nane
alipewa nguo za kuvaa alizoelezwa aliletewa
na mtu aliyefika gerezani hapo kumchukua.
Geofrey hakujiuliza maswali mengi akiamini
nguo hizo zilitoka kwa Magreth aliingia katika
chumba cha kubadilishia nguo na kuanza
kuvaa nguo hizo. Lilikuwapo shati moja rangi
nyekundu pia viatu na soksi vilikuwa vya
rangi hiyo pamoja na jinzi moja iliyovutia
kwa muonekano. Geofrey alivivaa na kuanza
kutembea akitoka katika chumba hicho askari
magereza walishtuka na kuanza kumshangilia
kwa mwonekano mzuri aliokuwa nao. Mkuu
wa gereza alimsifia kwa tabia yake nzuri
aliyokuwa nayo kipindi akiwa gerezani hapo
zaidi kitendo chake cha kuwatetea wanyonge.
Alimaliza akimwambia aliamini toka wakati
huo angekuwa raia mwema na mwishoe
alimhurusu aondoke. Geofrey alianza
kutembea kuelekea geti kuu la gereza hilo
kwa haraka akiwa hajiamini kwani alihisi
angeitwa tena kurudi kifungoni. Mara baada
ya kutoka katika geti hilo kidogo moyo wake
ulitulia lakini alihitaji kuondoka kabisa eneo
hilo. Alikuwa akimwangalia Magreth kama
alikuwapo eneo hilo kumchukua kama
alivyoelezwa na askari magereza.
Alizungusha kichwa kila upande eneo hilo
pasipo kumuona zaidi ya gari lililokuwa na
rangi nyekundu ambalo lilikuwa kando yake
kidogo ambalo vioo vyake havikuhurusu mtu
wa nje kuona ndani. Akiwa anatafakari juu ya
jambo la kufanya alishtushwa mlango wa
gari hilo uliokuwa ukifunguliwa, alielekeza
macho yake ili aone mtu ambaye angeshuka.
Alishuhudia mguu wa mwanamke ukiwa na
kiatu rangi nyekundu ukitoka kabla ya mtu
huyo kutoka kabisa. Mshtuko wake
uliongezeka zaidi baada ya kuona mtu huyo
alikuwa Magreth, alikuwa amevaa vitu vyenye
rangi nyekundu toka chini hadi juu. Alikuwa
na gauni la kuvutia na zaidi mkononi pia
alikuwa na maua ya rangi hiyo, alianza
kutembea akielekea eneo ambalo Geofrey
alikuwa amesimama. Mara baada ya
kumfikia alimkubatia kabla ya kusikika “ pole
sana Geoffur…..” “ahsante lakini zaidi
nashukuru kwa kunijali muda wote nikiwa
jela” Alijibu Geofrey ambaye mapigo yake ya
moyo yalimwenda mbio hakuelewa jambo
lililoendelea siku hiyo lakini rangi nyekundu
ndiyo ilimpa shaka zaidi. Aliongozwa mpaka
kwenye gari hilo lililokuwa Range Rover, kabla
ya kuondoka kwao Geofrey aliamua kuuliza
jambo lililomtatiza ingawaje lilimpa hisia za
ushindi moyoni mwake.
“kwa nini kila kitu kina rangi hii..” aliuliza
Geofrey baada ya kushindwa kujizuia,
Magreth alicheka kidogo kabla ya kumgeukia
akimtizama usoni “Geoffur leo ni tarehe kumi
na nne mwezi wa pili siku ya wapendanao
duniani, naamini tunapendana” alimjibu
jambo lililomfanya Geofrey acheke kwa furaha
ingawaje hakujibu kitu ila aliona kama vile
alikuwa amelala masikini na kuamka mfalme.
Tayari alijipa aslimia mia za kuwa na
Magreth mpaka mwisho wa maisha yake.
Waliongoza mpaka hoteli ya kifahari
iliyokuwapo katika jimbo hilo la Biloku na
huko ndipo uhusiano wao ulianza rasmi
baada ya ahadi nyingi walizowekeana. Siku
iliyofuata Magreth alianza kumtafutia Geofrey
hati ya kusafiria kurudi Tanzania.
Mara baada ya taratibu zote kukamilika
alimsindikiza Geofrey uwanja wa ndege tayari
kwa safari kurudi Tanzania, alimweleza
angerudi pia mara baada ya masomo yake
ya mwaka mmoja uliobakia. Magreth alikuwa
akilia kwani alihisi huo ndiyo ulikuwa kama
mwisho wa yeye kuonana na Geofrey, mara
baada ya kuagana alikuwa amempa namba
ya simu na fedha za kutosha akiwa
amemweleza mara baada ya kufika Tanzania
amjulishe. Safari hiyo ilianza na mwishoe
walifika Tanzania wakiwa wamepita
Uingereza, Ethiopia na nchi nyingine. Geofrey
bila kupoteza muda alikodi teski na
alimweleza dereva ampeleke eneo lililokuwa
na kampuni ya JAJHO, halikuwa jambo gumu
kwa dereva huyo kwani alidai kampuni hiyo
ilikuwa kubwa sana wakati huo. Alihitaji
kufikia katika kampuni hiyo kwani bado
Geofrey kumbukumbu alikuwa nazo juu ya
kampuni hiyo aliyoiacha akiwa anaelekea
Marekani na ilikuwa chini ya umiliki wa baba
yake na wenzie wanne.
Hatimaye walifika katika foleni ya magari
iliyokuwapo maeneo ya posta akiwa
ameelezwa walikaribia kufika katika eneo
lililokuwa na ofisi hizo za kampuni ya
JAJHO. Alikumbuka kumtaarifu Magreth
kuwa tayari alikuwa amefika Tanzania,
wakati huo alikuwa amekaa upande wa
mbele wa teski hiyo akiwa na dereva na kioo
cha gari kilikuwa wazi. Alichukua simu yake
na kumpigia mara baada ya kuita mara moja
ilipokelewa “nimeshafiaka Tanzania na niko
nae…..” kabla hajamalizia sentesi hiyo mara
baada ya kusalimiana kwao kibaka mmoja
aliinyan`ganya simu hiyo kwa nguvu na
kuondoka kwa kasi eneo hilo la foleni na
tayari magari yalikuwa yamehurusiwa.
Geofrey alichanganyikiwa ghafla juu ya tukio
hilo zaidi hakuwa na namba ya mawasiliano
ya Magreth ambayo ilihifadhiwa kwenye simu
hiyo. Baada ya jitihada za haraka za kuipata
simu hiyo kushindikana aliamua kukubaliana
na tukio hilo na alimhurusu dereva waendelee
na safari akiwa na imani kuwa angeitafuta
namba hiyo. Mara baada ya kufika eneo hilo
aliongozwa mpaka kwenye ofisi ya mmiliki
mkuu wa kampuni hiyo aliyekuwa na hisa
nyingi, aliamini alikuwa anaenda kuonana na
baba yake.
Mara baada ya kuingia katika ofisi hiyo
alikutana na sura tofauti na baba yake ila
kumbukumbu zake zilimjia kwa mbali juu ya
mtu huyo.
“ samahani namuulizia James Kibudo”
Alisikika Geofrey mara baada ya kuketi, mtu
huyo alishtuka kidogo kabla ya kumuuliza
“unamuulizia kama nani katika kampuni hii”
alijibu mtu huyo “kama mmoja wa wamiliki
wa kampuni hii” alijibu “sikiliza kijana James
Kibudo alifilisika miaka mingi iliyopita na
hayupo kwenye orodha ya wamiliki wa wa
kampuni hii, alituuzia hata jina lake ndiyo
maana hatujabadili jina la kampuni hii ya
JAJHO tukihofia soko letu mtaani, zaidi
alikutwa ameuuawa nch…” kabla hajamalizia
kuongea Geofrey alikurupuka na kumvamia
akitaka kujua vizuri sentesi ya mwisho
iliyohusu mauaji.
Walinzi kadhaa waliitwa ofisini hapo na
kumkamata zaidi mtu huyo aliyekuwa bosi
aliyejitambulisha kama Jackson aliwaita
wamiliki wenzie Amos, Hamis na Onesmo ili
wamhoji mtu huyo. Geofrey baada ya kutulia
kidogo alijieleza vizuri na mwishoe watu hao
walimpa taarifa za kuuawa kwa baba na
mama yake miaka kumi iliyopita na mdogo
wake Robert walidai hawakujua eneo
alilokuwapo na imani yao ilikuwa alikuwapo
Marekani.
Walimweleza juu ya taarifa walizokuwa nazo
juu ya kifo chake baada ya ajali ya ndege
iliyotokea nchini Guyana. Baada ya maelezo
hayo Geofrey akiwa na majonzi aliaga na
kuondoka eneo hilo la ofisi za JAJHO,
mawazo yake yalikuwa ni kuhakikisha
anaenda Kenya na kushuhudia kabuli la baba
na mama yake.Jackson na wamiliki wenzie
waliitana na kushangilia juu ya tukio hilo la
maelezo ya kifo cha James na mkewe
waliyoyatoa kwa mwanaye na waliamini siri
yao isingevuja.
Alielekea katika nyumba moja ya kulala
wageni maeneo hayo ya Posta na muda wote
alikuwa akilia juu ya tukio hilo alillolisikia,
siku iliyofuata alianza safari akielekea Kenya
kwa lengo la kwenda kuliona kabuli la baba
na mama yake. Mara baada ya kufika jijini
Nairobi aliongoza katika kituo kikuu cha polisi
cha jiji hilo na kuomba kuonyeshwa makabuli
hayo. Tayari alishaelezwa awali na mr.
Jackson kuwa askari wa kituo hicho
wangemsaidia kwani walihusika kwa kiasi
kikubwa na mazishi ya wazazi wake.

ITAENDELEAAA....
 
riwaya za kijinga kabisa hizi, hazifundishi kitu ndiyo maana zinaitwa za kusisimua basi. kidi kudi unatuuza.
 
riwaya za kijinga kabisa hizi, hazifundishi kitu ndiyo maana zinaitwa za kusisimua basi. kidi kudi unatuuza.

Sidhani kama unamtendea haki mtunzi pamoja na kidi kudi kwa kupondea ubora wa riwaya husika na hata aloileta humu, naamini hakuitwa mtu kuna kuisoma yanini kumshambulia mletaji? Siyo fresh
 
Last edited by a moderator:
Sidhani kama unamtendea haki mtunzi pamoja na kidi kudi kwa kupondea ubora wa riwaya husika na hata aloileta humu, naamini hakuitwa mtu kuna kuisoma yanini kumshambulia mletaji? Siyo fresh

Achana nae mkuu wasoma riwaya wanajulikana
 
Last edited by a moderator:
Sehemu ya 16

Tayari alishaelezwa awali na mr. Jackson
kuwa askari wa kituo hicho wangemsaidia
kwani walihusika kwa kiasi kikubwa na
mazishi ya wazazi wake.
Askari hao walimwelewa na mara baada ya
kurejea kumbukumbu zao aliongozwa na
askari mmoja hadi eneo la makabuli hayo.
Geofrey alilia kwa uchungu mara baada ya
kuona vibao ambavyo rangi yake ilikuwa
ikikwajuka vikiwa na majina ya wazazi wake
na aliamini aliloelezwa kuwa waliuawa. Siku
iliyofuata aliwatafuta mafundi ujenzi kadhaa
na kuwataka wamjengee makabuli hayo
yaliyokuwa katika hali mbaya ya kuweza
kupoteza kumbukumbu yake. Mara baada ya
zoezi hilo aliweka mataji kama ishara ya
kushiriki kwake katika msiba huo na kwa
wakati huo aliamini hata mdogo wake Robert
angeweza kwenda kuiona kumbukumbu hiyo
ya kifo cha wazazi wao.
Tayari alikuwa ameishiwa fedha zote
alizopewa na Magreth kabla ya kuondoka
kwake nchini Guyana na wakati huo aliona
hana njia ya kuweza kumuokoa. Aliamua
kumpigia simu mr. Jackson wa kampuni ya
JAJHO akiomba uwezekano wa kupatiwa kazi
lakini alijibiwa kwamba hawakuwa na nafasi
hiyo. Aliumia juu ya jibu hilo lakini alijipa
moyo ingawaje kuna wakati aliwahisi vibaya
wamiliki wa kampuni hiyo. Jambo lililomkaa
kichwani aliwaza kuwa ni lazima atafute
fedha kwa ajili ya kufuatilia watu waliofanya
mauaji dhidi ya familia yake. Akili yake
ilimtuma kuua kama akiwagundua watu
waliohusika na mauaji hayo kwani aliamini
jeshi la polisi la nchi zote mbili za Tanzania
na Kenya lilishindwa kazi yake.
Baada ya kujibiwa vibaya na mr. Jackson
alijichanganya katika mitaa ya jiji la Nairobi
ili kutafuta maisha akianza kwa kuuza vitu
tofauti barabarani. Wiki moja baadaye
aligundua kuwa alijichelewesha kufanya
malipo ya vifo kwa watu ambao walihusika
na kifo cha wazazi wake. Kwani aliamini
ilimbidi apate fedha ili afanye upelelezi na
mwishoe apange malipizi hayo, aliamua
kuanza kutafuta kundi la majambazi nchini
humo akiamini aliweza kazi hiyo kwani
alipata mafunzo mengi toka kwa mzee
Rogart akiwa nchini Guyana. Baada ya wiki
moja alikutana na mtu aliyejulikana kama mr.
Tyoso ambaye alikuwa na kundi lake la
majambazi, hivyo alianza kazi na watu hao.
Ndani ya mwezi mmoja kundi la mr. Tyoso
lilipata mafanikio kupindukia kupitia uwezo
mkubwa aliokuwa nao Geofrey. Kikubwa ni
utumiaji wake wa bunduki na zaidi upinde na
mishale walivyofanyia unyan`ganyi sehemu
tofauti nchini Kenya. Alikuwa akiishi na mr.
Tyoso mwenyewe kwa vile hakuwa na
nyumba katika jiji hilo. Baada ya miezi
mitano ya mafanikio tayari Geofrey pia
alikuwa ni mtaalamu wa kuendesha magari
hata pikipiki. Siku moja Geofrey alipatwa na
homa ya malaria na hivyo alibakia nyumbani
kwa mr. Tyoso wakati kundi hilo likiendelea
na ujambazi. Muda wote akiwa nyumbani
hapo alikuwa akisikiliza redio na mwishoe
nyakati za jioni aliamua kuigeukia luninga ya
mr. Tyoso. Alianza kuchagua filamu
mbalimbali ambazo angeweza kuangalia
lakini alivutiwa na moja iliyoonekana ilikuwa
ya wanyama kwani iliianza kwa kuonyesha
vyura. Ilimvutia zaidi kutokana na maisha ya
porini aliyokuwa ameishi kwa muda mrefu
nchini Guyana, ilionyesha ilikuwa imeandaliwa
na George Johnson raia wa Kenya miaka
kumi iliyokuwa imepita.
Aliendelea kuangalia filamu hiyo huku
akifurahia aina ya vyura walioonyeshwa,
ghafla filamu hiyo ilikatishwa katikati na
maneno yaliyoandikwa ‘MAUAJI YA KUTISHA’
yalitokea. Geofrey alikaa vizuri ili aone
kilichokuwa kikifuata, alishtushwa na filamu
hiyo iliyoendelea na baada ya sekunde
chache aliwaona wazazi wake wakiwa porini
kama wametekwa. Alikaa vizuri zaidi na
kutoa macho, alimwona Jackson,Hamis,Amos
na Onesmo wote wakiwa wamilikiwa kampuni
ya JAJHO wakiwa katika eneo hilo la tukio na
zaidi bosi wake mr. Tyoso alikuwapo. Jasho
lilimtoka kama maji mara baada ya kuanza
kushuhudia mauaji ya wazazi wake,
aliwashuhudia jinsi wamiliki wa JAJHO
walivyommiminia risasi baba yake wakati
mama yake akiuawa na mr. Jackson. Zaidi
aliona kila kitu katika tukio hilo kwani mpiga
picha aliwachukua wazazi wake kwa karibu
sana na kamera yake kabla ya wauaji hao
kurudi na kuwatupa wazazi wake katika mto
Tana.
Geofrey hakuamini vizuri na wakati huo
alichukua upinde na mishale yake tayari kwa
shari aliwaza kuanza mauaji na mr. Tyoso
aliyeonakana kuhusika. Tayari ilikuwa yapata
saa moja jioni, alikuwa ameirudisha kwa
mara ya pili filamu hiyo akiiangalia tena.
Ghafla wakati akiendelea kuangalia filamu
hiyo mr. Tyoso aliingia lakini Geofrey
hakusikia chochote kutokana na hali ya
kuchanganyikiwa aliyokuwa nayo juu ya
filamu hiyo. Shati lake lilikuwa limelowa
jasho kama vile alikuwa amenyeshewa na
mvua, mr Tyoso alishtushwa na filamu hiyo
iliyompa hisia za mauaji waliyoyafanya miaka
mingi iliyokuwa imepita. Alikurupuka na
kwenda kuitoa filamu hiyo kabla ya kuivunja
akikanyaga na buti lake lililokuwa kama la
jeshi, jambo hilo lilipelekea filamu hiyo
kugawanyika katika vipande.
Geofrey akili yake kidogo ilianza kumrudia
sawasawa akiwa amegundua kuwa mtu
aliyepaswa kuanza naye kumuua alikuwa
amefika. Mr. Tyoso akilini hakuwahi kuhisi
wala kuambiwa kuwa watu waliouawa katika
filamu hiyo walikuwa ni wazazi wa Geofrey.
Hata baada ya kuivunja filamu hiyo alielewa
lilikuwa jambo la kawaida kwani walikuwa
wamefanya mauaji kadhaa na Geofrey hivyo
aliamini alikuwa mtu muuaji kama yeye.
Wakati huo Geofrey mishipa ya hasira ilikuwa
imemtoka shingoni na usoni na alikuwa
kimya bila kusema kitu akiwa ameshika
upinde na mshale alioupachika sawasawa
lakini pembeni na eneo alilokaa akiweka
mishale mingine mingi.
“ebwana hili dili kuna mzushi alituona
tulivyokuwa tunawasaidia watanzania fulani
wa kampuni ya JAJHO kumuua mwenzao,
kwa hiyo huwa siipendi hiyo filamu kwanza
sikujua kama bado ipo” aliongea mr Tyoso
baada ya ukimya kwa muda mrefu. Geofrey
alisimama akiwa na mshale wake na upinde
akiwa amemwelekezea mr. Tyoso usoni ,
“piga magoti haraka sana” aliongea kauli
ambayo mr. Tyoso hakuitekeleza akijua ni
utani. “vipi tena tunataniana toka…..”alisikika
akijibu kauli ya Geofrey lakini kabla ya
kumalizia sentensi yake alipigwa teke la uso
lililompeleka mpaka chini. Hapo mr Tyoso
aligundua kulikuwa na shari hivyo alitekeleza
amri ya kupiga magoti, Geofrey aliivuta
kamba ya upinde wake ambao alipachika
mshale akiwa ameuelekeza kifuani kwa mr
Tyoso. “jina langu ni Geofrey James Kibudo
kwa hiyo wewe ulishiriki kuwaua wazazi
wangu sina zawadi ya kukupa zaidi ya hii….”
Aliongea Geofrey kauli iliyomshangaza mr
Tyoso na mara baada ya kuimaliza kauli hiyo
aliachia kamba ya upinde na mshale wake
kwa kasi ya ajabu ulielekea kifuani mwa mr
Tyoso na kupenya sawasawa ukiwa umeingia
zaidi ya nusu.
Mr. Tyoso alianza kupiga kelele za maumivu
aliyoyapata wakati damu ilianza kumtoka,
Geofrey aliingia kwenye chumba chake na
kuchukua fedha zake zote. Mara baada ya
kufanya hivyo alielekea katika chumba cha
mr. Tyoso na kuchukua bunduki mbili
walizozitumia kwa ujambazi lakini pia
alichukua fedha ambazo aliziona. Alirudi na
kuchukua funguo za gari katika suruali
aliyokuwa ameivaa mr. Tyoso ambaye bado
alikuwa akilalamika kwa maumivu makali.
Alifanikisha mambo hayo ndani ya dakika
saba na alitoka mbio nje akiwa pia amebeba
upinde na mishale, mara baada ya kupakia
vitu vyote kwenye gari alilitoa kwa kasi eneo
hilo la nyumba ya mr Tyoso. Alikuwa
amebeba bunduki, upinde na mishale
sambamba na fedha za kutosha kwani
alielewa jambo lililofuata lilikuwa malipizi ya
vifo vya wazazi wake.
Alikimbiza gari hilo aina ya ‘Land Cruiser’
akiwa na mpango wa kuvuka mipaka
kuelekea Tanzania na hatimaye kuingia Dar
es salaam kwa ajili ya kufanya malipo ya
mauaji. Wakati akiwa anaendelea kuliacha jiji
la Nairobi kuna jambo aligundua lilikuwa la
muhimu kulitekeleza, alichukua simu yake na
kumpigia mr Jackson ambaye baada ya simu
kuita kwa muda mfupi aliipokea “baada ya
kumuua mr. Tyoso nakuja kuwaangamiza na
nyinyi wote nawapa siku saba za uhai wenu”
alisikika Geofrey mara baada ya simu
kupokelewa kabla ya kukata na kuizima.
Aliendeleza kasi ya kuendesha gari lake,
hakuwa na mpango wa kuwashirikisha polisi
jambo hilo kwani aliamini walishindwa
kufanya kazi yao kwa zaidi ya miaka kumi,
alipanga kuwauwa wamiliki wa kampuni ya
JAJHO wote kwa mkono wake.
Mr. Jackson alishtushwa na kauli aliyoipokea
toka kwa mtu ambaye namba yake aliihifadhi
kama Geofrey akiwa mtoto wa marehemu
James. Hisia za kugundulika kwa siri yao
zilimjia jambo lililopelekea ampigie simu tena
Geofrey ili ajue kama alikuwa ameigundua
siri hiyo lakini simu ya kijana huyo
haikupatikana.


ITAENDELEA...
 
Hitimisho

Hisia za kugundulika kwa siri yao zilimjia
jambo lililopelekea ampigie simu tena
Geofrey ili ajue kama alikuwa ameigundua
siri hiyo lakini simu ya kijana huyo
haikupatikana.
Aliamua kumpigia simu mr Tyoso ili
ahakikishe kama kweli alikuwa ameuawa,
simu yake ilipokelewa na mtu mwingine
aliyemthibitishia kifo cha mr. Tyoso. Upelelezi
wa haraka alioufanya mr Jackson aligundua
Geofrey alikuwa akifanya kazi kama jambazi
chini ya usimamizi wa mr Tyoso.
Uthibitisho wa siri hiyo kuvuja ulikamilika na
aliwaita wenzie na kuwaeleza juu ya jambo
hilo lakini zaidi aliwataka wajiweke katika
tahadhari ili wafanikishe kumuua Geofrey
kabla ya kuuawa kwao. Walitafuta vijana
wakakamavu zaidi ya ishirini na kugawana
watano kila mmoja na zaidi waliwatafuta
wengine zaidi ya thelathini waliopewa jukumu
la kufuatilia nyendo za Geofrey waliyeamini
bado alikuwa hajaingia Dar es salaam.
Jackson na wenzie walijipa matumaini
wakiamini kuwa ni lazima Geofrey angeuawa
kabla yao kutokana na mikakati waliyoiweka.
Baada ya siku tatu Geofrey alikuwapo nchini
Tanzania, alikuwa amefikia wilaya ya
Bagamoyo katika kijiji cha Fukayosi akiwa
amejitambulisha kama mpangaji katika
nyumba yenye vyumba vitatu aliyoishi mzee
mmoja. Alikuwa amepewa chumba kimoja
kati ya hiyo vitatu wakati vingine vilitumiwa
na mzee huyo, alimtoa hofu mzee huyo akidai
kuwa alikuwa akifanya utafiti katika maeneo
hayo na angeishi kwa muda wa wiki mbili.
Mzee huyo hakuwa na ubishi kwani alipea
fedha za kutosha, tayari Geofrey alikuwa na
pikipiki aliyoinunua njiani wakati akitokea
Kenya. Siku iliyofuata aliondoka na pikipiki
akielekea jijini Dar es salaam ambako
alifanya zoezi la kuzitambua nyumba za
wamiliki wa kampuni ya JAJHO ambalo
halikuwa gumu kutokana na umaarufu na
utajiri waliokuwa nao. Tayari aliamua kuanza
mauaji na Onesmo baada ya kuona
uwezekano wote wa kufanikisha zoezi hilo,
alikuwa amepanga kuwauwa wamiliki hao
ndani ya usiku mmoja siku iliyofuata.
Siku iliyofuata majira ya saa tatu usiku
aliondoka Bagamoyo na pikipiki akielekea
jijini Dar es salaam akwa na lengo moja la
kwenda kuwauwa wamiliki wa kampuni ya
JAJHO. Alikuwa amebeba upinde na mishale
sambamba na na bunduki moja iliyokuwa na
risasi za kutosha, vyote alikuwa ameviweka
kwenye begi kubwa alilokuwa amelibeba
mgongoni lakini pia alikuwa na tochi pamoja
visu kadhaa vilivyozunguka kiunoni mwake.
Alikuwa hajatumia dawa zozote za kulevya
lakini akili yake kwa ujumla ilimtuma kuua,
alikuwa mtu aliyeathirika kisaikolojia ambaye
ilikuwa vigumu kuubadili msimamo wake.
Saa tano usiku alikuwa nje ya geti la mr.
Onesmo akiwa ameshaiegesha pikipiki yake
na bila kuchelewa aligonga akiwa amejitega
kwa shari pembeni na mlango mdogo wa geti
hilo. Alisikia vishindo mlinzi akijongea getini
na kuanza kufungua mlango mdogo wa geti
hilo, alijiweka tayari akiamini alipaswa
kuanza na mlinzi huyo akiwa ameshika moja
ya kisu kilichon`gaa kutokana na ukali wake.
Mara baada ya kutoka mlinzi huyo aliyekuwa
na bunduki yake alipokelewa na teke zito la
usoni lililomrudisha ndani ya geti hilo akiwa
ameanguka. Kabla hajafanya jambo lolote
alinyan`ganywa bunduki aliyokuwa nayo,
Geofrey alimwelekezea bunduki hiyo mlinzi
huyo kabla ya kuambiwa aongoze kwenye
chumba chake cha ulinzi kilichokuwa getini
hapo. Alitekeleza jambo hilo na kwa haraka
aliingia kwenye chumba hicho akifuatwa na
Geofrey ambaye alimuhoji maswali kadhaa na
aligundua Onesmo alikuwa hajarudi nyumbani
kwake. Alieleza lengo lake la kumuhitaji
Onesmo na si mlinzi huyo hivyo alitumia
kamba zilizokuwapo katika chumba hicho na
kumfunga mikono na miguu. Baada ya
kufanikisha zoezi hilo alimpiga mlinzi huyo na
kitako cha bunduki yake katika mishipa yake
ya fahamu ya shingoni iliyopelekea mlinzi
huyo aanguke chini akiwa amepoteza
fahamu.
Alitoka nje kwa kasi na kuchukua pikipiki
yake na kuiingiza ndani katika chumba hicho
cha cha mlinzi alibadilisha shati lake na
kuvaa la mlinzi huyo sambamba na kofia
yake hakubadili suruali kwa vile iliendana na
ya mlinzi huyo.Wakati akitafakari jambo la
kufanya alishtuhwa na honi za gari
zilizopigwa nje ya geti hilo. Bila kujiuliza
mara mbili aligundua mtu huyo alikuwa
Onesmo akirudi nyumbani kwake, alielekea
katika geti hilo na kulifungua kwa kasi la
kwanza na hatimaye la pili ambalo alijificha
nyuma yake. Alishuhudia gari mbili zikiingia
na kwenda kuegesha eneo la mbele la
nyumba ya hiyo alishuka Mr Onesmo na watu
zaidi ya kumi walioonekana walikuwa
wakimlinda.
Tayari alikuwa amefunga geti hilo na kurejea
katika kibanda chake, kwa sauti ya chini
alisikia maongezi yaliyoendelea “bosi leo
tunaomba tukapumzike ili turudi kwa kasi
mpya ya kesho lakini pia huna haja ya
kumuogopa Geofrey huyo ni mtu mdogo sana
hatuwezi” alisikika mmoja wa watu hao
aliyeonekana alikuwa kiongozi wao. “sawa
kwa leo tu ila saa kumi na moja muwe
mmefika hapa” Aliwajibu Onesmo ambaye
alianza kutembea akielekea katika nyumba
yake kabla ya kufunguliwa na kuingia. Watu
hao walioonekana kama walinzi wa Onesmo
waliingia kwenye gari hizo Mercedez Benz
mbili walizofika nazo na walianza
kuziendesha wakiziondoa eneo hilo. Geofrey
alijua jukumu lake kwa kasi alifungua geti na
watu hao waliondoka.
Hapo aliamini mchezo ulikuwa umeisha bila
kupoteza muda alichukua visu vitatu na
bunduki moja iliyokuwa na risasi za kutosha
aliongoza hadi kwenye mlango wa kuingilia
wa nyumba hiyo na kuanza kugonga.
Aliamini mtu aliyekuwa amemfungulia
Onesmo lazima angerudi kumfungulia baada
ya muda mfupi akisikia vishindo vya mtu
huku akiongea “jamani mlinzi nini tena….”
Aliongea dada huyo ambaye mara baada ya
kufungua mlango alipokelewa na bomba la
mbele la bunduki. “kwa usalama wako tulia
naomba unionyeshe chumba anacholala mr
Onesmo” Aliongea Geofrey akiwa amemkazia
macho dada huyo ambaye alinyosha mkono
akionyesha ghorofa ya kwanza ya nyumba
hiyo. Baada ya maelezo hayo Geofrey
akitumia nguvu alimpiga msichana huyo na
kitako cha bunduki na kupelekea kuanguka
kwake kabla ya kupoteza fahamu.
Bila kupoteza muda Geofrey alikimbia
akielekea ghorofani mwa nyumba hiyo
alipofika aliuona mlango mmoja ambao
ulikuwa haujafungwa vizuri huku taa yake
ikiwaka aliingia na kumshuhudia mr. Onesmo
akibadilisha nguo za kulalia huku mkewe
akiwa amelala “mamaaa weeee nafwaa
huwiiiii” alipiga kelele mr Onesmo ambazo
zilimwamsha hata mkewe. “tulia mbwa wewe
nisije nikakuua kabla ya wakati” aliongea
Geofrey akiwa amemwelekezea bunduki yake
jambo lililoleta utulivu hata kwa mkewe
Onesmo ambaye hakujua jambo lililoendelea.
“ nipe simu yako haraka iwezekanavyo”
alitoa agizo hilo ambalo Onesmo alilitekeleza.
“ulidhani mlivyowauwa wazazi wangu nisinge
wagundua” aliongea Geofrey wakati
akikipitisha kisu chake tumboni katika hali
iliyoonyesha alikisafisha na bado alikuwa
amemwelekezea bunduki mr Onesmo. Alikuwa
ameshika kisu kirefu mithili ya panga
kilichon`gaa kupindukia, ghafla alikurupuka
na kumvamia Onesmo akiwa amelekezea kisu
hicho tumboni kilichompata sawasawa. Wote
alianguka chini huku Geofrey akiwa bado
amekishikilia kisu, alikitoa kwa kasi na bila
huruma alishindilia mara tatu zaidi akichoma
na kuchomoa. Damu iliyotoka na kuruka
ilikuwa ni zaidi ya machinjio, jambo hilo ndilo
lililopelekea mkewe Onesmo kuzimia. Geofrey
akiwa amebeba bunduki yake alitoka mbio
chumbani hapo na kuongoza moja kwa moja
hadi kwenye kibanda cha mlinzi ambaye
alikuwa hajarudiwa na fahamu. Aliwasha
pikipiki na kuchukua vitu vyake vyote kabla
ya kuiondoa pikipiki hiyo kwa kasi eneo hilo
la nyumba ya Onesmo.
Baada ya saa moja alikuwa maeneo ya
Kimara katika hoteli iliyotambulika kwa jina la
`Mwalon West` ambako bila kupoteza muda
alilipia chumba kimoja.Tayari ilikuwa yapata
saa saba na nusu usiku bado lengo lake
lilikuwa ni kuhakikisha anakamilisha mauaji
kwa wamiliki wa kampuni ya JAJHO katika
usiku huo. Aliamini simu ya Onesmo
aliyoichukua kabla ya kumuua ndiyo
ingekamilisha zoezi hilo, aliandaa visu,
bunduki yake sambamba na upinde na
mishale ambavyo aliviweka chini ya uvungu.
Alikuwa amechanganyikiwa na hakuwaza
jambo lolote zaidi ya kuua, alichukua simu ya
Onesmo na kufanikiwa kuziona namba za
simu za Jackson, Hamis na Amos. Baada ya
kuziona namba hizo alifungua sehemu ya
ujumbe mfupi wa maandishi na kuanza
kuandika.
Baada ya kuziona namba hizo alifungua
sehemu ya ujumbe mfupi wa maandishi na
kuanza kuandika.
Alipanga kuwatumia wamiliki hao ujumbe wa
maandishi ili wafike hotelini hapo akiamini
wangeshawishika.
Baada ya dakika tatu alikamilisha ujumbe
huo uliokuwa hivi ‘Mkubwa Nimefanikiwa
Kumkamata Mshenzi Geofrey James Kibudo,
Fanya Haraka Uje Katika Hoteli Ya Mwalon
West Chumba Namba 25 . Njoo Peke Yako
Kama Unavyojua Inatubidi Tuue Na siri Hii
Asiijue Mtu…..! Nakusubiri!’ Alikamilisha
Geofrey ujumbe huo wa simu na kuutuma
kwa namba za watu hao kwa pamoja.
Ujumbe huo ulionyesha kupokelewa na Hamis
pamoja na Amos lakini haikuwa hivyo kwa
Jackson. Geofrey alijaribu kumpigia namba
yake ilikuwa haipatikani. Baada ya dakika
tatu akiwa anatafakari jambo la kufanya
alishtushwa na mlio wa simu hiyo kabla ya
kushuhudia ujumbe wa maandishi toka kwa
Hamis ulioandikwa ‘Msimuue Huyo Mshenzi
Nakuja Sasa Hivi…’ dakika moja baadaye
Amos naye alithibitisha kufika hotelini hapo.
Geofrey alijua kazi ilielekea kuisha aliandaa
upinde na mshale tayari kwa mauaji, alikuwa
akiwasubiri kwa hamu ili aendelee
kukamilisha ndoto yake ya kuwaua wote
usiku huo. Baada ya nusu saa alisikia mlango
ukigongwa, jambo lililompa hisia kuwa
mmoja wa watu hao alikuwa amefika, kwa
kasi alienda kusimama kando ya mlango huo
akiwa na upinde na mshale uliotegeshwa
tayari kwa shari. “tafadhari ingia…” alisikika
Geofrey na kumfanya mtu aliyekuwa angonga
kufungua mlango na kuanza kuingia. Mara
baada ya kuingia alianza kuangalia huku na
huku akionekana kama alitafuta kitu, Geofrey
alikuwa ametulia huku akiwa amegundua mtu
huyo alikuwa Hamis.
Akiwa bado hajatulia vizuri alishtushwa na
sauti ya mtu aliyekohoa alipogeuka alitoa
macho kabla kuanza kupiga kelele “siniue
usiniue tafadhari..” alipiga kelele Hamis
baada ya kumshuhudia Geofrey akiwa tayari
kwa kumuua “tulia we mbwa huna muda wa
kupoteza inakupasa uuangane na mwenzio
Onesmo…” alisikika Geofrey kabla kuachia
mshale ulioenda kumpata sawasawa Hamis
tumboni, akiwa hajatulia vizuri alisindikizwa
na teke la uso lililompeleka mpaka chini,
alianza kulalamika kutokana na maumivu
aliyoyapata. Geofrey alichukua bunduki chini
ya uvungu wa kitanda akiwa anahofia
usalama wake baada ya kelele zilizotolewa
na Hamis, aliiweka vizuri baada ya ya kusikia
vishindo vya mtu akija kwa kasi eneo la
chumba hicho. Punde alishtushwa na sura
mtu huyo aliyeingia bila kugonga baada ya
kuona alikuwa ni Amos “mikono juu kunguru
mkubwa na taratibu sogea kwa mwenzio…”
alisikika Geofrey kwa jazba na kumchanganya
Amos aliyetetemeka kupindukia baada ya
kumwona Hamis akiwa ametokwa na damu
nyingi na bado alikuwa akihangaika. Jambo
hilo lilimfanya Amos achanganyikiwe ghafla
na kushindwa kutimiza amri aliyopewa,
hasira za Geofrey ziliongezeka na kuamua
kuanza kumiminia risasi Amosi ambaye
alianguka baada ya muda mfupi.
Alimgeukia Hamis na kumpiga naye risasi ya
kichwa na kumfanya atulie kabisa. Kulikuwa
na kelele za watu waliohofia uhai wao baada
ya kusikia milio hiyo ya risasi. Bila kuchelewa
Geofrey alichukuwa funguo za pikipiki yake
pamoja na bundu ki hiyo aliyokuwa bado
kaishika alianza kukimbia akitoka katika
hoteli hiyo. Aligongana na watu waliokuwa
wamechanganyikiwa wakizunguka katika
hoteli hiyo, alipiga risasi nyingine mbili
sakafuni ambazo ziliwafanya hata walinzi
wakimbie. Geofrey alifanikiwa kuichukua
pikipiki yake na kuondoka kwa kasi eneo hilo
la hoteli ya Mwalon West. Alikimbiza pikipiki
yake akielekea Bagamoyo alikokuwa
amepanga chumba, tayari aliona ndoto zake
zilikuwa zimeingia dosari kwa vile
hakufanikisha mauaji ya watu wanne.
Alikuwa anawaza kuhakikisha anaenda
kujiandaa kwa ajili ya kurudi kumalizia
mauaji na Jackson.
* * * *
Magreth alikuwa ameshtushwa na kukatika
kwa mawasiliano ghafla kati yake na
mwanamme wa ndoto zake, Geofrey. Muda
wote alikuwa akilia akiwa hajui jambo
lililokuwa limemtokea, kuna wakati alikuwa
akihisi mwanamme huyo alikuwa amemsaliti.
Alikuwapo katika chuo cha Guyana akiwa
amebakiza muda mfupi ili amalize elimu ya
chuo, wakati huo maendeleo yake kitaaluma
yalikuwa mabovu kutokana na mawazo
aliyokuwa nayo juu ya Geofrey muda wote.
Baada ya miezi kadhaa alishindwa kuvumilia
na aliamua kuondoka chuoni hapo pasipo
kuaga na kuandaa safari yake ya kurudi
Tanzania. Hatimaye siku hiyo ilifika na safari
ilianza akiwa hajatoa taarifa ya safari hiyo
hata kwa wazazi wake.
Baada ya wiki moja alikuwapo nchini
Tanzania akimtafuta Geofrey kila kona ya jiji
la Dar es salaam pasipo mafanikio yeyote,
jambo lililomkatisha tamaa kwa kiasi
kikubwa.Alikuwa amefikia katika nyumba yao
na kila siku alitumia gari lake kumtafuta
Geofrey akiwa anatembea na picha yake
lakini hakuna mtu aliyemfahamu. Hapo ndipo
Magreth alipozidi kuchanganyikiwa zaidi
akiamini alikuwa amepoteza mwelekeo wa
kumpata. Siku moja akiwa Kariakoo katika
mizunguko yake hiyo ya kumtafuta, alishtuka
baada ya kumuona kwa umbali mtu
aliyeamini alikuwa ni Geofrey. Alishuka
kwenye gari na kuanza kumkimbilia mtu huyo
huku akimwita. “Geoffur!, Geoffur……..”
alimwita mtu huyo ambaye hakuitika na
baada ya sekunde kadhaa kelele za kuita
zikiwa zimeongezeka mtu huyo alisimama.
Magreth akiwa anakimbia alimrukia na
kumkumbatia na wote waliaanguka chini,
watu waliokuwa katika pilikapilika zao
walianza kushawashangaa. “ wewe dada
vipi? mbona unanirukia inakuwaje?” Alisikika
mwanamme huyo mara baada ya kusimama.
“samahani kaka unafanana sana na
mchumba wangu” aliongea Magreth huku
akiwa na anajisikia aibu ikiwa ni baada ya
kugundua mtu huyo hakuwa Geofrey ila
walifanana sana. “samahani naomba
tuondoke wote maana watu wanatushangaa
nitakueleza vizuri niko na gari” Alisikika
Magreth na walianza kutembea na
mwanamme huyo hadi kwenye gari na
kuondoka eneo hilo. Baada ya muda mfupi
wa maongezi Magreth aligundua jambo
lililompa matumaini, mwanamme huyo
alikuwa mdogo wake Geofrey aliyeitwa
Robert. Alikuwapo Tanzania kwa miezi zaidi
ya sita akiwa na mchumba wake wakitokea
Marekani na kazi aliyoifanya alikuwa
akipeleleza juu ya tukio la mauaji ya wazazi
wake zaidi alikuwa anaamini kaka yake
Geofrey alikufa katika tukio la ajali ya ndege
nchini Guyana. Robert alikuwa ameacha
biashara zake nchini Marekani na jambo
lililopelekea hayo yote lilihusiana na upelelezi
juu ya kifo cha wazazi wake. Magreth pia
aligundua juu ya kifo cha wazazi wa Geofrey
na zaidi alimweleza Robert kuwa kaka yake
bado alikuwa hai na alimsimulia kisa kizima
cha maisha ya kaka yake huyo na zaidi
alimwonyesha picha zake. Jambo hilo
lilimfurahisha kwa kiasi kikubwa Robert,
alijiona kama hakuwa mpweke kutokana na
uhai wa kaka yake.
Siku iliyofuata waliendeleza zoezi la
kumtafuta Geofrey wakati Robert alikuwa na
mchumba wake aliyeitwa Annie ambaye
alitoka naye Marekani. Ni siku ambayo
ilikuwa ngumu na iliwachanganya zaidi kwani
vyombo vingi vya habari vilitawaliwa na kisa
cha kuuawa matajiri wakubwa watatu
wakitanzania. Muuaji alitajwa kwa jina la
Geofrey James Kibudo, ingawaje picha zake
hazikupatikana lakini polisi walikuwa
wakiendelea na msako mkali ili kumnasa.
Magreth alichanganyikiwa hata hamu ya
kumtafuta Geofrey ilianza kupungua lakini
Robert naye hakuwa ametulia kwani
alishtushwa juu ya taarifa hizo. Annie
aliwapa moyo akiwaeleza huenda Geofrey
hakuhusika na waliendelea na zoezi lao hilo
la kumtafuta Geofrey. Muda wote Magreth
alikuwa akilia na kuonekana kujuta kukutana
na Geofrey lakini bado alithibitisha kuwa
Geofrey alikuwa mwanamme wa ndoto zake.
Siku tano zilikatika na kulikuwa hakuna
taarifa zozote kutoka jeshi la polisi juu ya
kupatikana kwa muuaji lakini bado Magreth
na wenzie walikuwa wakiendelea na zoezi la
kumtafuta Geofrey. Walikuwa wakilala
kwenye gari na walitembelea kila sehemu
waliyohisi wangempata, siku hiyo majira ya
saa mbili usiku walikuwa maeneo ya
Bagamoyo katika kituo cha kuuza mafuta ya
gari.Walikuwa wakiongeza mafuta katika gari
lao baada ya mizunguko mingi, wakati zoezi
hilo liliendelea kuna mtu alifika na pikipiki na
kuegesha eneo la mbele yao akiwa na nia ya
kuongeza mafuta. “Geoffur, Geoffur…..”
alipiga kelele Magreth huku akishuka kwenye
gari walilokuwa nalo na kumfuata mtu
aliyekuwa kwenye pikipiki ambaye pia
alishtuka kabla ya kushuka katika pikipiki.
Magreth alimkimbilia na kumkumbatia
Geofrey aliyeanza kulia baada ya kumwona.
Magreth alimkimbilia na kumkumbatia
Geofrey aliyeanza kulia baada ya kumwona.
Hatimaye Robert na Annie walijongea eneo
hilo, Robert alikurupuka kwa kasi na
kumkumbatia Geofrey na wote walianguka
chini. Geofrey ambaye alikuwa mnyonge huku
akiwa amebeba begi kubwa, hakuuliza na
alionekana kumkumbuka mdogo wake.
“Magreth nisamehe nadhani nimeharibu ahadi
yetu kwa vile sidhani kama ndoto zetu
zitatimia kama tulivyopanga, bado nahitajika
kuua mtu wa mwisho aliyewaua wazazi
wangu” alisikika Geofrey huku akiweka begi
lake vizuri alilolibeba mgongoni kabla ya
kuisogelea pikipiki na kupanda. “ nakupenda
sana Magreth lakini yanipasa niondoke,
Magreth, Roby aamh! Annie naenda, lakini
muwe waangalifu” Alisikika Geofrey kabla ya
kuwasha pikipiki yake na kuiondoa kwa kasi
eneo hilo.
Wote walibaki wamepigwa na butwaa na
zaidi Magreth aliyeonekana akilia, ghafla
aliacha kulia akasikika akisema “hapana,
hapana Geoffur nampenda…,haiwezekani..!
kama kufa tufe wote” alitoka akikimbia na
kwenda kuingia kwenye gari kabla ya
kuliwasha na kuliondoa kwa kasi eneo hilo
akiwa amemwacha Robert na Annie wakiwa
hawaelewi jambo la kufanya. Annie alimtuliza
Robert aliyechanganyikiwa kwa kiasi kikubwa
na alimtaka waende wakatulie ili watafakari
jambo la kufanya na ikawa hivyo. Walipata
chumba katika hoteli moja na walikuwa
wakitathimini juu ya matatizo hayo
waliyokumbana nayo.
Siku iliyofuata majira ya saa moja asubuhi
walipata taarifa za kifo cha Magreth
aliyepata ajali mbaya mara baada ya
kuondoka akiwa na lengo la kumfukuzia
mchumba wake Geofrey. Baada ya dakika
tano walipata taarifa nyingine iliyoeleza
Geofrey James Kibudo alikuwa katika hali
mbaya akiwa amelazwa katika hospitali ya
taifa ya Muhimbili baada ya kushambuliwa
na askari wakati akijaribu kumuua tajiri
Jackson. Ilielezwa alikuwa amepigwa risasi
zaidi ya nane, bila kupoteza muda Robert na
Annie walikodi teksi na kuondoka maeneo ya
Bagamoyo wakiwa na lengo la kwenda
kumuona. Robert alikuwa na hasira na
mpaka wakati huo alikuwa hajui juu ya jambo
lililoendelea juu ya mkasa huo.
“waliowaua wazazi wetu ni wamiliki wa
kampuni ya JAJHO na amebaki Jackson
John Samola hakikisha unamumaliza
mwenyewe kwa vile naamini jeshi la polisi
lilishindwa kazi hiyo” ilikuwa ni kauli ya
Geofrey aliyeongea kwa taabu sana mara
baada ya Robert na Annie kufika hospitali.
Alikuwa hajazungumza kitu kwa askari
waliokuwa wanamlinda zaidi ya kauli hiyo
aliyoitoa kwa Robert.Hata hivyo hakuna
askari aliyesikia maelezo hayo, na Geofrey
alionekana hakuwa na imani na jeshi la
polisi. Baada ya dakika chache alifariki na
Robert alilia kwa uchungu juu ya tukio hilo
lililomuuma na aliamini kuuawa kwa Jackson
ilikuwa ni kazi iliyokuwa mikononi mwake.
Alitoka mbio eneo hilo la hospitali kabla ya
kwenda kukodi teksi akihitaji apelekwe
Masaki katika nyumba aliyoishi Jackson.
Alikuwa hana silaha ya aina yeyote lakini
imani yake ilikuwa ni kufanikisha mauaji
hayo. Annie aliamua kuwaeleza askari juu ya
kila kitu alichokisikia na askari waliondoka
naye wakiwa na lengo la kwenda kumkamata
Jackson kwa kuhusika na mauaji.
Teski aliyokodi Robert ilienda kusimama nje
ya geti la nyumba ya Jackson, kulikuwa na
kundi kubwa la watu maeneo hayo. Mara
baada ya kumlipa dereva wa gari hilo
alishuka na kujichanganya na watu hao “du!
yani jamaa amejiua… aah! hii kali kaka…”
alisikika mmoja wa watu waliokuwapo eneo
hilo na kumfanya Robert aliyekuwa na hasira
kuuliza swali “nani kajiua na kwa nini….”
“Aah.. Mr Jackson Samola amejipiga risasi
kichwani…” alijibu mmoja wa watu hao.
Robert alianza kulia kwa sauti kama na yeye
alikuwa mfiwa wa tukio hilo, lakini hiyo yote
ilitokana na hasira alizokuwa nazo. Baada ya
dakika kadhaa askari walifika eneo hilo na
kukamilisha taratibu zote zilizohitajika.
Hatimaye Geofrey na Magreth walizikwa mjini
Moshi eneo ambalo baba yake Magreth
alizaliwa. Hiyo yote ilitokana na ombi la
Robert aliyependa watu hao wawekwe karibu
ingawaje hawakuwa katika ndoa. Jambo hilo
lilikuwa la kusikitishwa hasa kwa watu
waliopata kisa cha Magreth na Geofrey.Baada
ya maombolezo ya msiba huo Robert
alipanga safari tayari kwa kurudi na
mchumba wake Marekani kuendeleza
biashara zake. Siku moja kabla ya safari
alipigiwa simu na askari waliomhitaji, alitii
agizo hilo na mara baada ya kufika kituo cha
polisi alipewa ujumbe mfupi ulioandikwa
kwenye karatasi ambao Mr Jackson aliandika
kabla ya kujiua alianza kwa kuusoma
“…nilikuwa mpumbavu kwa kupingana na
mkono wa sheria ya nchi yangu, kwani sheria
ikiamua inapaswa itekelezwe lakini nilipinga
adhabu ya kunyongwa aliyopewa kaka na
baba yangu mzee Samola…, mwishoe
walinyongwa. Niliamua kulipa kisasi cha vifo
hivyo kwa James Kibudo na mkewe wasio na
hatia lakini nimesababisha madhara
makubwa kwani watoto wake nao
wananitafuta waniue. Nimeamua kujiua kwa
vile mimi pekee ndiye ‘MUUAJI ALIYEBAKIA’,
hata nikisubiri mkono wa sheria lazima
nitanyongwa na siri zangu
zimeshagundulika.Naomba nusu ya utajiri
wa kampuni ya JAJHO wapewe wanawe
James Kibudo…….” Alimaliza Robert kusoma
ujumbe huo ulioandikwa na Mr Jackson kabla
ya kujiua. “du! sichukui kitu kutoka kampuni
ya JAJHO, sihitaji kuona damu ikimwagika
zaidi, nawaachia kila kitu” alisikika Robert
mara baada ya kutoka kituoni hapo.
Hakuwa tayari kuchukua mali ya kampuni
hiyo iliyokuwa na historia ndefu ya mauaji,
aliona jambo la msingi ni kutochukua kitu na
zaidi biashara zake aliamini zilimtosha.
Baada ya miaka kumi Robert alikuwa tajiri
mkubwa katika jimbo la Illinois, Marekani na
tayari alishaanza kusahau matatizo
yaliyoikumba familia yake miaka kadhaa
iliyokuwa imepita. Tayari alikuwa na watoto
wawili na alikuwa akifurahia maisha ya ndoa
na Annie, kumbukumbu zake zilikuwa
hazimtoki kichwani juu ya kifo cha familia
yake na mchumba wa kaka yake Magreth.
Siku zote katika maisha yake sala zake
alimaliza kwa kusema ‘Mungu Azilaze Roho
Zao Mahali Pema Peponi’.


MWISHO.
 
kidi kudi asante sana aise achana na hao wanaokukatisha tamaa aise
 
Last edited by a moderator:
kid kud asante sana na hongera sana una hazina ya kutosha
 
bado luna haja ya kumalizia story ya U C H U mkubwa. hii ni story lkn uchu ni chiboko!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom