Izato
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 5,311
- 11,414
Kuna madhara makubwa anayoyapatia kiongozi mwenye hatia ya mauaji hata kama ana mamlaka makubwa juu ya wananchi wake. Kuuwa ni dhambi kubwa kwa hiyo basi kuna madhara makubwa ya kisheria, kijamii, na kiroho ama kisaikolojia.
Madhara ya Kisheria
1. Kufunguliwa kesi ya jinai mahakamani.
2. Rekodi ya jinai ya muaji itabakia maisha yote ya muuaji.
Madhara ya Kijamii
1. Kutengwa na jamii kwa kuwa watu watakuogopa na kuepuka kushirikiana na muuaji.
2. Kupoteza heshima mbele ya jamii.
3. Familia za wahanga daima hutafuta fursa ya kulipiza kisasi kwa muuaji
Madhara ya Kiroho na Kisaikolojia
1. Dhamiri inakusuta, kutopata usingizi. Kumbukumbu mbaya zitamfuatilia muuaji mchana na usiku, huku ukajihisi hatia moyoni mwake.
2. Hofu, wasiwasi au kuteseka moyoni.
3. Wauaji hupata "depression" ambayo hupelekea kutamani kujiua na hata kuishia kujiua kabisa
4. Kujitenga na Mungu
Mwanzo 4:10-11
Sauti ya damu ya ndugu yako inanena kutoka katika ardhi. Dhambi inamtenganisha muuaji na Mungu wake kwa Imani yoyote Ile aliyokuwa nayo.
5. Laana ya damu inamuandama na kizazi chake chote
Methali 28:17
Mtu aliyezongwa na hatia ya damu ya mtu, atakimbilia shimoni; mtu asimshike.
Kwa kawaida muuaji huwa anapata hasira za mara kwa mara kutokana kuandamwa na mawazo ya hatia ya mauaji. Kuuwa hakutatui tatizo badala yake inamletea muuaji matatizo zaidi.
Madhara ya Kisheria
1. Kufunguliwa kesi ya jinai mahakamani.
2. Rekodi ya jinai ya muaji itabakia maisha yote ya muuaji.
Madhara ya Kijamii
1. Kutengwa na jamii kwa kuwa watu watakuogopa na kuepuka kushirikiana na muuaji.
2. Kupoteza heshima mbele ya jamii.
3. Familia za wahanga daima hutafuta fursa ya kulipiza kisasi kwa muuaji
Madhara ya Kiroho na Kisaikolojia
1. Dhamiri inakusuta, kutopata usingizi. Kumbukumbu mbaya zitamfuatilia muuaji mchana na usiku, huku ukajihisi hatia moyoni mwake.
2. Hofu, wasiwasi au kuteseka moyoni.
3. Wauaji hupata "depression" ambayo hupelekea kutamani kujiua na hata kuishia kujiua kabisa
4. Kujitenga na Mungu
Mwanzo 4:10-11
Sauti ya damu ya ndugu yako inanena kutoka katika ardhi. Dhambi inamtenganisha muuaji na Mungu wake kwa Imani yoyote Ile aliyokuwa nayo.
5. Laana ya damu inamuandama na kizazi chake chote
Methali 28:17
Mtu aliyezongwa na hatia ya damu ya mtu, atakimbilia shimoni; mtu asimshike.
Kwa kawaida muuaji huwa anapata hasira za mara kwa mara kutokana kuandamwa na mawazo ya hatia ya mauaji. Kuuwa hakutatui tatizo badala yake inamletea muuaji matatizo zaidi.