RIWAYA: Mtumwa wa Ngono

RIWAYA: Mtumwa wa Ngono

I guess pastor Patrick is HIV carrier, Glory atavichukua na kumpelekea Nickson kisha Rukia. Guys will die and leave Sonia in a very terrible life. Finaly Sonia atakuwa dadapoa na kutokea yaliyomtokea Mzee Alex Mwandamo.
 
SLAVE SEX(mtumwa wa ngono)…….(31)
MTUNZI…EMMANUEL F.KWAY
Contact….+255718 862176
AGE….(18+)
ILIPOISHIA.
“Pepo la kiburi lishindwe katika jina la Yesu Shindwa katika jina la Yesu,huna mamlaka ya kunijibisha”
Mchungaji Patrick alizidi kuomba na wenzake wakazidi kulitaja jina la Yesu,Kwa upande wa Nickson hakuihi chochote, alivyozidi kuongea ndipo walizidi kupaza sauti wakisali, wakidhani kwamba wanabishana na pepo.
SONGA NAYO.
“Mchungaji,naomba mniachie niende bwana nina majukumu mengi sana ya kufanya,mimi sina mapepo”
Hilo ndilo kosa alilofanya Nickson la kupaza sauti huku akisimama,wakamtuliza kwenye kiti na kuzid kumshushia maombi,wachungaji wakazidi kuingia ndani kwa nia ya kutoa msaada baada ya kusikia kelele zinazidi!
“Pepo hili sugu Mchungaji,embu mwite Mchungaji Onesmo aje mara moja nayeye”
Wachungaji wakazidi kujazana na baadhi ya waumini waliokuwa kanisani siku hiyo wakisikiliza semina,Nickson akazidi kuombewa ilimbidi tu akae kimnya sababu alishaelewa kwamba akiendelea kupiga kelele wangezidi kumuombea.
“Sasa hivi unajisikiaje?”
Mchungaji Patrick alimuuliza Nickson baada ya kumuona yupo kimnya anawatizama.
“Niko sawa,naombeni niende”
“Hapana Nickson,huwezi kuondoka bila mke wako ni wazi kuwa unahitaji maombezi ya kina.Gloria amenieleza kila baya alilokufanyia hapo nyuma lakini hupaswi kufanya hayo mambo, inakubidi umsamehe”
“Mchungaji siwezi,nishasema”
Gloria aliangua kilio kwa sauti alivyosikia Nickson ametamka sentensi hiyo,akadondoka kwa magoti mpaka miguuni kwa Nickson akatubu dhambi zake zote.
“Nic..ckson mume wangu nisamaheee nakupenda bado, Yule ni shetani tu ali..kuwa nda..ni yangu”
Gloria alilia kwa kwikwi.
“Sio shetani,wacha kumsingizia shetani ni wewe mwenyewe, mara ngapi ulikuwa ukiniomba msamaha kama hivi mimi nakubali,mimi si uliniona fala nakupenda sana,eti”
“Usiseme ivyo Nickson,Mimi ni Gloria wa Tofauti,sio Yule tena”
“Acha unafki,kwanza naomba niondoke.Ahsanteni kwa maombi”
Nickson alivyosimama Gloria akawa ameushika mguu wa Nickson na kumfanya asiweze kutembea, kila alipotaka kujivuta alishindwa,Gloria aliung’ang’ania mguu wa Nickson huku akilia machozi kama mtoto mdogo, ni kweli moyoni alihisi anahitaji msamahaa na alielewa kuwa ni shetani ndiyo aliyempitia, akaapia kuwa hatorudia tena,hata wachungaji pia walikuwa kimnya wametulia wakawa kama watu wanaongalia sinema ya kuigiza tu.
Machozi ya Gloria na jinsi alivyokuwa akiomba msamaha ghafla Nickson akawa amerudisha moyo wake nyuma akaingiwa na huruma,picha ya mtoto wake Sonia ikamjia kichwani dakika hiyohiyo alishaelewa kwamba angeteseka bila ya kupata mapenzi ya Mama,hilo ndilo likamfanya amuinue Gloria taratibu juu ya sakafu!
“Gloria”
Nickson akaita huku akimfuta machozi mke wake akitumia viganja vyake.
“A..be …eee”
“Nimekusamehee mke wangu”
“Haleluyaaaaa”
Wachungaji wote wakakenua meno yao,huo ulikuwa ushindi mkubwa sana kwao.Nickson na Gloria wakakumbatiana, kabla ya kuondoka mchungaji aliomba wasali kwa pamoja wakimshukuru Mungu,baada ya sala fupi Nickson na Gloria wakatoka nje.
“Nickson nakupenda sana,naomba nikuhaidi kwamba sitorudia tena na kwa kukudhihirishia hili nimeamua kumpokea Yesu Kristo awe mwokozi wa maisha yangu,tafadhali naomba nawewe uokoke”
Gloria akawa anamshawishi Nickson ajaribu kulifuata neno la Mungu, hakuelewa kwamba haongei na mtu,mawazo ya Nickson yalisafiri maili nyingi akawa anamuwaza Rukia,ni jinsi gani atalifaidi penzi lake ni kweli alishaanza kumpenda Rukia kupita kiasi.
“Nickson,Nickson nakuongelesha”
“Naam,Naam Mke wangu.Tunaenda nyumbani bwana asifiwe, nilikuwa nakusikiliza hapa. Sawa nitaokoka namimi wala usijali kwa hilo”
Swala la Rukia likazidi kumchanganya, akili yake yote ilihama kabisa akajisahau kuwa yupo barabarani anaendesha gari, japokuwa macho yake yalikuwa mbele,mkono mmoja ulikuwa juu ya usukani huku mwingine akiwa ameweka kwenye kioo ameukunja ameshika tama.
Dakika kumi hazikuwa nyingi wakawa wamefika nyumbani tayari,Wa kwanza kuingia akawa Gloria akakutana na Rukia mlangoni.
“Shikam..o Mama”
“Marahaba za hapa Rukia,jamani ndiyo umenenepa kiasi hiki?”
“Ndiyo Mama,karibu ndani,Shikamoo Baba”
Rukia nayeye alikuwa ana akili ya kuzaliwa, akajiongeza hakutaka kuharibu mambo, japokuwa moyo wake ulijawa wivu ajabu.Nickson na Gloria wakapitiliza mpaka chumbani kwao kisha mlango ukafungwa.
*****
“Ahhhhsssh aaaah Nic….kson ba…si aaaassh ssshsss aaaah mhhh,na…kupenda saaana mmmhh aaahshhhhs”
Sikio la Rukia lilinasa mawimbi,alikuwa mlangoni amelitega na aliweza kusikia jinsi Gloria alivyokuwa akiguna chumbani, moyo ulimuuma kupita kiasi,alishazoea kulala na Nickson chumbani humo,Gloria akawa ameingilia penzi lao ambalo lilikuwa teyari limeanza kuiva.
Alichukia na akatamani kugonga mlango nayeye aweze kuingia ndani.Sauti ya Gloria ilizidi kuamsha wadudu wake.Mambo aliyokuwa akiyasikia ndivyo yalizidi kumuumiza nafsi,akiwa ana kanga moja peke yake nayeye alijikuta anajiingiza vidole ndani ya ikulu yake na kuanza kujishika shika kila sehemu mpaka maziwa yake ili kujiburudisha lakini hiyo haikutosha,
Ivyo ndivyo Rukia alikuwa akifanya kila siku ya Mungu ikifika usiku.Siku zikawa zinaenda mawasiliano aliyokuwa nayo na Nickson yakapungua kwa asilimia sabini,moyoni aliumia akawa anamchukia mno Gloria lakini hakutaka kulionyesha swala hilo waziwazi, alihofia kufukuzwa kazi na bosi wake Nickson.
Siku hiyo asubuhi alivyokuwa akitoka chumbani alikumbana na Nickson korido.
“Nickson”
Rukia akaita kwa sauti ya chini.
“Nini?”
“Mbona unanifanyia ivyo?”
“Nakufanyia nini?”
“Hujui au?mbona hunipi huduma?”
“Si unaona mke wangu amerudi,mambo hayo tuyaache tu”
“Unasema?”
Jinsi walivyokuwa wananong’ona,mfano angepita askari angewakamata hapohapo, hawakutofautishwa na watu wahalifu wanaopanga mikakati ya kuvamia benki kuu!
“Kama ulivyosikia”
“Nina mimba yako Nickson”
“Whaaaat?”(Nini)
Nickson aliuliza kwa kimombo, kuonesha kwamba ameshtuka kupita kiasi.
“Ndio ivyo,nina mimba tayari”
“Unasema una… una sema ukweli?”
“Ndio”
“Itoe,kama kweli itoe, sitaki kabisa mambo ya kuzaa nje ya ndoa”
“Siwezi Nickson”
“Kwanini?Kwanini usiwe…ze..? embu baki nasisi hapa, sasa ukiondoka unadhani itakuwaje hata kama kuna msiba mimi nitatuma rambi rambi Sonia si unajua bado mdogo sana,usiondoke Rukia,Ongea na Ndugu zako kwanza”
Ghafla Somo likabadilika, Nickson akazuga baada ya kusikia mlango wa chumbani kwake umefunguliwa,hakuna mtu mwingine ambaye angeweza kufungua mlango isipokuwa Gloria.
“Sawa!Shikamoo Mama”Rukia nayeye akajiongeza.
Ni kweli aliyetokeza alikuwa ni Gloria,akapita mpaka seblen na kuanza kunywa chai.
“Mama Sonia,mimi naenda! baadaye basi”
“Sawa Mpenzi,baadaye”
“Atakuwa kasikia nini?tulivyoongea na Rukia”
Nickson aliwaza huku akitoka Seblen na kuelekea nje akawasha gari na kutimua mbio mpaka ofisini kwake,aliwaza vitu vingi mno aliwaza kama ni kweli Rukia alikuwa ana mimba ingekuwaje,ilikuwa ni aibu kubwa kumpa ujauzito mfanyakazi wake wa ndani,akavuta picha mpaka kwa mama yake angefanya nini endapo angebaini ukweli huo.
Akatamani ardhi ipasuke aingie ndani ili akimbie aibu.
***
Ni kweli Rukia hakutania, alikuwa amenasa. Tayari alikuwa ana mimba, dalili zilionekana baada ya wiki tatu kupita ili kudhibitisha hilo alitumia kifaa kidogo cha kupima mimba ni kweli alikuwa nayo haikuwa utani,na baba wa mtoto huyo hakuwa mwingine bali ni Nickson bosi wake!kutapika na kulala mara kwa mara kulimfanya Gloria aanze kuhisi hali ya utofauti kwa mfanyakazi wake wa ndani.
“Wewe Rukia”
Siku hiyo saa tano asubuhi Gloria hakukuta chai mezani alivyofungua mlango alimkuta Gloria amelala.
“Abee Mama”
“Mbona sikuelewi siku izi?”
“Hapana Mama”
“Hapana Mama ndiyo nini?unaumwa?”
“Mhh mhhh”
Alitingisha kichwa kukataa.
“Sasa nini tatizo?”
“Hakuna kitu Mama”
“Sasa hakuna kitu mbona sioni chai mezani?alafu Sonia mpaka sasa hivi hujamuogesha,Eiii naongea nawewe”
Gloria alifoka kwa hasira akaacha maagizo kuwa Rukia awe keshapika chai na mtoto awe keshaogeshwa muda huo huo.Kadri siku zilkivyozidi kwenda ndipo hali ya Rukia ilizidi kuwa mbaya, alishikwa na homa kali kupita kiasi lakini alijikaza,alielewa kitendo cha kusema anaumwa angepimwa mimba na alitaka swala hilo liwe siri kubwa.
Siku hiyo ya Jumamosi kila mtu alikuwepo seblen asubuhi, Rukia akawa anaandaa chai akaweka vikombe na Semosi juu ya meza.Ghafla katika hali ya kushangaza alihisi kizunguzungu puu! akadondoka hapohapo mpaka chini,Nickson na Gloria walishindwa kuelewa ni kitu gani kilichomfanya adondoke, walichokifanya harakaharaka wakamchukua na kumpakiza ndani ya Gari,safari ya kwenda hospitali ikaanza mara moja.
“Huyu binti ana mimba ya miezi mitatu”Daktari alitoa majibu.
Nickson alihisi kinyesi kinambana,jasho jembamba lilimtoka, sio kwamba habari hizo zilikuwa ngeni kwake lakini alishindwa kuelewa ataiweka wapi sura yake na jinsi alivyokuwa anaheshimika, mbali na hapo Gloria alikuwa teyari amebadilika na kuwa mke mwema tayari.
“Dokta unasema?”
Gloria akauliza kwa shauku.
“Ana ujauzito”
“Okay sawa”
Gloria akajibu kinyonge,jambo hilo likazidi kumpagawisha Nickson,wote wakatoka kwenye viti na kwenda kumchukua Rukia,kutokana na hali yake kuwa shwari,wakaondoka naye mpaka nyumbani, mpaka hapo Gloria hakutaka kuuliza chochote.Jambo hilo likazidi kumuumiza sana akili Nickson, mawazo tele yakamjaa kichwani kupita kiasi hata siku moja hakumsikia Gloria anazungumzia habari za Rukia, zaidi alimuona akiwa ana habari na Sonia tu.
“Baby”
Siku hiyo Nickson akamuita Gloria wakiwa chumbani.
“Yes Darling”
“Hivi hujawahi kufanya utafiti juu ya huyu Rukia kuhusu mimba yake,mshaongea lolote kuhusiana na hiyo Mimba yake?”
Nickson alipima maji.Badala ya Gloria kujibu alimkata jicho kali la hasira.
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi kway insta@storyzakway
ITAENDELEA.
(kwa hadithi nyingi za kusisimua fuata hii link www.facebook.com/STORYZAKWAY.
 
SLAVE SEX(mtumwa wa ngono)……(32)
MTUNZI….EMMANUEL F.KWAY
Contact…+255718 862176
AGE…(18+)
ILIPOISHIA
“Baby”
Siku hiyo Nickson akamuita Gloria wakiwa chumbani.
“Yes Darling”
“Hivi hujawahi kufanya utafiti juu ya huyu Rukia kuhusu mimba yake,mshaongea lolote kuhusiana na hiyo Mimba yake?”
Nickson alipima maji.Badala ya Gloria kujibu alimkata jicho kali la hasira.
SONGA NAYO.

Jicho la Gloria lilimtisha Nickson akajua teyari mambo yameharibika,lakini hakutaka kulipa jambo hilo kipaumbele akajikausha kama hajui linaloendelea.
“Nickson”
“Naaam”
Gloria alimtizama Mume wake na kushusha pumzi ya uchovu na kuendelea kuongea.
“Unajua kuwa mimi siyo mtoto mdogo”
“Ndio najua Mke wangu”
“Unanipenda?”
“Sana tu”
“Sasa nachokuomba,Rukia sitaki kumuona hapa nyumbani kuanzia kesho,kama kweli unanipenda au kama kweli mimi ni mkeo”
“Rukia anatusaidia sana hapa nyu….”
“Nyamaza Nickson,mimi sio mjinga kiasi hicho,najua hiyo mimba ni yako hilo nalielewa sana kaniambia kila kitu, tafadhali sitaki kumuona hapa nyumbani maana nitamuuwa”
Gloria alitibuka kama kiboko Mtoni,akanyanyuka kwa hasira na kutoka nje.Damu ya Nickson ilimwenda mbio ikasukumiza mapigo yake ya moyo kwa nguvu,akashindwa kuelewa ni kitu gani akifanye kwa wakati huo.Alichoongea Gloria ni kweli alikimaanisha, aliingia chumbani kwa Rukia kwa hasira.
“wewe malaya naomba unisikilize kwa makini,kesho naomba uondoke hapa ndani kabla sijafanya kitu kingine kibaya,kwa usalama wako”
Nickson akawa amefika yupo nyuma ya Gloria anajitahidi kumvuta atoke nje waongee.
“Gloria njoo tuongee”
“Uongee nini sasa namimi?Utaongea nini Nickson?ishatokea maji yashamwagika huwezi kuyazoa,sitaki kumuona Rukia.FULL STOP”
“Gloria”
“SHUT UP NICKSON”
Gloria alizidi kufoka huku akitetemeka kwa hasira kifua chake kikapanda juu na kushuka hakuna siku aliyojaa wivu kama siku hiyo,hakutaka kuelewa chochote alichotaka ni Rukia aondoke mara moja,msimamo wake ukabaki kuwa ivyo ivyo.
Kama masihara, kesho yake Rukia alikuta vitu vyake vipo nje kuanzia nguo mpaka viatu, Gloria alidhamiria kumfukuza kabisa kabisa,hakutaka kuishi na mwanamke mwenye mimba ya Mume wake.
“Unachofanya sio vizuri Gloria”
“Sio vizuri nini?atoke hapa,Rukia ondoka sasa hivi,kama unataka uhai”
Mifuko ya nguo ilizidi kurushwa nje na Gloria,Nickson hakuwa na la kufanya jambo alilolifanya mke wake aliliona ni sawa kabisa,ni kweli alitenda kosa.Hakutaka kuhesabu mangapi aliyofanyiwa na Gloria sababu walishaamua kufungua ukurasa mpya wa mapenzi yao hakutaka kukumbuka lolote lile.
Huo ndiyo ukawa mwisho wa Rukia kufanya kazi kwa Nickson, akaokota mifuko yake huku akilia machozi, akatembea mpaka barabarani ili kutafuta dalaladala, kwa senti mbili tatu za mshahara alizokuwa nazo aliweza kupata usafiri na aliamini kwamba zingemfikisha mkoani kwao, akamzae mtoto wake na kumlea,hakutaka kuitoa mimba hiyo hata kidogo!
***
Maisha ya Gloria na Nickson yakazidi kusonga mbele.Hatimaye Nickson akaamua kuokoka kabisa akaongeza upendo mara dufu kwa mke wake,Miaka ilisogea huku Sonia akizidi kuwa mkubwa,mpaka hapo uzuri wa Sonia ukaonekana machoni mwa Watu,kila mwanamke aliyemuona Sonia alitamani mtoto huyo awe wake,Japo kuwa alikuwa mtoto mdogo lakini alitishia kwa uzuri.Akazidi kuwa mweupe kupindukia,rangi za wazazi wake zilimkaa vizuri.Uzuri wa Gloria na sura nzuri ya Nickson vikachanganyika ndani ya mtoto huyu akawa tetemesho, kila mtu alikuwa anasema yake.
“Mama Shayo,huyu mtoto wako ni mzuri khaaaa,kweli vya kuridhi vinazidi…Macho kachukua kwako Midomo ya Baba yake aisee hii combination nimeikubali,kama mmemuumba nyie”
Muumini mmoja wa Kanisa la Mchungaji Patrick alikuwa akiongea na kumsifia Sonia baada ya kumuona.
“Ni Mungu tu”
Gloria akajibu huku akitabasamu hata yeye alijivunia kuwa na mtoyo mzuri kama huyo,japokuwa yeye vilevile alikuwa keshazaa lakini uzuri wake ulitulia na ndiyo kwanza uliongezeka,kutokana na vipodozi alivyokuwa akivitumia.
Siku hiyo Nickson hakuongozana naye kanisani alikuwepo peke yake,akaingia ndani ya Landcruiser V8 na kumuweka Sonia vizuri kwenye viti vya Nyuma!
“Mamiiiiiiiii…chodaa nataka choooda na aichikrimu”
Sonia alisema na mama yake akatoka Nje kumtafutia mwanaye anachokitaka.
“Mama Shayo”
Sauti hiyo ikamshtua,akageuka nyuma.
“Mtumishi,bwana asifiwe”
“Amina ,Amina”
Muumini mwenzake aliyeitwa MTUMISHI alikuwa pia ni kiongozi wa kwaya kuu ya kanisani hapo.
“Nina maongezi nawewe”
“Sasa hivi?”
“Hapana,nadhani hata baadaye kidogo sio mbaya”
“sawa wacha nikamnunulie mtoto soda,tutazungumza, namba yangu si unayo?”
“Ndio ninayo”
“Aya”
Kitendo cha Gloria kuanza kutembea,kilimfanya Mtumishi aanze kumsindikiza kwa Macho ya kuibia huku akitembea mbele,alikuwa akigeuza shingo yake nyuma mara kwa mara ili amshuhudie Gloria anavyotingisha kwa nyuma,udenda ulimtoka katika hali ya kushangaza akagongana kikumbo na Mchungaji Patrick aliyekuwa mbele yake.
“Bwana asifiwe mchungaji.Nina mawazo mengi sana ala….”
“ULIKUWA ukiongea nini na Mama shayo?”
“Nilimwambia tuonane baadaye,kuhusiana na mambo ya Kwaya,nataka awe mwana kwaya”
“Naomba uje ofisini kwangu”
***
Sonia alizidi kutingisha kwa uzuri kupita kiasi,uzuri wake haukuweza kuelezeka kiwepesi wengi walimtabiria anaweza akawa miss Dunia miaka ya baadaye,nywele zake za singasinga ndiyo ikamfanya azidi kung’aa zaidi na zaidi,alikuwa ana umri wa miaka nane lakini alishaanza kuwa mrembo,hakuna mtu aliyeweza kuamini kuwa kuna watoto kama hao duniani,kila aliyemuona alimbeba.Baba yake alimpenda kupita kiasi, akamgharamia kumtafutia mwalimu atakayekuja kumfundisha mtoto wake nyumbani kwake.
“Mama Sonia,wiki ijayo tunahamia kwenye nyumba yetu ishaisha tayari”
“Ndio nilitaka nikuulize sasa hivi umeniwahi”
“Ndiyo ivyo wiki ijayo,anza kujiandaa”
Hivyo ndivyo ilivyokuwa, wiki moja ilivyokatika wakawa wamehama kwenye nyumba ya kampuni.Ikawa furaha kubwa sana kwa Nickson.Akatoa kanisani fungu la kumi kumshukuru Mungu wake kwa jambo alilomfanyia, aliamini kuwa bila MUNGU asingefanikiwa.Nyumba ikawa imeongezeka kuwa na furaha wote wakafunga macho na kusali.
SIKU ZOTE MCHUNGAJI PATRICK ndani ya moyo wake alitamani vibaya sana kuwa na Gloria kimapenzi na aliamini kwamba muda huo kwake ulikuwa muafaka,haraka akampa cheo kanisani ili iwe rahisi kwake kusafiri naye atakavyo,ivyo ndivyo ilivyokuwa, ghafla akawa kiongozi wa wana kwaya.Mipango ya safari ikaandaliwa na Gloria akateuliwa kwenda kutoa neno katika la kanisa kipentekonste Mkoani Iringa.Mambo yakafanyika haraka, kanisa likatoa shilingi milioni sabini kwa ajili tu ya safari.
“sawa sina neno Mke wangu.Ni kazi za Mungu hizo uzidi kutuombea tu”
“Amen Mume wangu nitafanya ivyo,kila siku ninaiombea familia hii”
Nickson alikuwa nyuma ya kila kitu,hakuelewa jambo lolote na mipango ilivyokwenda, alimuamini mke wake pia na Mchungaji Patrick akamruhusu Mke wake na kumpa kiasi cha shilingi laki tatu kama matumzi ya huko atakapokwenda.
Kesho yake Gloria akawa njiani kuelekea Iringa wakiwa kwenye msafara wa magari ya kanisa.Jioni ya siku hiyo wakafikia katika wilaya ya Kilolo,hapo walipokelewa kwa kuwa walijua ujio wao.WALIPIGA MAOMBI na kumshukuru Mungu kwa kuwa fikisha salama,wakatafuta nyumba za wageni kila mtu akatafuta chumba chake,kulikuwa kuna baridi mno hazikupita hata dakika tano mvua kubwa ikaanza kunyesha.Mchungaji Patrick akazinduka usiku mnene akasimama akagonga mlango wa Gloria.
“Nani?”
“Mchungaji Patrick”
Gloria hakuwa na tatizo akafungua mlango Mchungaji Patrick akazama ndani,japo alishindwa kuelewa ujio huo wa usiku ulikuwa una maana gani,hakutaka kuweka mashaka yoyote sababu alimuamini sana mtumishi huyu wa Mungu.
“Inabidi tuombe,kuna vitu nimeviota vibaya sana,Mungu naona anajaribu kunionesha kitu”
“Sawa tusali”
Hilo ndilo likawa kosa kubwa la Gloria kuyafumba macho yake,Mchungaji Patrick akatoa kitambaa chake alichokinyunyizia madawa makali mno ya usingizi, akampiga nacho Gloria puani huku akijifanya kusali,Kizunguzungu kikali kikamkamata Gloria,kabla ya kudondoka chini akadakwa na Mchungaji Patrick,akamuweka kitandani taratibu akaenda kuufunga mlango vizuri na ufunguo, hakuamini kama teyari yupo Chumba kimoja na Gloria tena wakiwa wawili tu,
kama umeme akaanza kuvua mkanda wake, akatoa nguo zake zote mwilini.Akamvua Gloria nguo zake kisha akapanda kitandani na kuanza kufanya tendo baya na mke wa muumini wake.
****
“Asshss ahhsss ahaaa na..ku..pen..da sana”
Hizo ndizo kelele alizokuwa akipiga Gloria baada ya kuwekwa Mbuzi kagoma, akiwa ameshika moja ya pembe ya kitanda,mchungaji Patrick tayari aliweza kumlanghai na pesa za kanisa,Gloria alivaa vitenge vya Wax vya bei mbaya kutoka Nigeria, akazidi kuwa mzuri akalewa na sifa za kila mtu,
hakukuwa na mtu hata mmoja aliyewawekea mashaka Mchungaji Patrick na Gloria,jambo hilo lilikuwa siri na mara nyingi walisafiri pamoja.Gloria alikuwa amelala kifudifudi Mchungaji Patrick yupo juu yake akavuta mto akauweka chini ya Tumbo la Gloria akawa amebinuka kwa nyuma kama bajaji za india,mambo yakazidi kuendelea huku Gloria akizidi kutoa miguno ya huba,ghafla akabinuliwa na kuwekwa kifo cha mende mguu wake mmoja ukawekwa mabegani mwa Mchungaji Patrick akazidi kukizungusha kiuoni kama sio yeye huku akitoa miguno ya ki utu uzima.

Hayo ndiyo yalikuwa maisha yao kila siku.Kuanzia hapo michango ya kanisani haikuisha waumini walichanga na pesa hizo zilitumiwa na Mchungaji Patrick pamoja na Gloria wakifanya starehe.Mara ghafla akaanza tena kuleta kiburi kwa mume wake, tabia zake zikabadilika, Mchungaji Patrick alimpa bichwa!
“Mke wangu mbona siku hizi sikuelewi?”
“Hunielewi kivipi tena?”
“SASA hivi unatoka wapi?”
“Kanisani”
“Kanisaniiiii?”
“Ndio,Kanisani”
Nickson akatupa macho yake juu ya saa ya ukutani ilikuwa ni saa nane ya usiku.
“Kanisa gani hilo usiku?”
“Wewe jua ivyo,naomba nipite nimechoka tafadhali”
Nickson hakutaka kuhoji tena.Kitu kilichomchanganya akili zaidi usiku huo Nickson, ni baada ya kunyimwa Unyumba, jambo hilo ndilo likamvuruga kabisa,alivyokuwa akimgusa Gloria kiuno, mkono wake ulitupwa mbali.
“Mke wangu”
“Nini?Nimechoka naomba nilale pleaseee niache”
“Mimi nina hamu sana,ni siku nyingi sana ujue tangu uondoke umekuwa bize mno,naomba haki yangu nimezidiwa”
“Nenda kapige puchu chooni leo”
Jibu hilo likamchanganya sana Nickson,alibaki akitetemeka, karoti yake ilikuwa imesimama na kweli alikuwa ana hamu na mke wake kupita kiasi na jinsi alivyokuwa amevalia nguo ya kulalia mishipa ya karoti yake ikawa imekakamaa kupita kiasi akitamani tendo la ndoa,kila alipojaribu kumshika mke wake alikaripiwa!
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi kway insta@storyzakway
ITAENDELEA.
(kwa hadithi nyingi za kusisimua fuata hii link www.facebook.com/STORYZAKWAY.)
 
SLAVE SEX(mtumwa wa ngono)…….(33)
MTUNZI….EMMANUEL F. KWAY
Contact….+255718 862176
AGE….(18+)
ILIPOISHIA.
“Nenda kapige puchu chooni leo”
Jibu hilo likamchanganya sana Nickson,alibaki akitetemeka, karoti yake ilikuwa imesimama na kweli alikuwa ana hamu na mke wake kupita kiasi na jinsi alivyokuwa amevalia nguo ya kulalia mishipa ya karoti yake ikawa imekakamaa kupita kiasi akitamani tendo la ndoa,kila alipojaribu kumshika mke wake alikaripiwa!
SONGA NAYO.

Pamoja na Nickson kutumia nyimbo zote za kumuimbisha akitumia saundi na ujanja wa mjini akitaka kumshika Gloria sehemu ambazo aliamini kuwa ni Udhaifu katika mwili wake lakini wapi!alikuwa anafanya kazi ya kutwanga maji kwenye kinu,Gloria alizidi kuutupa mkono wake mbali,hakutaka kabisa kushiriki naye kimwili,hisia na mume wake hakuwa nazo kabisa katika mwili wake,Nickson alijikaza akajikuta anajikamata mwenyewe,akatoka akatembea na kutoka chumbani ambapo alizama bafuni na kushusha boxa yake,alichokuwa anakifanya alikijua mwenyewe.Baada ya kukidhi haja zake alirudi kitandani na kulala.
****
Ilikuwa ni sherehe kubwa iliyokuwa ikifanyika nyumbani kwa Mchungaji Patrick,baada ya mtoto wake wa kiume kumaliza kidato cha nne na kupasua, alifaulu na kupata alama za juu yaani DIVION I.7, masomo yote alibutua akaweka alama A, Baba yake akamfurahia na ndiyo hiyo siku mama yake alirudi akitokea nchini Israel kuubiri injili,hiyo ikaongeza furaha.Waumini walijazana nyumbani kwa mchungaji Patrick.
“Alex Mwanangu,hongera sana hakika umeweka heshima kwenye ukoo wa Mwandambo,Mungu ni mwema sana.Na nina imani atakuongoza”
“Amen,Baba nimefurahi sana”
“Sasa Sisi wazazi wako tunakupenda,tunakupeleka ukasome Canada mpaka chuo kikuu”
Hayo ndiyo Maneno aliyokuwa akiyasema Mchungaji Patrick Mwandambo,akimpongeza mwanaye.Katika sherehe hiyo pia Nickson pamoja na Mke wake walikuwepo vile vile.Baada ya hapo waliimba nyimbo za kusifu na kuabudu wakimshukuru Mungu kwa kutenda miujiza,ilivyotimu saa mbili ya usiku kila mtu alisambaa kuelekea majumbani kwake.
**
Kwa mara ya kwanza alidhani wenda Gloria alikuwa akiumwa au hakuwa na hamu na tendo la ndoa lakini haikuwa ivyo,kila siku alimsihii mkewe aweze kushiriki naye, kila ilipofika usiku lakini alichomolewa na jibu la Gloria likawa ‘nimechoka sijisikii’ Nickson alivumilia lakini pia aliumia moyo kupita kiasi,hakutaka swala hilo alifumbie macho,ilivyofika Jumapili akamfuata mchungaji ofisini kwake baada ya ibada ya asubuhi kuisha ili kumueleza kila kilichotokea kwenye ndoa yake,hakuona aibu yoyote.
“Itakuwa labda pepo baya linamsumbua sana,yuko wapi kwani?”
Mchungaji alisema,akajifanya hajui kinachoendelea.
“Yupo hapo nje”
“Mwite hapa niwaombee”
Nickson akasimama na Kutoka nje,baada ya dakika mbili akaingia na Gloria ofisini.
“Mama Shayo,una tatizo gani na mumeo?”
Hilo ndilo swali la kwanza kulitupa,jinsi Mchungaji Patrick alivyojikausha haikuwa rahisi kwa Nickson kubutuka,alikuwa nyuma ya pazia!
“Abee Mchungaji,mbona sijafanya kosa”
“Sio Kweli,sijapendezwa na tabia zako,jirekebishe nyie ni wanandoa,nimeambiwa na mumeo kuwa unamnyima haki yake,mpaka amekuja kushtaki hapa ujue amekuvumilia sana”
Gloria akashindwa kuvumilia maigizo hayo,akajikuta anacheka bila kutegemea.Pamoja na Kucheka Mchungaji Patrick alijitahidi kujikausha.
“Mama Shayo unacheka?”
“Ha ha haaaa,nyie mnanifurahisha sana,eti nini?”
“Unasumbuliwa na mapepo wabaya sana,wamekufunga bila kujijua”
Hapo hapo mchungaji Patrick alisimama na kuanza kushusha maombi kwa wanandoa hawa,akajifanya kunena kwa lugha.
****
Tangu siku hiyo Ndoa ya Nickson ikawa shwari,akawa anapewa unyumba kama kawaida akazidi kumuamini mchungaji Patrick,akashindwa kwa namna gani amrudishie fadhila.Siku hiyo alivyotoka tu ofisini kwake akiwa mwenye furaha badala ya kwenda moja kwa moja nyumbani kwake yeye alinyoosha mpaka kanisani bila hata kumpigia simu kama alivyokuwa anafanya siku zote.
Kwa furaha aliyokuwa nayo akajikuta anaingia bila kupiga hodi ndani ya ofisi ya Mchungaji Patrick.Boxi la Vidonge vilivyokuwa mezani vilimshtua sana,japokuwa hakuwahi kuchukua masomo ya sayansi lakini alivijua vidonge ivyo hutumia watu wenye maambukizi ya ugonjwa hatari wa Ukimwi.Moyo wake ukamuenda mbio hakutaka kuchukuchua mawazo yake moja kwa moja kwamba vidonge ivyo anatumia Mchungaji Patrick.
“Shayooo”
Mchungaji Patrick alishtuka baada ya kutokeza ndani ya chumba kingine akachukua kiboxi cha dawa hizo na kuziweka kwenye droo lake.
“Mungu ni mkubwa sana,kuna mtu leo hapa nimemponya ugonjwa hatari wa Ukimwi,amenishukuru sana.Mwacheni Mungu aitwe Mungu”
Maneno aliyoongea mchungaji Patrick yakahamisha mawazo ya Nickson,akaaacha kufikiria vibaya,akayapuuza.
“Vipo leo mbona ghafla sana?”
“Leo nina furaha sana,mke wangu amebadilika sana,sina cha kukupa leo nimekuja kumtolea bwana Fungu la kumi”
“Amen,Amen”
Nickson akatoa bahasha ya kaki yenye pesa ndani yake akamkabidhi Mchungaji Patrick,wakapiga maombi kama kawaida na Nickson akaondoka zake.
*****
“NAKUPENDA SANA FAARIS”
“HATA MIMI LUCI WANGU”
“KWELI?”
“NIAMINI NAYOKWAMBIA”
Sauti hizo zilisikika ndani ya chumba namba 17 ndani ya hotel iliyoitwa Bondeni Hotel iliyokuwa Magomeni,hakuna kilichoendelea zaidi ya kupigana madenda,Luci akasogea taratibu kitandani na kujitupa puu kitandani akalala chali,Bwana Faaris taratibu akamsogelea na kuanza kushusha kimini alichokuwa amekivaa mpaka chini huku akijisogeza taratibu shingoni kwa msichana huyu akatoa ulimi wake na kuanza kuinyonya shingo kimahaba,alivyohakikisha kamtoa nguo ya chini,akapitisha kidole chake mpaka chini kabisa akaanza kufanya kama anapima oil taratibu mno.Kitendo cha kidole kuingizwa ndani ya Pango Luci alianza kukizungusha kiuno chake taratibu mno huku akionesha ushirikiano,jinsi alivyohema ilionekana kabisa alihisi raha za ajabu akajihisi yupo ulimwengu mwingime wa huba,mwenyewe akaitoa topu ya juu akitaka mechi hiyo ianze mara moja,hakutaka kuchelewa hata kidogo alikuwa ana kiu kupita kiasi.Hapo ndipo Bwana Faaris alipotoa mkanda wake na kupanda juu ya kitanda,kabla ya kufanya lolote aliipanua miguu ya Luci na kupitisha mdomo wake katikati akatoa ulimi wake na kuanza kudeki bahari,hapo ndipo msichana huyu alipokuwa anahisi moyo wake unaacha mwili,alibaki akiwa ameyafumba macho yake huku akiachama mdomo wake bila kujijua.
****
Nje ya Hotel hiyo ya Gorofa lilitokea gari aina ya CARINA nyeusi na kufunga breki za ghafla,likatimua vumbi ilionekana kwamba dereva huyo alikuwa kama amesahau kitu au alikuwa anataka kufumania,kama dakika tano nzima hakuna hata mmoja aliyeonaka kushuka ndani ya gari.
“Junior shemeji yangu,Mke wangu yupo humu ndani ya hii Hotel,si umesema dada yako namsingizia,leo nataka ujionee mwenyewe”
“Sio kweli”
“Wewe si unabisha,leo namuuwa mbele yako,niamini nayokwambia”
“Ilagaba”
“Ndio Mimi,siwezi kufanyiwa dharau kiasi hicho,muda mrefu sana nilikuwa nikimchora,kaniambia ameenda Songea,wakati mimi najua yupo hapa,mimi ni mtoto wa Mjini,hawezi kunichezea akili”
Hasira zilimkaba Ilagaba,hakutaka kuamini kama mke wake yupo ndani ya Hotel hiyo chumba namba 17 kama alivyoambiwa na marafiki zake wa karibu,hata yeye hakutaka kuamini lakini alitaka kushuhudia,hakuelewa angemfanya nini mke wake endapo atamkuta ‘Live’ na mwanaume mwingine,akachukua sigara akawasha na kupuliza moshi akavuta tena,kisha akaweka mkono wake kiunoni,alivyoutoa ulikuwa umeshika bastola.Jinsi alivyompenda Mke wake haikuwa rahisi kuelezea kwa maandishi.Junior Shemeji yake mdogo wake na Luci aliyekuwa pembeni, kijasho chembamba kilianza kumtoka kuanzia hapo hakutaka kutia neno lolote,Mguu wa kuku ulimtisha!
Giza lilivyoanza kuingia,Ilagaba akafungua mlango wa gari,kabla ya kufunga mlango akaingiza shingo ndani.
“Twende”
Kilichomtisha zaidi Junior ni baada ya kumuona Shemeji yake anachukua magazine nyingine chini ya kiti tena iliyojaa risasi,akatetemeka kupita kiasi,akashuka bila kutegemea.
“Wewe dada,hapo hapo ulipo inuka kwa usalama wako”
Msichana mdogo wa mapokezi almanusura akojoe ,alikumbana na mdomo wa bastola.
“Pe..sa hiz..i hapa kaka,hizi hapa ndio kwan…za nina La..ki ta…”
“Sitaki pesa,nataka unipeleke chumba namba 17 sasa hivi”
Msichana wa mapokezi,hakutaka kubisha akanyoosha mpaka mlangoni na kugonga mlango huku bastola ikiwa shingoni kwake,japokuwa Ilagaba alielewa anafanya jambo lililokuwa kinyume na sheria lakini hakujali.
“Ngo ngoo ngooo”
Msichana wa mapokezi aligonga mlango chumba namba 17.
Kwa kuwa Luci alikuwa bafuni anaoga ilimbidi Faaris atembee karibu kabisa na mlango.
“Naniii?”
“Muhudumu,fungua mara moja”
“Mbona ivyo,tupo kwenyew starehe zetu bwana”Maneno hayo yakazidi kumtia hasira Ilagaba,akatamani kuvunja mlango.
Bila kujua lolote Faaris alitembea mpaka kwenye kabati na kujizungusha taulo kiunoni,akafungua mlango,akakumbana na sura iliyokasirika bila kupiga kelele alipigwa ngumi akaingia nayo ndani.
“Yuko wapi Mke wangu?”
Ilagaba aliuliza na moja kwa moja akaingia bafuni,akamkuta mke wake anaoga,akazama ndani.Huo ndiyo ulikuwa upenyo wa Faris,kama Swala akasimama akatoa nduki,akaogopa kutoka nje akatafuta chumba kilichokuwa karibu na hapo ili ayaokoe maisha yake,akajikuta ameingia ndani ya chumba kingine.Akakumbana na watu wanafanya mapenzi.
“Kijana vipi?”
Mwanaume aliyekuwa juu ya Mwanamke wanafanya Ngono alikurupuka,kitendo hicho kilimshtua hata msichana aliyekuwa chali kifo cha mende.
“Shemeji Gloriaaaaaa”
Faaris hakuamini kuwa msichana huyo ni Gloria,alivyomuangalia vizuri mwanaume aliyekuwa ameduwaa aligundua kuwa ni Mchungaji Patrick,sura hiyo aliweza kuitambua sababu ya kumuona mara kwa mara kwenye televisheni.
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi kway insta@storyzakway
ITAENDELEA.
(kwa hadithi nyingi za kusisimua fuata hii link www.facebook.com/STORYZAKWAY.)
 
SLAVE SEX(mtumwa wa ngono)………(34)
MTUNZI…EMMANUEL F.KWAY
Contact….+255718 862176
AGE…..(18+)
ILIPOISHIA.
“Shemeji Gloriaaaaaa”
Faaris hakuamini kuwa msichana huyo ni Gloria,alivyomuangalia vizuri mwanaume aliyekuwa ameduwaa aligundua kuwa ni Mchungaji Patrick,sura hiyo aliweza kuitambua sababu ya kumuona mara kwa mara kwenye televisheni
SONGA NAYO.
Mapigo ya moyo ya Faaris yalimdunda kupita kiasi,moyo wake ukataka kutokeza nje ya kifua, mpaka hapo hakuamini kama ameponea chupchup kwenye tundu la sindano,jasho jingi lilimtoka mwilini akahisi nguo yake ya ndani ina majimaji bado hakuelewa kuwa ni mkojo au jasho.
“NIPELEKE AMEINGIA CHUMBA GANI?”
Sauti ilifoka kutokea nje ya korido ikafanya Faaris azidi kutumbua macho yake mbele, akataka kuingia chini ya uvungu mchungaji Patrick akamzuia.
“Vipi?”
“Baba Mchungaji,naomba uniombee nataka kutubu dhambi zangu zote leoleo”
Faaris aliongea harakaharaka kwa hofu huku akitetemeka kama mtu mwenye homa kali ya usiku.
“Tatizo lako nini?”
“Naomba unifiche kwanza”
“Kwanini?”
“Mchungaji nitwakwambia,okoa maisha yangu”
Faarisi alililia uzima,kuonekana kwake ndani ya chumba hicho kilimaanisha kifo chake tena kibaya cha maumivu ya kupigwa risasi,bastola aliyoiona ilimtisha,aliomba dua zote anazozijua yeye kwa Mungu wake huku akizidi kusisitizia mchungaji ayakoe maisha yake.
“HODI HUMU”
Sauti hiyo kubwa iliyojaa hasira ikamfanya Faaris tumbo limuume, hakuelewa kama ni tumbo la kuharisha au la uwoga wa kifo!Mchungaji Patrick alimtizama Faaris kabla ya kuuwendea mlango.
“Njoo huku”
Harakaharaka akaingizwa bafuni.Mlango ukafunguliwa Ilagaba akasimama huku akiwa na bastola mkononi mwake amejawa na hasira kali mchungaji akaogopa na hofu ikamtanda, Gloria ndiyo usiseme.Hali hiyo ilimtisha mno.
“Kuna mwizi namtafuta,yuko wapi?”
Ilagaba aliuliza huku akitaka kupitisha kichwa ndani.
“Mwizi?huku hajaingia mtu”
“Embu nipishe niingie ndani,kabla sijafumua huo ubongo wako haraka sana,kaa kando,Hunisikii?”
Mchungaji hata yeye alitamani amtaje mtu aliyemficha,hapo hapo alisali vile vile akaanza kujuta,Ilagaba akazama ndani akaanza kuangalia huku na kule akainama akachungulia uvunguni,akatembea mpaka kwenye makabati na kufungua.
“Bafuni kuna nani?”
Hilo lilikuwa swali kutoka kwa Ilagaba aliyekuwa ameshika bastola huku akioneshea bafuni.
“Nauliza hivi bafuni kuna nani?”
Kila kitu kilichokuwa kinaendelea nje Faaris alikisikia,jasho lilimtoka hakuna kitu alichowaza zaidi ya kifo, akajuta kutembea na mke wa mtu,akatizama choo cha kukaa kilichokuwa mita mbili mbele yake na kuanza kupiga hesabu za kuingia,ukweli ni kwamba upana wa tobo la sink hilo lilikuwa dogo kuliko mwili wake lakini akili yake ilimtuma aingie na kujificha ndani ya sink la maji machafu lililotumika kwa haja kubwa,Katika kujishauri kwake akasikia kitasa cha chooni kinazungushwa,hapo ndipo alihisi tumbo la kuharisha linambana aliingia Ilagaba akiwa na bastola mkononi,akiwa anamtizama kwa hasira.
“Simama mwenyewe kwa usalama wako,SIMAMA, wewe si hodari wa kuchukua wake za watu,sijakwambia upige magoti, inuka”
Faaris alikuwa kama mtu aliyetoka kuoga akanyong’onyea na kuwa kama kifaranga cha kuku kilichomwagiwa maji,alijikuta akipiga magoti huku akiiweka mikono yake kifuani kama mtu anayesali.
“Ndugu ya…ngu mimi mimi ni binadamu mwe…nzio,na.omba tuon.ng.e ili tu..”
Kabla ya kumalizia sentensi alipigwa teke la kifua akadondoka juu ya malumalu chali,Taulo likaruka pembeni.Ilagaba akamuinua na kutoka naye nje ivyo ivyo akiwa ana boxa yake,akamburuza wakapanda naye ngazi mpaka gorofa ya juu namba ishirini na moja.Walivyofika juu Faaris akasimamishwa.
“kacha kacha”
Ilagaba akakoki bastola yake na kumtizama Mbaya wake.
“Chagua kitu kimoja kati ya hivi,nikutie risasi ya kichwa au ujitupe gorofani mwenyewe dakika moja nakupa”
Kwa Faaris ilikuwa vigumu kutoa majibu kwa wakati huo,kila alivyotaka kutoa jibu alijikuta analia machozi,Kutokana na hasira alizokuwa nazo Ilagaba aliamini kuwa kifo ni halali yake.
“Blazza nisameheeee sisi ni wana..ume ni ka..ma ndugu”
Ilagaba hakuongea alimvuta Faaris na kuikandamiza bastola shingoni kwake mpaka walipofika kwenye ukingo,kichwa cha Faaris akaweka kichungulie chini.Akaona jinsi magari yanavyopita kwa chini akazidi kulia kwa sauti.
“WEKA BASTOLA JUU,UPO CHINI YA ULINZI..USIJARIBU KUFANYA KITU CHOCHOTE KILE CHA KIJINGA”
Askari wasiopungua tisa walitanda eneo hilo wakiwa na mitutu mkononi tayari kwa kufyatua risasi endapo Ilagaba ataenda kinyume na matakwa yao.Kwa hofu ya kushambuliwa na risasi Ilagaba akashusha bastola chini hapo hapo akapigwa pingu,hiyo ndiyo ikawa ponea ya Faaris.
*****
“HALLOOO”
“YES NANI?”
“FAARIS”
“FARIS… FARIIIS YUPI?”
“FARIS AMIR”
“AAH AH AH AH,ulikuwa wapi miaka yote nakutafuta swaiba wangu,hupatikani”
“Maisha Nickson,maisha si unajua mjini hapa mchaka mchaka”
“Upo wapi sasa hivi?”
“Mimi nipo kijiweni sasa hivi,nishatoka job”
“Aise siku nyingi sana,nitakuona lini?”
“sijui kwa kweli”
“Njoo kesho basi home,au?”
“Keshoo?kesho lini?”
“Jei Mosi”
“Sawa kesho nitatimba,kuna mambo nataka kuongea nawewe”
“Poa kesho basi”
Simu ikakatwa.Kesho yake asubuhi kama walivyohaidiana kukutana na Nickson ili waongee mambo mengi na ndivyo ilivyokuwa.Faaris akafika nyumbani kwa rafiki yake asubuhi ya saa tano akamkuta Nickson kibarazani anasoma kitabu kilichoandikwa BIKIRA YANGU,ilionekana kilikuwa kimemteka kupita kiasi.
“Nickson”
Faaris aliita huku akikaa pembeni ya kochi kubwa lililokuwa pembeni,lakini Nickson aliitikia na kuendelea kuzamisha macho yake kwenye kitabu.
“Naona kitabu kimekuweka bize sana”
“Ahh tangu jana,hiki kitabu kimeniteka sana aisee,huyu mtunzi aliyetunga hiki kitabu aise ni ametulia sana,huyu Catherine jamani….”
“Kinahusu nini kwani?”
“Mapenzi tu na maisha haya tunayoishi”
Nickson akakunja kurasa aliyoishia kuisoma ya kitabu alichodai kuwa kimemteka hisia zake ili baadaye aendelee.
“Sema kaka”
“Bwana mimi sikai sana,si unajua mimi sikai na kitu mdomoni alafu sipendi kuona vitu vibaya vinaendelea nikavifumbia macho”
“Nambie Faaris”
“Kwanza shemeji yupo?”
“Ametoka,yupo kwenye maombi si unajua siku hizi bila Mungu mambo hayaendi,nawewe inakubidi uokoke”
“Ni vizuri sana,Anasali kanisa gani?”
“Kwa mchungaji Patrick”
Faaris alimtizama rafiki yake kwa macho yaliyojaa huruma alimsikitikia kwa kuwa hakuelewa lolote linaloendelea,alikuwa nyuma ya mambo yote,hakuelewa ni kwa namna gani aanze kumpa mkanda mzima.
“Nickson”
“Nambie Faaris,kwani vipi?”
“Fanya uchunguzi Mkeo na huyo mchungaji Patrick,hakuna lolote hapo wanafanya ushenzi”
“Ushenzi kivipi?”
“Kwa macho yangu niliwakuta chumba kimoja wapo uchi wa mnyama,wanafanya mambo ya ajabu”
Nickson aliganda na kumtizama rafiki yake,hakuongea kitu kwa kama sekunde tano nzima akijaribu kuchanganua vitu ubongoni.
“Faaris mdogo wangu,mbona unakuwa huwaeshimu viongozi wa dini.Umefika mbali sana,wewe dini gani?”
“Mimi muislam lakini nayokwa…”
“Hapana umevuka mipaka,unamkufukuru Mungu,siwezi kukubaliana nawewe”
Nickson alikataa katakata kuamini kwamba Mchungaji aliyemuamini kuwa anatembea na mke wake,jambo ambalo hakutaka kuliweka kichwani hata siku moja.Kila Faaris alipotaka kumueleza ukweli Nickson alimkatisha na kumpa mistari ya Biblia.Alivyoamini yeye ni kwamba Faarisi ana mapepo tena mabaya yanayotaka kumgombanisha na mchungaji wake,Faris hakuwa na namna nyingine ya kufanya aliaga na kuondoka zake.
****
“ULISEMA UNANIPENDA?”
“NDIO”
“NIMEOLEWA LAKINI”
“MIMI SIJALI,HATA KAMA UNA MUME NJOO NIKUPE RAHA YA NDOA HATA MIMI NINA MKE PIA”
“SAWA BASI,UNAYAWEZA AU NDIYO UNIPAKE PAKE TU SHOMBO UNIACHE”
“MIMI NI MZIKI MNENE”
“MBALI NA MZIKI MNENE UNA NGAPI WEWE?”
“NGAPI KIVIPI?”
“UNA SHILINGI NGAPI MIMI NIJE NIKUPE PENZI?”
“ELFU ISHIRINI”
“MIMI SIO MWANAFUNZI,SIPOKEI PESA ZA MADAFU”
“UNATAKA NGAPI?”
“WEKA LAKI TANO”
“LAKI TANO?”
“NDIO SIKU MBILI”
“NA MUMEO?”
“WEWE NIACHIE MIMI”
“SAWA KESHO ASUBUHI TUWASILIANE”
“POA”
“USIZINGUE LAKINI”
“USIWAZE”
Kitu kama mkuki wenye moto ulitua ndani ya moyo wa Nickson ukazama ndani na kutokea mgongoni,alihisi mwili wake umepigwa na ganzi baada ya kusoma meseji za mke wake Gloria kwenye simu,alichoka akili.
Alivyoangalia namba iliseviwa MAMA UPENDO MAOMBI alijua kabisa ilikuwa ni zuga ya Gloria.Mkono wake ulitetemeka kama mtu aliyepigwa na shoti ya umeme jasho likazidi kumtoka hakuelewa ni kitu gani akifanye.Alivyosikia Gloria anatoka bafuni aliirudisha simu haraka haraka juu ya meza na kufumba macho yake akajifanya amelala.
Gloria akasimama mbele ya kioo huku akijipangusa mwili wake uliokuwa una maji.Alimtizama Nickson aliyekuwa amefumba macho yake amelala akatembea taratibu mpaka kwenye simu yake na kuendelea kuibonyeza akiendelea kuchat.
“Baby si ulale,unachati na nani usiku wote huu?”
Nickson alitupa swali huku akimtizama Gloria.
“Ohh alafu nimesahau kukwambia mume wangu,hapa nachat na Mama upendo,kesho tunaenda kwenye usharika mwingine kufanya maombi huko Tanga,ameniomba sana niende kesho,tutalala huko mpaka kesho kutwa hapa ndio ninamjibu kama nitaenda,ila nimeona kwanza nikuombe wewe ruksa”
Gloria alizungumza,kwa nia ya kujitetea hakuelewa kuwa Nickson anajua kila kitu.Alizidi kuongea mambo ya uongo huku Nickson akizidi kumsikiliza akashindwa kuelewa amfanye nini mwanamke huyu mpumbavu!
Sasa unaweza kusoma hadithi za mtunzi kway insta@storyzakway
ITAENDELEA.
(kwa hadithi nyingi za kusisimua fuata hii link www.facebook.com/STORYZAKWAY.)
 
Sorry guys, nimekosea kupost, sehemu ya 31 na 32 nazipachanisha. na 33.
 
I guess pastor Patrick is HIV carrier, Glory atavichukua na kumpelekea Nickson kisha Rukia. Guys will die and leave Sonia in a very terrible life. Finaly Sonia atakuwa dadapoa na kutokea yaliyomtokea Mzee Alex Mwandamo.
Slow down,unatumalizia utamu....
 
Ili uwe free kuGlorifika, huh😀😀
hahahahahaha wala sita glolifika kama Rukia tu haahahaha mtindo ni huu tu kila cku jioni kama tamthilia ya telemundo, watu wapo busy kwenye TV na mimi nipo busy na simu yangu mtumwa wa ngono hahahaha
 
Nick sasa ifike pahala awe mwanaume....
 
I guess pastor Patrick is HIV carrier, Glory atavichukua na kumpelekea Nickson kisha Rukia. Guys will die and leave Sonia in a very terrible life. Finaly Sonia atakuwa dadapoa na kutokea yaliyomtokea Mzee Alex Mwandamo.
Sawa kabisa.. unajua ku predict
 
Ila izoba wa nick mm hapana ningesha chinja mtu
 
Yani Nick unanichefua.... umemuacha Rukia kwnda kulihangaikia hilo guberi..!
 
Back
Top Bottom