Marilyn Monroe
Member
- Apr 2, 2020
- 80
- 167
SEHEMU YA 49
DAH, Wapi Jeff Bhijhajha...mzee wa mapama?
“Ulijiona una bahati sana ulipoponea chupu chupu siku ile tulipolipua lile gari la magereza kule Dar, eeenh?” Don alizidi kumuuliza huku bado akiwa amemlengeshea ile bastola.
Bado Jaka alikuwa amepigwa na butwaa.
“Halafu ukatutoka tena kwa namna ya ajabu kabisa pale darajani Manzese…” Don alizidi kumsimanga, na alipofikia hapo aliguna na kutoa sauti ya mfyatuko wa ulimi, kisha akaendelea, “…ila kwa hapo lazima nikupe sifa aisee…lile lilikuwa ni tendo la mwaka Jaka. Sijui kwa nini hujawa miongoni mwetu wewe, ungetufaa sana…sijui kama nitaona tena tendo la kudiriki kama lile!”
Sasa Jaka alianza kutembeza akili yake haraka haraka kutafuta namna ya kujinasua kutoka kwenye mtego ule, ingawa alijikubalisha kuwa hakika pale alikuwa amepatikana. Alitembeza macho huku na huko mle ndani kwa taharuki.
“Hebu fanya lililotuleta tuondoke, bwana!” Yule mwenzake alimhimiza, lakini Don bado alikuwa anataka kumpa Jaka maneno yake kabla hajamuua.
“Halafu ukawatoka vibaya sana vijana wetu wengine waliokukurupusha usiku ule ulipotaka kurudi nyumbani kwa mama yako baada ya kututoroka sisi kule darajani…Mungu wangu, Jaka! Yaani hadi leo wale vijana hawaelewi uliwezaje kuwaacha kizani namna ile!”
“Bosi nauweka bwana, akh!” Puzo alimkoromea tena mwenzake, na hapo hapo Jaka naye akaongea.
“Kwa…kwani nyie mnataka nini hasa kwangu?”
“Funga bakuli lako!” Don alimfokea, kisha akaendelea, “Sasa sijui leo umetuandalia mbinu gani ya kututoka…maana ulitaka kujiona mjanja sana ulivyonusurika kutawanywa vipande vipande kwa bomu pale sokoni…”
“Ha! Kumbe ni nyie? Yaani kweli mlikuwa tayari kuua na watu wengine wasio na hatia…?”
“Shut Up!” Don alimfokea tena na kumsogelea pale mezani kwa hatua moja kubwa huku bado akimlengeshea ile bastola. “Ulifikiria ni nani wengine, eenh? Huwezi kutukimbia namna ile halafu utegemee kuishi kwa amani tu…”
“Kwa nini…”
“Tulia kimya! Sasa umeshagundua kuwa huwezi kutukimbia? Nataka ujue hivyo kabla hujaaga dunia leo hii!”
“Don…hatuna siku nzima na hatukuja kutoa risala hapa! Fanya tuondoke!” Puzo Vurumai alimhimiza mwenzake na hapo ndipo Jaka alipojua jina la kila mmoja kati yao.
Hapo Don Sibazosi alimwamuru Jaka asimame na atoke nyuma ya meza ile. Jaka alitekeleza huku akiwa amenyoosha mikono yake juu, mwili ikimtetema. Don Sibazosi alimuwekea mdomo wa ile bastola kwenye paji la uso.
“Omba sala yako ya mwisho, sukununu we!” Alimkemea kwa hasira.
“Sala za nini lakini Don? Muwashe tutambae bwana…” Puzo alimfokea mwenzake na Jaka akafumba macho kwa woga huku akijua kuwa alikuwa anakabiliana na mauti.
Na hapo simu yake ya mezani iliita na wote mle ndani walishituka, Don akipeleka macho yake kule ulipotokea ule muito.
Jaka hakufanya ajizi.
Kwa nguzu aliupiga ngumi ule mkono uliokuwa umemshikia bastola naye akajikwepesha pembeni. Ile bastola ikaatupwa hewani huku akimsikia Don akipiga ukelele wa ghadhabu uliofuatana na mhemko wa hamaniko kutoka kwa Puzo. Alijirusha haraka kuiwahi ile bastola huku na Puzo naye akikurupuka kutoka pale alipokuwa amesimama kuiwahi ile bastola. Lakini Don alikuwa mwepesi zaidi.
Alijigeuza kistadi na kumtandika Jaka ngumi nzito iliyojikita sawia katikati ya mwamba wa pua na Jaka alibweka huku akijishika pua na kuinama kwa maumivu. Hapo hapo Don alimkamata ukosi wa koti lake kwa nyuma na kumshindilia futi la uso, na Jaka alitupwa chali mle ndani huku damu zikichuruzikaa kutoka puani na mdomoni. Don alimuinamia na kumkamata ukosi wa koti lake kwa mbele na kumnyanyua kimabavu huku akimtukania mama yake na kumbebesha kichwa kizito cha mdomo na Jaka alilia kama mfiwa huku akienda tena chini kama gunia.
Simu aliacha kuita.
Puzo akarudi kusimama pale pale ukutani kando ya mlango baada ya kuona kuwa Don alikuwa amelimudu pambano, Jaka alibaki akipapatika pale chini kwa maumivu na kiwewe cha kipigo.
“Inuka smart boy…nataka uone hasara ya kufanya mchezo na Don Sibazosi leo!” Mzee wa matabasamu alimtambia huku akimzunguka akiwa amelala pale chini akitweta kwa maumivu.
“Kwani nimewakisea nin…AAAAARGH!” Jaka alianza kuuliza lakini hapo hapo Don alimtandika teke kali mbavuni, kisha yule adui alimkwida na kumnyanyua tena kutoka pale chini, akamsukumia ukutani kwa nguvu, ambapo alijibamiza vibaya na na kabla hajaenda tena chini yule muuaji akamrukia na kumshindilia soli ya kiatu chake kifuani.
Jaka alilia kwa uchungu na kujibwaga sakafuni akiwa hoi.
“Sasa nenda ukasimulie hizo siri ulizoona jehannam, mpumbavu mkubwa!” Don Sibazosi alimwambia huku akitoa kamba ya nailoni kutoka kwenye mfuko wa suruali yake. Jaka alijaribu kuinuka kutoka pale chini lakini alipoinua kichwa tu, Don alimpitisha ile kamba shingoni na kuanza kumkaba kwa nguvu. Jaka alikurupuka na kujitupa na kufurukuta akijaribu kujinasua kutoka kwenye kitanzi kile, lakini Don aliyekuwa amemkaba kwa nguvu, alizidi kukikaza kile kitanzi na kuzidi kumkata pumzi.
Pumzi zilimuisha Jaka. Mapafu yakawa kama yanayomuwaka moto. Uso ukaimvimba. Alitupa mikono yake kwa nyuma akijaribu kumkamata Don lakini hakufanikiwa. Alijiinua kutoka pale chini na kusimama na Don akasimama pamoja naye huku akizidisha kumkaba kwa ile kamba. Alijaribu kupiga kelele lakini hilo halikuwezekana kabisa. Macho yalimtumbuka na mishipa ya kichwa ilimtutumka. Mikoromo ikamtoka na ulimi ukamtutumka na akajua kuwa pale uhai ulikuwa unamtoka.
Hakika hiki ni kifo kibaya kabisa…
Kwa nguvu zake zote alizodhani alikuwa amebakiwa nazo, alijitupa kwa mbele kuliendea dirisha, na akaangukia magoti karibu na lile dirisha, Don Sibazosi akiwa amemng’ang’ania kwa nguvu mgongoni huku akizidi kumkaba kwa ile kamba.
Aaa kwa heri mama…kwa heri Clara!
Akiwa amepiga magoti pale chini ya lile dirisha pana la kioo, aliweza kuwaona baadhi ya wafanyakazi wakipita kule chini lakini hakuweza kuwaita. Alikipigapiga kioo cha lile dirisha kwa matarajio kuwa wale waliokuwa kule chini wangeweza kusikia na kwenda kumsaidia, lakini mikono yake ilikuwa inaishiwa nguvu haraka sana na fahamu zilianza kumpotea.
Ah, jamaa ndio ananiua hivi…!
Alijikurupusha kutoka pale chini na kufanikiwa kusimama tena huku akitweta na akimsikia Don Sibazosi akigumia wakati akizidi kuikaza ile kamba shingoni kwake. Ile kamba ilianza kumkata shingoni na damu ikaanza kumchuruzika.
Ah, Kifo hiki sasa!
Alipiga ukelele na kwa nguvu zilizobakia alitupa juu miguu yake kwa nia ya kukipiga kile kioo na kukivunja, akiamini kuwa tendo hilo lingesababisha wafanyakazi walioko kule chini waje kuangalia kulikoni na hatimaye kumuokoa, lakini Don aliigundua mbinu hiyo na kabla miguu yake haijakifikia kile kioo, alimvuta nyuma kwa nguvu. Miguu yake ikatua kwenye ukingo wa lile dirisha na kukikosa kile kioo. Hapo hapo alijisukuma nyuma kwa nguvu kwa kutumia miguu yake iliyokuwa kwenye ukingo wa lile dirisha na wote wawili walijibwaga kwa kishindo juu ya meza, ile kamba ikamtoka Don naye akipindukia upande wa pili wa meza ile na kumuacha Jaka akiangukia sakafuni baina ya ile meza na lile dirisha. Jaka alikurupuka kutoka pale chini na kutambaa kwa pupa kuelekea dirishani huku akitweta kutafuta pumzi. Aliegemeza mikono yake kwenye kingo za dirisha na kujaribu kulifungua ili apate hewa huku akikohoa na machozi yakimtiririka akiwa amepiga magoti nyuma ya dirisha lile. Lakini mikono yake ilikuwa mizito, hivyo akabaki amejiinamia pale chini ya dirisha huku akitapatapa.
Puzo Vurumai aliyekuwa akifuatilia purukushani ile kwa makini alitoka mbio kutaka kumuwahi Jaka pale alipokuwa, lakini Don Sibazosi alikurupuka kwa ghadhabu kutoka pale alipoangukia huku akitoa tusi kali. Aliwahi kuiparamia ile meza na kudondokea upande ule aliokuwako Jaka hali kamba yake ikiwa mkononi.
Tukio lilifuatia hapo lilikuwa la haraka sana kiasi kwamba Puzo Vurumai aliyekuwa akikimbilia pale walipokuwa, hakuweza kufanya lolote zaidi ya kukodoa macho tu kwa kutoamini.
Don Sibazosi alimrukia Jaka akiwa ametanguliza mikono yake iliyoikamata ile kamba akitaka kumzungushia tena shingoni kwa Jaka, aliyekuwa amemgeuzia mgongo akitweta pale kwenye ukingo wa lile dirisha pana la kioo. Aliposikia vishindo vyake, Jaka aligeuka haraka kadiri alivyoweza huku akijitahidi kusimama wima. Na hapo ndipo alipoiona mikono ya Don ikimuendea usawa wa shingo yake ikiwa imeshika ile kamba. Bila ya kutarajia Jaka alijikuta akiinama kumkwepa, na mikono ya Don Sibazosi ikampitia juu ya kichwa, ile kamba ikiikosa shingo yake na kiwiliwili cha yule muuaji kikamkumba na kumsukuma kinyuma nyuma kuelekea kule dirishani, na hapo bila ya kujua kitakachofuatia, Jaka alimshika Don sehemu za mbele za mapaja yake, akarudisha nyuma mguu wake na kujizuia kwenye ukuta uliokuwa chini ya dirisha lile, na kwa nguvu zake zote alimtupa juu yule adui aliyemuiwa mwepesi kutokana na ile kasi aliyokuwa amekuja nayo.
Don Sibazosi alitupwa hewani huku akipiga kelele akiwa ametanguliza mbele mikono yake, alijiona wazi wazi akikiendea kwa kasi kioo cha lile dirisha. Macho yalimtumbuka na mdomo ukampanika sio kwa kutabasamu tena, bali kwa yowe kubwa la woga.
Ulisikika mlio wa kioo kikipasukia sanjari na ukelele wa Don Sibazosi ukipotelea nje ya lile dirisha lililokuwa ghorofa ya kwanza ya jengo lile.
“Doooonn!” Puzo Vurumai aliita kwa sauti iliyokuwa na mchanganyiko wa mshituko na woga mkubwa, akimuona mshirika wake akipotelea nje ya dirisha lile akifuatiwa na mapande ya vioo.
Na hata pale alipokuwa akimsikia Puzo ikiita jina la mshirika wake kwa hamaniko, Jaka alisikia kishindo kikubwa kutokea chini, nje ya lile dirisha. Aligeuka na kuona uwazi mkubwa pale dirishani ambapo awali kulikuwa kuna kioo. Vipande kadhaa vya kioo kilichokuwa pale dirishani vilibaki vikining’inia kwenye mbao za dirisha lile. Upepo ulivuma kwa nguvu na kuingia mle ndani kupitia kwenye uwazi ule na kupeperusha hovyo makaratasi kutoka pale mezani kwake. Mayowe ya wafanyakazi yalisikika kutokea kule chini naye akalisogelea lile dirisha na kuchungulia kule alipopotelea Don Sibazosi. Aliwahi kuuona mwili wa Don Sibazosi ukijitikisa kwa mara ya mwisho kabla ya kutulia ukiwa hauna uhai. Kutoka pale alipokuwa alihisi kuwa Don Sibazosi alikuwa amevunjika shingo.
Hapo alimkubuka mshirika wake na haraka akageuka nyuma na kumuona Puzo Vurumai akimuendea kwa kasi huku akiwa umekunja uso kwa hasira na dhamira ya mauaji. Na hata pale alipogeuka, Puzo alimrushia kisu kwa mkono wake wa kulia, na hapo hapo alihisi maumivu makali kwenye bega lake la kushoto, kilekisu kikijikita mwilini mwake. Yowe lilimtoka bila kupenda.
Puzo bado alikuwa akimuendea kwa kasi, naye bila ya kufikiri zaidi wala kujali maumivu, alikichomoa kile kisu na kumtupia. Puzo aliyumba na kile kisu kikamkosa, lakini tendo lile lilimpoteza lengo kidogo, na hapo hapo Jaka alijitupa sakafuni kuiwahi ile bastola ya Don Sibazosi. Puzo aliliona tendo lile na akajua kuwa usalama wake ulikuwa mdogo. Aligeuka na kutoka mbio kuuelekea mlango wa kutokea nje ya ofisi ile.Deusdedit Mahunda
Jaka aliikamata ile bastola na kumtupia risasi mbili za haraka haraka, ile Llama Automatic ikitoa sauti kama ya chafya ya mtoto mchanga wakati. Risasi zilichelewa kwani Puzo alikuwa ameshatokomea nje ya ofisi ile, risasi zikijikita ukutani, naye akisikia vishindo vya viatu vyake wakati akishuka ngazi kwa kasi huko nje.
Alijibweteka chini huku damu zikimtoka shingoni na puani hali mikono ikimtetemeka vibaya sana. Muda mfupi baadaye wafanyakazi wenzake walifika na kumkuta akigaragara pale zuliani mle ofisini kwake. Walianza kumpa msaada huku wakihoji kulikoni na Jaka akishindwa kuwaeleza lolote la kueleweka. Baadaye walinzi wa kawaida wa pale ofisini na askari wa jeshi la polisi waliingia, na hapo alijua kuwa alikuwa salama. Alijua kuwa Puzo atakuwa ametoroka bila ya kutiwa mbaroni, lakini kwa wakati ue hilo hakulijali.
Baada ya hekaheka na maswali mengi, hatimaye alitolewa na kukimbizwa hospitali kwa kutumia moja ya magari ya pale ofisini. Huku nyuma, wale askari wa jeshi la polisi waliubebea mwili wa marehemu Don Sibazosi na kuuondoa kutoka eneo lile.
MWISHO
DAH, Wapi Jeff Bhijhajha...mzee wa mapama?
“Ulijiona una bahati sana ulipoponea chupu chupu siku ile tulipolipua lile gari la magereza kule Dar, eeenh?” Don alizidi kumuuliza huku bado akiwa amemlengeshea ile bastola.
Bado Jaka alikuwa amepigwa na butwaa.
“Halafu ukatutoka tena kwa namna ya ajabu kabisa pale darajani Manzese…” Don alizidi kumsimanga, na alipofikia hapo aliguna na kutoa sauti ya mfyatuko wa ulimi, kisha akaendelea, “…ila kwa hapo lazima nikupe sifa aisee…lile lilikuwa ni tendo la mwaka Jaka. Sijui kwa nini hujawa miongoni mwetu wewe, ungetufaa sana…sijui kama nitaona tena tendo la kudiriki kama lile!”
Sasa Jaka alianza kutembeza akili yake haraka haraka kutafuta namna ya kujinasua kutoka kwenye mtego ule, ingawa alijikubalisha kuwa hakika pale alikuwa amepatikana. Alitembeza macho huku na huko mle ndani kwa taharuki.
“Hebu fanya lililotuleta tuondoke, bwana!” Yule mwenzake alimhimiza, lakini Don bado alikuwa anataka kumpa Jaka maneno yake kabla hajamuua.
“Halafu ukawatoka vibaya sana vijana wetu wengine waliokukurupusha usiku ule ulipotaka kurudi nyumbani kwa mama yako baada ya kututoroka sisi kule darajani…Mungu wangu, Jaka! Yaani hadi leo wale vijana hawaelewi uliwezaje kuwaacha kizani namna ile!”
“Bosi nauweka bwana, akh!” Puzo alimkoromea tena mwenzake, na hapo hapo Jaka naye akaongea.
“Kwa…kwani nyie mnataka nini hasa kwangu?”
“Funga bakuli lako!” Don alimfokea, kisha akaendelea, “Sasa sijui leo umetuandalia mbinu gani ya kututoka…maana ulitaka kujiona mjanja sana ulivyonusurika kutawanywa vipande vipande kwa bomu pale sokoni…”
“Ha! Kumbe ni nyie? Yaani kweli mlikuwa tayari kuua na watu wengine wasio na hatia…?”
“Shut Up!” Don alimfokea tena na kumsogelea pale mezani kwa hatua moja kubwa huku bado akimlengeshea ile bastola. “Ulifikiria ni nani wengine, eenh? Huwezi kutukimbia namna ile halafu utegemee kuishi kwa amani tu…”
“Kwa nini…”
“Tulia kimya! Sasa umeshagundua kuwa huwezi kutukimbia? Nataka ujue hivyo kabla hujaaga dunia leo hii!”
“Don…hatuna siku nzima na hatukuja kutoa risala hapa! Fanya tuondoke!” Puzo Vurumai alimhimiza mwenzake na hapo ndipo Jaka alipojua jina la kila mmoja kati yao.
Hapo Don Sibazosi alimwamuru Jaka asimame na atoke nyuma ya meza ile. Jaka alitekeleza huku akiwa amenyoosha mikono yake juu, mwili ikimtetema. Don Sibazosi alimuwekea mdomo wa ile bastola kwenye paji la uso.
“Omba sala yako ya mwisho, sukununu we!” Alimkemea kwa hasira.
“Sala za nini lakini Don? Muwashe tutambae bwana…” Puzo alimfokea mwenzake na Jaka akafumba macho kwa woga huku akijua kuwa alikuwa anakabiliana na mauti.
Na hapo simu yake ya mezani iliita na wote mle ndani walishituka, Don akipeleka macho yake kule ulipotokea ule muito.
Jaka hakufanya ajizi.
Kwa nguzu aliupiga ngumi ule mkono uliokuwa umemshikia bastola naye akajikwepesha pembeni. Ile bastola ikaatupwa hewani huku akimsikia Don akipiga ukelele wa ghadhabu uliofuatana na mhemko wa hamaniko kutoka kwa Puzo. Alijirusha haraka kuiwahi ile bastola huku na Puzo naye akikurupuka kutoka pale alipokuwa amesimama kuiwahi ile bastola. Lakini Don alikuwa mwepesi zaidi.
Alijigeuza kistadi na kumtandika Jaka ngumi nzito iliyojikita sawia katikati ya mwamba wa pua na Jaka alibweka huku akijishika pua na kuinama kwa maumivu. Hapo hapo Don alimkamata ukosi wa koti lake kwa nyuma na kumshindilia futi la uso, na Jaka alitupwa chali mle ndani huku damu zikichuruzikaa kutoka puani na mdomoni. Don alimuinamia na kumkamata ukosi wa koti lake kwa mbele na kumnyanyua kimabavu huku akimtukania mama yake na kumbebesha kichwa kizito cha mdomo na Jaka alilia kama mfiwa huku akienda tena chini kama gunia.
Simu aliacha kuita.
Puzo akarudi kusimama pale pale ukutani kando ya mlango baada ya kuona kuwa Don alikuwa amelimudu pambano, Jaka alibaki akipapatika pale chini kwa maumivu na kiwewe cha kipigo.
“Inuka smart boy…nataka uone hasara ya kufanya mchezo na Don Sibazosi leo!” Mzee wa matabasamu alimtambia huku akimzunguka akiwa amelala pale chini akitweta kwa maumivu.
“Kwani nimewakisea nin…AAAAARGH!” Jaka alianza kuuliza lakini hapo hapo Don alimtandika teke kali mbavuni, kisha yule adui alimkwida na kumnyanyua tena kutoka pale chini, akamsukumia ukutani kwa nguvu, ambapo alijibamiza vibaya na na kabla hajaenda tena chini yule muuaji akamrukia na kumshindilia soli ya kiatu chake kifuani.
Jaka alilia kwa uchungu na kujibwaga sakafuni akiwa hoi.
“Sasa nenda ukasimulie hizo siri ulizoona jehannam, mpumbavu mkubwa!” Don Sibazosi alimwambia huku akitoa kamba ya nailoni kutoka kwenye mfuko wa suruali yake. Jaka alijaribu kuinuka kutoka pale chini lakini alipoinua kichwa tu, Don alimpitisha ile kamba shingoni na kuanza kumkaba kwa nguvu. Jaka alikurupuka na kujitupa na kufurukuta akijaribu kujinasua kutoka kwenye kitanzi kile, lakini Don aliyekuwa amemkaba kwa nguvu, alizidi kukikaza kile kitanzi na kuzidi kumkata pumzi.
Pumzi zilimuisha Jaka. Mapafu yakawa kama yanayomuwaka moto. Uso ukaimvimba. Alitupa mikono yake kwa nyuma akijaribu kumkamata Don lakini hakufanikiwa. Alijiinua kutoka pale chini na kusimama na Don akasimama pamoja naye huku akizidisha kumkaba kwa ile kamba. Alijaribu kupiga kelele lakini hilo halikuwezekana kabisa. Macho yalimtumbuka na mishipa ya kichwa ilimtutumka. Mikoromo ikamtoka na ulimi ukamtutumka na akajua kuwa pale uhai ulikuwa unamtoka.
Hakika hiki ni kifo kibaya kabisa…
Kwa nguvu zake zote alizodhani alikuwa amebakiwa nazo, alijitupa kwa mbele kuliendea dirisha, na akaangukia magoti karibu na lile dirisha, Don Sibazosi akiwa amemng’ang’ania kwa nguvu mgongoni huku akizidi kumkaba kwa ile kamba.
Aaa kwa heri mama…kwa heri Clara!
Akiwa amepiga magoti pale chini ya lile dirisha pana la kioo, aliweza kuwaona baadhi ya wafanyakazi wakipita kule chini lakini hakuweza kuwaita. Alikipigapiga kioo cha lile dirisha kwa matarajio kuwa wale waliokuwa kule chini wangeweza kusikia na kwenda kumsaidia, lakini mikono yake ilikuwa inaishiwa nguvu haraka sana na fahamu zilianza kumpotea.
Ah, jamaa ndio ananiua hivi…!
Alijikurupusha kutoka pale chini na kufanikiwa kusimama tena huku akitweta na akimsikia Don Sibazosi akigumia wakati akizidi kuikaza ile kamba shingoni kwake. Ile kamba ilianza kumkata shingoni na damu ikaanza kumchuruzika.
Ah, Kifo hiki sasa!
Alipiga ukelele na kwa nguvu zilizobakia alitupa juu miguu yake kwa nia ya kukipiga kile kioo na kukivunja, akiamini kuwa tendo hilo lingesababisha wafanyakazi walioko kule chini waje kuangalia kulikoni na hatimaye kumuokoa, lakini Don aliigundua mbinu hiyo na kabla miguu yake haijakifikia kile kioo, alimvuta nyuma kwa nguvu. Miguu yake ikatua kwenye ukingo wa lile dirisha na kukikosa kile kioo. Hapo hapo alijisukuma nyuma kwa nguvu kwa kutumia miguu yake iliyokuwa kwenye ukingo wa lile dirisha na wote wawili walijibwaga kwa kishindo juu ya meza, ile kamba ikamtoka Don naye akipindukia upande wa pili wa meza ile na kumuacha Jaka akiangukia sakafuni baina ya ile meza na lile dirisha. Jaka alikurupuka kutoka pale chini na kutambaa kwa pupa kuelekea dirishani huku akitweta kutafuta pumzi. Aliegemeza mikono yake kwenye kingo za dirisha na kujaribu kulifungua ili apate hewa huku akikohoa na machozi yakimtiririka akiwa amepiga magoti nyuma ya dirisha lile. Lakini mikono yake ilikuwa mizito, hivyo akabaki amejiinamia pale chini ya dirisha huku akitapatapa.
Puzo Vurumai aliyekuwa akifuatilia purukushani ile kwa makini alitoka mbio kutaka kumuwahi Jaka pale alipokuwa, lakini Don Sibazosi alikurupuka kwa ghadhabu kutoka pale alipoangukia huku akitoa tusi kali. Aliwahi kuiparamia ile meza na kudondokea upande ule aliokuwako Jaka hali kamba yake ikiwa mkononi.
Tukio lilifuatia hapo lilikuwa la haraka sana kiasi kwamba Puzo Vurumai aliyekuwa akikimbilia pale walipokuwa, hakuweza kufanya lolote zaidi ya kukodoa macho tu kwa kutoamini.
Don Sibazosi alimrukia Jaka akiwa ametanguliza mikono yake iliyoikamata ile kamba akitaka kumzungushia tena shingoni kwa Jaka, aliyekuwa amemgeuzia mgongo akitweta pale kwenye ukingo wa lile dirisha pana la kioo. Aliposikia vishindo vyake, Jaka aligeuka haraka kadiri alivyoweza huku akijitahidi kusimama wima. Na hapo ndipo alipoiona mikono ya Don ikimuendea usawa wa shingo yake ikiwa imeshika ile kamba. Bila ya kutarajia Jaka alijikuta akiinama kumkwepa, na mikono ya Don Sibazosi ikampitia juu ya kichwa, ile kamba ikiikosa shingo yake na kiwiliwili cha yule muuaji kikamkumba na kumsukuma kinyuma nyuma kuelekea kule dirishani, na hapo bila ya kujua kitakachofuatia, Jaka alimshika Don sehemu za mbele za mapaja yake, akarudisha nyuma mguu wake na kujizuia kwenye ukuta uliokuwa chini ya dirisha lile, na kwa nguvu zake zote alimtupa juu yule adui aliyemuiwa mwepesi kutokana na ile kasi aliyokuwa amekuja nayo.
Don Sibazosi alitupwa hewani huku akipiga kelele akiwa ametanguliza mbele mikono yake, alijiona wazi wazi akikiendea kwa kasi kioo cha lile dirisha. Macho yalimtumbuka na mdomo ukampanika sio kwa kutabasamu tena, bali kwa yowe kubwa la woga.
Ulisikika mlio wa kioo kikipasukia sanjari na ukelele wa Don Sibazosi ukipotelea nje ya lile dirisha lililokuwa ghorofa ya kwanza ya jengo lile.
“Doooonn!” Puzo Vurumai aliita kwa sauti iliyokuwa na mchanganyiko wa mshituko na woga mkubwa, akimuona mshirika wake akipotelea nje ya dirisha lile akifuatiwa na mapande ya vioo.
Na hata pale alipokuwa akimsikia Puzo ikiita jina la mshirika wake kwa hamaniko, Jaka alisikia kishindo kikubwa kutokea chini, nje ya lile dirisha. Aligeuka na kuona uwazi mkubwa pale dirishani ambapo awali kulikuwa kuna kioo. Vipande kadhaa vya kioo kilichokuwa pale dirishani vilibaki vikining’inia kwenye mbao za dirisha lile. Upepo ulivuma kwa nguvu na kuingia mle ndani kupitia kwenye uwazi ule na kupeperusha hovyo makaratasi kutoka pale mezani kwake. Mayowe ya wafanyakazi yalisikika kutokea kule chini naye akalisogelea lile dirisha na kuchungulia kule alipopotelea Don Sibazosi. Aliwahi kuuona mwili wa Don Sibazosi ukijitikisa kwa mara ya mwisho kabla ya kutulia ukiwa hauna uhai. Kutoka pale alipokuwa alihisi kuwa Don Sibazosi alikuwa amevunjika shingo.
Hapo alimkubuka mshirika wake na haraka akageuka nyuma na kumuona Puzo Vurumai akimuendea kwa kasi huku akiwa umekunja uso kwa hasira na dhamira ya mauaji. Na hata pale alipogeuka, Puzo alimrushia kisu kwa mkono wake wa kulia, na hapo hapo alihisi maumivu makali kwenye bega lake la kushoto, kilekisu kikijikita mwilini mwake. Yowe lilimtoka bila kupenda.
Puzo bado alikuwa akimuendea kwa kasi, naye bila ya kufikiri zaidi wala kujali maumivu, alikichomoa kile kisu na kumtupia. Puzo aliyumba na kile kisu kikamkosa, lakini tendo lile lilimpoteza lengo kidogo, na hapo hapo Jaka alijitupa sakafuni kuiwahi ile bastola ya Don Sibazosi. Puzo aliliona tendo lile na akajua kuwa usalama wake ulikuwa mdogo. Aligeuka na kutoka mbio kuuelekea mlango wa kutokea nje ya ofisi ile.Deusdedit Mahunda
Jaka aliikamata ile bastola na kumtupia risasi mbili za haraka haraka, ile Llama Automatic ikitoa sauti kama ya chafya ya mtoto mchanga wakati. Risasi zilichelewa kwani Puzo alikuwa ameshatokomea nje ya ofisi ile, risasi zikijikita ukutani, naye akisikia vishindo vya viatu vyake wakati akishuka ngazi kwa kasi huko nje.
Alijibweteka chini huku damu zikimtoka shingoni na puani hali mikono ikimtetemeka vibaya sana. Muda mfupi baadaye wafanyakazi wenzake walifika na kumkuta akigaragara pale zuliani mle ofisini kwake. Walianza kumpa msaada huku wakihoji kulikoni na Jaka akishindwa kuwaeleza lolote la kueleweka. Baadaye walinzi wa kawaida wa pale ofisini na askari wa jeshi la polisi waliingia, na hapo alijua kuwa alikuwa salama. Alijua kuwa Puzo atakuwa ametoroka bila ya kutiwa mbaroni, lakini kwa wakati ue hilo hakulijali.
Baada ya hekaheka na maswali mengi, hatimaye alitolewa na kukimbizwa hospitali kwa kutumia moja ya magari ya pale ofisini. Huku nyuma, wale askari wa jeshi la polisi waliubebea mwili wa marehemu Don Sibazosi na kuuondoa kutoka eneo lile.
MWISHO