Riwaya: Msako wa mwehu

Riwaya: Msako wa mwehu

SEHEMU-32


Walikuwa wakiendelea kucheza muziki ule kwa mtindo wa kugandana "zero distance" na kwa mahaba makubwa. Laiti ungewaona wanavyocheza kiustadi mkubwa usingekubali kuwa huyu "Maso Maso" ni mfiadini. Kumbe wachamungu wakiwa hadharani tu mbele ya macho ya watu lakini wakiwa sirini wanayajua wao na Mungu wao wanayoyafanya. Yasmine sasa alikuwa amebakiwa na chupi tupu iliyositiri kipochi manyoya chake na chura wake. Huku macho yakiwa yamemtoka "Maso Maso" hayabanduki kuangalia mapaja meupe ya binti wa Kipemba kwa uchu wa fisi.
Alimuweka kwenye wakati mgumu sana Yasmine, huku anabinywa binywa maembe dodo yake, kifuani yaliyochongoka na "Maso Maso". Matiti ambayo yalikuwa yanatomaswa mithili ya mteja anayetaka kuchagua embe bora la kula sio rojo la juisi. Yasmine akaanza kuhema juu juu kama mtu aliyepandisha Jini subiani na kuanza kunena kwa lugha isiyoeleweka. Kipemba si Kipemba, Kichina si Kichina tabu mtindo mmoja. Alikuwa tayari ameshaingia kwenye kumi na nane ya lango la timu pinzani, akiguswa tu kidogo na beki refarii anafunika penati bila ajizi.
"Maso Maso" alishaona dalili zote za kuvikwa taji la ushujaa dakika 90 zikikaribia kuanza za mechi hiyo kali ya kuvunja springi ya meli. Ila hakutaka kuharakisha kuanza kwa pambano, akazidisha mbwembwe na vikorombwezo ili kuleta amsha amsha na mashamu mashamu kwa wachezaji wa pande zote mbili. Akaanzisha uchokozi wa mieleka ya ulimi kwa ulimi akaanza kudendeka nae.
Yasmine akajikuta hana nguvu tena, hawezi kujizuia akamuachia "Maso Maso" awe kama rubani wa ndege na yeye kubaki kuwa maamuma tu, asiyejua ndege rubani anaipeleka wapi na kituo cha Nyegezi kipo wapi na atashushwa kwa mitindo ipi, na wala hakutaka kujua tena, alishakuwa kichaa wa mapenzi.
Tayari alianza kuishiwa nguvu huku vidole vyake Kachero Yasmine vimeanza kutambaa juu ya kufuli alilovaa gaidi "Maso Maso" kuanza kupimisha urefu na saizi ya bakora ya gaidi. "Maso Maso" alivyoona hivyo, akajua tayari kituo cha Nyegezi wanakaribia kufika abiria anahitaji kushushwa. Akambeba mkewe kwa mikono miwili mpaka kitandani akamtupia juu ya uwanja huo wa godoro la "Super Banco Original", uwanja wa tokea enzi za Mababu na Mabibi zetu, ulioleta mabilioni ya watu waliomo ulimwengu hivi sasa. Yasmine alivyotua tu akajilaza kifudifudi huku ameibana miguu wala hatikisiki.
Yasmine alikuwa kama yupo ndotoni, nusu mfu nusu hai, alikuwa amepewa mambo adimu aliyokuwa anayakosa kipindi chote cha miaka 28 ya uhai wake. "Maso Maso" alivyomuona Yasmine kama anataka kupoteza fahamu, akaenda kwenye friza ndogo ya chumbani akachukua vipande virefu vya barafu kama vinne. akaviweka kwenye sahani ndogo akapanda navyo vile vipande kitandani.
Yasmine alikuwa anashuhudia hayo yote lakini anashindwa kuzungumza, alikuwa anaona ni mambo mapya kabisa kupata kutokea machoni mwake, daktari anataka kufanya operesheni ya kumpasua mgonjwa kwa kutumia vipande vya barafu, hajawahi kusikia hii hata kwa mashoga zake wanavyosimuliana huko saluni.
Akajisemea nafsini mwake "ama kweli ufundi wa mapenzi kuzidiana duniani". Alivyofika navyo vile vipande akakibana kipande kimoja kwa ncha ya meno yake ya mbele kisha akaanza kumsugua nacho kuanzia chini ya maoteo ya nywele kisogoni anashuka nacho hadi kwenye mfereji wa uti wa mgongo na kushuka nacho chini karibia na pingili ya mwisho ya uti wa mgongo kisha anapanda nacho tena juu.
Huu mchezo wa barafu wa panda shuka ulisababisha Kachero Yasmine arudiwe na fahamu zake akaanza kujinyonga nyonga na kupwiripwita kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa. "Maso Maso" macho yake yalimwiva na kuwa mekundu kama kavuta bangi, alikuwa mlaini kwa Yasmine huwezi kudhania ni yule anayewanyima usingizi zaidi ya Watanzania milioni 55 hawalali kwa raha, hawali wakanenepa kwa sababu ya ufedhuli wake wa matendo ya kigaidi.
Akalichukua dekio la mdomoni lile linaloonja ladha ya utamu wa chakula na kuanza sasa kupangusa maji ya kwenye kisima kilicholoweshwa tepetepe juu ya chupi ya Kachero Jasmine. Dekio lilipotua tu kwenye antena Kachero Yasmine alishindwa na uvumilivu, alipiga makelele huku akitaja jina "Maso Maso" halisi, "Masoud Masoud My love...Weeeeeh utaniua mtoto wa mwenzio". Jambo ambalo "Maso Maso" lilimshtua na kumfanya asite kuendelea na zoezi la kupiga deki.
"Masikio yangu yanaleta taarifa sahihi au ninaota mbona ananitaja kwa jina langu halisi la Masoud Masoud, amenijulia wapi kwa jina hili wakati jina feki la kufungia ndoa ni Abu Nufeil!" ni swali alilokuwa anajiuliza ndani ya sekunde kadhaa "Maso Maso" bila kupata jibu. Wakati huo huo yupo kwenye fikra hizo simu yake ya upepo ya tahadhari anayoitumia "Maso Maso" kwa dharura ikaanza kupigwa.
Ikabidi anyanyuke kitandani na kwenda kuichukua simu kwa ajili ya kuipokea. "Hallow Hallow...ovaaah....!", ikabidi atoke haraka nje ya chumba ili Yasmine asisikize maongezi yake. Alivyotoka chumbani ikawa nafuu kwa Kachero Yasmine amenusurika kuvunjwa kizinda chake cha ubikira na gaidi "Maso Maso". Kama "Maso Maso" angeendeleza utundu wake angefanikiwa kumla Kachero Yasmine katika usiku huo wa fungate.
Na yeye fahamu zikaanza kumrudia sasa kengele ya tahadhari ikalia kichwani mwake. "Kuna mazungumzo gani ya siri yaliyomfanya hata aache kuendelea na moja ya starehe tamu za dunia!" alijiuliza Kachero Yasmine. "Au wamenigundua kuwa mie ni shushushu hivyo wanampa taarifa?" Akakurupuka haraka kitandani na kukaa, anapanga na kupangua mipango ya kujiokoa kwenye mdomo wa mamba aliojiingiza kwa hiari yake mwenyewe.
Himahima akaenda mpaka pale ilipo sasa sahani ya nyama na sosi ya nyanya. Akachukua ile sosi ya nyanya akafunua chupi yake nyeupe akaminyia sosi ya kutosha tu, kisha akaifunga chupa na kurudi kitandani mbio mbio. Ile anatua tu kitandani hamadi! na "Maso Maso" huyo anarudi chumbani.
Sasa Kachero Yasmine alikuwa na akili timamu anamthaminisha "Maso Maso" bukta yake ilikuwa imetuna kama vile ameficha mguu wa mtoto mdogo mwenye umri wa nusu mwaka. "Aisee...leo mbona chamoto ningekionja, "Maso Maso" ana uume mkubwa utasema amechanjia dodoki..!.Leo huyu angenitoboa kizazi huenda ningekimbizwa Hospitali ya Mkoa ya Bombo, hawa wengine hawatakiwi kufanyiwa majaribu, ukiwabipu wanakupigia" alijiwazia Kachero Yasmine huku akijiona ana bahati sana kuepuka kucheza mechi ya kitandani na "Maso Maso". Alivyoingia ndani ya chumba akaenda moja kwa moja kwenye zile nyama zake za madawa ya kuongeza nguvu za kiume na kuanza kuzishambulia tena.
Alivyotafuna vipande kadhaa vya nyama ile akaanza kuja kitandani alipojilaza Yasmine kama mbogo aliyejeruhiwa risasi na jangili. Yasmine hakutaka tena amruhusu afanye utalii wa mwili wake tena alishaijua shughuli ya "Maso Maso" ni gaidi wa kila sekta.
Alivyotaka kumgusa tu, Yasmine akaaanza kupiga kelele. "Aaaah Aaah nakuf...aaaah tumboo langu". "Maso Maso" akashtuka na kuanza kumsaili tatizo lililompata. "Umepatwa na nini mke wangu mpendwa, nimuite daktari"?.
"Hapana ni ada tu za wakubwa za mwezi, wekundu wa msimbazi wamekuja wamelowesha kiwanja, hamna mechi tena wiki nzima mpaka nijitwaharishe, sasa huwa tumbo linaniuma hiyo hali ikinikuta" alifafanua kwa lugha ya mafumbo ambayo "Maso Maso" alielewa nini anachomaanisna mke wake baada ya kuiona chupi imelowa damu.
Kumbe usilolijua ni kama usiku wa giza, kachezewa picha la kihindi bila mwenyewe kufahamu. Biashara ikawa imeishia hapo kwa siku hiyo. "Maso Maso" akakumbuka kuitwa kwa jina la "Maso Maso" wakati mizuka ya mahanjamu imempanda Kachero Yasmine. Ikabidi amuweke kitimoto kwanini anamuita jina hilo.
Kachero Yasmine akakataa katakata kulijua jina hilo la Masoud Masoud. "Mie mume wangu nakujua kwa jina la Abu-Nufeil na ndio limeandikwa kwenye cheti cha ndoa yetu hilo ulilotaja ndio kwanza nalisikia kwako" alijitetea Kachero Yasmine huku akijilaumu sana kwa uzembe ambao unaweza kumgharimu maisha yake.
Kwa jinsi alivyomaliza viapo vyote vilivyoambatana na vilio feki, "Maso Maso" alimuelewa mkewe akajipa udhuru mwenyewe kuwa huenda alisikia vibaya. Akamuamini akaleta dhana ingine kuwa huenda huyo Masoud aliyekuwa anamtaja wakati anamsugua antena, ni mpenzi wake wa zamani ambaye alikuwa anamfikisha vilivyo.
"Maso Maso" aliaga siku hiyo hiyo kutokana na simu ya upepo aliyopigiwa kuna viongozi wa "Al-shabaab" toka Somalia walihitaji kuonana nae mkutano wa dharura. Ila kwa mkewe aliaga kuna mzigo wa biashara anatakiwa aende kuuangalia Mombasa hivyo hana budi ang'oe nanga usiku huo.
Yasmine akazuga kama na yeye anatamani sana afuatane nae, lakini kiuhalisia alitamani abakie hapo nyumbani ayasome mazingira vizuri. Hivyo usiku huo huo majira ya saa saba usiku "Maso Square The Duduman" akatimka zake, na kumuacha mkewe Kachero Yasmine akiwa amebaki makazi yake mapya na kundi la watumishi na masuria wa kumhudumia.
 
Kimasomaso mwanangu usimwone ndo basi tena anaondoka na mavumbi yake akirudi atakutana na vumbi la makachero ha haaaa haaaa kwishiney poti
 
SEHEMU-33



Kachero Manu katinga Kijiji cha Majimoto kuwafukunyua Magaidi
"Loooh salaleee...hasara tupu umepata wewe Babu, umelala mchana kweupeee mwenzako natakata tu, limeshaisha hili huniwezi wewe Mzee achana na bao tukuchangie pesa ukaperesheni busha hilooo" watazamaji wote wakaangua kicheko cha kwa kwa kwa, kumcheka Mzee Shadhili anavyotaniwa na mpinzani wake Kachero Manu.
Mzee wa watu alibaki kimya kama kumwagiwa maji baridi, anatafakari namna ya kuzichanga vyema kete zake za mchezo wa bao aweze kumgaragaza mshindani.
Ghafla Mzee Shadhili akaanza kupiga makelele "Sefu eeeeh...Sefu....ongezaa kikombe cha kahawa limeisha hili, aingie mwingine" alijitapa baada ya kufanikiwa kumsoma mpinzani wake na kugundua namna ya kumfunga mchezo huo uliokuwa una ushindani wa hali ya juu na kuteka hisia za mashabiki wao. Mzee Shadhili alisema maneno hayo huku anagida kahawa kwa mkupuo mmoja akaweka kikombe chini na mbwembwe na kuanza kuzisambaza kwa madaha kete zake kwenye mashimo ya upande wake wa kaskazini. Mzee Shadhili ndio alikuwa mbabe wao wa mchezo wa bao kijiji kizima cha Majimoto kilichopo jirani na mapango ya Amboni. Ndani ya wiki tatu tu alizokaa kijijini hapo Kachero Manu alijipambanua kama mshindani wa kweli wa Mzee Shadhili.
Kachero aliingia kijijini kwa gia za msimamizi wa mashamba ya zao la hiliki ya mwarabu mmoja anayekaa Tanga mjini. "Al-shabaab" walivyomtoa kule kambini Dibungo walivyomleta huku Amboni lengo lilikuwa ni kuchunga usalama wao pale kijijini. Alitakiwa anuse na kupeleleza kama kuna wanakijiji wanawafahamu na kuwachukulia vipi.
Walijua sasa serikali itakuwa wanafanya bidii ya kuwasaka kwa bidii na maarifa hivyo nao walitakiwa waweke watu makini kama Komandoo aboubakr (Kachero Manu). Haya yalikuwa ni kinyume kabisa na matarajio ya Kachero Manu. Alijua kuletwa kwake Amboni anakuja kuwekwa karibu na gaidi "Maso Maso" ili iwe rahisi kuandaa hujuma za kumkamata.
Mpaka sasa pia alikuwa hana mawasiliano kabisa na Kachero mwenzake Yasmine kinyume kabisa na matarajio yao kuwa watawasiliana kwa njia waliozoelekezana kwa haraka zaidi. Kuna wakati alikuwa anahisia mbaya kuwa huenda Yasmine ameuliwa na magaidi. Hisia ambazo kuna wakati usiku zilimletea njozi za mang'amung'amu na majinamizi. Anaota Yasmine amekamatwa, amefungwa minyororo kwenye viguzo anakatwa shingo yake kwa kuchinjwa na jambia lenye makali. Wakati mwingine anaota amebebwa na maharamia wa "Al-shabaab" kwenye meli kubwa na kutoswa katika kina kirefu cha bahari baada ya kufungwa shingoni jiwe zito. Pia mawazo juu ya mkewe nayo yalikuwa yanamsumbua.
Ambaye baada ya kuokolewa kwa watekaji aliomba ruhusa kazini likizo ya dharura na kurudi kwao Mwanza kwa wazazi wake kutuliza mawazo. Sasa alikuwa ndio anakaribia kurudi jijini Dodoma na hana mawasiliano nae kabisa. Alishaanza kutaka kuanza kukata tamaa ya kumkamata "Maso Maso". Alikiri kweli magaidi wapo makini na usalama wao.
Angewashangaa sana mtu mgeni kama yeye wamuweke karibu na kiongozi wao mkuu tegemeo, Afrika Mashariki na Kati, "Maso Maso". Katika harakati za kutaka kupoteza mawazo na kutengeneza fikra mpya za namna ya kumkamata "Maso Maso" bila msaada wa Yasmine akaamua wakati mwingine ajichanganye na raia wa mtaani, achezee nao pamoja mchezo wa bao ambao alikuwa anaumudu vilivyo.
Pia ajichanganye nao kwenye vijiwe vya kahawa kupata mpya mpya za pale kijijini. Haikumchukua muda wa siku nyingi kupata jina na kujitokeza kuwa mshindani mkuu wa Mzee Shadhili katika mchezo huo wa bao uliosambaa sana katika nchi za Afrika Mashariki, hasa Tanzania Bara (Tanganyika), Zanzibar na Kenya.
Kweli bana baada ya muda mfupi Kachero Manu akawa amekubali kipigo cha pili mfululizo toka kwa Mzee Shadhili. Ikabidi anyanyuke kiunyonge ampishe mpinzani mwengine. "Aingie mwingine mbona mnaogopa ogopa, nimekuja kugawa dozi hapa huyu Manamba mwacheni aende kijiweni kwa Sefu akamsaidie kuuza kahawa" alizungumza kwa kebehi na majigambo ya ushindi mzee Shadhili.
"Aah...leo umeniotea tu, ngoja nitulize bongo yangu narudi sasa hivi usinikimbie tu" Kachero Manu akajitetea kwa kipigo alichochapwa. Akawa anajivuta kwa unyonge kuelekea kijiweni kwa Sefu kwenye kahawa mkabala na pale wanapochezea mchezo wa bao. Alianza kwa kuwasalimia, "Asalaamu Aleikum, Je Waungwana hamjambo?.
Baadhi yao wakamjibu "Waleikum salaam Mtwana wajisikiaje na hali weye", huku wengine wakiendelea na maongezi yao ya siasa yalikuwa yamepamba moto. "Naam mie ni Mtwana wala sibishi ila nyie Bwana ni wavivu hamtaki kazi ngumu kabisa, pale shambani kwangu vibarua wa kulimia hiliki wanatoka Kigoma nyie mpo tu mnasogoa siasa sijui shusha Tanga, pandisha Tanga safari iendelee nakusikieni tu toka nipo kulee kwenye bao" aliwapiga madongo baada ya kumtania kwa kumuita Mtwana.
Soga zikaendelea zilizoamsha vicheko, huku wanasogezana Kachero Manu apate nafasi ya kukaa kwenye benchi. Alipokaa tu akapewa kikombe cha kahawa ns kashata za ufuta ili soga zizidi kuchangamsha kijiwe.
Ghafla wakiwa wamezama kwenye mazungumzo ya hapa na pale ya kusogeza muda jua lizame, likapita gari rangi nyeusi ambalo hakuna aliyeweza kudhibiti aina ya gari kutokana na mwendo wake wa kasi. Lilikuwa linayoyoma kutokomea mashambani. "Hili gari kama linawahisha mgonjwa hospitali" alichokoza mada mpya Kachero Manu makusudi kwa matarajio huenda akaambulia chochote kitu. Kwa majasusi kwao chochote mbele yao ni fursa. Na kweli uchokonozi wake ulizaa natija aliyokuwa anaihitaji.
"Gari lile habari zake Bwana mtafute dereva bodaboda anaitwa Juma Mavideo, huyu aliyetoka sasa hivi kumletea mkaa Bwana Sefu! " alijibu mmoja wa wana soga pale kijiweni. "Yaani kijiji chetu sasa wageni wametapakaa, huyo wa kwenye gari lililopita ni Mwarabu mmoja, lakini Juma Mavideo anasema nyumba anayohisi anakaa haiendani na hadhi yake, ni mashambani ndani ndani hukoo" alizungumza mwingine.
Kachero Manu alivyoangalia muda kwenye saa yake ya mkononi ulikuwa unasoma saa 12:00 jioni, ikabidi aage kimtindo, akiwaacha wameendelea kukaa mbumbumbu wanaukaribisha umaskini bila kujijua kwa soga zao zisizo na faida. Alichomoka ili akamtafute huyo Juma Mavideo huenda akaambulia chochote kitu. Hasa hapo aliposikia yule aliyewapita na gari la kifahari ni mtu mgeni, mwarabu, anatembelea gari la thamani lakini nyumba anayoishi haiendani na hadhi yake.

Ilimchukua robo saa tu, Kachero Manu kumtia mkononi Bwana Juma Mavideo. Alikuwa anaitwa hivyo kutokana na shughuli yake ya ziada mbali ya bodaboda ilikuwa ni kurekodi video za matukio ya sherehe pale kijijini. Alikuwa maarufu kwa shughuli hiyo hata ukimuuliza kwa watoto wadogo wanakuonyesha. Alichofanya ni kwenda kijiwe cha madereva bodaboda kumuuliza.
"Habari za sasa hivi vijana, samahani Bwana Juma Mavideo nimemkuta...!" aliuliza Kachero Manu pale kijiweni. "Daah una bahati mbaya umepishana nae muda sio mrefu kaelekea kwenye mishe mishe zake nasikia kuna ngoma ya sherehe ya kukesha kumtoa mwali kesho hapo juu mashambani" alijibu mmoja wa wale madereva bodaboda huku wengine wakiendelea na maongezi yao.
"Nikimbize mara moja basi nina shida nae kubwa sana" akaomba Kachero Manu. Bila kufanya ajizi yule dereva bodaboda akaingurumisha ikakubali, wakakwea na kuanza kukata vichochoro na vijia vidogo vidogo kuelekea huko ngomani. Baada ya muda wa robo saa na ushee hivi wakawa wameshawasili kwenye eneo la tukio.
Kulikuwa ni eneo lililojengwa nyumba zile za mbavu za mbwa. Ngoma ya baikoko ilikuwa hewani inarindima kwenye uwanja huku kigiza sasa kikianza kunyemelea eneo lile. Inaonyesha sherehe hizo zilianza kurindima tokea jua la mtikati kutokana na wachezaji wake kuwa wamejashuka vilivyo huku wamechafuka vumbi haswa. Ngoma hii ilikuwa imeanza kujipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya Tanzania kutokana na manjonjo yake wakati wa uchezaji wake. Kachero Manu akamalizana malipo na yule dereva bodaboda kisha akaanza kumsaka Juma Mavideo. Wakati anapasua makundi ya watazamaji alikuwa anashuhudia ustadi na uhodari wa ukataji viuno kwa wachezaji wa ngoma hiyo. Ikawa ni kivutio kikubwa sana kwa mtazamaji yeyote na mpenzi wa ngoma za asili.
Viuno vya akina dada hao vilifungwa kanga moja tu, vilikuwa vinazungushwa mithili ya kukosa mifupa kiunoni. Kuna wakati wapiga ngoma walibadili midundo ngoma ikawa inageuka kuwa mduara wa segere kama ilivyozoeleka. Mirindimo ya ngoma hiyo sambamba na kiuno cha jimama mmoja kilichokuwa kikizunguka kama feni mbovu iliyokata mota vikayafanya macho ya Kachero Manu yamkodolee kwa muda kama ujuavyo macho hayana pazia.
Lile jimama tinginya tinginya lilivyomuona Kachero Manu amelikodolea macho ndio likawa linazidisha kuzungusha kiuno kiuchokozi na kwa madaha kujionyesha kwa watazamaji kuwa amejaa tele kama pishi la mchele huku anamuangalia kwa tabasamu pana, na macho yake anarembua na kumkonyeza. Ni kana kwamba anamwambia lugha ya ishara Kachero Manu, ni wewe tu kama unataka usijivunge tuongee biashara, tukamalizane. Kachero Manu akampuuzilia mbali na kuendelea kuangazaangaza kumsaka mlengwa wake. "Huyu jimama anadhani mie ni mwanaume wa jicho la nje..!" alijisemeza moyoni mwake Kachero Manu.
Mungu si Athumani ghafla bin vuu, Juma Mavideo huyu hapa mbele ya Kachero Manu, anainama katika mapozi tofauti tofauti anamalizia malizia kupiga picha za mwisho mwisho kabla giza halijashitadi. Kachero Manu, akamgusa begani na kumnong'oneza sikio lake la kushoto "Juma nakutafuta sana nakuomba chemba kidogo".
Juma akageuka kumuangalia anayemuita kisha akajibu, "nisubiri kidogo nikadake mshiko wangu wa advansi ya kazi nakuja sasa hivi usijali". Kachero Manu akakubaliana nae akajivuta pembeni kidogo na ule umati wa watu uliokuwa bado unaserebuka kwa nguvu tena sasa kwa nguvu ya pombe ya kienyeji, kama ilivyo pombe ya ngomani ni "litekela mwene", unajichotea utakavyo haina kipimo cha unywaji.
Pombe hizo za kienyeji zilikuwa zimejazwa furifuri kwenye ndoo za plastiki. Jambo hilo la watu kuwa wamebobea kwenye ulevi lilimfurahisha Kachero Manu kwa sababu ingepunguza umakini wao wa kujua nani kamchukua Juma Mavideo. Kila wakati macho ya Kachero Manu yalikuwa juu juu huku na huko pia anaangalia muda kwenye saa yake ya mshale. Haikuzidi hata dakika kumi Juma Mavideo huyu hapa. "Salaamu aleikum kaka yangu, niambie shida yako" zilikuwa ni salamu zake kijana Juma huku akimpa kiganja cha mkono wa kulia kachero Manu. Wakashikana mikono kwa upendo huku wanajongea pembeni kuanza mazungumzo yao.
"Kuna mtu ana madini ya dhahabu ya dili katoka nayo Nyarugusu huko sasa kuna mwarabu katupita na gari moja jeusi pale kijiweni kwa muuza kahawa ulipoleta gunia la mkaa jioni, sasa nikiomba unipeleke nimeambiwa wewe unaweza kuwa unapajua" alijieleza Kachero Manu huku macho makavu kumbe anaongea uwongo mtupu akimjaza pampu ya tamaa ya pesa kijana wa watu.
Juma Mavideo kutajiwa mzigo wa dhahabu akili zikampaa, akashindwa hata kuuliza maswali ya udadisi yeye akaanza kuwaza mgao tu. "Ahaaa vizuri, si unamaanisha lile gari rangi nyeusi eeh la polisi?" aliuliza Juma Mavideo. Swali ambalo lilikuwa mtihani kwa Kachero Manu.
"Nadhani ni hilo hilo labda mie nachofahamu kuna mwarabu nimeelekezwa anatumia hiyo gari ndio taita wa madini nimeambiwa" alijibu Kachero Manu huku akisubiria mrejesho toka kwa Juma. "Itakuwa huyo huyo Bwana maana nishakutana nao kama mara mbili kule ng'ambo ya mashambani, ingawa siijui nyumba rasmi anayoishi ila tutafika tu, na huku hamna magari yanakujaga sana" alijieleza Juma kwa kujiamini huku anatikisa funguo zake za bodaboda yake kwa vidole vyake vya mkono wa shoto. "Sasa wewe unahitaji pesa kiasi gani kwa kunipeleka huko? "aliulizwa swali na Kachero Manu ili kuzidi kumsukasuka ajue ni kazi ya pesa ndefu atalipwa sio porojo za paukwa pakawa.
"Sasa kaka yangu wewe jichinje mwenyewe kisu nakuachia nakusikiliza tu najua hatuwezi kushindwana sie sote watoto wa kiumeni. Maana hapa umenichomoa kazini na bado ilikuwa nirudi tena kijiweni kwenye mishe zangu za bodaboda kutimiza hesabu yangu ya siku", alizungumza kimashaufu na kutingisha kiberiti kujionyesha ni mtu muhimu sana kufanikisha mchongo huo wa pesa ndefu, na bila yeye mambo hayatajipa.
Baada ya mvutano wa hapa na pale wakafikia makubaliano. Safari ikaanza ya kuelekea huko."Ila inabidi tupite kwenye kidebe tukajaze mafuta si unajua huku hatuna vituo vya mafuta" alisema Juma wakati tayari kachero Manu ameshakwea nyuma ya pikipiki. "Utaniacha pale wewe kajaze halafu unipitie si unajua nina mali adimu sitakiwi kuonekana ovyo" alizidi Kachero Manu kumtia shemere Juma.
Lengo la Kachero Manu hakutaka kuacha hata chembe ya ushahidi kwa sababu alijua huko wanakokwenda kuna kufa au kupona. Hisia zake mpaka akaamua amfuatilie huyo Mzee wa kiarabu zilimtuma kuwa baadhi ya washirika wa "Al-shabaab" wameanza kutafuta maficho hasa baada ya nyaraka za siri zilizonaswa na Kachero Manu kule Simba Hoteli, Dodoma, zenye majina yao kutua mikononi mwa serikali. "Wewe Juma nakukubali aisee umejuana nae vipi mtu muhimu kama huyu, ambaye ana utajiri chekwachekwa" alidodoswa Juma na Kachero Manu wakati tayari ameshajaza mafuta pomoni kwenye tenki la pikipiki sasa walikuwa wanakata msitu kuelekea huko mashambani.
 
Back
Top Bottom