big jambo
JF-Expert Member
- Sep 18, 2019
- 411
- 279
Mzigo unaenda kuliwa potiYaani nilikuwa naumia hatari mpaka najilazimisha kusoma
Mzigo unaenda kuliwa potiYaani nilikuwa naumia hatari mpaka najilazimisha kusoma














































DopeSEHEMU-37
️
Mkuu wa Magaidi mikononi mwa Kachero Manu️
Mambo yalikuwa tumbitumbi kwa Kachero Manu lakini muda hautoshi ikabidi ajitahidi ayakamilishe kwa wakati. Akaingia chumba cha kwanza kinachotazamana na kile alichokuwa anateswa. Akakuta chumba kina kitanda kikubwa kilichotandikwa nadhifu huku kukiwa na kabati lenye droo zake mbili pamoja na kioo. Hakukuwa na kitu chochote kingine.
Akavunja droo ya upande wa kushoto kwa kutumia bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Ikabidi aanze kucheka kwa alichokiona ndani ya droo hiyo. Alikuta paketi za kutosha za vidonge vya kuongeza nguvu za kiume maarufu kwa jina la "Viagra", na pia kulikuwa na paketi za kutosha za mipira ya kiume maarufu kwa jina la "kondomu". Akapiga risasi droo la upande wa kulia nalo likajibu na kujimanua likawa lipo wazi. Alichokiona humo alifurahi na roho yake sana tu.
Alikuta pesa taslimu za kigeni zikiwa zimepangwa bandali bandali. Lakini kilichomfurahisha zaidi ni kuipata ramani ya kutoka walipo pale kumfikisha mapango ya Amboni walipo viongozi wakuu wa "Al-shabaab". Baada ya kujiridhisha kuwa ndio yenyewe akaisunda kwenye mfuko wa suruali yake na kutoka nje kwa tahadhari kubwa. Hakutaka yale makosa ya kutekwa kirahisi yasijirudie tena.
Mpaka sasa alikuwa bado hatambui sehemu alipo. Akasogea kwenye chumba kingine akakuta mlango umefungwa lakini taa imewashwa. Akajaribu kukifungua kitasa taratibu, mlango ukaitika kwa kufunguka. Aliyoyashuhudia ni ya kustaajabisha. Hakutegemea Babu kikongwe kama huyo ayafanye. Alimkuta Mzee Abdallah mmiliki wa "Chops Carwash & Garage" mtuhumiwa wa mauaji ya Wabunge watano na madereva wao alikuwa anakula bata, habari hana kabisa.
Jamaa huyu aliwekwa juu ya meza uchi wa mnyama, halafu kumeletwa asali iliyowekwa kwenye kisahani, halafu zile korodani zake zinawekwa kwenye kisahani huku zinapakazwa asali, kisha msichana mbichi kabisa ananyonya korodani zake kimahaba zilizolowekwa kwenye asali.
Zinaponyonywa zile kokwa hiki kibabu kinapiga kelele za kupagawa, anazungumza maneno ya ahlan wa sahalan yasiyo na mtiririko wowote wenye kuleta maana. "Yaaaaah habibiiiii.... Zubeida mimi nataka kukununulia wewe ndege, nitakujengea ghorofa katikati ya Bahri Hindi Mashaallaah...Shallalaaaaah" Babu alikuwa hajiwezi kwa raha anayopata ya kunyonywa korodani zake.
Ndio alikuwa amekaribishwa Tanga, kashakuwa limbukeni wa mapenzi baada ya kuvitoroka vyombo vya dola vinavyomsaka kwa kesi ya ugaidi. Anavyopiga kelele hizo za maneno ya mporoto, yule binti ndio anazidisha manjonjo ya kumpagawisha Babu. Kiruka njia huyo alikuwa shombe shombe, kwani licha ya ngozi yake kuonyesha kuchanganya damu, bali nywele zake zilikuwa ni za kiarabu kwani alikuwa ameiteremsha ile shungi aliyojitanda kichwani.
Kachero Manu hakutaka waendelee na starehe zao na wamgeuze yeye kuwa kozibati. "Mpo chini ya ulinzi mafuska wakubwa nyie hata aibu hamuoni" alitoa ilani halafu akabutua risasi moja kupiga kwenye dirisha. Yule Babu alishtuka mpaka akaanguka chini ya meza, miguu juu kichwa chini. Huku yule kahaba amejifunika uso wake kwa kuona aibu ya yale waliyokuwa wakiyafanya.
Yule Babu alivyoamka akachomoka nduki utasema "Alphonce Simbu'' yule mkimbiaji mahiri wa Tanzania yupo kwenye mbio za Marathoni, anakimbilia kwenye mlango mdogo uliomo mle chumbani. Kachero Manu akaikohoza kidogo tu bastola yake, akaanguka chini Babu wa watu huku damu zinamvuja gotini. Akawa anajisuwira kwa maumivu makali anayoyapata huku analalamika.
Kachero Manu akawa anamsogelea huyu Babu ambaye ni mmoja wa kiungo muhimu wa Al-shabaab na ndio aliyemfadhili "Maso Maso" kwenda masomoni Uingereza kwenda kupikwa kwenye ugaidi.
"Nitakupeleka kwenye vyombo vya dola hata ikibidi nitembee kwa miguu kutoka Tanga mpaka Dar es Salaam ukiwa mgongoni mwangu nikufikishe ukajibu tuhuma zako za ugaidi mshenzi wewe" alikuwa anafoka Kachero Manu kumwambia maneno makavu Babu Abdullah mmiliki wa "Chops Carwash & Garage" aliyekuwa bado anagaragara pale chini.
Alipozidi kumsogelea, Mzee Abdullah akaanza kucheka kicheko cha kebehi "Ha... ha... ha.. ha.. ha... ha..!" kwa sauti ya juu kisha akamwaga matusi ya kutosha kwa Kachero Manu.
Kachero Manu akashtukia kitu kisicho cha kawaida kwa Mzee Abdullah akaanza kumwendea kwa kasi akamrukia na kuwahi kumkaba shingoni, lakini alikuwa ameshachelewa tayari amezidiwa ujanja.
Mzee Abdullah alikuwa na jino bandia ambalo ni kidonge cha sumu kitaalamu kinaitwa "Lethal Pill". Ambapo kidonge hiko kinavishwa raba kwa nje kumlinda mtumiaji kama akikimeza kwa bahati mbaya. Ndani ya hilo jino bandia kuna kemikali 'Potassium Cyanide' inayohifadhiwa kwenye glasi.
Hivyo anapotaka kujiua mhusika anavunja hiyo glasi hiyo sumu kwa meno yake moja kwa moja ikiingia mwilini inaenda kusimamisha mapigo ya moyo na kuharibu ubongo. Mzee Abdullah alikuwa amechagua njia ya marhaba yeye mwenyewe hakutaka kupata mateso ya Wanausalama. Alijua watamgombania kama mpira wa kona na kumletea usumbufu wa mateso mengi atakayoshindwa kuyabeba.
"Shenzi sana kasalimie jongomeo huko utaenda kujibu katika Mahakama ya Mwenyezi Mungu, hakuna ulichokikwepa...!" alisema Kachero Manu kwa hasira za mkizi mbele ya marehemu ambazo hazisaidii kitu. "Umekuja humu kwa kupitia wapi? " aliuliza Kachero Manu kumuuliza yule kahaba, sasa kasheshe la kumkosa Mzee Abdullah lilihamia kwake yule kahaba. Yule kahaba hakumjibu kitu kwa aibu na idhilali iliyomkuta huku akiwa amejiziba uso kwa mtandio wake, akajizoazoa pale chini alipokuwa amejibweteka na kutaka kuongoza njia kuonyesha njia aliyoingilia kule kwenye nyumba ya chini ya ardhi. Kachero Manu hakutaka kumuamini moja kwa moja yule mwanamke wa mahonyo, haraka haraka akamfanyia inspeksheni ya kutosha kuhakikisha hana chochote mwilini mwake.
Alipojiridhisha ni joka la kibisa hana madhara yoyote akamruhusu aongoze njia ya kutokea akafuata mlango ule ule aliotaka atokee marehemu Mzee Abdullah. Walipoufungua mlango wakakuta kuna ngazi zinapandisha juu wakazifuata mpaka wakaja kutokeza chumba kimojawapo katika ile nyumba ya udongo aliyotekwa kachero Manu.
"Haya ongoza njia ya kurudi ulipotokea potea hapa mara moja, kabla sijabadilisha mawazo na kukuchukulia hatua kwa kushirikiana na magaidi " yule kiruka njia hakusubiri tena amri nyingine akawa anatimka kuelekea mashambani ambapo hata hakujui anapoelekea akawa anachochora tu njia mbele kwa mbele atajua huko huko, cha muhimu kwake ilikuwa kusalimika na mkono mrefu wa dola. Kachero Manu haraka haraka akarudi ndani ya jengo lile akafanya haraka kutega mabomu kwenye ile nyumba huku akitega mabomu yale yasizidi muda wa nusu saa yalipuke.
Yalikuwa ni mabomu ambayo unaweka mwenyewe mtumiaji muda unaotaka yalipuke. Alipomaliza kutega tu akawa anasikia muungurumo wa gari kwa mbali akajua moja kwa moja ndio wanakuja walinzi wengine kuja kuchukua doria kama alivyopewa taarifa na rafiki yake Abu-fadhli. Akakimbilia juu kutoka kule mafichoni hima hima akaenda kujificha kichakani akisubiri matokeo chanya ya mitego yake.
Baada ya kutimia nusu saa huku jicho lake likiwa kwenye saa yake ya mkononi halibanduki, mabomu yalianza kulipuka kwa kishindo cha kutikisa eneo zima. Kukatimka vumbi zito kama lote eneo lile kukawa kama kuna kimbunga cha mchanga. Muda ulikuwa unasoma saa kumi na mbili kasoro ya jioni, akafanya ukaguzi wa eneo hilo sasa kukawa hamna jengo lolote lililosalia, kila kitu kuliteketea.
Akatumia gari walilokuja nalo maadui zake ambalo liliegeshwa mbali na eneo la jengo kurejea nalo Jijini Tanga kujiandaa na usiku wa mwisho wa hekaheka unaokuja mbele yake. Mipango iikuwa mpaka kufika alfajiri shughuli iwe imeshakamilika. Alitaka magaidi walie kilio cha kusaga na meno kwa pigo takatifu atakalowashushia, ambalo hawatasahau kamwe maishani mwao.
![]()
Pamoja mkuu.SEHEMU-37
️
Mkuu wa Magaidi mikononi mwa Kachero Manu️
Mambo yalikuwa tumbitumbi kwa Kachero Manu lakini muda hautoshi ikabidi ajitahidi ayakamilishe kwa wakati. Akaingia chumba cha kwanza kinachotazamana na kile alichokuwa anateswa. Akakuta chumba kina kitanda kikubwa kilichotandikwa nadhifu huku kukiwa na kabati lenye droo zake mbili pamoja na kioo. Hakukuwa na kitu chochote kingine.
Akavunja droo ya upande wa kushoto kwa kutumia bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Ikabidi aanze kucheka kwa alichokiona ndani ya droo hiyo. Alikuta paketi za kutosha za vidonge vya kuongeza nguvu za kiume maarufu kwa jina la "Viagra", na pia kulikuwa na paketi za kutosha za mipira ya kiume maarufu kwa jina la "kondomu". Akapiga risasi droo la upande wa kulia nalo likajibu na kujimanua likawa lipo wazi. Alichokiona humo alifurahi na roho yake sana tu.
Alikuta pesa taslimu za kigeni zikiwa zimepangwa bandali bandali. Lakini kilichomfurahisha zaidi ni kuipata ramani ya kutoka walipo pale kumfikisha mapango ya Amboni walipo viongozi wakuu wa "Al-shabaab". Baada ya kujiridhisha kuwa ndio yenyewe akaisunda kwenye mfuko wa suruali yake na kutoka nje kwa tahadhari kubwa. Hakutaka yale makosa ya kutekwa kirahisi yasijirudie tena.
Mpaka sasa alikuwa bado hatambui sehemu alipo. Akasogea kwenye chumba kingine akakuta mlango umefungwa lakini taa imewashwa. Akajaribu kukifungua kitasa taratibu, mlango ukaitika kwa kufunguka. Aliyoyashuhudia ni ya kustaajabisha. Hakutegemea Babu kikongwe kama huyo ayafanye. Alimkuta Mzee Abdallah mmiliki wa "Chops Carwash & Garage" mtuhumiwa wa mauaji ya Wabunge watano na madereva wao alikuwa anakula bata, habari hana kabisa.
Jamaa huyu aliwekwa juu ya meza uchi wa mnyama, halafu kumeletwa asali iliyowekwa kwenye kisahani, halafu zile korodani zake zinawekwa kwenye kisahani huku zinapakazwa asali, kisha msichana mbichi kabisa ananyonya korodani zake kimahaba zilizolowekwa kwenye asali.
Zinaponyonywa zile kokwa hiki kibabu kinapiga kelele za kupagawa, anazungumza maneno ya ahlan wa sahalan yasiyo na mtiririko wowote wenye kuleta maana. "Yaaaaah habibiiiii.... Zubeida mimi nataka kukununulia wewe ndege, nitakujengea ghorofa katikati ya Bahri Hindi Mashaallaah...Shallalaaaaah" Babu alikuwa hajiwezi kwa raha anayopata ya kunyonywa korodani zake.
Ndio alikuwa amekaribishwa Tanga, kashakuwa limbukeni wa mapenzi baada ya kuvitoroka vyombo vya dola vinavyomsaka kwa kesi ya ugaidi. Anavyopiga kelele hizo za maneno ya mporoto, yule binti ndio anazidisha manjonjo ya kumpagawisha Babu. Kiruka njia huyo alikuwa shombe shombe, kwani licha ya ngozi yake kuonyesha kuchanganya damu, bali nywele zake zilikuwa ni za kiarabu kwani alikuwa ameiteremsha ile shungi aliyojitanda kichwani.
Kachero Manu hakutaka waendelee na starehe zao na wamgeuze yeye kuwa kozibati. "Mpo chini ya ulinzi mafuska wakubwa nyie hata aibu hamuoni" alitoa ilani halafu akabutua risasi moja kupiga kwenye dirisha. Yule Babu alishtuka mpaka akaanguka chini ya meza, miguu juu kichwa chini. Huku yule kahaba amejifunika uso wake kwa kuona aibu ya yale waliyokuwa wakiyafanya.
Yule Babu alivyoamka akachomoka nduki utasema "Alphonce Simbu'' yule mkimbiaji mahiri wa Tanzania yupo kwenye mbio za Marathoni, anakimbilia kwenye mlango mdogo uliomo mle chumbani. Kachero Manu akaikohoza kidogo tu bastola yake, akaanguka chini Babu wa watu huku damu zinamvuja gotini. Akawa anajisuwira kwa maumivu makali anayoyapata huku analalamika.
Kachero Manu akawa anamsogelea huyu Babu ambaye ni mmoja wa kiungo muhimu wa Al-shabaab na ndio aliyemfadhili "Maso Maso" kwenda masomoni Uingereza kwenda kupikwa kwenye ugaidi.
"Nitakupeleka kwenye vyombo vya dola hata ikibidi nitembee kwa miguu kutoka Tanga mpaka Dar es Salaam ukiwa mgongoni mwangu nikufikishe ukajibu tuhuma zako za ugaidi mshenzi wewe" alikuwa anafoka Kachero Manu kumwambia maneno makavu Babu Abdullah mmiliki wa "Chops Carwash & Garage" aliyekuwa bado anagaragara pale chini.
Alipozidi kumsogelea, Mzee Abdullah akaanza kucheka kicheko cha kebehi "Ha... ha... ha.. ha.. ha... ha..!" kwa sauti ya juu kisha akamwaga matusi ya kutosha kwa Kachero Manu.
Kachero Manu akashtukia kitu kisicho cha kawaida kwa Mzee Abdullah akaanza kumwendea kwa kasi akamrukia na kuwahi kumkaba shingoni, lakini alikuwa ameshachelewa tayari amezidiwa ujanja.
Mzee Abdullah alikuwa na jino bandia ambalo ni kidonge cha sumu kitaalamu kinaitwa "Lethal Pill". Ambapo kidonge hiko kinavishwa raba kwa nje kumlinda mtumiaji kama akikimeza kwa bahati mbaya. Ndani ya hilo jino bandia kuna kemikali 'Potassium Cyanide' inayohifadhiwa kwenye glasi.
Hivyo anapotaka kujiua mhusika anavunja hiyo glasi hiyo sumu kwa meno yake moja kwa moja ikiingia mwilini inaenda kusimamisha mapigo ya moyo na kuharibu ubongo. Mzee Abdullah alikuwa amechagua njia ya marhaba yeye mwenyewe hakutaka kupata mateso ya Wanausalama. Alijua watamgombania kama mpira wa kona na kumletea usumbufu wa mateso mengi atakayoshindwa kuyabeba.
"Shenzi sana kasalimie jongomeo huko utaenda kujibu katika Mahakama ya Mwenyezi Mungu, hakuna ulichokikwepa...!" alisema Kachero Manu kwa hasira za mkizi mbele ya marehemu ambazo hazisaidii kitu. "Umekuja humu kwa kupitia wapi? " aliuliza Kachero Manu kumuuliza yule kahaba, sasa kasheshe la kumkosa Mzee Abdullah lilihamia kwake yule kahaba. Yule kahaba hakumjibu kitu kwa aibu na idhilali iliyomkuta huku akiwa amejiziba uso kwa mtandio wake, akajizoazoa pale chini alipokuwa amejibweteka na kutaka kuongoza njia kuonyesha njia aliyoingilia kule kwenye nyumba ya chini ya ardhi. Kachero Manu hakutaka kumuamini moja kwa moja yule mwanamke wa mahonyo, haraka haraka akamfanyia inspeksheni ya kutosha kuhakikisha hana chochote mwilini mwake.
Alipojiridhisha ni joka la kibisa hana madhara yoyote akamruhusu aongoze njia ya kutokea akafuata mlango ule ule aliotaka atokee marehemu Mzee Abdullah. Walipoufungua mlango wakakuta kuna ngazi zinapandisha juu wakazifuata mpaka wakaja kutokeza chumba kimojawapo katika ile nyumba ya udongo aliyotekwa kachero Manu.
"Haya ongoza njia ya kurudi ulipotokea potea hapa mara moja, kabla sijabadilisha mawazo na kukuchukulia hatua kwa kushirikiana na magaidi " yule kiruka njia hakusubiri tena amri nyingine akawa anatimka kuelekea mashambani ambapo hata hakujui anapoelekea akawa anachochora tu njia mbele kwa mbele atajua huko huko, cha muhimu kwake ilikuwa kusalimika na mkono mrefu wa dola. Kachero Manu haraka haraka akarudi ndani ya jengo lile akafanya haraka kutega mabomu kwenye ile nyumba huku akitega mabomu yale yasizidi muda wa nusu saa yalipuke.
Yalikuwa ni mabomu ambayo unaweka mwenyewe mtumiaji muda unaotaka yalipuke. Alipomaliza kutega tu akawa anasikia muungurumo wa gari kwa mbali akajua moja kwa moja ndio wanakuja walinzi wengine kuja kuchukua doria kama alivyopewa taarifa na rafiki yake Abu-fadhli. Akakimbilia juu kutoka kule mafichoni hima hima akaenda kujificha kichakani akisubiri matokeo chanya ya mitego yake.
Baada ya kutimia nusu saa huku jicho lake likiwa kwenye saa yake ya mkononi halibanduki, mabomu yalianza kulipuka kwa kishindo cha kutikisa eneo zima. Kukatimka vumbi zito kama lote eneo lile kukawa kama kuna kimbunga cha mchanga. Muda ulikuwa unasoma saa kumi na mbili kasoro ya jioni, akafanya ukaguzi wa eneo hilo sasa kukawa hamna jengo lolote lililosalia, kila kitu kuliteketea.
Akatumia gari walilokuja nalo maadui zake ambalo liliegeshwa mbali na eneo la jengo kurejea nalo Jijini Tanga kujiandaa na usiku wa mwisho wa hekaheka unaokuja mbele yake. Mipango iikuwa mpaka kufika alfajiri shughuli iwe imeshakamilika. Alitaka magaidi walie kilio cha kusaga na meno kwa pigo takatifu atakalowashushia, ambalo hawatasahau kamwe maishani mwao.
![]()
"Supu limetiwa nazi", Magaidi hatarini



























