Mbwa wa geti
Sehemu ya kumi na nane
Mtoto alishuhudia mama yake akiwa analazimishwa kutoa tarabu kwa makofi na bado kumbukumbu zake hazikuwa mbali hasa alipokumbuka yakuwa ni jana tu walipigwa yeye na *****,lakini mtoto yule hakuwa na nguvu za kupambana akabaki kuwa mtazamaji wa filamu ile ya kufedhehesha.
***
Tangu utoto wake hakuwa anapenda kuona mtu anamdharau na alikuwa tayari hata kuacha kitu anachokipenda kwa sababu tu ya dharau.
Alijikuta akiwa mgomvi shuleni hadi nyumbani kwa sababu ya kutokupenda dharau na sasa alikuwa amemweka kwene rada zake Burizozo kwa kuwa alikuwa akimdharau na pia aliona kitendo cha Kabah kumuua kijana wake ni sawa na kumdharau kupita kiasi.
Kabah alimwachia maagizo ya kupeleka wadudu flani huko Chamwino Ikulu.
Temba hakuwa anawajua wadudu wale na madhara yake ila alihisi tu ni wa hatari kwa mwonekano wao na tayari alikuwa ameagiza vijana wakatekeleze jukumu hilo yeye akiwa amebaki kuangalia usalama wa jumba lile na mzigo utakaokuwemo.
Wakati akiwa anawaza hili na lile akakumbuka Mina.
Mbali ya kumjua askari yule lakini walikuwa ni marafiki wakubwa waliokutana kwenye mkasa wa SIKU KABLA YA LEO ulioandikwa na mwandishi anaekuja kasi Bahati Mwamba.
Aliona kuingizwa Mina katika kesi ya mauji ya askari polisi aliekuwa anafuatilia nyendo zao ilikuwa ni kumsogeza karibu yeye kuwa adui wa Mina hakutaka hilo litokee,lakini pia hakutaka Mina ajue kama bado anaendelea na ujambazi wa kuua watu.
Akapanga kufanya kitu ili awe mbali na mikono ya Mina lakini kabla hajafanya hilo alitaka kwanza kuwasiliana na Mina amtahadharishe kuhusu wadudu wa ajabu wanaoenda kumwagwa maeneo ya Ikulu Chamwino.
Akatoa simu yake na kuzitafuta namba za Mina kisha akapiga na akasikia zikiita,akakata haraka na kuandika ujumbe mfupi afu akazima simu.
Wakati akijua kawauza wenzie kwa askari mtata Mina akanyanyuka alipokuwa na kujinyoosha kisha akaanza kuzunguka maeneo ya jumba lile na hapo ndipo aliponasa sauti ya hamaniko kutoka ndani.
Alizoea kusikia Tausi akilia kila siku,lakini sauti ya leo ilikuwa inautata,ilikuwa sio ya kilio alichozoea kukisikia wakati Tausi akipigwa,hiki cha leo kilikuwa ni kilio cha maumivu na majuto makubwa lakini pia alisikia killio cha mtoto mdogo
Akashawishika kutazama kupitia dirisha pana la vioo na hapo akaona jambo gumu kuvumilia na akachanganya na chuki yake kwa burizozo akaamua kusaliti mazima.
****
Mikono yake ikiwa imelowa mafuta kwa kukurukakara za kutaka kumruka ukuta Tausi,Burizozo alikuwa bado anafanya jitihada za kumdhibiti Tausi ili atimize haja zake.
Akampiga kofi lenye uzani wa kilo kadhaa na kumwangusha Tausi juu ya zulia na kisha akamfuata huku wololo yake ikiwa imesimama kama kijiti cha mwembe koi huku tabasamu la kifedhuli likiwa limemkaa usoni.
Akainama ili ammiliki Tausi.
Ni wakati mkono wake ukiwa unataka kushika wololo m, hapo ndipo akajikuta akipaa juu na kurudi chini kwa kasi ya umeme huku mbavu zake zikiwa zinauma.
Burizozo akatazama aliemfanyia shambulizi lile hakuamini kuona ni kutoka kwa kibaraka wao Temba.
Akasimama kwa jazba ili amshambulie,lakini ni kwa kuwa hakujua uwezo wa Temba upo vipi,yeye alikuwa anamchukulia kama mjinga flani hivi lakini hakujua ujuzi wa Temba kwenye uwanja wa vita vya mkono au silaha.
Akasimama kwa pupa ingali yu uchi,akaunguruma kwa hasira na kwenda kumvaa Temba,ila alikutana na pigo moja tu lililoondoka na ufahamu wake huku akijibwaga chini kama kiroba cha unga.
Temba hakutaka kukaa pale,akamhimiza Tausi avae nguo na achukue kile kinachomfaa kwa muda huo na watoke pale ndani.
Alimwacha ndani Taus akijiandaa na yeye akaenda kuchukua gari lake lililokuwa limepaki pale uwanjani,walinzi wenzie waliona tu hekaheka za Temba aliejiita Mbwa,lakini hawakujua ni za nini hekeheka zile.
Itaendelea