Mbwa wa geti
Sehemu ya Mwisho
Zedi hakutaka kuachwa nae akatoka kasi kuwahi upande wa mbele lakini alikuwa amechelewa alikutana na moshi wa gari
Hakuhangaika nae
Akaingia ndani haraka na kuongeza nguvu pale ndani huku nje vikisikika vingora vya polisi vikipiga kelele kusogea pale.
Wahalifu wote wakatiwa pingu kisha Zedi akaomba awasiliane na Ikulu Tanzania,na alipomaliza akaomba kuwasimamia wabunge wale na waziri wao had ndege binafsi itakapo kuja kuwachukua.
Waira akabaki na kazi moja tu kuchoma maabara zote zilizokuwa chini ya mbwa weupe na wanajeshi wa Kenya walielekea Karura forest kulikokuwa na kambi ya Mbwa weupe.
Kasiki ilioibwa kutoka kwenye nyumba ya mzee matare ilimshinda Mao Waira kuifungua,akamuomba Zedi na Zedi akatumia namba 0258 alizopewa wakati akiwa ametekwa na mzee matare.
Kasiki ile ndio ilibeba siri ya mkasa ule.
Mzee matare alikuwa ni dokta na mara nyingi alijikita kufanya tafiti za wadudu na hapo ndipo akapata wazo la kutengeneza aina ya wadudu watakao kuwa kama tiba kwenye mimea yaani wadudu watakao kuwa wanakula wadudu waharibifu wa mazao
Mzee huyu alitengeneza fomula za kisayansi na hatimae akafanikiwa wadudu wale.
Furaha yake ikapata doa baada ya kupata ugeni kutoka nchi za mbali,wao wakaja na wazo la kutengeneza wadudu wala nyama.
Kadri wafadhili wale walivyokuwa wakimfadhili wakaleta na watalamu wao,nasasa Mzee matare akaanza kuona hatari na kibaya zaidi akagundua mpango uliokuwa nyuma ya yote
Mpango ulikuwa ni kuwasambaza wadudu wale maeneo yote ya nchi za Afrika mashariki,kisha wao waje na tiba ya kuwaua wadudu wale,watapata pesa nyingi sana.
Lakini kikubwa walikuwa wanamwaga wale wadudu sehemu zilizokuwa zimegunduliwa madini na mafuta na ugunduzi huo ulikuwa haujafika mikononi mwa serikali yoyote katika nchi hizo.
Maeneo athirika yote wakazi wangehama hivyo,wao wangeingia ubia na serikali kuyamiliki kwa kigezo cha kutoa dawa ya kuwaangamiza wadudu wale.
Mzee yule akafanya hila akaiba ramani ya maeneo hayo yanayolengwa na akaificha ndani kwake na wakati anafanya jitihada za kuzuia akaangukia mikononi nwa wa wasaliti hatimae akaiaga dunia mbele ya macho ya Zedi.
****
Zedi alipokelewa kama shujaa uwanja wa Dodoma na waziri mkuu,IGP na CDF bwana Salim Komba.
Watuhumiwa wakachukuliwa na kupelekwa mahabusu.
Zedi akatoa ramani nzima na mpango mzima ulivyokuwa huko Kenya ila hakuwaambia kuhusu kutoroka kwa Kabah,alimhitaji akiwa mzima au mfu yeye mwenyewe.
****
Wakati Kabah akiwa ndani kwake na kudhani yupo salama,akashangaa kuona Burizozo anaingia kwa kasi na bastola mkononi.
“Tumevamiwa asee,Temba ana…” hakumaliza kauli yake Kabah akachukua bunduki yake na kutoka nje.
Kama alidhani vita ni ya kitoto alikosea
Alipata kushuhudia watu watatu tu wakiua kama mchezo tena kwa kasi na weledi wa hali ya juu.
Akamwacha Burizozo aendelee kupambana yeye akarudi ndani na kutaka kutumia mlango wa nyuma kutoka.
Ziga alimuona wakati akijaribu kukimbia,akamfuata huku sasa burizozo akiwa amebakia kutazamana na Temba na Mina akagwaya.
Temba akamrukia kwa aina ya Tailand kiki na goti lake likakutana na kifua cha Burizozo na kumpeleka chini,haraka akatak kujinyanyua lakini akachelewa kasi ya Temba ilikuwa ni kubwa akamtandika teke la mbavu.
Temba akataka kumuua lakini Mina akawahi na kumzuia kisha akampiga pingu na punde gari za polisi zikaingia kwa fujo na kukutana na maiti kadhaa za vijana wa Mbwa wa geti.
Kitu ambacho askari wale hawakujua ni kuwa Temba ndie alikuwa kiongozi wao ,ikabaki siri ya Mina,Ziga na Temba mwenyewe.
Wakati kabah anataka kutoka nje tu akaukatana na mtu ambae hakutegemea
Zedi alikuwa kasimama wima mlangoni huku silaha ikiwa mkononi na alipomuona tu akaitupa na bila kuulizana ukaanza mkono wa adabu.
Ziga alikuwa kasi kuwahi kummkamata Kabah lakini akakuta rafiki yake akiwa anapambana na jasusi Kabah,yeye akabaki kuwa mtazamaji.
Mpambano ulikuwa ndani ya dakika tano tu lakini tayari Kabah alikuwa amevunjwa mkono na Zedi.
Zedi kwa hasira alizokuwa nazo akapaa hewani ili kummliza Kabah lakini kabla hajashuka Mina akaingia na kumpitia kwa kasi Kabah kisha akamtia pingu huku RPC Mabeyo akiingia pale na kuwapigia makofi huku akiwapongeza vijana kwa kazi waliofanya ndani ya muda mfupi sana.
Kabah alikaguliwa nyumba yake na kukutwa shehena ya dawa za kulevya na watu kadhaa waliokuwa mateka pale ndani.
***
Zedi,Ziga,Mina na Temba waliingia ndani ya nyumba waliokuwa wameweka hifadhi kwa muda na walichokutana nacho hawakukitarajia.
Tausi alikuwa amelala juu ya sofa huku povu likimtoka,mtoto nae alikuwa amekaa tu huku hajui kipi cha kufanya.
Zedi akamkimbilia mwanae,huku kwa mara ya kwanza Ziga na Mina wakilishuhudia chozi la mbabe yule.
Zedi hakuumizwa na kifo cha mkewe Zaidi aliumizwa na mwonekano wa mwanae.
Taratibu zikafanyika na mtoto wa Zedi akapelekwa soba.
****
Baada ya Wiki mbili ndani ya gereza la Isango kulitokea mauaji ya askari magereza zaidi ya hamsini huku wafungwa kadhaa wakitoroka akiwemo na Kabah,huku gereza likiachwa na maandishi makubwa MBWA WA GETI.
Taarifa hizi Zedi alizipata akiwa anamwogesha mwanae ahsubuhi huku Ziga na Mina wakizipokea taarifa hizi wakiwa ndani ya hoteli ya nyota tano huko Zanzibar.
“Karibu tena kiumeni,safari hii nakuua Kabah” alijisemea Zedi huku akilitizama kovu la mwanae tumboni.
MWISHO
Ahsanten sana kwa kuwa nami mwanzo hadi mwisho wa riwaya hii.
Yule mwenye kuhitaji kutoa wazo ama ushauri basi fanya hivyo.
Mwisho wa riwaya hii ni mwanzo wa riwaya nyingine tena ahsanten