Riwaya mpya: Mbwa wa geti

Riwaya mpya: Mbwa wa geti

Mh
Kwahiyo umemuona huyo mama kitunguu wako tu tumosa makubwa haya sisi wengine vyeusi mangala cc @moneytalk
Mmh mwenzangu sisi hatuna uzito

Hapana jamani,ninyi huwa kila mkisoma mnaweka kakoment kidogo
Sasa ndugu yenu yeye ananiachiaga kalike tu msijisikie vibaya jaman kesi ilikuwa ya mmoja tu
 
Mbwa wa geti

Sehemu ya kumi na nne


Ni wakati alipokuwa akikaribia kufungua mlango wa gari akili yake ikamtuma atazame kwenye kioo na hapo hakuwia kugundua hawapo peke yao pale,kuna macho ya watu wawili yalikuwa yanawatizama,na sio kuwatizama tu yalikua yanawatizama kwa husda.

Ziga akashuka na bila kujali nae akazama ndani na kuyashudia yale alioyashuhudia Mina na kisha wakajikuta wote wapo ndani ya sebule iliojaa vumbi huku kukionekana kuna vurugu zilifanyika hapo ndani na matone ya damu yakiwa yameganda sakafuni.

Walitazamana

Kisha kila mmoja akaanza kukagua upande wake na kila mmoja akijaribu kuwaza alichokiona.

Lakini wote mawazo yao ni kama yalikuwa sawa wakajikuta wakielekea kwenye chumba cha Zedi maana walikijua na huko nako wakakutana na mapya.

Chumba kile kilionekana kina kaliwa na mtu na mtu yule ni mvuta sigara maana vipisi kadhaa vilikuwa chini na kiti kilikuwa kimewekwa pembeni kidogo ya mlango kuonesha mtu yule alipenda kukaa pale.

Kila mmoja alijua nini maana ya kiti kile,ilimaanisha mkaaji huwa anamsubiri mtu,mtu gani hawakumjua.

Ziga alishika hiki akashika kile ili mradi alijua anachokifanya.

“Nyumba hii inaonekana haikukaliwa na mwanamke muda mrefu zaidi kuliko siku alizokaa mwanaume”..yalikuwa maneno ya Ziga na yalisikiwa vizuri na Mina.

Namna ya upangiliaji wa muonekano wa chumba na baadhi ya sehemu za nyumba ile ndizo ziliwapa uhakika ya kuwa mwanamke hakuwa amekaaa pale ndani kwa muda mrefu kuliko mwanaume na ndivyo ilikuwa lakini Mina aliiuliza kitu.

“kwanini umeona mke wa Zedi hajakaa hapa kitambo kuliko Zedi!?”

“Nimeona mpangilio wa hiki chumba vitu vingi vimepangwa kiume na vitu vingi vipo mwonekano wa kiume japo kama huelewi utaona ni sawa tu..” alizungumza Ziga kisha akaendelea huku sasa akishika kitanda

“chumba chochote anachoishi mwanamke, lazima kitanda ukikute kushoto mwa chumba lakini pia kitanda anacholalia mwanamke lazima ukute kaambatanisha mito na mashuka.”alizungumza zedi huku wakati huo akikaribia kabati la nguo na kulifungua

“ona hata namna ya kukunja nguo,mwanamke hakunji hivi”alisema Ziga huku akimwonesha Mina nguo kadhaa zilizokuwa ndani ya kabati.

“Pia naona ni nguo za kiume tu zipo humu za mtoto na za mke hazipo hata moja.”alisema Mina huku sasa wakianza kutoka ndani ya nyumba ile

“kuna tatizo na Zedi yupo matatizoni”alisema Ziga huku sasa wakikaribia gari lao lililokuwa nje na walipolifikia wakapanda huku Ziga akirudia tena kutazama upande ule aliona watu wakitizama,hawakuwepo nae akatia moto wakatokomea eneo lile.

Licha ya mwendo waliokuwa wanatumia kuwa mkali kidogo lakini Ziga hakukawia kujua nyuma kuna gari inawafuata na ilikuwa nyuma yao kwa tofauti ya magari mawili tu.

Wakati wanafika forway,Mina akashauri wagawane lakini kisomi na hapo wakapaki ndani ya bar ya forway bar kisha wakateremka na wakapanga kukutana kwa Rpc Mabeyo .

Walipoingia ndani ya ile bar gari lilikokuwa linawafuata likapita na kuingia kituo cha kujazia mafuta kisha wakateremka vijana wawili shupavu na wakarudi kwa miguu hadi forway bar,lakini walichoenda kukishuhudia hawakukikuta,si mwanamke wala mwanaume zaidi waliona gari ikiwa imepaki pembeni na kijana mmoja akihangaika kuisafisha.

Mmoja wao akanyanyua simu na kupiga anakokujua kisha wakaondoka,lakini Ziga aliwaona na sasa wao ndio walianza kufuatiliwa yaani ile muwinda huwindwa.

*****

Mapambazuko yalimkuta Zedi akiwa nakuru nje kidogo ya jiji la Nairobi na huko alikuwa anaitafuta bank ya KCB ambayo aliakuwa na tetesi na tetesi za kuhusu mambo kadhaa.

Akamlipa dereva taxi aliemleta pale kisha akajongea hadi kwenye mgahawa uliokuwa pembeni ya bank ile na akatafuta pembe moja ya mgahawa na kukaa huku akimtizama kila aliengia na kutoka eneo mgahawani pale lakini pia aliona eneo zima la Kcb lililokuwa bado limefungwa kwa sababu muda wa kazi ulikuwa bado haujatimia.

Akaagiza supu ya mbuzi na chapati nne na kupoza njaa.

Muda ulizidi kusogea na sasa bank ile ya Kcb ilikuwa ipo wazi na watu walianza kuingia na kutoka huku magari kadhaa yakiwa yanapaki na kuondoka mbele ya bank ile.

Akasimama na kulipa pesa kisha akapiga hatua kutoka pale mgahawani huku uso wake akiwa kauweka nyuma ya mawani kubwa na kichwa kimezibwa na kofia ya kibitozi,miguuni alikuwa kavaa raba nyeusi na mwili wake ulisitiriwa na suruali nyeusi ya jeans na fulana mpauko

Akavuka barabara kuingia ndani ya bank ile na moja kwa moja akaelekea pahali pa huduma kwa wateja

“Dada naomba kuoneshwa ofisi ya meneja!!” aliomba Zedi huku akiwa yupo makini na kumtazama yule dada na hapo akauona mstuko wa wazi kabisa na akashindwa kujua kwanini yule dada alistuka na hapo Zedi tena akacheza pata potea

“ooh u mrembo sana wewe waitwa nani vile!” aliamua kuchombeza hata kabla hajajibiwa swali lake la awali na akaona tabasamu la aibu kwenye uso wa yule dada

“Naitwa Wambui”
“ooh Wambui!! Jina zuri sana unaishi wapi!?”

“naishi Kibira,vipi wataka kuonana nami!?”

“Ndio ningelifurahi sana Kama ingelikuwa hivyo”

“ok utanipigia kwa namba hii” Wambui alisema huku akimpa Zedi kadi ya biashara na alipokwisha kuipokea akawapisha wateja wengine huku akipokea maelezo machache kuhusu meneja na ofisi yake,Zedi akajivuta hadi kwenye mlango wa meneja na kugonga kidogo kisha akasubiri na ndani ya muda mfupi mtu alitoka ndani ya ofisi ile na wakati wanapishana na mtu akietoka ndani ya ofisi ya meneja Zedi akapata kugeuka na hapo macho yake yakakutana na macho ya Wambui akimtizama huku mkono wa kushoto ukiwa na simu kuonesha ametoka kuwasiliana ndani ya dakika moja iliopita.

Zedi akatabasamu huku akijua kabisa yule dada amepiga simu sehemu hatari,hakujali akausukuma mlango na kuingia hadi ndani na alipoingia tu akakuta meneja nae anashusha chini simu ya mezani.

Haraka haraka Zedi alikuwa ameona picha kadhaa zilizokuwa zimebandikwa ukutani hakuzijali na hapo macho yake yakadaka jina la meneja yule aliemkuta mle E. KWASI.

Zedi akasimama mbele ya meza iliokuwa mle ofisini na kufanya kuwe na utenganisho baina yao.

‘naomba kujulishwa ilipo ofisi ya bwana Kamau' aliongea zedi huku macho yake yakiwa makini juu ya mwili wa meneja Kwasi.

Itaendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom