RIWAYA : MKONO WA CHUMA
MTUNZI : ALEX KILEO
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA.
________________
ENDELEA....
_________________
Wakati BQ akiwa bado anapambana na lile giza machoni, akaamua aulegeze mwili kwanza, hicho kilisaidia kidogo,
"huyu atakuwa mlevi mbwa au wale watu wanaoishi katika mazingira magumu" Alisikia wale watu wakimjadili,
"kweli kamanda, huoni hata nguo zake zilivyochafuka, amelowana, nywele zimekaa hovyo" Wale watu waliendelea kumjadili BQ,
"hawa ndio wanaobakwaga maeneo haya, alafu kukicha lawama tunapewa sisi watu wa usalama" Wale watu waliendelea kuongea,
"sijui amezimia au amelala, ebu jaribuni kumtingisha" Wale watu waliendelea kumuongelea BQ na kipindi hicho alikuwa akiwaza ni kweli hao watu hawajamtambua au wanaigiza,
"ebu tuwapigie simu polisi tuwape habari, usikute amekufa huyu" Wale watu waliongea na kufanya BQ ajiulize wale watu ni wakina nani? Kwanini waseme wawapigie polisi, ina maana wao sio polisi? BQ alijiuliza na mwisho akaone bora afungue macho ili awaone vizuri watu hao, kwa maana hata nguvu zilianza kumrejea.
BQ akafungua macho, kweli akakuta watu wanne wote wanamtolea macho, na wote walikuwa wamevaa gwanda, BQ akakaza macho zaidi katika giza lile na kugundua kuwa rangi ya zile gwanda zilikuwa za blue,
"sio polisi awa" BQ aliongea moyoni kisha akatoa tabasamu usoni,
"huyu sio mzima, huoni anacheka peke yake?!" wale watu waliongea huku wakimtazama BQ aliyekuwa akijiinua taratibu, kisha akasimama huku akiendelea kutabasamu,
"tumpige hata makofi, atakujaje kulala eneo la hatari hivi wakati Kuna vibao vingi vinavyotahadharisha watu kutokaa eneo hili nyakati hizi?" mmoja kati ya watu wale aliongea na kumsogelea karibu BQ, kisha akamtandika kofi kali la shavu, BQ akasimama na kumuangalia,
"umoja security guard" BQ aliongea aliposoma maneno yalioyoandikwa kati gwanda ya yule mtu, kisha BQ akatabamu na kuondoka bila kujishika hata shavu, wale wagambo wakabaki wakimtazama,
"awa wanawake wengine ni majini, yaani mnapiga halii wala hajishiki shavu, anacheka tu" Wale mgambo waliongea huku wakimtazama BQ aliyekuwa akitembea mwendo wa kupepesuka, bado alikuwa akihisi kizunguzungu.
******************
Baada ya muda Rais alirejea kutoka mariwatoni, mkononi alikuwa na chupa nyingine ya mvinyo, akakaa katika kiti,
"Habari unazonipa leo sio mchezo" Yule bwana mwingine aliongea huku akifurahi,
"dunia ina mambo mengi sana, we iangalie hivi hivi" Rais aliongea na kutabasamu,
"Tuendelee na story" Yule bwana alizungumza na kupiga funda moja la mvinyo,
"Tuendelee sasa, ila sasa nitamzungumzia Ray Charles tu" Rais aliongea na kukaa vizuri, kisha akaendelea,
"baada ya kuona ubongo wa Ray Charles haufanyi kazi kwa kasi ya kawaida, ilibidi apandikizwe kifaa cha umeme katika kichwa chake ili ubongo wake ufanye kazi kawaida, ila kifaa alichowekewa, kilifanya ubongo wake usiwe wa kawaida, akawa ana uwezo wa kufikiri mara nne zaidi ya uwezo wake aliokuwa nao hawali, kisha wakamchoma sindano za kutanua misuli ya mwili, ambazo zilimrejeshea hisia za mwili baada ya wiki, yaani akaanza kuchezesha hata viungo vya mwili, kifupi mwili wake ukawa unafanya kazi, ila hakuwa na nguvu kabisa, hata za kuinuka, hapo madaktari waliangaika nae sana kumrejesha katika nguvu zake, ila walishindwa, na mwisho wakaja na wazo la kumpachika tena vifaa vya umeme katika mwili wake, walitaka kumpachika kwa ndani ya mwili, ila ikaonekana watamchana sehemu nyingi sana za mwili, sasa wakatafuta wazo jingne, nalo ni kumvalisha chuma nyepesi ambayo itawekewa huo mfumo wa umeme, na nyaya chache zitaunganishwa katika sehemu muhimu za mwili, hilo wazo likapitishwa na Tammy Semmy. Wale wachina wakatengeneza hizo chuma kulingana na mwili wa Ray Charles, zoezi lilichukua miezi sita hili kupata kitu bora, kisha akavalishwa Ray Charles, akaweza tena kuamka na kutembea. Ila nguvu ndani ya vile vyuma ni nyingi sana, zimegawanyika katika sehemu kuu Tatu, kuna nyeusi, ambayo ni nguvu zake za kawaida, kuna kijani, ambayo ni nguvu za ziada, ambazo hutumia akienda kupambana na watu wenye silaha nzito, na pia Kuna nyekundu, hii hatujawahi kuitumia kwa kuwa inaweza kuleta athari kwake na kwa watu wote walio karibu nae, yaani uwa ile nguvu akizidishiwa, akili pia hufanya kazi nje ya uwezo wake, uwa kama chizi, anaweza hata kuua watu wote waliopo eneo hilo" Rais aliongea na kutema mate pembeni,
"kwa hiyo Ray Charles alipatiwa muda wa kuishi kwa namna hiyo?" Yule bwana mwingine aliuliza,,
"kitu kingine usichokijua ni kuwa Ray Charles ni immortal" Rais aliongea na kumuangalia yule bwana,
"immortal ni mtu wa aina gani, au ni nini?" Yule bwana mwingine aliuliza,
"mtu akishakuwa immortal, yaani uwa anaishi bila kufa, yaani hafi labda mumuaribu tu, na kuharibika ni sehemu moja tu ninayoijua mimi, yaani maisha ya Ray Charles yapo mikononi kwangu" Rais aliongea na kutabasamu,
"duh, imekuwaje wewe ndio uwe unayaendesha maisha ya Ray Charles?" Yule bwana mwingine aliuliza,
"OK, sikia. Baada ya Ray Charles kukamilika na kuwa mtu anayeweza kujongea na kufanya mambo mengine kwa ufanisi, ndipo hapo mapinduzi yakafanyika nchini, jeshi lilichukua nchi baada ya kugundulika kuwa Tammy Semmy alimuua Rais ili yeye awe Rais. na mwisho at siku Tammy Semmy aliuawa katika ndege ya RUSSIA AIRLINE, maiti yake ilikutwa ndani na ikarejeshwa nchini kwa ndege ya mizigo, hapo chama chetu kikavurugiga na mambo mengi yakatokea, mpaka jeshi lilipoamua kunipa kushika madaraka kwa muda, kisha ukafanyika uchaguzi na nikashinda moja kwa moja. Baada ya hapo serikali ya China ikanipa taarifa juu ya Ray Charles, waliniuliza wamuharibu au ninaweza kumtumia? Ikabidi nifunge safari mpaka China, nikamuona Ray Charles sasa, nilishtuka kwa kuwa hata mimi niliamini amekufa, ndipo nikaelezwa na kupewa video iliyoonesha namna ilivyokuwa mpaka Ray Charles akawa hivyo, nilichoulizwa ni kuwa nitamchukua au nitamuacha? Nikasema nitamchukua, wakaniuliza kwa lengo gani? Nikasema kwa lengo alilokuwa kuwa nalo Tammy Semmy, yaani awe mlinzi wangu binafsi. Ila pia Ray Charles aliulizwa anataka aendelee kuishi chini ya mamlaka yangu? alijibu ataishi chini ya mamlaka yangu ila sio kwa ajili yangu, alipotakiwa aifafanue hiyo kauli yake, alisema kuwa ataishi kwa ajili ya familia yake , yaani mke na mtoto wake mdogo wa miaka sita, akaenda mbele zaidi na kusema hasingekuwa na familia, hasingetaka kuendelea kuishi huku amefungiwa machuma mwilini, nimesimama Basi nikapewa maelezo jinsi ya kumtumia na namna ya kumuendesha. Baada ya hapo nikakabidhiwa nyaraka muhimu za Ray Charles na nilichofanya, ni kumuamrisha Ray Charles auwe kiwanda chote kilichomtengeneza, akaua, kisha tukaondoka. Lengo lile la kumuamrisha kuua kiwanda kazima, lilikuwa kwa ajili ya siri hii nibaki nayo peke yangu, pia nilitaka kujua uwezo wa wa Ray Charles wa kupambana.
Baada ya hapo tulirudi huku kwa kutumia ndege ya Rais, ambaye ndio mimi, niliamua kumchukua na ndege yangu moja kwa moja ili tusipate usumbufu wa kukaguliwa uwanja wa ndege, na isitoshe katika iko kiwanda kulikuwa na uwanja wa ndege, kwa hiyo ndege ilitufuata hapo hapo, tukaondoka mimi na Ray Charles, huku kila mmoja akiwaza Lake, mimi nilichokuwa nakiwaza ni familia ya Ray Charles, sijui Ray Charles alikuwa akiwaza nini? Kwa hiyo nilivyofika nchini, kwa siri kubwa niliwatuma usalama wa Taifa wamteke mtoto wa Ray Charles bila Ray mwenyewe kujua, kwa sababu nilimzuia Ray kuonana na familia yake kwa muda. Walipomteka yule mtoto, nilimpandikiza mlipuko katika kifua chake, yaani alipasuliwa yule mtoto na kuwekewa bomu dogo tu, kama punje ya harage, kisha nikawaagiza wamrudishe kwa mama yake, kisha video ya lile tukio nikaliweka katika flash, nikamuonesha Ray Charles, alitaka kupaniki, ila nilikuwa na remote ya lile bomu alilopandikizwa mwanae, nikamwambia ukinifanyia chochote kibaya, namlipua mwanao, akawa mpole, na nikamwambia kuanzia sasa utaishi kwa ajili yangu na sio kwa ajili ya familia yako, hakuleta ubishi, na ndio maana mpaka leo unaona nipo nae" Rais alimaliza kuongea,
"na yule tuliyemzika na serikali ikasema ni Ray Charles, ni nani?" Yule bwana mwingine aliuliza,
"ni mwili wa mtu tu tulimuua na kisha tukauharibu vibaya kiasi kwamba alishindwa kutambulika, familia tukawapa majibu ya uongo kutoka hospital, wakaridhika tulipowapa na fungu kubwa la rambirambi kutoka serikalini, wakakaa kimya, wakazika mwili ule" Rais alijibu na kutabasamu,
"aisee, leo umenifungua ubongo, hata sikuwahi kuhisi kitu kama hiki" Yule bwana mwingine aliongea,
"hayo mambo nayajua mimi tu, wewe ni wa pili" Rais aliongea huku akitabasamu,
"dah, haya sasa niambie ulichoniitia ndugu yangu" Yule bwana mwingine aliuliza,
"hapa nimekuita kwa ajili ya BQ, yule mwanamke muuaji anayetafutwa na polisi" Rais aliongea na kumtazama yule bwana,
"mimi tena nipambane na BQ?, Ray Charles si yupo?" Yule bwana mwingine aliuliza kwa mshangao,
"sio kupambana kwa ngumi au mateke, nataka nikupe wizara ya katiba na sheria, maana tangu ameuawa yule mjinga niliyempa ile wizara, naona mambo bado hayajakaa sawa katika wizara hiyo, nataka umdhibiti BQ na ile mikataba yake" Rais aliongea na kumtazama yule bwana mwingine,
"Sasa jamaa yangu, mimi nitamdhibiti vipi? yaani nitafanyaje?" Yule bwana mwingine aliuliza huku akimuangalia Rais,
"hujui? wewe sheria si unaijua, tumia njia zozote kumdhibiti, lengo langu ni kumpata na auawe" Rais aliongea,
"mbona unatumia nguvu kubwa kupambana na mtu anayeidai serikali? kama ana mikataba so ipitiwe kama Kuna haki apewe" Yule bwana mwingine aliongea,
"ana haki, tena asilimia themanini, ila sasa, lile eneo ambalo ndio analotaka apewe, ni eneo la serikali ambalo ilipewa ile kampuni iliyomtengeneza Ray Charles, tena walipewa kwa mkataba wa miaka kumi, wafanye chochote kisha walirudishe lile eneo kwa Tammy Semmy, sasa Tammy Semmy alishakufa, hata wale wachina wameshakufa, kwa hiyo nilichofanya ni kufungua akaunti mpya ya benki kwa kampuni ile ile ya wachina, kwa hiyo serikali inaingiza pesa za kutumia yale majengo ya wizara yaliyojengwa na wale wachina katika eneo lile, serikali iliyakodi kwa msukumo wangu mie, kisha makubaliano yalifanyika kwa kuwaleta wachina feki walioingia makubaliano na viongozi kuhusu kodi za kuweka wizara hii ya katiba na sheria, kwa hiyo basi natumia nguvu kubwa huyu mwanamke hasipate haki yake kwa sababu pale napamiliki mimi ila kwa mgongo wa kampuni hewa, yaani haipo, kwa hiyo endapo BQ atafanikiwa kupachukua, kwanza nitakosa mapato, pia serikali inaweza kuchimbua sana mmiliki wa hili jengo, nikaonekana ni mimi, hapo walipa kodi hatoweza kunielewa, yaani wananchi" Rais aliongea na kumuangalia yule bwana mwingine aliyekuwa amejishika kidevu huku akionekana kutafakari,
"wewe ni rafiki yangu sana, nimeona hii ndio njia sahihi ya wewe kutajirika na mimi kulinda mali yangu, isitoshe mimi na wewe tumejuana muda mrefu, najua hata tabia tunaendana" Rais aliendelea kumshawishi yule bwana mwingine,
"mimi nitanufaikaje hapo?" Yule bwana mwingine aliuliza,
"kodi ya lile jengo ni million mia moja hamsini kwa mwezi, kila mwezi nitakupa million ishirini na tano katika kila kodi ya mwezi, na mshahara wako kama waziri, badala ya million tano, nitakupa million kumi" Rais aliongea na kumtazama yule bwana,
"hakuna shida jamaa yangu, sasa huo uwaziri utanipaje wakati mimi sio mbunge wala sio mfanyakazi wa serikali? " Yule bwana aliuliza,
"hiyo kazi niachie mimi, kesho nakupa ubunge wa kiteuliwa, kesho kutwa unaapishwa, alafu siku inayofuata nakupa uwaziri" Rais aliongea kwa utulivu,
"haina shida jamaa yangu" Yule bwana mwingine aliongea kwa furaha,
"hizi habari usimwambie mtu hii habari, yaani nataka huu uteuzi uwe kama wa kushtukiza, hata ujifanye hujategemea kwa huu uteuzi" Rais aliongea kwa utulivu,
"Sawa mkuu" Yule bwana mwingine alijibu,
"nadhani wewe ondoka tu, haya mambo mengine yatafuata" Rais aliongea huku akisimama na kumpa mkono yule bwana mwingine, yule bwana mwingine akapokea ule mkono wa kuagana, kisha akaondoka kwa furaha, alishayaweza maisha kimzamzaa tu, aliuona utajiri mkubwa mbele yake, kiasi kwamba akawa anatabasamu kila akipiga hatua.
**************×**
Sajenti Minja alifika kituo cha polisi na ile gari ya polisi, akakuta waandishi wa habari na watu wengine pamoja na Askari wenye vyeo zaidi yake wakimsubiri kama shujaa.
Waandishi wa habari walishaanza kupiga picha gari aliyopanda Sajenti Minja, kipindi hicho Sajenti Minja alikuwa bado amekaa ndani ya gari huku akiwaza atawaambia nini wakuu wake, alikaa ndani ya gari muda mrefu mpaka watu wakapata wasiwasi. Mwisho Sajenti Minja akatelemka peke yake, watu wakawa wanangoja kama ataenda upande wa pili wa mlango wa gari ili amtemleshe mtuhumiwa, lakini ilikuwa tofauti, Sajenti Minja alienda moja kwa moja mpaka mbele ya mkuu wake ambaye bado alikuwa akishangaa hali ya Sajenti Minja,
"vipi?" Mkuu wa polisi alimuuliza Sajenti Minja,
"ametoroka" Sajenti Minja aliongea kwa sauti ya chini,
"unasemaje Minja?" Mkuu wa polisi aliuliza,
"Yule mwanamke ametoroka" Sajenti Minja aliongea tena na kumfanya mkuu wake awaangalie Askari kadhaa waliokuwepo pale,
"kamateni hii mbwa na muiweke selo" Mkuu wa polisi aliongea kwa mamlaka huku Akiwatazama wale Askari, wale Askari wakamzunguka Sajenti Minja, Sajenti Minja akanyoosha mikono mbele, ishara ya kukubali kufungwa pingu, Askari wakamfunga pingu Sajenti Minja, wakaanza kumpeleka selo, kichwani Sajenti Minja alichokuwa anafikiria ni kifungo tu, kwa kosa kama lake la kuambiwa amemtorosha mtuhumiwa, lazima afungwe, hakwepeki hiyo........
********ITAENDELEA*********
the Legend☆