Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA THELATHINI NA NANE.

_____________
ENDELEA...
______________

Uzuri alimkuta Sajenti Minja akiwa amelalia tumbo, kisogo na mgongo ndio vitu pekee ambavyo Ray Charles aliviona,

"pole sana" Ray Charles alimwambia Sajenti Minja,

"asante" Sajenti Minja alijibu huku akitetemeka, maana alishamtambua kuwa huyo ni Ray Charles, kwa maana aliyasikia maongezi yao yote yeye na daktari. Simu ya Ray Charles ikaanza kuita, Ray Charles akatoka mule katika kile chumba,

"Hoya, kesho" Raa Charles alimwambia daktari huku akitoka nje na bado simu yake ilikuwa inaita,

"hey" Ray Charles aliongea baada ya kupokea simu,

"hiyo dawa umepata au bado?" Sauti ya upande wa pili iliuliza na kufanya Ray Charles aitoe simu sikioni na kuangalia namba ya mpigaji,

"naongea na nani?" Ray Charles aliuliza,

"Dokta Smith" Sauti ya upande wa pili ilijibu,

"namba yangu umeipata wapi?" Ray Charles aliuliza,

"dawa umepata?" Dokta Smith aliuliza bila kujibu swali la Ray, Ray Charles akakata simu na kuiweka mfukoni, akaelekea kwenye gari yake na kuingia, akaitoa gari kwa mwendo wa wastani, akatoka mpaka nje ya geti la hospital, akamuona Dizonga, ila Dizonga alikuwa bado hajamuona Ray Charles. Dizonga alishtuka gari ikisimama mbele yake,

"mi naondoka, ila kuhusu matibabu ya mgonjwa wako, usimlipe kitu daktari, nitamlipa mimi" Ray Charles aliongea na muda huo Dizonga alikuwa anajiuliza huyu Ray Charles amemtambua Sajenti Minja au hajamtambua,

"wewe mbona umezubaa?" Ray Charles alimstua Dizonga,

"umeonana nae lakini, umemuona jinsi alivyo?" Dizonga aliuliza,

"nimemuona, ila alikuwa amelala" Ray Charles aliongea,

"sura umeiona?" Dizonga aliuliza,

"hapana, kwani vipi?" Ray Charles aliuliza,

"tumefanana sana, ni kaka yangu" Dizonga aliongea,

"poa, acha mimi niwahi" Ray Charles aliongea na kuiondoa gari kwa kasi sana. Dizonga akabaki amesimama huku akiwa ahamini kama ni kweli Ray Charles hajamuona Sajenti Minja.

Dizonga akatoa simu yake ili ampigie Sajenti Minja, ila kabla hajampigia, simu yake ilianza kuita, alipoangalia jina la mpigaji, alikuta ni lile la yule daktari,

"sema" Dizonga aliongea baada ya kupokea simu,

"upo wapi, muda unaenda alafu unaniweka tu hapa " Daktari aliongea kwa ukali,

"nakuja, nipo nje hapa" Dizonga aliongea na kisha akakata simu, akaanza kutembea mwendo wa haraka haraka ili kuwahi wodini.

Alifika na kuingia katika kile chumba cha vipimo, akamkuta daktari ameshikilia majibu ya x-ray,

"kaka unajua usiku huu, mimi nilitakiwa niondoke mapema ila kwa ajili yako ndio maana nipo mpaka muda huu" Daktari aliongea kwa sauti ya kinyonge ila yenye hasira,

"samahani sana, nilidhani tunaweza kuchukua muda mrefu" Dizonga aliongea,

"kwani tunafanya operation mpaka tutumie muda mrefu? Majibu haya hapa, sasa utaamua mgonjwa wako atibiwe hapa, au uondoke nae" Daktari aliongea huku akimpatia Dizonga yale majibu,

"nitaondoka nae tu. Masuala ya pesa atamaliza Ray" Dizonga aliongea,

"Ray?? kwani mimi niliongea na Ray? Ray kaja amefanya mambo yake na kuondoka, sasa unasemaje huduma yako ailipie Ray?" Daktari aliuliza kwa ukali,

"basi haina shida, shilingi ngapi?" Dizonga aliuliza,

"laki tu" Daktari alijibu na kisha Dizonga akajipekua mfukoni na kutoa pesa, akampatia daktari,

"nashukuru kwa huduma yako" Dizonga aliongea huku akiingia katika kile chumba chenye mashuka na kumtoa Sajenti Minja, kisha wakatoka ndani ya jengo la hospital na kuingia katika gari, Dizonga akawasha na kuondoka.

"hivi unajua tukio lililotaka kutokea pale?" Dizonga alimuuliza Sajenti Minja,

"bwana we, yule daktari wako nae mpuuzi, yaani ningekuwa mimi mzima, ningemtwanga makofi vibaya mno" Sajenti Minja aliongea huku hasira zake zikiwa wazi kabisa,

"hivi alivyoingia ndani ni kweli hajakuona?" Dizonga aliuliza,

"si unajua pozi langu la kulala siku hizi ni sura chini kisogo juu, hiyo ilinisaidia" Sajenti Minja aliongea,

"ilikuwa hatari, ilikuwa wote tufe" Dizonga aliongea,

"mimi ningejaribu kupambana, nisingekubali kufa kirahisi hivyo" Sajenti Minja aliongea,

"ulimshindwa ukiwa mzima kabisa, sasa utamuweza vipi sasa hivi wakati hata kutembea huwezi" Dizonga aliuliza,

"ungeona wala usingeamini" Sajenti Minja aliongea,

"aisee nimeona majibu ya x-ray yako, ila nimeshindwa hata kuelewa, nimeiangalia zaidi ya mara mbili ila bado sijaelewa kitu" Dizonga aliongea,

"si ungemuuliza daktari?" Sajenti Minja aliuliza,

"mpuuzi yule, yaani amenitoka rohoni kweli, mwanajeshi gani anakuwa mbeya mbeya vile?" Dizonga alihoji,

"kwa hiyo hayo majibu ya x-ray tutajuaje kama wewe umeshindwa kuyaelewa?" Sajenti Minja aliuliza,

"nitampelekea Dokta Smith, yeye ni mtaalam zaidi" Dizonga aliongea,

"Sasa utampataje na ulisema kuwa Ray Charles alikuzuia kuonana nae tena?" Sajenti Minja aliuliza,

"hapo ndipo mbinu za kijeshi zitatumika sasa" Dizonga aliongea na kutabasamu,

"nakuaminia D" Sajenti Minja aliongea,

"haya mambo ni taratibu tu X soldier, utapona" Dizonga aliongea na kuongeza sauti ya gari, safari ikaendelea huku story mbili tatu zikiwapunguzia umbali wa safari.

*****************

Baada ya kutoka hospital, Ray Charles akielekea moja kwa moja mpaka nyumbani kwake, aliingiza gari ndani ya geti na kutelemka haraka haraka, akaingia mpaka katika chumba alichowafungia Dokta Smith na BQ, alivyoingia tu akampatia Dokta Smith zile dawa, Dokta Smith akazipokea na kuzitoa ndani ya mfuko, akaanza kuzikagua,

"safi, sasa kaandae uji mwepesi sana" Dokta Smith aliongea huku akiendelea kufungua zile dawa,

"mbona ndani hamna Unga wala jiko?" Ray Charles aliuliza,

"katafute, usiku huu yapo maduka mengi tu uwa yanakesha" Dokta Smith aliongea huku akivuta dawa katika bomba la sindano,

"asipoandaliwa huo uji inakuaje?" Ray Charles aliuliza,

"ni sawa na kufanya kazi bure, kwa maana hizi dawa zinanguvu sana, na hapa nampa dozi kubwa, kwa hiyo ni lazima awe na kitu tumboni, vinginevyo huyu atakufa" Dokta Smith aliongea huku akimchoma BQ sindano ya mkononi,

"sawa, ngoja nikatafute" Ray Charles aliongea na kutoka nje, kitu ambacho hakusahau ni kuwafungia kwa nje, hakutaka kabisa Dokta Smith atoke nje.

Dokta Smith hakujali kufungiwa, alichokuwa anakifukiria muda huo nikuhakikisha tu BQ anapata nafuu.

Baada ya kumchoma sindano, sasa alikuwa anataka kumfunua mdomo, ili amnyweshe dawa, ila alishindwa kumnywesha, meno ya BQ yalishikana sana, yaani mifupa ya mdomo ilikuwa imekakamaa kabisa, huo ni mtihani mwingine kwa Dokta Smith, alihitaji dawa ya kuchua ili aweze kulainisha mifupa ya mdomo wa BQ.

Dokta Smith akatoa simu yake na kumpigia tena.

"tafuta dawa yoyote ya kuchuwa na ya sindano za mifupa, kisha leta upesi" Dokta Smith aliongea baada ya Ray Charles kupokea simu,

"mbona unaagiza vitu nusunusu, unataka kumtorosha nini?" Ray Charles aliuliza kwa hasira, ila hakubahatika kupata jibu, tayari Dokta Smith alikuwa ameshakata simu muda mrefu tu mara baada ya kumaliza kutoa maagizo.

Ray Charles aliiangalia simu yake na kuiweka katika siti ya pembeni, akaanza kutafuta maduka ya madawa.

Hakupata shida sana kupata duka la dawa, aliingia katika duka la dawa na kuchukua dawa alizoagizwa, kisha akaingia katoka gari na safari ya kurudi kwake ikaanza.

Ilimchukua dakika chache kuweza kufika kwake, aliingiza gari ndani ya uzio, kisha akatereka na jiko la gesi pamoja na vitu vingine alivyoagizwa.

Aliviweka vitu sebuleni, kisha akaelekea katika chumba alichowafungia Dokta Smith na BQ, mkononi alikuwa na zile dawa alizoagizwa. Alifika mlangoni na kufungua, kisha akaingia ndani, akaziweka dawa juu ya meza,

"vitu vingine vipo wapi?" Dokta Smith aliuliza,

"vitu gani? Unataka nije na jiko na unga na masufuria huku?" Ray Charles aliuliza huku akimshangaa Dokta Smith,

"we kalete, mimi si ndio nimeagiza?" Dokta Smith aliongea huku akiendelea kuchanganya dawa zake, Ray Charles akaona isiwe tabu, akaenda mpaka sebuleni na kurudi na vitu vyote,

"kachote maji nusu sufuria, na uje uwashe jiko na bandika hayo maji" Dokta Smith aliongea huku akianza kuichuwa eneo lote la kuanzia mashavuni mpaka katika shingo ya BQ.

"unapika huo uji humu humu chumbani?" Ray Charles aliuliza,

"fanya nilivyokuagiza" Dokta Smith aliongea, Ray Charles akatoka na sufuria, akaelekea mpaka sehemu lilipo bomba, na kisha akarudi na maji, akawasha jiko na kubandika sufuria ile yenye maji.

"nipo sebuleni" Ray Charles aliongea huku akiwa anatoka nje,

"usitoke, mimi nina kazi hapa, kwa hiyo uji inabidi upike wewe, mimi siwezi kushika kazi mbili kwa wakati mmoja" Dokta Smith aliongea na kumfanya Ray Charles aendelee kubaki ndani na kusimamia matayarisho ya uji.

Ila baada ya kukaa kwa dakika tano mbele ya jiko, alianza kama kukosa amani , hiyo hali aliiona hata Dokta Smith, akawa anamuangalia Ray Charles kwa jicho la wizi, alimuona jinsi anavyopata tabu.

"ebu njoo hapa, unisaidie kumfungua mdomo huyu mwanamke" Dokta Smith alimwambia Ray Charles ambaye alisogea jirani na Dokta Smith kiasi kwamba wakagusana, Dokta Smith aliruka kidogo baada ya kuhisi kuungua alipogusana na Ray Charles,

"vipi?!" Ray Charles aliuliza huku akijitahidi hasigusane tena na Dokta Smith,

"hakuna kitu" Dokta Smith aliongea huku akipanda kitandani kabisa na kupakata kichwa cha BQ, kisha taratibu akaufunua mdomo wa BQ,

"leta huo uji, upooze kidogo tumnyweshe" Dokta Smith aliongea,

"Sasa mbona bado haujaiva?" Ray Charles aliuliza,

"leta hivo hivo, lengo langu sio uive" Dokta Smith aliongea na kisha Ray Charles akarudi jikoni, akazima jiko na kutoa sufuria jikoni, kisha akafungua dirisha na kumimina ule uji kwenye bakuli kubwa, na kuliweka dirishani ili uji upigwe na upepo.

**************

Ndani ya ofisi ya katiba na sheria, alikuwepo waziri mpya aliyeteuliwa na Rais, huyu waziri mpya jina lake no Said Tambala, alikuwa bize kupitia baadhi ya sheria za nchi na mambo mengine, ila macho yake yaligota katika sheria za mikataba, alisoma sheria ya mwaka 1957 iliyosema mkataba utakuwa hai mpaka utakapotekelezwa, bila kujali wahusika wapo hai au wamekufa, cha muhimu ni nakala original ikiwepo tu. Hiki kipengele alikirudia kukisoma zaidi ya mara mbili,

"huu ni upuuzi, lazima hii sheria ifutwe" Said Tambala aliongea na kutabasamu,

"hapa ni kumuingiza king na kisha unampoteza, kuaminiana kulishakufa zamani tu, hata biblia ina hadithi nyingi sana za usaliti, kwa hiyo suala la kusalitiana lipo enzi hadi enzi" Said Tambala aliongea na kuvuta droo katika meza yake, kisha akatoa chupa ndogo, akaimimina yote katika glass, japo aliimimina yote, ila bado haikuweza kujaza glass, alichofanya aliinuka na kwenda kwenye friji ndogo iliyokuwepo ndani ya ofisi yake na kutoa energy drink ya baridi, kisha akaimimina na yenyewe katika glass ile ile yenye pombe kali, akakaa juu ya meza na kuigida ile pombe yote,

"sheria uwa zinabadilishwa ili zinufaishe wachache" Said Tambala aliongea huku akiiweka glass ya pombe mezani, kisha akainuka na maker pen mkononi, akaenda mpaka ilipo picha ya Rais, akaiweka alama ya X,

"lazima ufe" Said Tambala aliongea huku akiiangalia ile picha na pia alitabasamu....

*********ITAENDELEA*********

the Legend☆

Mkuu nami naomba uniweke kwenye tag please


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Wakuu poleni na arosto. Msione kimya, ni kwamba jamaa mpaka leo hajaonekana hewani, na pia hajatoa pia taarifa yoyote. Tuendelee kua wavumilivu wakuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Nipo soba nakula drip za kutosha..
Asante kwa taarifa na awe salama huko aliko arudi na burudani(nadhani akija na BQ atakua amepona na Ray atakua amepikishwa uji mpk ameyeyuka)

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom