Riwaya: Mkono Wa Chuma

Riwaya: Mkono Wa Chuma

RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA TANO.

____________________
TEMBEA NAYO....
____________________
"lala chini na uweke mikono nyuma" Sajenti Minja aliongea kwa sauti kubwa kidogo kwa maana waliachana umbali wa mita kama sitini hivi.

Yule kijana hakutaka kuyafuatiliza masharti ya Sajenti Minja, ndio kwanza aliichomoa bastola yake,

"kaja kuniaharibia tu utaratibu" Kijana aliongea huku akianza kupiga hatua kumuelekea Sajenti Minja, Sajenti Minja kuona hivyo akaamua kumlenga yule kijana risasi ya mguuni, ila cha ajabu risasi ililenga na kumfanya yule kijana asimame kuungalia mguu wake, kisha akatabasamu, alafu akaanza kwenda mbio kumuelekea Sajenti Minja huku akipiga risasi mfululizo, Sajenti Minja kuona hivyo, akalala chini na kubingirita ardhini, akaenda kukaa nyuma ya mwamba mkubwa huku akiendelea kusikiliza vishindo vya hatua za yule kijana, lakini hakusikia kitu, ukimya tu ulitawala, akasubiri kwa dakika tano nzima, lakini bado ukimya ulitalawa, akaamua achungulie, hakukuta mtu, akatoka kabisa katika ule mwamba huku akiangalia kushoto na kulia, pia hakuona mtu,

"fala huyu, atakuwa amekimbia tu" Sajenti Minja aliongea huku akielekea katika mwamba ule ulio ukingoni ambapo BQ alipigwa risasi, alipofika ukingoni akatupa macho yake baharini, akauona mwili wa BQ ukizidi kuyoyoma kwenye kina kirefu cha maji, Sajenti Minja akaona ni bora azunguke upande wa chini ili aingie mwenyewe ndani ya maji akautoe ule mwili.

Akashuka mpaka upande wa chini na kuingia ndani ya maji, akaanza kuyakata mawimbi, nae alikuwa ni fundi wa kuogelea. Sajenti Minja akazidi kusogea mbele huku akiwa hakati tamaa, alipofika umbali wa mita mia kutoka ulipo mwili wa BQ, alishuhudia kitu cha ajabu, aliona ule mwili ukizungushwa na maji kwa muda wa dakika nzima, kisha ule mwili ukazamishwa pamoja na mabegi yake, Sajenti minja akahisi huenda yule Dada ni mzima, sasa Sajenti Minja akaongeza kasi ya kuogelea, nae alipofika pale pale, akaanza kuzungushwa kwa kasi ya hatari, akaona anaweza kuzamishwa, akajitahidi kushindana na nguvu ya maji, mwisho wake akafanikiwa kujinasua eneo lile na kurudi nyuma,

"hapa itakuwa ni njia ya mto imepita" Sajenti Minja aliongea peke yake huku akipumua haraka haraka, na wakati huo huo alishuhudia begi moja la BQ likiibuka kwa juu, kisha likasukumwa na wimbi na kumsolegea Sajenti Minja, Sajenti Minja akalivuta na kuliweka mgongoni mwake, kisha akawa anasubiri kwa imani kuwa na mwili wa BQ nao utaibuka, alisubiri kwa saa nzima akiwa ndani ya maji, lakini hakuna kilichotokea, akaamua ampigie simu mkuu wake kwa lengo la kuongezewa nguvu zaidi, mkuu wake hakusita, akatuma askari wa doria za baharini.

Baada ya nusu saa wale Askari walikuwa eneo lile huku wakiwa na boti zao.

Sajenti Minja akawaelekeza kwa kuwaonesha eneo alipozamia yule Dada, askari wakamtaka na Sajenti Minja aingie ndani ya boti ili awapeleke eneo husika. Sajenti Minja akaingia, walienda mpaka katika lile eneo,

"hili eneo Kuna mkondo wa mto, ni ngumu boti kuingia hapa" Askari ambaye alikuwa dereva wa boti aliongea,

"nyie humu si ni waogeleaji? Zamieni mjaribu kumtafuta" Sajenti Minja aliongea,

"hapa mkuu ni kuhatarisha maisha tu, kuingia hapa na kutoka salama Haiwezekani, cha muhimu ni kuendelea kufanya doria eneo lote la bahari, huenda mwili wa huyo Dada unaweza kuibuka eneo jingine" Askari mwingine aliongea,

"sawa, nirudisheni nchi kavu, nyie endeleeni na ukaguzi mpaka asubuhi" Sajenti Minja aliongea huku akionekana hajaridhishwa na majibu aliyokuwa akipewa na wale Askari wa doria za baharini.

Ile boti ilimrudisha mpaka ng'ambo Sajenti Minja, kisha akawasisitiza wale Askari wakae mpaka asubuhi wakiutafuta mwili wa yule Dada, baada ya hapo Sajenti Minja akaondoka zake.

*******************

Yule kijana ambaye hutumiwa na Rais, aliondoka huku akiwa na hasira, hasira ya kushindwa kuipata ile mikataba, ambayo inaweza kuingiza hasara katika serikali.

Ingawa BQ alikuwa amekufa, ila bado mikataba iliitajika, kwa maana mikataba uwa inaishi miaka na miaka. Basi yule kijana baada ya kumkimbia Sajenti Minja, hakuondoka eneo lile, alitafuta upande mwingine uliopo mbali kidogo ila ambao unaweza kusimama na kuuona upande wa bahari ambao BQ alikuwa amezamishwa.

Basi yule kijana kwa kusimama eneo lile, aliweza kumshuhudia Sajenti Minja alivyokuwa anaogelea ili amuokoe BQ, pia aliweza kushuhudia lile tukio la BQ kuzamishwa na maji, ila kati ya matukio yote hayo, tukio lililompa furaha ni lile tukio la kuona eneo lile alipozamia BQ, Kuna begi liliibuka, akajua sasa inawezekana kule ndani ya lile begi kunaweza kuwa na mikataba anayoitaka yeye. Sasa wakati yule kijana akitaka kwenda chini kukabiliana na Sajenti Minja ili achukue lile begi, aliweza kuona boti ikija na askari, yule kijana ikambidi asitishe mpango wake, akawa anaangalia namna Sajenti Minja anavyoongea na wale Askari, akaona pia Sajenti Minja na wale Askari walivyoenda eneo lile alipozamia BQ na wao kushindwa kufanya chochote, na mwisho aliweza kumuona Sajenti Minja akiondoka kinyonge huku akiwa na begi lile la BQ. Yule kijana akaanza kumfuata Sajenti Minja, alimfuta mpaka katika lile eneo ambalo yule kijana aliilipua gari ya polisi na kukuta gari ikiwa bado umelala ila majeruhi walikuwa wameshaondolewa eneo la tukio.

Kijana aliweza kumuona Sajenti Minja akiongea na askari kadhaa kwa muda wa nusu saa, kisha akamuona Sajenti Minja akiingia katika gari na kuanza kuondoka, yule kijana akaanza kukimbia taratibu kuifuata gari ya Sajenti Minja, aliendelea kukimbia kwa kuachana kidogo na ile gari, cha ajabu huyu kijana hakuonekana kuchoka ingawa alikuwa anakimbia kwa kasi kulingana na mwendo wa gari.

Alizidi kukimbia na lile gari bila Sajenti Minja kujua kama anafuatiliwa. Baada ya saa zima ndipo Sajenti Minja aliweza kufika anapoishi, alishuka na kufungua geti, kisha akarudi katika gari na kuiingiza gari ndani ya geti, baada ya hapo alitelemka na kwenda kufunga geti, alafu akaelekea katika mlango wa mbele wa sebuleni na kuufungua, kisha akaingia. Alipoingia alienda moja kwa moja katika friji na kutoa maji ya baridi na kuyanywa.

Baada ya hapo akaelekea bafuni na kuvua zile nguo alizokuwa amezivaa, kwa maana zilikuwa zimeloana sana kutokana na kuingia nazo katika bahari kipindi alipotaka kwenda kuuokoa mwili wa BQ. Alipovua nguo aliamua kuoga kabisa.

Baada ya dakika chache, alitoka bafuni na kuelekea chumbani kwake, akavaa kaptula fupi na kurudi sebuleni.

"Yule jamaa aliyempiga risasi yule Dada, alikuwa ni nani? Na alimpiga kwa lengo gani? au huyu Dada ana ugomvi na upande mwingine tofauti na polisi na serikali?" Sajenti Minja alijiuliza maswali mfululizo huku ile taswira ya yule kijana wa rais ikimjia kichwani, kiukwei yeye hakumjua kama yule ni kijana wa rais, hakujua chochote kuhusu yule kijana.

Baada ya muda mrefu wa tafakari, Sajenti Minja akaichukua simu yake iliyokuwa pale mezani, kisha akaitafuta namba ya Tom na kumpigia, simu ikaanza kuita,

"upo wapi dogo?" Sajenti Minja aliuliza baada ya Tom kupokea simu,

"nipo hom, vipi Kaka?" Tom alihoji,

"kuna tukio baya sana limetokea muda mchache uliopita, tunaweza kuonana usiku huu?" Sajenti Minja aliuliza,

"ndio inawezekana, upo wapi kwani?! " Tom aliuliza,

"nipo nyumbani, ila wewe si hupajui? ngoja nije uko" Sajenti Minja aliongea,

"huku usije, we nielekeze tu, nitafika hapo" Tom aliongea,

"kwanini hutaki nije uko?! " Sajenti Minja aliuliza huku akicheka,

"utakuja siku nyingine, wewe nielekeze tu mimi nije uko" Tom alijibu,

"poa basi, we jiandae alafu nipigie simu, nitakuelekeza" Sajenti Minja aliongea,

"Hakuna shida bro" Tom alijibu na kukata simu. Sajenti Minja akainuka na kwenda kuwasha Runinga, aliamua kumsubiri Tom huku akiwa hapo hapo sebuleni.

****************

Wakati Sajenti Minja akiendelea ndani na mambo yake, huku nje yule kijana wa Rais alikuwa anaondoka baada ya kuyajua makazi ya Sajenti Minja. Yule kijana aliondoka kwa mwendo ule ule aliokuja nao, safari yake iliishia nje ya geti la ikulu, akasalimiana na walinzi, kisha akaruhusiwa kuingia, akamkuta Rais akiwa amekaa nje katika bustani,

"mkuu wa polisi amenipigia simu na kuniambia kuwa polisi wake wamejeruhiwa, pia mshtakiwa ametoroshwa" Rais aliongea huku akimtazama yule kijana,

"ndcho nilichofanya" Kijana alijibu,

"umefanikisha kumuua yule binti?" Rais aliuliza,

"ndio, nimemuua" Kijana alijibu huku akijikuna kichwa,

"mwili wake umeuweka wapi? na vipi kuhusu mikataba, umefanikiwa kuipata?" Rais aliendelea kuuliza,

"Yule binti nilimpiga risasi mbili, moja ya kifua upande wa kushoto, na nyingine ya kichwa, akaangukia baharini, sasa wakati nataka kwenda kule alipoangukia ili nikampekue katika mabegi yake, Kuna askari alitokea huku akiwa na silaha, na alinipiga mguuni, inanibidi nikimbie" Kijana alijibu,

"mjinga wewe, kwanini usingemmaliza huyo askari?" Rais aliuliza kwa hasira,

"mheshimiwa, si unajua mimi siwezi kuua mpaka unipe ruhusa?" Kijana aliuliza kwa upole,

"huyo askari ni wapi? nae ni miongoni mwa waliokuwa katika lile gari ulilolilipua?'" Rais aliuliza,

"hapana hakuwepo, ila yule askari mimi namfahamu, ni Sajenti Minja" Kijana alijibu,

"Sajenti Minja??? Ndio nani?!" Rais aliuliza,

"ni askari hodari aliyewahi kupeleleza kesi kadhaa zilizoleta matokeo chanya katika taifa letu" Kijana alijibu,

"kesi kama zipi?" Rais aliuliza,

"ile kesi ya memory card iliyobeba ajenda ya kupindua taifa, na ile kesi ya Tammy Semmy, rais aliyekuachia madaraka" Kijana alijibu kwa utulivu,

"Kwa hiyo huyo Minja ndio amepewa hii kesi tena?'" Rais aliuliza,

"ndio, jukumu la kuifuatilia hii kesi amepewa yeye, ila amekuwa kikwazo kwangu kwa leo, kwa maana nimeshindwa kuipata ile mikataba ingawa yule binti nimemuua" Kijana aliongea,

"kamuue Minja, si ulisema unaua ukiambiwa? Sasa nenda kammalize Minja, maana anaweza kuwa shida hapo mbeleni" Rais aliongea huku akijikuna kipara chake,

"Hakuna shida, hiyo kazi naenda kuifanya sasa hivi mheshimiwa" Kijana alijibu,

"sasa hivi? utampata wapi?!" Rais aliuliza,

"napajua anapokaa" Kijana alijibu,

"sawa kafanye hivyo, alafu kesho endelea kuutafuta ule mwili wa binti" Rais alitoa agizo,

"sawa mheshimiwa" Kijana alijibu,

"unaweza kwenda" Rais aliongea, kisha kijana akasimama na kuondoka.

*********

Sajenti Minja alikuwa bado yupo sebuleni, alikuwa akimsubiri Tom ambaye waliongea nae muda mchache uliopita na akamuelekeza namna ya kufika hapo nyumbani kwa Sajenti Minja.

Baada ya kama dakika tano, Sajenti Minja alisikia mlango wa sebuleni ukigongwa, akainuka huku akijua kuwa Tom amefika, ila alijiuliza mbona amekuja moja kwa moja kugonga mlango wa sebuleni, nani kamfungulia geti?

"au huenda nilisahau kufunga nilipoingiza gari?" Sajenti Minja alijiuliza huku akienda kufungua mlango wa sebuleni, hakuwa na wasiwasi kabisa, kwa maana aliamini nyumbani kwake ni eneo la amani kabisa. Sajenti Minja alipofikia mlango na kutaka kufungua, hata kabla mkono haujagusa kitasa, alishuhudia mlango ukichomoka mzima mzima kwa nguvu na kuja kumpiga, Sajenti akaanguka chini huku mlango ukimlalia kwa juu, akakurupuka huku akijiuliza ni nani aliyeingia kibabe hivyo? Sajenti Minja akainuka na kutupa macho mlangoni, hakukuta mtu, akapigwa na mshangao huku akijiuliza ni nini sasa kimetokea?

"nimetumwa kukuua" Sajenti Minja aliisikia hiyo Sauti ikitoka kwa nyuma yake na kumfanya ageuke kwa kasi, akakutana na mdomo wa bastola ukimuangalia, alipomtupia jicho mtu yule aliyemshikia bastola, akakumbuka, ni yule kijana waliyetoka kurushiana risasi masaa machache yaliyopita. Sajenti Minja akameza mate, ila mdomo ulikuwa umeshakauka muda mrefu tu, kwa hiyo hata hayo mate hayakuwepo mdomoni, na wakati huo yule kijana alikuwa akiikoti bastola yake huku akiwa hana sura ya ubinadamu hata kidogo......

**********ITAENDELEA************

the Legend☆
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA SITA

________________
TEMBEA NAYO
________________
Ila kabla yule kijana hajaruhusu risasi kutoka, Tom aliingia ghafla na yeye akakutana na hilo tukio, akataka kukimbia, yule kijana akarusha risasi iliyopiga chini pembeni kidogo ya mguu wa Tom, Tom akasimama ghafla kisha akadondoka chini kama mzigo, alipoteza fahamu baada ya risasi ile kumkosa, maana alipata mshtuko mkubwa, yeye alihisi imemkosa bahati mbaya, ila mpigaji mwenyewe ndio aliamua kupiga lile eneo makusudi, hakutaka kumpiga Tom.

Sasa Sajenti Minja akatumia mwanya huo kujitetea, akateleza akapita chini Ya meza ambapo kulikuwa na bastola ndogo, kisha akageuka na kumpiga yule kijana risasi nyingi za kifuani, ila alichoshangaa sasa, zile risasi zilikuwa zinatoboa shati tu la yule kijana na kuanguka chini, Sajenti Minja akapata hofu, akainuka na kwenda kujificha nyuma ya friji,

"mtu au robot?" Sajenti Minja alijiuliza huku akipumua haraka haraka, kisha akatoa kichwa ili amchungulie yule mtu, alipotoa tu kichwa, alikutana na risasi nyingi lakini hazikumpata, zote ziliishia katika friji, ila yule jamaa aliendelea kupiga mpaka bastola ikawa inapiga tu kelele ila haotoi risasi, hapo Sajenti Minja akaelewa sasa yule jamaa risasi zimemuishia, akawa anapanga atoke ili akimbie, kwa maana hakutaka tena kupambana na mtu ambaye risasi hazipiti katika mwili wake. Wakati Sajenti Minja akiwaza hayo, yule kijana yeye alikuwa anairudisha ile bastola katika mkanda wake, kisha akaichomoa bastola nyingine inayoitwa BROWNING HI POWER, hii ni bastola iliyotayarishwa na kuanza kutengenezwa na mtu mmoja aitwae John browning mnamo mwaka 1920, ila kabla hajaimaliza kutengeneza hii bastola, alifariki, kwa hiyo matengenezo yalimaliziwa na kampuni ya FN. Hii bastola ilitumika katika vita yote ya pili ya dunia.

sasa tuendelee na mkasa wetu, wakati yule kijana akiichomoa ile bastola, Sajenti Minja akachungulia tena, hapo ndipo alipoweza kumuona yule kijana akiwa anaikagua kama ile bastola ina risasi, Sajenti Minja alipoiona ile bastola, alishtuka, maana analijua balaa la ile bastola, maana risasi zake zilikuwa na uwezo wa kupenya hata katika ukuta mgumu, sembuse hiyo friji aliyojificha nyuma yake?
Sajenti Minja aliinama na kuishika friji kwa chini, aloposimama akainuka na ile friji, yule jamaa akashangaa kwa maana kilikuwa ni kitendo cha haraka sana. Wakati yule kijana akishangaa, alishuhudia ile friji ikirushwa kumuendea, kwa kuwa ilikuwa na kasi, akashindwa kuikwepa, ile friji ikamvaa mwilini na kwenda chini mzima mzima. Sajenti Minja akapata upenyo, akachomoka kwa kasi kuelekea nje na kumuacha yule jamaa akijiinua pale katika sakafu huku ile friji ikiwa pembeni yake. Alijiinua na kusimama, kisha akampita Tom ambaye bado alikuwa amepoteza fahamu, yupo chini.

Yule jamaa akatoka mpaka nje na kupepesa macho kushoto na kulia, kisha akapiga hatua kuelekea nje ya geti, alipotoka tu nje ya geti, alishika ile njia aliyokuja nayo na kuanza kuondoka kwa mwendo wa haraka haraka.

Tom alikuja kupata fahamu baadae sana, alipofungua macho, aliikuta hali ya kutisha pale sebuleni, vitu vilikuwa katika mazingira ya hovyo, alikuta maganda kadhaa ya risasi yakiwa yamezagaa chini. Tom akainuka na kupepesa macho kushoto na kulia, kisha akaona bora aondoke zake, hakutaka kujua hali ya Sajenti Minja, wala hakutaka kujua Sajenti Minja yupo wapi muda huo.

Tom alianza kuondoka kwa mwendo wa kukimbia, ila alipofika getini tu na gari ya polisi nayo ilikuwa inafika hapo nje ya geti,

"huu msala sasa" Tom alijisemea huku akisimama na hasijue atajiteteaje ili polisi wamuelewe.
Polisi wakatelemka kwa kasi, kisha wakamuelekezea mitutu Tom,

"lala chini" Askari mmoja aliongea kwa sauti kubwa, Tom akalala chini huku akijilaumu kwa kuukubali wito wa Sajenti Minja.

"wewe ni nani na unafanya nini kwenye nyumba ya watu?" Askari yule aliuliza huku akiwa anamkanyaga mgongoni Tom,

"muache huyo" Sajenti Minja aliongea huku akitelemka katika gari lile waliotelemka wale Askari wingine, Tom aliisikia sauti ya Sajenti Minja, akapata tumaini, aliona mtu pekee wa kusema ukweli ni Sajenti Minja.

"kwanini tumuache?" Askari mwingine aliuliza,

"wakati tukio linatokea, huyo nae alikuwepo ndani, alikuwa mgeni wangu" Sajenti Minja aliongea huku akimvuta mkono Tom ili ainuke, Tom akainuka huku akimshukuru Mungu kwa namna alivyomtendea wema muda huo.
"vipi, upo salama?" Sajenti Minja alimuuliza Tom,
"mi mzima" Tom aliongea huku akijifuta vumbi lililomtapakaa baada ya kuangushwa na polisi,
"huyu jamaa aliyenivamia ulimuona wakati akitoka?" Sajenti Minja alimuuliza Tom,

"bwana we, mimi nimezinduka nimejikuta nipo peke yangu, nimekuta sebule ipo hovyo hovyo, nilichoamua kufanya ni kuondoka mbio tu, ndio kwa bahati mmenikuta hapa mlangoni" Tom aliongea huku akiwatazama Askari wengine ambao nao walikuwa wakisikiliza maelezo yake,

"Mkuu hatujaona kitu chochote cha hatari zaidi ya maganda ya risasi tu, kwa hiyo unaweza kurudi tu ndani kuendelea na shughuli zako" Askari mmoja aliongea huku akitoka ndani kwa Sajenti Minja, na nyuma yake walikuwepo askari wengine watatu walioongozana nae,

"humu sikai tena, hapa nitaingia tu kubadili nguo, alafu nitapahama hapa kwa muda" Sajenti Minja aliongea huku akiingia ndani, na wale polisi walibaki nje wakimsubiri pamoja na Tom.

Sajenti Minja aliingia ndani kwake, akavaa surual na sweta jepesi, kisha akachukua simu zake na kuziweka mfukoni, akachukua pia lile begi la BQ aliloliopoa baharini, kisha akatoka mpaka nje ya nyumba yake na kuwakuta Askari wenzake wakimsubiri.

"sasa mkuu sisi tunaomba tuondoke, nadhani tumeshafanya ukaguzi wa hawali" Askari mmoja alimwambia Sajenti Minja,

"tunaondoka wote, itabidi mnisaidie kutafuta lodge moja tulivu ili nikae kwa muda, kwa maana hapa kwangu sio salama tena" Sajenti Minja aliongea,

"Mkuu si una usafiri wako, kwanini usiutumie huo" Askari aliuliza,
"hapa hakuna kitu ambacho naamini kipo salama, huenda hata yule bwana aliyenivamia ameacha mabomu humu" Sajenti Minja alijibu,

"sawa mkuu, twendeni jamani" Askari mwingine aliongea kisha Askari wakaingia katika gari walilokuja nao,
"Tom, ingia katika gari, bado nina maongezi na wewe" Sajenti Minja alimwambia Tom,

"aah, sawa" Tom alijibu na kwenda kurukia katika bodi ya land cruiser ya polisi, lakini aliteleza na kuanguka chini, polisi wakamcheka,

"mwanaume unatakiwa uwe mkakamavu, sio lazy lazy hivyo" Polisi mmoja alimwambia Tom ambaye alikuwa akiugulia maumivu chini, kisha akasimama kinyonge na kuingia katika gari, gari ikaondoka.

Gari ya polisi ilitembea mpaka nje ya hotel moja kubwa ya ghorofa, ikasimama, na kisha Sajenti Minja akatelemka,

"shuka Tom, tumefika" Sajenti Minja aliongea kisha Tom akashuka katika gari, Sajenti Minja akaagana na wenzake, kisha ile gari ya polisi ikaondoka.

Sajenti Minja alianza kupiga hatua kuelekea katika geti la Ile hotel, Tom alikuwa akimfuata kwa nyuma. Walifika getini na kueleza shida yao, wakaelekezwa sehemu ya mapokezi ilipo, wakanyoosha mpaka mapokezi, wakamkuta dada mmoja nadhifu akiwa amekaa ndani eneo moja zuri lililozungukwa na vioo na kuacha kanafasi kadogo kama dirisha kwa ajili ya kuwasiliana na wateja wanaofika hapo.

Sajenti Minja na Tom wakamsabahi mwanadada yule, nae akaitikia kwa uchangamfu, kwa kweli alijua kuchangamkia wateja,

"nahitaji chumba" Sajenti Minja aliongea mara baada ya salamu,

"chumba au vyumba? maana mpo wawili" Mwanadada aliuliza huku akitabasamu,
"chumba komoja tu, huyu amenisindikiza tu" Sajenti Minja alijibu kwa utulivu,
"sawa kaka, chumba utapata. Je unapenda by ghorofa ya juu, ya kati so chini?" Mwanadada aliuliza,

"chini, juu nitakuwa napata uvivu kupanda" Sajenti Minja alijibu na kumfanya yule mwanadada acheke,

"jina niandike nani?" Mwanadada aliuliza huku akipeleka vidole vyake katika vitufe vya kompyuta yake iliyopo mezani,

"Joel Minja" Sajenti Minja alijibu,

"nipatie na kitambulisho chako" Mwanadada aliongea huku akiandika jina, na wakati huo Sajenti Minja alitoa kitambulisho chake na kuweka katika kidirisha kile, mwanadada akakichukua na kukiangalia kwa muda,

"kumbe ni polisi?, bora uje utusaidie na kulinda" Mwanadada alimtania Sajenti Minja,

"hata usijali, nitakuja kukesha hapa na wewe ili tuimarishe ulinzi" Sajenti Minja nae aliongea kwa utani,

"chukueni funguo hii, lifti ile pale, mkifika ghorofa ya kwanza mtakuta wahudumu wamevaa sare kama nilizovaa mimi, uwape huu ufunguo, watakuongoza mpaka chumba husika" Mwanadada aliongea,

"ok, asante" Sajenti Minja aliongea na kuelekea katika lift huku Tom akiwa nyuma yake. Walifika ghorofa husika na kukuta wahudumu, wakawapa ile funguo, kisha wakaongozwa mpaka katika chumba husika, baada ya hapo muhudumu akaondoka na kuwaacha Tom na Sajenti Minja tu.

"kwa kuwa muda umeenda sana, ngoja nikueleze kitu ambacho niliikutia, na kwa bahati nzuri yule bwana aliyekuja kunivamia umemuona vizuri kabisa, sasa yule bwana usiku huu kabla hajanivamia, nilimkuta kule baharini akimpiga risasi yule dada kichaa anayetuhumiwa kwa mauaji ya vigogo wa serikali" Sajenti Minja aliongea na kumtazama Tom aliyekuwa makini kusikiliza,

"yule dada kichaa amepigwa risasi?" Tom aliuliza kwa mshangao,

"amepigwa bwana, na sidhani kama yupo hai tena, kwa maana alipelekwa na maji mpaka katika kina ambacho kuna muingiliano wa maji ya bahari na mto, ndipo akspotelea hapo. Sasa sijajua huyu jamaa ambaye amekuja kunishambulia, ana uhusiano gani na yule dada, na kwanini amuue, na pia kwanini atake kunidhuru na mimi?" Sajenti Minja aliuliza huku akijua fika kati yao hapo, hakuna mwenye jibu,

"alafu nimekumbuka, yule jamaa ndiye niliyemuona siku ile pale guest, ulipokuja na tukamkuta yule dada wa guest akiwa amekatwa mkono" Tom aliongea,

"kumbe ni huyu? sasa ni nani?" Sajenti Minja aliuliza,

"swali gumu hilo, ila sio mtu mzuri kabisa" Tom aliongea,

"sio mzuri kwangu, kama angekuwa mbaya kwako, angekuua pale kwangu, wewe si ulipoteza fahamu na bado hajakudhuru" Sajenti Minja aliongea,

"kweli, ila huyo jamaa unatakiwa nae umfuatilie kwa ukaribu" Tom aliongea,

"alafu cha kushangaza, yule jamaa huenda sio mtu wa kawaida, maana nimempiga risasi nyingi tu, ila sijakuta hata tone la damu, au unataka kuniambia risasi zote nilimkosa?" Sajenti Minja alimuuliza Tom,

"sasa mimi nitajuaje kama ulimkosa au ulimpata?" Tom nae aliuliza,

"napata mashaka kuhusu mtu huyu, huenda sio mtu wa kawaida" Sajenti Minja aliongea,

"ndio hivyo, inapaswa umfuatilie kwa ukaribu" Tom alijibu,

"sawa, sasa wewe unaweza kwenda, nilitaka nikupe habari tu za yaliyojili leo uko baharini" Sajenti Minja aliongea,

"alafu hilo begi mbona kama la yule dada kichaa?" Tom aliuliza mara baada ya kuliona begi la BQ,

"ndio unaliona sasa hivi?" Sajenti Minja aliuliza huku akishangaa,

"nimeliona muda tu, nilikuwa natafuta muda sahihi wa kuuliza" Tom alijibu,

"ndio, hili begi ni la yule dada kichaa, liliibuliwa na maji baada ya yule dada kuzama, tena ngoja niangalie kilichopo ndani" Sajenti Minja aliongea huku akilifungua zipu lile begi, akamwaga vitu sakafuni, hakukuta kitu zaidi ya nguo tu.

"Kuna nguo tu" Sajenti Minja aliongea huku akifungua na zipu ndogo ndogo za pembeni, ambazo nazo hazikuwa na kitu.

"haya bwana, acha mimi niondoke, tutawasiliana zaidi" Tom aliongea huku akiinuka kitandani,.

"poa dogo, mimi hata sikutoi" Sajenti Minja aliongea,

"usijali " Tom aliongea huku akitoka nje na kumuacha Sajenti Minja akizirudisha nguo za BQ ndani ya begi.

******************

Ndani ya msitu mmoja wanaonekana watu wawili wenye umri wa makamo, mmoja ni mzungu na mwingine ni mtu mweusi.
Mzungu alikuwa na begi mgongoni na mkononi alikuwa na jembe dogo, wakati mswahili alikuwa na camera aliyeitundika shingoni, na mkononi alikuwa na karatasi kadhaa na katika mfuko wake wa shati alichomeka kalamu.

Walisogea mpaka eneo la mtoni, wakachutama na kuanza kunawa mikono na miguu. Wakiwa bado wanaendelea na zoezi lao hilo, waliweza kuona mabegi mawili yakiongozana ndani ya maji, wakashtuka,

"yatakuwa mabegi ya watalii nini?" Mzungu aliuliza huku akijaribu kuyazuia, lakini yule mswahili hakujibu, aliinua shingo na kutazama kule mabegi yanapotokea, hakuona kitu yalikuwa ni mabegi ya BQ, mara wakaona maji yakija na damu, hapo wakashtuka, maana huo mto una mamba wengi sana, wakatoka pale na kuanza kukimbia kule mabegi yalipotokea, baada ya dakika moja ya kukimbia, waliweza kuona kundi la mamba likishambulia kitu, mamba walikuwa wanagawana tu vipande vya nyama,

"ni mtu yule, atakuwa mtalii ameangukia mtoni" Mzungu aliongea kwa masikitiko wakati mswahili alikuwa bize akichukua picha za lile tukio.....

***********ITAENDELEA**********,

the Legend☆
 
RIWAYA : MKONO WA CHUMA.

MTUNZI : ALEX KILEO.

SEHEMU YA KUMI NA SABA.

___________
ENDELEA...
_____________
Wakati wakiendelea kutazama namna mamba wanavyogawana ridhiki yao, huku yule bwana mwingine akiwa bize na camera yake kuchukua matukio, ghafla aliiondoa camera machoni na kutupa macho pembezoni mwa mto, akapata mshangao,

"Dokta Smith, yule sio mtu kweli?" Yule bwana mswahili alimuuliza yule mzungu huku akionesha kwa kidole upande ule ambapo aliuona mwili wa mtu. Yule mzungu aitwae Dokta Smith, akatupa macho upande ule, akaweza kuuona mwili wa mwanamke ukiwa ufukweni katika mto, Dokta Smith ikabidi asogee mpaka lile eneo, maana sio rahisi kuwe na mtu wa kawaida eneo lile, tena mwanamke kuwepo katikati ya ule msitu wa kutisha.

Dokta Smith alipomsogelea, alimkuta yule binti akiwa amelalia tumbo, pua na mdomo vilikuwa chini, kwa hiyo hakuwa na uwezo wa kupumua, Dokta Smith akamgeuza kwa haraka, akaona ana tundu la risasi kichwani, akashtuka, ila haikumzuia kupeleka mkono wake katika kifua cha binti ili aangalie mapigo ya moyo ya yule dada, hakubahatika kusikia kitu, ikambidi aichane fulana aliyoivaa yule mdada na kumfanya kubaki maziwa yakiwa nje, aligundua kuwa kifuani kwa yule binti Kuna tundu jingine la risasi,

"huyu ni jangili nini amepigwa na Askari wa msituni?" Dokta Smith alijiuliza huku akipapasa tundu la risasi lililopo kifuani kwa yule dada,

"we mzungu unataka kufanya nini hapo? Mbona unampapasa maziwa huyo maiti?" Yule mswahili aliuliza huku akiwa mbali na eneo alilokuwa Dokta Smith,

"sogea ili uone ninachokifanya, huyu dada amepigwa risasi" Dokta Smith aliongea huku akipekeka sikio lake katika kifua cha yule dada, tena upande ambapo moyo unasadikiwa unakaa. Baada ya kupeleka sikio na kulikandamiza kwa nguvu kifuani kwa yule dada, aliweza kusikia mapigo ya moyo ya yule dada yakipiga kwa mbali, Dokta Smith akafungua begi lake na kutoa dawa ya maji na kumnywesha yule binti, kisha akambeba na kumuweka begani,

"beba yale mabegi, yatakuwa ni mabegi yake tu" Dokta Smith alimwambia mwenzake ambaye muda wote alikuwa na camera akichukua kila tukio na kisha alitumia muda mdogo kuandika katika karatasi yake.

"mhmmmm, huyu mzungu nae kwa kujipa majukumu, sasa ameokota mtu anamatundu ya risasi, yeye anabeba tu, hata kama Dokta sio kwa dizaini hii" Mswahili aliongea huku akielekea ule upande ambapo mabegi yalikuwepo, alipoyafikia aliinama na kuyabeba, kisha akafuata ile ile njia aliyoelekea Dokta Smith.

Alitembea kwa mwendo wa dakika kumi mpaka alipofika katika sehemu moja ambapo kulikuwa na uzio wa wavu ulioshikiliwa na vyuma vilivyochimbiwa chini, ule uzio wa wavu ulikuwa umezunguka hema moja kubwa lililokuwa katikati ya uzio ule.

Yule bwana Mswahili alipofika pale alifungua komeo na kisha akaingia ndani ya uzio, alafu akafunga mlango wa uzio kwa kutumia kufuri kabisa, kisha akaelekea katika hema na kumkuta Dokta Smith akiwa amemlaza yule binti ambaye hakuwa na mkono mmoja, na pia Dokta Smith alikuwa akitwanga mizizi ya miti, ambayo ile mizizi ilitoa maji ambayo aliyajaza katika kikombe na kumnywesha yule dada.

"huyo mzima kweli?" Mswahili aliuliza huku akimtupia jicho yule dada ambaye alikuwa hajitambui,

"anapumua kwa mbali, nadhani alizamishwa na maji, maana nilimkamua tumbo na ametapika maji mengi tu, sasa hapa nampa dawa ya kumuongezea nguvu, ili baadae nimuondoe hizo risasi" Dokta Smith aliongea huku akijaribu kumvua suruali yule dada,

"wewe bwana wewe, usimvue" Mswahili aliongea huku akimtazama yule dada kwa uchu,

"mwili wake unahitaji hewa ya kutosha kwa ajili ya kurejesha fahamu yake. Kama hutoweza kuvumilia nenda kakae nje tu" Dokta Smith aliongea huku akiwa ameshaitoa mwilini ile suruali ya dada, kisha akamtoa na nguo ya ndani, na kumuacha hapo, akatoka nje kuendelea na shughuli zake,

"na wewe toka uko ndani, huyo ni nusu mtu nusu mfu, usije ukaendekeza tamaa zako ukamuua bure binti wa watu" Dokta Smith alimwambia yule Mswahili,

"nenda uko, mimi sio mtu wa hivyo" Mswahili aliongea huku akitoka ndani ya hema.

**************

Asubuhi hii ilimkuta Sajenti Minja akiwa njiani akielekea kituo cha polisi, alipanga kuonana na mkuu wake, alitaka kumpa taarifa juu ya upelelezi wake ulipofikia.

Sajenti Minja alifika kituoni na kuelekea moja kwa moja mpaka katika ofisi ya mkuu wa polisi, akagonga mlango na kukaribishwa, akaingia na kutoa heshima kwa ukakamavu,

"kaa" Mkuu wa polisi aliongea kisha Sajenti Minja akakaa katika kiti,

"jana baada ya yule mwanamke mtuhumiwa kukamatwa, nasikia gari ya polisi ilipata ajali na kisha yule mwanamke akatoroka. Je ulifika eneo la tukio?" Mkuu wa polisi alimuuliza Sajenti Minja, Sajenti Minja akakaa kimya kidogo kisha akamuangalia mkuu wa polisi, akakuta yupo bize na makabrasha yake yaliyopo juu ya meza,

"nilifika muda ule ule wakati ajali imetokea, ila nilichogundua ni kuwa ile ajali sio ya bahati mbaya, ni ajali iliyosababishwa na mtu" Sajenti Minja aliongea na kumfanya mkuu wa polisi amtupie jicho,

"kivipi?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"mimi nilifika wakati ajali ikitokea, ila baada ya ajali niliweza kumuona mwanaume mmoja akikimbia na yule dada mtuhumiwa, walikimbia mpaka eneo la ufukweni upande wa juu, mimi nilikuwa nawafuatilia tu. Walipofika pale ufukweni, walisimama na kuanza kuongea, sikuweza kuwasikia kwa kuwa nilikuwa mbali kidogo. Ila ghafla nilishuhudia yule kijana akichomoa bastola na kumuelekezea yule dada mtuhumiwa, nikiwa katika hali ya taharuki, niliweza kumshuhudia yule mwanaume akimpiga risasi ya kifua yule binti, papo hapo tena akampiga risasi ya kichwa, yule binti akaangukia baharini, na mimi nikajitokeza na kumtaka yule kijana ajisalimishe, lakini hakujisalimisha, akaanza kunishambulia, nikajificha nyuma ya mwamba, nilipoona milio ya risasi imepoa, nikachungulia, ila sijakuta mtu, nikatoka mbio mpaka katika eneo alipoangukia yule dada mtuhumiwa, nikamuona akielea ndani zaidi ya maji, ikabidi niingie baharini ili nimuokoe, ila sikufanikiwa, yule dada alizamishwa na maji, baada ya muda liliibuka hili begi tu" Sajenti Minja aliongea huku akilinyanyua lile begi la BQ,

"umelikagua hilo begi?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Kuna nguo tu, sijabahatika kupata kitu kingine" Sajenti Minja alijibu,

"kwa hiyo huyo dada alikutoroka kwa mbinu hiyo?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"hapana hakunitoroka, ila atakuwa amekufa na amesombwa na maji, ni ngumu sana mtu kupigwa risasi ya kichwa na kupona" Sajenti Minja alijitetea,

"utasemaje amekufa wakati mwili bado haujapatikana? Kupigwa risasi ya kichwa sio sababu ya kufa. Unamfahamu 50 cent yule msanii wa marekani, alishawahi kupigwa risasi tisa, na nyingine zilimpiga kichwani, ila mpaka leo anaishi" Mkuu wa polisi aliongea,

"ni bahati sana kwa mtu kupigwa risasi na kuishi, ila siwezi kukataa husemi wako, kuwa nisiseme amekufa mpaka mwili wake upatikane" Sajenti Minja aliongea,

"sio husemi wangu, hiyo ndiyo kanuni ya kipelelezi" Mkuu wa polisi aliongea,

"sawa mkuu" Sajenti Minja aliongea,

"pia jana nimesikia umevamiwa usiku, na ulirushiana risasi na mtu" Mkuu wa polisi aliongea,

"ni kweli, na aliyenivamia ndio yule yule kijana aliyempiga risasi yule binti mtuhumiwa" Sajenti Minja alijibu na kumfanya mkuu wa polisi avue miwani na kumtazama,

"kwanini alikuvamia, hakukupa sababu?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"hakunipa, nadhani alikuja kuniua tu, hakuja kujadiliana" Sajenti Minja alijibu,

"pia nimesikia ulitumia risasi nyingi sana kupambana na huyo mtu, imekuwaje risasi zote zimemkosa?" Mkuu wa polisi aliendelea kuuliza,

"sio zote zimemkosa, asilimia themanini ya risasi nilizomrushia zilimpiga" Sajenti Minja alijibu na kumfanya mkuu wake ashangae,

"kama umempiga mbona hakupata jeraha na wala hakufa" Mkuu wa polisi aliuliza,

"Yule sio mtu wa kawaida" Sajenti Minja alijibu,

"ni mchawi? kumbuka sisi hatuamini katika hizo imani" Mkuu wa polisi aliuliza huku akiendelea kupekua makabrasha yake,

"sijasema ni mchawi, ila katika risasi zote nilizompiga, hakuna hata moja iliyopenya katika mwili wake" Sajenti Minja aliongea,

"kwa hiyo unataka kusemaje sasa?" Mkuu wa polisi alihoji,

"kwa sasa sina cha kasema, ila nitapofanikiwa kukutana nae tena, nitakuwa nimepata jibu" Sajenti Minja aliongea,

"ila sura ya huyo mwanaume si umeikariri?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"ndio, ingawa sio kwa asilimia mia" Sajenti Minja alijibu,

"ukitoka hapa pitia ofisi namba nane, utakutana na mchoraji, mpe maelezo ili amchore huyo mtu" Mkuu wa polisi aliongea,

"sawa mkuu" Sajenti Minja alijibu,

"vipi kuhusu kifo cha waziri wa katiba na sheria, umefikia wapi?" Mkuu wa polisi aliuliza,

"na hilo pia nilitaka kulizungumzia, nilichogundua pia, kuwa kifo cha waziri wa katiba na sheria sio kazi ya yule dada mtuhumiwa, itakuwa ni kazi ya yule mwanaume aliyenivamia, kwa kuwa katika mwili wa waziri kulikuwa na matundu ya risasi, tena risasi zenyewe ni kama zile zilizofyatuliwa na yule jamaa aliyenivamia jana" Sajenti Minja aliongea,

"hiyo sio sababu ya kumuondoa huyo mwanamke mtuhumiwa katika katika kifo cha waziri, au labda kama ipo sababu nyungine" Mkuu wa polisi aliongea,

"ni hiyo tu, kwa maana nilifuatilia kuanzia kifo cha mkuu wa wilaya, kifo cha msaidizi wa mkuu wa wilaya, kifo cha mkuu wa mkoa na kifo cha naibu waziri, hakuna hata mmoja aliyepigwa risasi, wote wameuawa eidha kwa kukabwa au kushambuliwa kwa mkono tu" Sajenti Minja aliongea na kumfanya mkuu wake amuangalie huku akionesha hilo neno limemuingia,

"nenda katoe maelezo ya mchoro, kesho mapema ulete huo mchoro" Mkuu polisi aliongea na kumfanya Sajenti Minja ainuke na kutoka nje,

"huyu mzee bwana, mimi naongea yeye anapinga. Ananifundisha kazi??? sasa akaifanye yeye" Sajenti Minja aliongea huku akielekea katika ofisi namba nane, ofisi inayohusiana na mambo ya michoro.

************

Kule msituni, baada ya nusu saa ya kumuacha BQ dawa ifanye kazi mwilini, Dokta Smith alirudi ndani ya hema na kukagua yale matundu ya risasi, kisha akaenda mpaka katika sanduku lake kubwa lililotengenezwa kwa bati, akafungua na kutoa vifaa vipya kabisa via upasuaji, vilikuwa vifaa vya kisasa. Dokta Smith akavaa mipira mkononi, na kuusogelea mwili wa BQ, kisha akapeleka kisu katika kifua upande wa kushoto kabisa, na kupasua kidogo katika eneo ambalo risasi iliingia, kisha akaingiza kifaa kidogo chenye umbo kama la bikali, ila chenyewe hakikuwa na ncha kali.

Baada ya kuingiza kifaa kile, akakivuta juu, kikatoka na risasi, Dokta Smith akaiweka ile risasi katika mfuko mdogo wa nailoni, kisha akamshona BQ katika jeraha.

"umeshaanaza kumtoa risasi kumbe?" Mswahili aliongea huku akiingia ndani,

"ndio, nimeanza na hii ya kifuani kwa kuwa haikuwa eneo baya sana, ingawa ilichimba sana ila ilipita mbali na moyo" Dokta Smith aliongea huku akimalizia kushona jeraha la kifuani kwa BQ,

"sasa hiyo iliyoingia kichwani si ni hatari zaidi?" Mswahili alihoji huku akimtazana BQ ambaye alikuwa amelala bila fahamu,

"hii hatari kweli, ila haijaingia sana, huenda imepasua kidogo fuvu la kichwa, angekuwa mjini angefanyiwa x-ray ili kujua kama imeingia sana" Dokta Smith aliongea,

"sasa si tupeleke tu mjini?! " Mswahili alitoa pendekezo,

"hii risasi kuendelea kukaa kichwani ni hatari zaidi, kwa maana kuna risasi nyingine zina sumu, inavyozidi kukaa mwilini ndivyo inavyozidi kuhatarisha maisha" Dokta Smith aliongea,

"alafu katika mabegi yake hatukukagua" Mswahili aliongea huku akivuta begi moja na kulifungua, akakuta vipande vya vyuma vilivyotengenezwa katika umbo la mkono,

"huo ni mkono wake wa kutumia, si unaona hapa hana mkono mmoja?" Dokta Smith aliongea huku akimpora yule Mswahili ule mkono na kuanza kuuangalia yeye,

"sasa ndio unipore, we mzungu gani una mambo ya kiswahili" Mswahili aliongea kwa jazba huku akilichukua lile begi jingine na kulifungua, akatoa laptop ndogo na kuikagua kwa kuigeuza geuza, kisha akaweka pembeni na kuingiza tena mkono ndani ya begi, akatoa mfuko wa Rambo uliokuwa na karatasi ndani yake, akazitoa zile karatasi,

"hii mikataba" Mswahili aliongea huku akianza kuisoma,

"mikataba inahusu nini?" Dokta Smith aliuliza,

"sasa si ungoje nimalize kuisoma" Mswahili aliongea kisha akaendelea kuisoma, akashtuka baada ya kusoma jina la huyo mwanamke, kisha akasimama na kwenda kumuangalia vizuri,

"vipi?" Dokta Smith aliuliza baada ya kumuona mwenzake akimtazama kwa mashaka binti yule,

"ah hakuna kitu" Mswahili alijibu huku akiendelea kutazama, hata furaha aliyokuwa nayo hapo hawali ilipotea,

"Kuna nini kwani?" Dokta Smith aliuliza huku akiinyakua ile mikataba na kuanza kuisoma yeye, aliisoma kwa muda mchache tu,

"kumbe huyu mwanamke ana utajiri mkubwa? ndio maana umehamaki" Dokta Smith aliongea huku akiendekea kuisoma ile mikataba,

"tatizo sio utajiri, huyo mwanamke namjua vizuri, tena vizuri sana" Mswahili aliongea huku akielekea nje, hakuwa tena na amani kuanzia muda huo.

Dokta Smith akaamua amuache tu, akaona atamuuliza baadae kuwa amemjuaje huyo mwanamke.

Dokta Smith akaendelea na kazi, muda huu alikuwa anamtoa ile risasi ya kwenye kichwa, hii ilimchukua muda wa saa na nusu mpaka alipofanikiwa kumtoa ile risasi, kisha akamfunga bandeji.

Baada ya hapo Dokta Smith aliingia msituni kuendelea kutafuta mizizi na miti kwa ajili ya utafiti anaoufanya wa kutengeneza dawa.

*************

Mswahili tangu asome ile mikataba na kulijua jina la yule dada, alijikuta akiwaza sana, kwani anamfahamu vizuri yule dada, na isitoshe anajua kuwa yule dada alishakufa muda tu kutokana na ajali ya ndege, na mbaya zaidi anamfahamu fika ukatili wa huyo dada.

"huyu sio wa kuishi, ni wa kufa tu" Mswahili aliongea huku akiingia ndani ya hema, akapekua sanduku la Dokta Smith na kuchukua bomba la sindano, kisha akachukua kichupa kidogo cha dawa, kilichoandikwa pembeni "POISON" akaingiza sindano katika kile kichupa na kuivuta ile sumu, kisha akamsogelea BQ aliyekuwa amelala hajitambui, akamchoma ile sindano mkononi katika mshipa, na kuiminya ile dawa, kisha akalitupa lile bomba la sindano na kuirudisha ile sumu katika sanduku la Dokta Smith.

Baada ya hapo Mswahili akachukua camera yake na kuelekea msituni, alishatimiza adhma yake, sasa angalau alipata amani, maana tayari alishaua, aliamini amemuua mtu mbaya kabisa, amemuua kiumbe ambaye hastahili kuishi.
Ni kweli, BQ hakustahili kuishi tena.

**********ITAENDELEA************

the Legend☆
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom