Riwaya: Mke wa Rais

Nilimpoteza mtu muhimu sana katika maisha yangu. Picha mnayoiona hapo ni yakipenzi changu Neema. Mwanamke ambaye alikuwa ndio furaha yangu. Lakini Mungu aliamua kunipokonya kwa kuwa alimpenda kuliko mimi. Ndio nimeinuka naendelea kukusanya nguvu ili kuifikisha tamati. Nipo kwenye kipindi kigumu sana lakini nisameheni sana kwa muda wote huo.
 
Pole sana ibra. Maumivu ya msiba ni makali mno,mwaka uishe tu hata mie yalinikuta.
Nilimpoteza mtu muhimu sana katika maisha yangu. Picha mnayoiona hapo ni yakipenzi changu Neema. Mwanamke ambaye alikuwa ndio furaha yangu. Lakini Mungu aliamua kunipokonya kwa kuwa alimpenda kuliko mimi. Ndio nimeinuka naendelea kukusanya nguvu ili kuifikisha tamati. Nipo kwenye kipindi kigumu sana lakini nisameheni sana kwa muda wote huo.
 
Nilimpoteza mtu muhimu sana katika maisha yangu. Picha mnayoiona hapo ni yakipenzi changu Neema. Mwanamke ambaye alikuwa ndio furaha yangu. Lakini Mungu aliamua kunipokonya kwa kuwa alimpenda kuliko mimi. Ndio nimeinuka naendelea kukusanya nguvu ili kuifikisha tamati. Nipo kwenye kipindi kigumu sana lakini nisameheni sana kwa muda wote huo.
Pole sana boss Kumbuka hakuna jipya chini ya jua
 
Nilimpoteza mtu muhimu sana katika maisha yangu. Picha mnayoiona hapo ni yakipenzi changu Neema. Mwanamke ambaye alikuwa ndio furaha yangu. Lakini Mungu aliamua kunipokonya kwa kuwa alimpenda kuliko mimi. Ndio nimeinuka naendelea kukusanya nguvu ili kuifikisha tamati. Nipo kwenye kipindi kigumu sana lakini nisameheni sana kwa muda wote huo.
Pole sana mkuu ibra87,.may her soul rest in peace
 
Pole Sana mkuu kwani alipangalo mungu Hakuna binadamu yoyote atakayeweza kulipangua cha msingi ni kumuombea dua aishi kwa Amani ktk makazi yake YA milele
 
MKE WA RAIS

MTUNZI: Ibrahim Masimba

Phone: 0743990480

WhatsAPp :0675191162

Ilikuwa kazi ngumu na ya hatari ambayo ilikuwa mbele yao. Ulikuwa ni wakati wa kuhakikisha kuwa wanarudi na watu ambao waliwahitaji. Baada ya kuuchukua ule mkoba Mudy hakuhitaji kuchelewa kuondoka katika eneo lile kwa kutokea mlango wa nyuma. Haikuwa kazi ndogo kupambana na mashirika manne ya kijasusi, mashirika ambayo yalikuwa na uwezo na nguvu kubwa sana dunia. Angewezaje kupambana na kuwashinda watu kama KGB? Ataondoka vipi mikononi mwa MOSSAD NA CIA? Alitakiwa mbinu za hali ya juu. Sikuzote Mudi hakuwa anaamini katika kushindwa. Siku zote aliamini kuwa yeye ni bora pengine kuliko hata CIA. Akaendelea usiku ule kwa tahadhali kubwa akiangalia huku na huko. Mkoba mdogo ulikuwa kwapani huku bastola mbili zikiwa umbali mdogo ndani ya mavazi yake. Mikono yake ilikuwa ikienda sambamba na macho yake. Akaupita mtaa wa kwanza na kuingia kwenye uchochoro fulani ambao ulionekana kuwa kimya kupindukia. Muda wote Mudy alikuwa alitabasamu. Muda wote MUdy alikuwa akikenua. Hakuogopa giza wala hakuhofia chochote. Alilipenda giza kama anavyopenda kupambana. Aliuchukia mchana kwa kuwa hamkumpa muda wa kufanya anachotaka. Alitembea akiiona thamani ya nchi yake ikiwa moyoni. Alibeba jukumu kubwa juu ya usalama wa Tanzania. Akaupita uchochoro na kutokea sehemu fulani ambayo ilionekana kuwa na nyumba chache sana. Licha ya kuwepo kwa nyumba hizo, pia palikuwa na ukimya wa hali ya juu. Akatembea huku tahadhali ikiongezeka. Wakati anaikaribia nyumba ambayo alihitajika kuwa pale kwa mbali akamuona mtu, akamuona mtu akipotelea kwa mbali. Ingawa palikuwa na giza lakini hakushindwa kumjua yule mtu alikuwa nani. Tembea ya mtu ambaye alikuwa mbele yake ilikuwa ni tembea ya Sohwa. Hapakuwa na utafauti na kile anachokiwaza. Alipowaza kwanini Sohwa yupo pale usiku huu!! Hakupata jibu na asingepata majibu kwa wakati ule. Mkono ukashuka kiunoni, muda mfupi mkono wake ukachomoka ukiwa umekamatia bastola. Akazidi kusogea kwenye nyumba ile, hatua chache akakiona kivuli, kivuli cha mtu. Akairudisha bastola mahali pake kisha kuinuka na kuanza kwenda taratibu kwa hatua za paka, hatua ambazo hazikusikika hata kama ungekuwa na masikio makubwa kiasi gani. Akarudi nyuma ya nyumba ile lengo likiwa kutokea kwa nyuma. Lakini kabla hajafanya chochote akausikia mngurumo wa gari ukija katika eneo lile. Akachepuka haraka na kuangukia pembeni kukwepa mwanga wa taa. Alipoanguka alijiinua tena na kusogea. Akashangaa kuwaona watu wanne wakishuka tena mikononi wakiwa na silaha nzito. Kabla Hajajua kipi ambacho wamefuata watu wale akamuona Sohwa akishuka sambamba na mwanaume mmoja wa makamo mwenye muonekano wa kutisha sana. Mudy akatulia huku akiwa makini na kila kitu. Akiwa bado anaangalia kule akamuona mtu mwingine akiruka kutoka ndani ya gari. Kushuka kwa mtu yule hakukumshangaza, kilichomshangaza ni kumuona mtu yule akienda sehemu nyingine tofauti na walipoelekea wengine na kingine ambacho kilimburudisha ni kwamba alimtambua mtu yule. Alimtambua kwa uzuri wake na utaalam wake. Huyu Alikuwa Jenifer.

Alikuwa Jenipher ndio, alikuwa yeye tena akitoka ndani ya gari ambayo walipanda watu ambao hawakuonyesha utani. Watu ambao walikuwa wamoja katika medani ya mapambano, lakini wakiwa katika mahitaji tofauti na lengo kinzani. Akatulia akiwaangalia watu wale kwa makini huku akiwa na hamu ya kutaka kujua kipi ambacho wamefuata watu wale. Huku akiwa amechutama punde akakiona kivuli kikitokea kwa nyuma yake. Akataka kugeuka nyuma lakini hakuipata nafasi hiyo. Akahisi kitu kama sindano kikichoma sehemu ya mbavu zake, akahisi ubaridi ukitamalaki mwilini. Punde akaanza kukiona kila kitu kilichopo mbele yake kikizunguka. Macho yakaanza kupatwa na giza, punde alikuwa akifumba macho huku akishindwa kuona tena.

*****************
Jenipher alikuwa amebana sehemu akiangalia kule walipoelekea watu wale. Hakuwepo pale kwa bahati mbaya bali alikuwepo kwa mpango maalum. Mpango ambao ulisimamiwa na sohwa juu ya sehemu husika ambayo waliishi watu ambao walikuwa wakitafutwa na serikali ya Tanzania. Akiwa amesimama pale akiangalia kinachoendelea mara akamuona mtu akichepuka na kuzunguka nyuma ya jengo fulani, punde akawaona watu wakirushiana makonde na muda mfupi akamuona mtu mmoja akitoka pale akiwa amemuweka mtu begani akikimbia naye. Kutoka na umbali harafu ukichanganya na giza Jennifer hakuweza kumuona mtu aliyebebwa wala kumbeba. Hilo likampa hamu ya kujua kile kilichokuwa kikiendelea kule. " ni nani amebebwa? Nani amembeba mwenzie? Na kwa nini? Yalikuwa maswali yaliomsukuma Jenifer kusogea kwa kutambaa na tumbo mpaka usawa ule ambao alimuona mtu yule akitokea. Kufikia hapo bastola yake ikatangulia mbele, akapiga hatua ya kwanza kisha ya pili, hatua ya tatu akapokelewa na mwili wa mtu ukivuja damu
 
MKE WA RAIS

Mwandishi: Ibrahim Masimba

Phone: 0743990480

WhatsAp: 0675191162

******
Hatua ya tatu akapokewa na mwili wa binadamu, mwili ambao ulionekana kulala kihasara kuonyesha kuwa haukuwa na uhai. Kengere ya hatari ikazidi kulia kichwani. Akaikamata vizuri bastola yake, akatembea zaidi kuusogelea mwili ule. Aliusogelea akihitaji kuujua ulikuwa wa nani. Kila kitu kilikuwa huru mwilini mwake. Alihitaji kurudi katika uhalisia wa kimapambano. Hapo akakumbuka alipokuwa kwenye msitu wa Katanga katika nchi ya congo. Alikumbuka Mission ile ya kuwakomboa watafiti. Akaukumbuka ugumu wa kimapambano na kimbinu aliokutana nao huko. Kulifikiria hilo kulimfanya azidi kusogea huku akijiamini zaidi. Alitembea kama paka na hata kugeuka aligeuka mfano wa bundi. Akairuhusu miguu kutembea huku macho yakishuhudia. Alitembea mdomo wa bastola ukiwa mbele tayari kwa mauaji. Akaufikia mwili na kuinama kwa makini kuugusa. Ulikuwa wa moto, ulikuwa moto kuonyesha uhai wake haukuondolewa muda mrefu. Aliamini alichokiona muda mfupi ndio chanzo, alitambua mtu alieondoka muda mfupi ndie aliefanya mauaji yale. Hakutaka kukisumbua kichwa chake kuhoji. Hakutaka kuuchelewa kuupekua mwili ule. Lakini hata alipopekua hakuambulia chochote. Akajua alieondoka pale alifanya kazi zote kuonyesha hata yeye ni Jasusi alieiva. Atakuwa nani? Hatimaye akaruhusu nafsi yake kujiuliza mwenyewe. Ni Mudy? Hapana! Angekuwa Mudy asingembeba mtu. Sasa ni nani? Bado swali lake halikuwa na majibu. Akamgeuza mtu yule akakutana na sura ambayo hakuwahi kuiona. Akaamua kuachana naye sasa alikuwa Akielekea kule ambapo walielekea Sohwa pamoja na majasusi wa CIA na KGB. Alikuwa akielekea sehemu hatari sana, alikuwa akielekea kwenye mdomo wa kifo. Akafuata ramani ambayo alipewa na Sohwa. Ramani ya kumfikisha sehemu ambayo ilikuwa ni lazima afike. Hilo likafanyika katika utimamu, hilo likafanyika katika utulivu wa mwili na kiakili. Akanesa kama kinyonga akihama hapa na kuangukia pale. Hatua kumi mbele akamuona mtu amesimama gizani. Akaona ni wakati wa kuitumia mikono yake. Akairudisha bastola mahala pake kisha kusogea adui yule kwa kuzunguka kwa upande mwingine. Akatembea kisha akafanikiwa kutokea kwa nyuma yake. Pigo moja la kareti lilitosha kumnyamazisha. Akamvuta taratibu na kumlaza chini kwa utulivu. Akaupeleka mkono mfukoni kwa maiti yule, lakini kabla hajafanya lolote akashangazwa na kishindo na sauti ya mtu Vikitokea nyuma yake. Akageuka huku muda huo huo mkono ukizama na kuibuka na bastola. Sauti ndogo mfano wa chafya ukatamalaki katika ngoma za masikio yake, muda ule ule akamuona mtu yule akipaa angani kisha kuanguka chini. Akatulia. Akaondoka hapo akisogea ndani zaidi
Kila wakati alikuwa akiitizama saa yake ya mkononi. Alitakiwa kufika sehemu aliyoambiwa na sohwa ndani ya dakika tano. Hakutakiwa kuchelewa wala kuongeza hata sekunde katika Muda ule. Saa yake ilimwambia bado dakika tano tu kwahiyo ni lazima aingie. Ilikuwa ni lazima aingie, ilikuwa ni lazima afike kwa kuwa ilikuwa ni muhimu katika kupambana na watu hatari kama KGB,MOSSAD na CIA. Ilikuwa ni kazi ya kuuza roho zao, ilikuwa kazi ya kuhatarisha maisha yao. Lakini waliibeba kazi hiyo kwa ajili ya Watanzania, na Kwa ajili ya bara la africa. Waliapa kutokupumzika mpaka pale watakapoondoka na watu wao. Akasonga mbele mpaka kuufikia mlango ambao ulikuwa ukiingilia huko anakotakiwa aende. Akabonyeza namba alizopewa na Sohwa mara akaliona lango likifunguka. Akaingia ndani huku bastola mkononi.

Alipoingia tu akapokelewa na ukimya wa ajabu kisha akalishuhudia lango likijifunga tena. Akasimama katikati ya varanda huku giza likimpa tabu kujua wapi anatakiwa kuelekea. Akachomoa kikaratasi akakiangalia akatingisha kichwa. Alipeleka macho yake kwenye saa yake, akakuta zimebaki dakika mbili tu kufika sehemu ambayo ilikuwa lazima afike. Akachepuka haraka na kuufuata mlango wa chumba cha pili, chumba ambacho alitakiwa kuingia ndani yake. CHumba ambacho ilikuwa lazima afike katika muda husika. Akaufikia mlango kisha kuchomoa kitu kama sindano na kuichomeka kwenye tundu la funguo, mlango ukaachia na kumpa uhuru wa kuingia. Muda wote mdomo wa bastola ulikuwa umetangulia mbele tayari kwa kumwaga ubongo wa mtu. Mbele ya chumba kile akawa anatizamana na mitambo mingi sana. Akafuata alichoambiwa kuwa katikati ya ile mitambo kuna kitu ambacho anatakiwa akichukue na kuondoka nacho.

*****

Wakati Jenipher akikaribia kuuchukua mzigo alioambiwa kuuchukua, huku upande mwingine Sohwa alikuwa kwenye chumba fulani sambamba na Jasusi mwenzake wakifanya mapenzi. Ilikuwa ni picha nzuri kuitizama pale Sohwa alipokuwa akiumenya mhogo na kuutumbukiza kinywani. Ilikuwa tamu pale alipokuwa akiuruhusu ulimi wake utue juu ya kichwa cha nyoka na kupalaza pale. Hakuyafanya hayo kwa mapenzi yake, hakufanya hivyo sababu alipenda kufanya hivyo, bali alifanya hayo akiuvuta muda ili Jenipher achukue kile ambacho alitaka. Kilikuwa kitendo kilichopagawisha hata wale wengine ambao walikuwa wakiisikia sauti na hata kuchungulia. Kila mmoja alituliza macho yake kuangalia jinsi Sohwa alivyokuwa akijihukumu juu ya mnazi. Alikipekecha kiuno huku akibadili mikao ya kila aina. Akafanikiwa kuwapumbaza wote, aliweza kuwafanya wote wamtizame yeye. Alifanya hivyo kwa muda maalum na kwa dakika maalum. Alijua tayari Jenipher atakuwa ameshafanikisha kile ambacho alihitaji akichukue. Kitu ambacho kilikuwa muhimu sana katika kuwapata na kuwarudisha wahaini katika ardhi ya Tanzania bila kumwaga damu za watu wengi. Pia aliogopa kushtukiwa kama yupo sambamba na watu hao.

Jenipher akaufikia ule mtambo na kuanza kuutizama kwa makini. Alikuwa ni jasusi wa hali ya juu kwahiyo asingeweza kuamini kila neno kirahisi. Akaitizama saa yake tena, akakuta zimebaki sekunde thelathini kufika mwisho wa muda sahihi. Akaupeleka mkono na kukishika kile ambacho alitakiwa kuchukua. Lakini kabla hajajua nini afanye Taa zikawashwaaa......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom