MKE WA RAIS
Hawakujua kuwa Neema ameshakufa na hawakuwa na habari katika hilo. Ilikuwa safari ya kuelekea Johnesburg hotel sinza. Kila kitu katika mwili na akili yake vilikuwa kwenye utimamu. Utimamu wa kuamua kile ambacho alitaka kukifanya. Bastola zilikuwa sehemu mbali mbali katika mavazi yake. Aliutumia muda mfupi kuondoka katika ya jiji kuelekea Sinza. Hakutaka kumuacha mtu katika mission hii. Kila mtu ambaye angemuhisi basi nilazima angeondoka. Jiji lilikuwa kimya kutokana na kilekilichokuwa kikiendelea. Alipita sehemu ngumu zenye mapambano makali. Hapo Moyo wake ukarudi katika kuamini kuwa Jenipher bado alikuwa akipambana. Jenipher bado alikuwa akiipigania Tanzania Yake. Hakuhitaji kuchelewa, alikuwa na kisasi na Carl Jack. Kisasi cha kumuua Ummu Sammy kinyama. Muda mfupi baadae alikuwa akishuka sinza umbali wa mita mia mbili kutoka ilipo hotel. Akatembea kwa Miguu bila wasiwasi. Kutokana na Eneo lote kuwa kimya hakuuona wasiwasi. Alitembea kana kwamba hakuna chochote. Alipoingia ndani ya Hoteli akalakiwa na tabasamu mwanana kutoka kwa mhudumu wa hoteli Ile. Tabasamu ambalo alilijibu kwa tabasamu kabla hajamuuliza kuhusu ujio wake pale.
Kwa kuwa alikuwa na maelezo yote kuhusu alipo Badest Man hakuchelewa kuruhusiwa. Akazikwea ngazi kwa umakini mkubwa. Mikono yake myepesi ilikuwa tayari kuzifikia silaha zake kwa nukta moja. Akamaliza kukwea ngazi kisha akaingia sehemu ambayo kulikuwa na Korido ndefu. Hapo umakini ukaongezeka. Akaongoza mpaka kilipo Chumba Alichoambiwa ndimo alimo Badest. Akasimama hatua tano Nyuma kisha kutizama kulia na kushoto alipoona hakuna Hatari Yoyote akaamua kurudi mapokezi kwanza. Alitaka kurudi mapokezi ili aonekane ametoka ili iwe rahisi Kurudi Kwa kupitia njia nyingine. Hilo likafanikiwa, Muda Mfupi alikuwa nyuma ya Ua wa Hotel akitizama jinsi ya Kuingia ndani. Akiwa hapo akitizama huku na kule ndipo alipoona kivuli kama cha mtu kikizunguka Eneo fulani katika uzio wa Jengo lile. Wakati akiongeza umakini akamuona mtu mwingine akiruka uzio wa Hotel na kuangukia ndani. Mohamed akatulia, alikuwa ametulia huku mkono wake ukishuka paka sehemu ilipo bastola yake. Bado watu wale walionekana kutulia hata baada ya kutua. Mohamed naye hakutaka kuwahi katika hilo. Akaupa moyo wake subira katika kukabiliana na kilicho mbele yake. Punde akauona mlango wa Siri Wa hotel ile kufunguliwa. Kufunguliwa kwa Mlango ule kukafuatiwa na Mwanamke kutokeza. Mwanamke aliyekamatia Bastola mkononi. Alikuwa ni mwanamke yule aliyemkuta mapokezi, alikuwa ni mwanamke yule mhudumu wa hoteli. Akatulia kwa muda akiangalia kile ambacho kinataka kufanyika. Hakujua kuwa ndani kulikuwa na mtu ambaye kuuawa kwake kilikuwa kitu cha kawaida. Watu wale wakaongea machache bila kutambua uwepo wa Mohamed. Hata pale mlango ulifunguliwa zaidi na watu wale kuingia ndani, bado Mohamed aliendelea kutulia kwa kuwa wakati yupo pale alikiona kivuli cha mtu. Mtu ambaye aliendelea kutulia pale hata baada ya watu wengine kuingia ndani wakitumia mlango wa uani. Akataka kumjua alikuwa nani. Punde akamuona Kijana wa kizungu akitokea katikati ya giza totoro na kuruka katika namna ya kipekee na kuingia ndani ya Hoteli. Ulikuwa urukaji uliosisimua na kuamsha Moyo wa mapigano. Urukaji ambao hutumiwa zaidi na watu ambao ni hatari. Mohammed akatabasamu, hatua ya pili alikuwa akiuparamia uzio na kutua ndani bila kutoa kishindo wala ukelele. Kutua hapo akaongoza mpaka nyuma ya vyumba vya hoteli hiyo. Hapo akasikia minong'ono, minong'one kutoka ndani chumba kimoja, punde akaisikia sauti, sauti za mahaba zikihanikiza katika chumba kimoja wapo. Watu walikuwa katika kile ambacho kilimshangaza Mohammed. Nchi ilikuwa katika hatari huku milipuko ikitanda katika jiji zima lakini watu hawakuwa wakiogopa, watu hawakuhofia, walikuwa wakiiburudisha Miili yao, Walikuwa wakiiburusha katika namna ambayo ilikuwa Ya kipekee. Hawakuogopa milipuko wala Risasi. Mwanamke alikuwa akihanikiza katika aina ambayo hata uwe mgumu vipi lazima ungesimama na kutega sikio. Alikuwa akilia kama ameonewa, alikuwa akilia kanakwamba anaadhibiwa. Mohammed hakusumbuliwa na hilo, akalipita Dirisha na kusonga mbele, hatua nne mbele akasikia minong'ono mingine, minong'ono ambayo ilikuwa tofauti na pale mwanzo. Hii ilikuwa Minong'one ambayo haikusikika kabisa, wakati Muddy Akiendelea kusikiliza kwa Umakini akahisi kama miguu ya mtu kutokea ndani ikielekea nyuma alipo. Vishindo vya mtu huyu vikamfanya ajiandae kwa pigo la Maana. Vishindo vya miguu bado vizidi kusogea, muddy akahesabu hatua baada ya Hatua, Lakini kinyume cha alivyotarajia vile vishindo vikakoma. Kukoma kwa vishindo kukaongeza umakini, umakini katika kufanya kile ambacho kilipaswa kufanya. Punde akamuona mwanadada Yule wa mapokezi akitokea, lakini kabla hajaamua kipi Cha kufanya, tukio la kutisha likatokea mbele ya Macho yake pale alipokiona kichwa cha binti kikisambaratika na Ubongo kusambaa sehemu Yote. Risasi ilikuwa imefanyakazi Yake, tena mbele ya Macho ya Mohammed.. HALI ILITISHAAA