Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

Naomba mniwie Radhi ndugu zangu kesho nitafanya hivyo. Bado nipo kwenye majukumu mpaka muda huu

Sawa mkuu kesho weekend sitoki kabisa nasubiri hizo nondo daah hakyamungu ukimaliza kabisa lete nondo mpya mkuu
 
Asante sana ibra nimeinjoy sana haichoshi ila naomba kesho uendelee maana x kwa kutamani kujua yanayojiri thnx
 
Ibra8,naona nnakusubiri bila mafanikio,ni saangapi sasa unaleta mzigo??
Fanya Hivyo tafadhali
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 73

Akageukaaa.. Lakini hakufika katika usawa sahihi. Akasikia sauti ya mwanadada ikinguruma kutoka nyuma yake. Sauti ambayo haikuonyesha masihara. Sauti ambayo haikuwa na utani ndani yake. Sauti ya Amri, sauti ya kukulazimisha kutii hata kama haupo tayari. Jenipher akatii bila kuonyesha ubishi wowote. Hakujua aliyekuwepo nyuma yake ni nani lakini akiusikia mdomo wa bastola Ukiigusa ngozi yake. Akatulia kama maji mtungini, akatulia kanakwamba ameogopeshwa na tukio lile. Hata pale alipokuwa akiamriwa atembee kuelekea alipotakiwa alifanya hivyo. Alifanya bila wasiwasi wowote, alifanya akiamini Ummu Yupo Sehemu Sahihi akimuangalia na akishudia kile kilichomtokea. Kitu hicho kikampa imani kubwa, imani iliyomfanya atulie bila wasiwasi. Hivi sasa walikuwa wakiiacha Hongera Bar na kutaka kuivuka barabara kuiendea gari yao ambayo ilishageuzwa kurudi ilipotoka. Wakatizama kulia na Kushoto kama kuna watu wanatizama, hawakuliona hilo. Kilichofuata ni kupiga hatua kuvuka barabara; muda wote bastola ilikuwa ipo mgongoni kwa Jenipher. Hatua ya kwanza ikapita bila chochote. Hatua ya pili akaenda pasipokutokea chochote, hatua ya Tatu haikupita wala haikupigwa popote, pikipiki ikaonekana kuja kwa kasi, pikipiki ambayo haikuwa ikiendeshwa na mlevi wala mvuta bangi. Bali alikuwa Ummu, Ummu Sammy bastola mkononi mwake.

Jenipher alikisoma kile kitendo na hata Neema Alikitambua mapema sana. Licha ya Neema kutambua lakini hakuweza kujiandaa katika hilo, hakuweza kuzuia kile ambacho kilipangwa kitokee. Muda mfupi alikuwa amepaa Hewani na sekunde ya pili alikuwa akianguka katikati ya barabara akiwa hana uhai tena. Risasi tatu kutoka kwenye Bastola ya Jenifer iliweza kumnyamazisha Neema. Hakuujua wepesi wa Jenipher pale alipokuwa akimuongoza. Hakuiona bastola ambayo ilikuwa katika mfuko wa Siri wa Jenifer. Hata pale alipoiona pikipiki ikija kwa kasi kisha yeye kugeuka kuangalia kule, hakuweza kumuona Jenipher alivyoichomoa bastola bali alikuja kushangaa pale kitu cha baridi zaidi ya kimoja kikipenya kifuani kwake.

Hata pale Ummu Sammy alipokuja kufika maeneo yale hawakutaka kujiuliza bali waliondoka kati mwendo ambao uliwashangaza wapita Njia Wachache hasa pale Jenipher alipochupa kisha kutua kwenye pikipiki, na muda ule ule pikipiki kuondoshwa. Hakukuwa na kushangaa wala hapakuwa na msikilizano, Maiti ya mwanadada Neema Mtobwa Ilikuwa Chini katikati ya Barabara damu ikichuruzika taratibu na kuweka kidimbwi kidogo. Ingawa ulikuwa usiku lakini mlipuko ule wa bastola Uliwafikia watu wachache. Kati ya Watu hao mmoja wao alikuwa ni Mohamedi. Ndio kwanza alikuwa amefika maeneo yale baada ya kutorokwa na Wakora katika mapambano yaliotokea Muda Mfupi uliopita. Ingawa alikuwa na Haraka Ya kuutafuta mwili wa mwanamke uliotoroshwa na Neema. Hiyo haikumzuia kwenda sehemu ya tukio. Sehemu ambayo alirakiwa na Watu waliozunguka kitu kama Mwili wa mwanamke. Licha ya watu hao lakini pia kulikuwa na polisi Wengi kutoka Kijitonyama polisi na pia walikuwepo Mashushushu kutoka Idara Ya Usalama wa Taifa.

Mohamedi akaendelea kusogea akiwapita watu mmoja baada ya Mwingine. Hakufanya hivyo kwa kupenda bali alivutiwa na mavazi aliovaa mwanamke Yule aliyekuwa amelala katikati ya Dimbwi la Damu. Mavazi ambayo muda mfupi Uliyopita yalivaliwa na mwanadada Shupavu Neema Mtobwa. Hilo likamvutia na kumfanya asogee. Kweli alisogea na kusogea na hata alipoupita Utepe uliozungushiwa na Polisi Hakuna aliyemuuliza. Wote walikuwa wakimuangalia kwa mshangao, mshangao ambao haukudumu sana baada ya mtu wanayemshangaa kuonyesha kuguswa na kifo cha mwanamke aliyelala katika dimbwi la damu. Naam, Mohamed alikuwa akimtizama Neema Mtobwa. Mwanamke aliyemtoroka Muda mfupi uliyopita tena akiondoka na mwili wa mwanamke ambaye alikuwa na sura ya bandia yenye kufanana na Sura ya mke wa Rais. Neema ambaye angepatikana angeweza kueleza alikuwa akimtumikia Nani katika mpango Huu. Aliuangalia Mwili wa Neema Mtobwa kwa muda mrefu bila kufanya kitu chochote kile. Lakini Muda mfupi baadae mikono Yake ilikuwa nddani ya mifuko ya Marehemu Yule akiangalia hiki na kuangalia kile. Hapo akakutana na Simu ya Marehemu akaichukua na kuiweka mfukoni mwa koti lake. Baada ya hapo akachukua vitu vingine ambavyo aliviona ni Muhimu kisha akainuka na kuanza kuondoka huku akiacha maagizo kadha wa kadha kwa askari wale ambao wengi walitii ingawa hawakumjua. Hata pale alipotoweka katika Upeo wa macho Yao Hakuna aliyemuona Zaidi ya kujikuta wakiongeza Mshangao katika hilo.

Mohamed alijitokeza pale makusudi akiamini kuwa palikuwa na watu sehemu wakimtizama. Na hilo ndilo ambalo alilitaka, alitaka wamtizame na wamjue ili waanze kumfuatilia. Alitaka kufuatiliwa ili aupate ukweli, ukweli Juu ya Mapinduzi, Ukweli Juu Ya Mpango Ovu kutoka kwa mtu ambaye bado nikitendawili. Alitembea akiamini kuna macho mahala yakimtizama na kuna watu sehemu wakimfuatilia. Naam Hakukosea na Hakuwa mbali na Ukweli.
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 074

Mawazo yake hayakuwa mbali na ukweli wa mambo. Hayakuwa mbali kwa kuwa ni kweli alikuwa akifuatwa, ni kweli alikuwa akiandamwa na watu. Hilo alilipenda na hilo lilimvutia. Lilimvutia kulitizama na hata kwa kulitenda. Hakuwa na wasiwasi na wala hakuwa na hofu. Hata kitendo cha kumkuta Neema ameuawa haikumtia hofu kwa kuwa alijua kuwa ni kazi ambayo Imefanywa na Watu anaowaamini. Alitambua walioifanya kazi ile ni Ummu ama Jenifer. Akauruhusu mwili wake uwe kwenye utayari wa kimapambano, aliuruhusu Mwili wake uwe kwenye utayari wa kushambuliwa. Bastola zake mbili zilikuwa karibu, karibu kabisa katika kufikiwa na mikono myepesi. Aendelea kutembea bila wasiwasi, akihama pale na kuingia hapa. Mpaka anafika maeneo ya Ambiance club hakuona mtu yoyote akimzengea. Wakati akitaka kuingia kushoto kukifuata kituo fulani cha bodaboda ambacho kilikuwa pembezoni mwa barabara akasita kwanza baada ya kuoina Gari Aina ya Ranger Rover Nyeusi ikimpita kwa kasi na kitendo bila kuchelewa akafunga breki wakati huo huo milango ikifunguliwa na Kuruhusu watu watano kushuka wakiwa katika aina fulani hivi ambayo iliburudisha machoni kwa watu wachache ambao walikuwepo Eneo hilo.

Kila mmoja alikuwa akipendeza katika kunesa na kutembea, alipendeza katika kuikamata bastola na alipendeza katika kutenda kile ambacho walitaka kukifanya. Wakati wakishuka walikuwa na Uhakika kwamba wanayemuona alikuwa Mohamedi, lakini kufika chini na kutizama huku na huko hawakuambulia kumuona Mohamed. Hawakuambulia kukiona kivuli Chake. Wote wakashikwa na Mshangao ambao haukudumu sana pale walipojikuta watatu kati yao wakiisalimia Ardhi huku wakivuja Damu. Risasi kutoka hatua Chache aliposimama Mohamedi Zilitosha kuwalaza vijana wale. Eneo lote likawa katika Taharuki. Kile kilichotokea Afrikasana muda mfupi uliopita, sasa kilikuwa kikirokea pale. Vijana watatu walikuwa maiti huku damu zikionekana kuvuja. Wakati watu wakijazana kushangaa Mohamed alikuwa pembeni mwa ile Range Rover akimuendea Dereva ambaye hakuwa na Habari kuhusu kilichotokea. Akaufikia mlango na kuugonga kwa tahadhali kubwa lakini ukimya ukaendelea kutawala, Hata alipougonga kwa mara Ya pili bado hapakuwa na Majibu. Akaamua kuufungua mlango kwa nguvu. Kitendo cha kuufungua mlango wa gari akashuhudia Mwili wa mtu ukianguka chini huku ukiwa hauna Uhai. Kichwa kilikuwa kimefumuliwa kwa Risasi. Mudy akatabasamu. Halikuwa tabasamu la furaha, hili lilikuwa tabasamu la karaha. Nani amemuua Huyu Dereva? Kwa nini amemuua? Amemuua kuficha kitu Gani? Hayo yalikuwa maswali kichwani kwa Mohamed. Maswali ambayo alijiuliza akiwa ameshatoweka Eneo la Tukio. Hakutaka kulala Usiku ule mpaka aifanyie kazi Simu aliyoichukua kutoka kwa Marehemu Neema Mtobwa.

******

Ulikuwa Mkutano wa siri katika jumba fulani pembezoni mwa bahari Ya Hindi. Mkutano ambao ulihudhuriwa na watu wasiopungua Ishirini. Ulikuwa mkutano ulioitishwa baada ya kuona mapambano bado yanaendelea huku dalili za kushindwa zikionekana kabisa. Leo Hii mbele ya wanamkakati Wenzie mwenyekiti Wa kikao Hiki Ambaye ni Makamu Wa Rais Wa Nchi hii alikuwa ameketi Huku uso Wake Umesawajika. Alikosa imani kutokana na kile ambacho kinaendelea katika mkakati Ovu. Kila mmoja alikuwa ametulia tuli akimuangalia Mheshimiwa Yule. Kila mmoja alikuwa katika hofu ya mwisho katika mkakati huu. Hofu iliyoletwa na watu watatu ambao ndio waliosimama kidete kumpigania Rais Aliyepo Madarakani. Kushindwa katika Mkakati Huu Ovu ni kushindwa kuendelea na Maisha. Kushindwa katika mkakati Huu ni kuruhusu kuuawa kwa kupigwa Risasi pale itakapogundulika kuwa Wameshindwa katika Vita Hii. Ukimya ukatawala tena na tena, Hata mwenyekiti alikuwa katika sintofahamu. Aliuona Mwisho Wake mbaya na Aliyaona maisha yake kuwa mafupi. Je Atakubali Vipi katika Hili? Ndicho kilichomfanya Aitishe Mkutano na washirika wake katika mkakati Huu. Mkutano ambao Ulihiludhuriwa na Mabalozi wa Nchi Tano za Ulaya na America. Mabalozi ambao nchi zao ndizo zilikuwa chokochoko ya Vugu vugu hili. Nchi kama Uingereza, Marekani, Urusi, Israel na Italy ndizo zilizokuwa Nyuma ya Mpango Huu. Mpango wa Kuwahusisha CIA,MOSSAD,KGB na hata M16 ulitengenezwa na Viongozi Wa Nchi Husika ili kusaidia mapinduzi ambayo kama Yakifanikiwa Wangevuna Dhahabu na Almasi Nyingi kutoka Hapa Nchini. Wangevuna Pembe za ndovu Za kutosha kutokana na Makubaliano ambayo yalifikiwa.

Baada ya ukimya wa Muda mrefu na kila mmoja kufikiria lake. Mheshimiwa Mwenyekiti akasimama Huku akionyesha Wasiwasi mkubwa machoni na Hata Usoni. Wakati Akijiandaa kuongea, akashangaa Kumuona Mtu Akiingia, hakuwa peke yake bali alizungukwa na Watu Wasiopungua Kumi. Kila mmoja aliyekuwepo Ndani Ya Ukumbi ule Akashangaa.. Hakuna aliyeamini Macho Yake. Mbele Yao Alisimama Rais Wa Nchi akiwa sanbamba na Askari Wake watiifu. Askari ambao waliongozwa Na Wasichana Wawili. Wasichana ambao hawakuwa wageni kwao. Wote Wakaduwaa na Kushindwa Kuamini pale Jengo lilipovamiwa Na Askari Wengi Zaidi, kisha Wajumbe wote Kutiwa nguvuni.
 
[QUOTninacholeta post: 17563893, member: 268654"]Mkuu ukimaliza hii kuna moja ilikua inaitwa Ama zetu nmesahau jina ni Ama zangu au Ama zetu utanirekebisha kama nimekosea ya longi kidogo[/QUOTE]
Mkuu ninacholeta hapa huwa mwandishi ni Mimi mwenyewe kwahiyo AMA zao miye sio niliyekiandika.
 
Mkuu ninacholeta hapa huwa mwandishi ni Mimi mwenyewe kwahiyo AMA zao miye sio niliyekiandika.[/QUOTE]

shem nimefikiri umekopi mahali daaah speechless!!!!!
 
Back
Top Bottom