Riwaya: Mke wa Rais

Riwaya: Mke wa Rais

Nimeianza jana mpaka kufikia sasa nineimaliza yote.!!

Kazi nzuri kijana, inavutia, inashawishi kuisoma, inaondoa stress..!! Halafu nikupongeze kitu kimoja, Huboi....Hunanyodo... Unatupia story kila siku, kila baada ya masaa kadhaa, Yaani hauzingui. Ni tofauti na baadhi ya waandishi wa Story wengine Uchwara ambao hawaandiki story bila kuwabembeleza..!!

Hongera kwa hilo, kazi yangu ni kusoma na kugonga like!!

BACK TANGANYIKA
Ahsante mkuu
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 070

Wakati anatoka ndani ya kichumba kile akapokewa na mkono wenye nguvu. Mkono ambao ukifanikiwa kumpeleka chini na kumuangusha mfano wa mzigo mkubwa. Ni wakati Mohamedi akitaka kuamka kukabiliana na mwanamume yule, akamuona hewani akija huku ametanguliza miguu yake. Angeruhusu limfikie asingekuwa Mohamedi. Hakuujua wepesi wa Mohamedi wala mtu yule hakujua Mohamedi alikuwa Nani. Wakati akiwa hewani Mohamedi akajipindua pale pale Chini. Bastola ikatangulia mbele yake. Kilichotokea ni Mlipuko ambao haukufika popote kutokana na bastola kuwa na kiwambo cha kuzuia mlio. Mtu Yule akaanguka chini Huku akitapatapa. Hakutaka kuupoteza Muda akairuhusu risasi tena kutua kwenye paji la uso la Mkora yule. Risasi ambayo ilitosha kumuangamiza kabisa. Akampekuwa Mifukoni akabahatika kupata Kakitabu kadogo na Bastola nyingine mbili. Alivichukua vyote na kuanza kuingia ndani zaidi Ya Jengo lile. Alikuwa akimtafuta Rais pamoja na watoto wake. Hakutaka kujisumbua na mwanamke aliyemshuti wakati anaingia. Alijua hakuwa mke wa rais bali zilikuwa mbinu za Warusi kumuwekea Sura inayofanana na ya Mke Wa Rais.

Alitembea kwa Umakini Mkubwa akiamini hatari iliombele yake. Hatari ambayo hakuujua mwanzo na chimbuko lake. Bado aliteswa na kizungumkuti cha kilichokuwa kikiendelea. Hakuwahi kuona Idara Nyeti kama ya Usalama wa Taifa kumezwa na kutawaliwa na Mashirika kama MOSSAD NA CIA PAMOJA NA KGB. Idara Ya Usalama Wa Taifa Ilikuwa Idara Nyeti Katika Usalama Wa Nchi Yoyote Duniani. Hawandio wanampangia Rais Ratiba ya kila inachokifanya. Hawa ndio wanaamri ya kumwambia Rais atoke ama Asitoke kwenda popote. Hawa ndio wenye uwezo wa kumwambia Rais huu ni wakati wa kupumzika, Rais naye akatii bila kutia Neno. Hawa ndio watu pekee wenye uwezo wa kuratibu Usalama na Ziara Za Rais kwa nchi Yote. Huwepo sehemu husika mwezi Mmoja kabla ya Tarehe Husika Ya mkutano ama Ziara Ya kiongozi wa nchi. Kujipenyeza kwa watu kama KGB NA CIA kilikuwa kitendo hatari kwa Usalama Wa nchi. Hawa ni watu ambao hujiingiza sehemu kutokana na Faida ya Mataifa Yao. Huwezi kuwakuta Majasusi Wa CIA wakiingia katika nchi ambayo haina Impact kwao. Muda Wote Waliangalia Fursa. Hata walipomuua Sadaam Hussein Na Kanali Muamar Ghadaf walifanya hivyo kutokana na kuwepo na Visima vya Mafuta. Huo ndio mkakati wa Mataifa Makubwa Ya Ulaya na Marekani. Sasa Kuwepo Kwenye Mfumo wa Usalama wa Nchi Kilikuwa kitu Hatari Sana.

Mohamedi aliitambua Hatari hiyo. Hatari ya kupambana na majasusi Wa KGB kunahitajika kazi ya Ziada. Akatembea Taratibu huku bastola Mkononi. Alikuwa akichungula Chumba kimoja baada ya kingine. Kila alipohisi mchakacho wa kitu alijitahidi kupafikia. Jumba lote lilikuwa kimya kabisa. Ukimya huo ndio uliendelea kumpa hamu ya kusonga mbele katika Jengo lile. Wakati akiimaliza korido ili kuingia upande mwingine, akisikia milio ya Risasi Ikilindima kutokea Nje. Hakushangaa wala kustaajabu. Alitambua kuwa hao ni Watu wake katika kupambana. Alitambua Hao ni Askari Wake Shupavu. Askari ambao walijuwa wakiipigania Nchi Yao. Hawa walikuwa ni Jenifer na Ummu. Alijua ni Wao kutokana na Upambanaji wao. Risasi zilikuwa Zikilindima kila Sehemu, Zikirushwa kwa Utaalam Uliopitiliza. Kufika kwa Wapambanaji WEnzake kulimpa nguvu Ya kuendelea kusonga mbele. Hatua zisizopungua Hamsini mbele Yake akaikuta michirizi Ya Damu. Michirizi Ambayo ilionekana ni ya Mtu aliyejeruhiwa. Mohamed akaongeza Umakini, akaendelea kuufuatilia Mchirizi ule ulipoelekea. Mdomo wa bastola Ulitangulia mbele kuisafisha njia. Kuangamiza kile ambacho kingejitokeza. Mbele Yake kidogo alikutana na Milango mitatu, milango ambayo ilikuwa katika vyumba vyenye idadi Hiyo. Kuikuta milango hiyo kulihitimisha safari ya kufuatilia ile michirizi. Milango Yote ilikuwa imetapakaa damu na Michirizi Haikuendelea tena. Kengele Za Hatari Zikagonga kichwani kwake. Hakuujua ni Mlango gani mtu huyu atakuwa ameingia. Hakutaka kufanya papara. Alijua majeruhi Alikuwa ndani ya Chumba kimoja akiwa na Silaha Mkononi. Kwahiyo alitakiwa awe makini, alitakiwa kuicheza Karata yake Vizuri.

Macho Yake Yaliendelea kuitizama milango mitatu Iliyotapakaa damu. Akiuangalia Mlango sahihi ambao ungeweza kuwa ndimo alipoingia Majeruhi. Akainyanyua bastola yake kisha kusogea. Alitembea kwa Mwendo wa ninja, mwendo usiokuwa na kishindo wala kelele. Akakishika kitasa Cha mlango Wa Kwanza na kukitingisha huku akiwa amesimama pembeni. Hapakuwa na mtu. Akakiendea kitasa cha mlango Wa pili akafanya kama Mlango Uliopita. Hapo akapokelewa Na Risasi Mfululizo. Risasi ambazo Zilipita patupu. Kilikuwa kitendo kilichofanyika kwa Sekunde tano, kitendo kilichotosha kumnyamazisha Yule Majeruhi. Mohamed akaufungua mlango kwa Umakini Zaidi. Ingawa alikuwa na Uhakika kuwa ameshaua, lakini Hakutaka Kuamini. Kuufungua Mlango Macho Yake yakatua Kwenye Sura Ile ile ya Mke Wa Rais. Akaingia Zaidi Bastola ikiwa imetangulia Mbele. Alitaka kujua huyu mwanamke Alikuwa nani, Alitaka kujua kwa nini amevaa sura ya bandia inayofanana na Sura Ya Mke Wa Rais
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 071

Alitaka kumjua alikuwa nani? Alitaka kumjua kwa nini alikuwa ameweka sura ya bandia yenye kufanana na mke wa rais ambaye tayari alishaakufa. Lilikuwa ni jibu pekee, lilikuwa jibu lililobaki katika kumpa Mohamedi majibu ya mkasa huu. Akapiga hatua huku bastola mkononi, akainama na kukishika kichwa cha mwanamke yule ambaye alilala katikati ya dimbwi la Damu. Kile alichokitegemea ndicho alichokikuta. Alikuwa amevikwa kitu kama sura. Sura yenye kufanana na mke wa Rais. Mohamed akatizama kwa umakini wa hali ya juu. Hakutaka kuwa na papara. Alitaka kuujua ukweli wenyewe. Punde alikuwa akitoka na mwili wa mwanamama Yule Ukiwa begani. Alitembea huku masikio, macho na miguu vikiwa sambamba katika kufanya kile ambacho kingetokea. Bastola mkono wa kulia na marehemu bega la kushoto. Akakivuka kizingiti cha kwanza bila wasiwasi. Akakiendea kizingiti cha pili kwa tahadhali kubwa. Masikio yake yakahisi mchakato wa viatu kutoka ndani. Akautua mwili wa mwanamke yule na kuuweka pembeni. Aliziamini hisia zake kuliko kitu kingine. Punde mlango ukasukumwa kisha mbele yake akamuona mwanamke Mrembo. Huyu alikuwa mpya katika macho yake. Mpya katika mapambano na mpya katika hisia zake. Licha ya Upya Huo lakini kuna kitu kama alikihisi na kukikumbuka Juu ya Binti Huyu. Naam alimtambua, alikuwa Ni Neema Ben Mtobwa. Msichana Shupavu kutoka kikosi maalum. Msichana ambaye mara ya Mwisho alimuacha kule Cuba akiwa katika mafunzo ya Juu ya kikomando.

Leo alikuwa machoni mwake na leo alikuwa hatua chake kutoka alipo yeye. Tena alikuwa akitembea bila wasiwasi. Alikuwa akitembea kuonyesha kuwa hakuwa akiogopa kitu. Kwa nini haonyeshi kuogopa? Kwa nini Yuko hapa mbele Yangu na anahusika vipi katika mission Hii? Yalikuwa maswali yaliyopita kichwani kwa Mohamedi kwa sekunde moja. Hakutaka kuendelea kusimama, akajitokeza Na kukutana uso kwa macho na Neema Mtobwa. Wakatizamana katika namna ya kipekee, mtazamo wa kila mmoja akimuacha mwenzake asome kile kilichopo ndani yake. Ndicho kilichofanyika na ndicho kilichotendeka. Hapakuwa masihara machoni kwa mwanadada Neema Mtobwa. Hakuuona urafiki uliokuwepo wakati walipokutana Cuba. Macho ya Neema yalisadifu vita, tamaa na kubwa zaidi ni Damu. Mohamedi akahisi ni wakati husika wa kufanyakile ambacho anataka kukifanya. Wakati anajiandaa kutenda kitu mlango ukasukumwa kisha Vijana wanne kuingia wa aina ambayo ilimburudisha Mohamedi katika macho na mwili wake. Licha ya kuburudika kule lakini hakubakia pale, hakuendelea kusimama pale, alikuwa ameshajitupa na kuangukia pembeni huku Risasi zikipita na kuuchimba Ukuta. Akaangukia Sehemu huku akiamini kuwa hata mwanadada Yule inawezekana ameshapigwa Risasi. Lakini alipoona ukimya umetawala akajua wote walioingia pamoja na Neema Mtobwa walikuwa ni wa moja. Hapo ndipo alipoamini kuwa mapinduzi yalikuwa yamepangwa kwa muda mrefu sana. Kuwepo kwa majasusi wa CIA NA MOSSAD kuliimaanisha Mipango ya mapinduzi ilipangwa huko nje. Aliamini mipango hii inabaraka za serikali ya Marekani ndio maana hawakuonyesha kushtuka kwa tukio la Mke wa Rais kuuawa ndani ya IKULU. Hapo akauona Ugumu wa hii kazi. Kama watu wote waliopo mafunzoni Nchi mbalimbali wamekubali kuasi na kutengeneza mapinduzi, Basi Shughuli itakuwa ngumu kupindukia,

aliujua uwezo wa kimkakati na kimapigano kwa vijana waliopelekwa nje. Aliuona ugumu wa kupambana na watu wa aina hiyo, lakini alipomkumbuka Ummu Sammy Na Jenipher Dominic alitabasamu. Lilikuwa tabasamu la karaha. Bado hakutaka kuinuka na bado hakutaka kufanya lolote. Aliendelea kutulia akipanga hili na kupangua lile.

******

wakati Mohamed Akiendelea kutulia pale chini, huku upande wa pili Neema na Vijana wake walikuwa wameshaondoka Sehemu ile. Hawakuwa wao tu bali waliondoka na mwili wa mwanamke ambaye alikuwa na sura ya bandia Yenye kufanana na Mke Wa Rais. Ulikuwa ni mpango maalum ulioandaliwa na Makamo wa Rais Wa nchi kuhakikisha kila kitu kinafichwa ili kupoteza ushahidi wa kuhusika kwake Katika mkakati Ovu. Hata kile ambacho kilikuwa kikitokea kipindi kile hakikuwa kinatokea Kwa bahati mbaya. Kuletwa kwa Neema Mtobwa katika Mission hii ni kujaribu kuficha kile ambacho kilikuwa kinakwenda kugundulika. Na hilo wakafanikiwa baada ya kumdhidi Mohamedi. Licha ya kufanikiwa katika hilo lakini hawakujua kuwa eneo lile hakuwa Mohamedi peke Yake bali kulikuwepo na Ummu Pamoja na Jenifer ambao waliushuhudia mchezo wote ukitendendeka na hata pale Neema na Watu wake walipoamua kuondoka walionekana na walifuatiliwa kwa nyuma.

*****

Ukimya Ulizidi kutawala Eneo lote. Mohamed hakuona Sababu ya kuendelea kukaa. Aliamua kutambaa Chini kwa Chini, akafanikiwa kutokea upande wa pili. Alipofika hapo alisimama na Kuchungulia kwa Chati, lakini akashangazwa na Ukimya. Ukimya ambao ulitafsiri Vitu vingine. Kufikia hapo Akaukumbuka Mwili wa mwanamke Yule, Mwili ambao ungetegua kitendawili juu Ya mkasa wa Kuuawa Kwa MKE WA RAIS...
 
MKE WA RAIS

SEHEMU YA 072

Ulikuwa mwili wa mwanamke, mwanamke ambaye angetegua kitendawili juu ya kuuawa kwa Mke Wa Rais. Kuukumbuka mwili ule kulimpa nafasi ya kujaribu kurudi alipouacha. Macho na masikio yake vilikuwa katika kiwango cha juu cha Uthubutu. Kiwango ambacho kilikuwa na uwezo wa kuona ama kusikia mchakato hata wa sisimizi. Akatembea kana kwamba hakuwa Mohamedi. Alitembea huku akihesabu hatua za miguu yake. Kila hatua moja ya miguu, macho yalitizama hatua kumi. Akavuka salama katika sehemu ambazo alizihofia. Bado ukimya uliendelea kutawala Eneo lote, ukimya ambao haukuwepo hapo Mwanzo, ukimya ambao bado haukuleta majibu sahihi kichwani kwa mpelelezi yule. Akaipa akili yake uhuru wa kufikiria zaidi. Sio kufikiri Huku amesimama bali alikuwa akifikiri Huku akitembea. Hata alipoufungua mlango kuingia chumba husika hakusikia kishindo wala kitu chochote zaidi ya ukimya wa Eneo lote. Punde alipoingia katika chumba kile likatokea tulio ambalo MohaMedi alilitarajia. Taa zilizimwa baada ya hatua zake mbili kuingia chumba kile, na risasi zikasikika kuelekea pale aliposimama. Ni kitu ambacho alitarajia hivyo baada ya Taa kuzimwa yeye aliruka kutoka pale alipo na kuangukia Kando. Risasi zikapita patupu na kuchimba Ukutani. Sekunde kumi baadae chumba kikarudi kwenye Ukimya. Ukimya ambaao haukupita sekunde Nyingine Tano akasikia sauti za Watu wakinong'ona.

Ingawa wazungumzaji walikuwa wakiongea sauti ya chini lakini kwa Mohamed ilionekana kuwa ni sauti kubwa sana. Ndani ya Nukta mbili alikuwa akisimama na nukta ya tatu Bastola yake ikakohoa kama mara tatu. Mayowe yakasikika, Mayowee ambayo hayakuwa maigizo bali lilikuwa yowe la Uchungu. Hakuhangaika Kuwaangalia watu hao. Alichofanya Yeye ni Kuutaka Mwili wa mwanamke Yule ili atoweke Maeneo Yale. Hakutaka kuondoka pale mpaka pale atakapoufikia Mwili wa mwanamke Yule. Hakujua kama tayari Neema Mtobwa Na Vijana wake walishauchukua. Hakujua kuwa mwili haukuwa pale, laiti angejua asingeupoteza Muda wake kubaki Sehemu ile. Akaendelea kutembea kwa mwendo ule ule wa nyau, bastola Mkononi huku masikio yakiwa katika kiwango kile kile alichojifunza kule Israel. Bado hakuwajali wale watu aliowachapa Risasi. Akaifikia Sehemu ambayo aliuacha mwili wa mwanamke Yule. Lakini akakuta ni patupu. Hapakuwa na mwili wa mwanamke wala hapakuwa na chochote. Hasira zikaongezeka Juu ya Neema. Hasira ambazo zilimfanya Awarudie Wale Marehemu ambao Hawakutaka Kuwaangalia.

******

Baada ya Neema Mtobwa na Vijana wake kuondoka na mwili wa yule mwanamke, Huku nyuma Ummu Sammy Na Jenipher walikuwa nyuma yao wakiwafuatilia kwa umakini mkubwa. Waliruhusu magari manne yawatangulie ili wasiwagutushe kina Neema kwamba walikuwa wakiwafuatilia. Kila mmoja alikuwa makini kwa kila hatua. Walijua hawakuwa wakipambana na Watu wakawaida. Kukutana na Majasusi wa Kirusi katika hili kuliwafanya waamini kuwa haya mapinduzi yalipangwa kwa Umakini mkubwa na kama Sio Kuuawa kwa Mke Wa Rais basi kila kitu kingeshaharibika. Kuwepo kwa viongozi waandamizi Wa serikali katika mkakati Huo Ovu kuliwapa picha ambayo Isingekuwa Nzuri Kwa Nchi. Viongozi wengi wa Ulinzi na Usalama Walikuwa ndio waanzilishi wa mpango mkakati wa kufanya mapinduzi. Lakini licha ya kujua hilo, bado hawakujua Sababu ya Mke wa Rais kuuawa na Hawakujua ni nani yule mwanamke ananyefanana na Mke Wa Rais Aliyeuawa. Hawakujua ni Wapi alipo Rais Baada ya kumkosa katika Jengo lile ambalo ni moja kati ya Majengo ya Siri ya Usalama Wa Taifa baada ya kumkabidhi yule mwanamke akiwa ni pamoja na Watoto Wa Rais.

Bado Hali ilikuwa tata na bado walikuwa ndani ya kiza kinene. Kiza ambacho kingetenguka pale watakapo mpata mpangaji wa mpango huu ambao umeifanya nchi hii kuwa katika Taharuki muda Wote. Muda wote walikuwa wakiitizama gari wanayoifuatilia. Hawakutaka kupotezwa wala kuipoteza. Muda Mfupi baadae wakaiona gari ile ikisimama Mbele Ya Jengo Moja maeneo Ya Sinza Africasana. Wakashuka Vijana wawili wa kiume sambamba na mwanadada mmoja mwembamba. Baada ya kushuka Watu wale walionekana wakiangaza huku na Huko kanakwamba kuna kitu wanakiangalia. Ummu na Janipher Wakapita kama hawakuwa na Habari nao. Walipohakikisha Hawaonekani na watu wale, nao wakashuka kisha Jenipher akamuita Dereva Wa boda boda na kumuomba ampeleke pale Hongera Bar. Kwanza Yule boda boda alishangaa na kuonyesha Mashaka. Kutoka Alipo Jenipher na Mpaka Hongera Bar Ulikuwa ni Umbali wa hatua Hamsini ama Sitini. Lakini alipoona Jane akimaanisha aliamua kumbeba akiamini ni mmoja Wa machangudoa Wanaofanya Biashara Ya kuuza Miili yao maeneo Yale. Jenife akapanda pikipiki ikawashwa, muda mfupi pikipiki ilikuwa Ikisimama Pembeni mwa Chuo Cha Ustawi Wa Jamii. Jenifer akashuka na Kumlipa Dereva kisha Bila Hata Kusubiri Chenji Yake akachepuka na Kuingia ndani Ya Bar. Muda Wote Macho Yake Yalikuwa Yakiangaza huku na huko katika namna ambayo hakuna ambaye angemtilia Mashaka. Akiwa bado amesimama Akiangalia ni Wapi Pakukaa Akahisi Kitu Cha Baridi Kikimgusa Kwenye mgongo wake.. AKAGEUKAAAAAA
 
Back
Top Bottom