MAGNUM22
Sehemu 14
UWANJA WA NDEGE WA LUNGI
FREETOWN
Saa sita usiku, ndege iliyombeba Kamanda Amata ikakanyaga ardhi ya jiji hilo, na baada ya hpo ikaegeshwa vyema kabisa mahala pake na abiria wakaanza kuteremka mmoja mmoja. Watu kama hawa, wanaintelijensia daima hisia kali au hupenda kuita mlango wa sita wa fahamu huwaongoza katika mambo mengi, akiwa bado ameketi kitini na abiria wengine wamekwishaanza kuteremka, Kamanda Amata alihisi kwa vyovyote kuna wenyeji wanaomsubiri.
Ili wanione vizuri ngoja niwe wa mwisho! Akawaza huku akinyayuka na kushusha mkoba wake kutoka kwenye keria ya ndani, akaupachika begani na kuvuta hatua akiwa kama mtu wan ne hivi kutoka mwisho. Mataa ya kupendeza ya jiji hilo yakamlaki, kana kwamba yanamwambia ‘karibu katika jiji la dhahabu’.
Akiwa katika foleni ya ukaguzi wa vibali vya kuingilia nchini humo, Amata akawa akiangaza huku na huko kuangalia kupitia vyoo vikubwa kabisa, kama kuna anayemhisi kumsubiri. Naam macho yake yakagongana na Amanda, japo hakuwahi kumwona viozuri huko nyuma zaidi ya picha tu ambayo alikuwa ameiweka akilini, tayari nywele zake zilisisimka akajua, tayari.
Nimeshapata mrembo! Akajisemea huku akimkabidhi pasipoti yake mwanadada wa uhamiaji.
“Karibu sana Sierra Leone!” Yule mwanadada akamwambia huku akimkabidhi pasi’ yake.
“Asante kwa ukarimu wako, nimekaribia,” Amata akajibu na kuitia mfukoni pasipoti yake, akainua macho kuitazama tena pale alipo Yule mwanamke, hayupo. Kwa kitendo hicho akajua sasa kazi imeanza kwa maana hakujua hata ni wapi mwanamke huyo kaenda, hivyo ni ngumu kujua atatokea upande gani. Akameza funda la mate, na kuvuta hatua ndogo ndogo kuelekea nje, hatua mbili tatu hivi kabla hajafika katika mlango huo, akamwona mtu ambaye akamhisi vibaya. Amata akaingia upande wa kushoto, akapita kando ya maboksio mengi yaliyolundikwa hapo, akavuta hatua za haraka haraka na kuliacha lile eneo, akajikuta kwenye bohari kubwa ya cargo. Kutoka kule akatafuta wapi panaweza kuwa na mlango wa kuendea nje, kwa bahati akauona, akenda na kuufungua, ulikuwa umerudishiwa tu, akaingia na kukutana na ngazi zikiteremka chini. Hakuuliza wala kufikiri, akashuka nazo mpaka chini kabisa, huko akatembea kwa hadhari kubwa sana akihofia kamaera za uslama kumnasa na kumletea shida kwa walinzi. Bahati mbaya au nzuri hakukuwa na hata moja.
‘Emergecy Exit’. Akaona kibao kimeabndikwa hivyo.
Ningeshangaa! Akajisemea moyoni na kuingia hapo palipowekwa mshakle wa uelekeo, milango miwili mitatu akajikuta nje, upande mwingine kabisa wa uwanja.
Mtanitafuta kwa gharama! Akasema tena na kuendelea na safari, bahati nzuri hakukutana na mtu yeyote mpaka alipofikia seng’enge zilizotenganisha eneo ambalo watu wanaruhusiwa, yaani maegesho na shughuli nyingine muhimu na lile ambalo hairuhusiwi kwa mtu mwingine kuingia. Akatazama huku na huko, akaona walinzi tu wakiwa mbali kabisa, akaendelea kutalii kwa macho hakuona kitakachomzuia kufanya atakalo. Kutoka katika mkoba wake akachukua mkasi mdogo lakini wenye uwezo wa kukata waya, akafanya hivyo na kutengeneza tundu kubwa tu, akapita na kupotelea kwenye magari mengi yaliyojipanga hapo na kujaribu kutafuta kama anaweza kumuona yule mwanamke.
Kwa upande wa Amanda na Fredy walijikuta bado wanasubiri mgeni wao atoke lakini haikuwa hivyo.
“Mbona hatoki?” Fredy akauliza.
“Mh! Sijui ila nilimuona kwenye foleni na aliyekuwa mbele na nyuma yake wameshatoka nje,” Amanda akajibu.
“Ametupiga chenga, keshagundua kuwa tupo!” Fredy akasema.
“Come on!” Amanda akatamka huku akitoka eneo lile na kuchukua simu yake, akampigia Martin na kumpa taarifa hiyo.
“Yupo hapo hapo, hakikisheni mnampata au mnamuona, hata tukijua tu ni wapi anafikia kwetu irakuwa sawa,” Martin akawaambia nao wakaendelea kusaka hapa na pale kwa kutazama.
Mara baada ya simu hiyo, Fredy na Amanda wakatawanyika na kuendelea kuangalia hapa na pale labda wangeweza kumuona lakini haikuwa hivyo.
“Tunafanyaje?” Amanda akamuuliza Fredy mara walipokutana baada ya kutafuta kila mtu upande wake.
“Huyu mtata, sasa tukisema tuondoke, itakuwa haina maana ya kuja, tukisema tukae pia tunaweza kupoteza muda,” Fredy akamwambia Amanda.
“Anyway twende kwenye gari, tukaone cha kufanya….”
“Aaaaaaa nimepata mbinu ya kumnasa kama yupo hapa bado,” Fredy akamwambia Amanda.
“Enhe…”
“Twende kwenye gari kisha tuondoke, kama yupo na katugundua, atatufuata ndipo tutampata…” Fredy akatoa wazo, likaafikiwa na wote wakaingia garini.
* * *
Kamanda Amata akatamani kucheka lakini akajikaza akiwa sambamba na ua kubwa lililowekwa kama urembo katika eneo hilo, vivuli vya vichaka vya ua hilo vilimfanya asionekane kirahisi na jinsi alivyojiweka. Michezo hii ya kujificha au kujipoteza asionekane alijifunza huko Japan wakati akichukua mafunzo ya Ninjutsu.
Lazima nitumie mbinu za hali ya juu kuwakwepa hawa jamaa! Akajisemea moyoni wakati akiwatazama Fredy na Amanda wakiingia maegeshoni na kuingia ndani ya gari mojawapo ambao Amata alikuwa akiliona vyema. Kutoka waiposimama wakati wakiongea mpaka alipokuwa Amata ni kama mita nne hivi, ni ua kubwa tu lililowatenganisha, hawakuweza kumwona Amata kutokana na kutumia kivuli kujificha.
Baada ya jamaa hao kutulia garini, Amata akatoka pale na kutembea kwa mwendo wa paka mpaka kwenye magari mengine ya nyuma, akachukua kifaa chake cha kufyatulia vitasa vya gari, hakuchukua hata dakika, tayari alikuwa ameketi kwenye gari asiyeijua hata mmiliki wake, akafunga mkanda huku macho yake yakiwa yanalitazama lile analolilenga.
Fredy akawasha gari na kuliondoa, Amata akasubiri kama dakika hivi nay eye akawasha na kuwafuata.
“Nitafanya kama mlivyofikiri!” akasema kwa sauti kana kwamba kuna mtu anayeongea naye. Baada ya kuicha barabara itokayo uwanja wa ndege na kukunja kushoto kuifuata ile ya Airport Ferry. Kutoka yeye na ‘kina Fredy kulikuwa na gari kama tano hivi katikati.
* * *
Amanda akatazama kwenye kioo kisha akakaa sawa kitini, Fredy naye muda wote alikuwa akitazama kioo cha ndani na kile cha upande wake.
“Vipi?” Amanda akauliza.
“Sioni kama anatufuata!” akajibu.
“Sasa atakuwa kaenda wapi mshenzi huyu?” Amanda akauliza.
“Huyu si wa kuchezea, anaonekana na mjuzi sana wa mambo,” Fredy akajibu.
Wakiwa wamezama kwenye mazungumzo, gari aliyokuwa anaendesha Amata, ilikuwa ikipita kwenye upande mwingine wa barabara hiyohiyo, taratibu alikuwa akiyaovateki magari ya upande ule mwingine ambao Fredy alikuwa akiendeshea. Alipolifikia gari la akina Amanda, akaweka la kwake sambamba kabisa, wakawa wakienda pamoja.
Ghafla macho ya Amanda yakagongana na mgeni wao.
“Shiiiit!!!!” akapiga ukulele na Fredy akageuka kutazama.
“Come on!” naye akajikuta akitamka kabla hawajatahamaki, Amata akayumbisha gari lake na kulipigiza kwa nguvu kwenye lile la akina Amanda. Akahakikisha analisukuma mpaka nje ya barabara na kugonga ukingo wake. Baada ya ukingo ule kuvunjika, Gari walilopanda Fredy na yule mawanamke likaacha barabara na kutoka nje likagonga nguzo ya taa na kuanguka vibaya. l
“Fredy! Fredy!” Amanda akaita kwa shida, Fredy akatoka kwa kutumia kioo cha mbele, akamtoa Amanda ambaye alikuwa na michaniko ya kutosha usoni mwake. Haraka sana, Fredy akamwacha Amanda chini, akachomoa bastola na kuliwahi gari la Kamanda ambalo nalo liliishi kugongo kizuizi imara cha barabara hiyo kubwa na kusababisha ajali kubwa. Fredy akalifikia na kuweka bastola yake tayari huku usoni mwake akitiririkwa na damu. Kutahamaki, Amata hayupo garini, akatazama huku na kule hakumwona zaidi ya madereva wa magari mwngine waliokuwa wakitukana ovyo.
* * *
Kamanda Amata tayari alikuwa upande wa pili wa barabara, akajibana karibu na ukuta wa kutenga barabara ya magari na watembea kwa miguu, akachungulia kwa chati na kumwona Fredy akaihangaika na yule mwanamke anavyomwacha na kuja kwenye gari alilokuwamo yeye, anavyoshangaa shangaa mpaka anaamua kurudi garini.
Ningeamua kuwaua ningewaua sasa wote wawili au hata kuwakamata, lakini wakati wenu bado nyau nyinyi! Amata akaongea mwenyewe moyoni mwake wakati akiwashuhudia wawili hao wakakokotana na kuingia kwenye taksi moja iliyosimama hapo. Baada ya wao kuondoka, Amata akaruka ule ukuta na kuliendea lile gari kabla askari hawajafika, akalifikia na kupekua haraka haraka hapa na pale. Hakupata vingi ni kadi ya gari na kadikazi moja ikiwa juu ya kiti. Mara akasikia ving’ora vya magari ya polisi vikija upande huo. Akaingiza mkono katika mkoba wake akatoa kijichupa kidogo mithili ya cha dawa ya minyoo akakirushia ndani ya gari lile kisha yeye akaanza kutembea taratibu kuelekea upande mwingine. Baada ya hatua kama mia hivi akachukua simu yake na kuwasha tab maalum akaminya ‘kitufe tepe’ kilichoandikwa ‘Fire’, mlipuko mkubwa ukatokea na lile gari likapaishwa juu juu na kutupwa chini likiendelea kuwaka.
HOTEL YA SWISS SPIRIT
HOTELI YA KAWAIDA kabisa iliyojengwa katika jiji la Freetown, ndiyo ambayo kijana huyu aliichagua kama sehemu yake ya mapumziko kwa usiku huo kiwezekana na siku nyingine ambazo atakuwa mjini hapo. Bahati pekee aliyokuwa nayo ni kwamba kila anapoingia hukaribishwa na mwanamke mrembo katika meza ya mapokezi.
“Chumba kipo, tena kimebaki kimoja nafikiri kilikuwa kwa ajili yako,” mwanadada huyu akamwambia huku akiweka vizuri kipanya cha kompyuta yake, “Pasipoti tafadhali…” akamwambia. Amata akaingiza mkono katika mfuko wa koti lake na kuchomoa pasipoti akampatia. Yule mwanadada akaifanyia kazi kisha akachukua na kadipesa yake akaichanja kwenye kifaa maalum, Amata akaingiza namba zake za siri na kisha akarudishiwa vitu vyake.
“Karibu Swiss Spirit Mr. Maturin!” akakaribiswa na mwanadada yule na sekunde hiyohiyo akaja kijana mwingine akachukua mizigo na kutangulia nayo.
“Asante sana, nafurahi kukaribishwa na kiumbe mrembo kama wewe, hakika Mungu bado hajachoka kuumba na isitoshe ana sampuli mpya ya udongo…”Amata akamjibu huku akimpa lile tabasamu lake hadimu sana ambalo hulitoa kwa nadra sana. Macho ya wawili hawa yakagongana na kushikana kama sekunde tano hivi. Yule mwanadada akashusha pumzi ndefu na kuinama chini kidogo.
“203!” akatamka.
“Asante sana, lunch kesho…” Amata akaanza ubembe.
“Saa saba kamili….”
“A aaaa najua, wapi? Ikiwezekana mi na wewe!” akamwambia huku akijivuta tayari kwa kuondoka.
“Mmmmm wewe! Wacha nihudumie wageni kwanza…”
“Halafu…”
“Nenda bwana!” yule mwanamke akamwambia Amata naye akaondoka mezani hapo taratibu kuelekea katika chumba alichokwishaelekezwa.
Mlangoni mwa chumba hicho, akamkuta kijana yule aliyempokea na kutangulia akiwa amesimama nje, Amata akafika na kufungua mlango, kisha akamwacha yule kijana amsaidie kuweka begi lake na baadae yeye mwenyewe akaingia ndani na kusimama katikati ya chumba hicho. Hakikuwa kidogo wala kikubwa bali cha wastani chenye kitanda kikubwa, kiti cha vono na kijimeza kidogo, pembeni mwa kiti hicho kwenye kona kuna nguzo ya taa hafifu iliyokuwa ikiwaka. Akatazama kila kona kwa macho tu, kisha akainua mkono na kuizungusha saa yake kwa namna fulani na kusubiri kwa sekumde kadhaa, kimya. Alipohakikisha usalama wa chumba upo akavuta kiti kingine ambacho kiikuwa kwenye dressing table na kukivuta mpaka mlangoni, pale akakiweka na upande wa mgongo akauweka chini ya kitasa kana kwamba kimepimwa urefu, kikakaa sawasawa n kukizuia kitasa kisiweze kufunguka. Kisha akavua koti lake na kulitupia kitandani, akachomoa ile kadi ya gari na kusoma ilikuwa imeandikwa kifaransa tu. Hakuona shida, akachukua jina la mmiliki na anwani yake kisha akahamia kwenye simu yake na kuanza kutafuta mtu huyo anaweza kumpata wapi.
Laurent Yonibana, Western Province 25, Domatou Road! Akaandika kwenye kijikaratasi kisha akachukua ile kadikazi aliyoiokota mle garini akaigeuzageuza na kuisoma maelezo.
Jean de Pierre! Akasoma na kutazama namba za simu na ofisi gani anapatikana.
“Nitakuwa wageni wenu kesho,” akasema na kujiweka tayari kwa kuoga na kupumzika.
WATERLOO
Martin Gupter alikuwa akiendelea kupiga maji tu huku akusubiri simu yoyote kutoka kwa washirika wake huku akilini mwake akifikiria tu ni jinsi gani ambavyo atamwadhibu adui yake pindi tu akiletewa. Akiwa katika mawazo hayo simu yake ikaitwa kwa fujo, akainyakuwa na kutazama, Fredy, akajikuta moyo ukimwenda mbiyo.
“Safi sana Fredy! Umemtia mkononi?” akamuuliza kwa jazba kuu.
“Kumtia mkononi, siyo rahisi namna hiyo, keshatuumiza vibaya hivi hapa tupo, 5 Point Clinic kwa matibabu,” akamwambia. Martin akarukaruka kwa hasira, akasimama wima na kuongea na Fredy akitaka kujua kulikoni mpaka mtu huyo awazidi ujanja. Akatoka nje ya nyumba hiyo na kuingia garini, akawasha na kuondoka kuelekea Freetown ili kuwaona wenza wake.
* * *
Fredy na Amanda walikwishapata matibabu, alfajiri ya siku hiyo Martin aliingia kwenye Clinic hiyo akiwa kafura kwa hasira.
“Que c’est il passé?” (kumetokea nini?) akamuuliza Amanda, na mwanamke huyo akamweleza kila kitu. Martin alishikwa na hasira zaidi, akatembea huku na huko kisha akatulia huku mishipa ya kichwa ikiwa imemdinda kwa hasira.
“Je vais le tuer!” (nitamuua!) akasema huku akiwa ameshika tama na kukalia kitanda cha mgonjwa. Kisha akamtazama Fredy, “washa kamera zote za siri!” akamwambia kisha akasimama na kutoka nje huku akifuatiwa na vijana hao, wakaingia garini na kuondoka zao. Martin hakwenda mbali, breki ya kwanza ni eneo ajali ambako hakukuta gari lolote mahali hapo zaidi ya majivu tu. Akaendelea mpaka kituo cha polisi na kuripoti juu ya ajali hiyo ndipo akaambiwa hata gari lenyewe limekwishateketea kwa moto. Martin akafikiri kwa nukta kadhaa kisha akatazamana na askari huyo macho kwa macho. Maswali yake yote akajibiwa na alipowaambia kuwa walikuwa wakifunkuzwa na jambazi akakubaliwa hivyo polisi wakaingia katika kazi ya kumsaka jambazi huyo, haya yote ylifanyika tu kwa sababu mlalamikaji ni Mzungu na si vinginevyo.
Baada ya kukiacha kituo hicho, Martin akagesha katika amgahawa mmoja mjini hapo kwa kupata kifungua kinywa na mazungumzo machache.
“Lazima afe taratibu, cha kufanya sasa ni kujua vipi tutampata!” akawaambia Fredy na Amata.
“Sawasawa, ila inabidi tujiweke vyama huyu jamaa anaonekana ni mjanja sana,” Fredy akasema.
“Atakamatika tu, nakwambia atakamatika tu sasa nimeamua, hawezi kufanya sisi watotot wadogo!” Amanda akalalamika huku akifunga nywele zake vizuri.
“Yeyote anayefuata nyayo hizi, yupo hatarini, tumpate huyu tumchanganye na yule bwege mwingiene kisha tuwazike wazima,” Martin akawaambia.
“Ndiyo dawa yao!” wakamjibu.
Martin akaondoa gari taratibu na kuingia barabarani, lakini ghafla simu yake ikapata uhai, akaiinua na kuitazama, akampa Fredy aasome ujumbe huo.
“Swiss Spirit Hotel!” akasema.
“Basi mchezo umeisha, mpigie simu Imlan Marikante, mwambie tuonane Sea Port leo saa nne!” Martin akatoa maagizo na Fredy akafanya hivyo.
* * *
Saa nne asubuhi hiyo Martin alikutana na Imlan Marikante katika mgahawa wa Sea Port kwa mazungumzo mafupi huku akiwa kawaacha Fredy na Amata garini wakajadilialiana hili na lile.
“Namhitaji huyu mgeni kwa pesa yoyote ile!” Martina akamwambia Imlan.
Martin Gupter na Imlan Marikante walikuwa marafiki wa muda mrefu hasa kwenye kazi nyeti kama hii. Haikuwa mara ya kwanza ila tofauti tu ni kuwa huyu aikuwa akimtaka hai mara zote alitekeleza mauaji tu kwa njia mbalimbali kwa kumtumia kijana huyu huyu kwenye hoteli mbalimbali jijini hapo na pembezoni.
“Kwa nini unamtaka hai?” Imlan akamuuliza.
“Ana mengi ya kulipa, na ninataka afe kwa kuonja uchungu wa kaburi,” akamwambia.
“Sawa, kumpata utaweza, tena leo hii hii, nilimwona akiongez kimahaba sana na mhudumu wa mapokezi pale Swiss Spirit, tunaweza kumtumia yeye akamtia penzini kisha tukamnasa,” Imlan akapendekeza mbinu ambayo Martin hakuifikiria kabla.
“Unafikiri ataweza kumtia mkononi? Maana huyu jamaa nimeshaanza kumsoma, si wa kumkamata kijinga…”
“Martin! Hakuna mkate mgumu mbele ya chai, atakamatika, anda fungu la maana nimsuke yule mwanamke, tena ni vyema akimtoa pale na kwenda naye mahala pengine,” Imlan akasema.
“Sawa!” Martin akakubali na kuondoka na jamaa huyo mpaka benki, akachukua pesa iliyotakata na kumpatia.
“Nakuamini!” akamwambia Imlan.
* * *
Wakati huo huo, Kamanda Amata saa nne hiyo alikuwa mbali kidogo na Jiji katika eneo linalojuikana kama Western Province katika Barabara ya Domatou. Mbele yake alismama mzee wa makamo kadiri ya miaka sitini au sabini hivi, aliyechakaa kwa jua la Afrika.
“Unazungumzia gari, Renault Station Wagon?” yule mzee akauliza.
“Ndiyo, kabisa, hili gari bado ni mali yako au?” akamuuliza.
“Hapana hili gari kwangu lilishapotea miaka mingi sana, nimebaki na risiti za manunusi tu basi, we umeliona wapi?” akauliza yule mzee.
“Siyo tu kuliona, limepata ajali nikafikiri waliokufa ni kati ya wanao maana walikuwa wawili,” akamwambia kwa Kifaransa safi. Katika ya ugha chache ambazo Kamanda Amata alizijua kwa ufasaha, nah ii ni mojawapo.
“Ooooo, nashukuru sana kwa taarifa hili gari nilishaibiwa, polisi wamelitafuta sana laki hawakulipa, basi nikanunu jingine!” yule mzee akasema. Baada ya mazungumzo kama ya dakika arobaini na tano hivi, wakaagana na Kamanda Amata akawasha gari lake la kukodi na kurudi mjini.
Saa saba mchana alikuwa mbele ya Clinic ya 5 Point, akaingia kwa hatua fupifupi mpaka mapokezi, akamuulizia anayetaka kuonana naye, akapelekwa. Huyu hakuwa mzee, kijana mshupavu daktari kutokana na jinsi alivyovaa. Baada ya maamkiano, Amata akaiweka ile kadikazi mezani.
“Kadi hii imeokotwa kwenye eneo la ajali jana usiku, tunapenda kujua kama marehemu ni ndugu zako au marafiki!” Amata akamwambia na yule daktari akaichukua na kuitia mfukoni huku akimwangalia kwa makini sana.
“No labda ni wateja tu, maana kuna wateja wangu walikuja hapa jana usiku kutibiwa, wakanambia wamepata ajali mbaya jana usiku, na wao najua kuwa nimewapa hii kadi muda mrefu tu, sasa sijui hiyo ni ajali nyingine au! Maana kama ni vifo hakuna kifo katika ajali hiyo,” yule daktari akamwambia Amata.
“Ooooh Good! Naweza kuwaona?”
“Hawapo wameshaondoka kwani ni mikwaruzo tu hawakuumia sana!” akamjibu. Mara hii Amata akajikuta amekosea kwa jinsi alivyomwingia mtu huyo. Hakuwa na budi kuaga lakini tayari alikwishajua kuwa adui wake watajua ndani ya sekunde chache kuwa alikuwa hapo.
Baada ya hapa wameenda wapi washenzi hawa? Akajiuliza mwenyewe huku akiwasha gari na kuingia barabarani kurudi hotelini. Nusu saa ilimchukua barabarani, akawasili hotelini na kuegesha gari, akashuka na kuingia ndani. Kabla hajazikwea ngazi kwenda ghorofa ya pili ambako chumba chake kilikuwapo, akakutana na yule mwanamke wa jana, mfupi mwenye nyama zilizonona katika mwili wake.
Huwa napenda shepu za mtindo huu! Akawaza huku akizidi kukaribiana naye na kumwona akitabasamu.
“Ndiyo unatoka?” akamuuliza.
“Yes! Nitakuwa off siku mbili kisha nitaingia kazini tena,” yule mwanamke akajibu.
“Kwa hiyo siku mbili zote sintokuona? Mbona utakuta nimekonda mwenzio,” Amata akamwambia.
“Njoo nyumbani kwangu!”
“Namwogopa shemeji,” akamjibu.
“Mbona jana ulizungumzia chakula cha mchana nyumbani kwangu? Hukujuan kama kuna shemeji yako?” yule mwanamke akamwambia, “Bahati yako ni leo tu, ukiikosa utajutia,” akangeza kumwambia huku akivuta hatua kama anaondoka.
“So?” Amata akamtupia swali.
“Kama una mambo mengi basi wakati mwingine,”
“Kwa leo nimemaliza, na hata hivyo nilikuwa nafikiri kupata mwenyeji wa kwenda kuspenda naye jioni hii ili kesho niwe na akili mpya,” Amata akamwambia huyo mwanamke.
“Ndiyo umempata!” akajibiwa. Kamanda Amata akatoa tena lile tabasamu lake la nadra, akampa funguo ya gari na kumtaka amsubiri garini, naye akafanya hivyo. TSA 1 akazikwea ngazi kuelekea chumbani kwake, akafungua na kuingia ndani kwa tahadhari kubwa, baada ya hatu kama tatu nne hivi zilizomfikisha katikati mwa chumba hicho jicho lake likanasa kwenye kile anachokiona kitandani. Akabaki na mbung’ao, ua, waridi jekundu lilikuwa juu ya shuka jeupe kitandani hapo.
“Nini hiki?” akajiuliza huku akiendelea kutazama kitandani, akachukua simu yake