Riwaya magnum22

Riwaya magnum22

Mkuu tupia basi sehemu zinazofuata za huu mzigo! Nmekuwa teja wa hii riwaya, kuikosa hii naishiwa raha kabisa mkuu!
 
MAGNUM22

Sehemu 14

UWANJA WA NDEGE WA LUNGI
FREETOWN
Saa sita usiku, ndege iliyombeba Kamanda Amata ikakanyaga ardhi ya jiji hilo, na baada ya hpo ikaegeshwa vyema kabisa mahala pake na abiria wakaanza kuteremka mmoja mmoja. Watu kama hawa, wanaintelijensia daima hisia kali au hupenda kuita mlango wa sita wa fahamu huwaongoza katika mambo mengi, akiwa bado ameketi kitini na abiria wengine wamekwishaanza kuteremka, Kamanda Amata alihisi kwa vyovyote kuna wenyeji wanaomsubiri.
Ili wanione vizuri ngoja niwe wa mwisho! Akawaza huku akinyayuka na kushusha mkoba wake kutoka kwenye keria ya ndani, akaupachika begani na kuvuta hatua akiwa kama mtu wan ne hivi kutoka mwisho. Mataa ya kupendeza ya jiji hilo yakamlaki, kana kwamba yanamwambia ‘karibu katika jiji la dhahabu’.
Akiwa katika foleni ya ukaguzi wa vibali vya kuingilia nchini humo, Amata akawa akiangaza huku na huko kuangalia kupitia vyoo vikubwa kabisa, kama kuna anayemhisi kumsubiri. Naam macho yake yakagongana na Amanda, japo hakuwahi kumwona viozuri huko nyuma zaidi ya picha tu ambayo alikuwa ameiweka akilini, tayari nywele zake zilisisimka akajua, tayari.
Nimeshapata mrembo! Akajisemea huku akimkabidhi pasipoti yake mwanadada wa uhamiaji.
“Karibu sana Sierra Leone!” Yule mwanadada akamwambia huku akimkabidhi pasi’ yake.
“Asante kwa ukarimu wako, nimekaribia,” Amata akajibu na kuitia mfukoni pasipoti yake, akainua macho kuitazama tena pale alipo Yule mwanamke, hayupo. Kwa kitendo hicho akajua sasa kazi imeanza kwa maana hakujua hata ni wapi mwanamke huyo kaenda, hivyo ni ngumu kujua atatokea upande gani. Akameza funda la mate, na kuvuta hatua ndogo ndogo kuelekea nje, hatua mbili tatu hivi kabla hajafika katika mlango huo, akamwona mtu ambaye akamhisi vibaya. Amata akaingia upande wa kushoto, akapita kando ya maboksio mengi yaliyolundikwa hapo, akavuta hatua za haraka haraka na kuliacha lile eneo, akajikuta kwenye bohari kubwa ya cargo. Kutoka kule akatafuta wapi panaweza kuwa na mlango wa kuendea nje, kwa bahati akauona, akenda na kuufungua, ulikuwa umerudishiwa tu, akaingia na kukutana na ngazi zikiteremka chini. Hakuuliza wala kufikiri, akashuka nazo mpaka chini kabisa, huko akatembea kwa hadhari kubwa sana akihofia kamaera za uslama kumnasa na kumletea shida kwa walinzi. Bahati mbaya au nzuri hakukuwa na hata moja.
‘Emergecy Exit’. Akaona kibao kimeabndikwa hivyo.
Ningeshangaa! Akajisemea moyoni na kuingia hapo palipowekwa mshakle wa uelekeo, milango miwili mitatu akajikuta nje, upande mwingine kabisa wa uwanja.
Mtanitafuta kwa gharama! Akasema tena na kuendelea na safari, bahati nzuri hakukutana na mtu yeyote mpaka alipofikia seng’enge zilizotenganisha eneo ambalo watu wanaruhusiwa, yaani maegesho na shughuli nyingine muhimu na lile ambalo hairuhusiwi kwa mtu mwingine kuingia. Akatazama huku na huko, akaona walinzi tu wakiwa mbali kabisa, akaendelea kutalii kwa macho hakuona kitakachomzuia kufanya atakalo. Kutoka katika mkoba wake akachukua mkasi mdogo lakini wenye uwezo wa kukata waya, akafanya hivyo na kutengeneza tundu kubwa tu, akapita na kupotelea kwenye magari mengi yaliyojipanga hapo na kujaribu kutafuta kama anaweza kumuona yule mwanamke.
Kwa upande wa Amanda na Fredy walijikuta bado wanasubiri mgeni wao atoke lakini haikuwa hivyo.
“Mbona hatoki?” Fredy akauliza.
“Mh! Sijui ila nilimuona kwenye foleni na aliyekuwa mbele na nyuma yake wameshatoka nje,” Amanda akajibu.
“Ametupiga chenga, keshagundua kuwa tupo!” Fredy akasema.
“Come on!” Amanda akatamka huku akitoka eneo lile na kuchukua simu yake, akampigia Martin na kumpa taarifa hiyo.
“Yupo hapo hapo, hakikisheni mnampata au mnamuona, hata tukijua tu ni wapi anafikia kwetu irakuwa sawa,” Martin akawaambia nao wakaendelea kusaka hapa na pale kwa kutazama.
Mara baada ya simu hiyo, Fredy na Amanda wakatawanyika na kuendelea kuangalia hapa na pale labda wangeweza kumuona lakini haikuwa hivyo.
“Tunafanyaje?” Amanda akamuuliza Fredy mara walipokutana baada ya kutafuta kila mtu upande wake.
“Huyu mtata, sasa tukisema tuondoke, itakuwa haina maana ya kuja, tukisema tukae pia tunaweza kupoteza muda,” Fredy akamwambia Amanda.
“Anyway twende kwenye gari, tukaone cha kufanya….”
“Aaaaaaa nimepata mbinu ya kumnasa kama yupo hapa bado,” Fredy akamwambia Amanda.
“Enhe…”
“Twende kwenye gari kisha tuondoke, kama yupo na katugundua, atatufuata ndipo tutampata…” Fredy akatoa wazo, likaafikiwa na wote wakaingia garini.
* * *
Kamanda Amata akatamani kucheka lakini akajikaza akiwa sambamba na ua kubwa lililowekwa kama urembo katika eneo hilo, vivuli vya vichaka vya ua hilo vilimfanya asionekane kirahisi na jinsi alivyojiweka. Michezo hii ya kujificha au kujipoteza asionekane alijifunza huko Japan wakati akichukua mafunzo ya Ninjutsu.
Lazima nitumie mbinu za hali ya juu kuwakwepa hawa jamaa! Akajisemea moyoni wakati akiwatazama Fredy na Amanda wakiingia maegeshoni na kuingia ndani ya gari mojawapo ambao Amata alikuwa akiliona vyema. Kutoka waiposimama wakati wakiongea mpaka alipokuwa Amata ni kama mita nne hivi, ni ua kubwa tu lililowatenganisha, hawakuweza kumwona Amata kutokana na kutumia kivuli kujificha.
Baada ya jamaa hao kutulia garini, Amata akatoka pale na kutembea kwa mwendo wa paka mpaka kwenye magari mengine ya nyuma, akachukua kifaa chake cha kufyatulia vitasa vya gari, hakuchukua hata dakika, tayari alikuwa ameketi kwenye gari asiyeijua hata mmiliki wake, akafunga mkanda huku macho yake yakiwa yanalitazama lile analolilenga.
Fredy akawasha gari na kuliondoa, Amata akasubiri kama dakika hivi nay eye akawasha na kuwafuata.
“Nitafanya kama mlivyofikiri!” akasema kwa sauti kana kwamba kuna mtu anayeongea naye. Baada ya kuicha barabara itokayo uwanja wa ndege na kukunja kushoto kuifuata ile ya Airport Ferry. Kutoka yeye na ‘kina Fredy kulikuwa na gari kama tano hivi katikati.
* * *
Amanda akatazama kwenye kioo kisha akakaa sawa kitini, Fredy naye muda wote alikuwa akitazama kioo cha ndani na kile cha upande wake.
“Vipi?” Amanda akauliza.
“Sioni kama anatufuata!” akajibu.
“Sasa atakuwa kaenda wapi mshenzi huyu?” Amanda akauliza.
“Huyu si wa kuchezea, anaonekana na mjuzi sana wa mambo,” Fredy akajibu.
Wakiwa wamezama kwenye mazungumzo, gari aliyokuwa anaendesha Amata, ilikuwa ikipita kwenye upande mwingine wa barabara hiyohiyo, taratibu alikuwa akiyaovateki magari ya upande ule mwingine ambao Fredy alikuwa akiendeshea. Alipolifikia gari la akina Amanda, akaweka la kwake sambamba kabisa, wakawa wakienda pamoja.
Ghafla macho ya Amanda yakagongana na mgeni wao.
“Shiiiit!!!!” akapiga ukulele na Fredy akageuka kutazama.
“Come on!” naye akajikuta akitamka kabla hawajatahamaki, Amata akayumbisha gari lake na kulipigiza kwa nguvu kwenye lile la akina Amanda. Akahakikisha analisukuma mpaka nje ya barabara na kugonga ukingo wake. Baada ya ukingo ule kuvunjika, Gari walilopanda Fredy na yule mawanamke likaacha barabara na kutoka nje likagonga nguzo ya taa na kuanguka vibaya. l
“Fredy! Fredy!” Amanda akaita kwa shida, Fredy akatoka kwa kutumia kioo cha mbele, akamtoa Amanda ambaye alikuwa na michaniko ya kutosha usoni mwake. Haraka sana, Fredy akamwacha Amanda chini, akachomoa bastola na kuliwahi gari la Kamanda ambalo nalo liliishi kugongo kizuizi imara cha barabara hiyo kubwa na kusababisha ajali kubwa. Fredy akalifikia na kuweka bastola yake tayari huku usoni mwake akitiririkwa na damu. Kutahamaki, Amata hayupo garini, akatazama huku na kule hakumwona zaidi ya madereva wa magari mwngine waliokuwa wakitukana ovyo.
* * *
Kamanda Amata tayari alikuwa upande wa pili wa barabara, akajibana karibu na ukuta wa kutenga barabara ya magari na watembea kwa miguu, akachungulia kwa chati na kumwona Fredy akaihangaika na yule mwanamke anavyomwacha na kuja kwenye gari alilokuwamo yeye, anavyoshangaa shangaa mpaka anaamua kurudi garini.
Ningeamua kuwaua ningewaua sasa wote wawili au hata kuwakamata, lakini wakati wenu bado nyau nyinyi! Amata akaongea mwenyewe moyoni mwake wakati akiwashuhudia wawili hao wakakokotana na kuingia kwenye taksi moja iliyosimama hapo. Baada ya wao kuondoka, Amata akaruka ule ukuta na kuliendea lile gari kabla askari hawajafika, akalifikia na kupekua haraka haraka hapa na pale. Hakupata vingi ni kadi ya gari na kadikazi moja ikiwa juu ya kiti. Mara akasikia ving’ora vya magari ya polisi vikija upande huo. Akaingiza mkono katika mkoba wake akatoa kijichupa kidogo mithili ya cha dawa ya minyoo akakirushia ndani ya gari lile kisha yeye akaanza kutembea taratibu kuelekea upande mwingine. Baada ya hatua kama mia hivi akachukua simu yake na kuwasha tab maalum akaminya ‘kitufe tepe’ kilichoandikwa ‘Fire’, mlipuko mkubwa ukatokea na lile gari likapaishwa juu juu na kutupwa chini likiendelea kuwaka.
HOTEL YA SWISS SPIRIT
HOTELI YA KAWAIDA kabisa iliyojengwa katika jiji la Freetown, ndiyo ambayo kijana huyu aliichagua kama sehemu yake ya mapumziko kwa usiku huo kiwezekana na siku nyingine ambazo atakuwa mjini hapo. Bahati pekee aliyokuwa nayo ni kwamba kila anapoingia hukaribishwa na mwanamke mrembo katika meza ya mapokezi.
“Chumba kipo, tena kimebaki kimoja nafikiri kilikuwa kwa ajili yako,” mwanadada huyu akamwambia huku akiweka vizuri kipanya cha kompyuta yake, “Pasipoti tafadhali…” akamwambia. Amata akaingiza mkono katika mfuko wa koti lake na kuchomoa pasipoti akampatia. Yule mwanadada akaifanyia kazi kisha akachukua na kadipesa yake akaichanja kwenye kifaa maalum, Amata akaingiza namba zake za siri na kisha akarudishiwa vitu vyake.
“Karibu Swiss Spirit Mr. Maturin!” akakaribiswa na mwanadada yule na sekunde hiyohiyo akaja kijana mwingine akachukua mizigo na kutangulia nayo.
“Asante sana, nafurahi kukaribishwa na kiumbe mrembo kama wewe, hakika Mungu bado hajachoka kuumba na isitoshe ana sampuli mpya ya udongo…”Amata akamjibu huku akimpa lile tabasamu lake hadimu sana ambalo hulitoa kwa nadra sana. Macho ya wawili hawa yakagongana na kushikana kama sekunde tano hivi. Yule mwanadada akashusha pumzi ndefu na kuinama chini kidogo.
“203!” akatamka.
“Asante sana, lunch kesho…” Amata akaanza ubembe.
“Saa saba kamili….”
“A aaaa najua, wapi? Ikiwezekana mi na wewe!” akamwambia huku akijivuta tayari kwa kuondoka.
“Mmmmm wewe! Wacha nihudumie wageni kwanza…”
“Halafu…”
“Nenda bwana!” yule mwanamke akamwambia Amata naye akaondoka mezani hapo taratibu kuelekea katika chumba alichokwishaelekezwa.
Mlangoni mwa chumba hicho, akamkuta kijana yule aliyempokea na kutangulia akiwa amesimama nje, Amata akafika na kufungua mlango, kisha akamwacha yule kijana amsaidie kuweka begi lake na baadae yeye mwenyewe akaingia ndani na kusimama katikati ya chumba hicho. Hakikuwa kidogo wala kikubwa bali cha wastani chenye kitanda kikubwa, kiti cha vono na kijimeza kidogo, pembeni mwa kiti hicho kwenye kona kuna nguzo ya taa hafifu iliyokuwa ikiwaka. Akatazama kila kona kwa macho tu, kisha akainua mkono na kuizungusha saa yake kwa namna fulani na kusubiri kwa sekumde kadhaa, kimya. Alipohakikisha usalama wa chumba upo akavuta kiti kingine ambacho kiikuwa kwenye dressing table na kukivuta mpaka mlangoni, pale akakiweka na upande wa mgongo akauweka chini ya kitasa kana kwamba kimepimwa urefu, kikakaa sawasawa n kukizuia kitasa kisiweze kufunguka. Kisha akavua koti lake na kulitupia kitandani, akachomoa ile kadi ya gari na kusoma ilikuwa imeandikwa kifaransa tu. Hakuona shida, akachukua jina la mmiliki na anwani yake kisha akahamia kwenye simu yake na kuanza kutafuta mtu huyo anaweza kumpata wapi.
Laurent Yonibana, Western Province 25, Domatou Road! Akaandika kwenye kijikaratasi kisha akachukua ile kadikazi aliyoiokota mle garini akaigeuzageuza na kuisoma maelezo.
Jean de Pierre! Akasoma na kutazama namba za simu na ofisi gani anapatikana.
“Nitakuwa wageni wenu kesho,” akasema na kujiweka tayari kwa kuoga na kupumzika.

WATERLOO
Martin Gupter alikuwa akiendelea kupiga maji tu huku akusubiri simu yoyote kutoka kwa washirika wake huku akilini mwake akifikiria tu ni jinsi gani ambavyo atamwadhibu adui yake pindi tu akiletewa. Akiwa katika mawazo hayo simu yake ikaitwa kwa fujo, akainyakuwa na kutazama, Fredy, akajikuta moyo ukimwenda mbiyo.
“Safi sana Fredy! Umemtia mkononi?” akamuuliza kwa jazba kuu.
“Kumtia mkononi, siyo rahisi namna hiyo, keshatuumiza vibaya hivi hapa tupo, 5 Point Clinic kwa matibabu,” akamwambia. Martin akarukaruka kwa hasira, akasimama wima na kuongea na Fredy akitaka kujua kulikoni mpaka mtu huyo awazidi ujanja. Akatoka nje ya nyumba hiyo na kuingia garini, akawasha na kuondoka kuelekea Freetown ili kuwaona wenza wake.
* * *
Fredy na Amanda walikwishapata matibabu, alfajiri ya siku hiyo Martin aliingia kwenye Clinic hiyo akiwa kafura kwa hasira.
“Que c’est il passé?” (kumetokea nini?) akamuuliza Amanda, na mwanamke huyo akamweleza kila kitu. Martin alishikwa na hasira zaidi, akatembea huku na huko kisha akatulia huku mishipa ya kichwa ikiwa imemdinda kwa hasira.
“Je vais le tuer!” (nitamuua!) akasema huku akiwa ameshika tama na kukalia kitanda cha mgonjwa. Kisha akamtazama Fredy, “washa kamera zote za siri!” akamwambia kisha akasimama na kutoka nje huku akifuatiwa na vijana hao, wakaingia garini na kuondoka zao. Martin hakwenda mbali, breki ya kwanza ni eneo ajali ambako hakukuta gari lolote mahali hapo zaidi ya majivu tu. Akaendelea mpaka kituo cha polisi na kuripoti juu ya ajali hiyo ndipo akaambiwa hata gari lenyewe limekwishateketea kwa moto. Martin akafikiri kwa nukta kadhaa kisha akatazamana na askari huyo macho kwa macho. Maswali yake yote akajibiwa na alipowaambia kuwa walikuwa wakifunkuzwa na jambazi akakubaliwa hivyo polisi wakaingia katika kazi ya kumsaka jambazi huyo, haya yote ylifanyika tu kwa sababu mlalamikaji ni Mzungu na si vinginevyo.
Baada ya kukiacha kituo hicho, Martin akagesha katika amgahawa mmoja mjini hapo kwa kupata kifungua kinywa na mazungumzo machache.
“Lazima afe taratibu, cha kufanya sasa ni kujua vipi tutampata!” akawaambia Fredy na Amata.
“Sawasawa, ila inabidi tujiweke vyama huyu jamaa anaonekana ni mjanja sana,” Fredy akasema.
“Atakamatika tu, nakwambia atakamatika tu sasa nimeamua, hawezi kufanya sisi watotot wadogo!” Amanda akalalamika huku akifunga nywele zake vizuri.
“Yeyote anayefuata nyayo hizi, yupo hatarini, tumpate huyu tumchanganye na yule bwege mwingiene kisha tuwazike wazima,” Martin akawaambia.
“Ndiyo dawa yao!” wakamjibu.
Martin akaondoa gari taratibu na kuingia barabarani, lakini ghafla simu yake ikapata uhai, akaiinua na kuitazama, akampa Fredy aasome ujumbe huo.
“Swiss Spirit Hotel!” akasema.
“Basi mchezo umeisha, mpigie simu Imlan Marikante, mwambie tuonane Sea Port leo saa nne!” Martin akatoa maagizo na Fredy akafanya hivyo.
* * *
Saa nne asubuhi hiyo Martin alikutana na Imlan Marikante katika mgahawa wa Sea Port kwa mazungumzo mafupi huku akiwa kawaacha Fredy na Amata garini wakajadilialiana hili na lile.
“Namhitaji huyu mgeni kwa pesa yoyote ile!” Martina akamwambia Imlan.
Martin Gupter na Imlan Marikante walikuwa marafiki wa muda mrefu hasa kwenye kazi nyeti kama hii. Haikuwa mara ya kwanza ila tofauti tu ni kuwa huyu aikuwa akimtaka hai mara zote alitekeleza mauaji tu kwa njia mbalimbali kwa kumtumia kijana huyu huyu kwenye hoteli mbalimbali jijini hapo na pembezoni.
“Kwa nini unamtaka hai?” Imlan akamuuliza.
“Ana mengi ya kulipa, na ninataka afe kwa kuonja uchungu wa kaburi,” akamwambia.
“Sawa, kumpata utaweza, tena leo hii hii, nilimwona akiongez kimahaba sana na mhudumu wa mapokezi pale Swiss Spirit, tunaweza kumtumia yeye akamtia penzini kisha tukamnasa,” Imlan akapendekeza mbinu ambayo Martin hakuifikiria kabla.
“Unafikiri ataweza kumtia mkononi? Maana huyu jamaa nimeshaanza kumsoma, si wa kumkamata kijinga…”
“Martin! Hakuna mkate mgumu mbele ya chai, atakamatika, anda fungu la maana nimsuke yule mwanamke, tena ni vyema akimtoa pale na kwenda naye mahala pengine,” Imlan akasema.
“Sawa!” Martin akakubali na kuondoka na jamaa huyo mpaka benki, akachukua pesa iliyotakata na kumpatia.
“Nakuamini!” akamwambia Imlan.
* * *
Wakati huo huo, Kamanda Amata saa nne hiyo alikuwa mbali kidogo na Jiji katika eneo linalojuikana kama Western Province katika Barabara ya Domatou. Mbele yake alismama mzee wa makamo kadiri ya miaka sitini au sabini hivi, aliyechakaa kwa jua la Afrika.
“Unazungumzia gari, Renault Station Wagon?” yule mzee akauliza.
“Ndiyo, kabisa, hili gari bado ni mali yako au?” akamuuliza.
“Hapana hili gari kwangu lilishapotea miaka mingi sana, nimebaki na risiti za manunusi tu basi, we umeliona wapi?” akauliza yule mzee.
“Siyo tu kuliona, limepata ajali nikafikiri waliokufa ni kati ya wanao maana walikuwa wawili,” akamwambia kwa Kifaransa safi. Katika ya ugha chache ambazo Kamanda Amata alizijua kwa ufasaha, nah ii ni mojawapo.
“Ooooo, nashukuru sana kwa taarifa hili gari nilishaibiwa, polisi wamelitafuta sana laki hawakulipa, basi nikanunu jingine!” yule mzee akasema. Baada ya mazungumzo kama ya dakika arobaini na tano hivi, wakaagana na Kamanda Amata akawasha gari lake la kukodi na kurudi mjini.
Saa saba mchana alikuwa mbele ya Clinic ya 5 Point, akaingia kwa hatua fupifupi mpaka mapokezi, akamuulizia anayetaka kuonana naye, akapelekwa. Huyu hakuwa mzee, kijana mshupavu daktari kutokana na jinsi alivyovaa. Baada ya maamkiano, Amata akaiweka ile kadikazi mezani.
“Kadi hii imeokotwa kwenye eneo la ajali jana usiku, tunapenda kujua kama marehemu ni ndugu zako au marafiki!” Amata akamwambia na yule daktari akaichukua na kuitia mfukoni huku akimwangalia kwa makini sana.
“No labda ni wateja tu, maana kuna wateja wangu walikuja hapa jana usiku kutibiwa, wakanambia wamepata ajali mbaya jana usiku, na wao najua kuwa nimewapa hii kadi muda mrefu tu, sasa sijui hiyo ni ajali nyingine au! Maana kama ni vifo hakuna kifo katika ajali hiyo,” yule daktari akamwambia Amata.
“Ooooh Good! Naweza kuwaona?”
“Hawapo wameshaondoka kwani ni mikwaruzo tu hawakuumia sana!” akamjibu. Mara hii Amata akajikuta amekosea kwa jinsi alivyomwingia mtu huyo. Hakuwa na budi kuaga lakini tayari alikwishajua kuwa adui wake watajua ndani ya sekunde chache kuwa alikuwa hapo.
Baada ya hapa wameenda wapi washenzi hawa? Akajiuliza mwenyewe huku akiwasha gari na kuingia barabarani kurudi hotelini. Nusu saa ilimchukua barabarani, akawasili hotelini na kuegesha gari, akashuka na kuingia ndani. Kabla hajazikwea ngazi kwenda ghorofa ya pili ambako chumba chake kilikuwapo, akakutana na yule mwanamke wa jana, mfupi mwenye nyama zilizonona katika mwili wake.
Huwa napenda shepu za mtindo huu! Akawaza huku akizidi kukaribiana naye na kumwona akitabasamu.
“Ndiyo unatoka?” akamuuliza.
“Yes! Nitakuwa off siku mbili kisha nitaingia kazini tena,” yule mwanamke akajibu.
“Kwa hiyo siku mbili zote sintokuona? Mbona utakuta nimekonda mwenzio,” Amata akamwambia.
“Njoo nyumbani kwangu!”
“Namwogopa shemeji,” akamjibu.
“Mbona jana ulizungumzia chakula cha mchana nyumbani kwangu? Hukujuan kama kuna shemeji yako?” yule mwanamke akamwambia, “Bahati yako ni leo tu, ukiikosa utajutia,” akangeza kumwambia huku akivuta hatua kama anaondoka.
“So?” Amata akamtupia swali.
“Kama una mambo mengi basi wakati mwingine,”
“Kwa leo nimemaliza, na hata hivyo nilikuwa nafikiri kupata mwenyeji wa kwenda kuspenda naye jioni hii ili kesho niwe na akili mpya,” Amata akamwambia huyo mwanamke.
“Ndiyo umempata!” akajibiwa. Kamanda Amata akatoa tena lile tabasamu lake la nadra, akampa funguo ya gari na kumtaka amsubiri garini, naye akafanya hivyo. TSA 1 akazikwea ngazi kuelekea chumbani kwake, akafungua na kuingia ndani kwa tahadhari kubwa, baada ya hatu kama tatu nne hivi zilizomfikisha katikati mwa chumba hicho jicho lake likanasa kwenye kile anachokiona kitandani. Akabaki na mbung’ao, ua, waridi jekundu lilikuwa juu ya shuka jeupe kitandani hapo.
“Nini hiki?” akajiuliza huku akiendelea kutazama kitandani, akachukua simu yake
 
MAGNUM22

Sehemu 14

UWANJA WA NDEGE WA LUNGI
FREETOWN
Saa sita usiku, ndege iliyombeba Kamanda Amata ikakanyaga ardhi ya jiji hilo, na baada ya hpo ikaegeshwa vyema kabisa mahala pake na abiria wakaanza kuteremka mmoja mmoja. Watu kama hawa, wanaintelijensia daima hisia kali au hupenda kuita mlango wa sita wa fahamu huwaongoza katika mambo mengi, akiwa bado ameketi kitini na abiria wengine wamekwishaanza kuteremka, Kamanda Amata alihisi kwa vyovyote kuna wenyeji wanaomsubiri.
Ili wanione vizuri ngoja niwe wa mwisho! Akawaza huku akinyayuka na kushusha mkoba wake kutoka kwenye keria ya ndani, akaupachika begani na kuvuta hatua akiwa kama mtu wan ne hivi kutoka mwisho. Mataa ya kupendeza ya jiji hilo yakamlaki, kana kwamba yanamwambia ‘karibu katika jiji la dhahabu’.
Akiwa katika foleni ya ukaguzi wa vibali vya kuingilia nchini humo, Amata akawa akiangaza huku na huko kuangalia kupitia vyoo vikubwa kabisa, kama kuna anayemhisi kumsubiri. Naam macho yake yakagongana na Amanda, japo hakuwahi kumwona viozuri huko nyuma zaidi ya picha tu ambayo alikuwa ameiweka akilini, tayari nywele zake zilisisimka akajua, tayari.
Nimeshapata mrembo! Akajisemea huku akimkabidhi pasipoti yake mwanadada wa uhamiaji.
“Karibu sana Sierra Leone!” Yule mwanadada akamwambia huku akimkabidhi pasi’ yake.
“Asante kwa ukarimu wako, nimekaribia,” Amata akajibu na kuitia mfukoni pasipoti yake, akainua macho kuitazama tena pale alipo Yule mwanamke, hayupo. Kwa kitendo hicho akajua sasa kazi imeanza kwa maana hakujua hata ni wapi mwanamke huyo kaenda, hivyo ni ngumu kujua atatokea upande gani. Akameza funda la mate, na kuvuta hatua ndogo ndogo kuelekea nje, hatua mbili tatu hivi kabla hajafika katika mlango huo, akamwona mtu ambaye akamhisi vibaya. Amata akaingia upande wa kushoto, akapita kando ya maboksio mengi yaliyolundikwa hapo, akavuta hatua za haraka haraka na kuliacha lile eneo, akajikuta kwenye bohari kubwa ya cargo. Kutoka kule akatafuta wapi panaweza kuwa na mlango wa kuendea nje, kwa bahati akauona, akenda na kuufungua, ulikuwa umerudishiwa tu, akaingia na kukutana na ngazi zikiteremka chini. Hakuuliza wala kufikiri, akashuka nazo mpaka chini kabisa, huko akatembea kwa hadhari kubwa sana akihofia kamaera za uslama kumnasa na kumletea shida kwa walinzi. Bahati mbaya au nzuri hakukuwa na hata moja.
‘Emergecy Exit’. Akaona kibao kimeabndikwa hivyo.
Ningeshangaa! Akajisemea moyoni na kuingia hapo palipowekwa mshakle wa uelekeo, milango miwili mitatu akajikuta nje, upande mwingine kabisa wa uwanja.
Mtanitafuta kwa gharama! Akasema tena na kuendelea na safari, bahati nzuri hakukutana na mtu yeyote mpaka alipofikia seng’enge zilizotenganisha eneo ambalo watu wanaruhusiwa, yaani maegesho na shughuli nyingine muhimu na lile ambalo hairuhusiwi kwa mtu mwingine kuingia. Akatazama huku na huko, akaona walinzi tu wakiwa mbali kabisa, akaendelea kutalii kwa macho hakuona kitakachomzuia kufanya atakalo. Kutoka katika mkoba wake akachukua mkasi mdogo lakini wenye uwezo wa kukata waya, akafanya hivyo na kutengeneza tundu kubwa tu, akapita na kupotelea kwenye magari mengi yaliyojipanga hapo na kujaribu kutafuta kama anaweza kumuona yule mwanamke.
Kwa upande wa Amanda na Fredy walijikuta bado wanasubiri mgeni wao atoke lakini haikuwa hivyo.
“Mbona hatoki?” Fredy akauliza.
“Mh! Sijui ila nilimuona kwenye foleni na aliyekuwa mbele na nyuma yake wameshatoka nje,” Amanda akajibu.
“Ametupiga chenga, keshagundua kuwa tupo!” Fredy akasema.
“Come on!” Amanda akatamka huku akitoka eneo lile na kuchukua simu yake, akampigia Martin na kumpa taarifa hiyo.
“Yupo hapo hapo, hakikisheni mnampata au mnamuona, hata tukijua tu ni wapi anafikia kwetu irakuwa sawa,” Martin akawaambia nao wakaendelea kusaka hapa na pale kwa kutazama.
Mara baada ya simu hiyo, Fredy na Amanda wakatawanyika na kuendelea kuangalia hapa na pale labda wangeweza kumuona lakini haikuwa hivyo.
“Tunafanyaje?” Amanda akamuuliza Fredy mara walipokutana baada ya kutafuta kila mtu upande wake.
“Huyu mtata, sasa tukisema tuondoke, itakuwa haina maana ya kuja, tukisema tukae pia tunaweza kupoteza muda,” Fredy akamwambia Amanda.
“Anyway twende kwenye gari, tukaone cha kufanya….”
“Aaaaaaa nimepata mbinu ya kumnasa kama yupo hapa bado,” Fredy akamwambia Amanda.
“Enhe…”
“Twende kwenye gari kisha tuondoke, kama yupo na katugundua, atatufuata ndipo tutampata…” Fredy akatoa wazo, likaafikiwa na wote wakaingia garini.
* * *
Kamanda Amata akatamani kucheka lakini akajikaza akiwa sambamba na ua kubwa lililowekwa kama urembo katika eneo hilo, vivuli vya vichaka vya ua hilo vilimfanya asionekane kirahisi na jinsi alivyojiweka. Michezo hii ya kujificha au kujipoteza asionekane alijifunza huko Japan wakati akichukua mafunzo ya Ninjutsu.
Lazima nitumie mbinu za hali ya juu kuwakwepa hawa jamaa! Akajisemea moyoni wakati akiwatazama Fredy na Amanda wakiingia maegeshoni na kuingia ndani ya gari mojawapo ambao Amata alikuwa akiliona vyema. Kutoka waiposimama wakati wakiongea mpaka alipokuwa Amata ni kama mita nne hivi, ni ua kubwa tu lililowatenganisha, hawakuweza kumwona Amata kutokana na kutumia kivuli kujificha.
Baada ya jamaa hao kutulia garini, Amata akatoka pale na kutembea kwa mwendo wa paka mpaka kwenye magari mengine ya nyuma, akachukua kifaa chake cha kufyatulia vitasa vya gari, hakuchukua hata dakika, tayari alikuwa ameketi kwenye gari asiyeijua hata mmiliki wake, akafunga mkanda huku macho yake yakiwa yanalitazama lile analolilenga.
Fredy akawasha gari na kuliondoa, Amata akasubiri kama dakika hivi nay eye akawasha na kuwafuata.
“Nitafanya kama mlivyofikiri!” akasema kwa sauti kana kwamba kuna mtu anayeongea naye. Baada ya kuicha barabara itokayo uwanja wa ndege na kukunja kushoto kuifuata ile ya Airport Ferry. Kutoka yeye na ‘kina Fredy kulikuwa na gari kama tano hivi katikati.
* * *
Amanda akatazama kwenye kioo kisha akakaa sawa kitini, Fredy naye muda wote alikuwa akitazama kioo cha ndani na kile cha upande wake.
“Vipi?” Amanda akauliza.
“Sioni kama anatufuata!” akajibu.
“Sasa atakuwa kaenda wapi mshenzi huyu?” Amanda akauliza.
“Huyu si wa kuchezea, anaonekana na mjuzi sana wa mambo,” Fredy akajibu.
Wakiwa wamezama kwenye mazungumzo, gari aliyokuwa anaendesha Amata, ilikuwa ikipita kwenye upande mwingine wa barabara hiyohiyo, taratibu alikuwa akiyaovateki magari ya upande ule mwingine ambao Fredy alikuwa akiendeshea. Alipolifikia gari la akina Amanda, akaweka la kwake sambamba kabisa, wakawa wakienda pamoja.
Ghafla macho ya Amanda yakagongana na mgeni wao.
“Shiiiit!!!!” akapiga ukulele na Fredy akageuka kutazama.
“Come on!” naye akajikuta akitamka kabla hawajatahamaki, Amata akayumbisha gari lake na kulipigiza kwa nguvu kwenye lile la akina Amanda. Akahakikisha analisukuma mpaka nje ya barabara na kugonga ukingo wake. Baada ya ukingo ule kuvunjika, Gari walilopanda Fredy na yule mawanamke likaacha barabara na kutoka nje likagonga nguzo ya taa na kuanguka vibaya. l
“Fredy! Fredy!” Amanda akaita kwa shida, Fredy akatoka kwa kutumia kioo cha mbele, akamtoa Amanda ambaye alikuwa na michaniko ya kutosha usoni mwake. Haraka sana, Fredy akamwacha Amanda chini, akachomoa bastola na kuliwahi gari la Kamanda ambalo nalo liliishi kugongo kizuizi imara cha barabara hiyo kubwa na kusababisha ajali kubwa. Fredy akalifikia na kuweka bastola yake tayari huku usoni mwake akitiririkwa na damu. Kutahamaki, Amata hayupo garini, akatazama huku na kule hakumwona zaidi ya madereva wa magari mwngine waliokuwa wakitukana ovyo.
* * *
Kamanda Amata tayari alikuwa upande wa pili wa barabara, akajibana karibu na ukuta wa kutenga barabara ya magari na watembea kwa miguu, akachungulia kwa chati na kumwona Fredy akaihangaika na yule mwanamke anavyomwacha na kuja kwenye gari alilokuwamo yeye, anavyoshangaa shangaa mpaka anaamua kurudi garini.
Ningeamua kuwaua ningewaua sasa wote wawili au hata kuwakamata, lakini wakati wenu bado nyau nyinyi! Amata akaongea mwenyewe moyoni mwake wakati akiwashuhudia wawili hao wakakokotana na kuingia kwenye taksi moja iliyosimama hapo. Baada ya wao kuondoka, Amata akaruka ule ukuta na kuliendea lile gari kabla askari hawajafika, akalifikia na kupekua haraka haraka hapa na pale. Hakupata vingi ni kadi ya gari na kadikazi moja ikiwa juu ya kiti. Mara akasikia ving’ora vya magari ya polisi vikija upande huo. Akaingiza mkono katika mkoba wake akatoa kijichupa kidogo mithili ya cha dawa ya minyoo akakirushia ndani ya gari lile kisha yeye akaanza kutembea taratibu kuelekea upande mwingine. Baada ya hatua kama mia hivi akachukua simu yake na kuwasha tab maalum akaminya ‘kitufe tepe’ kilichoandikwa ‘Fire’, mlipuko mkubwa ukatokea na lile gari likapaishwa juu juu na kutupwa chini likiendelea kuwaka.
HOTEL YA SWISS SPIRIT
HOTELI YA KAWAIDA kabisa iliyojengwa katika jiji la Freetown, ndiyo ambayo kijana huyu aliichagua kama sehemu yake ya mapumziko kwa usiku huo kiwezekana na siku nyingine ambazo atakuwa mjini hapo. Bahati pekee aliyokuwa nayo ni kwamba kila anapoingia hukaribishwa na mwanamke mrembo katika meza ya mapokezi.
“Chumba kipo, tena kimebaki kimoja nafikiri kilikuwa kwa ajili yako,” mwanadada huyu akamwambia huku akiweka vizuri kipanya cha kompyuta yake, “Pasipoti tafadhali…” akamwambia. Amata akaingiza mkono katika mfuko wa koti lake na kuchomoa pasipoti akampatia. Yule mwanadada akaifanyia kazi kisha akachukua na kadipesa yake akaichanja kwenye kifaa maalum, Amata akaingiza namba zake za siri na kisha akarudishiwa vitu vyake.
“Karibu Swiss Spirit Mr. Maturin!” akakaribiswa na mwanadada yule na sekunde hiyohiyo akaja kijana mwingine akachukua mizigo na kutangulia nayo.
“Asante sana, nafurahi kukaribishwa na kiumbe mrembo kama wewe, hakika Mungu bado hajachoka kuumba na isitoshe ana sampuli mpya ya udongo…”Amata akamjibu huku akimpa lile tabasamu lake hadimu sana ambalo hulitoa kwa nadra sana. Macho ya wawili hawa yakagongana na kushikana kama sekunde tano hivi. Yule mwanadada akashusha pumzi ndefu na kuinama chini kidogo.
“203!” akatamka.
“Asante sana, lunch kesho…” Amata akaanza ubembe.
“Saa saba kamili….”
“A aaaa najua, wapi? Ikiwezekana mi na wewe!” akamwambia huku akijivuta tayari kwa kuondoka.
“Mmmmm wewe! Wacha nihudumie wageni kwanza…”
“Halafu…”
“Nenda bwana!” yule mwanamke akamwambia Amata naye akaondoka mezani hapo taratibu kuelekea katika chumba alichokwishaelekezwa.
Mlangoni mwa chumba hicho, akamkuta kijana yule aliyempokea na kutangulia akiwa amesimama nje, Amata akafika na kufungua mlango, kisha akamwacha yule kijana amsaidie kuweka begi lake na baadae yeye mwenyewe akaingia ndani na kusimama katikati ya chumba hicho. Hakikuwa kidogo wala kikubwa bali cha wastani chenye kitanda kikubwa, kiti cha vono na kijimeza kidogo, pembeni mwa kiti hicho kwenye kona kuna nguzo ya taa hafifu iliyokuwa ikiwaka. Akatazama kila kona kwa macho tu, kisha akainua mkono na kuizungusha saa yake kwa namna fulani na kusubiri kwa sekumde kadhaa, kimya. Alipohakikisha usalama wa chumba upo akavuta kiti kingine ambacho kiikuwa kwenye dressing table na kukivuta mpaka mlangoni, pale akakiweka na upande wa mgongo akauweka chini ya kitasa kana kwamba kimepimwa urefu, kikakaa sawasawa n kukizuia kitasa kisiweze kufunguka. Kisha akavua koti lake na kulitupia kitandani, akachomoa ile kadi ya gari na kusoma ilikuwa imeandikwa kifaransa tu. Hakuona shida, akachukua jina la mmiliki na anwani yake kisha akahamia kwenye simu yake na kuanza kutafuta mtu huyo anaweza kumpata wapi.
Laurent Yonibana, Western Province 25, Domatou Road! Akaandika kwenye kijikaratasi kisha akachukua ile kadikazi aliyoiokota mle garini akaigeuzageuza na kuisoma maelezo.
Jean de Pierre! Akasoma na kutazama namba za simu na ofisi gani anapatikana.
“Nitakuwa wageni wenu kesho,” akasema na kujiweka tayari kwa kuoga na kupumzika.

WATERLOO
Martin Gupter alikuwa akiendelea kupiga maji tu huku akusubiri simu yoyote kutoka kwa washirika wake huku akilini mwake akifikiria tu ni jinsi gani ambavyo atamwadhibu adui yake pindi tu akiletewa. Akiwa katika mawazo hayo simu yake ikaitwa kwa fujo, akainyakuwa na kutazama, Fredy, akajikuta moyo ukimwenda mbiyo.
“Safi sana Fredy! Umemtia mkononi?” akamuuliza kwa jazba kuu.
“Kumtia mkononi, siyo rahisi namna hiyo, keshatuumiza vibaya hivi hapa tupo, 5 Point Clinic kwa matibabu,” akamwambia. Martin akarukaruka kwa hasira, akasimama wima na kuongea na Fredy akitaka kujua kulikoni mpaka mtu huyo awazidi ujanja. Akatoka nje ya nyumba hiyo na kuingia garini, akawasha na kuondoka kuelekea Freetown ili kuwaona wenza wake.
* * *
Fredy na Amanda walikwishapata matibabu, alfajiri ya siku hiyo Martin aliingia kwenye Clinic hiyo akiwa kafura kwa hasira.
“Que c’est il passé?” (kumetokea nini?) akamuuliza Amanda, na mwanamke huyo akamweleza kila kitu. Martin alishikwa na hasira zaidi, akatembea huku na huko kisha akatulia huku mishipa ya kichwa ikiwa imemdinda kwa hasira.
“Je vais le tuer!” (nitamuua!) akasema huku akiwa ameshika tama na kukalia kitanda cha mgonjwa. Kisha akamtazama Fredy, “washa kamera zote za siri!” akamwambia kisha akasimama na kutoka nje huku akifuatiwa na vijana hao, wakaingia garini na kuondoka zao. Martin hakwenda mbali, breki ya kwanza ni eneo ajali ambako hakukuta gari lolote mahali hapo zaidi ya majivu tu. Akaendelea mpaka kituo cha polisi na kuripoti juu ya ajali hiyo ndipo akaambiwa hata gari lenyewe limekwishateketea kwa moto. Martin akafikiri kwa nukta kadhaa kisha akatazamana na askari huyo macho kwa macho. Maswali yake yote akajibiwa na alipowaambia kuwa walikuwa wakifunkuzwa na jambazi akakubaliwa hivyo polisi wakaingia katika kazi ya kumsaka jambazi huyo, haya yote ylifanyika tu kwa sababu mlalamikaji ni Mzungu na si vinginevyo.
Baada ya kukiacha kituo hicho, Martin akagesha katika amgahawa mmoja mjini hapo kwa kupata kifungua kinywa na mazungumzo machache.
“Lazima afe taratibu, cha kufanya sasa ni kujua vipi tutampata!” akawaambia Fredy na Amata.
“Sawasawa, ila inabidi tujiweke vyama huyu jamaa anaonekana ni mjanja sana,” Fredy akasema.
“Atakamatika tu, nakwambia atakamatika tu sasa nimeamua, hawezi kufanya sisi watotot wadogo!” Amanda akalalamika huku akifunga nywele zake vizuri.
“Yeyote anayefuata nyayo hizi, yupo hatarini, tumpate huyu tumchanganye na yule bwege mwingiene kisha tuwazike wazima,” Martin akawaambia.
“Ndiyo dawa yao!” wakamjibu.
Martin akaondoa gari taratibu na kuingia barabarani, lakini ghafla simu yake ikapata uhai, akaiinua na kuitazama, akampa Fredy aasome ujumbe huo.
“Swiss Spirit Hotel!” akasema.
“Basi mchezo umeisha, mpigie simu Imlan Marikante, mwambie tuonane Sea Port leo saa nne!” Martin akatoa maagizo na Fredy akafanya hivyo.
* * *
Saa nne asubuhi hiyo Martin alikutana na Imlan Marikante katika mgahawa wa Sea Port kwa mazungumzo mafupi huku akiwa kawaacha Fredy na Amata garini wakajadilialiana hili na lile.
“Namhitaji huyu mgeni kwa pesa yoyote ile!” Martina akamwambia Imlan.
Martin Gupter na Imlan Marikante walikuwa marafiki wa muda mrefu hasa kwenye kazi nyeti kama hii. Haikuwa mara ya kwanza ila tofauti tu ni kuwa huyu aikuwa akimtaka hai mara zote alitekeleza mauaji tu kwa njia mbalimbali kwa kumtumia kijana huyu huyu kwenye hoteli mbalimbali jijini hapo na pembezoni.
“Kwa nini unamtaka hai?” Imlan akamuuliza.
“Ana mengi ya kulipa, na ninataka afe kwa kuonja uchungu wa kaburi,” akamwambia.
“Sawa, kumpata utaweza, tena leo hii hii, nilimwona akiongez kimahaba sana na mhudumu wa mapokezi pale Swiss Spirit, tunaweza kumtumia yeye akamtia penzini kisha tukamnasa,” Imlan akapendekeza mbinu ambayo Martin hakuifikiria kabla.
“Unafikiri ataweza kumtia mkononi? Maana huyu jamaa nimeshaanza kumsoma, si wa kumkamata kijinga…”
“Martin! Hakuna mkate mgumu mbele ya chai, atakamatika, anda fungu la maana nimsuke yule mwanamke, tena ni vyema akimtoa pale na kwenda naye mahala pengine,” Imlan akasema.
“Sawa!” Martin akakubali na kuondoka na jamaa huyo mpaka benki, akachukua pesa iliyotakata na kumpatia.
“Nakuamini!” akamwambia Imlan.
* * *
Wakati huo huo, Kamanda Amata saa nne hiyo alikuwa mbali kidogo na Jiji katika eneo linalojuikana kama Western Province katika Barabara ya Domatou. Mbele yake alismama mzee wa makamo kadiri ya miaka sitini au sabini hivi, aliyechakaa kwa jua la Afrika.
“Unazungumzia gari, Renault Station Wagon?” yule mzee akauliza.
“Ndiyo, kabisa, hili gari bado ni mali yako au?” akamuuliza.
“Hapana hili gari kwangu lilishapotea miaka mingi sana, nimebaki na risiti za manunusi tu basi, we umeliona wapi?” akauliza yule mzee.
“Siyo tu kuliona, limepata ajali nikafikiri waliokufa ni kati ya wanao maana walikuwa wawili,” akamwambia kwa Kifaransa safi. Katika ya ugha chache ambazo Kamanda Amata alizijua kwa ufasaha, nah ii ni mojawapo.
“Ooooo, nashukuru sana kwa taarifa hili gari nilishaibiwa, polisi wamelitafuta sana laki hawakulipa, basi nikanunu jingine!” yule mzee akasema. Baada ya mazungumzo kama ya dakika arobaini na tano hivi, wakaagana na Kamanda Amata akawasha gari lake la kukodi na kurudi mjini.
Saa saba mchana alikuwa mbele ya Clinic ya 5 Point, akaingia kwa hatua fupifupi mpaka mapokezi, akamuulizia anayetaka kuonana naye, akapelekwa. Huyu hakuwa mzee, kijana mshupavu daktari kutokana na jinsi alivyovaa. Baada ya maamkiano, Amata akaiweka ile kadikazi mezani.
“Kadi hii imeokotwa kwenye eneo la ajali jana usiku, tunapenda kujua kama marehemu ni ndugu zako au marafiki!” Amata akamwambia na yule daktari akaichukua na kuitia mfukoni huku akimwangalia kwa makini sana.
“No labda ni wateja tu, maana kuna wateja wangu walikuja hapa jana usiku kutibiwa, wakanambia wamepata ajali mbaya jana usiku, na wao najua kuwa nimewapa hii kadi muda mrefu tu, sasa sijui hiyo ni ajali nyingine au! Maana kama ni vifo hakuna kifo katika ajali hiyo,” yule daktari akamwambia Amata.
“Ooooh Good! Naweza kuwaona?”
“Hawapo wameshaondoka kwani ni mikwaruzo tu hawakuumia sana!” akamjibu. Mara hii Amata akajikuta amekosea kwa jinsi alivyomwingia mtu huyo. Hakuwa na budi kuaga lakini tayari alikwishajua kuwa adui wake watajua ndani ya sekunde chache kuwa alikuwa hapo.
Baada ya hapa wameenda wapi washenzi hawa? Akajiuliza mwenyewe huku akiwasha gari na kuingia barabarani kurudi hotelini. Nusu saa ilimchukua barabarani, akawasili hotelini na kuegesha gari, akashuka na kuingia ndani. Kabla hajazikwea ngazi kwenda ghorofa ya pili ambako chumba chake kilikuwapo, akakutana na yule mwanamke wa jana, mfupi mwenye nyama zilizonona katika mwili wake.
Huwa napenda shepu za mtindo huu! Akawaza huku akizidi kukaribiana naye na kumwona akitabasamu.
“Ndiyo unatoka?” akamuuliza.
“Yes! Nitakuwa off siku mbili kisha nitaingia kazini tena,” yule mwanamke akajibu.
“Kwa hiyo siku mbili zote sintokuona? Mbona utakuta nimekonda mwenzio,” Amata akamwambia.
“Njoo nyumbani kwangu!”
“Namwogopa shemeji,” akamjibu.
“Mbona jana ulizungumzia chakula cha mchana nyumbani kwangu? Hukujuan kama kuna shemeji yako?” yule mwanamke akamwambia, “Bahati yako ni leo tu, ukiikosa utajutia,” akangeza kumwambia huku akivuta hatua kama anaondoka.
“So?” Amata akamtupia swali.
“Kama una mambo mengi basi wakati mwingine,”
“Kwa leo nimemaliza, na hata hivyo nilikuwa nafikiri kupata mwenyeji wa kwenda kuspenda naye jioni hii ili kesho niwe na akili mpya,” Amata akamwambia huyo mwanamke.
“Ndiyo umempata!” akajibiwa. Kamanda Amata akatoa tena lile tabasamu lake la nadra, akampa funguo ya gari na kumtaka amsubiri garini, naye akafanya hivyo. TSA 1 akazikwea ngazi kuelekea chumbani kwake, akafungua na kuingia ndani kwa tahadhari kubwa, baada ya hatu kama tatu nne hivi zilizomfikisha katikati mwa chumba hicho jicho lake likanasa kwenye kile anachokiona kitandani. Akabaki na mbung’ao, ua, waridi jekundu lilikuwa juu ya shuka jeupe kitandani hapo.
“Nini hiki?” akajiuliza huku akiendelea kutazama kitandani, akachukua simu yake
Shukran mkuu!
 
MAGNUM22

Sehemu 15


na kupiga picha. Kisha akalichukua na kuliweka kwenye chupa ya maua, akaingia maliwato na kujiweka sawa kisha akabadili nguo na kutoka ndani humo akiwa amechukua mkoba wake. Katika kazi kama hizi hupenda kutumia mkoba huu ambao hata akitoka katika chumba alichopanga huondoka nao akiwa na maana kwamba kuna kurudi au hakuna.
Ndani ya gari alimkuta yule mwanamke akisikiliza muziki wa Richard Bona uliokuwa ukirindima ndani ya redio. Safari ikaanza ikisindikizwa na mazungumzo machache kati ya wawili hao huku wakipigana vikofi vya kimahaba. Mara tu walipowasili nyumbani kwa mwanamke huyo walijibwaga sebuleni kwenye busati la pesa nyingi, mabusu motomoto yakachukua nafasi, dakika kumi, kumi na tano tayari vifua zilikuwa wazi, miili ikakutana na mahaba mazito yakachukua nafasi.
* * *
Saa kumi na mbili jioni, Martin Gupter, Fredy na Amanda wakawasili katika nyumba hiyo wakiongozwa na Imlan ambaye alikuwa akipajua vyema kabisa. Wakaegesha gari mbali kidogo na kuteremka wakiwa na silaha mbalimbali, kila mmoja alibeba ile aliyoona inafaa. Hakuna aliyekuwa akiongea na mwenzake, kimya kimya, walizipita nyumba kadhaa na kuielea ile ya yule mwanamke.
Mita chache kabla ya kuifikia, Martin akawasimamisha na kuwapa maneno machache, “Tunatakiwa kuizunguka nyumba, tutavamia na hakuna kuuliza, piga yaani piga mpaka awe unconfotable, kisha tutambeba kuondoka naye. Kama akiwa mkaidi zaidi hatuna budi kumuua tu hapo hapo,” akawaambia kisha wakaendelea kwenda na kugawana; Fredy na Imlan wakazunguka mbele, Amanda na Martin wakazunguka nyuma tayari kwa shambulizi la ghafla.
NDANI YA NYUMBA…
Amata akamaliza kazi pale sakafuni na kumwacha mwanamke yule akiwa vipandevipande kwa mapenzi mazito aliyopewa, macho yalimlegea kiasi kwamba hata hakuweza kuona vizuri kinachoendelea zaidi ya kukumbuka tu burudani aliyopewa na mwanaume huyo, moyoni akakiri kuwa hajawahi kuipata tangua azaliwe.
Amenikuna vilivyo! Akawaza na kuanza kujiokota tayari kuinuka. Kamanda Amata akalifikia jokofu na kufungua ndani, hakuna kinywaji kikali zaidi ya sharubati na vinywaji vitamu. Akapita na kuingia maliwato akajiweka sawa na kutoka.
“Vipi mbona kama unaondoka? Hapa ni kwako vaa taulo tu, kila nikihitaji unanipa maana lleo kwangu ni neema au hujui?” yule mwanamke akamwambia Amata na nukta hiyo hiyo, mlango wa mbele ukafunguliwa kwa kupigwa kwa nguvu nao ukatii na wa nyuma nao vivyo hivyo. Wanaume watatu na mwanamke mmoja wakaingia ndani ya nyumba hiyo. Kamanda akawatazama kwa zamu, akamtambua haraka Imlan na wale Wazungu akawatambua kwa kuwa alikwishawaona picha zao isipokuwa Martin huyu alimkumbuka kwani alimsulubu kidogo pale Dar es salaam.
Yule mwanamke akasimama kando akitetemeka huku akiwa kajisitiri matiti yake kwa kipande cha nguo na huku chini alibaki na nguo ya ndani tu. Fredy akamsukuma kando, naye akaangukia kwenye kochi, akamfuata Amata huku akiwa na mnyororo mkononi mwake, akauinua na kumtandika, Amata akauepa na wakati huohuo akamona Amanda akija kasi, akainua jagi la maji na kumtishia kama anarusha, Amanda akaepa lakini hakujua hila za adui yake. Lile jagi likatua usoni mwa mwanamke huyo na kumchana vibaya. Fredy alijaribu tena pigo lile lile lakini kabla hajafanikiwa Kamanda aliruka kwa ustadi na kumtandika teke la uso, akmbwaga upande mwingine wa chumba. Akaokota ule mnyororo na kukumbana na gongo zito kutoka kwa Martin, akalinasa na mnyororo ule, akauachia upande mmoja na kulifunga. Akamvuta kwake na kumpa kichwa kilichompepesua, akamwendea na kumkamata barabara. Pigo moja toka kwa Imlan likampotezea lengo Amata alipomwacha Martin akachomoka na kisu kutoka kiunoni mwa Martin, alipogeuka akamdidimizia Imlan tumboni kisha akamsindikiza kwa teke zito na kumwacha akienda kufia chini.
Akaruka hewani na kumtandika Amanda teke la shavu, akamng’oa jino moja, Martin akamwahi na gongo lake, Amata akainua kiti na kukinga, kikavunjika katikati. Akajikuta akipigwa pigo moja matata zana ambalo likamshtua pingili za mgongo, akageuka kumtazama Fredi akajikuta akipokea gongo la kisogoni liliompelekea kwenda chini. Amata akatowa yowe la uchungu, akapigwa tena gongo lingine lililomzima chini.
Akajaribu kuinua kichwa, hakuwesa, damu zikaanza kumvuja kisogoni, mchaniko ulionekana wazi kabisa. Amata akafunikwa na giza kuu, akajikuta akihama ulimwengu mmoja kwenda mwingine.
* * *
Giza kama giza nene lilinifunika na kuniacha hivyo nilivyo. Siwezi kuelezea nini hasa nilikuwa nakiona katika ulimwengu mpya zaidi ya kelele za watoto wachanga, watu wakiimba nyimbo wakati mwingine nilikuwa nasikia sauti za ndege zikiimba mara mvumo wa upepo na wakati mwingine maji yatirirkayo.
Nikajaribu kuita laziki sauti haikutoka, nikajaribu kuinua mkono lakini haikuwezekana, kando yangu kulikuwa kuna wanyama wane wakubwa tena wanyama wakali wakiwa wamenizunguka huku ndimi zao zikiwa nje kwa kuchoka zikionesha uchu wa nyama ya mwanadamu. Ni ngumu kukwambia ni wanyama gani ila niligundua kuwa ni wakali kutokana na macho yao na meno marefu.
“Kkaaffaa aauu bbaaddoo mmzziimmaa!!??” nikasikia sauti ya mnyama mmoja ikiuliza. Kisha mnyama mwingine akaanza kuninusa na kunilambalamba kwa ulimi wake mchafu unaonuka.
“Hhannaa mmaaiisshhaa mmaarreeffuu,, ttuukkaammttiiee kkaabbuurriinnii,” yule mnyama akanambia. Nikachukuliwa mahali nisipopajua, ambako niliona mambo mengi ya kutisha, pia niliona viumbe kama watu vikitembea kando yangu vikicheka na vingine vikilia. Nikaingizwa ndani ya kitu kama chumba na kufungikwa, huku sikuona chochote zaidi ya sauti ya giza kuu.
* * *
WATERLOO
Martin alibonyeza kitufe fulani ukutani na sehemu moja ya sakafu ikafunguka, kisha akawapa vijana wake ishara ya kichwa kuwa wawatumbukize hao watu ndani yake. Mwili wa Imlan ukatupiwa ndani ya shimo hilo, kisha mwili wa Amata nao ukatupiwa humo humo.
“Mwanadamu u mavumbi, na mavumbini utarudi na sijui kama bwana atakufufua siku ya mwisho!” Marini akasema huku akicheka.
“Hash to hash!” Amanda akasema na ile sakafu ikajifunga tena kama mwanzo na zuri la kisasa likafunika juu yake. Kilichofuata hapo ni kugangana kila mmoja alipoumia. Martin akatoa chip mfukoni mwake na kuiweka mezani.
“Hii ilikuwa inawapa taarifa Tanzani mahala alipo,” akawaambia wenzake na kuitia kwenye moto, “sasa watatafuta mpaka wakome!” akasema.
“What’s next?” Fredy akauliza huku akijishikashika mbavu zake.
“Tunaanza mipango ya kutekeleza mpango wetu wa mwisho, mara hii ni two in one,” Martin akawaambia.
Martin na wenzake walitoa taarifa hiyo kwa tajiri wao, nayo ikapokelewa kwa furaha, sasa kilichobaki ilikuwa ni kumaliza misheni yao ambayo iliingia doa siku za nyuma.























X













DAR ES SALAAM
…REJEA KWA CHIBA NA AMATA…
SAA KUMI NA MOJA jioni ndege ya Ethiopia ilitua katika Uwanja wa Julius Kambarage Nyerere, Chiba na Amata walikuwa ndani ya dege hilo. Machozi yakamtoka Amata alipotazama majengo na uoto wa asili wa nchi yake.
“Home sweet home!” Amata akasema na kujifuta machozi, akainuka kitini na taratibu wakatoka katika ndege hiyo. Badala ya kupitia njia ambayo wageni wengine wanapita, wawilia hawa wakafungua kijimlango kimoja na kushuka moja kwa moja uwanjani na kutembea mpaka chumba cha VIP. Gina alishindwa kuvumilia aliinuka kitini na kumkumbatia kwa nguvu Kamanda Amata hukua akilia kwa uchungu. Madam S akasabahiana na kijana wake, wakajuliana hali, lakini aligundua wazi kuwa Amata hayuko sawa. Mbele yao kulikuwa na Scoba na Dkt. Jasmine.
“Tusichelewe, tuondoke!” Madam S akawaambia, wakatoka na kufika katika magari ambayo yalikuwa yameandaliwa.
Dkt. Jasmine alimchukua Kamanda Amata na kuingia naye kwenye gari la wagonjwa, “lala hapa!” akamwambia naye akapanda juu ya kitanda na kujilaza, Jasmine akamchoma sindano na kumlaza usingizi.

SHAMBA
Madam S alitaka kujua kila jambo analolifanya Jasmine kwa Amata, siku hii yeye ndiye alikuwa msaidizi wa daktari katika procedure zote.
“Yaani kwa hili jeraha lake, tumshukuru Mungu tu alipona, maana tungeshamkosa,” Jasmine akamwambia Madam S.
“Kwa nini?”
“Kuna damu nyingi sana hapa, ena nahisi imeingia hata sehemu fulani fulani za mfupa wa kichwa,” akamwambia.
“Oh shit, don’t say that!!!” Madam S hakutaka hata kusikia habari hizo. Baada kama ya saa nzima kupita wakiwa nd.ani ya chumba hiki kidogo chenye vifaa tiba vilivyokamilika, kazi aliyokuwa akiifanya Daktari Jasmine ikakamilika.
“Ataamka baada ya muda gani?” Madam akauliza.
“Si muda mrefu kama nusu saa au dakika ishirini hivi,”
“Ok!” Madam akaitika na kuitazama saa yake, “lakini hatoweza kufanya kazi za mikikimikiki kwa muda gani?” akaongeza swali
“Inabidi apumzike kwa muda kama wa mwezi mmoja hivi…”
“Mwezi mmoja!... atakubai mwenyewe huyu, na hapo alipo akiamka tu atataka kumtafuta mbaya wake, kama alimpasua kichwani basi na yeye atataka kufanya hivyo hivyo…”
“Kwa nini unasema hivyo?” Jasmine akauliza.
“Namjua huyu, we ngoja aamke utaniambia,”
“Ok tumwache apumzike!”
Madam S na Jasmine wakatoka ndani ya kile chumba na kuja katika chumba kingine cha mazungumzo, ni sebule ndogo yenye viti kama sita hivi vya kisasa, luninga kubwa ukutani na redio yenye muziki mnene, mahali hapa hupatumia tu kama sehemu ya mapumziko. Katika sebule hiyo, walimkuta Chiba, Gina na Scoba wakiangalia mpira wa miguu katika luninga hiyo.
Mara tu baada ya kuingia sebuleni hapo, Gina alikuwa wa kwanza kumuuliza Madam S kuhusu maendeleo ya Amata, akajibiwa na kidogo roho yake ikatulia.
“Ulimkuta wapi?” Madam S akamuuliza Chiba.
“Inaonekana aliokotwa tu, nimemkuta katika mji mdogo wa Waterloo, yaani hata hakumbukii vitu vyake viko wapi,” Chiba akaeleza.
“Sasa hii ni hatari maana anaweza akasahau hata mambo muhimu ya kazi,” Madam akaongeza kusema.
“Ila tu asinisahau mimi?” Gina akadakia na watu wote wakaangua kicheko.
Daktari Jasmine alikuwa kimya muda wote huo, akisikiliza wanayoyaongea, alionekana wazi kuwa kuna kitu kinachomsumbua akilini mwake.
“Jasmine vipi?” Chiba akamuuliza.
“Safi tu!”
“Naona umetekwa na mawazo, sijui umezama wapi, tuambie ukweli bwana, au TSA 1 ni wa kufunga minyororo? Maana kama akipata kichaa atagonga watu ngumi humu mpaka tukimbiane,” akamtania.
“Hamna, jamaa yuko poa, na ataamka muda si mrefu,” akawapa moyo.
“Kwa hiyo Madam S, kazi tunaisitisha au vipi?” Chiba akamuuliza swali bosi wake.
“Sisi tumeondolewa, yaani ninyi hamuhusiki kabisa kabisa, wamekuja wapelelezi wengine kama nilivyokwambia, na tayari wameanza kazi, hapa Tanzania yupo mmoja, Angola kaenda mmoja, Ivory Coast kaenda pia na Somalia, kisha watakutana Addis Ababa kwa majumuisho ya kazi na kutoa uamuzi mmoja wa nini cha kufanya!” akajibu.
“Basi sisi wacha tule bata!” Chiba akasema na wengine wakaunga mkono.
“Of coz, kuleni mpaka kunguru ila mjue kuwa kazi hii sisi tutaifanya kama Tanzania kwa sababu hapa kwetu kumetokea shambulizi kwa hiyo lazima tukusanye information,” Madam S akawaambia.
SOMALIA
KATIKA HOTELI kubwa ya kisasa, Fadicky Al Habib alikuwa ametulia kimya huku vijana wake kama kumi hivi wakiwa wamemzunguka. Kama ungemwona ni kama anatafakari jambo hivi, maana mikono yake miwili ilikuwa kichwani huku viwiko vikiwa vimejitegemeza kwenye magoti yake. Baada ya muda kidogo akainua uso wake na kuwatazama hao vijana.
“Mna uhakika?” akawauliza.
“Ndiyo, sisi huwa hatufanyi kazi kwa kubahatisha!” kijana aliyeonekana kama kiongozi wao akajibu kwa niaba, “nilipigiwa simu, nikafuatilia, nikamwona, na hakika hata mimi nimeona yule ni kama mpelelezi fulani hivi,” akaeleza zaidi.
“Ok, si mnajua kiapo chetu?” akauliza.
“Ndiyo! Aliye kinyume chetu na akatwe shingo!” akajibu yule kijana kiongozi.
“Yatupasa kuzuia njia zote za kutunyima ardhi ya mama zetu, damu itamwagika kama kaka yangu Jaffery anavyosema na tutahakikisha tutaikomboa Somali yetum,” akawaambia nao wakaitikia.
“Hatutakiwi kuua mtu asiye na hatia, kwa hiyo mumpeleleze, mkimgundua kuwa anatutafuta sisi basi haina budi akatwe shingo, nimemaliza,” akaongeza kusema na wale jamaa wakatawanyika na kubaki mmoja tu aliyekuwa kama kiongozi wao.
“Kuna hatihati ya kuingiza vikosi mjini maana hawa wanaojiita AU wamegoma kuaichia ardhi yetu,” akamwambia yule kijana.
“Ni sawa tu, si unaona sasa wametawanya wapelelezi wao kila kona na ofisi yao wameiweka Dar es salaam!” yule kijana akasema.
“Nina mpango mmoja kichwani…”
“Upi?”
“Chunguza ujue lini wanafanya kikao kisha tunalipua wote wakiwa mkutanoni…” Fadicky akasema.
“Yesssss!!!! Nipe kazi nianze kuandaa mpango wa siri,” yule kijana akamwambia Fadicky.
“Bila shaka, ni wewe nimekuteua, hakikisha unafanya hilo, nitakuwezesha kila kinachotakiwa,” Fadicky akamwambia.
Mkakati huo ukaanza kusukwa kati ya wawili hawa, lengo ni kukomesha kabisa mikutano ya baraza la usalama.
* * *
DAR ES SALAAM
Kamanda Amata alirudiwa na fahamu na kuamka kama saa moja baadae, akajikuta chumbani peke yake, akapepesa macho yake mazito na kutazama huku na huko, akajaribu kuvuta kumbukumbu ya wapi alipo na baadae akakumbuka.
“Shamba!” akajisemea na kuinuka taratibu kwani hakuwa amefungwa popote, akaketi katika kitanda hiki kidogo. Akajishika jeraha lake kisogoni na kugundua kuwa amefungwa kitu kama plasta hivi, akajiminya kwa nguvu na kuhisi maumivu kwa mbali tofauti na mwanzoni. Dakika hiyo hiyo, mlango ukafunguliwa, Jasmin akaingia ndani.
“Anhaaaaa!!!! Umeamka ee, safi sana na sasa nilikuwa nakuja kukutazama,” Jasmine akamwambia.
“Aaaaa nimeamka, nilikuwa na usingizi mzito kidogo usio na ndoto…” Amata akaeleza.
“Ndiyo, unajisikiaje sasa?”
“Najisikia ok, nahitaji mazoezi zaidi ya kuuweka mwili fresh!” akasema.
“Hapana, unahitaji mapumziko Kamanda!” Jasmine akamwambia.
Kamanda Amata akamwita Daktari huyo karibu na kumnong’oneza, “Sina muda, nitapumzika tu nikimtia kwenye Martin Gupter kwenye mkono wa sheria,” akamwambia.
“Martin Gupter?”
“Yes!”
Jasmin akatulia kimya kwa nukta kadhaa huku mikono yake ikiwa kiunoni, “No!”
“Never say no!” Amata akamwambia na kusimama sakafuni wima, kwanza akayumba kidogo na baadae akasimama.
“Pole!” Jasmine akamwambia Amata.
“Asante! Asante sana…” akajibu huku akitembea kutoka upande huu kwenda mwingine, “Kule Sierra walinipa dawa za kienyeji, zilinisaidia sana kwani mara tu baada ya kupaka nikapata nafuu kubwa sana!” akamwambia Jasmine.
“Unakumbuka nini kilikupata?”
“Yeah! Ila siwezi kukieleza nitakiandika kama kitabu,” Amata akasema huku akiendelea kutembeatembea.
“Kitaitwaje?” Jasmine akauliza.
“Magnum 22,” Amata akajibu.
“Magnum 22?”
“Ndiyo, na jalada lake litakuwa na vitu viwili…”
“Vipi?”
“Ua Waridi jekundu na bunduki ya Magnum 22 rifle,” Amata akaeleza huku akifungua mlango kutoka na Jasmine akamfuata nyuma.
“Hizo picha zina maana gani?” Jasmine akazidi kumuuliza, si kwamba alikuwa akimuuzi ila alijaribu kuna uwezo wa ubongo wake kama unachokifanya unakikumbuka na bado una uwezo wa kufikiri.
“Yaani kifo na mapenzi. Mapenzi ndiyo yaliyonifanya nife!”
“Kwani ulikufa?”
“Kabisa kabisa, ndo maana nakwambia kuwa sitaki kupumzika mpaka nimvunje shingo Martin Gupter anayejificha nyuma ya sura tofauti na kuihadaa dunia, anayetafutwa kona mbalimbali kwa kutekeleza mauaji mepesi na magumu akitumia zaidi ya pasipoti na vitambulisho 100,” akaeleza. Wakati wakizungumza hivyo Madam S akaungana nao.
“TSA 1!” akaita.
“HOT” akajibu.
Madam S akatikisa kichwa na kumtazama Jasmine, “Unamwonaje?”
“Yupo sawa kabisa!”
“Good!”
Wakati wao wakizungumza Amata tayari alikuwa ndani ya chumba maalumu cha kulega shabaha, akachukua bastola na kujaza risasi zilizokuwa hapo mezani, akapachika magazine na kuanza kufyatua kulenga shabaha. Kati ya risasi kumi na mbili ni mbili tu zilikosa tena sentimita moja kutoka tundu la shabaha.
Kutoka nyuma yake, Amata akasikia watu wakipiga makofi, akageuka nyuma na kukutana na timu yake yote ikiwa imekamilika. Gina alikuwa wa kwanza kumkumbati na kumbusu kisha wengine wakapata muda wa kusalimiana naye. Si kwamba hawakumsalimia mwanzoni bali salamu hii ilikuwa maalumu sana. Nusu saa baadae alikuwa kwenye chumba cha mazoezi akipigana na punch bag kwa nguvu zote, jasho likimtiririka.
“Nani uliyempania hivyo?” Madam akamuuliza, mara hii wakiwa wawili tu ndani ya chumba hicho.
“Martin Gupter, Fredy na Amanda, haya ndiyo majina yao halisi,” akajibu na kuendelea kucheza na punch bag lake.
“Ujue kuwa misheni imekuwa aborted,” Madam S akamwambia Amata.
“Kwa nini?” akajibu huku sasa akiwa kaacha kupiga lile begi, akageuka kumtazama bosi wake.
“Baraza la usalama la AU limeamua kuhamisha misheni hiyo kutoka kwetu na kuwapatia kikosi maalum cha wapelelezi kilichoundwa na wao!” akasema.
“Kwa kuwa si hatuwezi kazi au?” akauliza.
“Wanasema tumekiuka makubaliano..” Madam S akamwambia Amata kila kitu kilichoamriwa katika kikao chao ijapokuwa hakutakiwa kumwambia mtu yeyote.
“Kawaambie, hicho wanachojaribu au kutaka kufanya kitawagharimu kwa sababu hawa jamaa wana mtandao wa hatari, yaani si ajabu wanatoka tu katika milango ya afisi zenu wameshaonwa… Gupter si wa kumfuata kama unavyomfuata paka wako, yule jamaa ni hatari, ana mtanda wa kutisha na sasa anafanya kazi na wanamtandao wengine nao wana masikio marefu kama yeye,” akatulia kidogo na kunywa maji, “mimi nilipoishia ndipo nitapoanzia,” akamwambia Madam.
“No! alzima uheshimu maamuzi ya kamati…”
“Siendi kwa ajili ya kamati, naenda kumsaka Gupter personally nina miadi naye,” akaanza kupiga tena begi lake mara hii kwa nguvu zaidi ya mwanzo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom