RIWAYA;
KISASI
MTUNZI;
FRANK MUSHI
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
Nimeshafanikisha kutega mawasiliano yote ya
Mary na Mark ya barua pepe na hapo ni pa
kuanzia tu. Khajat atafatilia ya Dany na
tukifanikiwa kumpata yeye ndo atatusaidia.
Alisema Felly. Nilikaa kimya tu sikujua cha
kusema niliamua kushukuru lakini nilichokuja
pia kugundua kumbe Pamela alikuwa pia
akiwalipa kama motisha ya kufanya kazi hiyo,
nilifarijika lakini kazi kubwa ilikuwa ni je nini
kitafata????
Unafikiri kuwa kwakuwa hakupendi basi wewe
huna thamani. Unafikiri hivyo kwakuwa tu
hakutaki tena, na kwamba yuko sahihi,
kwakuwa mawazo yake na Hukumu yake juu
yako iko sahihi. Kama amekufukuza na
kukupiga basi wewe ni takataka. Unahisi yeye ni
wako kwakuwa unataka uwe wake. Hapana
usifanye hivyo. Ni neno baya sana kusema ni WAKO. Hasa unavyolitumia kwa mtu unayempenda WEWE. Mapenzi hayatakiwi kuwa
hivyo. Umeshawahi kuona jinsi mawingu
yanavyopenda mlima? Hujizungusha pembeni
yake na kuna wakati huwezi kuuona mlima
kwakuwa tu mawingu yameufunika. Lakini
unajua kuwa ukienda juu ya mlima utaona kilele
chake? Na hii ni kwakuwa mawingu hayafuniki
kilele cha mlima. Kilele cha mlima huonekana
kwa juu kwakuwa mawingu hukiachia,
haikifuniki. Huuacha mlima uweke kichwa chake juu, huru bila kuwa na kitu cha kuuficha juu au kuusonga. HUWEZI KUMILIKI MTU. Huwezi
kupoteza usichokuwa nacho. Kuna muda jifunze kuwa mbinafsi ili kuzuia kuumia na wale uwapendao. HII NI SEHEMU YA KUMI NAMOJA,
**PATRICK**
Kuna mambo nilikuwa nikiona hayawezkutokea
kwa binadamu wa kawaida. Kuna mambo
mengine niliona ni kama simulizi za kusadikika
na kwamba hayawezi kumtokea mtu kabisa.
Kila mtu ni kipofu wa kesho yake, laiti kama
ningejua nini kitanitokea katika maisha yangu
basi pengine ningetumia uwezo wangu na pesa
zangu zote kuzuia haya yasitokee. Maswali
yalikuwa ni mengi sana, swali kubwa ni kwamba
Mary alikuwa na mpango gani na mimi. Mark
anahusikaje toka mwanzo kabisa wa mapenzi
yangu na Mary. Majibu yalikuwa ni machache
na yasiyo ya kuaminika kabisa kwa maswali
yote niliyojiuliza. Dany angepatikana ndiye
pengine angeweza kunipatia majibu machache
kati ya mengi niliyoyawaza.
*******
Kesho yake asubuhi nilikwenda kazini kama
kawaida na nilipofika pale maaskari na maafisa
upelelezi walikuwa wakinisubiri kwaajili ya
kumalizia upelelezi wa awali. Tulikaa pamoja
na kuzungumza na walipomaliza waliondoka na
mimi niliendelea na kazi.
Ngriiiiiiiii,,,ngriiiiii. Simu yangu ilikuwa ikiita na
nilipoitazama nilikuta ni Khajat.
Hallow Khajat. Nilimsalimu huku nikitabasamu
kama vile aliniona.
Hallow Patrick, kuna Maswali nilitaka kukuuliza
kwanza. Aliongea na kusikika kama alikuwa
akichapa kitu kwenye kompyuta.
Sawa uliza nakusikiliza. Nilijiweka tayari
kujibu maswali yake sawia.
Ulisema Dany anaitwa nani jina lake kamili?
Aliuliza na kunyamaza kidogo.
Daniel Mfangavo. Nilimjibu na yeye alikuwa
kama anaandika.
Je inawezekana ndio yeye anaitwa Daniel
Fredrick? aliniuliza tena na mimi nilikaa kwa
muda nikitafakari kama anaweza kuwa yeye.
Ndio, jina la baba yake ni Fredrick Mfangavo.
Nilimjibu na yeye aliendelea kuuliza.
Je unafahamu jina la mke wake? aliuliza swali
hilo ambalo lilikuwa jepesi kwangu kwakuwa
mke wa Dany alikuwa ni rafiki yangu mkubwa
sana toka kipindi tukiwa sekondari.
Ndio, anaitwa Catherine Cathbert. Nilimpa jibu
lakini akaonekana kama kuguna vile.
Umesema Catherine Cathbert? aliniuliza tena
na kunyamaza kidogo.
Ndio, vipi kwani? nilimuuliza tena. Kwa
vyovyote nilijua kuwa kuna kitu hakipo sawa.
Subiri kidogo usikate simu. Aliniambia hayo na
nilisikia kupitia simu kama vile akibonyeza
vitufe vya simu kama ishara ya kwamba
alikuwa akipiga simu, kisha baada ya muda
kidogo nikasikia akiongea kwenye simu.
Hivi uliniambia umekutana na jina Catherine
Cathbert? alimuuliza huyo aliyekuwa akiongea naye kwenye simu, ikaonekana kama vile
ameshapata jibu la swali alilouliza na kisha aliendelea.
Ni mke wa Dany, hivyo endelea kuanzia hapo.
Alimaliza kuongea na nikasikia akikata simu.
Patrick. Alirudi tena kwenye simu tuliyokuwa tukizungumza na kuniita na nilipoitika hakunipa
muda wa kumuuliza chochote bali aliendelea na maswali.
Dany na Mary walijuana lini? aliniuliza na
nilikuwa nikisikia kabisa akiandika kwenye kompyuta.
Aah Dany alimjua Mary wakati nilipoanza
mahusiano na Mary na si kabla ya hapo.
Nilimjibu na hapo Khajat aliniambia nisubiri kidogo, alipomaliza kuandika aliongea tena.
Dany anafanya biashara gani? aliniuliza tena na hapo sikuwa na ushahidi na biashara
anayofanya kwa sasa lakini nikijuacho ni kwamba Dany alikuwa ni meneja wa hoteli kubwa jijini Dar es Salaam na alikuwa akimiliki
kampuni ya utalii ambayo hata hivyo ilikuwa ni
ndogo sana ambayo nilikuwa na mpango wa
kuja kuiunganisha na kampuni yangu
niliyotegemea kufungua hapo baadaye.
Ni meneja wa hoteli na anamiliki kampuni ya utalii. Baada ya kumjibu aliendelea tena na maswali.
Urafiki wenu na Dany ulikuwaje. Aliuliza swali jingine.
Alikuwa ndiye mtu ambaye alijua siri zangu zote, kila kitu kwenye maisha yangu yeye ndiye alijua na kila kitu chake aliniambia. Ni rafiki yangu mkubwa na ninayemuamini kama nilivyokuwa nikimwamini mama yangu. Baada ya hapo Khajat aliniulizwa swali la mwisho.
Je mpaka sasa kwa walioko Tanzania ni nani unamuamini sana? sikuwa nimemuelewa vizuri sana.
Sijakuelewa swali lako. Nilimuomba alirudie tena swali hilo.
Kuacha mimi, Pamela na Felly, nani mwingine unamuamini? lilikuwa swali gumu sana lakini sikuwa na namna zaidi ya kueleza ukweli wa hisia zangu.
Namuamini sana Dany, ni kwa vile tu hajajua
ukweli kuwa niko hai na nimehujumiwa sana, na
ninajua kama akijua ukweli atatusaidia
kurudisha kila kitu changu. Nilimueleza hayo
kisha aliniaga na kukata simu.Baada ya muda
kidogo Pamela alikuja pale kazini na alipita
moja kwa moja mpaka ofisini kwangu, nilijiuliza
ni kwanini alikuja ofisini kwa muda ule lakini
nilituliza akili ya kujiuliza baada ya yeye
kunieleza nia yake ya kuja pale.
Ni mekuja kukuambia kuwa tunaenda na Felly
sehemu fulani hivi kuna rafiki yangu nampeleka
akamuone ilikumsaidia kwaajili ya mambo yake
kisha tutawahi kurudi. Alineleza hayo lakini
moyoni nilikuwa na wasiwasi sana juu ya
walikokuwa wanatakiwa kwenda.
Lakini sio hatari huko mnakokwenda Pamela?
nilimuuliza na kuonyesha dhahiri wasiwasi
wangu kitu kilichoonekana kumvunja moyo.
Sio hatari Patrick, ingekuwa hatari wala
nisingethubutu kabisa kwenda, najua nimetoka
hospitali muda si mrefu sana na ninatakiwa
nipumzike angalau miezi mitatu lakini huku
tuendako ni muhimu zaidi kwa Felly kukamilisha
uchunguzi wake ili jioni atupe mrejesho wa
alichokuwa akikifanyia uchunguzi. Alijitahidi
kunishawishi na mimi sikuwa na kitu cha
kupinga. Alikaa pale kidogo na Felly alikuja.
Hey Patrick najua utakuwa na wasiwasi,
atakuwa sawa ili mradi yuko na mimi,
ananifikisha kwa huyo mtu kisha nitampa
dereva amrudishe. Aliongea Felly na hapo
waliondoka. Kwenye majira ya saa tisa mchana
kazi zilikuwa zimekwisha na Khajat alikuja
kunifata pale ofisini.
Patrick nimefanikiwa kujua kujua Dany alipo
sasa nataka twende wote ila utajificha sehemu
nakuwekea hivi vidude masikioni utakuwa
ukisikia nikiongea nae na hata wewe utaweza
kuniambia chochote kama ukitaka, nataka
nimfate kwanza mimi nimjue vizuri kisha
tutaangalia kitu kingine cha kufanya. Aliongea
Khajat na hapo aliniwekea kidude fulani hivi
kama kifungo na kuongea kisha nilimsikia
kupitia kile kidude, akawasha gari na sasa
tukaondoka mpaka kwenye bar moja maarufu
sana pale Fiji, tulipofika Khajat alishuka na
kuniambia nimfate. Tukaenda mpaka kwenye
sehemu fulani kulikuwa na kona ya kupumzikia
watu na pale tukakutana na dada mwingine
ambaye sikuwa namfahamu.
Vipi yuko wapi? Khajat alimuuliza yule dada.
Nimeshamtengea sehemu ya peke yake yuko
kwenye ile kona pale una muona? yule dada
akamuonyesha Khajat.
Patrick, Dany ni mdhaifu wa nini mana kila mtu
anaudhaifu wake. Aliniuliza Khajat na kunifanya
nicheke.
Dany anapenda sana wanawake. Nikamjibu
huku nikiendelea kucheka.
Najua Dany ni mdhaifu wa wanawake lakini
unajua ni mdhaifu wa sehemu gani ya
mwanamke? aliuliza tena Khajat na kunifanya
akili yangu irudi nyuma na kukumbuka kipindi
tukiwa shuleni. Kabla ya Dany kuwa na Cathe
alikuwa akimpenda sana msichana mmoja
aliyekuwa akiitwa Anjela, sio kwamba alikuwa
akimpenda sana, hapana alikuwa akimtamani zaidi, kilichokuwa kinamfanya amtamani Anjela ni mapaja yake meupe, na kila mara alikuwa akiniambia hilo. Hata mama yake Dany kabla ya kufariki kipindi Dany akiwa shule ya msingi aliwahi kusema mwanae ni mbaguzi sana hata marafiki huwa anapenda weupe tu. Hivyo ugonjwa wa Dany ni mapaja meupe.
Anapenda sana mapaja hasa meupe kama
yako. Nilimjibu Khajat na yeye alicheka kisha aliniambia nimsubiri pale. Akaondoka na yule.msichana na baada kama ya dakika kumi alirejea pale. Alikuwa kapendeza sana ndani ya sketi fupi sana iliyoacha mapaja yake nje.
Kama hivi. Aligeuka huku na huko ili
nimtazame.
hahaa, ndio kama hivyo, umependeza sana. Nilimwambia Khajat na yeye alicheka na.kukonyeza.
Sasa, mimi nitaenda kuonana na Dany pale.Wewe utakuwa hapa utasikiliza anayoniambia kama ni ya kweli ama la kama ikitokea nimemuuliza kitu unachokijua, uwe mvumilivu inaweza kuchukua zaidi hata ya masaa 8 kuwa na mazoea nae. Ukiona tumeondoka nitakupa.ishara na wewe utakuwa na huyu dada hapa atakuongoza kila kitu na sehemu ya kwenda,nataka kujua vitu vingi sana kwake hivyo itachukua muda. Aliongea Khajat.
Sawa, hilo kwangu mimi sio tatizo.
Nilimwambia na hapo alianza kufikicha macho yake mpaka yakawa mekundu kabisa.
Khajati ndo unafanya nini hivyo. Nilimuuliza kwa mshangao, macho yake yalikuwa mekundu.kama vile alikuwa akilia.
Hii ni sehemu ya mchezo, nitakie mafanikio basi. Alicheka wakati akijibu.
Nakutakia mafanikio mema. Aliondoka pale na nilimuona akielekea kwenye ile meza aliyokaa Dany. Sikujua alikuwa anataka kufanya lipi na
lipi, sikuelewa kabisa angefanyaje ili kufanikisha hayo aliyoyakusudia. Nilikuwa nimekaa pale nikitamani sana kuongea na Dany, huyu jamaa ni rafiki yangu sana, tulianza wote kutafuta maisha na kutembeza wasifu wetu kila sehemu kabla ya kuamua kujiajiri wenyewe. Mara zote nilikuwa nikikaa kwao na yeye akikaa kwetu.
Dany hakuwa na mama kwakuwa mama yake
alishafariki toka yeye akiwa shule ya msingi
hivyo nyumbani kwao walikuwa watoto wa
kiume tu lakini pia wawili walifariki kwa ajali kipindi tukiwa wakubwa kabisa, hivyo Dany alibaki kuwa peke yake. Hivyo mimi ndiye nilikuwa ndugu yake wa kipekee kabisa.
Dada unalia nini? Nilishtuka na kusikia sauti ikiuliza swali hilo. Mh! nikaguna na kutazama
kule alikokuwa Khajat. Nikaona Dany akiwa.karibu naye na Khajat alikuwa ameinama akilia. Sikujua imetokeaje.
Khajat mbona unalia nini kimetokea.
Nilimuuliza Khajat kwakuwa nilijua angenisikia
kupitia kile kidude alichoniwekea.
Niko sawa usijali hakuna tatizo lolote. Alinijibu
na mimi nilisikia nikamuelewa lakini jibu
alilonipa liliendana na swali alilouliza na Dany
hivyo Dany alidakia.
Hakuna tatizo wakati unalia dada, nambie nini
tatizo naweza kukusaidia. Dany alidakia na
kuonyesha nia ya ukaribu.
Nyie wanaume ni nyoka kabisa, nimempenda
alaf leo anakuja kuniacha pasipo sababu,
kwanini jamani? Khajat alizidi kulia mpaka
ikabidi mimi nitoe kile kidude nicheke kwanza.
Dany ikabidi aanze kumbembeleza pale mpaka
Khajat akanyamaza. Nikarudisha tena kile
kidude sikioni ili niweze kusikia yanayojiri.
Usijali maisha ndivyo yalivyo, haimaanishi
mmoja kukufanyia hivyo basi wote ni ndivyo
walivyo. Kuna muda lazima ujifunze kuacha mtu
aondoke kama hataki kukuthamini, ujifunze
kujali zaidi furaha yako kuliko ya mtu asiyejali
ya kwako. Kuna muda lazima mambo fulani
yatokee ili dunia izunguke. Maisha yataenda
kama utajifunza kuwa mbinafsi muda
mwingine. Aliongea Dany kwa busara ya hali
ya juu.
Uuf angalau nina jisikia nafuu kwasasa,
naomba muite muhudumu nataka pombe kali.
Aliongea Khajat na hapo Dany alimuita
muhudumu na kumuagizia amletee pombe kali.
Dany hakuwa mnywaji toka zamani sasa
sikujua itakuwaje hapo kwenye kunywa ila
Khajat alimlazimisha kunywa na muda si muda
niliona wakikumbatiana na kupigana mabusu.
Dany alishaanza kulewa na kuongeaongea.
Muda ulizidi kwenda na mimi nilikaa pale tu
nikisubiri maelekezo yoyote. Nikamuona Khajat
akitoka pale na kuelekea chooni kisha
aliniambia nimfate, muda huo giza lilikuwa
limeshaingia. Nilikwenda mpaka choo cha
wanawake.
Patrick wewe unatakiwa sasa uende nyumbani,
Felly anakuja hapa utaondoka akishafika, nenda
akae na Pamela. Aliongea hayo na mimi
sikuwa na pingamizi kwakuwa nilikuwa
nimechoka.
Sasa na wewe unavyokunywa pombe hivyo
siutashindwa kufanya kazi? nilimuuliza huku
nikimtazama.
Hahaaa, hizi kazi nimefanya kwa miaka mingi
sana Patrick, hata ninywe ndoo nzima pale
silewi, atalewa yeye, kwenye ile glasi
ninayotumia nimeweka kidonge cha kukata
kilevi, hivyo mimi pale nakunywa pombe tu
isiyo na kilevi ila yeye ndiye anayekunywa yenye
kilevi ndo mana unamuona hajielewi. Felly
ameshafika fanya uende. Aliniongelesha na
tuliagana akaondoka, bado aliniambia kuwa
nitamsikia kupitia kile kidude nisikitoe.
Nikaondoka mpaka nyumbani na nikiwa njiani
nilisikia bado Khajat akimsisitiza Dany
wakalale. Kwasauti ya Dany niliyoisikia ni kama
vile alikuwa kalewa sana. Baadaye nilisikia tena
sauti ya Khajat ikimuelekeza Felly namba ya
chumba na hoteli waliyokuwa wakienda na Felly
alimwambia CC2 italetwa kwenye chakula na
muhudumu kisha anajua cha kufanya ili
wafanye kazi kwa ukaribu. Sikuwa nimeelewa ni
nini na mimi ikabidi niingilie.
Hey CC2 ndo nini nyie watu. Niliuliza na
nilisikia sauti ya Khajat ikicheka.
Ni Coca kete mbili, coca ndiyo mmea
unaotumika kutengenezea madawa ya kulevya
ya kokein. Alinijibu na hata kabla sijauliza
chochote waliendelea na mazungumzo yao na
baada ya muda mfupi sikusikia kitu tena kwa
maana ya kwamba mawasiliano nao yalikatika.
Nilifikia nyumbani na tulikaa na Pamela na
mtoto wetu Cris na hadi tunaenda kulala
hakukuwa na taarifa yoyote toka kwa Khajat
wala Felly na kwakuwa kesho yake haikuwa
siku ya kazi basi wao walikuwa wa kwanza
kufika kwetu asubuhi na kutuchukua mpaka
kwa Felly kwakuwa kule ndio kulikuwa na vifaa
vya uhakika vya kutufanya tuelewe vizuri
watakayokuwa wanatuambia.
Twendeni kule chini nikatumie ile kompyuta
kubwa. Aliongea Felly na hapo tulishuka ngazi
na kwenye kwenye chumba kilichokuwa chini ya
ardhi.
Ataanza kuongea Khajat kisha mimi
nitamalizia. Aliongea Felly.
hahaa aanze dogo sio. Nilitania na wote
walicheka.
Hahaa, sawa bhana, ila dogo sasa hivi ni
Cris. Walicheka tena wote na Khajat alianza
kuongea.
Jana nilianza kazi ya kumtafuta Dany na
nikagundua ameingia nchini kwa biashara,
amekuja kufatilia magari ya kitalii aliyonunu
kwenye kampuni moja iliyoko huku.
Nikabahatika kupata namba yake ya simu
aliyoitumia kumpigia afisa mmoja wa uhamiaji
na ndipo nilipotafuta eneo ambapo ile namba
ipo kwa wakati huo, nikaenda na Patrick mpaka
pale na nilifanikiwa kumpata Dany zaidi ya vile
nilivyotarajia. Baadaye Patrick ulipoondoka
mimi nilikwenda na Dany hotelini na nilifanikiwa
kumuwekea dawa na hapo alilala kabisa. Hivyo
mimi na Felly tulipata muda wa kupekuwa
kompyuta yake na simu na kutambua
mawasiliano yake mengine. Alimaliza Khajat na
Felly alidakia.
Katika kutafuta Dany, jana nilikuta mawasiliano
ya barua pepe toka kwa mtu anayeitwa
Catherine kwenda kwa Mary, ujumbe ulikuwa
ukieleza juu ya kuingiza magari yake kwenye
mzunguko wa kampuni yake kama vile walivyo
ahidiana, hii ilikuwa ni mwezi mmoja toka baba
yako afariki, lakini ujumbe huo ulijibiwa na
ulisomeka kama ifuatavyo nakumbuka shem,
tena najua unadai mengi sana na asante kwa
uvumilivu wako, kesho nitamu assign mtu
atakuja kuyaingiza kwenye payroll na wewe
utatuma vijana wako wayalete sehemu ya
ujumbe huo ambao ulisomeka hivyo ulikuwa
kwenye anuani ya
cathe.co@gmail.com na
uliandikwa kwa mchanganyiko wa lugha ya
kingereza na Kiswahili na Pamela ndiye
aliyetusaidia kutafsiri maneno ya Kiswahili.
Ujumbe huo pia ukajibiwa tena kwa lugha ya
kingereza kuwa thanks, though it was a great
pain but atlist we have accomplished the
mission (asante, japokuwa yalikuwa ni
maumivu makubwa lakini angalau
tumekamilisha mpango), swali nililojiuliza
lilikuwa ni huo mpango ulikuwa upi? Na pia
aliyetuma barua pepe hii alikuwa ni nani, je ni
Dany au ni Catherine, jibu lilikuwa ni dogo tu,
kama Cathe ndiye angekuwa ametuma ule
ujumbe basi Mary asingemwita shemeji, hivyo
aliyetuma ule ujumbe alikuwa ni Dany. Baadaye
siku hiyo hiyo ile anuani ya barua pepe ilituma
ujumbe kwa mtu aliyeitwa Paul akimwambia
nilitambulishwa kwako na Mary, nimefurahia
kazi yako ya nje na ya ndani. Nategemea
kufanya kazi na wewe ikitokea kuna ulazima,
ujumbe uliishia hapo na Paul aliujibu. Hapa
kumbuka kuwa Paul ni yule ambaye Mary
alimtumia ujumbe kumwambia juu ya
kukamilika kwa mpango wa kuchomoa zile
karatasi lakini zaidi kumwambia ajiandae kwa
mpango mkubwa utakao fata. Hivyo mpaka
hapa Paul ndiye kijana wa kazi za kihalifu wa
Mary. Kuna wasiliano pia ya Mary kwenda kwa
Paul akimwambia tembea juu ya nyayo za
Mark, subiri ujumbe wenye G na O itakuwa ni
red light and when it turns green, you know
what to do, mind you, this is the master plan,
after this we will be done with all the shit and
you will go back to Al Hamid for the Pritoria
event(itakuwa ni taa nyekundu, na ikibadilika
kuwa ya kijani, unajua cha kufanya,
nikukumbushe kuwa huu ndo mpango mkubwa,
baada ya hili tutakuwa tumemaliza upuuzi wote
na utarudi kwa Al Hamid kwaajili ya tukio la
Pritoria), huu ulikuwa ujumbe toka kwa Mary
kwenda kwa Paul uliotumwa siku tatu kabla ya
leo, meneno ya Kiswahili tumepata tafsiri toka
google. Pia kwa kipindi cha nyuma kuna ujumbe
ulitoka kwa Dany kwenda kwa Mary na hiki ni
kipindi kile Mary akiwa bado yuko huku, ujumbe
huo ulikuwa ukisomeka Hey Mary, you didnt
bring me up t speed for two day, is there a
prob? Setup is in place, green code to
you. (Hey Mary, hujanipa taarifa kwa siku
mbili, kuna tatizo lolote?, mazingira yako sawa,
unaweza kuendelea) maneno yaliyotumika hapa
ya green code na mengine ni maneno ambayo
hutumiwa na watu wenye mafunzo ya kijeshi au
wapelelezi au majasusi au majambazi wenye
uelewa wa lugha za kijeshi. Hii ikanipa
wasiwasi sana, nikaendelea kutafuta
mawasiliano mengine ambayo yalikuwa kati ya
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Alsad
Drilling Company ya Urusi na Mary
akimuelekeza kuwa atakuwa tayari kununua
hisa zote na kuihamishia kampuni hiyo nchini
Tanzania baada ya kukamilisha mpango wa
kumuondoa mtu ambaye ni kikwazo, ujumbe
unamueleza jinsi alivyofurahishwa na mbinu
aliyompa ya kufungua kampuni Maputo na
Afrika ya kusini ila pia anashukuru kwa zile
sanduku za silaha zilizofanikiwa kumfikia bila
tatizo na hivyo ameimarika na sasa yuko tayari
kwa kazi baada ya vijana wake kumaliza
mafunzo. Hizo ni habari chache tu, lakini kubwa
ni kwamba tunaye Dany hapa ndani. Felly
alifungua mlango mmoja uliokuwa pale ndani
na nikamuona Dany akiwa amefungwa kwenye
kiti na mdomo wake ukiwa umefungwa pia,
alikuwa na majeraha kiasi usoni.
Dany!! nikamsikia Pamela akimwita kwa
mshangao.
Unamjua? Nilimuuliza Pamela.
Huyu ndiye aliyenibaka yeye na ndugu zake
kipindi kile nikiwa nafanya kazi kwao. Sikujua
cha kusema, Khajat aliufunga ule mlango na
kutugeukia tena.
Kibaya zaidi ni kwamba leo asubuhi Mary
amemtumia Dany ujumbe kuwa tayari
wameshafanikiwa kumuua MARK usiku wa leo
na sasa wako huru kuendelea na mambo
mengine. Aliongea Khajat.
ITAENDELEA