Sehemu ya Tano
Kwa Mary Robert.2010
Hakuna haja ya kukata tamaa na kujiona kuwa huna thamani katika mapenzi yako kwakuwa tu kila mahusiano uanzishayo hayawi na mwisho
mzuri au ulioutarajia, maisha ya mapenzi ni maisha dhalimu muda mwingine. Unaweza
kukutana na mtu sahihi katika muda usio sahihi,na unaweza kukutana na aliyesahihi katika muda usio sahihi. Unachotakiwa kufanya si kukata tamaa bali kuwa makini na muda na unaokutana nao. Kila mtu anapacha wake hapa duniani,inapotokea umekutana na pacha wa mtu, ndipo shida na matatizo huanzia hapo. ATAKUJA MTU KATIKA MAISHA YAKO ATAKAYEKUFANYA UGUNDUE KWANINI HUKUDUMU NA ULIOACHANA NAO HII NI SEHEMU YA TANO.
Msisimko wa simulizi ile uliufanya uso wangu upauke kama kipande cha muogo wa kiangazi,niligundua kuwa baridi lilikuwa likipenya kwenye lile dirisha dogo la chumba changu na kunifanya nikakamae, lakini hiyo haikunifanya nichoke kusikiliza, tayari yule msichana Felicity ambaye ni mpelelezi alikuwa ameshagundua kuwa Nancy ndiye aliyefyatua ile risasi, moyoni nikajiuliza
kwanini Nancy afanye hivyo, lakini sikuwa na jibu.
Nilifunga lile dirisha vizuri na kuchomeka makaratasi ili lisifunguke tena na kupitisha baridi
kisha nikachukua headphones zangu na
kuchomeka kwenye redio kisha nikaweka masikioni ili nipate kusikia kwa ukaribu zaidi. Na sasa Pamela alikuwa na kibarua kizito cha kueleza Nancy ni nani. Ikawa hivi;
***PAMELA***
Hapana Nancy hawezi kufanya hivyo, hanasababu ya kufanya hivyo nilitokwa na machozi
kila nilipokuwa nikimtetea, nilimpenda sana Nancy
japo nilimpenda sana Patrick kuliko mtu yeyote.
Nancy ni nani aliuliza Patrick huku akinitazama
kwa jicho kali, sikuwa na la kumjibu kwakuwa
ilitakiwa nitumie mda mrefu kumuelezea kuhusu
Nancy ili anielewa na awe tayari kuyapokea yale
nitakayomwambia.
Nancy ndiye aliyetenda hili na si mtu mwingine
Pamela alidakia Felly kabla sijamjibu Patrick swali
lake, nilikuwa nikimtazama Felly na hapo alifungua
tena ile laptop yake na kuendelea kuelezea;
Nilikuambia mapema kuwa kama mpigaji alikuwa
ni mtu mwenye uzoefu wa kushika bastola basi
asingiweza kumkosa Patrick kwa ile kona aliyokaa
(huku akielekeza kwenye projekta), na kama
angemkosa au kucheza mkono kidogo basi
ingemchubua mkono wake wa kushoto, lakini
haikuwa hivyo badala yake ilipita futi 6 toka
alipokuwa Patrick, kwa maneno mengine mtu huyo
mkono wake ulicheza kutokana na ule mtikisiko wa
risasi ilipokuwa inatoka. Sasa kama ulicheza na
kama alikuwa sio mzoefu basi inamaana mkono
ulishtuka, na kama ulishtuka basi ni wazi kuwa
lazima atakuwa ameufunga mkono kwa sasa
alivuta pumzi na kufungua tena sehemu nyingine
kisha aliendelea.
hii hapa ni picha iliyopatikana kwenye kamera za
zahanati ya Hilton, mita mia saba hamsini kutoka
hapa, ilikuwa ni picha iliyonaswa lisaa limoja
baada ya tukiohilo kutokea, itazame kwa makini
huyu ni Nancy, alikwenda siku hiyo akiwa
ameushikilia mkono, na alifungwa bandeji mkononi,
sasa ukiangalia alifungwa mkono wa kushoto hii
inamaana kuwa Nancy anatumia mkono wa
kushoto, baada ya mimi kufatilia juu ya faili la
Nancy katika zahanati hiyo nilikuta limeandikwa
kuwa alianguka kwenye ngazi. Kwenye siku ya
tukio Nancy hakwenda kazini, alikuwa nyumbani
siku nzima kwakuwa siku hiyo haikuwa siku ya
kazi, hii inamaana kuwa kama Nancy alikuwa
hayupo kazini basi angekuwa ameanguka kwenye
ngazi za nyumbani kwake, lakini pia nyumbani
kwake yeye hakuna ngazi fupi wala ndefu hivyo ni
ngumu sana kwa yeye kuwa ameanguka kwenye
ngazi aliongea Felicity na mimi nilikosa namna ya
kumtetea tena Nancy, ilikuwa wazi kuwa yeye
ndiye aliyehusika.
Kwahiyo unataka tuliweke vipi hili jambo,
uchunguzi wote nimeufanya kwa siri bila
kushirikisha ofisi hivyo nasubiri uniambie nini cha
kufanya Felicity aliniweka katika wakati mgumu
sana wa kufanya maamuzi.
Naomba tuongee nje Felly nilijivuta pale na
kufungwa taulo langu vizuri kisha nilitoka nje na
Felly nae alitoka.
Tushughulike na hili swala nje ya ofisi yako,
unajua dhahiri kujaribu kuua ni kosa kubwa sana,
nipe muda niongee na Nancy juu ya hili, sitakuwa
tayari kumuona Nancy akienda jela Felly niliongea
na Felly huku machozi yakinitoka. Nilifahamu kuwa
nilimuumiza sana Nancy kwa kumwambia kuwa
nisingeweza tena kuwa na yeye kwakuwa
nilimpenda sana Patrick, mimi na Nancy
tulipendana sana na naelewa kuwa alifanya vile
kwakuwa hakuwa tayari kunipoteza. Nancy alikuwa
mtu mzuri sana na mpaka kufikia kufanya vile
inaonyesha kiasi gani alishindwa kuvumilia
maumivu ya nilichomwambia, hivyo huo ulikuwa
muda wangu wa kumfanya aachane na anachotaka
kukifanya.
****
Kazi kubwa niliyokuwa nayo ilikuwa kumueleza
Patrick ukweli wa kila jambo, nilimkwepa sana
lakini kila mara aliponitazama usoni niliona kabisa
deni nililokuwa nalo kwake na sasa niliona ipo haja
ya kumuambia ukweli.
Patrick nadhani sasa ni wakati muafaka wa
kukueleza kila kitu kuhusu mimi na pia kuhusu
Nancy nilimwambia huku nikitazama chini kwa
aibu.
Am listening(nakusikiliza) alinijibu na kukaa
sawa akinitazama, nilianza kumueleza historia
yangu yote ya kipindi cha nyuma toka udogo
wangu ila nilipofika kwenye kuelezea kuhusu mimi
na Nancy nilisita kwanza nilijiuliza Patrick
atanichukuliaje.
Nancy ni nani na kwanini atake kuniua aliniuliza
huku akiwa amenishika mikono yangu kama ishara
ya upole.
Baada ya hayo yote kunitokea, niliwachukia sana
wanaume, sikuwa na hisia na wanaume. Mbali na
dokta Anderson kujitahidi kunisihi nisahau kila kitu
lakini haikuwa rahisi, hivyo nikiwa kazini kama
daktari kipindi cha mwanzoni, alikuja mgonjwa
aliyekuwa na ugonjwa wa kutokwa na damu
mfululizo, nilitakiwa kumfanyia uchunguzi lakini
nilikuja kugundua kuna dawa alikuwa akimeza
ndizo zilimletea tatizo hilo, hivyo nikalazimika
kumpangia kliniki ili kumpa ushauri nasaha na
kumfanya aachane na zile dawa, nikiwa kwenye
kliniki siku moja yule mgonjwa alikuja na tulikuwa
tumejifungia ofisini kwangu akawa amelala
kitandani kavua nguo zote ili nimfanyie uchunguzi,
alinishika mkono wangu na kuupeleka kwenye uke
wake akawa kama ananisugulia, nilipata msisimko
wa ajabu na siku hiyo ndipo niligundua kuwa
nilikuwa na hisia na mwanamke mwenzangu,
sikuipenda ile tabia lakini taratibu nilizoea na hati
maye nilimfanya yule Mgonjwa kuwa mpenzi
wangu, na ndiye huyu Nancy, nilimpenda sana na
nlijitoa kwake, nikilala kwake na yeye akilala
kwangu na kufanya mambo yote kama wapenzi,
malengo yetu ya yalikuwa motomoto na wote
tulijaliana katika kila hali, siku zote Nancy alikuwa
akinipenda na kuvutiwa na mwili wangu, vivyo hivyo na mimi nilimpenda sana na nilivutiwa na kili
kilichokuwa katika mwili wake nilivuta pumzi kidogo na kumtazama Patrick aliyekuwa ametoa macho kama vile anaota;
hali ilikuja kuwa tofauti wewe ulipoletwa pale hospitali, haswa pale Mary alipokuacha na kuondoka zake, nilikuwa nikikuhudumia kwa karibu sana na sikuwa na mtu mwingine wa kumwangalia kwa ukaribu bali wewe tu, nilianza kukupenda taratibu na hisia zangu juu ya Nancy zilianza kupotea na nilianza kumkwepa, nilikuwa nataka kuanza maisha mapya hasa kwakuwa kupitia wewe niliona Tumaini jipya tena hapo hisia juu ya wanawake wenzangu zilikatika kwakuwa haikuwa utamaduni wangu, nilifahamu kuwa nilichokifanya kilikuwa ni kosa hata mbele za mungu lakini sikuwa nikifikiria sawia, hivyo nilitaka kulibadilisha
hilo kwa kuanza tena upya kila kile nilichokuwa nikikiamini, hivyo siku moja asubuhi nilimuita Nancy nyumbani kwangu na hapo nilikuwa na nia ya kumueleza kubadilisha kwangu mawazo juu ya hisia zangu kwake
******
Ilikuwa majira ya saa nne asubuhi nikiwa najiandaa kwenda kazini, jana yake nilikuwa nimempigia simu Nancy kuwa ningetaka kuongea nae na hapo ilikuwa ni wiki mbili toka mara ya mwisho nilipoonana nae. Wakati niko chumbani nikipaka mafuta mlango ulifunguliwa na Nancy aliingia moja kwa moja bila ya kupiga hodi, alianza kunishikashika na kunibusu kila sehemu huku mikono yake akiipitisha kwenye sehemu zangu za siri, sikuwa na hamu ya kufanya alichotaka lakini kwakuwa nilikuwa ninatafuta njia rahisi ya kumuambia ili anielewa nilijilazimisha na kuanza kumshikashika na yeye, tulianza kufanya tulichokuwa tukikifanya na baada ya kumaliza tulikwenda kuoga na baada ya hapo, Nancy alichukua nguo yangu ya ndani na kuanza kunivalisha, ndipo nilipomshika mkono nakumuomba tuongee.
Kuna kitu nataka kukuambia Nancy nilimvuta na kumkalisha chini wakati huo wote tukiwa watupu, alipandisha miguu yake kitandani na kuweka kichwa chake kwenye mapaja yangu na kunitazama.
Nancy kwenye maisha kuna muda kila mtu
hufanya mambo fulani kwasababu, kila mtu hujikuta katika mkondo mbovu kwasababu tu alitaka mwenyewe au maisha yalimchagulia namna ya kuishi, lakini hayo yote huwa ni matokeo ya bahati mbaya ambayo kuna muda kwa uzembe wetu au kwa kuyaamini yale tusiyoyasimamia tunajikuta tukiyatenda yasiyo mema, nimegundua nilipojikwaa Nancy na ninataka nirudi nyuma nianze upya, sifurahishwi tena na mahusiano tuliyonayo kwani huu sio utamaduni wa mwanamke, hisia zangu kwako zimeyeyuka mfano wa theluji ichemshwayo, nakupenda lakini sitaki tena tuendelee hivi alinyanyuka baada ya kusikia maneno yale na kuamua kukaa huku akilia.
haiwezekani mpenzi, siku zote tumekuwa pamoja leo hii unataka uniache kwa kusingizia huna hisia na mimi? Niambie ni nini unataka nikufanyie,unataka nini mpenzi wangu na mimi nitafanya,niambie tafadhali Nancy aliongea huku akilia kama mtoto, nilimuonea huruma sana lakini huo ulikuwa msimamo wangu na nilikuwa tayari kuusimamia mda wowote.
sitaki chochote Nancy, umekuwa mtu mzuri sana kwangu na umenionyesha mapenzi ya kweli na mimi nashukuru sana kwa hilo lakini kwasasa yupo ambaye inanibidi niwe naye nilimueleza kwakujikaza lakini huo ndio ulikuwa ukweli wangu.
ni nani huyo aliuliza.
ni Patrick, yule mgonjwa ninayemuhudumia pale hospitali.
yani unaniacha kisa yule mfu? Nini kimekupata Pamela,,eehh, unahitajika kupumzisha akili mpenzi,yani yule mtu amekaa miaka na miaka hajaamika,mtu anayetegemea kufa muda wowote ndo akuchanganye kisi hicho kweli? kabla hajamaliza kuongea tayari alikuwa ameshanichefua kumuita Patrick mfu.
ishia hapohapo Nancy, vaa nguo zako ondoka sitaki kukuona, nampenda sana huyo unayemuita mfu, hivyo nakuomba wewe uondoke hapa
nilimsukuma na kuchukua nguo zangu kisha nilikwenda kuvalia nguo sebuleni.
Pamela naomba unisamehe sikuwa na maana ya kukuudhi mpenzi wangu, naomba unielewe
alinifata huku akinishika na kujaribu kunituliza.
Nimekuelewa Nancy ila mimi na wewe basi, sitaki tena usagaji, siko tayari tena na nina uhakika kama wazazi wangu wangekuwa hai wangeniua kwa hili, nampenda Patrick huo ndio ukweli mpya ambao inabidi mimi na wewe tuwe nao kichwani na tujue kuwa mambo yameishia hapo nilimuambia hivyo na kuondoka pale sebuleni nikamuacha akilia, nilichukua vitu vyangu na nilipofika pale sebuleni nilisimama na kumtazama.
Nancy hakuna jinsi inabidi ukubaliane na hilo nililokuambia kwakuwa hakuna suluhu zaidi ya wewe kukubali, tafadhali nyanyuka tuondoke nataka nifunge nyumba yangu. Hapo ndo ilikuwa mwisho wa mapenzi yangu na Nancy.
***********
Yalikuwa matarajio yangu kuwa Patrick angekuwa mkali na pengine angeweza hata kutaka kuondoka na kuniacha lakini hali ilikuwa tofauti kabisa,baada ya kumueleza ukweli wa kila jambo Patrick alinivuta na kunikumbatia.
usijali kila mtu anahistoria mbaya katika maisha yake, lakini ikitokea ukajua unapokosea na kuamua kujirudi na kujirekebisha basi hiyo ni faraja ndani ya moyo wa kila mmoja aliyechukizwa na tabia yako ya awali, hivyo usiwe na hofu, nenda kanisani katubu zambi zako na mungu atakusaidia, ila ipo haja ya kuongea taratibu na Nancy, na mimi ndiye nitakwenda kuongea nae nilishtuka kwakuwa sikutegemea awe mpole kiasi kile lakini kilichonichaosha ni pale aliposema kuwa anataka kuongea na Nancy.
**SIKU MBILI MBELE**
Jioni tukiwa tumetoka matembezini Felicity alinipigia simu na kunitaarifu kuwa alikuwa ameshakamilisha uchunguzi kuhusu ajali aliyoipata Patrick miaka zaidi ya sita iliyopita, hivyo aliniambia twende mimi na Patrick nyumbani kwake kwakuwa ndiko kuna vifaa anavyoweza kutumia kutuelezea.
Tuliondoka hadi kwa Felicity na tulipofika kwake alitukaribisha kisha tukakaa kwa muda kidogo wakati yeye akiwa ndani na baadaye alituchukua na kutupeleka kwenye chumba fulani kama darasa dogo kisha aliwasha kompyuta kubwa iliyokuwaukutani na kama kawaida yake alianza kuelezea.
nilianzankufanya uchunguzi juu ya ile ajali kwa kufatilia wale trafiki waliokuwa wakifatilia ile kesi,sikuile wakati ile ajali inatokea inaonekana njiani kulikuwa na ile gari iliyosababisha ajali kwa zaidi ya masaa mawili ikifanya doria njia ile, mazingira ya ajali yanaonyesha kuwa ile ilikuwa ajali ya kupangwa, swali ni je nani alipanga ajali hiyo? Na majibu ni kwamba, toka Patrick aje huku kulikuwa na mawasiliano yakifanyika kwenye mgahawa wa Roshan uliopo chini ya hoteli aliyofikia,mawasiliano hayo yalikuwa yakifanywa kati ya mtu anayeitwa George mwenye namba yenye code namba +255 ambayo ni ya nchini Tanzania na Mary ambaye ndiye mkeo uliyekuwa naye.Mawasiliano hayo ambayo tumefanikiwa kuyapata yalikuwa yakifanyika kila siku kati ya saa 9:45 na10:34 usiku. Mawasiliano hayo yalikuwa ya aina nyingi, kuna siku walifanya mawasiliano ya simu na kuna kipindi waliwasiliana kupitia barua pepe.Maongezi hayakuwa wazi kwakuwa walikuwa wakiongea katika lugha ambayo waliijua wao wenyewe, lakini tulichofanikiwa kukijua ni kwamba mawasiliano haya kila mara yalitaja kampuni iitwayo PATRIMARY, na pia kuna barua pepe moja ilikuwa ikiuliza aina ya jina jipya ambalo lingefaa kuwa mbadala wa lile la mwanzo, na katika majibu ya Mary pamoja na mambo mengi anamtaarifu George kuwa jina mbadala ni GEOMARY. Baada ya siku tatu toka wafanye mawasiliano hayo, George alituma ujumbe kwenye simu ya Mary akimtaarifu kuwa tayari ameshafanikiwa kubadilisha na akamwambia sasa anaweza kuingia kwenye tovuti ya
www.geomary.co.tz kuangalia kama mambo yote yalikuwa sawa, tulichogundua ni kwamba wakati huu walikuwa wakiandaa tovuti kwaajili ya kazi waliyokuwa waifanye baadaye. Siku ya tukio la ajali magazeti ya nchini Tanzania yaliripoti juu ya ajali ile na waliambiwa kuwa hali ilikuwa mbaya
sana, lakini baada ya Mary kuondoka huku na alipofika Tanzania aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kuelezea kuwa mumewe alifariki na
kupotelea baharini wakati wakiwa wanamuhamisha kutoka Fiji kwenda Suva ambapo ndege yao ilipata
ajali na kuangukia baharini ila yeye Mary alipona.Waandishi walilipwa ili kuandika habari hiyo na baada ya wiki mtu anayeitwa wakili Mrutu
aliwasilisha maombi mahakamani akiiomba
mahakama ipokee wosia wa marehemu yaani
Patrick alioandika na kuuweka kwa huyo
mwanasheria juu ya nani amiliki mali za
marehemu. Wosia uliwataja watu wawili tu ambao ni Mary na George, na baada ya mahakama kupokea waliamuru wahusika wapewe mali zile.Majina ya kampuni na mali nyingine yalibadilishwa,na cha kushangaza miezi 9 mbele Mary alijifungua,upelelezi unaonyesha George alifunga ndoa na Mary miezi michache baadaye, hii inamaana kuwa
mimba hii Mary aliipata siku alivyokuwa ameshukaTanzania.
unasemaje? Mimba? nilimuona Patrick akishtuka kwa kuhamaki.
NINI SABABU YA YOTE HAYAAAA???.........JE UPI
MWISHO WA PATRICK NA PAMELA?
KWANINI FELICITY ANAJITOLEA SANA KUFANYA
KAZI HII KWA PAMELA??
FATILIA SEHEMU ITAKAYOFUATA