RIWAYA: Kikosi cha Pili

RIWAYA: Kikosi cha Pili

Sehemu ya 18*

Hata ungelibahatika kumuona ungelijua kabisa anapata tabu kufikiria namna ya kuukwea ukuta ule mrefu wa jumba la Papaa Deo Mukamba.
Koplo makame akasema na peke yake.
"Tutumie mbinu nyingine"
Akasikiliza kidogo kisha akahama eneo alilokuwa akaambaa na ukuta mrefu akafika nyuma ya kasiri lile,huko akakutana na koplo Ziga wakateta kidogo kisha kwa wepesi wa kustukiza Ziga akawa mabegani mwa Makame,na kitendo kilichofuatia ni koplo Ziga kutua taratibu ndani ya jumba lile la kifahari,akajipa utulivu wa kuyasoma mazingira.
Akakutana na miti mizuri ya maua iliokuwa imesimama mithili ya miti ya Azuni,akautazama mlango wa mbele wa jumba lile,hapo akaona walinzi wawili wakiwa wamesimama wima,upande wa kushoto mwake kulikuwa na magari kadhaa ya kifahari,akatazama kuuzunguka ukuta ule hapo akakutana na taa kali zilizokuwa zikimulika uwanja mzima,ina maana hakuna kitu ambacho kingekakatiza mbele bila kuonekana na walinzi,lakini pia nyuma ya kila taa kulikuwa na kamera ndogo.
Akajivuta kwa hatua za mtu anaeogopa kukanyaga moto.
Hatua ya kwanza,ya pili,akajikuta akitoa tusi kubwa la nguoni huku mguu mmoja ukiwa umebaki hewani bila kutua kumalizia hatua ya tatu,akaurudisha mguu ule hivyo akawa amebaki na hatua zilezile mbili.
Zilikuwa ni nyaya ndogo zilizokuwa zimetawanywa chini, nyaya hizi zilitumika kutoa tahadhari ndani kama zingeguswa na kiumbe yoyote.
Akaangaza kwa macho ya paka hapo akaona upande mwingine kukiwa na mitego kadhaa ya kunasia miguu au kiumbe ambae angeligusa pale,akatabasamu kisha akatoa vibati kadhaa kutoka mifukoni kwake,akatupia kimoja kwenye mtego ukafyatuka nae akarukia hapo hapo.

Akafika hadi karibu na dirisha kubwa akatazama ndani akaona watu watatu wakiwa wamezunguka meza wakizungumza,akafungua kioo kile polepole akawa anapiga hesabu za kuingia ndani kabla hakafanya hivyo akamwona mtu aliemfahamu.
Akaduwaa kwa sekunde kadhaa na akapoteza umakini kwa kumshangaa mtu yule,akiwa hivyo ametulia akawashuhudia watu wale wakisimama na kuondoka mle ndani akanong'ona kidogo kisha akatumia utalamu mdogo kioo kile kikaachia akazama ndani ya jumba lile huku kwa nje akisikia miungurumo ya gari kuashiria gari zilikuwa zikiondoka eneo lile.

Koplo Makame alipokea taarifa kutoka kwa koplo Ziga,punde akaona gari mbili za kifahari zikitoka pale,akapiga hesabu za kijeshi akaona umbali uliopo kati yake na usafiri wao uliowaleta Goma upo mbali,hivyo asingeliweza kuwahi gari zile akajipapasa akatoa kidude kidogo mfano wa betri ya saa kwa wepesi wa ajabu akakirusha kikaenda kukita nyuma ya gari moja wapo,kisha akageuka na kurudi kuendelea na harakati zake.

Ziga alinyata hadi karibu na korido ya kulia chakula,hapo akatulia kuyasoma mazingira ya nyumba ile,hakukawia kuziona ngazi zilizokuwa zikipandisha juu,pia upande wake wa mbele akaiona sebule pana iliopambwa kwa samani za kisasa,akajivuta baada ya kuhakikisha hakuna mtu kwenye sebule ile.

Wakati akikaribia kuifikia sebule ile akazisikia hatua za mtu akija kwa kasi akiwa anatokea kwenye vyumba vilivyojuu,akasimama punde akamwona mwanajeshi wa wa jeshi la Kongo akiifikia sebule ile na kuchukua kitu kwa haraka na kurudi juu haraka,hapo akagundua kuna watu upande huo.

Akaifikia sebule ile na kunyata akaziendea ngazi kwa hatua za haraka na bila kelele,akajikuta akikutana na uwazi mpana huku mbele yake kukiwa na milango mitatu iliopangana,akaisogelea milango ile ni wakati akitaka kujipa umakini wa kama wa popo akasikia nyuma yake.
"freezee"
Hakutaka kusubiri akaruka pembeni ni kama alijua alipotoka tu zikafuatia risasi tatu na zilipomkosa zikapiga mlango na mmoja wapo na kuwastua waliomo.

Ziga kwa wepesi ule ule akarusha kisu chake kikatua kichwani kwa mtu yule alietoka nyuma yake,alipogeuka nyuma akaona mlango ukifunguliwa na kutoka wanajeshi watatu wakiwa na silaha zao mikononi.
Akabiringita chini na kuzikwepa risasi kadhaa zilizovurumishwa na wanajeshi wale hakutaka kuwa mzembe akawahi kuipiga taa iliokuwa ikitoa mwanga ikazima kukabaki kiza ndani ya korido ile,na kwa kutumia tumbo akaanza kutambaa kisogea pembeni kulikokuwa na milango mingine.
Akiwa katika harakati hizo koplo ziga akajikuta akiguswa na kitu cha baridi upande wake wa kulia kisha akaamuliwa kusimama,ni wakati akisimama kukawaka taa za dharura mle ndani hapo akakutana na midomo minne ya bastola ikimtazama

Asalaaam Kudo
 
[HASHTAG]#xutyo[/HASHTAG] xutyani,maxmizer,Tumosa,moneytalk,kiahjr23,user2008,Augostino87,shaban lee,i keep ma promise,madame s,kiker,swahiba92,[HASHTAG]#kigongoi[/HASHTAG],bright platnumz,sirbuf,wolf man,kichwa kikubwa,donlucchese,songa kheri,Black coffee#
 
Kidadadeki hii kazi ilitakiwa iuzwe Hollywood watu wafanye movie
 
Sehemu ya 19*

Ziga akanyang'anywa silaha aliokuwa nayo na mmoja kati ya wale wanajeshi wanne,akaamuliwa kutangulia mbele huku akiwa kanyoosha mikono juu nae akatii.
Kwa mwendo wa mateka akaanza kupiga hatua kuzifuata ngazi zilizokuwa zikiteremka chini kwenye sebule ya nyumba ile.

Koplo Ziga maisha yake yote furaha yake ni kuona akiingia mikononi mwa adui kisha atumie maarifa kuwatoka huku akiamini zaidi mikono na miguu yake katika mapambano.
Kadri alivyokuwa akipiga hatua kuzishuka ngazi alikuwa anapiga hesabu za kufanya lolote.Aliamini adui yake hawezi kumuua kwa sababu watataka kujua yeye ni nani.

Alibakisha ngazi tatu kuikanyaga sebule pana iliozungukwa na samani za kisasa huku kukiwa na utulivu wa hali ya juu,ukimya ule aliutumia vyema koplo Ziga akatega sikio na kizisikia hatua za watu walioko nyuma katika utembeaji wao.
Akakanyaga hatua kama anasita akaweka utulivu kichwani pake akazisikia hatua za walioko nyuma yake zikakanyaga kwa pupa hapo akapata jawabu ya kuwa watu hao hawako katika umakini ila wanawahi kufamfanyia jambo.

Wakati akitafakari kwa muda huo akasukumwa na mtu aliekuwa karibu yake,alilitegemea hilo akajirusha kutoka pale alipokuwa akadondokea kwenye zulia na kwa haraka akasimama na kunyoosha mikono juu huku akiwatizama watekaji wake wakiwa wamesimama imara na mitutu mikononi.

Mmoja kati ya watekaji wale akapiga hatua na kumfuata akamtazama machoni kisha akamuuliza kwa lugha ya kingereza cha kuhangaika

"Who are you"
Ziga hakujibu nae akauliza

"Who is Papaa "

Wanajeshi wale wakatazamana kisha wakasemezana kwa lugha ya kilingala punde wakamzunguka wote na kuendelea kumuuliza mwaswali ambayo hayakujibiwa na koplo Ziga.
Kuona vile wakasemezana tena kwa kilingala,hapo Ziga akajua wanataka kuumaliza mchezo na yeye hapaswi kupoteza Muda,
Akakohoa kidogo na kikohozi chake hakikwenda bure akaona alie nyuma yake ndie hatari zaidi kuliko walioko mbele alipokohoa tu kikafuata kitendo cha kuruka sarakasi ya nyuma huku mikono ikifanya egemeo kwenye mabega ya mwanajeshi alienyuma yake,alipotua chini mwanajeshi yule tayari alikuwa ngao yake na kitendo bila kuchelewa akampiga pigo dhaifu kwa kutumia ubapa wa kiganja chake nyuma ya shingo lengo ni kumzimisha kwa muda kidogo kitendo hiki hakikuchukua hata dakika moja.
Wale watatu wakashindwa cha kufanya wakipiga risasi watamuua mwenzao wakaanza kucheza pata potea nae Ziga akaliona hilo kwa kutumia mtu aliemweka mbele akataka kumfanya silaha yake akampiga nyuma ya magoti bwana yule akawa kama anataka kujiandaa kukimbia,Ziga akaruka na kumpita juu kisha akiwa hewani akatawanya miguu yake teke moja likampata mmoja na kumdondosha chini na teke lingine likamkosa mmoja wake na kumfanya akose mhimili wa kusimama baada ya kulikwepa teke la Ziga.

Ziga hakutaka kupoteza muda akatumia uzoefu wake katika medani za kivita na ndani ya dakika tatu akawa anamalizia kuivunja shingo ya mmoja wa wanajeshi wale kisha akasimama na kuwatazama akajisemea


"sory soldier!"kisha akaweka kidole sikioni pake akasema tena

"All clear" bila kusubiri jibu akanwendea yule mtu aliemzimisha akampigapiga usoni akaona itamchukua muda kuamuka akajipapasa akatoka na kichupa kidogo mithili ya dawa ya mafua au vikiskingo kabla hajakifungua akasikia mlango wa hapo sebuleni ukifunguka akaruka pembeni kutazama vizuri alikuwa ni koplo Makame,Ziga akasimama akajitokeza akampa koplo makame kile kichupa kisha akanena,

"Napanda juu mtemeshe huyo bwege"

"Copied"
Ndani ya muda mfupi Ziga alikuwa akipotelea juu ya ngazi za nyumba ile,huko hakukaa sana punde akatoka na mikaratasi kadhaa mkononi mwake akamfikia Makame wakateta.

"Lolote?"

"Nimemhoji kanambia Papaa Deo Mukamba anakikao Ashton Hotel usiku huu,zaidi ya hapo inaonekana hajui lolote na hapa anadai walikuwepo kwa ulinzi wa nyumba hii"

"OK soldier hana thamani huyu kuku"
Ziga akanyanyau bastola yake na kumwagia risasi kadhaa bwana yule na wakaanza safari huku wakipanga kwenda kumtafuta yule mtu kutoka tanzania alieonekana usiku ule kwa kufuata maelekezo ya saa ya Makame iliokuwa ikisoma mwenendo wa kifaa alichokirusha kwenye magari yaliokuwa na mtu yule.

****



.
Asalaam Kudo.




Nb:Ndugu zangu wa kule kwa Uhuru tukutane JamiiForums.com,pia nashukuru kwa mwitikio wenu japo mpo wachache lakini mnaspoti kuliko hata hapa kwetu endeleeni na moyo huohuo sisi sote ni wamoja.

Hapa kwetu bado naihitaji sapoti yenu kwa hali na mali japo mwitikio ni mdogo ila mungu ataweka mkono wake.
Mwenye kusapoti tuwasiliane kwa no hizi.
0758573660
0658564341.
 
mkuu siku ya3 sasa bado umeme haujarudi, nambie ni mtaa gani na wilaya na mkoa?? nafanya kazi Tanesco.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom