Sehemu ya 23*
Meja Salim komba aliwasha gari yake na kuingia barabarani,alitaka kukutana na Zedi chalinze bar kama kawaida yao ili amshirikishe katika jambo alilodokezwa na makomando walioko nchini Kongo kinyume cha taratibu.
Akakanyaga mafuta na kuzidi kuiacha Msata,lakini kitu ambacho hakujua ni kuwa wakati anaondoka nyumbani kwake kuna mtu alikuwa akimtizama,na kuondoka kwake machoni mwa mtu yule nae akapiga simu anakokujua kutoa taarifa ya kuonekana kwa meja kuifunga safari kusiko julikana.
****
Ibra mbaya ndie aliepokea simu yenye taarifa za nyendo za Meja Salim komba,akatabasamu kidogo na kujipa tafakari kidogo
"Baada ya miaka mingi hatimae leo naenda kukutana na mbaya wangu,atashangaa kuniona mbwa yule,na kama alidhani nimekufa au kuzeeka basi leo nitamwonesha mimi huwa sifi kizembe na..."
Ibra hakumalizia kauli yake akasikia tusi zito likimtoka dereva wa gari lao aliekuwa akijaribu kuliweka sawa gari baada ya kupitwa na gari flani kwa kasi ya ajabu.
Ibra mbaya alipojua kisa cha dereva wao kutukana akaamuru dereva alifukuze gari lile na alipite au amsimashe wazungumze kwanini anaendesha usiku kwa mwendo ule,dereva nae akatii ukawa mfukuzano wa magari mawili ya mahisimu ambao hawakujuana wakati huo.
Meja Salim komba ndie alikuwa wa kwanza kufika pale bar,akapaki gari lake na kushuka kisha akaangaza kushoto na kulia hakuona mtu akachepuka kidogo na kulisogelea gari lingine na kufungua mlango kisha kukaa ndani ya gari lile huku mawazo yakipita kichwani pake.
***
Zedi alipolipita gari lile hakuwa na Shaka nalo,lakini kadri muda ulivyokuwa unazidi kusogea ndivyo alivyohisi tofauti hasa pale gari lile lilipoanza kumfuata nyuma kwa kasi mara kwa mara dereva wa gari lile akimulika taa kumpa ishara zedi asimame.
Ili kujiridhisha na hisia zake akapunguza mwendo wa gari lake na kuwa kama anaetaka kusimama,na kabla hajatimiza azma yake akavaa mawani zilizomsaidia kuona kizani hata nyuma ya kioo kisha akasimama.
Wakati gari lile lilipokuwa likimpita kwa mbele ili lisimame alipata kuona watu watatu wakiwa wamekaa viti vya nyuma huku mmoja Kati yao akiwa na bastola mkononi na hapo akajiwa na hisia mbaya zaidi.
Baada ya gari lile kusimama,tofauti na matarajio yao Zedi yeye akiingia barabarani na kukanya mafuta hadi mwisho na kufanya kina Ibra wasipate tena kumuona japo walijitahidi kumfukuzia lengo wamtie adabu mtu yule,ila ni kwa kuwa hawakujua adui yao ndie walie mwacha awatangulie kufika kwa Meja Salim komba.
Meja Salim komba alimwona zedi wakati akipaki,akampa ishara ya kijasusi,nae akapaki pembeni na kuchepuka kuingia ndani ya gari lile alilokuwako Meja.
***
Walitazamana kisha Meja akasema
"wako wapi wageni wangu uliosema upo nao?"
Zedi hakujibu kitu akageuka na kutizama nyuma,jambo lile likamfanya Meja nae ageuke na hapo akashuhudia wanaume wanne wakiteremka haraka haraka ndani ya gari lao na kuliendea gari la Zedi na kuanza kulilagua.
Meja Salim hakuwa anawajua watu wale ila alijua ni watu wa kazi,pia hakujua kwanini wanajiamini vile lakini majibu aliyapata baada ya mmoja wa watu wale kuvua kofia kwa minajili ya kujikuna kichwa.
Alimanusura Meja salimu komba augue kifafa baada ya kumtambua mtu yule kwa msaada wa taa za nje ya bar ile na akajikuta akitamka taratibu kwa mzubao
"Ibra Mbaya"
Baada ya kutajwa jina hilo tu Zedi nae akageuka kutazama nae mwili ukamfa ganzi kwa sekunde kadhaa..
***
Nb:karibu kwenye kundi la riwaya la whatsapp kwa malipo ya Tsh 2500/=
Karibu usome riwaya ya KISA CHA WAFU riwaya ya kipelelezi na mambo ya dunia ya pili,karibu usome elimu ya Tafakari(meditation)ndani ya riwaya hii.
Karibu usome riwaya ya UTATA na nyinginezo namba kwa ajili ya whatsapp
0658564341
Kwa malipo ni 0758573660
Asalaam Kudo