RIWAYA: Kikosi cha Pili

RIWAYA: Kikosi cha Pili

Sehemu ya 20*


Zagamba akaona bora afe kuliko kusubiri kuuawa na mtu kama kepteni Zegera,alimjua nje ndani bwana yule alivyokatili akaona hana la kujitetea mbele yake,atamwambia nini ikiwa mvamizi mwenyewe alikuwa ni mmoja tu na wao walikuwa watatu fadhaa ikamkumba.

Alimtazama Zedi anavyoondoka katika nyumba ile,akaonelea bora afanye kitu ili amshawishi mwamaume mwenzake amtoe uhai katika utaritibu pasipo maumivu kuliko kutolewa uhai kwa maumivu makubwa.
Kwa taabu akaipata sauti yake nayo ikamfikia Zedi,Zedi akageuka.

"umenipiga nakubali,ukaona haitoshi ukanivunja uti wa mgongo,hata nisipokwambia ninachokijua itakuwa kazi bure maana sintoweza kujitetea kwa lolote"

Zedi akamtazama akavutiwa na maneno ya Zagamba,jambazi maarufu katika vyombo vya dola,anatafutwa kwa garama kama shilingi ya kale.
Zedi akaacha hatua zake zimfikie mhalifu yule pale chini,alipomfikia akamwinamia nae akaipata sauti yake katika utulivu wa mume kuomba unyumba kwa mkewe.

"waeza zungumza sasa nami nitakusaidia!"

"Namfahamu Zegera ni mtu anaetumia vibaya vazi lake la taifa,amekuwa akinitumia katika matukio mengi ya uhalifu,anahusika na Ibrahim wa dawa za kulevya,lakini kubwa zaidi hivi sasa anampango tikisa na kuna mtu alinikutanisha nae anaitwa Ibra Mbaya....."

"Hebu ngoja we unamjua vizuri Ibra au umetamka tu hilo jina!"

"Namfahamu nimekutana nae juzi na kesho alinambia atanipangia kazi ambayo sikuijua.
Mwonekano wake ni mrefu sawa na wewe ni mpole anapozungumza ila ni hatari na maamuzi magumu,jana to ameua mtu mbele yangu baada ya kukosea mpango fulani na hivi sasa yupo mahali anafanya jambo pamoja Zegera".

"unahisi wanafanya nini huko waliko?"

"Siwezi jua ila nahisi wapo bandarini na...... "

Zagamba hakumaliza kauli yake risasi ikatua kichwani pake na kuutawanya ubongo wake huku na huko na mwingine ukamrukia Zedi mwilini kwake.
Zedi hakuwa amempiga risasi Zagamba alishangaa risasi ilipotokea nae hakungoja akaruka upande mwingine na kuiweka sawa silaha yake lakini wakati akiijaribu bahati yake akashangaa risasi nyingine ikizipasua taa zilizokuwa zikiwaka subuleni pale.

Zedi akiwa anapambana na giza akasikia mdondoko wa kitu kama paka,wakati akijiuliza na kupambana na kulizoe giza la gafla kutoka pale alipo kwa mbali aliona kama mtu akinyata na kusogea mahali kulipokuwa na meza kisha akaruka na kulikumba dirisha la kioo na kutokomea kusiko julikana.

Zedi akaliona tukio lile akajiuliza pale mtu yule alifuata nini,hapo akakumbuka hata yeye aliona kitu pale ila hakukitilia maanani Sana,hapo akajikuta akitukana tusi zito la nguoni na kunyanyuka alipokuwa baada ya kuhisi usalama eneo lile na lengo lake ni kuwahi huko bandarini usiku huo.

Nusu saa nyuma...

Zegera alikuwa kimya ndani ya gari lake alikuwa akiiacha moroko ili aikamate kawe,huko alikuwa na miadi ya kukutana na mkurugenzai wa bandari ambapo angemchukua na kufanya nae mazungumzo kisha yeye angelienda bandarini ili kufanya hila mizigo yao iwahi kutoka lakini alikumbuka jambo.
Katika mpango tikisa huwa anahifadhi kila kitu kwenye kihifadhi kumbukumbu au kwa lugha rahisi kwa wengi Flash,na hata wakati huo alipaswa kuwa nayo ili achukue baadhi ya mambo ya muhimu kwa mkurugenzi wa bandari,akajipapasa hakuwa nayo,akapaki pembeni na kukagua gari ila hakuambulia kitu.

Kumbukumbu zake zikamwambia aliiaahau nyumbani kwake mezani na alipaswa kuifuata,ila muda haukuwa rafiki,hapo akaamua jambo,akanyanyua simu yake na kupiga

"Yes!!"

"Nenda kwangu kunamzigo upo mezani niletee kawe"

"sawa mkuu"

"ila yupo Zagamba"

'"Hapana Shaka mkuu"

"Dula fanya chapu"

"ok"

Dula hakutaka kuchelewa akajipaki ajuavyo na begi lake mgongoni akachukua pikipiki yake na kuingia barabarani.
Haikuchukua muda akawa yupo nje ya geti la nyumba ya Zegera,akataka kupiga honi afunguliwe,akasita baada ya kuona mlango mdogo ukiwa wazi,akajua kuna la zaidi hapo ndani.
Aliingiwa na hisia za jambo baya maana hakuwa mgeni katika kazi ya ushushushu,akaona asijipe tabu,anajua njia mbadala ya kuingilia pale ndani akazunguka nyuma ya nyumba ile akaangaza kushoto na kulia hakuona kitu akasimama katikati ya barabara hapo akatazamana na bampa la kuzibia mifereji ya maji machafu,akatumia nguvu kidogo akabetua bampa lile kisha akazama ndani.
Haikuwa njia ya maji machafu ila ni njia ya kuingilia au kutokea ndani ya nyumba ya kepteni zegera.
Ndani ya dakika chache akatokezea kwene chumba cha bwana zegera.
Wakati akipiga hatua ili afungue mlango akasikia miguno ya mtu aliekatika mateso,akaweka umakini zaidi na kwa kutumia utalaamu wa kijasusi akafungua mlango bila mtu kusikia hata yeye aliefungua hakusikia sauti yoyote kisha taratibu mwendo wa teja akasogea kutazama ilipo sebule,hakuamini macho yake akamwona mwanaume mrefu akiwa ameikamata vyema bastola yake huku akisikiliza maongezi flani kutoka kwa zagamba.

Alifikia maamuzi ya kumuua zagamba baada ya kuona Zagamba hana nguvu za kujiokoa hata kama yeye atakuwa kamsaidia kufanya hivyo,pia aliiona Flash ikiwa bado mezani hivyo hakuwa na namna ya kuichukua isipokuwa kucheza pata potea,akanyoosha mkono na kidole kikacheza risasi ikampata Zagamba na hapo akaona wepesi wa mtesaji yule alivyoruka kuikwepa risasi iliomlenga baada ya ile ya kwanza kumpata mhusika,l.
Dula akaona sio muda wa kujipima ubavu na kiumbe yule ila ni kuichukua flash na atamtafuta wakati mwingine kwa mchezo kama ule,na bila kupoteza muda akapiga taa ikazima kisha kwa wepesi wa moshi wa sigara akaruka na kutua kama paka na kupiga hesabu za kichwa namna ilivyokaa ile Flash mezani akaikwapua ilipojaa mkononi akatumia begi lake kulikumba dirisha la vioo na sekunde chache alikuwa nje ya nyumba ile akiipeleka flash kwa mwenyewe huku nyuma akimwacha Zedi akiwasha usafiri wake kuwahi bandarini ila ni kwa kuwa hakujua huko anapoteza atakutana na nini heri angelibakia kumtafuta Dula kwanza.


******



Nb:Maisha ni kusaidiana ukinisaidia leo niweze timiza malengo yangu huwezi jua kesho yetu Mimi na wewe itakwaje japo hatujuani.
Changia chochote ulichonacho,
Nawashukuru wale wanaochangia hadi sasa na mungu awabariki wewe ambae hujafanya hivyo hujachelewa ni Wakati wako sasa kuonesha sapoti kwa waandishi waliohai,
Usisubiri tukifa utoe pongezi kwenye mandiko yetu ikiwa hukutusapoti tukiwa hai.

0758573660
0658564341

Asalaam kudo.
 
Sehemu ya 21*

Zedi alikuwa akitembea kwa mguu kuikaribia bandari kuu ya Tanzania,alitazama upande wa kuingilia bandarini pale,akastaajabu kwa alichokiona.

Dakika kumi nyuma....

Dula baada ya kumtoroka Zedi,akaamua kumpigia simu kepten Zegera,akampasha habari ya uvamizi nyumbani kwake,kisha akakata simu na kuendelea na safari kumfuata Zegera Kawe ili ampe mzigo wake.

Kuvamiwa nyumbani kwake kisha kuelekezwa mwonekano wa mvamizi yule,hakuwa na mashaka kabisa ya mtu aliefanya vile zaidi ya Zedi Wimba.
Alimjua Zagamba nje ndani ila alipofikiria uwezo wa Zedi akatoa mawazo ya kumlaumu Zagamba kutepeta mbele ya kiumbe yule.

Alijua kama Zagamba alitamka neno bandari basi muda huo Zedi atakuwa njiani kuelekea bandarini,akaona maongezi yake na mkurugenzi hayafai kwa muda huo,akatoka nje akapiga simu mahali na kutoa maelekezo flani kisha akapanda gari na kuondoka mahali pale huku akimwelekeza Dula mahali pa kukutana na si kawe tena.
****
Wakati Zedi akizidi kulisogelea eneo la bandari,akashuhudia gari za jeshi zaidi ya kumi zikiingia pale kwa fujo,huku wanajeshi wakiruka kwa weledi wa hali ya juu kabla gari hazijasimama.

Zedi akashangaa inakwaje wanajeshi wavamie eneo lile kuna nini,hakupata majibu,si yeye tu aliejiuliza hata baadhi ya walinzi wanaolinda bandari ile hawakujua nini kinaendelea,punde akasikika sauti kutoka kwenye kipaza sauti ilioamuru walinzi wote wajisalimishe kutoka kwenye maeneo yao ni amri si ombi.

Walinzi wote wakasogea na silaha zao kisha wakaamriwa kila alipo mlinzi mmoja awepo na askari mmoja wa jeshi la wananchi,amri ikatekelezwa bila kupoteza Wakati.

Zedi akiwa kajibana pahali aliyashuhudia yote yale lakini aligundua kitu kwa kiongozi wa msafara ule,hakuwa kiongozi aliestahili kuongoza kundi lile la wanajeshi wengi vile,lakini pia hakuwa akitoa amri katika weledi wa kijeshi,kikubwa zaidi alikuwa na bastola ya rangi nyeupe,ambapo katika majeshi yote nchini hakuna silaha yenye mwonekano ule,akapiga hesabu za kiutu uzima na mwongozo wa sheria za kivita.

Pale alipokuwa kulikuwa na kontena kadhaa upande wake wa kulia na kiongozi yule alikuwa upande wa mbele wa kontena zile na kabla hujamfikia ilibidi uwapite askari watatu waliokuwa wakilinda upande ule.

Akanyata na kuvuka kipenyo flani akalifikia moja ya kontena zile,kama paka akadandia na kutua juu yake kisha akaanza kutambaa kama mamba,akafika hadi usawa wa mwisho wa kontena lile,na kwa wepesi wa mwewe kwa kifaranga cha kuku Zedi akatua kwenye gari moja wapo kisha akaruka na kutua chini bila kujiuliza akafyatuka kama mpira na kumzoa kiongozi yule na hakusubiri aanguke akamdaka na kumkaba kabari ya ngao kisha yeye akajiegemeza kwenye gari ili alienyuma yake asimfanyie shambulizi kisha akatulia kujipa ujatulivu namna ya kuwatoka wanajeshi wengi walioanza kujaa pale huku silaha zao zikiwa tayari kwa lolote.

Palepale alipokuwa akatoa mkono mmoja na kufungua mlango wa gari ya kijeshi kisha akatangulia kuingia ndani huku akimburuza bwana yule katika namna ya Simba aburuzavyo windo lake alipokwisha kujaa ndani ya gari ile akaitia moto,lakini akagundua jambo.
Mateka wake hakuwa na uhai akapigwa na mzubao si yeye alieshambulia wala kabali yake haikuwa ya kuua.
Akiwa katika tafakuri akasikia amri kutoka kwa mtu ambae hakumuona,punde zikafuatia risasi za moto kuliendea gari lile nae zedi akainama kidogo na kuliondoa kwa kasi akiwa na maiti na alipotazama vizuri mateka wake alikuwa na tundu la risasi kwenye paji la uso
Akajisemea
"Mdunguaji".....





Asalaam kudo.
 
Sehemu ya 22*


Moja ya taarifa mbaya kwa Ibra ni hii aliopokea akiwa kakaa kwenye kiti cha mbao huku akiwatizama vijana zaidi ya themanini wakicheza michezo ya judo chini ya usimamizi wake.

Hakupenda kuwa mbali na hekaheka katika maisha yake yote,na hapo akamtazama Deepaklipa akiwa pembeni akimtizama kwa woga.

Ibra Mbaya alimtazama juu mpaka chini Deepaklipa,akamtathomini katika umbo lake na uwezo wake anashindwaje kumaliza kazi katika muda muafaka.

Aliwaza kushindwa kwao kukamilisha mipango kunawarudisha nyuma kila siku,akaona hana sababu ya kuendelea kuwa mkufunzi katika kambi ya maficho huku harakati zikiwa zipo mikononi mwa wavivu.

Akasimama na kumwita kijana mmoja wapo katika wale anawaamini,kisha akamkabidhi madaraka ya kuisimamia kambi ile haramu.

Na bila kusema neno akamgeukia Deepaklipa na kumpa ishara amfuate na hilo likatekelezwa.

Alinyanyua simu yake na kupiga mahali kisha akasikiliza kidogo na kumpa Deepaklipa,nae akasikiliza kidogo na kumrudishia Ibra Mbaya.
Na baada ya kujiandaa wajuavyo wakapanda gari na kutokomea kuitafuta mjini Dar iliokuwa kilomita kumi tu kutoka walipokuwa kwa muda huo.

****
Kapteni Zegera alikuwa amekaa akitazamana na Ibra Mbaya na pembeni yake alikaa Dula na Deepaklipa,huku kulia kwake wakikaa watu wengine watatu ambao walikuwa ni wageni machoni kwa wengine isipokuwa kapteni Zegera.

Macho ya watu wote yalimtazama Zegera,Zegera nae akaelewa nini maana ya kutazamwa kule na hapo akanena ili kuwaweka sawa wageni wake.

"Tunapokea lawama nyingi kutoka kwa bwana mkubwa,na kwa hili hata mimi naona wanastahili kutulaumu.
Tumeshindwa kumuua Zedi na anazidi kutuumbua na kwa hili limedhihirika usiku huu,ametuzidi akili bandarini na hivyo silaha zetu hazitatoka maana vyombo vya habari visharipoti na watu watataka kujua kinachoendelea.
Lakini tumeshindwa pia kummliza waziri wa viwanda na taarifa nilionayo ni kuonekana kwa watu wawili wakike eneo lile.
Kia kuuona ugumu wa katika harakati hizi tumepokea usaidizi kutoka kwa wenzetu Kongo wametuletea watu hawa waliokaa hapa,huyu wa kwanza anaitwa Sanko,anaefuatia anaitwa Niyankuru na yule anaitwa Bedo.
Kwa taarifa nilizonazo hawa watu ni wazuri kila idara ila hilo litathibitika katika kazi,lakini kabla hatujasambaratika Ibra naomba mikakati yako"

Akasimama Ibra Mbaya,akawatizama watu wote kisha akasema mipango yote mezani.

"Zedi hayuko peke yake kuna mtu nyuma yake, na taarifa za awali zinatwambia hakuna mtu alienyuma yake anaejulikana ila Mimi nasema yupo na si mwingine ni Meja Salim komba.
Na ili tumtoe katika ubora wake lazima tumtoe kafara Meja Salim Komba hatuna namna.
Pia kuna huyu malaya wa kike Sajini Mina asiachwe hata kidogo na tukiondoka hapa kila mtu ajue jukumu lake"

Akamaliza tena kusema na kukaa na kilichofuatia ni vijana kusambaratika katika makundi matatu
Kundi la kwanza liliongozwa na Zegera na vijana wawili akiwepo Bedo.
Kundi la pili liliongozwa na Deepaklipa na vijana wengine wawili akiwemo Sanko na kundi la tatu liliongozwa na Ibra Mbaya na kundi hili lilimjumisha Niyankuru na ndilo lilikuwa na kazi ya kumuua meja Salim komba.
****
Meja Salimu komba aliisikia muito mdogo katika kompyuta yake iliokuwa wazi na alijisahau kuizima akapitiwa na usingizi.

Alistuka kutoka alipokuwa amekaa na kusonya kisha akajinyoosha viuongo vyake na kujisemea
'"Dah uzee huu kazi yaani nalala bila kujijua"alipiga mwayo na kujongea kwenye kioo cha kompyuta yake na kutazama upande wa jumbe zilizoingia kwenye email yake na hakukagua sana akapigwa na butwaa kwa alichokiona kwenye ujumbe ule na kwa wahaka mkubwa akasogeza macho asiamini anachokiona ila ndicho alichokiona.

Ulikuwa ni ujumbe wa kimafumbo kutoka kwa moja ya vijana wake katika kazi alitambua ujumbe ule uliotumwa katika lugha ya mafumbo ukiambatana na utambulisho wa mtumaji.

Kufupi ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Ziga na Makame,makomando waliofuzu katika medani zote za kivita,walimtaarifu kwa kifupi uwepo wao nchini Kongo.
Hilo lilimshangaza hakuwa na taarifa hiyo lakini kilichomshangaza zaidi ni picha zilizombatanishwa katika ujumbe ule akapagawa kupita maelezo,akachukua simu ili apige ikulu kutoa taarifa ila akasita kufanya hivyo na njia pekee ilikuwa ni kumtafuta Zedi usiku huo,na kweli akapiga namba ya zedi ikapokelewa akasema kidogo kisha akaitupa mezani na kubeba kilichomfaa usiku ule na kutokomea na gari akiitafuta chalinze.

Kitu kimoja hakujua aendako kuna zahama inamnyemelea na angejua ni bora safari yake angeipeleka kwenye kikosi chake anachokisimamia angalau angelipata msaada lakini hakujua,hakujua
****
***

Nb:kuna group la whatsapp kwa malipo kidogo na huko kuna simulizi zitaanza kuwepo kuanzia kesho kujiunga ni Tsh 2500/=

0758573660 kwa malipo na text tu

0658564341kwa whatsapp tu.

Asalaam kudo.
 
[HASHTAG]#Black[/HASHTAG] coffee,Tumosa,moneytalk,iii i keep ma promise,kiker,[HASHTAG]#songa[/HASHTAG] heri,donlucchese,kichwa kikubwa,kigongoi,#
 
Imekaa vizuri! Naomba muwe mnanitag na mimi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom