Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,450
- Thread starter
- #21
RIWAYA: KICHAA.
Na: ZUBER R. MAVUGO.
N0. 16.
ENDELEA.
"Wewe Moyo wangu. Hebu usiniumbue mwenzio. Nakuomba usimuweke mtu, tafadhali nakusihi. Mama alisema mapenzi ndio muharibifu wa maisha, sasa mbona wewe Moyo unaishara za kupenda? Nakuuliza wewe.. Unajifanya hunisikii eti? Kwani sio wewe uliyeshauriana na akili huko nyuma na kuahidi kupenda masomo? Sasa mbona najihisi mapenzi,mapenzi tu. Aaah! Usijifanye huijui ilekauli ya baba. Mimi ni mwamba, popote na timba tu." Ni baadhi tu ya mashtaka aliyoyatoa Neema kuupatia Moyo wake. Alijilaumu kujikuta amependa lakini pia alifurahia jinsi mapenzi yalivyompeleka.
Kesho yake alienda shule baada ya kufanya mazoezi kwenye chumba chake cha mazoezi.
... .. ...
Siku hiyo Mama Neema aliamka vizuri na kufanya usafi kama kawaida. Alipomaliza kazi aliamua kwenda kwa rafiki yake kwa ajili ya kupiga stori maana hakuwa na kazi ya kufanya kwa muda huo. Huko kwa rafiki yake waliteta wakiwa kwenye maongezi yao mara ghafla alipita Kichaa mmoja aliyekuwa ameshikilia mfuniko wa ndoo huku mdomo wake akiutumia kama sauti ya gari. Alipiga sauti za honi kwa mdomo huku akitumia mfuniko kama usukani wa gari yake. Alifika hadi maeneo waliyokuwepo kina Mama Neema.
"Wewe.. Mwehu wewe. Hebu toka hapa nyie ndio waleta nuksi." Ni sauti ya rafiki yake na Mama Neema iliyofoka.
"Jamaniii... Sio vizuri hivyo dada Suzi..." Alidakia Mama Neema baada ya kumsikia shoga yake akiendelea kumfokea yule kichaa.
"Kumbe vizuri niaje Mama Neema!.. We unadhani hiyo harufu ya jalala anayonuka nani wa kuivumilia." Alidakia shoga yake mama Neema ajulikanae kwa jina la Suzi.
"Ni kweli, ananuka.. Lakini ungemwambia tu vizuri. Nasiyo kumfokea kama hivyo."
"Ma. Neema.. Mimi siyokuwafokea tu. Hata maji ya moto huwa nawamwagia kabisa. Hawana adabu wala heshima. Hebu lione hapo nimelitukana ilabado linajichekelesha. Licheki na miudende yake inalitoka tu mdomoni hadi kinyaa." Akatema mate chini kisha akafoka, "We mwehu inamaana bado husikii eti?" Akachukua kikombe cha maji kilichokuwa karibu na mguu wa Ma'Neema. Akampondea mwehu yule.
"Jamaani... Mungu hapendi hivyo da'Suzi. Hebu jiulize hata kama ungekuwa wewe au ndugu yako anafanyiwa hivyo ungejisikiaje. Sio vi..."
"E..eee.. Ma'Neema usinichefue... Kama unatetea wehu kivyako. Mimi siwezi hurumia mwehu tena niache tusije tukakosana. Ohooo, kwanza toka.. Sitaki kukuona hata hapa kwangu." Suzi alisema maneno yale baada ya kudakia kauli ya mama Neema. Hapo akajiinua kwenye mkeka alipokuwa ameyatunza makaliyo yake. Kisha akavaa viatu na kujiingiza ndani mwake huku amefura.
Mama Neema. Alibaki pale nje akimshuhudia Mwehu yule ambae kwa muda huo alikuwa akiendesha gari lake la mfuniko wa ndoo. Alimuhurumia sana lakini asimsaidie.
Hakuwa najinsi zaidi ya kuchukuliwa na miguu yake kwa hiyari na kupelekwa moja kwa moja hadi ndani ya nyumbani kwake alipofika alijibwaga kwenye sofa huku akili yake akiirudisha kwa Suzi ambae alionekana kutokuwa na huruma hata kidogo. Kitendo kile kilimfanya akumbuke kesi ambayo ingemfanya aingize shingo yake kwenye kitanzi au ahukumiwe kifungo cha maisha. Alimkumbuka sana yule mtu aliyemsaidia kuepuka kesi ile. Mtu aliyeonekana kama kichaa. Akakumbuka ushauri wa kichaa yule kipindi anamnyanganya kile kisu alichokitumia kuuchomoa uhai wa Afande Kipara. Akakumbuka kuwa, Kichaa yule aliyemuokoa na kesi ya mauaji ndie aliyemfanya awaheshimu watu wote wanaotembea jalalani na mitaani huku miili yao wameivika madaso yaliyooza, midomo yao muda wote ikiropoka pasina kujali muktadha. Hapo tena akamfikilia huyo shoga yake suzi ambae bila haya alimtukana Mwehu kwa kosa tu lakupita pembezoni mwa mkeka waliyokuwa wamewekea makalio na miguu yao.
"Eee Mungu.. Najua yule kichaa wa watu aliejitolea kifo kwa ajili ya kunihurumia. Kwa sasa atakuwa yupo mbele ya haki. Nakuomba msamehe madhambi yake na umpatie uzima na faraja ya roho huko aliko." Alijitamkia Mama Neema huku akimkumbuka kichaa yule aliyejitambulisha kwa jina la Mavugo, huku akiamini kabisa.. Kichaa yule hatokuwa duniani kwa muda ule kwani ni miaka mingi imeshapita toka waachane siku ile ambayo mama Neema hatoisahau ingawa kwa kipindi kile hakuwa anaitwa Mama Neema bali Aisha Mapuya. Alipitiwa na usingizi palepale kwenye sofa.
.... ...
Siku hiyo Neema hakuwa na raha kabisa hasa kila alipotupa jicho upande wa nyuma kule kwenye madawati ya mwisho na kuiona sura ya upole aliyoivaa Musa. Muda wote Neema alijihisi aibu. Musa na Neema waliendelea kukatana macho kwa mavizio ya zamu. Mwalimu akigeuka kuandika Neema aligeuza shingo yake na kuyatupa macho yake usoni mwa Musa ambae kwa muda huo yeye aliyatupa chini ya dawati ilikuyasitili. Kwa upande wa Musa yeye aliyatupa Macho yake mwilini mwa neema pindi ambapo mwalimu alikuwa bize kwenye maongezi. Waliendelea na kamchezo kao kakutupiana macho na wakati mwingine walipata ajali za kugongana uso kwa uso lakini wote kwa pamoja walijishtukia na kuyainamisha chini macho yao ilimradi tu aibu aibu.
Ulipoisha muda wa vipindi, Neema alienda kwenye dawati la Musa na kuwaomba wale marafiki wa musa wa mpishe kidogo kwani alikuwa na maongezi kidogo na Musa.
Rafiki wa Musa pamoja na wanafunzi wengine walishangazwa sana na kitendo kile maana wanajua wazi kuwa Neema na Musa si marafiki kwani walitukanana na kupelekana hadi kwa walimu. Wale wanafunzi wenye midomo walianza minong'ong'ono ya chini,chini. Huku vichwa vya habari vyao vikiwa ni Neema na Musa.
"vipi Musa bado umenikasirikia?" Aliuliza Neema baada ya kujuliana hali na kupeana salamu.
"Hapana Neema. Mbona nipo fresh tu."
"Anhaa.. Poa."
"Ok. Usijali."
Ukazuka ukimya wa muda kati yao. Huku wote wawili wakipatwa nauoga uliopelekea hata sauti zao kujawa na mitetemiko ya hapa na pale.
Musa akajitutumua na kuuliza,"Vipi.. Unamishe yeyote mbona backbench?" hapo Neema akaanza kujing'atang'ata kutafuta maneno. Huku jasho likianza kumtoka kwapani.
"Nn..nili...nilii.. Hapana. Nilitaka tu kukuomba unifunze alichofundisha mwalimu maana sikumuelewa kabisa." Alijibu Neema huku akiikanyagakanyaga miguu yake.
"Kwanini hujamuelewa mwalimu? Au haukuwa makini, e?" Alihoji Musa.
"Hapana nilikuwa makini lakini sijamuelewa. Ufundishaji wake sijui haukuwa mzuri?" Alijitetea Neema.
"Mmmh! Mbona ameeleweka tu. Ok, na mbona alipotoa ruhusa ya wanafunzi ambao hawajaelewa kunyoosha mkono. Wewe hauku nyoosha wakati haukuelewa." Musa aliendelea kutengeneza hoja mbalimbali ilikumfanya Neema azidi kujitetea zaidi.
Mwisho wa siku Musa aliamua kumuelekeza yale aliyofundisha mwalimu. Alimsihi kuwa awe makini sana pindi mwalimu awamo darasani na kumwambia kuwa kuna mambo ambayo huwa ni ya siri sana yamtokayo mwalimu pindi afundishapo jambo fulani hivyo nijukumu lake kuwa msikivu na mtulivu. Neema aliinua kichwa chake kuonesha amekubali yaliyosemwa na Musa.
Siku hiyo Neema alikuwa muda wote yupo na Musa kwanzia ndani na hata nje ya darasa jambo lililopelekea walimu na wanafunzi hasa wanaofahamu ugomvi wa wawili hao kupata hofu.
"Neema... Umenisindikiza hadi huku halafu ushindwe kuingia home. Kweli?"
"Usijali, acha niende nyumbani kwanza huwa sipendi kupitia kwenye nyumba yeyote kabla ya kupitia kwetu."
"Kwanini, hupendi? Au ukipita huwa unakaukiwa damu?" Alipohoji swali lile Musa ni kama alimtekenya Neema. Hapo akaanza kucheka. Kishaakasema," Yaani wewe unavituko." Akawa makini kidogo na kuendelea, "Hapana.. Hapana hayo ni maisha yangu na sheria zangu binafsi." Maneno yake yaka sababisha mshangao wa hiari kutoka kwa Musa.
"Kumbe sheria tu!! Mi nilidhani labda una sababu ile yamsingi au labda ushachanjiwa dawa kumbe sheria tu. Twende bana.. Sheria zinatenguliwaga tu. Siunajua sheria si, Msahafu eti hazitotenguliwa. Fanya hivyo." Akamaliza maneno yake na kumshika mkono Neema. Neema hakutaka kuelewa somo hata kidogo. Akaendelea kugoma mpaka Musa akaishiwa maneno ya kuongea..
"Sawa.. Umeshinda. Hebu tuachane na hayo. Vipi, ulilikiria kwa mara ya pili ombi langu?" Aliuliza huku nafsi yake ikivuka ujasiri na kuanza kuleta uoga.
"Hivi, Musa.. Ina maana tuseme wewe huwa kichwa ngumu eti! Yaani mimi niache kufanya mambo yangu nianze kukufikilia wewe sindio?" Neema alibadilika na kuongea sauti ya juu. Tena ile ya kuogofya, sauti ile ikazidisha uoga kwa Musa na kuhisi huenda akizidisha king'ang'anizi hata uo urafiki utakufa akose yote.
"Basi... Yaishe, lakini sio vizuri hivyo."
"Kumbe, vizuri niaje Musa. Acha mie niende." Akaondoka. Musa ile furaha yake ya siku nzima ikaisha ghafla. Alipofika nyumbani kwake kitandani hapo akaanza kutalii ndani ya bahari lile la mawazo. Mawazo yalimshinda na kuamua angalau amtafute rafiki yake amshauri.
.... ...
"Afya.. Eee. E.e. Afya ni kitu bora. Ya kwanza mchicha ya pili mayai. Na maharage pia.." Ni sauti ya Baba Neema. Alikuwa akiimba moja kati ya nyimbo azipendazo pindi awapo kwenye akili ya pombe.
"We.. Neema? Wewe Mwanangu." Aliita huku akigonga mlango kwa hodi. Neema aliisikia sauti ya Baba yake kipenzi na kwenda kufungua mlango.
"Karibu baba."Alimkaribisha Baada ya kumsalimu na kumjulia hali.
"Ahsante sana mwamba, popote unatimba.. Eee nakutegemea wewe. Uje urithi hadi pombe sawa mwanangu." Neema alimuitikia Baba yake kwa kila alichosema kwakuwa anamjua baba yake pindi anukiapo pombe kinywani huwaje.
Mzee alimpigisha mwanae hadithi mbili tatu kishaakakaribishwa chakula na mke wake. Alienda na kula chakula kile. Waliagana na kila mmoja akaenda kulala.
Upande wa Musa. Yeye alikuwa kwa rafiki yake akipata ushauri.
"Unajua wewe Musa. Uache ushamba wako. Elimika, oohooo. We jifanye domo zege. Labda ni kwambie kitu. Mwanamke kama nilivyokwisha kwambia, huwa anatabia ya kujifanya anamaamuzi ya mdomo. Wewe kama mwanamume unachotakiwa sio kushughulika na utatuzi wa maamuzi yake ya mdomo bali shughulika na moyo wake tu." Aliongea Side na kumfanya Musa aendelee kujenga maswali mengi kichwani.
"Sawa nimekusikia mzee wa mipango. Samahani natakaniulize ila usinicheke.. Umesema kuwa mwanamke akiongea mimi nisijali maneno ya mdomo wake bali niongee na Moyo wake." akaitikia Side kumaanisha kuwa alitamka jambo lile. Kisha Musa akaendelea, "Sasa ndugu yangu.. Hebu nielekeze jinsi ya kuongea na Moyo wa mwanamke. Maana labda hilo ndilo kosa langu kubwa." Aliomba msaada wa elimu kwa rafiki yake.
Na: ZUBER R. MAVUGO.
N0. 16.
ENDELEA.
"Wewe Moyo wangu. Hebu usiniumbue mwenzio. Nakuomba usimuweke mtu, tafadhali nakusihi. Mama alisema mapenzi ndio muharibifu wa maisha, sasa mbona wewe Moyo unaishara za kupenda? Nakuuliza wewe.. Unajifanya hunisikii eti? Kwani sio wewe uliyeshauriana na akili huko nyuma na kuahidi kupenda masomo? Sasa mbona najihisi mapenzi,mapenzi tu. Aaah! Usijifanye huijui ilekauli ya baba. Mimi ni mwamba, popote na timba tu." Ni baadhi tu ya mashtaka aliyoyatoa Neema kuupatia Moyo wake. Alijilaumu kujikuta amependa lakini pia alifurahia jinsi mapenzi yalivyompeleka.
Kesho yake alienda shule baada ya kufanya mazoezi kwenye chumba chake cha mazoezi.
... .. ...
Siku hiyo Mama Neema aliamka vizuri na kufanya usafi kama kawaida. Alipomaliza kazi aliamua kwenda kwa rafiki yake kwa ajili ya kupiga stori maana hakuwa na kazi ya kufanya kwa muda huo. Huko kwa rafiki yake waliteta wakiwa kwenye maongezi yao mara ghafla alipita Kichaa mmoja aliyekuwa ameshikilia mfuniko wa ndoo huku mdomo wake akiutumia kama sauti ya gari. Alipiga sauti za honi kwa mdomo huku akitumia mfuniko kama usukani wa gari yake. Alifika hadi maeneo waliyokuwepo kina Mama Neema.
"Wewe.. Mwehu wewe. Hebu toka hapa nyie ndio waleta nuksi." Ni sauti ya rafiki yake na Mama Neema iliyofoka.
"Jamaniii... Sio vizuri hivyo dada Suzi..." Alidakia Mama Neema baada ya kumsikia shoga yake akiendelea kumfokea yule kichaa.
"Kumbe vizuri niaje Mama Neema!.. We unadhani hiyo harufu ya jalala anayonuka nani wa kuivumilia." Alidakia shoga yake mama Neema ajulikanae kwa jina la Suzi.
"Ni kweli, ananuka.. Lakini ungemwambia tu vizuri. Nasiyo kumfokea kama hivyo."
"Ma. Neema.. Mimi siyokuwafokea tu. Hata maji ya moto huwa nawamwagia kabisa. Hawana adabu wala heshima. Hebu lione hapo nimelitukana ilabado linajichekelesha. Licheki na miudende yake inalitoka tu mdomoni hadi kinyaa." Akatema mate chini kisha akafoka, "We mwehu inamaana bado husikii eti?" Akachukua kikombe cha maji kilichokuwa karibu na mguu wa Ma'Neema. Akampondea mwehu yule.
"Jamaani... Mungu hapendi hivyo da'Suzi. Hebu jiulize hata kama ungekuwa wewe au ndugu yako anafanyiwa hivyo ungejisikiaje. Sio vi..."
"E..eee.. Ma'Neema usinichefue... Kama unatetea wehu kivyako. Mimi siwezi hurumia mwehu tena niache tusije tukakosana. Ohooo, kwanza toka.. Sitaki kukuona hata hapa kwangu." Suzi alisema maneno yale baada ya kudakia kauli ya mama Neema. Hapo akajiinua kwenye mkeka alipokuwa ameyatunza makaliyo yake. Kisha akavaa viatu na kujiingiza ndani mwake huku amefura.
Mama Neema. Alibaki pale nje akimshuhudia Mwehu yule ambae kwa muda huo alikuwa akiendesha gari lake la mfuniko wa ndoo. Alimuhurumia sana lakini asimsaidie.
Hakuwa najinsi zaidi ya kuchukuliwa na miguu yake kwa hiyari na kupelekwa moja kwa moja hadi ndani ya nyumbani kwake alipofika alijibwaga kwenye sofa huku akili yake akiirudisha kwa Suzi ambae alionekana kutokuwa na huruma hata kidogo. Kitendo kile kilimfanya akumbuke kesi ambayo ingemfanya aingize shingo yake kwenye kitanzi au ahukumiwe kifungo cha maisha. Alimkumbuka sana yule mtu aliyemsaidia kuepuka kesi ile. Mtu aliyeonekana kama kichaa. Akakumbuka ushauri wa kichaa yule kipindi anamnyanganya kile kisu alichokitumia kuuchomoa uhai wa Afande Kipara. Akakumbuka kuwa, Kichaa yule aliyemuokoa na kesi ya mauaji ndie aliyemfanya awaheshimu watu wote wanaotembea jalalani na mitaani huku miili yao wameivika madaso yaliyooza, midomo yao muda wote ikiropoka pasina kujali muktadha. Hapo tena akamfikilia huyo shoga yake suzi ambae bila haya alimtukana Mwehu kwa kosa tu lakupita pembezoni mwa mkeka waliyokuwa wamewekea makalio na miguu yao.
"Eee Mungu.. Najua yule kichaa wa watu aliejitolea kifo kwa ajili ya kunihurumia. Kwa sasa atakuwa yupo mbele ya haki. Nakuomba msamehe madhambi yake na umpatie uzima na faraja ya roho huko aliko." Alijitamkia Mama Neema huku akimkumbuka kichaa yule aliyejitambulisha kwa jina la Mavugo, huku akiamini kabisa.. Kichaa yule hatokuwa duniani kwa muda ule kwani ni miaka mingi imeshapita toka waachane siku ile ambayo mama Neema hatoisahau ingawa kwa kipindi kile hakuwa anaitwa Mama Neema bali Aisha Mapuya. Alipitiwa na usingizi palepale kwenye sofa.
.... ...
Siku hiyo Neema hakuwa na raha kabisa hasa kila alipotupa jicho upande wa nyuma kule kwenye madawati ya mwisho na kuiona sura ya upole aliyoivaa Musa. Muda wote Neema alijihisi aibu. Musa na Neema waliendelea kukatana macho kwa mavizio ya zamu. Mwalimu akigeuka kuandika Neema aligeuza shingo yake na kuyatupa macho yake usoni mwa Musa ambae kwa muda huo yeye aliyatupa chini ya dawati ilikuyasitili. Kwa upande wa Musa yeye aliyatupa Macho yake mwilini mwa neema pindi ambapo mwalimu alikuwa bize kwenye maongezi. Waliendelea na kamchezo kao kakutupiana macho na wakati mwingine walipata ajali za kugongana uso kwa uso lakini wote kwa pamoja walijishtukia na kuyainamisha chini macho yao ilimradi tu aibu aibu.
Ulipoisha muda wa vipindi, Neema alienda kwenye dawati la Musa na kuwaomba wale marafiki wa musa wa mpishe kidogo kwani alikuwa na maongezi kidogo na Musa.
Rafiki wa Musa pamoja na wanafunzi wengine walishangazwa sana na kitendo kile maana wanajua wazi kuwa Neema na Musa si marafiki kwani walitukanana na kupelekana hadi kwa walimu. Wale wanafunzi wenye midomo walianza minong'ong'ono ya chini,chini. Huku vichwa vya habari vyao vikiwa ni Neema na Musa.
"vipi Musa bado umenikasirikia?" Aliuliza Neema baada ya kujuliana hali na kupeana salamu.
"Hapana Neema. Mbona nipo fresh tu."
"Anhaa.. Poa."
"Ok. Usijali."
Ukazuka ukimya wa muda kati yao. Huku wote wawili wakipatwa nauoga uliopelekea hata sauti zao kujawa na mitetemiko ya hapa na pale.
Musa akajitutumua na kuuliza,"Vipi.. Unamishe yeyote mbona backbench?" hapo Neema akaanza kujing'atang'ata kutafuta maneno. Huku jasho likianza kumtoka kwapani.
"Nn..nili...nilii.. Hapana. Nilitaka tu kukuomba unifunze alichofundisha mwalimu maana sikumuelewa kabisa." Alijibu Neema huku akiikanyagakanyaga miguu yake.
"Kwanini hujamuelewa mwalimu? Au haukuwa makini, e?" Alihoji Musa.
"Hapana nilikuwa makini lakini sijamuelewa. Ufundishaji wake sijui haukuwa mzuri?" Alijitetea Neema.
"Mmmh! Mbona ameeleweka tu. Ok, na mbona alipotoa ruhusa ya wanafunzi ambao hawajaelewa kunyoosha mkono. Wewe hauku nyoosha wakati haukuelewa." Musa aliendelea kutengeneza hoja mbalimbali ilikumfanya Neema azidi kujitetea zaidi.
Mwisho wa siku Musa aliamua kumuelekeza yale aliyofundisha mwalimu. Alimsihi kuwa awe makini sana pindi mwalimu awamo darasani na kumwambia kuwa kuna mambo ambayo huwa ni ya siri sana yamtokayo mwalimu pindi afundishapo jambo fulani hivyo nijukumu lake kuwa msikivu na mtulivu. Neema aliinua kichwa chake kuonesha amekubali yaliyosemwa na Musa.
Siku hiyo Neema alikuwa muda wote yupo na Musa kwanzia ndani na hata nje ya darasa jambo lililopelekea walimu na wanafunzi hasa wanaofahamu ugomvi wa wawili hao kupata hofu.
"Neema... Umenisindikiza hadi huku halafu ushindwe kuingia home. Kweli?"
"Usijali, acha niende nyumbani kwanza huwa sipendi kupitia kwenye nyumba yeyote kabla ya kupitia kwetu."
"Kwanini, hupendi? Au ukipita huwa unakaukiwa damu?" Alipohoji swali lile Musa ni kama alimtekenya Neema. Hapo akaanza kucheka. Kishaakasema," Yaani wewe unavituko." Akawa makini kidogo na kuendelea, "Hapana.. Hapana hayo ni maisha yangu na sheria zangu binafsi." Maneno yake yaka sababisha mshangao wa hiari kutoka kwa Musa.
"Kumbe sheria tu!! Mi nilidhani labda una sababu ile yamsingi au labda ushachanjiwa dawa kumbe sheria tu. Twende bana.. Sheria zinatenguliwaga tu. Siunajua sheria si, Msahafu eti hazitotenguliwa. Fanya hivyo." Akamaliza maneno yake na kumshika mkono Neema. Neema hakutaka kuelewa somo hata kidogo. Akaendelea kugoma mpaka Musa akaishiwa maneno ya kuongea..
"Sawa.. Umeshinda. Hebu tuachane na hayo. Vipi, ulilikiria kwa mara ya pili ombi langu?" Aliuliza huku nafsi yake ikivuka ujasiri na kuanza kuleta uoga.
"Hivi, Musa.. Ina maana tuseme wewe huwa kichwa ngumu eti! Yaani mimi niache kufanya mambo yangu nianze kukufikilia wewe sindio?" Neema alibadilika na kuongea sauti ya juu. Tena ile ya kuogofya, sauti ile ikazidisha uoga kwa Musa na kuhisi huenda akizidisha king'ang'anizi hata uo urafiki utakufa akose yote.
"Basi... Yaishe, lakini sio vizuri hivyo."
"Kumbe, vizuri niaje Musa. Acha mie niende." Akaondoka. Musa ile furaha yake ya siku nzima ikaisha ghafla. Alipofika nyumbani kwake kitandani hapo akaanza kutalii ndani ya bahari lile la mawazo. Mawazo yalimshinda na kuamua angalau amtafute rafiki yake amshauri.
.... ...
"Afya.. Eee. E.e. Afya ni kitu bora. Ya kwanza mchicha ya pili mayai. Na maharage pia.." Ni sauti ya Baba Neema. Alikuwa akiimba moja kati ya nyimbo azipendazo pindi awapo kwenye akili ya pombe.
"We.. Neema? Wewe Mwanangu." Aliita huku akigonga mlango kwa hodi. Neema aliisikia sauti ya Baba yake kipenzi na kwenda kufungua mlango.
"Karibu baba."Alimkaribisha Baada ya kumsalimu na kumjulia hali.
"Ahsante sana mwamba, popote unatimba.. Eee nakutegemea wewe. Uje urithi hadi pombe sawa mwanangu." Neema alimuitikia Baba yake kwa kila alichosema kwakuwa anamjua baba yake pindi anukiapo pombe kinywani huwaje.
Mzee alimpigisha mwanae hadithi mbili tatu kishaakakaribishwa chakula na mke wake. Alienda na kula chakula kile. Waliagana na kila mmoja akaenda kulala.
Upande wa Musa. Yeye alikuwa kwa rafiki yake akipata ushauri.
"Unajua wewe Musa. Uache ushamba wako. Elimika, oohooo. We jifanye domo zege. Labda ni kwambie kitu. Mwanamke kama nilivyokwisha kwambia, huwa anatabia ya kujifanya anamaamuzi ya mdomo. Wewe kama mwanamume unachotakiwa sio kushughulika na utatuzi wa maamuzi yake ya mdomo bali shughulika na moyo wake tu." Aliongea Side na kumfanya Musa aendelee kujenga maswali mengi kichwani.
"Sawa nimekusikia mzee wa mipango. Samahani natakaniulize ila usinicheke.. Umesema kuwa mwanamke akiongea mimi nisijali maneno ya mdomo wake bali niongee na Moyo wake." akaitikia Side kumaanisha kuwa alitamka jambo lile. Kisha Musa akaendelea, "Sasa ndugu yangu.. Hebu nielekeze jinsi ya kuongea na Moyo wa mwanamke. Maana labda hilo ndilo kosa langu kubwa." Aliomba msaada wa elimu kwa rafiki yake.