Lumbi9
JF-Expert Member
- Oct 12, 2014
- 8,566
- 11,808
MTUNZI: George Iron
SEHEMU YA KWANZA
Safari nzima hakutaka kuzungumza na mtu yeyote hivyo alikuwa amepachika �earphone� masikioni mwake ili hata asiweze kusikiliza watu walikuwa wanazungumza nini mara chache sana alipata nafasi ya kusikia mawili matatu hasahasa pale wimbo ulipokuwa unaisha na kuachia nafasi ya wimbo mwingine kuingia, katika kibegi chake kidogo alikuwa na takribani betri nne zilizokuwa zimechajiwa usiku uliopita ili asipatwe na usumbufu wa kuzimikiwa simu katika safari yake hiyo ndefu kiasi ya kuelekea wilayani Serengeti mkoa wa Mara.
Hivi wazazi wangu ni wendawazimu�sasa waliniita Michael ili iweje kwa nini hawakuniita hata Masumbuko?. Alijiuliza kijana huyu mrefu wa wastani ambaye umbo lake kwa kumtazama ungemkadiria kuwa na miaka ipatayo thelathini lakini kiukweli ndio kwanza siku tatu zilizopita alikuwa ametoka kusheherekea kutimiza miaka ishirini na tano siku ambayo ilianza vizuri sana asubuhi kwa kupokea jumbe tofautitofauti kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki waliokuwa wanaikumbuka tarehe hiyo. Karibia kila mmoja alimtakia heri na fanaka katika maisha yake, huku wakikumbuka pia kumtakia aishi miaka mingi. Kuna ujumbe mmoja alioutegemea lakini hadi wakati huo hakuwa ameupata!!!!
Joyce atakuwa ameisahau hii siku au kuna tatizo jingine?? Michael alijiuliza baada ya kutouona ujumbe wake kati ya jumbe zote alizopokea. Kwa kuwa Joyce hakuwa akikaa mbali sana na mtaa anaoishi Michael jijini Dar es salaam, basi Michael alitumia fursa hii kwenda kumpa surprise rafiki yake huyo wa kike tangu utotoni japo hawakuwahi kuvuka urafiki na kuwa wapenzi lakini ndipo walikuwa wanaelekea. Alitaka kuifanya siku hii iwe ya kukumbukwa.
Michael alikuwa anatabasamu njia nzima, kwani aliamini kuwa ile hali tu ya kumkumbusha Joyce tukio hili ni lazima atamrukia na kumkumbatia, kitendo ambacho kwa Michael ni zaidi ya zawadi, lile joto la kipekee la binti huyo lingeweza kumchangamsha na kujisikia kweli amezaliwa siku hiyo.
Utajuaje, huenda pia atanibusu?? Alijisemea Michael kisha akafanya kicheko kidogo cha kujilazimisha. Kisha akatikisa kichwa kama vile kuna jambo alikuwa analikataa.
Sasa alikuwa ameufikia mlango. Akalazimika kunyata ili amshtue Joyce, na hatimaye apokee lile kumbatizi maridhawa.
Alichokikuta Michael nyumbani kwa akina Joyce ndicho kilibadili ghafla mipango yake ya kufanyia mazoezi ya vitendo (field) katika jiji la Dar es salaam na kuamua kuelekea mji mdogo wa Mugumu Serengeti mkoa wa Mara bila kutarajia. Hakujua kwa nini ameuchagua mji huo lakini alijikuta katika maamuzi hayo. Maamuzi ya kuishi mbali na uchungu ule. Wivu wa kimapenzi ulimsulubisha na kumpelekesha kwa kiasi kikubwa.
�Lakini kwani nilikuwa nimemtamkia kuwa nampenda?...mimi ni mpuuzi huenda labda ndio maana hakushtuka nilipomkuta.� Alijiuliza Michael huku akijaribu kunywa maji ili kulegeza donge la hasira lililokuwa limemkaba kooni .
�Hivi ninachokasirika ni nini hasa wakati hajui kama nilikuwa namtaka?...ah!! huu ni upuuzi hakika.� Alijiliwaza Michael huku akishindwa kuyanywa yale maji na kuyafunika kisha kuendelea kupata burudani ya muziki baada ya muda alipitiwa na usingizi alikuja kushtuka baada ya mwanamama aliyekuwa pembeni yake kumlaumu kuwa alikuwa anamlalia kila anaposinzia.
�Unasema??.� Aliuliza kwa sauti ya juu Michael baada ya kuwa ameathiriwa na sauti kali ya muziki masikioni.
�Unanilalia bwana!!!.�
�Ah!! Samahani�� Wakati huu alikuwa ameondoa �earphone� masikioni mwake. Safari ilikuwa inaendelea, safari ya kutoka jijini Dar es salaam kuelekea Mwanza kisha mkoa wa Mara. Hii ndio ilikuwa mipango yake. Mipango ya kukimbia maumivu. Kuikimbia vita ya mapenzi badala ya kukabiliana nayo.
Baada ya kuomba radhi alitaka kurejesha tena earphone masikioni lakini alisita kidogo baada ya kuvutiwa na vurumai iliyokuwa inaendelea kati ya makondakta wa hilo basi na mwanadada, kisa kilikuwa ni kukosa nauli kwa huyo dada huku akidai kuna mtu anamlipia yuko nyuma.
�We mbona unasema kuwa kuna mtu analipa na sisi hatumuoni�nenda ukamguse basi mwambie alipe, yaani wewe umepandia njiani halafu unasema kuna mtu anakulipia, acha kutuzingua basi na ujanja wa kizamani. Hakuna lifti siku hizi ujue� Kondakta mmoja alibwatuka kwa ghadhabu akionyesha dhahiri kukerwa na maneno ya yule dada aliyekuwa hajakaa kisafari ndefu kabisa.
�Ebwana anayemlipia huyu dada yuko wapi?? Sisi tunamshusha hivyo.� alitangaza kondakta lakini hakuna aliyejitokeza kubeba mzigo huo.
�Mi sishukiiiii�sishuki, niacheni, niache hukooo, sitaki kushukaa.� Alilia yule dada kwa sauti ya juu huku akiwa ameng�ang�ania mkono wa yule kondakta hapo ni baada ya gari kuwa limesimama ili ashushwe. Kila mtu alikuwa na shughuli zake hakuna aliyejishughulisha na sakata hili kwa asilimia kubwa. Waliojaribu kujishughulisha walikuwa wakitabasamu ama kucheka huku wengine wakiongea sauti za chinichini. Haikujulikana wapo upande upi.
Michael alikuwa bado anaangalia hilo vurumai linavyoendelea, kitendo cha huyo dada kilimkumbusha adha ya usafiri katika jiji alilokuwa ametoka la Dar es salaam lakini kikubwa zaidi ni umasikini unaotawala sehemu kubwa ya Tanzania, lakini kilichomuumiza ni unyanyasaji wa wanawake katika jamii jambo ambalo alikuwa analipinga na hadi kufikia kusomea masuala ya sheria na haki za binadamu akiwa mwaka wa pili katika chuo kikuu cha Dar es salaam na sasa alikuwa anaelekea katika field.
Alikumbuka jinsi alivyokuwa anajisikia vibaya iwapo mzee wake anatokea kumnyanyasa mama yake. Ile hali ikajirudia tena baada ya sakata hili. Moyo ukamuuma!!!
�Nipo naye huyo!!!.� Alitamka kwa sauti kuu Michael. Hakujua maneno haya aliyatoa wapi lakini aliyatamka kiufasaha na kusikiwa na kila abiria ndani ya basi hilo la Najimunisa wakati huo tayari tairi sita za basi hilo zilikuwa katika ardhi ya Dodoma. Watu wote waligeuka kumtazama kwa mshangao huku kondakta akitaharuki na uso wake haukutabasamu bali ulipambwa na ndita zilizomaanisha hasira.
�Sasa muda wote huo ulikuwa wapi kujibu mbona mnaleta ujanja wa kishamba hapa..sasa ulitegemea nitamuacha huyu malaya wako asafiri bure au, acha hizo jombaaa!! Mbona tunatafutiana sababu za kutukana halafu mwishowe mnasema makonda wana matusi.� Kondakta ambaye kimabavu alimzidi Michael alitoa karipio.
�Nauli ni shilingi ngapi??.� Badala ya kujibu lawama za yule Kondakta Michael kwa kujiamini kabisa aliuliza swali bila wasiwasi. Ilikuwa ni kama hakumsikia kipindi anabwatuka.
�Sio ishu hizo kaka�nigei elfu ishirini na tisa hiyo.� Alijibiwa kwa jazba. Taratibu alijipekua na kutoa noti tatu za elfu kumi kumi akampatia akarudishiwa elfu moja.
�Kakae kule nyuma na jamaa yako nafasi inatosha ile pale.� Alielekezwa yule binti ambaye bado machozi yalikuwa yanamtiririka mashavuni na kudondoka chini.
Kwa kusuasua alienda na kujibanabana pembeni ya Michael wakati huo gari zima lilikuwa linaitazama filamu hii tamu ya kusisimua. Binti alipofika pale tayari Michael alikuwa amerejesha �earphone� masikioni mwake na wala hakumjibu alipotoa shukrani ya msaada huo.
Michael alitegemea kumuuliza maswali yule binti baada ya muda fulani. Lakini ajabu mdomo wake ukawa mzito.
Alihofia kuwa kuanzisha kwake maongezi na msichana yule anaweza kuzua mambo mengine. Hakutaka kabisa kujiweka karibu na msichana kimaongezi, aliiona taswira ya Joyce katika uso wa kila mwanamke. Akampuuzia binti yule.
�Mh!! Wanaume wanajua kutesa wanawake da!! Sasa hapo wamegombana nyumbani anauleta ugomvi wao kwenye usafiri ah!!! Ujinga kweli huu.� Alisikika abiria mmoja mwanamke wa makamo akilalamika lawama ambazo hazikupenya katika masikio ya Michael.
�Pole dadangu!!!.� mwanaume mwingine upande wa kulia alimwambia yule binti naye akamjibu kwa kichwa.
Muziki ulipomchosha Michael, akapekua begi lake dogo akaibuka na kitabu. Akakifunua ukurasa alioishia kabla ya kukifunika. CHUKI ndio lilikuwa jina la kitabu kile.
Yule binti ambaye alikuwa mkimya, akajigeuza na kuanza kusoma ukurasa wa mbele wa kitabu kile. Umakini aliouweka ni kama vile kuna kitu alikuwa anafahamu.
�Haa!!� akashangaa kwa sauti ya chini sana kama anajishangaa mwenyewe, Michael akasita kusoma lakini hakumtazama machoni, kisha yule binti akasema, �Huyu jamaa ametoa kingine mh!! Vipi ni muendelezo wa ROHO YA MWISHO au?� Aliuliza kwa furaha binti yule huku akionyesha kumjua vyema mtunzi wa kitabu kile cha hadithi. Kauli za dada huyu zikamgusa Michael, akajikuta akivunja kiburi chake cha kukaa kimya.
�Hamna hiki kipo kivyake tu, ni kali kuliko ROHO YA MWISHO lakini hakifikii HILA� Alimjibu kwa uchangamfu baada ya kugundua kuwa yule dada naye alikuwa akimfahamu mtunzi wa hadithi ile wote walikuwa wakimzungumzia George Iron mtunzi wa vitabu vya HILA, ROHO YA MWISHO na riwaya yake ya kushangaza ya NILIKUFA JANA. Mwandishi aliyeikonga ipasavyo roho yake. Michael akataka kuzungumza mengi juu ya mwandishi huyu, lakini akajionya asiweke mazoea ya ukaribu sana na msichana huyu ambaye hakuwa akimfahamu hata kidogo.
�Vipi hivi unaweza kuwa nacho kile cha HILA maana jamaa alitoa vichache halafu vikapotea kama vile hakutoa. Nasikitika sikupata bahati ya kukisoma.� Alijieleza kwa malalamiko yule dada lakini hakujibiwa na badala yake yule Michael alikichomoa kitabu cha HILA kutoka katika maficho ya begi lake dogowa, akampatia yule binti asiyemfahamu. Alionyesha kujisikia fahari sana kumiliki kazi zote zinazotolewa na mwandishi huyu.
Kimya kikatanda baada ya kila mmoja kujikita katika kusoma simulizi.
Urafiki wao ukaanzishwa rasmi na hobi zao katika kusoma vitabu.
Michael akayasahau machungu ya Joyce kwa muda!!
Akili yake yote ikajikita katika kitabu cha hadithi!!! Chuki!!
Walipoviacha vitabu vyao, mazungumzo yalikuwa mengine. Hawakuwa wakimzungumzia tena mwandishi yule wa vitabu walivyomaliza kuvisoma.
Wakajikuta wanajenga mazoea ya hali ya juu. Cha ajabu hawakuulizana majina. Kila mmoja alikuwa akimtegea mwenzake aanze kuuliza. Huku Michael akijiweka katika tahadhari ya kujikita katika maumivu mengine kwa kumwendekeza yule binti.
Kadri muda ulivyokwenda ndivyo wawili hawa walikuwa kama wapenzi!! Huku yule binti akiifurahia zaidi hali ile.
******
Basi lilikuwa katika mwendo mkali sana hapo likikaribia ardhi ya Shinyanga majira ya saa mbili kasorobo usiku, dereva ambaye tangu safari ianze alikuwa anazungumza mara kwa mara na abiria aliyekuwa pembeni yake alijikuta akifumba macho na kuyafumbua ghafla huku masikio yake yakijibiwa kwa kilio kikali kutoka upande fulani wa gari, ni uzoefu aliokuwa nao ndio sababu pekee iliyozuia gari lile lisipinduke baada ya kulivaa shimo ambalo hakuliona kwa kukosa umakini wakati wa kuendesha.
Gari liliposimama, Michael alikuwa wima, macho yamemtoka pima huku chini akiwepo yule binti ametulia tuli huku akitoa kilio kwa sauti ya chini mno. Abiria kadhaa walisogea kule alipokuwa Michael na kumsaidia kushangaa huku hata mmoja hakuthubutu kumgusa yule binti kwa jinsi alivyokuwa amejikunjakunja katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa.
�Gari ilipopiga lile bonde tulirushwa juu niliweza kumshuhudia akitua kwenye siti yake kwa kishindo halafu�sijui ni nini kimetokea baada ya hapo.� Alizungumza Michael baada ya maswali kumwangukia yeye juu ya kilichomsibu yule binti ambaye watu walimtambua kama mpenzi ama ndugu yake.
�Mambo mengine kujitakia tu tazama sasa huyu wamegombana nyumbani amemnyanyasa kwenye gari hadi ameaibika ona sasa mwisho wake.� Alilalamika mwanamke mmoja aliyeonekana kuguswa sana na hilo jambo.
Michael alitamani sana kujieleza kwamba hafahamiani na yule binti lakini aliamini kwamba hakuna hata mtu mmoja ambaye angeamini hivyo aliendelea kubaki kimya asijue la kufanya. Ile kauli aliyoitoa kuwa yeye yupo na yule binti tayari ikaanza kumuingiza matatani. Na hakuwa na ujanja wa kujinasua. Kauli ile ilisikiwa na wengi!!!
Hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa ujumla haikuwa mbali sana kutoka mahali basi hilo la Najimunisa lilipopatia hiyo tafrani, kwa maamuzi yaliyoafikiwa na kila abiria yule binti walimzoazoa kutoka pale chini na kumweka katika siti ya mbele ambayo ilikuwa na uwezo wa kupokea watu watatu, hakuwa akitokwa na damu lakini alikuwa akigumia kwa sauti ya chini sana, mwanamke mmoja alikaa pamoja naye kwa ajili ya kumsaidia huku Michael naye akiwa karibu yake.
******
Hospitali ya mkoa wa Shinyanga ndio kwanza ilikuwa katika mgomo wa madaktari wakitaka mwenzao aliyewekewa zengwe na kufukuzwa kazi baada ya kushindwa kuokoa maisha ya mtoto wa Kigogo arejeshwe kazini hivyo hakuna huduma zilizokuwa zikitolewa pale licha ya madaktari kuwepo eneo hilo la Hospitali mjini Shinyanga. Kundi la wanaume wanne wakiwa wamembeba mgonjwa wao liliingia kwa uharaka wa kuhitaji huduma pale ndani, hakuna yeyote aliyewakaribisha zaidi ya ukarimu walioupata kwa mlinzi pale mlangoni huku akiwaonea huruma, kila mtu alikuwa bize sana na mambo yake binafsi yasiyoendana na mandhari ya hospitali.
�Nesi nesi�� mwanamme moja aliita lakini alijibiwa kwa jicho kali kisha mwanamama huyo akatoweka. Kwa ujasiri waliamua kujitafutia wodi mojawapo na kumlaza yule binti kitandani kisha wakaanza kuhaha kuwatafuta madaktari ambao hata hawakuonyesha kujali. Mwanzoni walikuwa wanaume wanne pamoja na mwanadada asiyejitambua hata kidogo akiwa katika maumivu makali sana ambayo hakuhitaji kujieleza mwenyewe bali jinsi alivyokuwa ameuma meno na kuikunja sura yake lilikuwa jibu tosha, baada ya muda wakabaki watatu, wawili na hatimaye mmoja Michael!! Ndio alikuwa Michael peke yake pamoja na binti.
Nafsi ya Michael ikaingia katika mgogoro mkali, mgogoro binafsi, maamuzi yalikuwa mengi lakini hakujua lipi ni sahihi. Akiwa katika wimbi la mawazo alisikia anaguswa begani.
�Aah!! Kijana nimekutafuta kweli, ni zaidi ya saa zima sasa nilikuwa napita hapa lakini sijui kwa nini hii wodi nilikuwa naivuka.� sauti nzito kutokana na umri kwenda ilimweleza Michael ambaye alibaki kuduwaa ilikuwa mara yake ya kwanza kufika katika mkoa huu uliotawaliwa na jamii ya wasukuma halafu anatokea mtu anamfahamu.
�Mimi?.�
�Ndio wewe!!!.�
�Aaah!!! Eheee.� aliuliza Michael ili apate kujua shida ya yule mtu.
�Unawahi kusahau wewe, mimi ni yule mlinzi wa pale getini mwanangu poleni sana baba!!!! Pole sana� alijieleza yule mlinzi. Michael hakuwa na kumbukumbu kabisa kwamba pale kwenye basi walipofikia muafaka wa kumwahisha binti hospitali watu walichangachanga walichonacho na kufikisha shilingi laki mbili na nusu ambayo walimkabidhi, alipozipokea mkononi ndivyo hivyo hivyo alizishika hadi waliposhuka na kumfikia mlinzi wa geti, wakati anaandika jina lake katika kitabu cha orodha ya wageni ndio wakati huo huo aliziachia zile pesa na kuzisahau, jambo jema mlinzi huyu aliyejitambulisha kama mzee Matata aliona tukio hilo na kuokoa pesa za Michael na sasa alikuwa amempata kwa ajili ya kumpatia.
Michael alishangazwa na uaminifu aliokuwa nao babu huyu wa makamo mrefu, mwenye mwili uliojengeka na ndevu zake zilizokuwa na mvi kiasi,
�Kwa nini amenirejeshea hizi pesa??.� Alijiuliza Michael
�Asante sana mzee wangu asante sana.� Michael alijaribu kumpatia kiasi fulani cha pesa lakini mzee Matata alikataa kabisa huku akimwonea huruma Michael kwa hali aliyokuwa nayo.
�Ngoja niangalie kama utapata huduma walau ya kwanza maana huyu nani vile anaitwa??.�
�Aaah!!! Mhh!! Huyu?? Anaitwa nanii Mariam eeh!!! Mariam.� alijibu Michael kwa kujiumauma
Mzee Matata alipotoka Michael naye alifikiria kuondoka na kumwacha binti peke yake, akili ilikuwa imemruhusu lakini wakati anapiga hatua mlangoni aliisikia nafsi yake ikimtamkia neno �NIPO NAYE� ambalo alilitaja pale ndani ya basi, nafsi pia ilimsuta kwa pesa aliyorejeshewa na mzee Matata, kwa kutoroka ilimaanisha kwamba amefanya dhulumati na kuweka maisha ya binti katika hatihati. Michael alizishusha pumzi zake kisha akarejea tena pale wodini kusubiria harakati za mzee Matata kama zitazaa matunda.
Michael amejikuta akimsaidia binti asiyemfahamu hata kidogo!!! Hajui kwanini amemsaidia ghafla kiasi hicho�.akiwa hata hajatambua jina la binti huyo yanatokea ya kutokea na sasa wapo hospitali�huduma hakuna kutokana na mgomo!!!!
****Ni HATIA gani inayozungumzwa katika simulizi hii.
SEHEMU YA KWANZA
Safari nzima hakutaka kuzungumza na mtu yeyote hivyo alikuwa amepachika �earphone� masikioni mwake ili hata asiweze kusikiliza watu walikuwa wanazungumza nini mara chache sana alipata nafasi ya kusikia mawili matatu hasahasa pale wimbo ulipokuwa unaisha na kuachia nafasi ya wimbo mwingine kuingia, katika kibegi chake kidogo alikuwa na takribani betri nne zilizokuwa zimechajiwa usiku uliopita ili asipatwe na usumbufu wa kuzimikiwa simu katika safari yake hiyo ndefu kiasi ya kuelekea wilayani Serengeti mkoa wa Mara.
Hivi wazazi wangu ni wendawazimu�sasa waliniita Michael ili iweje kwa nini hawakuniita hata Masumbuko?. Alijiuliza kijana huyu mrefu wa wastani ambaye umbo lake kwa kumtazama ungemkadiria kuwa na miaka ipatayo thelathini lakini kiukweli ndio kwanza siku tatu zilizopita alikuwa ametoka kusheherekea kutimiza miaka ishirini na tano siku ambayo ilianza vizuri sana asubuhi kwa kupokea jumbe tofautitofauti kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki waliokuwa wanaikumbuka tarehe hiyo. Karibia kila mmoja alimtakia heri na fanaka katika maisha yake, huku wakikumbuka pia kumtakia aishi miaka mingi. Kuna ujumbe mmoja alioutegemea lakini hadi wakati huo hakuwa ameupata!!!!
Joyce atakuwa ameisahau hii siku au kuna tatizo jingine?? Michael alijiuliza baada ya kutouona ujumbe wake kati ya jumbe zote alizopokea. Kwa kuwa Joyce hakuwa akikaa mbali sana na mtaa anaoishi Michael jijini Dar es salaam, basi Michael alitumia fursa hii kwenda kumpa surprise rafiki yake huyo wa kike tangu utotoni japo hawakuwahi kuvuka urafiki na kuwa wapenzi lakini ndipo walikuwa wanaelekea. Alitaka kuifanya siku hii iwe ya kukumbukwa.
Michael alikuwa anatabasamu njia nzima, kwani aliamini kuwa ile hali tu ya kumkumbusha Joyce tukio hili ni lazima atamrukia na kumkumbatia, kitendo ambacho kwa Michael ni zaidi ya zawadi, lile joto la kipekee la binti huyo lingeweza kumchangamsha na kujisikia kweli amezaliwa siku hiyo.
Utajuaje, huenda pia atanibusu?? Alijisemea Michael kisha akafanya kicheko kidogo cha kujilazimisha. Kisha akatikisa kichwa kama vile kuna jambo alikuwa analikataa.
Sasa alikuwa ameufikia mlango. Akalazimika kunyata ili amshtue Joyce, na hatimaye apokee lile kumbatizi maridhawa.
Alichokikuta Michael nyumbani kwa akina Joyce ndicho kilibadili ghafla mipango yake ya kufanyia mazoezi ya vitendo (field) katika jiji la Dar es salaam na kuamua kuelekea mji mdogo wa Mugumu Serengeti mkoa wa Mara bila kutarajia. Hakujua kwa nini ameuchagua mji huo lakini alijikuta katika maamuzi hayo. Maamuzi ya kuishi mbali na uchungu ule. Wivu wa kimapenzi ulimsulubisha na kumpelekesha kwa kiasi kikubwa.
�Lakini kwani nilikuwa nimemtamkia kuwa nampenda?...mimi ni mpuuzi huenda labda ndio maana hakushtuka nilipomkuta.� Alijiuliza Michael huku akijaribu kunywa maji ili kulegeza donge la hasira lililokuwa limemkaba kooni .
�Hivi ninachokasirika ni nini hasa wakati hajui kama nilikuwa namtaka?...ah!! huu ni upuuzi hakika.� Alijiliwaza Michael huku akishindwa kuyanywa yale maji na kuyafunika kisha kuendelea kupata burudani ya muziki baada ya muda alipitiwa na usingizi alikuja kushtuka baada ya mwanamama aliyekuwa pembeni yake kumlaumu kuwa alikuwa anamlalia kila anaposinzia.
�Unasema??.� Aliuliza kwa sauti ya juu Michael baada ya kuwa ameathiriwa na sauti kali ya muziki masikioni.
�Unanilalia bwana!!!.�
�Ah!! Samahani�� Wakati huu alikuwa ameondoa �earphone� masikioni mwake. Safari ilikuwa inaendelea, safari ya kutoka jijini Dar es salaam kuelekea Mwanza kisha mkoa wa Mara. Hii ndio ilikuwa mipango yake. Mipango ya kukimbia maumivu. Kuikimbia vita ya mapenzi badala ya kukabiliana nayo.
Baada ya kuomba radhi alitaka kurejesha tena earphone masikioni lakini alisita kidogo baada ya kuvutiwa na vurumai iliyokuwa inaendelea kati ya makondakta wa hilo basi na mwanadada, kisa kilikuwa ni kukosa nauli kwa huyo dada huku akidai kuna mtu anamlipia yuko nyuma.
�We mbona unasema kuwa kuna mtu analipa na sisi hatumuoni�nenda ukamguse basi mwambie alipe, yaani wewe umepandia njiani halafu unasema kuna mtu anakulipia, acha kutuzingua basi na ujanja wa kizamani. Hakuna lifti siku hizi ujue� Kondakta mmoja alibwatuka kwa ghadhabu akionyesha dhahiri kukerwa na maneno ya yule dada aliyekuwa hajakaa kisafari ndefu kabisa.
�Ebwana anayemlipia huyu dada yuko wapi?? Sisi tunamshusha hivyo.� alitangaza kondakta lakini hakuna aliyejitokeza kubeba mzigo huo.
�Mi sishukiiiii�sishuki, niacheni, niache hukooo, sitaki kushukaa.� Alilia yule dada kwa sauti ya juu huku akiwa ameng�ang�ania mkono wa yule kondakta hapo ni baada ya gari kuwa limesimama ili ashushwe. Kila mtu alikuwa na shughuli zake hakuna aliyejishughulisha na sakata hili kwa asilimia kubwa. Waliojaribu kujishughulisha walikuwa wakitabasamu ama kucheka huku wengine wakiongea sauti za chinichini. Haikujulikana wapo upande upi.
Michael alikuwa bado anaangalia hilo vurumai linavyoendelea, kitendo cha huyo dada kilimkumbusha adha ya usafiri katika jiji alilokuwa ametoka la Dar es salaam lakini kikubwa zaidi ni umasikini unaotawala sehemu kubwa ya Tanzania, lakini kilichomuumiza ni unyanyasaji wa wanawake katika jamii jambo ambalo alikuwa analipinga na hadi kufikia kusomea masuala ya sheria na haki za binadamu akiwa mwaka wa pili katika chuo kikuu cha Dar es salaam na sasa alikuwa anaelekea katika field.
Alikumbuka jinsi alivyokuwa anajisikia vibaya iwapo mzee wake anatokea kumnyanyasa mama yake. Ile hali ikajirudia tena baada ya sakata hili. Moyo ukamuuma!!!
�Nipo naye huyo!!!.� Alitamka kwa sauti kuu Michael. Hakujua maneno haya aliyatoa wapi lakini aliyatamka kiufasaha na kusikiwa na kila abiria ndani ya basi hilo la Najimunisa wakati huo tayari tairi sita za basi hilo zilikuwa katika ardhi ya Dodoma. Watu wote waligeuka kumtazama kwa mshangao huku kondakta akitaharuki na uso wake haukutabasamu bali ulipambwa na ndita zilizomaanisha hasira.
�Sasa muda wote huo ulikuwa wapi kujibu mbona mnaleta ujanja wa kishamba hapa..sasa ulitegemea nitamuacha huyu malaya wako asafiri bure au, acha hizo jombaaa!! Mbona tunatafutiana sababu za kutukana halafu mwishowe mnasema makonda wana matusi.� Kondakta ambaye kimabavu alimzidi Michael alitoa karipio.
�Nauli ni shilingi ngapi??.� Badala ya kujibu lawama za yule Kondakta Michael kwa kujiamini kabisa aliuliza swali bila wasiwasi. Ilikuwa ni kama hakumsikia kipindi anabwatuka.
�Sio ishu hizo kaka�nigei elfu ishirini na tisa hiyo.� Alijibiwa kwa jazba. Taratibu alijipekua na kutoa noti tatu za elfu kumi kumi akampatia akarudishiwa elfu moja.
�Kakae kule nyuma na jamaa yako nafasi inatosha ile pale.� Alielekezwa yule binti ambaye bado machozi yalikuwa yanamtiririka mashavuni na kudondoka chini.
Kwa kusuasua alienda na kujibanabana pembeni ya Michael wakati huo gari zima lilikuwa linaitazama filamu hii tamu ya kusisimua. Binti alipofika pale tayari Michael alikuwa amerejesha �earphone� masikioni mwake na wala hakumjibu alipotoa shukrani ya msaada huo.
Michael alitegemea kumuuliza maswali yule binti baada ya muda fulani. Lakini ajabu mdomo wake ukawa mzito.
Alihofia kuwa kuanzisha kwake maongezi na msichana yule anaweza kuzua mambo mengine. Hakutaka kabisa kujiweka karibu na msichana kimaongezi, aliiona taswira ya Joyce katika uso wa kila mwanamke. Akampuuzia binti yule.
�Mh!! Wanaume wanajua kutesa wanawake da!! Sasa hapo wamegombana nyumbani anauleta ugomvi wao kwenye usafiri ah!!! Ujinga kweli huu.� Alisikika abiria mmoja mwanamke wa makamo akilalamika lawama ambazo hazikupenya katika masikio ya Michael.
�Pole dadangu!!!.� mwanaume mwingine upande wa kulia alimwambia yule binti naye akamjibu kwa kichwa.
Muziki ulipomchosha Michael, akapekua begi lake dogo akaibuka na kitabu. Akakifunua ukurasa alioishia kabla ya kukifunika. CHUKI ndio lilikuwa jina la kitabu kile.
Yule binti ambaye alikuwa mkimya, akajigeuza na kuanza kusoma ukurasa wa mbele wa kitabu kile. Umakini aliouweka ni kama vile kuna kitu alikuwa anafahamu.
�Haa!!� akashangaa kwa sauti ya chini sana kama anajishangaa mwenyewe, Michael akasita kusoma lakini hakumtazama machoni, kisha yule binti akasema, �Huyu jamaa ametoa kingine mh!! Vipi ni muendelezo wa ROHO YA MWISHO au?� Aliuliza kwa furaha binti yule huku akionyesha kumjua vyema mtunzi wa kitabu kile cha hadithi. Kauli za dada huyu zikamgusa Michael, akajikuta akivunja kiburi chake cha kukaa kimya.
�Hamna hiki kipo kivyake tu, ni kali kuliko ROHO YA MWISHO lakini hakifikii HILA� Alimjibu kwa uchangamfu baada ya kugundua kuwa yule dada naye alikuwa akimfahamu mtunzi wa hadithi ile wote walikuwa wakimzungumzia George Iron mtunzi wa vitabu vya HILA, ROHO YA MWISHO na riwaya yake ya kushangaza ya NILIKUFA JANA. Mwandishi aliyeikonga ipasavyo roho yake. Michael akataka kuzungumza mengi juu ya mwandishi huyu, lakini akajionya asiweke mazoea ya ukaribu sana na msichana huyu ambaye hakuwa akimfahamu hata kidogo.
�Vipi hivi unaweza kuwa nacho kile cha HILA maana jamaa alitoa vichache halafu vikapotea kama vile hakutoa. Nasikitika sikupata bahati ya kukisoma.� Alijieleza kwa malalamiko yule dada lakini hakujibiwa na badala yake yule Michael alikichomoa kitabu cha HILA kutoka katika maficho ya begi lake dogowa, akampatia yule binti asiyemfahamu. Alionyesha kujisikia fahari sana kumiliki kazi zote zinazotolewa na mwandishi huyu.
Kimya kikatanda baada ya kila mmoja kujikita katika kusoma simulizi.
Urafiki wao ukaanzishwa rasmi na hobi zao katika kusoma vitabu.
Michael akayasahau machungu ya Joyce kwa muda!!
Akili yake yote ikajikita katika kitabu cha hadithi!!! Chuki!!
Walipoviacha vitabu vyao, mazungumzo yalikuwa mengine. Hawakuwa wakimzungumzia tena mwandishi yule wa vitabu walivyomaliza kuvisoma.
Wakajikuta wanajenga mazoea ya hali ya juu. Cha ajabu hawakuulizana majina. Kila mmoja alikuwa akimtegea mwenzake aanze kuuliza. Huku Michael akijiweka katika tahadhari ya kujikita katika maumivu mengine kwa kumwendekeza yule binti.
Kadri muda ulivyokwenda ndivyo wawili hawa walikuwa kama wapenzi!! Huku yule binti akiifurahia zaidi hali ile.
******
Basi lilikuwa katika mwendo mkali sana hapo likikaribia ardhi ya Shinyanga majira ya saa mbili kasorobo usiku, dereva ambaye tangu safari ianze alikuwa anazungumza mara kwa mara na abiria aliyekuwa pembeni yake alijikuta akifumba macho na kuyafumbua ghafla huku masikio yake yakijibiwa kwa kilio kikali kutoka upande fulani wa gari, ni uzoefu aliokuwa nao ndio sababu pekee iliyozuia gari lile lisipinduke baada ya kulivaa shimo ambalo hakuliona kwa kukosa umakini wakati wa kuendesha.
Gari liliposimama, Michael alikuwa wima, macho yamemtoka pima huku chini akiwepo yule binti ametulia tuli huku akitoa kilio kwa sauti ya chini mno. Abiria kadhaa walisogea kule alipokuwa Michael na kumsaidia kushangaa huku hata mmoja hakuthubutu kumgusa yule binti kwa jinsi alivyokuwa amejikunjakunja katika hali isiyokuwa ya kawaida kabisa.
�Gari ilipopiga lile bonde tulirushwa juu niliweza kumshuhudia akitua kwenye siti yake kwa kishindo halafu�sijui ni nini kimetokea baada ya hapo.� Alizungumza Michael baada ya maswali kumwangukia yeye juu ya kilichomsibu yule binti ambaye watu walimtambua kama mpenzi ama ndugu yake.
�Mambo mengine kujitakia tu tazama sasa huyu wamegombana nyumbani amemnyanyasa kwenye gari hadi ameaibika ona sasa mwisho wake.� Alilalamika mwanamke mmoja aliyeonekana kuguswa sana na hilo jambo.
Michael alitamani sana kujieleza kwamba hafahamiani na yule binti lakini aliamini kwamba hakuna hata mtu mmoja ambaye angeamini hivyo aliendelea kubaki kimya asijue la kufanya. Ile kauli aliyoitoa kuwa yeye yupo na yule binti tayari ikaanza kumuingiza matatani. Na hakuwa na ujanja wa kujinasua. Kauli ile ilisikiwa na wengi!!!
Hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa ujumla haikuwa mbali sana kutoka mahali basi hilo la Najimunisa lilipopatia hiyo tafrani, kwa maamuzi yaliyoafikiwa na kila abiria yule binti walimzoazoa kutoka pale chini na kumweka katika siti ya mbele ambayo ilikuwa na uwezo wa kupokea watu watatu, hakuwa akitokwa na damu lakini alikuwa akigumia kwa sauti ya chini sana, mwanamke mmoja alikaa pamoja naye kwa ajili ya kumsaidia huku Michael naye akiwa karibu yake.
******
Hospitali ya mkoa wa Shinyanga ndio kwanza ilikuwa katika mgomo wa madaktari wakitaka mwenzao aliyewekewa zengwe na kufukuzwa kazi baada ya kushindwa kuokoa maisha ya mtoto wa Kigogo arejeshwe kazini hivyo hakuna huduma zilizokuwa zikitolewa pale licha ya madaktari kuwepo eneo hilo la Hospitali mjini Shinyanga. Kundi la wanaume wanne wakiwa wamembeba mgonjwa wao liliingia kwa uharaka wa kuhitaji huduma pale ndani, hakuna yeyote aliyewakaribisha zaidi ya ukarimu walioupata kwa mlinzi pale mlangoni huku akiwaonea huruma, kila mtu alikuwa bize sana na mambo yake binafsi yasiyoendana na mandhari ya hospitali.
�Nesi nesi�� mwanamme moja aliita lakini alijibiwa kwa jicho kali kisha mwanamama huyo akatoweka. Kwa ujasiri waliamua kujitafutia wodi mojawapo na kumlaza yule binti kitandani kisha wakaanza kuhaha kuwatafuta madaktari ambao hata hawakuonyesha kujali. Mwanzoni walikuwa wanaume wanne pamoja na mwanadada asiyejitambua hata kidogo akiwa katika maumivu makali sana ambayo hakuhitaji kujieleza mwenyewe bali jinsi alivyokuwa ameuma meno na kuikunja sura yake lilikuwa jibu tosha, baada ya muda wakabaki watatu, wawili na hatimaye mmoja Michael!! Ndio alikuwa Michael peke yake pamoja na binti.
Nafsi ya Michael ikaingia katika mgogoro mkali, mgogoro binafsi, maamuzi yalikuwa mengi lakini hakujua lipi ni sahihi. Akiwa katika wimbi la mawazo alisikia anaguswa begani.
�Aah!! Kijana nimekutafuta kweli, ni zaidi ya saa zima sasa nilikuwa napita hapa lakini sijui kwa nini hii wodi nilikuwa naivuka.� sauti nzito kutokana na umri kwenda ilimweleza Michael ambaye alibaki kuduwaa ilikuwa mara yake ya kwanza kufika katika mkoa huu uliotawaliwa na jamii ya wasukuma halafu anatokea mtu anamfahamu.
�Mimi?.�
�Ndio wewe!!!.�
�Aaah!!! Eheee.� aliuliza Michael ili apate kujua shida ya yule mtu.
�Unawahi kusahau wewe, mimi ni yule mlinzi wa pale getini mwanangu poleni sana baba!!!! Pole sana� alijieleza yule mlinzi. Michael hakuwa na kumbukumbu kabisa kwamba pale kwenye basi walipofikia muafaka wa kumwahisha binti hospitali watu walichangachanga walichonacho na kufikisha shilingi laki mbili na nusu ambayo walimkabidhi, alipozipokea mkononi ndivyo hivyo hivyo alizishika hadi waliposhuka na kumfikia mlinzi wa geti, wakati anaandika jina lake katika kitabu cha orodha ya wageni ndio wakati huo huo aliziachia zile pesa na kuzisahau, jambo jema mlinzi huyu aliyejitambulisha kama mzee Matata aliona tukio hilo na kuokoa pesa za Michael na sasa alikuwa amempata kwa ajili ya kumpatia.
Michael alishangazwa na uaminifu aliokuwa nao babu huyu wa makamo mrefu, mwenye mwili uliojengeka na ndevu zake zilizokuwa na mvi kiasi,
�Kwa nini amenirejeshea hizi pesa??.� Alijiuliza Michael
�Asante sana mzee wangu asante sana.� Michael alijaribu kumpatia kiasi fulani cha pesa lakini mzee Matata alikataa kabisa huku akimwonea huruma Michael kwa hali aliyokuwa nayo.
�Ngoja niangalie kama utapata huduma walau ya kwanza maana huyu nani vile anaitwa??.�
�Aaah!!! Mhh!! Huyu?? Anaitwa nanii Mariam eeh!!! Mariam.� alijibu Michael kwa kujiumauma
Mzee Matata alipotoka Michael naye alifikiria kuondoka na kumwacha binti peke yake, akili ilikuwa imemruhusu lakini wakati anapiga hatua mlangoni aliisikia nafsi yake ikimtamkia neno �NIPO NAYE� ambalo alilitaja pale ndani ya basi, nafsi pia ilimsuta kwa pesa aliyorejeshewa na mzee Matata, kwa kutoroka ilimaanisha kwamba amefanya dhulumati na kuweka maisha ya binti katika hatihati. Michael alizishusha pumzi zake kisha akarejea tena pale wodini kusubiria harakati za mzee Matata kama zitazaa matunda.
Michael amejikuta akimsaidia binti asiyemfahamu hata kidogo!!! Hajui kwanini amemsaidia ghafla kiasi hicho�.akiwa hata hajatambua jina la binti huyo yanatokea ya kutokea na sasa wapo hospitali�huduma hakuna kutokana na mgomo!!!!
****Ni HATIA gani inayozungumzwa katika simulizi hii.