Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 22,616
- 33,200
MAKTABA YAPOKEA KITABU CHA MICHAEL MOORE KUTOKA MBALI
Rafiki yangu kipenzi leo adhuhuri kaniletea kitabu cha Michael Moore.
Huyu ndugu yangu ni mpenzi wa Maktaba hii na kaitunuku vitabu vingi.
Kwa wale wenzangu mie wasiomjua Michael Moore hakuna tatizo waingie kwa Prof. Google watapata habari zake zote humo ndani.
Kabla sijasema mengi nataka nikiri kitu.
Mimi sikuwa namjua mwandishi huyu Michael Moore hadi rafiki yangu huyu aliponiletea kitabu chake miaka ya nyuma.
Lakini huyu Michael Moore huu uandishi ni moja tu katika mengi aliyojaaliwa.
Michael Moore kalamu yake na filamu zake anazotengeneza ni kujaribu kuirekebisha serikali ya nchi yake ithamini utu na ubinaadamu ili amani ipatikane duniani.
Sasa kitabu hiki ndugu yangu kaniletea kwa mnasaba huu wa Donald Trump kuwa Rais kigeugeu asiyeweza kuaminika kwa lolote kiasi hata akikuambia rangi ya maziwa ni nyeupe kaulize kwa mtu mwingine.
Kitabu hiki jina lake ni: "Will They Ever Trust Us Again? Letters From the War Zone."
Rafiki yangu kipenzi leo adhuhuri kaniletea kitabu cha Michael Moore.
Huyu ndugu yangu ni mpenzi wa Maktaba hii na kaitunuku vitabu vingi.
Kwa wale wenzangu mie wasiomjua Michael Moore hakuna tatizo waingie kwa Prof. Google watapata habari zake zote humo ndani.
Kabla sijasema mengi nataka nikiri kitu.
Mimi sikuwa namjua mwandishi huyu Michael Moore hadi rafiki yangu huyu aliponiletea kitabu chake miaka ya nyuma.
Lakini huyu Michael Moore huu uandishi ni moja tu katika mengi aliyojaaliwa.
Michael Moore kalamu yake na filamu zake anazotengeneza ni kujaribu kuirekebisha serikali ya nchi yake ithamini utu na ubinaadamu ili amani ipatikane duniani.
Sasa kitabu hiki ndugu yangu kaniletea kwa mnasaba huu wa Donald Trump kuwa Rais kigeugeu asiyeweza kuaminika kwa lolote kiasi hata akikuambia rangi ya maziwa ni nyeupe kaulize kwa mtu mwingine.
Kitabu hiki jina lake ni: "Will They Ever Trust Us Again? Letters From the War Zone."