BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMU YA 36
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Tonny we’re done here.Muda wa mchezo umekwisha sasa ni muda wa kazi” akasema kwa ukali Salvatory huku akipiga simu na mara wakaingia polisi wanne wenye silaha wakamfunga pingu Tonny na kumuongoza kurudi katika seli yake.
“Salvatory kama huniamini naomba basi unipe walau nafasi niweze kufanya mikakati ya kuiokoa familia ya Ithan .Nilimuahidi kuwa nitahakikisha familia yake inakuwa salama”
“Tonny kila kitu kitashughulikiwa na jeshi la polisi.” Salvatory akasema kwa ukali huku akiinama na kukishika kichwa chake.Alikuwa na mawazo mengi mno.
" Umefanya kosa kubwa sana Salvatory ..utaikumbuka siku hii ya leo" akasema Tonny lakini Salvatory hakumuangalia tena.
Tonny akarudishwa katika seli yake na kwa mara nyingine kusudio lake la kutaka kulizuia shambulio la kigaidi lisitokee likagonga ukuta.Alisikia uchungu moyoni kwa kutoitimiza ahadi yake aliyompa Ithan kwamba atahakikisha familia yake inakuwa salama.
ENDELEA..............................................
Baada ya Ithan kushuka katika gari la akina Rahim na kuanza kupiga hatua kuelekea gerezani Rahim na timu yake wakageuza gari na kuvuka ng’ambo ya pili ya bahari.Hawakutaka kukaa karibu na gereza lile kwa sababu walikuwa na wasi wasi kwamba lolote linaweza likatokea hivyo ikawalazimu kuchukua tahadhari mapema.Wakiwa katika ng’ambo ya bahari waliweza kumfuatilia Ithan kupitia mitambo yao iliyokuwa katika lile gari.
Ithan alipoingia katika chumba cha Tonny na kumkabidhi keki , walilitazama tukio hilo katika runinga kubwa iliyokuwamo garini na kila mmoja akabaki kimya akisubiri Tonny ale ile keki
“C’mon Tonny eat that cake” Rahim akanong’ona akiwa ameuweka mkono wake mdomoni .Ghafla kikatokea kitu ambacho hawakuwa wamekitegemea kama kingetokea.Ithan aliupiga ngumi mkono wa Tonny uliokuwa umeishika ile keki na kwa kasi ya ajabu Ithan akamvuta Tonny kutoka katika kile chumba na hakuweza tena kuonekana katika kamera.
“bastard !!! Rahim akasema kwa hasiara huku akiipiga meza kwa mkono wake
“Ithan umefanya nini tena? Rahim akauliza kwa ukali
“Ithan….Ithan…Itha…………..” Rahim akaendelea kuita lakini ghalfa mawasiliano yakakatika.
Huku akitweta kwa hasira akavua spika za masikioni alizokuwa amevaa akazitupa mezani.
" Bastard !!!!..." akafoka Rahim
“Rahim tunafanya nini sasa ..? akauliza mmoja wa vijana wake
Rahim akafuta jasho lililoanza kumtirrika usoni na kusema
“Sielewi tunafanya nini tena.Ithan amebadili maamuzi.Ameamua kumuokoa Tonny asife.Nina uhakika atamueleza Tonny kila kitu na hiyo inaweza ikasababisha kuanza msako mkali wa kututafuta.” Akasema Rahim huku akihema kwa kasi.
“Jamal ,funga kila kitu tulichokiunganisha na kamera zao kule gerezani tuondoke zetu haraka sana hapa.Muda si mrefu wataanza kutusaka.” Akaamuru Rahim na kwa haraka vijana wake wakaanza kazi ya kufunga kila kitu .Baada ya dakika tano kila kitu kikawa tayari na Rahim akamuamuru dereva kuliondoa gari haraka.
“Sikutegemea kama Ithan angeweza kufanya kitendo cha namna hii.” Rahim akasema .Alihisi kuchanganyikiwa.Akaitoa simu yake na kuwapigia wakuu wake jijini Arusha.
“Hallo Rahim.Nipe taarifa za maendeleo.Kazi imekwenda vizuri? Akauliza Sultan.
Rahim akasita kidogo kuongea .Hakujua aseme kitu gani
“Rahim nini kinaendelea huko ? Zoezi la kumuua Tonny limekamilika? Akauliza tena Sultan
“ Sultan …aah….” Rahim akashindwa kuongea.
“Rahim kuna tatizo gani? Akauliza Sultan kwa ukali kidogo
“Sultan..kuna tatizo limetokea.Zoezi lile limeshindikana.” Akasema Rahim kwa sauti ya upole.
“Zoezi limeshindkana? C’mon Rahim how could that happen? Sultan akauliza kwa mshangao
“Kila kitu kilienda kama tulivyokuwa tumepanga na Ithan akafanikiwa kuingia gerezani na akafanya kila tulichokuwa tumemuelekeza .Tulikuwa tukifuatilia kila jambo alilokuwa akilifanya Ithan pale gerezani.Tulihakikisha amempa Tonny keki ile yenye sumu lakini kitu cha kushangaza kilichotokea ni kwamba kabla Tonny hajaitia mdomoni keki ile Ithan alimuwahi akaupiga mkono uliokuwa umeishika ile keki ikaanguka chini na kisha akamtoa Tonny mle chumbani na baada ya hapo mawasiliano na Ithan yakakatika.Hakuweza tena kuonekana katika kamera.Kwa ajili ya usalama wetu ,tumeamua kuondoka eneo tulilokuwa tumejificha.I’m sorry Sultan,I failed you “ rahim akasema na kisha kikapita kimya kifupi.
“Nimekuelewa Rahim.Inaonekana Ithan aliamua kuzuia Tonny asife kwa sababu maalum.Inaonekana alikwisha gundua kwamba hata kama angetekeleza kila kitu mlichomtaka atekeleze,isingekuwa rahisi kumuacha huru na ndiyo maana akaamua kuiacha familia yake na kuamua kumuokoa Tonny.Kwa kuwa alichagua kumuokoa Tonny badala ya familia yake ni wazi atamueleza kila kitu kilichokuwa kimetokea.kwa maana hiyo wanaweza wakaanzisha uchunguzi kuhusiana na suala hilo.Kwa kutegemea suala kama hilo linaweza kutokea mnatakiwa mfanye hivi,msiwafanye lolote familia ya Ithan kwa sasa.Lengo la kuwafanya hivyo ni ili kulifanya jeshi la polisi kuelekeza nguvu zake katika kuitafuta familia ya Ithan na kutupa sisi wasaa wa kutekeleza shughuli yetu hapa Arusha bila vikwazo.Suala hili badi halinipi shida kwa sababu mtandao wetu ni mkubwa na kila kitu kimepangwa kwa umakini mkubwa sana.Kwa hiyo endeleeni kuishikilia familia ya Ithan hadi hapo baadae mtakapopata maelekezo mengine.Kwa sasa msifanye kazi yoyote ile ila kaeni tayari tayari kwani muda wowote inaweza ikatokea kazi ya kufanya “ Sultan akamwambia Rahim na kukata simu.
**************************
Tonny alikuwa ameketi kitandani baada ya kurudishwa katika seli yake.Jasho lilikuwa likimtiririka.Akasimama na kuzunguka zunguka mle chumbani akakaa tena kitandani
“Nimeponea tundu la sindano.Bila Ithan ningekuwa nimekwisha fariki muda mrefu.Kwa sasa ninaamini kweli kuna jambo linakwenda kutokea Arusha.Watu hawa tayari wana mtu wao katika idara yetu ya ujasusi na ndiyo maana kwa haraka hivi tayari wanataarifa kwamba ninafahamu mpango wao na ndiyo maana walifanya juu chini ili waniue.Kinachoniuma ni kwamba ninafahamu kinachokwenda kutokea huko Arusha lakini sina namna ya kufanya kuweza kulizuia shambulio hilo nikiwa humu gerezani.Serikali niliyoitumikia kwa muda mrefu na kwa uadilifu mkubwa hainitambui tena.Viongozi wangu kwa sababu wanazozijua wao wenyewe waliamua kunitelekeza hapa gerezani.Ninaozea hapa gerezani bila msaada wowote na sielewi nitatoka lini .Kama nisingekuwa nimefanyiwa hivi walivyonifanyia ningeweza kutafuta namna ya kuweza kulizuia shambulio hili lisitokee lakini kila nikikumbuka jinsi nilivyotelekezwa humu gerezani najikuta sina tena hamu ya kufanya jambo lolote lile .” Akawaza Tonny kisha akainama akaitazama keki ile iliyoletwa na Ithan ambayo ilikuwa na sumu
“Ithan ameyaokoa maisha yangu leo.Nasikitika kwa sababu sina uwezo wa kuweza kumsaidia kuiokoa familia yake ambayo inashikiliwa na hawa magaidi.Baada ya Ithan kushindwa kutimiza matakwa yao hawatakuwa na manufaa na familia yake hivyo watawatekeza wote.Inauma sana lakini sina namna ya kufanya kuzuia hilo lisitokee.”
Wakati akiwaza hayo mara mlango ukafunguliwa na akaingia mkuu wa gereza Mr Salvatory akiwa na maafisa wanne wa polisi.Watau kati yao walikuwa na wamevaa sare na mmoja hakuwa amevaa sare
“Tonny hawa ni maafisa toka jeshi la polisi ambao wamekuja kuchukua maelezo yako kuhusiana na tukio lililotokea leo.Watakuuliza maswali machache kuhusiana na kilichotokea leo.Naomba uwape ushirikiano mzuri ili kwa pamoja tuweze kusaidia kuiokoa familia ya Ithan” akasema Salvatory .
“Bwana Tonny ,tumepata taarifa kutoka kwa askari magereza ajulikanaye kwa jina la Ithan akidai kwamba ulimtuma apeleke barua katika ofisi ambazo ulikuwa ukifanya kazi kabla hujawekwa humu gerezani.” Akauliza afisa wa kwanza ambaye alikuwa na cheo cha mkaguzi wa polisi.
Tonny akawaangalia maafisa wale kwa zamu na kusema
“Ndiyo nilimtuma”
“Unaweza ukatueleza ujumbe huo uliomtuma ulihusu nini?
Tonny akafikiri na kusema
“Niliwaandikia ujumbe ule kuwakumbusha kwamba washughulikie suala langu kwani miaka inazidi kwenda na sielewi ni lini nitatoka gerezani.” Akadanganya .Salvatory akamuangalia kwa macho makali ya mshangao
“Una hakika hicho ndicho ulichokiandika Tonny? Akauliza Salvatory hukuakimkazia macho
“Ndiyo Mr Salvatory .Hicho ndicho nilichokiandika” akasisitiza Tonny
“Jana usiku watu wasiojulikana wamemvamia Ithan nyumbani kwake na kumteka yeye na familia yake na kuwapeleka mahala kusikojulikana na kisha wakamuamuru Ithan aingie kazini na ili familia yake iwe huru alitakiwa kutekeleza yale yote watakayomuamuru.Kwa ajili ya kuiokoa familia yake ilimlazimu kufanya kila walichomtaka kukifanya.Maelekezo waliyompa ilikuwa ni kuhakikisha kwamba anafanikiwa kukufikia na kukupa keki ambayo inasemekana kuwa na sumu na lengo la watu hao lilikiwa ni kukuua kwani kwa mujibu wa maelezo yao hao jamaa ni kwamba kuna mambo unayoyafahamu ambayo hukupaswa kuyajua.Unaweza ukatuambia ni mambo gani hayo unayoyafahamu yaliyopelekea mtiririko huu wa matukio ya utekaji nyara na wewe kutakiwa kuuawa?
Tonny akawatazama maafisa wale wa polisi halafu akatabasamu na kusema
“Ndugui zangu nadhani nyote mnafahamu kazi niliyokuwa naifanya.Katika kazi kama hii ni wazi lazima utafahamu mambo mengi sana na siri za watu mbali mbali .Ni muda mrefu sasa nimekuwa humu gerezani na siwezi kukumbuka ni jambo gani hasa ninalolifahamu ambalo linaweza likawafanya watu hawa wapange mpango wa kuniua .Ninachofahamu ni kwamba kazi hii ya ujasusi inakufanya uwe na maadui wengi sana wa ndani na nje ya nchi kwa maana hiyo inawezekana watu hao wakawa ni maadui zangu na wana lengo la kulipiza kisasi.” Tonny akaendelea kudanganya.Salvatory akaghafilika
“C’mon Tonny.Hebu sema ukweli wako.Muda ule wakati unataka nikupe nafasi ili uweze kuiokoa familia ya Ithan ulisema kwamba kuna jambo kubwa unalolifahamu na ambalo limepangwa kufanywa na watu hao walioiteka familia ya Ithan lakini nikakukatalia na kukwambia kwamba suala hilolinatakiwa kushughulikiwa na vyombo vya usalama.Nakushangaa unapotoa taarifa za tofauti kwa maafisa wa polisi.Maafisa hawa wamekuja hapa ili kupata mwanga wa nini kinachoendelea na kuanza mchakato wa kuiokoa familia ya Ithan na hatimaye kuzuia hicho unachosema kinaweza kutokea.Tafadhali Tonny,kama kuna jambo lolote unalolifahamu ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi tafadhali naomba uliweke wazi kwa maafisa hawa wa jeshi la polisi ambao watalifanyia kazi.” Akasema Salvatory
Tonny akamtazama tena Salvatory na kusema
“Salvatory mambo yote niliyokuambia hayakuwa ya kweli.Nilikudanganya ili niweze kupata nafasi ya kutoroka gerezani.Hakuna hata suala moja lililokuwa na ukweli.Samahani sana kwa hilo” akasema Tonny na kuzipandisha hasira za Salvatory
“Bastard !!…. Kumbe muda wote huu ulikuwa na unanichezea akili yangu? Akasema kwa hasira Salvatory ikamlazimu afisa mmoja wa polisi amtulize
“Tonny ,kama kuna jambo lolote unalolifahamu linaloweza kutusaidia kuiokoa familia ya Ithan pamoja na askari magereza ambaye naye anashikiliwa na watu hawa tafadhali tueleze.Kumbuka kwamba ni Ithan ndiye aliyeyaokoa maisha yako leo hii.Tafadhali tunaomba ushirikiano wako” akabembeleza mkaguzi yule wa polisi
“Afisa,namshukuru sana Ithan kwa kuyaokoa maisha yangu.Nina deni kubwa kwake .Laiti kama ningekuwa nikifahamu lolote ambalo lingesaidia katika kuipata familia ya Ithan ningewasaidia lakini kwa sasa sina chochote ninachokifahamu.Mnaweza kuniruhusu kupumzika tafadhali? Akasema Tonny.
Maafisa wale wa polisi wakiongozwa na mkuu wa gereza la Uwangwa Mr Salvatory wakaondoka mle chumbani kwa ahadi ya kwenda kuendelea na uchunguzi wa jambo lile na kuahidi kurejea tena baadae kama kungekuwa na jambo lolote ambalo wangehitaji ufafanuzi kutoka kwa Tonny
“ Nimemuudhi sana Salvatory lakini nilifanya vile kwa sababu maalum.Suala hili ni gumu na linapaswa kushughulikiwa na vyombo vinavyohusika na ugaidi.Sina maana kwamba jeshi la polisi hawana uwezo wa kushughulikia suala hili lakini kuna vyombo mahsusi vyenye watu wenye mafunzo ya hali ya juu katika kukabiliana na mambo kama haya ya kigaidi.Kwa kuwa idara ya ujasusi wameamua kulipuuza onyo langu sioni tena kama kuna haja yoyote ya kuendelea kuumiza kichwa kuhusiana na kinachokwenda kutokea.” Akawaza Tonny halafu akajilaza kitandani.
Akiwa amejilaza kitandani mlango ukafunguliwa tena na akaingia mkuu wa gereza akiwa amefura kwa hasira
“Tonny nimerudi tena safari hii nikiwa mwenyewe.Naomba unieleze ni kwa nini uliamua kuichezea akili yangu kwa kunidanganya na kunifanya nihatarishe usalama wa gereza? Iwapo ningekupa nafasi kama ulivyokuwa ukiomba halafu ukatoroka unahani ningekwua wapi mida hii? Nilikwisha anza kukuamini lakini baada ya kukiri kwamba ulikuwa ukinidanganya kwa dhumuni la kutoroka nilipatwa na hasira kali sana .Kwa nini uamue kufanya hivyo Tonny? Kwa nini uamue kunidanganya? Tonny naomba unipe majibu haraka sana “ akasema Salvatory akiwa amevimba kwa hasira
“Mr Salvatory ,nakufahamu wewe ni mtu makini na mwerevu.tafadhali punguza hasira na unisikilize kwa makini” Tonny akasema.
“I didn’t lie to you.” Akasema Tonny
“Yote niliyokueleza yalikuwa ni mambo ya kweli. Taarifa nilizonazo ni taarifa nyeti sana ambazo zinahusiana na usalama wa taifa kwa maana hiyo siko tayari kumweleza kila mtu na kama unavyojua kwamba kwa sasa sioni mtu yeyote wa kumuamini kwa sababu tayari kuna mawakala karibu kila idara nyeti ya serikali ambao wanadaka kila taarifa na kuzipeleka kwa watu wao .”
“Damn you Tonny..kila mara unasema una taarifa nyeti..kwa nini sasa hutaki kuziweka wazi tarifa hizo ili zifanyiwe kazi? Akafoka Salvatory
“Mr Salvatory ningependa sana kuzitoa tarifa hizi ili zifanyiwe kazi lakini ninasita kufanya hivyo kwa sababu sioni mtu wa kumwamini kwa sasa.Nimejaribu kuitaarifu idara yangu lakini kupitia huko ndiko taarifa hizi zimevuja na kusababisha tukio la kutekwa kwa familia ya Ithan.”
“Tonny kama huna mtu mwingine unayeweza kumuamini tafadhali naomba uniamini mimi.Start with me” akasema Salvatory
“Salvatory naomba unisikilize kwa makini sana.” Akasema Tonny huku akimsogelea Salvatory
“jambo ninalolifahamu linalokwenda kutokea ni jambo zito na halitasahaulika kwa vizazi hadi vizazi.Napenda nikuhakikishie kwamba hakuna mtu anayeweza kuzuia jambo hilo lisitoke zaidi yangu.Ni mimi pekee ambaye nina uwezo wa kulizuia suala hilo kwa sababu ninafahamu wapi pa kuanzia na nini cha kufanya.Waluioniweka hapa ndani walisahau kwamba bado taifa hili linanihitaji.Angalia haya maajabu mimi niliye gerezani nina taarifa nyeti sana za usalama wa taifa hili lakini wao walioko huru hawaelewi chochote. Kwa bahati mbaya sana sintaweza kufanya jambo lolote la kuzuia jambo hilo baya kwa taifa letu lisitokee kwa sababu ninaozea humu gerezani na hakuna hata mmoja anayeukumbuka mchango wangu kwa taifa hili.Kama watakuwa wakiutambua na kuuthamini mchango wangu kwa taifa hili basi huu ni wakati wangu wa kuniachai huru” akasema Tonny
“Tonny naomba ufahamu kwamba kuwa na taarifa muhimu inayohusu usalama wa nchi na ukashindwa kuiwasilisha kwa vyombo husika ili ifanyiwe kazi ni kosa kisheia na kama kutatokea tukio lolote la umwagikaji wa damu basi damu yote itakayomwagika itakuwa juu yako.Damu za watanzania zinakulilia Tonny.Tafadhali waokoe na jambo hilo linalokwenda kutokea.”Salvatory akasisitiza
“Damu ya watanzania haitakuwa juu yangu mimi bali itakuwa juu ya wale walioamua kuniweka humu gerezani kwa manufaa yao wenyewe na kusahau mchango wangu kwa taifa hili.Sikufichi salvatory kinachokwenda kutokea hakitaweza kufutika kwa vizazi na vizazi vya nchi hii” Tonny akasema
“C’mon Tonny tell me what to do to stop that !! Akasema Salvatory kwa ukali
‘You want to know what to do to stop what’s going to happen? Get me prime minister..nahitaji kuongea na waziri mkuu uso kwa uso..Kama ikishindikana kuongea na waziri mkuu basi jiandaeni kwa msiba wa kitaifa” Tonny akasema
“Tonny ngoja nijitahidi nione nitakachoweza kukifanya ili kumpata waziri mkuu”
akasema Salvatory huku akitoka mle chumbani kwa kasi
“Ninamfahamu vizuri mheshimiwa waziri mkuu .kama nikimueleza vizuri kuhusiana na suala hili anaweza akanisikiliza na kunitoa humu gerezani.Kama hawatakuwa tayari kunitoa humu gerezani sintaweza kuwasaidia kwa lolote lile.Wajiandae kwa msiba wa kitaifa.” Akawaza Tonny.
*********************
Saa sita na dakika kumi na saba za mchana ndege ya kwanza iliyowabeba wageni wanaokuja kuhudhuria mkutano wa Sulivan wakitokea nchini Marekani ikatua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro. Ulinzi mkali ulikuwa umeimarishwa uwanjani hapo. Kila kona ya uwanja huu askari walikuwa wakizunguka na kuhakikisha kwamba hakuna tukio lolote lenye kuhatarisha amani linaweza kutokea.Wageni walianza kushuka ndegeni na kila aliyeshuka alikuwa akitabasamu.Wengi wa wageni hawa ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuigusa ardhi ya Tanzania.Vikundi mbali mbali vya ngoma za asili vilikuwepo uwanjani kwa ajili ya kuwaburudisha wageni ambao hawakusita kuonyesha furaha yao na wengine walioshindwa kujizuia wakajiunga na wenyeji wao katika kucheza ili mradi ikawa ni furaha kubwa hapo uwanjani.Mabasi manne yalikuwa yameandaliwa kwa ajili ya kuwabeba wageni na kuwapeka katika hoteli walizokuwa wameandaliwa.Msafara wa magari hayo ulitanguliwa na piki piki ya polisi ili kuongoza njia na nyuma kabisa kulikuwa na gari mbili za wanausalama.Kila mahala walikokuwa wakipita wageni hawa walikuwa wakiwapungia mikono wenyeji na kuonyesha furaha yao ya kukanyaga tena ardhi ya Afrika kwani wote waliamini kwamba afrika ndilo bara la asili yao.
Safari yao ikaishia katika hoteli ya kimataifa ya Arusha green Valley ambayo ndiko wageni wengi walipangiwa kukaa.pale nje kulikuwepo vikundi mbali mbali vya ngoma za kiasili vilivyowatumbuiza wageni na kuwafanya wazidi kufurahi.
***************
Saa saba za mchana mlango wa chumba cha Tonny ukafunguliwa na akaingia Salvatory mkuu wa gereza.Alikuwa na uso uliosawajika sana Bila kupoteza muda akasema
“Tonny ninaufahamu mchango wako katika nchi hii.Umefanya mambo mengi sana mazuri kwa nchi hii.Kusema ukweli sifahamu ni kwa kosa gani umefungwa hapa gerezani na ndiyo maana siku zote nimekuwa nikihakikisha kwamba unapata kila aina ya huduma unayoitaka hapa gerezani.Ninaamini maneno yako kwamba kuna jambo ambalo unalifahamu linakwenda kutokea na ninapenda kukuhakikishia kwamba niko nawe bega kwa bega katika kuhakikisha kwamba suala lako linamalizika haraka iwezekanavyo na unaruhusiwa kutoka gerezani ili ukashughulikie jambo hilo .Nimejaribu kufanya kila linalowezekana ili kumpata waziri mkuu kama ulivyokuwa umeomba lakini jibu nililolipata linakatisha tamaa sana” akasema Salvatory
“Umepata jibu gani? Akauliza Tonny
“Nimempata waziri mkuu katika simu na nikamueleza kila kitu akadai kwamba kama kuna kitu unakifahamu kuhusu jambo lolote lile linalohusu usalama wa taifa basi uniambie ili niweze kuliwasilisha sehemu husika.Amedai kwamba hana muda kwa sasa ametingwa na shughuli nyingi za kiserikali”
Huku akitabasamu Tonny akasema
“nashukuru sana Salvatory kwa kuniamini .Kama waziri mkuu naye amekataa kuja kunisikiliza basi hakuna tatizo lakini nina imani siku moja watanifuata wao wenyewe humu gerezani lakini watakuwa wamekwisha chelewa sana.Ahsante sana kwa msaada wako Mr Salvatory” akasema Tonny kwa kukata tamaa.
“Juhudi zote za kunitoa humu gerezani zimeshindikana kabisa.Ninamuachia Mungu suala hili pengine siku moja nitafanikiwa kutoka humu gerezani” akawaza Tonny akiwa ameinamisha kichwa akiwaza.
USIKOSE SEHEMU IJAYO........................................