mtugani wa wapi huyo
JF-Expert Member
- Dec 5, 2012
- 1,239
- 1,477
- Thread starter
- #61
BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMU YA 26
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kwa mara nyingine tena ,nchi yetu imepewa heshima kubwa kuandaa mkutano huu mkubwa.Ni nchi nyingi zingetaka kupewa ziandae mkutano huu lakini sisi tumeonekana tunafaa kupewa nafasi hii adimu.Ni heshima kubwa sana kwetu.Hii ni fursa nzuri kwetu kuitangaza nchi yetu,kutangaza maliasili zetu,bidhaa zetu ,ikiwa ni pamoja na wafanya biashara wetu kutanua wigo wa biashara zao kimataifa.Nashukuru kwamba katika maadalizi yenu mmeyazingatia hayo yote.” Waziri mkuu akatulia na kwa mara nyingine tena ukumbi ukapiga makofi ya kushangilia.
“Ndugu zangu sihitaji kusema mengi kwa sababu bado tuna ziara ndefu ya kuzungukia sehemu mbali mbali kukagua maandalizi yanavyokwenda.Ni matumaini yangu kwamba ndani ya muda mfupi ujao yale mambo yote ambayo yalikuwa hayajakamilika ,yatakamilishwa ili tujiridhishe kwamba hakuna tatizo lolote kubwa litakalojitokeza zaidi ya changamoto ndogo ndogo zitakazojitokeza wakati wa mkutano.Narudia tena kuwapa hongera kwa kazi nzuri mliyoifanya na ninawatakieni mafanikio katika kumalizia yale mamboyote ambayo bado hayajakamilika.” Waziri mkuu akasema na kukaa chini huku akisindikizwa na makofi ya kushangilia.Baada ya shughuli ile iliyompeleka pale kumalizika mheshimiwa waziri mkuu akaondoka na kwenda kuendelea na ziara yake ya kukagua maandalizi mengine yanayohusiana na mkutano ule.
ENDELEA…………………………………………
UWANGWA PRISON – KIGAMBONI DAR ES SALAAM
Gereza la Uwangwa lilikuwa ni gereza kubwa na la kisasa kabisa kuwahi kujengwa nchini Tanzania.Gereza hili lililojengwa Kigamboni jijini Dar es salaam lilikuwa ni maalum kwa ajili ya kuwahifadhi wafungwa wenye makosa makubwa kama ya mauaji,wafungwa wanaosubiri kunyongwa na pia wafungwa wa kisiasa.Gereza hili pia limekuwa likihifadhi watuhumiwa wa makosa mbali mbali mbali ya kivita ambao kesi zao zinaendelea kusikilizwa katika mahakama kuu ya makosa ya jinai ya Afrika iliyojengwa jijini Arusha.
Baada ya kufanikisha kukamatwa tena kwa Abdool bin sahel mtu aliyeratibu milipuko ya mabomu katika balozi za marekani jijini Dar es salaam na Nairobi aliyekuwa ametoroshwa na mtandao wa alqaeda,Tonny alikuwa amewekwa kizuizini katika gereza hili kubwa .Miaka miwili imekwisha pita sasa tangu awekwe kizuizini na hakuwa akijua ni lini atakuwa huru.Tonny amekuwa ni mtu mwenye kuishi kwa uchungu mwingi na hakuwa akitaka kuonana na mtu yeyote yule..
Haikuwa siku ya kutazama wafungwa na mahabudu lakini nje ya ofisi ya mkuu wa gereza la Uwanga mwanadada mrembo aliyevalia suruali ya jeans ya bluu na fulana nyeupe akiwa na nywele ndefu zilizosukwa kwa ustadi mkubwa,alikuwa akisubiri mkuu wa gereza amalize mkutano wake na wageni waliokuwamo mle ofisini.Toka saa tatu asubuhi mwanadada huyu mrembo kupindukia alikuwa hapa akisubiri kuonana na mkuu wa gereza.
Saa sita za mchana ndipo mkuu wa gereza alipomaliza kikao chake na wale wageni.Baada ya wageni wale kuondoka katibu muhtasi wa mkuu wa gereza akamwita yule dada na kumkaribisha kuonana na Bw.Salvatory mpimwe mkuu wa gereza la uwanga.Baada ya kuingia mle ofisini dada yule alijitambulisha kama Slish McBenard akitokea jijini Washington Dc marekani.
“Karibu sana Slish.Naitwa Salvatory Mpimwe,mkuu wa gereza hili” akajitambulisha bw Salvatory.
“Mr Salvatory nimekuja toka Marekani kwa lengo moja tu la kuonana na rafiki yangu aitwaye Tonny mkisa ambaye nimeelekezwa kwamba anashikiliwa katika gereza hili.Tonny amekuwa rafiki yangu mkubwa kwa muda mrefu .Baada ya kuona kimya kimekuwa kingi na hakuna mawasiliano baina yetu niliamua nije nimtazame ili nijue ni kitu gani kimemsibu.Baada ya kufika hapa nikaambiwa kwamba anashikiliwa katika gereza hili.Kwa hiyo Mr salvatory nimekuja hapa ili niombe nipatiwe nafasi ya kuonana na Tonny walau hata kwa dakika kumi kwa sababu natakiwa kurudi Marekani leo jioni.”
Slish akasema huku akitoa baadhi ya nyaraka zake za kuthibitisha kile alichokuwa akikisema .Salvatory akazipitia nyaraka zile ikiwa ni pamoja na tiketi ya ndege inayoonyesha kwamba anatakiwa kuondoka na ndege ya saa kumi na mbili za jioni kurejea nchini Marekani.Baada ya kumaliza kuzipitia nyaraka zile akamwangalia Slish usoni kwa makini halafu akasema
“Slish ,ni kweli Tonny anashikiliwa katika gereza hili kwa muda sasa .hatuwezi kusema kwamba amefungwa lakini amezuiliwa hapa kwa kwa ajili ya uchunguzi wa mambo Fulani ya kiserikali.Uchunguzi huo bado unaendelea.Pamoja na safari ndefu ya kutoka Marekani mpaka hapa kwa lengo moja tu la kumuona rafiki yako Tonny ,napenda kukutaarifu kwamba siku ya leo si maalum kwa ajili ya kutazama wafungwa na mahabusu.Ili kuonana na rafiki yako unatakiwa kufika hapa katika siku iliyotengwa maalum kwa ajili hiyo.Ili kukusaidia itanilazimu kuvunja taratibu za gereza na kukuruhusu uonane na Tonny kwa siku ya leo.Ni kinyume cha utaratibu kufanya hivi lakini kutokana na kwamba hutaweza kusubiri hadi siku hiyo ifike kwa kuwa unatakiwa kuondoka leo nitakupeleka ukaonane na Tonny. Ila kwa tahadhari ni kwamba kwa siku za karibuni Tonny amekuwa ni mtu asiyetaka kuonana na mtu yeyote.Kwa mujibu wa madaktari wetu ni kwamba Tonny anasumbuliwa na tatizo la kisaikolojia.Kuwa mwangalifu sana wakati ukiongea naye.”
Mkuu wa gereza akainuka akamwambia Slish amfuate.
“Umefahamiana na Tonny lini? “ Bw Salvatory akamuuliza Slish wakati wakitembea kuelekea katika chumba ambacho wafungwa hukitumia kukutana na ndugu na jamaa zao
“Tonny nimefahamiana naye miaka kama saba iliyopita alipokuja Marekani kusoma.Toka wakati huo tumekuwa marafiki wakubwa” Slish akajibu kwa ufupi.Salvatory hakuuliza tena swali lingine.
Mwendo wa kama dakika kumi na mbili hivi,wakawasili katika chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na meza kadhaa.Salvatry akamwelekeza Slish akae katika meza moja asubiri pale wakati akienda kumchukua Tonny.
Pamoja na kwamba kila kitu katika gereza lile kilikuwa kikiongozwa na mitambo maalum ya usalama,lakini bado chumba cha Tonny kiliendelea kulindwa na askari wawili wenye silaha kwa saa ishirini na nne.Tonny alifahamika kwa jinsi alivyokuwa mtu hatari hivyo hawakutaka kumpa nafasi hata ndogo ya kutoroka gerezani.
Salvatory akasalimiwa kijeshi na askari magereza wale waliokuwa wakilinda chumba cha Tonny ,akaitikia salamu ile halafu akachukua redio call toka kwa mmoja wa wale askari akaomba afunguliwe chumba namba 22D,.Sekunde chache baadae lango likafunguka akaingia ndani. Tonny alikuwa amejilaza kitandani,akageuza shingo na kumuona aliyeingia mle chumbani kuwa ni mkuu wa gereza ,hakumjali akaendelea kujilaza.
“Habari yako Tonny? Bw Salvatory akasema
Tonny hakujibu kitu wala hakusumbuka kumuangalia
“Tonny ,nafahamu hutaki kuonana na mtu yeyote kwa sasa,lakini nimekuja mwenyewe na ninaomba unisikilze.” Akasema Salvatory huku akimsogelea Tonny ambaye alionekana mawazo yake yalikuwa mbali sana na wala hakuwa na muda wa kumsikiliza.
“Tonny nimekuletea taarifa.Kuna rafiki yako anaitwa Slish amekuja kutoka Marekani kwa ajili ya kukujulia hali.Siku ya leo si siku maalum ya kutazama wafungwa na mahabusu lakini nimeamua kuvunja taratibu za gereza na kumruhusu aje akuone kwa sababu natakiwa leo hii hii aondoke kurudi zake Marekani.Yuko katika chumba cha maongezi akikusubiri.tafadhali Tonny nakuomba kubali kuonana naye,ametoka mbali kwa ajili ya kuja kukuona wewe” Salvatory akasema lakini bado Tonny hakuonekana kumjali wala kumtazama.Mkuu wa gereza akamtazama Tonny kwa sekunde kadhaa na kuita
“Tonny…” tonny hakujibu kitu.
Salvatory hakutaka kuendelea tena kumsisitiza Tonny kuonana na Slish akageuka na kuanza kuondoka zake.Wakati amefika mlangoni Tonny akainuka na kusema
“Wait !!…Salvatory akasimama akageuka na kumtazama Tonny ambaye sasa alikuwa amekaa kitandani.
“Nakwenda kumuona” Tonny akainuka pale kitandani huku akitembea kwa mwendo wa uchovu kuonyesha ni jinsi gani alivyochoshwa na maisha yale ya gerezani.Mkuu wa gereza akiongozana na wale askari wawili wenye silaha wakamuongoza Tonny hadi katika ukumbi wa maongezi ambako Slish alikuwa amekaa akimsubiri Tonny.Mara tu Tonny alipotokeza Slish akasimama huku akionyesha dhahiri kupatwa na mshangao mkubwa kwa kuiona hali ya Tonny.Machozi yalikuwa yakimlenga.Tonny alikuwa amechoka sana.Salvatory akamuongoza Tonny hadi katika meza ile aliyokuwa amekaa Slish .
“Slish rafiki yako huyu hapa.Una dakika ishirini za kuongea naye” Akasema Salvatory huku akiondoka na kuwaacha wale askari wakiwalinda
“Excuse me officers,Could you give us some privacy ?? Slish akawaomba wale askari magereza ambao walimwelewa wakajisogeza pemBeni na kuwaacha Slish na Tonny peke yao mezani. Tonny akamkazia macho Slish halafu akasema
“sina kumbu kumbu kama tumewahi kuonana” Tonny akasema
“Shhhhhh….” Slish akasema huku akiweka kidole mdomoni mwake kumuashiria Tonny anyamaze.
“Nina dakika ishirini tu za kuongea nawe.Naomba niongelee moja kwa moja suala lililonileta hapa.” Slish akasema na kumtazama Tonny usoni.
“Monica amenituma “ Slish akasema na kukaa kimya.
“Monica !!!! Tonny akauliza kwa mstuko.
“ndiyo Monica” Slish akajibu
“Ouh Monica I miss her so much.Anaendeleaje?
“Monica anaendelea vizuri .Pamoja na mambo aliyonituma kwako ,ameniomba nikufikishie salamu nyingi sana .Anasema kwamba hataweza kukusahau katika maisha yake na hatachoka kukusubiri hadi pale utakapokuwa umetoka gerezani” Slish akasema na kumtazama Tonny ambaye alizama ghafla katika mawazo mengi.Ni wazi alikuwa amekumbuka mbali mno.
“Amekutuma nini ? Tonny akauliza
“Amenituma nikupe miwani hii” Slish akasema huku akiitoa miwani Fulani mikubwa katika pochi lake iliyoonekana kama miwani ya jua akamkabidhi Tonny ambaye moja kwa moja alijua miwani ile ilimaanisha nini.Aliitazama miwani ile akaikunjua na kuivaa.
USIKOSE SEHEMU IJAYO..........................................
SEHEMU YA 26
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“ Kwa mara nyingine tena ,nchi yetu imepewa heshima kubwa kuandaa mkutano huu mkubwa.Ni nchi nyingi zingetaka kupewa ziandae mkutano huu lakini sisi tumeonekana tunafaa kupewa nafasi hii adimu.Ni heshima kubwa sana kwetu.Hii ni fursa nzuri kwetu kuitangaza nchi yetu,kutangaza maliasili zetu,bidhaa zetu ,ikiwa ni pamoja na wafanya biashara wetu kutanua wigo wa biashara zao kimataifa.Nashukuru kwamba katika maadalizi yenu mmeyazingatia hayo yote.” Waziri mkuu akatulia na kwa mara nyingine tena ukumbi ukapiga makofi ya kushangilia.
“Ndugu zangu sihitaji kusema mengi kwa sababu bado tuna ziara ndefu ya kuzungukia sehemu mbali mbali kukagua maandalizi yanavyokwenda.Ni matumaini yangu kwamba ndani ya muda mfupi ujao yale mambo yote ambayo yalikuwa hayajakamilika ,yatakamilishwa ili tujiridhishe kwamba hakuna tatizo lolote kubwa litakalojitokeza zaidi ya changamoto ndogo ndogo zitakazojitokeza wakati wa mkutano.Narudia tena kuwapa hongera kwa kazi nzuri mliyoifanya na ninawatakieni mafanikio katika kumalizia yale mamboyote ambayo bado hayajakamilika.” Waziri mkuu akasema na kukaa chini huku akisindikizwa na makofi ya kushangilia.Baada ya shughuli ile iliyompeleka pale kumalizika mheshimiwa waziri mkuu akaondoka na kwenda kuendelea na ziara yake ya kukagua maandalizi mengine yanayohusiana na mkutano ule.
ENDELEA…………………………………………
UWANGWA PRISON – KIGAMBONI DAR ES SALAAM
Gereza la Uwangwa lilikuwa ni gereza kubwa na la kisasa kabisa kuwahi kujengwa nchini Tanzania.Gereza hili lililojengwa Kigamboni jijini Dar es salaam lilikuwa ni maalum kwa ajili ya kuwahifadhi wafungwa wenye makosa makubwa kama ya mauaji,wafungwa wanaosubiri kunyongwa na pia wafungwa wa kisiasa.Gereza hili pia limekuwa likihifadhi watuhumiwa wa makosa mbali mbali mbali ya kivita ambao kesi zao zinaendelea kusikilizwa katika mahakama kuu ya makosa ya jinai ya Afrika iliyojengwa jijini Arusha.
Baada ya kufanikisha kukamatwa tena kwa Abdool bin sahel mtu aliyeratibu milipuko ya mabomu katika balozi za marekani jijini Dar es salaam na Nairobi aliyekuwa ametoroshwa na mtandao wa alqaeda,Tonny alikuwa amewekwa kizuizini katika gereza hili kubwa .Miaka miwili imekwisha pita sasa tangu awekwe kizuizini na hakuwa akijua ni lini atakuwa huru.Tonny amekuwa ni mtu mwenye kuishi kwa uchungu mwingi na hakuwa akitaka kuonana na mtu yeyote yule..
Haikuwa siku ya kutazama wafungwa na mahabudu lakini nje ya ofisi ya mkuu wa gereza la Uwanga mwanadada mrembo aliyevalia suruali ya jeans ya bluu na fulana nyeupe akiwa na nywele ndefu zilizosukwa kwa ustadi mkubwa,alikuwa akisubiri mkuu wa gereza amalize mkutano wake na wageni waliokuwamo mle ofisini.Toka saa tatu asubuhi mwanadada huyu mrembo kupindukia alikuwa hapa akisubiri kuonana na mkuu wa gereza.
Saa sita za mchana ndipo mkuu wa gereza alipomaliza kikao chake na wale wageni.Baada ya wageni wale kuondoka katibu muhtasi wa mkuu wa gereza akamwita yule dada na kumkaribisha kuonana na Bw.Salvatory mpimwe mkuu wa gereza la uwanga.Baada ya kuingia mle ofisini dada yule alijitambulisha kama Slish McBenard akitokea jijini Washington Dc marekani.
“Karibu sana Slish.Naitwa Salvatory Mpimwe,mkuu wa gereza hili” akajitambulisha bw Salvatory.
“Mr Salvatory nimekuja toka Marekani kwa lengo moja tu la kuonana na rafiki yangu aitwaye Tonny mkisa ambaye nimeelekezwa kwamba anashikiliwa katika gereza hili.Tonny amekuwa rafiki yangu mkubwa kwa muda mrefu .Baada ya kuona kimya kimekuwa kingi na hakuna mawasiliano baina yetu niliamua nije nimtazame ili nijue ni kitu gani kimemsibu.Baada ya kufika hapa nikaambiwa kwamba anashikiliwa katika gereza hili.Kwa hiyo Mr salvatory nimekuja hapa ili niombe nipatiwe nafasi ya kuonana na Tonny walau hata kwa dakika kumi kwa sababu natakiwa kurudi Marekani leo jioni.”
Slish akasema huku akitoa baadhi ya nyaraka zake za kuthibitisha kile alichokuwa akikisema .Salvatory akazipitia nyaraka zile ikiwa ni pamoja na tiketi ya ndege inayoonyesha kwamba anatakiwa kuondoka na ndege ya saa kumi na mbili za jioni kurejea nchini Marekani.Baada ya kumaliza kuzipitia nyaraka zile akamwangalia Slish usoni kwa makini halafu akasema
“Slish ,ni kweli Tonny anashikiliwa katika gereza hili kwa muda sasa .hatuwezi kusema kwamba amefungwa lakini amezuiliwa hapa kwa kwa ajili ya uchunguzi wa mambo Fulani ya kiserikali.Uchunguzi huo bado unaendelea.Pamoja na safari ndefu ya kutoka Marekani mpaka hapa kwa lengo moja tu la kumuona rafiki yako Tonny ,napenda kukutaarifu kwamba siku ya leo si maalum kwa ajili ya kutazama wafungwa na mahabusu.Ili kuonana na rafiki yako unatakiwa kufika hapa katika siku iliyotengwa maalum kwa ajili hiyo.Ili kukusaidia itanilazimu kuvunja taratibu za gereza na kukuruhusu uonane na Tonny kwa siku ya leo.Ni kinyume cha utaratibu kufanya hivi lakini kutokana na kwamba hutaweza kusubiri hadi siku hiyo ifike kwa kuwa unatakiwa kuondoka leo nitakupeleka ukaonane na Tonny. Ila kwa tahadhari ni kwamba kwa siku za karibuni Tonny amekuwa ni mtu asiyetaka kuonana na mtu yeyote.Kwa mujibu wa madaktari wetu ni kwamba Tonny anasumbuliwa na tatizo la kisaikolojia.Kuwa mwangalifu sana wakati ukiongea naye.”
Mkuu wa gereza akainuka akamwambia Slish amfuate.
“Umefahamiana na Tonny lini? “ Bw Salvatory akamuuliza Slish wakati wakitembea kuelekea katika chumba ambacho wafungwa hukitumia kukutana na ndugu na jamaa zao
“Tonny nimefahamiana naye miaka kama saba iliyopita alipokuja Marekani kusoma.Toka wakati huo tumekuwa marafiki wakubwa” Slish akajibu kwa ufupi.Salvatory hakuuliza tena swali lingine.
Mwendo wa kama dakika kumi na mbili hivi,wakawasili katika chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na meza kadhaa.Salvatry akamwelekeza Slish akae katika meza moja asubiri pale wakati akienda kumchukua Tonny.
Pamoja na kwamba kila kitu katika gereza lile kilikuwa kikiongozwa na mitambo maalum ya usalama,lakini bado chumba cha Tonny kiliendelea kulindwa na askari wawili wenye silaha kwa saa ishirini na nne.Tonny alifahamika kwa jinsi alivyokuwa mtu hatari hivyo hawakutaka kumpa nafasi hata ndogo ya kutoroka gerezani.
Salvatory akasalimiwa kijeshi na askari magereza wale waliokuwa wakilinda chumba cha Tonny ,akaitikia salamu ile halafu akachukua redio call toka kwa mmoja wa wale askari akaomba afunguliwe chumba namba 22D,.Sekunde chache baadae lango likafunguka akaingia ndani. Tonny alikuwa amejilaza kitandani,akageuza shingo na kumuona aliyeingia mle chumbani kuwa ni mkuu wa gereza ,hakumjali akaendelea kujilaza.
“Habari yako Tonny? Bw Salvatory akasema
Tonny hakujibu kitu wala hakusumbuka kumuangalia
“Tonny ,nafahamu hutaki kuonana na mtu yeyote kwa sasa,lakini nimekuja mwenyewe na ninaomba unisikilze.” Akasema Salvatory huku akimsogelea Tonny ambaye alionekana mawazo yake yalikuwa mbali sana na wala hakuwa na muda wa kumsikiliza.
“Tonny nimekuletea taarifa.Kuna rafiki yako anaitwa Slish amekuja kutoka Marekani kwa ajili ya kukujulia hali.Siku ya leo si siku maalum ya kutazama wafungwa na mahabusu lakini nimeamua kuvunja taratibu za gereza na kumruhusu aje akuone kwa sababu natakiwa leo hii hii aondoke kurudi zake Marekani.Yuko katika chumba cha maongezi akikusubiri.tafadhali Tonny nakuomba kubali kuonana naye,ametoka mbali kwa ajili ya kuja kukuona wewe” Salvatory akasema lakini bado Tonny hakuonekana kumjali wala kumtazama.Mkuu wa gereza akamtazama Tonny kwa sekunde kadhaa na kuita
“Tonny…” tonny hakujibu kitu.
Salvatory hakutaka kuendelea tena kumsisitiza Tonny kuonana na Slish akageuka na kuanza kuondoka zake.Wakati amefika mlangoni Tonny akainuka na kusema
“Wait !!…Salvatory akasimama akageuka na kumtazama Tonny ambaye sasa alikuwa amekaa kitandani.
“Nakwenda kumuona” Tonny akainuka pale kitandani huku akitembea kwa mwendo wa uchovu kuonyesha ni jinsi gani alivyochoshwa na maisha yale ya gerezani.Mkuu wa gereza akiongozana na wale askari wawili wenye silaha wakamuongoza Tonny hadi katika ukumbi wa maongezi ambako Slish alikuwa amekaa akimsubiri Tonny.Mara tu Tonny alipotokeza Slish akasimama huku akionyesha dhahiri kupatwa na mshangao mkubwa kwa kuiona hali ya Tonny.Machozi yalikuwa yakimlenga.Tonny alikuwa amechoka sana.Salvatory akamuongoza Tonny hadi katika meza ile aliyokuwa amekaa Slish .
“Slish rafiki yako huyu hapa.Una dakika ishirini za kuongea naye” Akasema Salvatory huku akiondoka na kuwaacha wale askari wakiwalinda
“Excuse me officers,Could you give us some privacy ?? Slish akawaomba wale askari magereza ambao walimwelewa wakajisogeza pemBeni na kuwaacha Slish na Tonny peke yao mezani. Tonny akamkazia macho Slish halafu akasema
“sina kumbu kumbu kama tumewahi kuonana” Tonny akasema
“Shhhhhh….” Slish akasema huku akiweka kidole mdomoni mwake kumuashiria Tonny anyamaze.
“Nina dakika ishirini tu za kuongea nawe.Naomba niongelee moja kwa moja suala lililonileta hapa.” Slish akasema na kumtazama Tonny usoni.
“Monica amenituma “ Slish akasema na kukaa kimya.
“Monica !!!! Tonny akauliza kwa mstuko.
“ndiyo Monica” Slish akajibu
“Ouh Monica I miss her so much.Anaendeleaje?
“Monica anaendelea vizuri .Pamoja na mambo aliyonituma kwako ,ameniomba nikufikishie salamu nyingi sana .Anasema kwamba hataweza kukusahau katika maisha yake na hatachoka kukusubiri hadi pale utakapokuwa umetoka gerezani” Slish akasema na kumtazama Tonny ambaye alizama ghafla katika mawazo mengi.Ni wazi alikuwa amekumbuka mbali mno.
“Amekutuma nini ? Tonny akauliza
“Amenituma nikupe miwani hii” Slish akasema huku akiitoa miwani Fulani mikubwa katika pochi lake iliyoonekana kama miwani ya jua akamkabidhi Tonny ambaye moja kwa moja alijua miwani ile ilimaanisha nini.Aliitazama miwani ile akaikunjua na kuivaa.
USIKOSE SEHEMU IJAYO..........................................