Riwaya: Bring back our girls

Riwaya: Bring back our girls

BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMU YA 22
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“kazi nzuri sana vijana.Endeleeni kutufuatilia” Nikasema baada ya kumaliza kuwakagua wale jamaa bila kupata chochote cha kuweza kunisaidia.Niwazi vijana wale walistahili pongezi kwa kazi nzuri waliyokuwa wameifanya.kama si wao wakati huu tungekwisha uawa .Niliazimia baada ya suala hili kumalizika ningeongea na wakuu wao wa kazi ili waweze kuangalia namna bora ya kuwatuza vijana wale kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa taifa lao.Kwa sasa hali ilikuwa imetulia na watu walianza kusogelea mahala tulipokuwa tumesimama ili kuishuhudia miili ya watu wale waliouawa kwa risasi.kwa mbali tukasikia ving’ora vya gari za polisi zikija.Nadhani walikwisha pata taarifa.
“Tuondokeni mahala hapa,tuwapishe polisi wafanye kazi yao.Catherine mpigie simu mkuu wa polisi na umtaarifu kwamba unahusika na tukio hili” Nikasema baada ya kuliona gari la polisi likiingia pale kwa kasi kubwa.Sikutaka kuonekana na polisi ,tukaingia katika gari letu na kuondoka

ENDELEA……………………………………..

“Tonny, ninaona kama muujiza kwa jinsi tulivyonusurika kuuawa.Watu hawa tunaopambana nao ni watu hatari sana” Catherine akasema huku akifuta vumbi lililokuwa limemjaa mwilini.Nilimuonea huruma binti yule kwa sababu toka ameanza kazi hakuwahi kukumbana na kadhia ya hatari kama hii.Nikatabasamu na kusema
“Pole sana Catherine.Hapa ndipo kazi hii inapokuwa ngumu.Kifo kinaweza kutokea dakika yoyote ile.Pamoja na yote yaliyotokea , kuna kitu nimekigundua.Kampuni ile ya Chem chem. Sequrity ni wakala wa mtandao wa kigaidi hapa nchini na kwa kupitia kampuni hii wameweza kuingiza silaha ,zana na watu wao katika mpango mzima wa kumtorosha Abdool.Nimepata uhakika huu mkubwa kwa sababu baada ya sisi kuondoka katika ofisi kuu za Chem chem. Sequrity waliamua kutufuatilia kwa vile walijua wazi kwamba tunaelekea katika ofisi zao ndogo ili kuweza kuujua undani wa mtu wao tuliyemuua kule kwa Rachel.Nadhani walikwisha tung’aza sisi ni akina nani na hivyo lengo lao lilikuwa kutumaliza haraka iwezekanavyo.Baada ya kufanikiwa kuwaua watu wao kwa hivi sasa mapambano yatakuwa makali sana.Kitu muhimu kwa sasa ni kumuwahi huyu dada aitwaye Sesi ambaye ndiye anayesemwa kumpeleka Danford katika kampuni ile.Huyu Sesi ni lazima atakuwa anafahamu mambo Fulani Fulani kuhusiana na kampuni hii.iwapo tutampata huyu Sesi anaweza akatusaidia kutupa mwanga Fulani.Kama kuna kitu anakifahamu kuhusiana na kampuni hii basi naye atakuwa katika orodha ya watu wanaotakiwa kuuawa kwa haraka sana.Tunatakiwa tumuwahi” Nikasema
“hata mimi nafikiri hivyo Tonny.Hawa jamaa ni lazima watakuwa wanafahamu kwamba tunaelekea kwa Sesi hivyo watajitahidi kumuwahi Sesi kabla hatujamfikia.Mimi naona ingekuwa vizuri kama ungewasiliana naye ili tujue yuko wapi kwa sasa.” Nilikubaliana na mawazo ya Catherine nikachukua simu na kuzipiga namba za sesi.
“hallow “ Ikaita sauti ya upande wa pili wa simu
“Hallow naongea na nani? Niliuliza
“Sesi hapa anaongea ,nani mwenzangu?
“Mimi ni binamu yake na Danford ,kuna ujumbe amenipa ili nije nikuone ,uko wapi kwa sasa?
“ Kwa sasa niko nyumbani Sinza”
“Sipafahamu nyumbani kwako,naomba unielekeze tafadhali ” Sesi bila hiyana akanielekeza nyumbani kwake..Nikamwambia asitoke anisubiri.

************************

Nilisimamisha gari nje ya nyumba ya Sesi maeneo ya Sinza kama alivyokuwa amenielekeza.Sikuwa na shaka kwamba tumepotea kwani nilifuata maelekezo yote aliyokuwa ametupatia.Nyumba hii haikuwa na uzio wowote ,nje kulikuwa na mitungi minne ya maua.
Baada ya kuhakikisha usalama upo,tukauendea mlango wa mbele na kuugonga.Mlango ukafunguliwa na dada mmoja mnene mfupi
“karibuni” akasema dada yule mwenye macho mazuri.
“Ahsante sana ,habari yako” tukasema kwa pamoja.
“Nzuri karibuni ndani” Alitukaribisha ndani ,tukaingia katika sebule ile kubwa na nzuri.Dada yule alikuwa akituangalia kwa macho yaliyojaa wasi wasi mwingi.nafikiri ni kwa sababu ya kutowahi kutuona hapo kabla.Sikuweza kujua kama huyu ndiye Sesi mwenyewe au siye.
“Tunahitaji kuonana na Sesi,” Nikasema bila kupoteza wakati.
“Sesi ametoka kidogo ameenda hapo nyumba ya jirani.Ila ameacha maagizo kwamba wageni wake wakifika nimpigie simu.Ninyi ndio wageni aliokuwa anawasubiri?” akasema dada yule huku akichukua simu yake.
“Nadhani ni sisi kwa sababu tuliongea naye kwa simu muda si mrefu na akasema kwamba yuko nyumbani.”
Yule dada akaongea na Sesi katika simu halafu akatugeukia.
“Amesema mumsubiri atakuja muda si mrefui” Akasema mwanadada yule huku akilifungua friji na kutupatia juice.Mimi nilikuwa nimekaa katika sofa lililoelekea dirishani.Toka pale nilipokuwa nimekaa niliweza kuona kila aliyekuwa akipita nje ya nyumba.Dakika kumi zikakatika bila ya Sesi kutokea hivyo yule dada akainuka na kwenda kusimama mlangoni kwa lengo la kumfuata dada yake.
“anakuja” akasema yule dada huku akirudi ndani baada ya kumuona dada yake akija .Ghafla lilitokea tukio moja ambalo lilitokea kwa haraka sana .Gari moja dogo jeupe likatokea kwa kasi kubwa sana likielekea katika nyumba ile ya Sesi na mara ikasikika milio ya risasi hatua chache toka ile nyumba ya Sesi Kama umeme nikatoa bastora yangu kwani tayari nilikwisha inusa hatari,nikamfanyia ishara Catherine tukatoka kwa tahadhari kwenda nje.Mita chache toka nyumba ile ya sesi nililiona gari moja likiondoka kwa kasi ya ajabu
“My God” Nilijikuta nikitamka maneno yale huku nikiuma meno kwa hasira
Hatua chache mbele yetu dada mmoja alikuwa amelala katika dimbwi la damu Kwa haraka na kwa tahadhari kubwa nikamuendea na kumchunguza.hakuwa na uhai ,alikuwa amekwisha fariki.Alipigwa risasi nyingi kifuani.Machozi yalikaribia kunitoka baada ya kumsikia yule msichana tuliyemkuta ndani mwa Sesi akipiga yowe la uchungu kuwa yule aliyekuwa amepigwa risasi pale nje ndiye Sesi dada yake .. Sesi alikuwa amelala katika dimbwi la damu.tayari alikuwa amekwisha fariki kitambo.Alikuwa amechakazwa kwa risasi nyingi kifuani.Roho iliniuma sana kwa msichana mrembo kama yule kufa kikatili namna ile.Nikiwa bado nimeinama nikimuangalaia Sesi huku umati wa watu ukianza kujikusanya eneo lile Catherine akaingia katika gari letu lakini nikahisi miguu inaishiwa nguvu baada ya kugundua kwamba tairi za gari letu hazikuwa na upepo,zilikuwa zimepigwa risasi na hivyo gari lisingeweza kutembea tena.Kwa mara nyingine tena walikuwa wametuzidi ujanja.Nywele zikanisimama.Mwili ukachemka kwa hasira.Muda ulizidi kuyoyoma lakini bado hatukuwa na mwanga wowote wapi alipokuwa Abdool.Iwe isiwe Gaidi huyu alitakiwa apatikane siku ya leo
Nilichekecha akili tutafanya nini ili tuweze kuondoka .Watu walikuwa wakija kwa wingi eneo lile nikaanza kuingiwa na wasi wasi pengine wangedhani kwamba sisi ndio tuliohusika na mauaji yale kisha wakaanza kutushambulia.Wakati nimesimama nikijaribu kuchekecha akili mara nikamuona Catherine amechomoka kwa kasi akaelekea katika gari moja lililokuwa limesimama pale karibu na nyumba ya Sesi.Dereva wake alikuwa ameshusha kioo cha gari akishangaa kitu gani kilichokuwa kimetokea pale.Kwa kasi ya aina yake Catherine akamnyooshea bastora na kumuamuru ashuke chini.Bila ubishi dereva yule akashuka ndani ya lile gari. “Tonny twende tuondoke .” Akasema Cathe kwa sauti kubwa.Nilimuacha Sesi pale chini nikaingia katika lile gari alilokuwa ameliteka Sesi.Idadi ya raia ilizidi kuongezeka.Kama nilivyokuwa nimehisi ndivyo ilivyokuwa imetokea,raia wale walikuwa wakija na silaha pamoja na mawe.Ili kupata nafasi ya kuondoka eneo lile salama nilipiga risasi tatu hewani na ndani ya sekunde kadhaa eneo lote likawa jeupe.Kila mmoja alikimbia na kwenda kujificha kujinusuru.Kwa kasi ya ajabu Catherine akaiondoa gari tukaanza kuifukuzia ile gari ya wale watu waliokuwa wamempiga risasi Sesi. .
Moyo ulikuwa ukinienda mbio kwa hofu iliyokuwa imechanganyika na hasira kubwa.Mapambano yalianza kuwa makali sana kwa kadiri dakika zinavyosonga mbele.Kila tunavyojitahidi kupiga hatua moja wao walikuwa wanaturudisha nyuma hatua mbili.Hii ilionyesha ni jinsi gani jamaa walivyokuwa wamejipanga kikamilifu.Hawakutaka kutupatia hata chembe ya nafasi ambayo ingeweza kutupatia mwanga wa wapi alipo Abdool .Muda ulizidi kusonga mbele na bado hatukuwa na mwanga wowote wa wapi alipo gaidi huyu hatari aliyetoroshwa alfajiri ya leo.Inawezekana Sesi alikuwa na taarifa muhimu kuhusiana na wao ndiyo maana wameamua kumuwahi kabla hatujaonana naye.Walifahamu fika kwamba ni lazima tungeonana na Sesi ambaye angeweza kutupatia taarifa muhimu ambazo zingetusaidia kufahamu kuhusiaa na mtandao huu.Kwa kumuua Sesi walikuwa wameturudisha nyuma mno.Kwa sasa hatukuwa tena na chanzo kingine ambacho kingeweza kutupatia taarifa za magaidi hawa.Hali ilikuwa ikiogopesha.Niliamini jamaa lazima wangekuwa wakituwinda na sisi ili watumalize kabisa kwa sababu tayari tumekwisha onekana ni kizingiti kwao.
Wakati nawaza haya Catherine alikuwa akiyapita magari ili kuifukuzia gari la wale jamaa.Niliustaajabia uhodari wake katika kuendesha gari.
“wale pale” akasema Catherine na kunionesha gari aina ya Vitara nyeupe ambayo ilikuwa magari mawili mbele yetu.

*********************

Tuliendelea kuwafuatilia wale jamaa kwa ufundi mkubwa bila ya wao kutambua kwamba walikuwa wakifuatiliwa.Catherine alinifurahisha sana kwa jinsi alivyotumia mbinu za hali ya juu za kijasusi katika kuwafuatilia wale jamaa.Mara gari ya wale jamaa iliwasha taa kuashiria kwamba ilikuwa ikikata kona na kuingia katika mgahawa maarufu ulioko katikati ya jiji.Jamaa wale walipaki gari na kushuka .Toka ndani ya gari lile wakashuka jamaa watatu.Tukiwa ndani ya gari yetu niliweza kuwatazama wale jamaa wakiingia mgahawani.Mmoja ambaye ndiye aliyekuwa dereva wa gari ile alikuwa mweupe mwenye nywele fupi zilizosokotwa kwa mtindo wa rasta.Aliyefuatia alikuwa na asili ya kiarabu ,alikuwa amevaa suti nyeusi iliyomkaa vyema ,macho yake yalifunikwa na miwani myeusi.Wa mwisho alivaa suti ya kijivu na huyu alikuwa mrefu kiasi ,mwembamba na macho yake yalionyesha kuwa hakuwa mtu wa masihara.
Taratibu waliingia ndani ya mgahawa kisha nasi tukashuka toka ndani ya gari.Tulihakiki usalama wetu kwanza halafu kwa tahadhari kubwa tukaingia ndani ya mgahawa.Tulikaribishwa na wahudumu wenye uchangamfu mkubwa.Tukakaa katika meza moja ya pemBeni kabisa.Watu walikuwa si wengi sana.Toka pale tulipokaa tuliweza kuwaona wale jamaa wakiwa wamekaa katika meza moja ambayo haikuwa mbali sana na mlango wa kuingilia pale mgahawani.Tuliagiza vinywaji na kuendelea kunywa taratibu huku tukiendelea kuwachunguza wale jamaa .
“Catherine una uhakika gari uliyokuwa ukiifuatilia ni ya wale watu waliomuua Sesi? Nikamuuliza Cathe baada ya kuona muda unazidi kusonga mbele na wale jamaa wakiwa wametulia bila kuwa na wasiwasi wa aina yoyote.
‘NdiyoTonny.Wakati wewe umeinama pale ukimtazama Sesi mimi niliitazama vizuri gari ile ya wale jamaa japokuwa ilikuwa mbali kidogo.Nina uhakika mkubwa kwamba gari tuliyokuwa tukiifuatilia ni ya wale jamaa.”
“Ok kama ni wao basi lazima watakuwa wanahusika moja kwa moja na mtandao huu na ndio watakaotupatia majibu ni wapi alipo abdool.” Nikasema huku nikiendelea kuwatazama wakinywa mvinyo huku wakiongea.Muda ule ule yule jamaa mwenye asili ya kiarabu na suti nyeusi aliinuka na kuufuata ujia uliokuwa ukielekea maliwatoni.Sikupoteza hata sekunde nami nikainuka.
“cathe ninamfuata yule jamaa anayeelekea chooni.Wakati naelekea chooni wachunguze hawa jamaa waliokaa pale mezani kama wataonyesha dalili zozote za kunitilia shaka.Iwapo wataonyesha wasi wasi wowote basi nitaarifu haraka kwa kubeep simu yangu mara mbili haraka haraka.” Nikamwambia Catherine naye akatikisa kichwa huku akiwa na uso wenye wasi wasi.Hakuwa amekutana na kadhia ya hatari kama hii toka alipoanza kazi.
Nilitembea kwa tahadhari huku nikijaribu kuwachunguza wale jamaa waliokuwa wamebaki pale mezani kama wamenitilia shaka au vipi.Lakini jamaa bado walikuwa wakiendelea na kupata mvinyo na hawakuwa na habari yoyote na mimi.Nilipohakikisha kwamba hawakuwa na mashaka na mimi niliushika ujia uliokuwa ukielekea maliwato .Nilimuomba Mungu watu wasije upande ule kwa dakika chache ili niweze kuimaliza kazi iliyonipeleka kule.Mlango wa vyoo vya wanaume ulikuwa umefungwa.Nikachungulia katika kioo kizito kilichokuwa mlangoni pale nikaiona taswira ya mtu akiwa mle ndani.Nikaishika bastora yangu na kuiweka tayari kisha nikakinyonga kitasa na mlango ukafunguka nikaingia ndani.Mle maliwato alikuwemo yule jamaa peke yake akijisaidia haja ndogo.Nilienda kusimama pemBeni yake na kuanza kufungua zipu ya suruali .Nikampiga chabo yule jamaa na kumuona akimalizia kuifunga zipu ya suruali yake.Sikutaka kupoteza hata sekunde moja .Kwa kasi ya aina yake nikatoa bastora yangu na kumuwekea kichwani .
“Tulia hivyo hivyo ulivyo.Usijaribu kufanya lolote” Nikasema kwa sauti kali.Jamaa hakuamini macho yake .Aliona ni kama njozi .
USIKOSE SEHEMU IJAYO……………….
 
Mimi nipo tokea mwanzo wa stori. Shusha vitu.
 
BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMU YA 23
23
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Nilitembea kwa tahadhari huku nikijaribu kuwachunguza wale jamaa waliokuwa wamebaki pale mezani kama wamenitilia shaka au vipi.Lakini jamaa bado walikuwa wakiendelea na kupata mvinyo na hawakuwa na habari yoyote na mimi.Nilipohakikisha kwamba hawakuwa na mashaka na mimi niliushika ujia uliokuwa ukielekea maliwato .Nilimuomba Mungu watu wasije upande ule kwa dakika chache ili niweze kuimaliza kazi iliyonipeleka kule.Mlango wa vyoo vya wanaume ulikuwa umefungwa.Nikachungulia katika kioo kizito kilichokuwa mlangoni pale nikaiona taswira ya mtu akiwa mle ndani.Nikaishika bastora yangu na kuiweka tayari kisha nikakinyonga kitasa na mlango ukafunguka nikaingia ndani.Mle maliwato alikuwemo yule jamaa peke yake akijisaidia haja ndogo.Nilienda kusimama pemBeni yake na kuanza kufungua zipu ya suruali .Nikampiga chabo yule jamaa na kumuona akimalizia kuifunga zipu ya suruali yake.Sikutaka kupoteza hata sekunde moja .Kwa kasi ya aina yake nikatoa bastora yangu na kumuwekea kichwani .
“Tulia hivyo hivyo ulivyo.Usijaribu kufanya lolote” Nikasema kwa sauti kali.Jamaa hakuamini macho yake .Aliona ni kama njozi .


ENDELEA………………………………….


“taratibu toa bastora yako na uitupe chini “ Nikamuamrisha yule jamaa ambaye alinza kuongea lugha ambayo niliamini ni kiarabu.Sikuwa nafahamu kiarabu kwa hasira nikasema
“Shut up bastard..Slowly take out your gun “ Hakutaka tena ubishi baada ya kuyatazama macho yangu yaliyokuwa yakionyesha nilikuwa tayari kuua muda wowote.Jamaa yule taratibu akaitoa bastora yake na kuiweka chini
Nikamuamuru tena.aipige teke ile bastora ili ije kwangu.Jamaa akainua mguu na kuipiga teke bastora yake ikasogea kwangu .Huku mkono mmoja ukimuelekezea bastora kichwani ,niliinama kidogo ili kuiokota bastora ile ya yule jamaa lakini kumbe nilikuwa nafanya kosa kubwa ,kifundi sana na kwa kasi ya umeme jamaa aliipiga teke la nyuma bastora yangu ,ikaruka juu kisha kufumba na kufumbua nikastukia teke zito likitua usoni ,nikaona kiza na kupepesuka.Kabla sijajiweka sawa nikastukia ngumi mbili nzito zikitua usoni na kunipeleka chini.Niliustaajabu wepesi wa yule jamaa.Ni mtu ambaye alionesha kuwa na mazoezi makali sana ya karate.Nikiwa nimeanguka pale chini nilimuona yule jamaa akiinama kwa ajili ya kuiokota bastora ,nilijitutumua mzima mzima na kumpiga mateke mawili mazito yanayomrusha jamaa hadi ukutani.Niliiwahi bastora yangu pale chini nikaikota na kuinua kichwa nikamkuta jamaa anajizoa zoa pale chini alipokuwa ameanguka.,sikumkawiza nikampa ngumi mbili nzito zinazomrudisha tena chini.Damu ilianza kumtoka mdomoni.Nilimfuata pale chini alipolala na kumkalia tumboni.Moyo ulifyatuka baada ya kugundua kwamba lile tumbo kubwa lililoonekana kama kitambi,hakikuwa kitambi cha kweli bali ni vitu vilivyokuwa vimefungwa.tumboni.Nilipogundua kwamba nimekalia kitu ambacho nilihisi moja kwa moja lingekuwa ni bomu.nilijiinua haraka sana lakini kumbe nilikuwa nimefanya kosa kubwa.jamaa alinipiga teke kali la shingo linalonirusha na kuniangusha kwa mbele.Kwa kasi ya ajabu jamaa akainuka na kutoka kwa kasi akaanza kutimua mbio kurudi mgahawani.Damu ilikuwa ikimchuruzika.Alikuwa akikimbia huku akiongea maneno ya kiarabu ambayo sikuweza kufahamu maana yake kwa kuwa siifahamu lugha hiyo.Nilitamani kumchakaza jamaa kwa risasi lakini niliogopa baada ya kuona watu watatu wakielekea pande zile za maliwatoni.Nikaanza kumkimbiza yule jamaa bastora yangu ikiwa mkononi.Mwarabu yule alikimbia kwa kasi na kwa mbali nikamuona akiwa ameikaribia meza ya wale wenzake ambao walipomuona mwenzao akija anakimbia huku akitamka maneno ya kiarabu wakasima kwa haraka na mara yule mwenzao akawarukia na wote wakaanguka chini .Ghafla kikasikika kishindo kizito sana.Jengo lote la mgahawa lilitetemeka.Nilichoweza kushuhudia ulikuwa ni moshi na vumbi kubwa sana.Ulikuwa ni mlipuko.
Nilihisi maumivu makali na nilipojaribu kuuinua mkono wangu ulikuwa umegandamizwa na kitu kizito.Kwa mbali nikasikia vilio na makelele ya watu kumbu kumbu zikaanza kunirudia .Nilikumbuka kwamba muda mchache uliopita mmoja kati ya watu tuliokuwa tukiwafukuzia alijilipua kwa bomu ili kutuzuia tusimkamate yeye na wenzake.Nilihisi maumivu makali mwili mzima.Nilianza kupatwa na wasi wasi kama Katherine atakuwa ni mzima.Kwa kutumia mkono mmoja nilitumia nguvu na kuanza kujivuta na mkono wangu mwingine ukawa huru japokuwa ulikuwa na maumivu makali.Ulikuwa ukivuja damu mahala nilipokuwa nimeumia jana yake nilipokuwa nikijaribu kutoroka pale ofisini kwetu baada ya kuzuiliwa na askari.
Nilizivuta mbao pemBeni nikapata nafasi ya kukaa.Moshi ulikuwa umetanda mahala hapa na kuna baadhi ya sehemu moto ulikuwa ukiwaka.Hali ya hapa ilikuwa ya kutisha sana.Kwa mbali nilisikia ving’ora vya polisi vikija eneo lile .Sikutaka polisi wanikute pale kwani ningezuiliwa na kila kitu kingeharibika.Huku nikichechemea kwa maumivu makali ya miguu na mkono nilijivuta kuelekea mahala ambako nilikuwa nimemuacha Catherine.
“Catherine !!!!! Catherine !! Nikaita kwa sauti kubwa nikiwa eneo lile
“ Msaada ! Nikasikia sauti ikisema kwa mbali ambayo moja kwa moja niliitambua ilikuwa ni ya Catherine.Kwa haraka nikaanza kuzipangua mbao za meza zilizokuwa zimevurugika na kumkuta Catherine akiwa chini hatamaniki kwa vumbi.
“Are you ok catherine? Nikauliza
“nasikia maumivu makali sana Tonny” Catherine akasema
“Ok Polisi wanakuja tafadhali inuka twende” Nikasema na Catherine akajitahidi kuinuka na kukaa.
“Jitahidi Catherine polisi wako karibu.Haitakiwi watukute hapa”
Catherine akajitahidi kusimama.Nikamshika mkono na kumsaidia kutembea kuelekea katika gari.Watu wengi walikuwa wamelala chini sikujua kama wamekufa ama ni mstuko wa kishindo kile kikubwa.Haraka yangu ilikuwa ni kuondoka mahala pale kabla ya polisi hawajafika.Watu waliokuwa maeneo ya jirani walianza kusogelea mahala pale ili kuangalia nini kimetokea.Nilishukuru Mungu nilipomfikisha Catherine katika gari letu.Nikaliwasha na tukaondoka mahala pale huku tukipishana na magari ya zimamoto na mawili ya polisi waliokuwa doria.
“Tonny nini kilitokea pale mgahawani? Catherine akauliza akiwa anapumua kwa nguvu baada ya kuhakikisha kwamba tumetoka eneo lile salama.Nilimtazama usoni alikuwa ameoga vumbi.Ukimtazama ungefikiri labda amejimwagia unga kumbe ni vumbi lililokuwa limetimka baada ya mlipuko ule kutokea.
“Ina maana hukuona kilichotokea? Nikauliza
“Niliona yule mtu uliyekuwa umemfuata kule chooni akija huku akikimbia na mara ukatokea mlipuko” Catherine akasema
Nilimuonea huruma binti huyu kwa sababu tayari alianza kuonyesha kukata tamaa kutokana na mambo yalivyokuwa yakiendelea.Alikuwa ameanza kuogopa.Niligugumia kwa maumivu makali niliyokuwa nayasikia katika mguu wangu wa kushoto.
“Baada ya mimi kumfuata yule jamaa kule chooni " nilianza kumuelezea Catherine kilichokuwa kimetokea.
"nilifanikiwa kumweka chini ya ulinzi lakini jamaa akawa mwepesi mno hivyo yakaanza mapambano .Tulipambana vikali sana na hatimaye nikafanikia kumdhibiti.Nilipotaka kumkalia tumboni nikahisi kitu ambacho si cha kawaida.Lile tumbo kubwa aliloonekana kuwa nalo halikuwa tumbo bali ni bomu alilokuwa amejifunga kwa ajili ya tahadhari kwa nyakati kama zile.katika purukushani jamaa alifanikiwa kunitoroka na kuanza kukimbia kuelekea kule alikokuwa amewaacha wenzake na ndipo alipowavaa na mlipuko ukatokea.Nadhani jamaa aligundua kwamba tayari walikuwa wamejulikana na kwamba hawangeweza kutoka pale salama hivyo njia bora kwao ya kuepuka kukamatwa na kuuvuruga mpango wao ni kujilipua na kuzidi kuturudisha nyuma.Tumerudi tena kizani.Hatuna chanzo chenye kueleweka kitakachoweza kutusaidia kupata mwanga wa wapi alipo gaidi abdool.Hawa jamaa wamejipanga vilivyop na wako makini katika kila wanachokifanya ili wasitupe mwanya wa kuwafuatilia.Watu wako tayari kufa kuliko kuacha Abdool akakamatwa tena.Kila tunapojaribu kupiga hatua moja wao wanaturudisha nyuma hatua mbili..”
Nilisema huku nikiwa makini katika usukani.Bado niliendelea kuhisi maumivu makali katika mkono uliokuwa umegandamizwa na kitu kizito.
“Tonny nafikiri nahitaji kwenda nyumbani kwanza ili nikajigange pamoja na kuchukua baadhi ya silaha na nyenzo muhimu kwa sababu hawa jamaa tunaowatafuta ni watu hatari na makini mno hivyo yatupasa na sisi kujizatiti kikamilifu kwa zana mbali mbali.Papo hapo inatubidi tufikiri jinsi ya kuianza awamu ya pili ambayo ninatumai itakuwa ngumu sana kutokana na umahiri wa watu hawa.Muda unazidi kwenda na hii ni awamu ya lala salama,ama zetu ama zao,lazima Abdool apatikane leo ".Catherine akasema huku ameinama chini.
Nilielewa mara moja kwamba lengo la Catherine ni kwenda kupumzisha akili baada ya kukutana na mikiki mikiki ya aina yake siku ya leo.Hajawahi kukutana na matukio ya kutisha na kustusha namna ile.Kilichomtisha zaidi ni mlipuko huu uliotokea ambao tumejikuta tukipona kimiujiza japokuwa tumepata michubuko na maumivu ya ndani baada ya kugandamizwa na vitu kama mbao .Nilimuonea huruma sana Catherine kwa kuamua kushiriki kwake katika kadhia ya hatari kama hii.
“Ok Catherine kama unataka kwenda nyumbani mimi itanibidi nikashuke pale Afrique Casino halafu wewe uondoke na gari.Pale kuna gari moja la ziada ambalo nitalitumia iwapo nitahitaji gari.Usisahau kuwataarifu ofisini ili waweze kulichukua gari hili na kumtafuta mwenyewe” Nikasema na Caherine akatabasamu.

************************************************

Saa tisa kasoro dakika tatu nikatia tena mguu katika chumba nilichokuwa nimepanga pale Afrique casino.Nilijiegemeza katika sofa na kurudisha kumbu kumbu ya matukio yote yaliyotokea kuanzia asubuhi.Baada ya uchambuzi wa kina nikang’amua kwamba kampuni ya ulinzi ya Chem chechem ni lazima inahusika kwa kiasi kikubwa sana na tukio zima la kupotea kwa Abdool.Kampuni hii ndiyo inayotumiwa na magaidi kwa ajili ya kupitishia silaha na zana nyingine na hata kupata taarifa mbali mbali za kiusalama.Kampuni hii imekuwa ikiwapatia mafunzo baadhi ya vijana na kuwatumia katika shughuli zake zilizojificha nyuma ya pazia.
Niliwaza sana na kujaribu kupanga mikakati mipya nini cha kufanya jioni ya leo.Awamu tunayoingia ni awamu ngumu kwa sababu jamaa wamekuwa wakijitahidi kutudhibiti kuanzia asubuhi na hivyo hawatakubali kutupa mwanya wowote kwa jioni hii ya leo.
“Pamoja na hayo lazima kabla hakujapambazuka kesho asubuhi Abdool awe ametiwa nguvuni” Nikasema mwenyewe.
Nilipiga simu hotelini na kuomba niletewe chakula .Sikuwa nimetia chochote tumboni toka asubuhi.Wakati chakula kikiletwa niliingia bafuni na kujimwagia maji.Chakula kikaletwa nikala kisha nikaamua kujipumzisha kwa muda mfupi kabla ya kukutana tena na Catherine jioni ya siku hii .Niliiseti saa yangu iniamshe saa kumi na mbili za jioni iwapo nitakuwa nimepitiwa na usingizi.

USIKOSE SEHEMU IJAYO……..
 
BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMUYA 24
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Niliwaza sana na kujaribu kupanga mikakati mipya nini cha kufanya jioni ya leo.Awamu tunayoingia ni awamu ngumu kwa sababu jamaa wamekuwa wakijitahidi kutudhibiti kuanzia asubuhi na hivyo hawatakubali kutupa mwanya wowote kwa jioni hii ya leo.
“Pamoja na hayo lazima kabla hakujapambazuka kesho asubuhi Abdool awe ametiwa nguvuni” Nikasema mwenyewe.
Nilipiga simu hotelini na kuomba niletewe chakula .Sikuwa nimetia chochote tumboni toka asubuhi.Wakati chakula kikiletwa niliingia bafuni na kujimwagia maji.Chakula kikaletwa nikala kisha nikaamua kujipumzisha kwa muda mfupi kabla ya kukutana tena na Catherine jioni ya siku hii .Niliiseti saa yangu iniamshe saa kumi na mbili za jioni iwapo nitakuwa nimepitiwa na usingizi.

ENDELEA……………………………………………

Ngrii……ngriii………ngriiii….. Ulikuwa ni mlio wa saa ikinikumbusha kwamba muda huo ilipata saa kumi na mbili za jioni.Haraka haraka nikainuka na kuanza kujiweka sawa.Dakika tano zilitosha kabisa kufanya maandalizi ya kazi ngumu ya usiku wa leo.Mpaka namalizia kujiandaa badoCatherine alikuwa hajatokea.Niliendelea kumsubiri hadi ilipofika saa kumi na mbili na nusu lakini hakuonekana hali iliyonilazimu kushuka chini na kwenda kuangalia katika maegesho ya magari kama amekwisha fika pale au la.Niliangaza angaza pande zote lakini cathe hakuwepo .Mawazo mengi yakaanza kunijia.”yawezekana akawa ameamua kutokuendelea kushirikiana na mimi baada ya matukio ya hatari ya siku ya leo?Wasi wasi ukaanza kuniingia.Nilianza kuamini kwamba anaweza akawa ameamua kutokuendelea na kazi hii kwani niliziona dalili za kukata tamaa katika macho yake.Niliendelea kutazama katika geti la kuingilia kama anaweza akatokea lakini hakukuwa na dalili zozote za kutokea.Nikanyoosha moja kwa moja hadi mapokezi na kupiga simu ya kulipia.
“hallo “ Iliita sauti ya upande wa pili ambayo niliitambua ilikuwa ni ya Catherine.
“hallow Tonny hapa naongea.Uko wapi cathe?
“Samahani kwa kuchelewa Tonny .Nimechelewa kwa sababu kuna gari mbili zimekuwa zinanifuata toka nilipotoka nyumbani hivyo ikanibidi kuwazungusha mjini ili kuhakiki kama ni kweli wananifuata lakini mpaka sasa bado wananiandama.Nafikiri watakuwa ni wale jamaa zetu.Niko karibu sana kufika hapo afrique casino,jiandae kwa show” Catherine akasema.Nywele zikanisisima na,hasira zikanipanda.Nilitoka pale mapokezi kwa haraka nikaelekea moja kwa moja chumbani nikachukua mkoba wangu mdogo wenye silaha halafu nikashuka kwa kasi na kuelekea katika moja ya gari nilizokuwa nimemuamuru Catherine aiweke pale casino kwa ajili ya dharura.Niiingia ndani ya ile gari na kujiweka tayari kwa mapambano.Niliamini kabisa kwamba kama ni kweli Cathe alikuwa anafuatiliwa basi lazima kungetokea na mapambano.Ndani ya ile gari niliikuta kuna simu mpya pamoja na kikaratasi kinachoonyesha mahali funguo ilipo.Nilichukua ufunguo na kuuchomeka mahala pake na mara nikaiona gari ya Kate ikiingia getini na nyuma yake zikafuata gari mbili .
Niliamua kuitumia simu ile kumpigia simu Catherine ili nimuulize kama gari alizokuwa anasema zinamfuata ni zile zilizokuwa nyuma yake lakini kabla sijafanya hivyo gari moja kati ya zile mbili zilizokuwa nyuma yake iliingia ndani kwa kasi ya ajabu na kulikinga gari la kate kwa mbele.Lile gari lingine lililobaki nyuma yake nalo likaja kwa kasi na kuliziba gari la Kate kwa ubavuni ili asiweze kupita kwa pemBeni.
Kwa kasi ya aina yake watu watatu walishuka toka katika gari la mbele na kulivamia gari la Kate ambaye alitolewa haraka haraka na kuingizwa katika gari lile la mbele kisha gari zile mbili zikaondoka kwa kasi ya ajabu.Catherine alikuwa ametekwa.
Nilivuta pumzi ndefu huku nikizishuhudia zile gari zikitokomea kuelekea barabarani.Tukio lile lilikuwa limetokea kwa haraka mno kiasi kwamba hata watu wengine hawakuelewa nini kilikuwa kimetokea Pamoja na mstuko ule lakini akili yangu ilifanya kazi haraka haraka ,nikaligeuza gari na kuondoka kwa kasi.Watu walikuwa wakikimbia kujinusuru baada ya kuuona mwendo niliotoka nao.Niliingia barabarani kwa fujo bila kufuata sheria za barabara,sikuwa na muda wa kusubiri kwani sikutaka kuwaacha wale jamaa wafike mbali.Kwa kutumia uzoefu wangu niliweza kupenya msururu mkubwa wa magari na kuzikaribia zile gari mbili.Nilikuwa nyuma yao kwa magari matatu.haikuwa rahisi kwao kunitamua kwa sababu gari nililokuwa nikilitumia lilikuwa tofauti na lile walilolizoea.Ukiwa katika kazi hii ya ujasusi unatakiwa uwe unatumia akili nyingi kila mara,haikuwa kazi rahisi kuupenya msururu ule mrefu wa magari na kuwafikia wale jamaa.Nilikuwa nikiomba Mungu anisaidie awe upande wangu ili niweze kuwafuatilia wale jamaa na kupata majibu ya maswali niliyokuwa nikijiuliza hasa ni wapi alikokuwa gaidi aliyetoroshwa Abdool .
Kiza tayari kilikwisha tanda na kuifanya shughuli ya kuwafuatilia wale jamaa kuwa ngumu,lakini kwa kutumia uzoefu wangu niliweza kumudu kuwafuatilia bila ya wao kujua.Kichwani nilikuwa nikijiuliza maswali mengi sana jinsa jamaa wale walivyofanikiwa kumfuatilia na hatimaye kufanikiwa kumteka Catherine.Ni wazi mtandao wao ulikuwa mkubwa .Nilimshukuru Mungu kwa kunipa akili ile ya kuwa na magari ya ziada ambayo yangetumika kwa nyakati kama hizi. Niliendelea kuwafuatilia jamaa wale kwa makini sana bila kuwapa mwanya wa kunitambua.
Zoezi zima la kuwafuatilia wale jamaa liliishia katika jumba moja kubwa lililokuwa limezingirwa na miti mirefu kiasi cha kutoweza kuona ndani .Toka umbali wa mita kadhaa nilikosimamisha gari langu ,niliweza kushuhudia geti likifunguliwa na gari mbili zile zikaingia na geti likafungwa tena.Nilijua ni katika jumba lile ndiko ningeweza kupata majibu ya maswali yangu Nililiangalia jumba lile kwa hasira nikachukua simu niliyoikuta ndani ya gari nikaandika namba za siri za mkurugenzi wetu na kupiga.
“hallo” Iliita sauti nzito ya mkurugenzi wetu Mr Meshack Jumbo.
“hallo Mkurugenzi,Tonny hapa ninaongea” Nikasema
“wewe kijana umejificha wapi? Nakwa……………………” Sikutaka mkurugenzi aendelee na maongezi yake nikamkatisha ghafla
“Mkurugenzi sina muda mrefu wa kuongea na wewe kwa hiyo naomba tuelekee moja kwa moja katika dhumuni la kukupigia.simu.Mzee naomba kama uko ofisini usitoke wala usizime simu yako kwa sababu nitakupigia baada ya muda si mrefu ,kuna jambo zito nadhani utahitaji kulishuhudia wewe pamoja na wenzio”
Nilimaliza na kukata simu bila kumpa nafasi ya kuuliza kitu chochote.Akili yangu ilikuwa imenituma kwamba usiku huu ni lazima kuna jambo litatokea.
Nililitazama geti la jumba lile lililokuwa limefungwa,nikaanza kunyata kuliendea jumba lile ambao lilikuwa kimya kabisa.Nikiwa umbali wa kama mita kadhaa,niligundua ugumu uliokuwapo katika kuingia ndani ya jumba ya lile.Ukuta uliolizunguka ulikuwa mrefu na isitoshe ulizungushiwa nyaya maalumu za usalama.iwapo ningejaribu kuigusa hata nyaya moja basi ningekuwa nimeharibu kila kitu.Nilikuna kichwa ili kuangalia ni jinsi gani ningeweza kuingia mle ndani.Wakati nikikuna kichwa ili kupata namna ya kuingia mle ndani ,nikasikia muungurumo wa gari .Haraka nikajibanza katika mti mmoja mkubwa ili nisionekane iwapo gari zile zingekuwa zikija upande ule.Kama nilivyotabiri gari zile zilikuwa zikielekea katika jumba lile.Zilikuwa gari nne .Nilizidi kupatwa na shauku ya kutaka kujua kilichokuwa kinaendelea ndani ya ile nyumba.
Geti likafunguliwa na kuziruhusu gari zile kuingia ndani.Kwa kuwa sikuwa mbali sana na geti niliweza kuona ndani .Kulikuwa na magari mengi yaliyojipanga lakini sikuweza kuona mtu yeyote zaidi ya mtu mmoja aliyevaa koti refu akiwa ameshika bunduki,amesimama mlangoni.
Baada ya gari zile kuingia ndani geti likafungwa .mara moja nikapata wazo.Katika begi langu kulikuwa na miwani maalum kwa ajili ya kuonea sehemu zeye giza.Nikavaa na kwa hatua za kunyata nikaikaribia nguzo ya umeme .Niliitoa bastora yangu yenye kiwambo cha sauti nikaachia risasi mbili na kuzikata nyaya zinazopeleka umeme katika jumba lile.Ghafla jumba lote likawa giza.Nilikuwa nikilihitaji giza lile.Kama umeme nikakimbia na kuelekea katika ukuta ule mrefu .Ulikuwa ni ukuta mrefu kuupanda lakini siku zote Mungu huwa yuko upande wangu kwani hatua chache toka niliposimama pemBeni ya ule ukuta niliona fungu la matofali yaliyopangwa. Kwa kasi ya ajabu nikapanga matofali kama sita hivi kalafu nikarudi nyuma na kukimbia kwa kasi nikasimama juu ya matofali na kuuparamia ukuta.Sekunde chache nilikuwa juu ya ukuta ,nikatoa mkasi mdogo na kuzikata nyaya zilizokuwa juu ya ule ukuta.Sasa nilikuwa huru.Niliangaza upande ule niliokuwepo sikuona mtu yeyote .Nikarukia ndani na kutoa ukelele kidogo.Nilijibanza nyuma ya mti mdogo uliokuwa karibu .Ghafla mwanga mkubwa ukatokea taa zote zikawaka.Nilisikia muungurumo wa jenereta.Pamoja na kurudisha umeme lakini hawakuwa na ujanja tena kwa sababu tayari nilikwisha jitoma ndani .Nikiwa pale chini nilitumia dakika kama mbili hivi kuisoma hali ya usalama wa mle ndani,.Niliweza kuwaona jamaa kadhaa wakizunguka zunguka humo ndani wote wakiwa na bunduki.Nafikiri walikuwa wakitafuta chanzo cha kukatika kwa umeme.
Toka pale nilipokuwa nilitambaa kwa tumbo kuelekea yalipokuwa yamepaki magari.Nilitambaa chini ya vungu za magari nikielekea mahala ulipo mlango wa kuingilia ndani.Sikuweza kuonekana kiurahisi kwa sababu magari yalikuwa yamekaribiana sana.Dakika kama tano baadae nilikuwa nikiutazama mlango wa kuingilia ndani ambao ulikuwa ukilindwa na watu wawili wenye silaha.Nilihitaji kuingia ndani kwa kupitia ule mlango waliokuwa wakiulinda wale jamaa,mara nikapata wazo.Nikatambaa tena kwa tumbo kurundi nyuma.Nikatoa chombo Fulani nikakiweka chini ya gari.Chombo hiki hutoa mwanga mithili ya mlipuko wa umeme.Lengo lilikuwa ni kuwaondoa wale jamaa pale mlangoni.Kama nilivyokuwa nimepanga chombo kile kilianza kutoa mwanga mithili ya ule unaotokea pindi panapokuwa na shoti ya umeme.Jamaa wale walikuja kwa kasi ya ajabu wakidhani kwamba kuna hitilafu katika moja ya magari .Wote wawili wakainama chini ya uvungu ili kuangalia kuna nini.Hii ndiyo fursa niliyokuwa nikiisubiri.kwa kutumia bastora yangu yenye kiwambo cha sauti niliwapa usingizi wa milele wote wawili kwa kuwafumua vichwa vyao kwa risasi.Haraka haraka nikamvua mmoja wao sare zake za ulinzi nikavaa.Kwa jinsi nilivyokuwa nimeivuta kofia usoni haikuwa rahisi kutambulika.Niliwasukumia wale jamaa katika uvungu wa gari na kuelekea mlangoni.Nilisimama mlangoni na kuangalia kama kuna mtu yeyote anayeweza kuzusha udadisi kwangu.Hakukuwa na mtu yeyote aliyenitilia shaka.Nilipohakikisha mahala pale ni shwari,nikakinyonga kitasa na mlango ukafunguka .taratibu nikaingia ndani na kuufunga tena mlango bila kutoa ukelele.
Nilikuwa katika varanda kubwa .Nilitembea kwa tahadhari kubwa na kwa mbele nikakutana tena na varanda jingine lililoelekea upande wa kulia.Wakati nikiangaza angaza ili nijue wapi pa kwenda nikasikia sauti za watu wakija.Haraka haraka nikajibanza katika ua kubwa .Watu wawili waliovaa suti nyeusi wakapita kwa kasi pale nilipojificha.Nilipohakikisha wamepotea kabisa nikaibuka.Kwa haraka nikaifuata ile njia wale jamaa walikotokea na mara nikakuta mlango wa chumba kimoja ukiwa wazi.Nilisimama pale mlangoni lakini sikusikia sauti ya mtu yeyote mle chumbani,nikanyata na kuingia ndani.Mle ndani kulikuwa na kompyuta nne na mbili kati ya hizo zilikuwa zikionyesha alama ya “communication error” yaani hitilafu katika mawasiliano.Nilitambua mara moja kwamba kilichosababisha hitilafu ile ni zile nyaya nilizozikata kule juu ya ukuta.
Niligeuza jicho kulia nikajikuta nikilazimika kuisogelea kwa karibu zaidi kompyuta mojawapo kati ya zile mbili zilizokuwa zinaonyesha picha.Niliitazama kwa ukaribu nikahisi kama sikuwa naona vizuri kutokana na mambo niliyoyaona.Picha iliyokuwa ikionekana katika kompyuta ile ni picha ya sherehe iliyokuwa ikiendelea katika ukumbi mmoja ndani ya jumba lile.Watu walikuwa wameizunguka meza moja kubwa ya duara huku wakiburudika kwa chakula na vinywaji.Kitu kilichoyabadili mapigo yangu ya moyo ni kumuona gaidi aliyetoroshwa Abdool akiwa sambamba na watu wengine i wakifurahi na kugonganisha glasi.huku nyuma yao kukiwa na watu wawili wakiwalinda.Moyo ulinipaa baada ya kumuona Monica akiwa amefungwa kwenye kiti na pemBeni yake akiwepo Catherine ambaye alionyesha kuvuja damu .
Sikupoteza wakati nikatoa simu na kumpigia mkurugenzi wetu nikamuelekeza afike mahala pale haraka iwezekanavyo yeye pamoja na maafisa wengine pamoja na polisi wa kutosha ili waweze kulishuhudia jambo lile.
Nilitoka nje ya kile chumba na kuufuata ujia ule na mara nikajikuta nikitazamana na mlango mkubwa wa vioo ambao mara tu nilipoukaribia ukafunguka nikaingia.Hii ni ile milango maalum ambayo mtu huhitaji kuigusa,kwani unapoikaribia inajifungua yenyewe.Nilikuwa nimeufikia ukumbi ulimokuwa unafanyikia sherehe ile.Ukumbi ulikuwa wa duara na kulikuwa na korido kubwa kuuzunguka na kufanya ukumbi ule ukae kati kati.Nilitembea hatua nne nikakutana na mlango.Nilijaribu kuufungua lakini ulikuwa umefungwa kwa ndani.Nilitoa funguo yangu yenye kufungua kila kitasa na kuichomeka mlangoni,mlango ukafunguka.Nilichungulia ndani na niliweza kuwaona watu wote wazi wazi.Nilimuomba Mungu awe upande wangu katika kumalizia kazi hii.Kwa kasi ya aina yake nikajiviringisha hewani na kuingia ndani ndani .Nilisimama juu ya boksi kubwa lililokuwa si mbali sana na pale mlangoni.
“All of you ,you are under arrest.Hands on your heads !!...” Nilisema kwa sauti kali.hakuna aliyeweza kuamini.Niliwaona watu wawili wakijaribu kuzishika bastora zao na bila huruma nikaachia risasi toka katika bastora zangu na kuwafumua vichwa vyao kwa risasi
Haikuwa rahisi kuamini kama walikuwa chini ya ulinzi .Baada ya kuona jinsi nilivyovifumua vichwa vya wale watu kwa risasi ,wote wakaogopa na kuweka mikono yao nyuma ya vichwa vyao.Upande wa kushoto kwangu nilimuona Monica akinitazama kwa mstuko mkubwa.Hakuamini kama ni mimi kweli ndiye nimesimama pale.Pamoja na kwamba nilikuwa na kazi nzito lakini moyoni nilikuwa na furaha sana baada ya kumuona Monica.Kumbe majahili hawa walikuwa wamemteka nyara.Catherine naye alikuwa kama yuko ndotoni.Bado hakumini kilichotokea.Taratibu nilirudi nyuma nikiwa katika tahadhari kubwa nikachomoa kisu na kukata kamba katika kiti alichokuwa amefungwa Monica.Baada ya kuikata kamba ile moja akaendelea kujifungua na baada ya sekunde kadhaa akawa huru.nikamkabishi bastora moja halafu nikamfungua na Catherine.Nilizichukua bastora za wale jamaa niliowapiga risasi .Tuliuzingira ule ukumbi mimi nikiwa upande wa mbele,Catherine akiwa kulia na Monica kushoto.Dakika ishirini tangu tuuzingire ukumbi ule ghafla mlango ukasukumwa kwa nguvu ukafunguka.tayari bastora zangu zilikuwa mkononi.kabla sijaachia risasi nilistuka baada ya kulishuhudia kundi kubwa la askari wakiingia mle ndani.Ghafla nikagonganisha macho na mkurugenzi wangu Mr Meshack Jumbo.Moja kwa moja akanifuata na kunishika mkono.
“Kijana hongera sana.kazi nzuri Tonny” akasema huku akitabasamu.
“mkurugenzi kwa mara nyingine tena ninakukabidhi gaidi Abdool bin sahel bin Abdool aliyekuwa ametoroshwa asubuhi ya leo.”Nilisema huku nikienda mezani na kumuinua Abdool nikamleta mbele ya mkurugenzi ambaye akaamuru afungwe pingu na kuondolewa pale chini ya ulinzi mkali.
“Mkurugenzi ningependa vile vile kumtambulisha kwako mtu aliyesaidia mpaka tukaweza kuufahamu mpango huu “ Nilimfanyia ishara Monica akaja.
“Huyu ndiye aliyesababisha kujulikana kwa mpango huu wa kutoroshwa Abdool.Anaitwa Monica.Nitamtambulisha rasmi kiofisi kwa mujibu wa taratibu” Nilimaliza utambulisho ule na ghafla nikajikuta nikitazamana na askari sita wenye silaha.Kwa haraka nikajikuta mikono yangu ikikamatwa na kufungwa pingu kwa nyuma.
" Nini kinaendelea hapa " nikauliza kwa mshangao huku nikimuangalia mkurugenzi
“Tonny tunakuweka chini ya ulinzi kwa sababu tunahitaji kujiridhisha na uchunguzi wetu kwamba uliufahamu mpango wa magaidi hawa ambao ni hatari kwa nchi yetu na hukutoa taarifa kwa vyombo husika jambo ambalo lilihatarisha usalama wa nchi..Mambo mengi yametokea kwa muda mfupi hivyo tunataka tujiridhishe katika uchunguzi wetu kwamba hukuwa ukihusika kwa namna yoyote ile na tukio hili .Umefanya kazi kubwa Tonny unastahili pongezi lakini huu ni utaratibu wa kikazi ambao siwezi kuupindisha” akasema mkurugenzi wetu
“Mkurugenzi !!!! … “ Nikasema kwa hamaki
“Mpelekeni Tonny kituoni haraka pamoja na huyu mwenzake” Mkurugenzi wetu akaamuru.
Mimi na Monica tukapakiwa katika gari huku tukiwa chini ya ulinzi mkali tukapelekewa kituoni kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi kama wanavyodai.Pamoja na kushikiliwa na jeshi la polisi nilikuwa na furaha moyoni baada ya kuonana tena na Monica na vile vile kufanikisha kukamatwa tena kwa gaidi Abdool.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………………
 
BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMU YA 25
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
“Huyu ndiye aliyesababisha kujulikana kwa mpango huu wa kutoroshwa Abdool.Anaitwa Monica.Nitamtambulisha rasmi kiofisi kwa mujibu wa taratibu” Nilimaliza utambulisho ule na ghafla nikajikuta nikitazamana na askari sita wenye silaha.Kwa haraka nikajikuta mikono yangu ikikamatwa na kufungwa pingu kwa nyuma.
" Nini kinaendelea hapa " nikauliza kwa mshangao huku nikimuangalia mkurugenzi
“Tonny tunakuweka chini ya ulinzi kwa sababu tunahitaji kujiridhisha na uchunguzi wetu kwamba uliufahamu mpango wa magaidi hawa ambao ni hatari kwa nchi yetu na hukutoa taarifa kwa vyombo husika jambo ambalo lilihatarisha usalama wa nchi..Mambo mengi yametokea kwa muda mfupi hivyo tunataka tujiridhishe katika uchunguzi wetu kwamba hukuwa ukihusika kwa namna yoyote ile na tukio hili .Umefanya kazi kubwa Tonny unastahili pongezi lakini huu ni utaratibu wa kikazi ambao siwezi kuupindisha” akasema mkurugenzi wetu
“Mkurugenzi !!!! … “ Nikasema kwa hamaki
“Mpelekeni Tonny kituoni haraka pamoja na huyu mwenzake” Mkurugenzi wetu akaamuru.
Mimi na Monica tukapakiwa katika gari huku tukiwa chini ya ulinzi mkali tukapelekewa kituoni kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi kama wanavyodai.Pamoja na kushikiliwa na jeshi la polisi nilikuwa na furaha moyoni baada ya kuonana tena na Monica na vile vile kufanikisha kukamatwa tena kwa gaidi Abdool


ENDELEA.......................................


" Tonny nini kimetokea? Mbona tumefungwa pingu ? Tunapelekwa wapi? akauliza Monica kwa mshangao
" Monica hizi ni taratibu za kiusalama.Tukio kama hili lililotokea lilikuwa ni tukio zito sana kwa nchi yetu na tuliokuwa tukifahamu kilichokuwa kinaendelea ni sisi wawili pekee na hatukuitaarifu serikali kuhusiana na kilichokuwa kikiendelea.Hilo ndilo kosa .Tumehatarisha usalama wa taifa kwa kuwa na taarifa zinazohusiana na usalama wa nchi bila kuziwasilisha sehemu husika." Nikasema.
" Usihofu Tonny .Hakuna tena hatari yoyote katika nchi yenu.Tayari Abdool na washirika wake wote wametiwa nguvuni.Kinachotakiwa kwa sasa ni kwa serikali yenu kufanya kila iwezalo kuweza kuikata kabisa mzizi yote ya mtandao wa kigaidi hapa nchini.Inaweza ikaomba ushirikiano wa kimataifa na nchi yangu iko tayari kushirikiana na serikali yoyote ile katika jitihada za kutokomeza ugaidi duniani." akasema Monica.Bado nilikuwa nikimuangalia nisiyaamini macho yangu.Awali nilikwisha amini kwamba Monica alikuwa mmoja wa magaidi na alitumia nafasi ya kuwa karibu nami ili aweze kuzipata siri zangu mbali mbali zinazohusiana na usalama wa nchi lakini kumbe alikuwa ametekwa na wale magaidi.Kimya kifupi kilitanda mle ndani ya gari.Tulikuwa tunatazamana.
" Tonny sipati neno la kukushukuru kwa kuja kuniokoa leo.You are my hero" akasema Monica.T
" Ulikuwa ni wajibu wangu kuja kukuokoa Monica." nikajibu kwa ufupi.
" Nikiwa mikononi mwa wale magaidi nilikuwa na matumaini kwamba lazima ungekuja kuniokoa.Mawazo yangu yalikuwa kweli .Umeniokoa Tonny toka katika mikono ya magaidi" akasema Monica huku huku macho yake yakiwa na machozi.
" Pole sana Monica.hawakukuumiza washenzi wale?
" Walinitesa sana wakitaka niwaeleze chochote ninachokijua kuhusiana na wewe lakini sikuwa tayari kuwaeleza chochote.Nilikuwa radhi nife lakini si kuwapa majibu ya maswali yao. Walinileta pale ukumbini iliniweze kushuhudia jinsi Abdool atakavyoondoka nchini kisha waniue mimi na yule mwanadada uliyekuwa naye.Mwanadada yule ni jasiri sana.Aliteswa sana lakini hakuweza kusema chochote" akasema Monica
" Yule anaitwa Catherine ni mmoja kati ya vijana wapya katika idara yetu.Anastahili pongezi amenisaidia sana kufanikisha kazi hii " nikasema halafu nikamtazama tna Monica usoni .
" Monica utanisamehe kwa sababu nilikuhisi vibaya kwamba ulikuwa ni mshirika wa magaidi pale niliporudi nyumbani na kukuta nyumba ikiwa tupu .Sikujua kama wamekuteka nyara" nikasema .Monica akatabasamu na kusema
" Tonny pale ulipoondoka niliendelea na kuwasiliana na ofisi yetu kuu .Nikiwa katika mawasiliano nilisikia kama nyayo za mtu .Nikadhani labda umerejea.Nilijaribu kukuita lakini hukuitika.Nikatoka mle chumbani kwa dhumuni la kuangalia ni nani aliyekuwa akitembea mle ndani na ndipo nilipojikuta nikiwekewa bastora mbili kichwani na watu wawili waliokuwa mlangoni.Walinifunga na kisha wakaendelea kukipekua chumba kile na baada ya kama nusu saa hivi wakanipakia garini wakanipeleka sehemu ambayo siifahamu.Pamoja na yote bado nilikuwa na imani na kitu kimoja tu kwamba utakuja kuniokoa.Sijui kwa nini nilkuwa na imani hii na ndiyo maana sikuwa na wasi wasi kabisa hata pale nilipokuwa nikitishiwa kuuawa.Nilijua tu kabla hawajaniua utakuwa umeshafika.Namshukuru Mungu kwani alikuleta kwa wakati muafaka kabisa.Tonny sina cha kukuambia zaidi ya ahsante sana kwa kuniokoa.Siku zote utakuwa moyoni mwangu." akasema Monica na kunifanya nitabasamu
Tulifikishwa katika kituo cha kati cha polisi tukashushwa chini ya ulinzi mkali sana tukaingizwa kituoni ambako hatukukaa sana tukatolewa na tukakabidhiwa kwa maafisa wa kijeshi.Tukaingizwa katika gari la jeshi na msafara wa gari nne za kijeshi ukaondoka pale kituo cha kati cha polisi hadi katika kambi ya jeshi ambako tulihifadhiwa kule.

*****************************************

Kwa muda wa wiki tatu bado tuliendelea kuwepo katika kambi ile ya kijeshi tukifanyiwa mahojiano na hatimaye baada ya wiki tatu ikabainika kwamba tulikuwa na makosa kwa kuamua kulifanya jambo lile liwe siri huku tukiamini kwamba lilikuwa ni jambo hatari kwa usalama wa nchi.Ili kutouharibu uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Marekani, serikali ikaamuru Monica arejeshwe Marekani lakini kwa sharti la kutokuruhusiwa kuingia tena nchini Tanzania kwa namna yoyote ile. Mimi nilionekana kama ni mtu hatari kwa taifa na ambaye taifa limepoteza imani naye kwa hiyo nikaamriwa kwamba nipelekwe katika gereza la Uwangwa na niwekwe pale kwa muda ambao itaonekana unafaa lakini haukutajwa ni muda gani.
Nilisikitika sana kwa maamuzi haya lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya zaidi ya kukubaliana na maamuzi hayo.Monica alilia sana na kabla ya kuondoka alipewa nafasi ya kuagana nami
" Tonny,ninaondoka nikiwa na furaha na machozi.Ninafurahi kwa sababu tumeweza kulizima jaribio la kumtorosha Abdool na kufanikisha kufumuliwa kwa mtandao wa Alqaeda nchini Tanzania .Huu ni ushindi mkubwa kwa nchi yangu na yako pia dhidi ya vita ya ugaidi. Ninaondoka na machozi kwa kitendo hiki cha kukufungia kwa kuonekana ni mtu hatari kwa usalama wa taifa.Binafsi sijaridhishwa kabisa na maamuzi haya ,.Ninaondoka Tonny na siruhusiwi tena kukanyaga ardhi ya Tanzania.Nilitamani sana kuendelea kukaa hapa na wewe kwa sababu ndani ya muda huu mfupi umeuteka moyo wangu kwa kiasi ambacho siwezi kueleza. Nitakuombea kwa Mungu na siku moja adhabu hii itakwisha.Ninakuomba pindi tu adhabu hii itakapokwisha njoo Marekani nitakuwa nikikusubiri kule ili tuweze kuwa pamoja.Maisha yangu yatakuwa na furaha kubwa iwapo nitaishi nawe.Ninakupenda sana Tonny na ninaapa kwamba sintakuwa na mwanaume ambaye si wewe.Nitakusubiri hata kama itanichukua maisha yangu yote kusubiri nitakusubiri..Tonny usisikitike sana kwa maamuzi haya ya viongozi wako kwani wamefanya hivi kwa sababu zao wenyewe .Muda huu ulipaswa kuonekana shujaa kwa kitendo cha kishujaa ulichokifanya. Taifa lako linatakiwa kujivunia kwa kuwa na mtu kama wewe.Ni fahari kubwa kwa Tanzania.Kwa heri Tonny.Siku zote utakuwa hapa moyoni mwangu...." Haya yalikuwa ni maneno ya mwisho ya Monica aliyoyaongea huku akiwa amesimamiwa na wanajeshi kisha akanibusu na kuongozwa kupanda helkopta ya jeshi akaondoka.Niliitazama helkopta ile hadi ilipopotea kabisa machoni pangu.Nilichukuliwa chini ya ulinzi mkali na kupelekwa katika gereza jipya la uwangwa Kigamboni ambako nilianza kutumikia adhabu yangu ya kukaa kizuizini kwa muda usiojulikana kwa sababu eti ni mtu hatari kwa taifa.


MIAKA MIWILI BAADAE


Msururu mrefu wa magari yaliyokuwa katika msafara wa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania unawasili katika jengo kubwa la mikutano ya kimataifa la Kawawa International conference center jijini Arusha.Kituo hiki kipya cha mikutano cha kimataifa jijini Arusha kilipewa jina hilo ili kuuenzi mchango wa mmoja wa waasisi wa taifa hili ambaye alijulikana kama simba wa vita enzi za kudai uhuru.Ukiacha jengo la awali la AICC lililoifanya Arusha kuwa kitovu cha mikutano ya kimataifa katika ukanda huu wa afrika mashariki na kati,jengo hili la Kawawa international conference centre ambalo ni kubwa na la kisasa sana linazidi kuufanya mji huu wa Arusha kuwa wa kimataifa zaidi.
Mheshimiwa Didas Ezekiel wakwi,waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania akashuka garini baada ya gari lake kusimama na kupokelewa na mkurugenzi wa kituo hiki cha mikutano cha kimataifa ndugu Leonard Mosha.Kama ilivyo ada,huku akiongozwa na Leonard ,waziri mkuu akatambulishwa kwa baadhi ya wafanyakazi wa kituo kile waliokuwa amejipanga mstari wakiwa na Bendera zao mikononi.Kila mmoja alionekana ni mwenye furaha na tabasamu kwa ujio ule wa waziri mkuu wa Tanzania.Baada ya kutambulishwa kwa wafanyakazi wa kituo hiki,waziri mkuu akapelekwa kufanya kazi iliyompeleka pale ya kukagua maandalizi ya mkutano mkubwa wa kimataifa wa Sulivan uliotarajiwa kufanyika katika kituo kile siku chache zijazo.Baada ya mkutano wa nane wa Sulivan kufanyika jijini Arusha Tanzania june 2008 kwa mara nyingine tena nchi ya Tanzania imepewa heshima ya kuandaa mkutano mwingine wa Sullivan baada ya mkutano ule wa kwanza kuonyesha mafanikio makubwa.Maandalizi yalikuwa ni makubwa na kila kitu kilikuwa kimekamilika kwa asilimia tisini.Hoteli za kulala wageni zilikwisha andaliwa,magari ya kutembelea wageni yalikuwa tayari na ratiba nzima ya mkutano ule ilikuwa imekamilika.
Hata kabla ya mkutano wenyewe kuanza,jiji la arusha lilikwisha anza kufurika watu waliotoka katika kila pembe ya Afrika ili kuushuhudia mkutano huu muhimu.Wajasiriamali wa kitanzania waliokuwa wametengewa soko maalum kwa ajili ya kuonyesha bidhaa zao za ubunifu nao walikuwa ni wengi na bidhaa zao zilikuwa nzuri na za kuvutia..Hii ilikuwa ni fursa pekee kwa wajasiriamali wa Kitanzania na afrika mashariki kuzitangaza bidhaa zao kimataifa na kutafuta masoko ya nje ya bidhaa zao.
Kazi ya kukagua mahala utakapofanyikia mkutano ule mkubwa ilichukua takribani masaa mawili na kisha waziri mkuu ,pamoja na ujumbe wake mkubwa wakakutana katika ukumbi mdogo ili kumpa nafasi mheshimiwa waziri mkuu kufanya majumuisho ya ziara yake ile kabla ya kwenda kuendelea na kukagua maandalizi mengine yanayohusiana na mkutano ule wa Sullivan. kama vile hoteli na baadhi ya sehemu watakazotembelea wageni wanaotarajia kuhudhuria.Baada ya maelezo ya utangulizi toka kwa mkurugenzi wa kituo kile,mheshimiwa waziri mkuu akapewa nafasi ya kufanya majumuisho ya ziara yake.
“Mheshimiwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi,mheshimiwa waziri wa mambo ya nje ya nchi,mheshimiwa mkuu wa mkoa wa Arusha,mheshimiwa mkurugenzi wa jiji la arusha,mheshimiwa mkuu wa wilaya,mheshimiwa mkurugenzi wa kituo hiki cha mikutano,waheshimiwa viongozi mbali mbali mlioambatana nami katika ziara hii,mabibi na mabwana napenda kuchukua nafasi hii kwa dhati kabisa kutoa shukurani zangu za kipekee kabisa kwa uongozi na wafanyakazi wa kituo hiki kwa juhudi kubwa ya kuweza kufanikisha maandalizi ya mkutano huu mkubwa wa Sullivan ,kwa asilimia tisini.Napenda kwa dhati ya moyo wangu niseme nimeridhishwa na kufurahishwa na maandalizi haya mliyoyafanya.Nafahamu haikuiwa kazi ndogo kufanya maandalizi haya makubwa lakini kwa juhudi zenu ,mkishirikiana na wadau mbali mbali pamoja na serikali mmeweza kufanikisha hilo.Kilichobaki ni kidogo sana na nina hakika kwamba ndani ya muda mfupi ujao kazi hii itakuwa imekamilika kwa asilimia mia moja.Hongereni sana” Waziri mkuu akasema na kuufanya ukumbi wote ulipuke kwa makofi ya kushangilia.
“ Kwa mara nyingine tena ,nchi yetu imepewa heshima kubwa kuandaa mkutano huu mkubwa.Ni nchi nyingi zingetaka kupewa ziandae mkutano huu lakini sisi tumeonekana tunafaa kupewa nafasi hii adimu.Ni heshima kubwa sana kwetu.Hii ni fursa nzuri kwetu kuitangaza nchi yetu,kutangaza maliasili zetu,bidhaa zetu ,ikiwa ni pamoja na wafanya biashara wetu kutanua wigo wa biashara zao kimataifa.Nashukuru kwamba katika maadalizi yenu mmeyazingatia hayo yote.” Waziri mkuu akatulia na kwa mara nyingine tena ukumbi ukapiga makofi ya kushangilia.
“Ndugu zangu sihitaji kusema mengi kwa sababu bado tuna ziara ndefu ya kuzungukia sehemu mbali mbali kukagua maandalizi yanavyokwenda.Ni matumaini yangu kwamba ndani ya muda mfupi ujao yale mambo yote ambayo yalikuwa hayajakamilika ,yatakamilishwa ili tujiridhishe kwamba hakuna tatizo lolote kubwa litakalojitokeza zaidi ya changamoto ndogo ndogo zitakazojitokeza wakati wa mkutano.Narudia tena kuwapa hongera kwa kazi nzuri mliyoifanya na ninawatakieni mafanikio katika kumalizia yale mamboyote ambayo bado hayajakamilika.” Waziri mkuu akasema na kukaa chini huku akisindikizwa na makofi ya kushangilia.Baada ya shughuli ile iliyompeleka pale kumalizika mheshimiwa waziri mkuu akaondoka na kwenda kuendelea na ziara yake ya kukagua maandalizi mengine yanayohusiana na mkutano ule.

USIKOSE SEHEMU IJAYO……………………..
 
Back
Top Bottom