BRING BACKOUR GIRLS
SEHEMU YA 17
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Kimya cha sekunde kadhaa kikapita na David akauliza swali.
”Mkurugenzi ,je hakuna taarifa zozote za kiintelijensia zinazoweza kutupa japo mwanga wowote kuhusu mahala pa kuanzia?
“Mpaka hivi sasa hakuna taarifa yoyote inayoonesha ni wapi Tonny anaweza kuwa amejificha.Nyumbani kwake kumekutwa walinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi wanalinda na kwa mujibu wa maelezo waliyoyatoa ni kwamba wamepewa taarifa na wakubwa zao kuwa waende wakailinde ile nyumba.Polisi walifanikiwa kuingia ndani ya nyumba yake ili kuangalia kama kuna chochote kinachoweza kuwasaidia kupata walau fununu za mahala anakoweza kuwa amejificha Tonny lakini hawakuweza kupata kitu chochote.Nyumba yote ilikuwa imevurugwa hovyo hovyo.Lakini bado tuna matumaini makubwa kuwa bado Tonny yuko jijini Dar”
“Ok tumekuelewa mkurugenzi na tuko tayari kulitekeleza jukumu hili zito la kumtafuta Tonny.na tutakuwa tukikupa taarifa ya kila hatua tunayoifikia.”
David akasema kisha wakaagana na mkurugenzi wakatoka kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa jukumu la kumtafuta Tonny.
ENDELEA………………………..
Nilistuka toka usingizini na kuangalia saa.Ilikuwa ni saa sita na dakika kumi na nane.Nilijaribu kuinua kichwa lakini kilikuwa kizito mno isitoshe nilihisi maumivu makali sana .Niliutazama mshale wa saa ulivyokuwa ukijisogeza taratibu,na sasa ilikuwa ni saa sita na dakika ishirini na sita.Nilijikaza nikainuka na kuchukua simu ya Rose iliyokuwa karibu.Rose alikuwa katika usingizi mzito.Nazifahamu namba za simu za David nikaziandika na kupiga.Simu ikaita kwa sekunde chache halafu ikapokelewa.
“hallow” Ilikuwa ni sauti ya upande wa pili ambayo niliitambua kuwa ilikuwa ya David.
“hallow David,Tonny anaongea hapa”
Kimya kidogo kikatanda ,nahisi David alistuka baada ya kusikia kuwa anayeongea simuni ni mimi.Hakuwa ametegemea kama ningeweza kumpigia simu kwa muda kama ule.
“Tonny ,uko wapi kaka? Pole sana kwa matatizo” akasema David kwa sauti ambayo niliweza kung’amua mara mja kuwa ilibadilika ghafla na kuwa ya wasi wasi mwingi.
“Nimerudi Dar toka jana .Nilipatwa na matatizo kidogo.”Nikasema
“nilisikia ulipatwa na matatizo Tonny.Pole sana.”
“ahsante sana David.Uko wapi kwa sasa?
“kwa sasa ninaelekea nyumbani kwangu”
“ david ninaomba tuonane usiku huu nina shida na wewe kubwa sana.Kwa sasa ni saa sita na nusu naomba kabla ya saa saba kamili tuwe tumeonana.fanya juu chini tukutane Afrique Casino kaunta C”
“Sawa Tony,naelekea huko sasa hivi” akajibu kwa sauti iliyojaa uoga.Nikakata simu na nilipogeuka nikamkuta Rose ameamka ananiangalia kwa macho makali.
“mwanaume usiye na haya wewe! Hiyo ni mikutano gani tena ya saa saba za usiku wakati hali yako unaiona si nzuri? Akasema Rose kwa ukali
“Usiogope Rose ni masuala ya kikazi tu”
“kazi gani hizo za usiku wa manane?Wakati watu wamelala nyie mnafanya kazi,kazi gani hizo? Mnawanga? Sitaki kusikia upuuzi wako Tonny.Kwanza nitaaminije kuwa ni masuala ya kikazi na si miadi na hao wanawake wako walio kila pande za jiji?
Rose akasema kwa hasira
Sikumlaumu Rose kwa sababu hakujua kitu gani kilichokuwa kikiendelea.Zaidi ya yote hakujua kama mimi ninafanya kazi katika idara ya ujasusi
Sikumjibu kitu kwa sababu tayari alikwisha kasirika na hivyo kumjibu lolote kungemuongezea hasira mara dufu kitu ambacho sikutaka kitokee.Taratibu nikaamka na kufungua kabati.Nikachukua suruali ya Jeans na fulana nikavaa,.Rose akainuka na kunifuata.
“Sorry baby,I have to go”Nikasema
“You wont go Tonny.Please stay”
“Please Rose .nakuahidi baada ya kazi hii kuisha nitakuja kwako na kukaa mwezi au miwili au hata mwaka ukitaka lakini tonight let me go please.I have to do this.”
Rose machozi yalikuwa yakimdondoka,sikumjali nikachukua kibegi changu kidogo cha kazi klichokuwa na zana mbali mbali nikafungua mlango na kuondoka.
********************
Afrique casino ni moja kati ya kasino mpya kabisa na za kisasa kuwahi kutokea jijini Dar.Kasino hii ilikuwa imejengwa kati kati kabisa ya jiji .Kwa muda wa masaa ishirini na manne kasino hili lilikuwa limesheheni watu lukuki.Hiki ndio kitovu cha burudani za aina zote,hakukuwa na starehe ambayo ungeikosa ndani ya jumba hili ambalo wenyewe wapenda starehe waliliita kama Africa paradise wakiwa na maana ya bustani nzuri na ya kupendeza .Ukiwa ndani ya jumba hili hutatamani kuondoka kwa sababu kuna kila kitu unachokihitaji,.Mara nyingi huwa napenda kuja hapa kutuliza mawazo na kukutana na watu mbali mbali.Pamoja na starehe zote kuwamo humu lakini pia kulikuwa na uchafu wa kila aina.Biashara ya ngono ,dawa za kulevya vilikuwa ni vitu vya kawaida..
Nilipaki gari maegesho na kutazama pande zote kuhakiki usalama wangu na kisha nikaingia ndani ya jumba hili.Kwa jinsi watu walivyokuwa wengi ndani ya jumba hili ni vigumu sana kubainika hata kama unatafutwa .Nilifululiza moja kwa moja mpaka sehemu ambayo nilipanga nikutane na David,.nikakaa katika kona ya kaunta sehemu iliyokuwa na mwanga hafifu ili niweze kumuona kila ajaye upande ule.Niliitupia macho saa kubwa iliyokuwa pale kaunta ilionyesha ni saa saba na na dakika ishirini na mbili.
Niliendelea kumsubiri David huku nikipitisha macho kwa warembo kadhaa waliokuwa karibu yangu wakiwa wamevaa nusu utupu.Mara moja sura ya Monica ikanijia tena kichwani,nikasikia uchungu mwingi kwa kitendo alichonifanyia binti huyu.Kwa mbali nikamwona David akiangaza angaza,nikamfanyia Ishara,akaniona.Akaja kule nilikokuwa kwa haraka.Tulisalimiana ,nikamwagizia kinywaji.Tukakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha david akasema
“Ndiyo Tonny leta habari”
“habari si nzuri david kama ulivyosikia.Pamoja na hayo napenda kwanza nikushukuru kwa kukubali kuonana nami usiku huu..Ni kutokana na habari hizo kuwa mbaya ndio maana nimekuita kwa ajili ya kuongea mawili matatu .”
Nilivuta pumzi nikanywa funda la mvinyo .David akanitazama kisha akasema
“ Tonny hata mimi nilistuka sana niliposikia mambo yaliyokupata.Nimefurahi sana kwa kuniamini na kuona ninafaa kwa kipindi kama hiki kukaa na kujadili nawe mambo mawili matatu.Pili kabla hujanieleza kile ulichoniitia,nimeng’amua unaweza kuwa na jambo zito na la maana kubwa, na kwa mantiki hiyo sidhani kama hapa panafaa kuongelea suala lolote la kikazi.Nadhani ingekuwa vizuri kama tungeenda kuongelea katika gari langu hapo nje au sehemu yoyote nyingine.”
Akasema david huku akiangaza angaza pande zote kana kwamba kuna mtu alikuwa akimtafuta.Kwa jinsi nilivyomsoma kwa haraka haraka alionekana ni mtu mwenye wasi wasi mwingi.Sikumtilia maanani sana,nikamfanyia ishara tukainuka na kutoka nje kuelekea mahala alikopaki gari lake.
Tulipolifikia gari lake akanifungulia mlango wa mbele nikajitoma ndani naye akaingia akaliwasha na taratibu tukaanza kuondoka maeneo hayo ya afrique casino.Nilishangaa kwa kitendo kile cha kuliwasha gari na kuliondoa hapo kasino kwa sababu hatukuwa tumeelewana kuwa tuende mahalikokote kwingine.Mwazoni nikafikiri kuwa labda ameona ni busara kama tungetoka kabisa nje ya jingo hili.Tukiwa katika mzunguko wa kuondokea hapo kasino taratibu nikaiskia kitu cha baridi kinanigusa shingo.Nilitaka kugeuka lakini nikasikia sauti kali ya mwanamke ikiniamuru
“Hivyohivyo ulivyo,usijaribu kugeuka”
Nywele zikanisimama.Sikutaka kuumiza kichwa kung’amua kuwa nilikuwa nimekamatwa.Kumbe David alikuwa ameweka mtego.
“Damn you David” Nikasema moyoni kwa hasira.
Kama vile mtu aliyeamriwa David akakanyaga mafuta na gari ikaondoka mithili ya ndege inayotaka kupaa.Hii ilitosha kabisa kunidhihirishia kuwa huu ulikuwa ni mpango uliosukwa na David ili kunikamata.Kukamatwa kirahisi namna hii kulinipa shida sana.Kama kawaida akili yangu ikaanza kufanya kazi haraka haraka ni jinsi gani ningeweza kujitoa mikononi mwa david na huyo mwenzake.Sikuamini kama David anaweza akanifanyia kitendio kama kile kutokana na jinsi nilivyokuwa nikimuamini.Kwa upande mwingine sikumlaumu sana David kwa sababu alikuwa kazini na ninajua alifanya kitendo kwa kutekeleza amri ya wakuu wake.wa kazi.
Sauti iliyokuwa nyuma yangu haikuwa ngeni sana masikioni mwangu.ni sauti ambayo nimewahi kusikia ,ni sauiti ambayo niliifananisha na sauti ya mtu Fulani ambaye si mgeni kwangu.”Lakini hii inaweza kuwa sauti ya nani? Nilibaki nikijiuliza bila kupata jibu.Tofauti na sauti ile niliyoizoea hii ilikuwa nzito kidogo na yenye mkwaruzo.
“Mpaka hapa hakuna mtu yeyote ninayepaswa kumuamini kwa sasa..Hakuna mtu yeyiote anayeweza kunisaidia.Watu wote wameamini kuwa ninahusika na milipuko ya Arusha na kila mmoja anajitahidi anitie nguvuni.Isiwe taabu,I’ll fight on my own” Nikajisemea moyoni huku nikijaribu kuangalia kama ninaweza kupata mwanya wowote wa kuweza kujiokoa.
Bastora mbili zilikuwa kichwani kwangu.Sikutakiwa hata kugeuza shingo yangu,kwa sababu kitendo hicho kingenisbabaishia matatizo makubwa.Siku zote mtu akikuelekezea bastora ni lazima uwe mpole na mtii kwa sababu tayari dhamira ya kuua iko moyoni mwake hivyo ukimletea shida anaweza akakuua muda wowote ule.
Gari lilikuwa likenda kwa kasi ya ajabu.Sikujua walikuwa wakielekea wapi.Sikuamini kama David angeweza kuwa dereva mzuri kiasi kile.Dakika kama ishirini baadae toka tuondoke pale afrique kasino ,gari likakata kulia na kuanza kuelekea kituo cha kati cha polisi.Akili yangu ikafanya kazi haraka haraka nikang’gamua kuwa walikuwa wakinipeleka kituoni.Kufikishwa polisi kungeharibu na kutibua mpango mzima.Sikutaka jambo kama hilo linitokee na hapo nikafanya jambo ambalo hakuna aliyelitegemea.
Kama umeme nikainua mkono wangu wa kushoto na kumpiga David ngumi kali sana ya uso inayomfanya aone nyota na kupoteza uelekeo.Akiwa bado katika taharuki ,kufumba na kumbua nikageuka na kumpiga yule mtu wa nnyuma aliyekuwa ameniwekea bastora kichwani ngumi nzito inayomfanya aanguke katika kiti.kwa haraka nikamkusanya shati lake,nikamvutia kwangu na kumpiga kichwa kizito kinachompoteza fahamu.gari ilikuwa ikiserereka kuelekea pemBeni kutokana na mwendo mkali lililokuwa likienda.Bado David alikuwa akicheza na usukani ili kuliepusha gari lisiweze kugonga miti iliyokuwa pemBeni ya barabara.Lengo lake lilikuwa ni kuwahi kufika pale polisi.Sikumkawiza nikampa kichwa kizito sana kinachomfanya aachie usukani na kutoa yowe la uchungu.Nikaushika usukani halafu nikaupenyeza mguu na kukanyaga pedeli ya breki na gari ikasimama huku matairi yakilalama kwa ukelele mkubwa.Kwa kasi ya ajabu nikaufungua mlango na kumpiga David teke kali la mbavu linalomtoa nje .Sikuwa na imani kama mbavu zake zilikuwa salama kutokana na uzito wa teke lile.Nikaukalia usukani na kuligeuza gari ,nikaliweka kati kati ya barabara na kuondoka kwa mwendo mkali .Kwa mara nyingine tena nilikuwa nimefanikiwa kulizima shambulio la kunikamata.
Nikiwa katika mwendo mkali ,pamoja na mateka wangu nyuma ya gari nilikuwa nikigeuka mara kwa mara na kuangalia kama nilikuwa nikifuatiliwa.Kitendo nilichokifanya pale mbele ya kituo cha polisi ni lazima kingezua udadisi na kuwafanya waanze kunifuatilia.
Kwa wakati huu nilihitaji kupata mahala ambako ningefanya ofisi ya muda kwa sababu sikuwa na sehemu yoyote yenye usalama ambayo ingeniwezesha kufanya kazi zangu kwa amani bila kuwa na wasi wowote wa kufuatiliwa na vyombo vya usalama.Mateka wangu niliyekuwa naye ndani ya gari nilitegemea ni lazima angenisaidia kupata taarifa muhimu nilizozihitaji kwa maaana hiyo nilihitaji kupata sehemu nzuri yenye utulivu ambayo ningeitumia kumuhifadhi na kumuhoji.Nilifikiria kwenda tena kwa Rose lakini nikalifuta wazo hilo haraka.Wanawake si watu wa kuwaamini hata kidogo katika shughuli hatari kama hizi.Nimekwisha jifunza toka kwa Monica.Ningeweza kwenda nyumbani kwangu lakini kwa sasa hapaingiliki na nina imani lazima ofisi yetu na jeshi la polisi watakuwa wameweka ulinzi ili nikijitokeza tu wanikamate.Sikupendelea vile vile kwenda katika nyumba za kulala wageni kwa sababu si sehemu muafaka kwa kazi hii na isitoshe kwa hivi sasa kutakuwa na msako mkali sana wa kunitafuta katika nyumba zote za wageni.Nilichekecha akili na hatimaye nikapata jibu.Afrique Casino.Nitaweka makazi ya muda pale.Sehemu ili ni sehemu yenye umati wa watu kwa masaa ishirini na manne na ni sehemu ya starehe na hivyo hawawezi kamwe kufikiri kuwa ninaweza kwenda kujificha pale.Katika kasino hii kulikuwa na vyumba vya kulala ambavyo gharama yake ilikuwa ya juu mno.Katika kibegi changu kidogo kilichokuwa na zana zangu za kazi kulikuwa na kiasi cha shilingi laki saba nlizozichukua nyumbani kwa ajili ya kunisaidia pale itakapobidi.Kadhia kama hizi mara nyingi huwa zinahitaji pesa ya kutosha.
Haikunichukua muda mrefu kufika Afrique Casino.Nilipaki gari maegesho na kumgeukia mateka wangu ambaye bado alikuwa hajapata fahamu.Nikainama ili kumtazama vizuri na kujua hali yake.Lo ! Nikakapatwa na mshangao mkubwa.Mateka wangu alikuwa ni Catherine Bhoke.Nilitabasamu huku nikimhurumia binti yule kwa kitendo alichokifanya kwa sababu kilihatarisha maisha yake.Ningeweza hata kumuua mwenzangu bila kujua.Pamoja na kumhurumia nilimsifu vile vile kwa kuwa na ujasiri wa kuamua kupambana na mimi..
Niliziokota bastora zake mbili zilizoanguka pemBeni yake nikazifutika kiunoni nikambeba na kuingia naye ndani.Nilisimama sehemu ya mapokezi na mateka wangu akiwa begani,Hapo mapokezi kulikuwa na mwanadada mmoja aliyeonyesha kuwa alikuwa akisinzia.Nilikodisha chumba kikubwa ambacho thamani yake ilikuwa dola mia moja kwa usiku mmoja.Chumba hiki kilikuwa ghorofa ya juu kabisa.Mimi na mateka wangu begani tukapanda lifti hadi ghorofa ya juu kilipo chumba nilichokodisha.Kila niliyekutana naye aliamini kuwa binti yule alikuwa amezidiwa na kilevi.haikunichukua muda mrefu kukipata chumba kile namba 364 R.Niifungua mlango na kujitoma ndani.Nilipapasa ukutani na kuwasha taa.Chumba kilikuwa kikubwa na kizuri.Kulikuwa na kitanda cha futi sita,sofa nzuri,televisheni,friji n.k.Nilimlaza Catherine katika sofa na kuanza kukikagua chumba chote..Niliporidhika na usalama wa chumba kile nikawasha kiyoyozi ili kuipooza hali ya hewa mle chumbani.Dakika kama saba hivi toka tuingie mle chumbani Catherine akafumbua macho taratibu.Akazungusha macho ili kutambua mahala alipo.
“Hallo Catherine” Nikasema huku nikitabasamu.
Hakunijibu kitu badala yake akakunja uso kwa hasira.
Tulibaki tumetazamana na Catherine kwa takribani dakika kumi hivi,nikahisi Catherine ameanza kuogopa.Niliinuka pale nilipokuwa nimekaa ,nikatoa bastora zile mbili za Catherine na kumpatia.
“bastora zako hizo Cathe.Mimi sizihitaji.Wakati mwingine ukitumwa kazi unatakiwa uwe makini sana.” Nilisema huku Catherine akiniangalia kwa mshangao mkubwa wa kutokuamini.
Nilimwangalia Catherine kwa macho makali halafu nikamwambia
“Sikiliza kate.Nataka unipe ukweli.Ni ukweli huo tu ninaoutaka ndio utakaotuweka wewe na mimi salama.Iwapo utanidanganya au kutokunipa ushirikiano wa kutosha basi mambo yatakuwa magumu na nitakulaumu sana katika maisha yangu yote”
Cathe akanitazama kwa makini na kwa mara ya kwanza toka amefika mle chumbani akasema
‘” Ni mambo gani unataka kujua na kwa nini useme mimi na wewe tuko hatarini?
“Vizuri Catherine.usiwe na haraka utafahamu kila kitu ,muhimu naomba ushirikiano wako wa dhati kabisa.Kitu cha kwanza ninachotaka kufahamu nini lilikuwa kusudio la kutumwa mnikamate?
Catherine akaniangalia kwa macho yake makubwa halafu akasema
“Sikiliza Tonny,usinidanganye kuwa hujui ni kwa nini unatafutwa .Serikali na Umma wote wa Tanzania wanafahamu kuwa wewe ndiye mtuhumiwa namba moja wa mauaji ya Arusha.Serikali inakutafuta kwa nguvu zote.Na wala usijidanganye kuwa huwezi kupatikana.Nina uhakika siku ya leo haitaweza kuisha kabla haujatiwa nguvuni.”
Catherine akasema kwa kujiamini.Alikuwa akijiamini kupita kiasi .
“naelewa hilo Catherine.Je mna taarifa zozote ni jinsi gani ninahusika na mlipuko wa Arusha? Nikauliza tena.
“Si kazi yangu mimi kujua ni jinsi gani unahusika na tukio la arusha.Kazi yangu mimi ni kuhakikisha unatiwa nguvuni haraka iwezekanavyo.” Cathe akasema kwa ukali.Sikutaka kuendelea kumuuliza kitu chochote nikasubiri hadi hasira zake zipungue.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…………..