Riwaya: Barua Kutoka Jela

Riwaya: Barua Kutoka Jela

Bravo Mr Rocky Sayari yetu hii, PESA imeshika katikati ya ufahamu wa mwanadamu,sasa inasakwa kwa njia halali au haramu.
^^


Mkuu Himidini nilimuona mmoja alianzisha lake mahali tena kwenye bustani zile za jiji hana waumini akaanza kuhubiria wale wanaokuja kupumzika kwenye zile bustani mara kapata watu wawili watatu akatafuta sehem kwa mtu akakodisha akaweza hema mara waumini wakaongezeka akaongeza eneo na kuanza kujenga kwa mbao nyumba ya ibada
Miaka miwili iliyofuata mama ana V8 mpya tatu na ana kanisa kubwa na kile kiwanja kashanunua


Mwingine kaanzisha la kwake nyumbani waumini wanawahi asubuhi kwake kumfanyia usafi wa nyumba yake na kulisha mifugo yake na kuhakikisha nyumba ya mama mtumishi iko safi
Mtumishi anatakiwa asiishiwe sukari wala mafuta wala mchele so waumini ni kujichanga kununua sukari, mchele, mafuta, unga, sabuni mtumishi asiteseke
Sasa hao waumini sasa badala ya kufanya biashara waendeleze kwao wao wanakazana kumpelekea mtumishi ambaye bado na sadaka anawakamua pia
Na wewe muumini ambaye saa moja uko kwa mtumishi ni muda gani utafanya kazi za kwako
Tumeingilia thread ya watu mkuu Himidini
 
Last edited by a moderator:
RIWAYA: BARUA KUTOKA JELA
MTUNZI: GAMA Ibrahim


SEHEMU YA KUMI NA TANO




Dokta Masawe alifuta machozi kisha akaendelea.
*Nilipomkubalia alinipiga busu zito, akaniachia na pesa shilingi Elfu hamsini tasilimu, akaniaga nakutoka. Baada ya kama wiki tatu baadae Hamida alikuja na mumewe ili kuja kupima ujauzito, nami nikajua mchezo umeshaanza! Nilimchukua vipimo vya damu ya mshipa pamoja na mkojo wake nikajifungia navyo maabara, nilipotoka nilimpa Hongera Bwana Bartazal na atarajie mtoto wa kiume!
Kwa kweli Bwana Bartazal alionyesha furaha isiyo kifani, kwani alimkumbatia mkewe na kumbusu mbele yangu, huku akiniambia, Dokta niliwahi kuahidi mbele yako kuwa mke wangu akipata ujauzito, nitamuandikisha mali zangu zote, kwa kuwa hili limetimia, basi na mimi sina budi ila kutimiza ahadi yangu kwani Ahadi ni deni!*
*Bwana Bartazal alimuandikisha mali zake zote mkewe.
Ilipofika miezi mitatu Hamida akanijia nakuniambia, sasa umefika wakati wakupata Robo ya mali yangu, kama tulivyokubaliana, na ili jambo hilo litimie, bado juhudi zangu zinahitajika!
Nazo nikumpa mbinu ya kumuuwa mume wake mpendwa Bwana Bartazal Halim.
Nikifanikisha hilo, muda si mrefu nitafungua Hospitali kabisa, badala ya Zahanati! Nami kwa kuwa Shetani alikuwa anatawala mbele yangu, nikampa vidonge vya SALBUTAMOL kumi ili amtilie kwenye Juice. Nakweli Hamida alivichukua vidonge vile nakumtilia mumewe vyote kwenye Juice kama nilivyomuagiza, na mara yule bwana alipokunywa Juice ile, saa moja baadae akawa marehemu Baltazar!*
Inspekta Jamila na Afande Kubuta walikuwa wanatingisha vichwa kwa huzuni ,wakimsikitikia marehemu Bartazal kwani niya yake njema, imemtoa roho yake.
Ama kwa hakika Mbega hufa kwa uzuri wake!
Dokta Masawe alikuwa anafuta machozi pamoja na uharamia wake alioufanya lakini alikuwa anaijutia nafsi yake, ama kweli Damu nzito kuliko maji.
*Okey nini kikaendelea?*
Afande Kubuta akamuuliza Dokta Masawe.
*Kilichoendelea Hamida saa moja baadae alipohakikisha kuwa mumewe amekwisha fariki, alikwenda kuimwaga ile juisi iliyobaki, na akatungua kilio kikubwa ili kujaza watu, na kweli majirani zake wakajaa nyumba tele nakuuliza kulikoni, akawaambia kilichojiri ni kwamba, yeye Hamida alikuwa amelala akamuacha mumewe anaangalia Tv, sasa baada yakugeuka nakuona mumewe hajarudi kitandani, akatoka sebuleni ndipo alipomkuta mumewe yupo katika hali hiyo wanayomuona nayo, huku akisisitiza kuwa ameshamuamsha sana bila mafanikio!
Na hapo wale majirani wakatoa wazo la mwili ule kupelekwa Hospitali ili ukachunguzwe kilichomsibu bwana Bartazal, lakini pia Daktari ndiyo akathibitishe kama Bartaza amekufa!
Hapo Hamida akashauri mwili ule uletwe kwangu kwakuwa mimi ndiyo Daktari wao, na hata waliponipigia simu kunifahamisha kilichojiri, mimi niliwaambia nitakwenda mwenyewe pale kwake ili nikamchunguze na kumchukua vipimo!
Hata nilipofika pale na kumchunguza yule Bwana ukweli ulibaki palepale kuwa yule bwana alikwisha fariki!
Niliwathibitishia kwamba mwili ule ni wa marehemu, na amekufa kiasi cha saa moja nyuma, na kilichosababisha kifo chake ni Presha! Iliyosababishwa na mshtuko wa kuona au kusikia jambo lililompa mshtuko nakupelekea kifo chake!*
*Sawa Dokta Masawe hadi sasa tumeelewa Makoko na Matandu ya kifo cha Bwana Bartazal Halim, je na kifo cha Hamida nini kilikuwa chanzo kwa jinsi unavyoelewa, kumbuka kutuambia ukweli kwako kunaweza kusababisha tusichukue hata senti tano yako, na wewe tukakuachia huru!*
Inspekta Jamila alikuwa anatumia DIPLOMASIA zaidi ili kumlegeza Dokta Masawe, kuliko kutumia nguvu isiyokuwa na lazima.
Kama wafanyavyo baadhi ya askari wenzake, wanapotaka kujua jambo Fulani kwa mtuhumiwa!
*Kifo cha Hamida kwa kweli kilitokana na yeye kunizima mafao yangu. Baada yakumkamilishia kazi yake, kwani alikuwa ananikimbia akabadilisha mpaka namba ya simu, kwa kuwa Mshahara wa dhambi ni mauti, nami sikukubali kupata Dhambi za kuua bure bileshi, hivyo nikawatuma majambazi wakenda kummaliza Hamida ili tukose sote. Nalitote tugawane mbao!*
Dokta Masawe kwakadiri alivyokuwa akisema ukweli, alijuwa baadae atakuwa huru hivyo hakuona sababu ya kupindisha maelezo!
Afande Kubuta akamuuliza Dokta Masawe. *Hao Majambazi uliowatuma uliwapataje?*
*Majambazi walio wengi ninawafahamu. Kwani wanapopambana na polisi,na kujeruhiwa na risasi huja katika Zahanati yangu nami huwatibia kwa siri, kisha hunipa pesa nyingi sana, ambapo mgonjwa wa kawaida hawezi kutoa pesa hiyo hata kwa nini, na kwa kiasi kikubwa ukiwa na watu wale kazi ya Udaktari utaiona inalipa sana, ingawa kuanzia sasa sitaki tena kufanya biashara ile!*
Inspekta Jamila akamuangalia Dokta Masawe kutoka chini hadi juu, kisha akatingisha kichwa na akasema.
*Unazo taarifa kama Dereva wa Taxi anaeitwa Mwaduga Dingo, yupo ndani mahabusu kwa kosa la mauaji ya Hamida? Na Je! Unamfahamu kijana huyo, na anahusika na chochote katika mauwaji yale, kwani wewe ndiyo ulieyapanga mauaji ya Hamida na unawajuwa watu waliofanya mauwaji yale!*
*Hapana yule Chalii hausiki hata kidogo, kwani yule aliwapakia kina Baajuni siku ile wakitokea Zahanati kwangu kuchukua malipo ya kazi yao, na walikuwa wanakwenda Baa ya Macheni ili kukutana na Kiongozi wao, ambae mimi sijawahi kukutana nae hata siku moja.
Sasa walipofika pale wakawaona askari wa Doria, na wao kwa mapepe yao wakakimbia bila sababu, wakidhani kuwa bosi wao ameshakamatwa, na pale walikuwa wanasubiriwa wao, kumbe sivyo!*
Dokta Masawe alikuwa akimkataa Mwaduga Dingo kwamba hamfahamu ila bahati mbaya tu imemkumba kwani LILILOKUWA LA KUKUPATA, HALIKUWA LA KUKUKOSA NA LAKUVUNDA HALINA UBANI!
Na mara simu ya Inspekta Jamila ikaita. Alipoangalia saa yake ilikuwa inaonyesha ni saa tisa na robo!
*Duh kumbe muda umekwenda hivi!* aliwaza kisha akaipokea simu, mambo aliyoelezwa kwenye simu kamwe hakuyaamini masikio yake, lakini ndivyo ukweli ulivyotokea.
Wale askari walioagizwa na Inspekta Jamila kwenda kule Baracuda, wamempigia simu wakimueleza kuwa; Jambazi Geradi Mwaipopo limevunja mtego wa polisi, nakufanikiwa kutoroka, lakini pia amejeruhi askari wawili kwa risasi!
Taarifa hiyo ilimpa wakati mgumu sana Inspekta Jamila na hakutaka kusema taarifa ile kumwambia Afande Kubuta mbele ya Dokta Masawe, hivyo wakaendelea kunyonya taarifa kutoka kwa Dokta Masawe mpaka waliporizika kwa yale waliyoyapata!
Ila kitu ambacho sio Dokta Masawe, wala Afande kubuta alichokuwa anajuwa kuwa mazungumzo yale Inspekta Jamila alikuwa Anaya record kupitia Simu yake kwa njia ya Video na Audio!
*Haya sasa jamani yote mliokuwa mnayataka kutoka kwangu, nimewaeleza,na hata aliyonihadithia Marehemu Hamida nimewaambia, basi tumalizane ndugu zangu na nawaahidi sitofanya tena jambo kama lile Yesu na Maria!*
Dokta Masawe alikuwa anataka msamaha kwa gharama yoyote ile!
*Sawa Dokta Masawe tumekuelewa, lakini bado hujatupeleka au kutuelekeza wanapo patikana wale watu tunaowatafuta, hivyo kuwa kwako nje kutatufanya tuharibu upelelezi, au kwa njia rahisi tu niseme, sisi askari polisi, hatuna mamlaka ya kumaliza kesi kienyeji, hivyo fanya subira ili sheria ichukue mkondo wake, kwani hadi hapa tulipo una mashitaka mawili yakujibu tena yote ya mauaji, yaliyotokea katika nyumba moja na yanawahusu Mke na mume!*
Inspekta Jamila aliposema maneno haya, Dokta Masawe alikuwa analia kama mtoto mdogo aliekimbiwa na mzazi wake!
****
Siku ya jumatano katika jiji la Dar es salaam, upepo ulikuwa unavuma kutoka mashariki kwenda magharibi, hivyo kufanya eneo lile la Mwambao wa pwani, kuwa na hewa safi.
Watu walikuwa wengi katika eneo la Mahakama ya Mkoa wa Dar es salaam, Maarufu kwa jina la Mahakama ya Kisutu.
Mahabusu walikuwa wameshaletwa kutoka magerezani na vituo vya Polisi, miongoni mwao alikuwepo mtuhumiwa wa kesi ya Mauaji, dereva wa Taxi, Mwaduga Dingo aliekuwa ameshika tama muda wote toka waliposhushwa kutoka katika basi la magereza wakitokea Gereza la Keko, wakikutana na watuhumiwa kutoka katika gereza la mahabusu la Segerea.
Nje ya mahakama walikuwepo watu wengi waliokuwa wakiwafuatilia ndugu zao, walikuwepo waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali, na katika pembe moja ya eneo lile alikuwepo Eshe Muhidini mke wa Mwaduga Dingo, na jirani yao Bwana Masudi pamoja na mkewe.
mtoto wa Mwaduga anaeitwa Marijani, anaepata miaka mitatu na nusu au mine akiwa amekaa chini katika kivuli cha mti, jirani na mama yake akichezea kokoto wala hana habari na dunia inavyokwenda. Mara ikasikika sauti ikisema
*Mahakama karibu inaanza, hivyo wale wote waliokuja katika mashauri ya kesi, waingie mahakamani na muhakikishe mnazima simu zenu*
Lilipokwisha tangazo lile, Eshe alimbeba mtoto wake na akajongea Karibu huku akiwa ana kiherehere cha hali ya juu sana.
*COOOOOOOOOOOORT*
Sauti ya askari mkakamavu ilikuwa inaashiria kuwa Muheshimiwa Hakimu alikuwa akiingia mahakamani hivyo pia kuashiria watu wote wasimame ili kumpa heshima muheshimiwa.
Muheshimiwa Hakimu mkazi alikaa katika sehemu yake, na mara moja taratibu za kimahakama zikaanza.
Kesi ya tatu kutajwa ilikuwa inamuhusu Mwaduga Dingo,na ilipotajwa namba ya kesi yake na karani wa Mahakama, Mwendesha mashtaka wa serikali akasimama baada ya karani kukaa katika kiti chake, akiwa na faili la kesi ile akasema.
*Niipendeze Mahakama yako Muheshimiwa, naitwa Mabewa wakili wa Serikali naiwakilisha Jamhuri, Shauri hili lilikuja kwa kutajwa upelelezi wake bado unaendelea, ila kutoka kwa mkurugenzi wa mashitaka kanda ya Dar es salaam nina NOLLE PROSEQUI UNDER SECTION 91(1) OF CRIMINAL PROCEDURE ACT, 1985 (CAP 20 R.E 2002)*
Ilikuwa ni kauli ya muendesha mashtaka Wakili wa Serikali akiifahamisha Mahakama hatua ya kesi ya Mwaduga ilipofikia wakati huo huo alifungua Jalada la Kesi ile na kutoa Ganda gumu la njano na kumkabidhi Karani wa Mahakama ili ampe Muheshimiwa Hakimu kwa uthibitisho, na hatimae kutoa maamuzi.
*Mshitakiwa Mwaduga Dingo kuanzia sasa Mahakama yangu imekuachia huru unaweza kwenda.*
Muheshimiwa hakimu baada ya kuipitia ile karatasi ya njano, alitoa maamuzi.
Ama kwa hakika Mwaduga Dingo aliiona nyota ya Jaha!
Furaha iliyochanganyika na huzuni ilitawala katika kichwa chake, akashindwa kuamini ukweli kwamba yupo huru,alihisi yupo ndotoni.
machozi yakambubujika mfululizo, huku akiwa anateremka kutoka kizimbani, akawa anajisemea ndani ya moyo wake.
*Yote yalionifika, namuachia manani
Ni yeye alietaka, mimi kuwa gerezani
Tabu dhiki na mashaka, nivijuwe kwa undani
Katu sidai fidia, mola atanilipia!*


*Mke wangu mtukuka, na mwanangu Marijani
Sameheni bila shaka, mtaingia peponi
Kila linalokufika, mja kwako mtihani
Katu sidai fidia, mola atanilipia!*
*Kusamehe kwa hakika, ndiyo bora duniani
Kwa dhati ninatamka, sina kinyongo moyoni
Ila hayatafutika, hadi niwe kaburini
Katu sidai fidia, mola atanilipia!*
Eshe akiwa na mtoto mgongoni, alishindwa kujizuia alipomuona mumewe anatoka nje ya Mahakama ile akiwa huru, alilia kilio cha furaha huku mke wa Masudi akimbembeleza.
Mwaduga alipotoka tu pale nje ya mahakama waandishi wa habari walimzonga, huku Camera zao zikichukua picha kwa ajili ya magazeti na picha za Televisheni.
Wakiwa katika mahojiano. Mara walitokea polisi na kutimua watu kisha wakamkamata Mwaduga na kumtia ndani ya gari ya polisi aina ya Land Rover Difender 110 na kuondoka nae kituuteni, hadi kituo cha kati cha polisi mkabala na Relwe Stesheni.


***HATIMAYE Mwaduga huru…….
LAKINI ghafla tena mikononi mwa polisi nini tatizo???

Jagarld Jullie Z Sangomwile Khantwe Mr Rocky Gunda66 Himidini VAN HEIST BPM ABUBAKAR SHEKAU NYIROmamsapkhan born again pagan princetx Ennie mcubic jonnie_vincy slim5 MAVUNO mp anold amoneyazan
 
ram pande hz panakuhusu
 
Last edited by a moderator:
Hadith ni tamm sana
Sasa mwaduga amekamatwa tena au mwaipopo katuma askali nini??
 
RIWAYA: BARUA KUTOKA JELA
MTUNZI: GAMA Ibrahim


SEHEMU YA KUMI NA SITA

Eshe akiwa na mtoto mgongoni, alishindwa kujizuia alipomuona mumewe anatoka nje ya Mahakama ile akiwa huru, alilia kilio cha furaha huku mke wa Masudi akimbembeleza.
Mwaduga alipotoka tu pale nje ya mahakama waandishi wa habari walimzonga, huku Camera zao zikichukua picha kwa ajili ya magazeti na picha za Televisheni.
Wakiwa katika mahojiano. Mara walitokea polisi na kutimua watu kisha wakamkamata Mwaduga na kumtia ndani ya gari ya polisi aina ya Land Rover Difender 110 na kuondoka nae kituuteni, hadi kituo cha kati cha polisi mkabala na Relwe Stesheni.
Huku nyuma yakaachwa maswali kadhaa, huku wale waandishi wakifanikiwa kupiga picha za video tukio lile!
Eshe sasa alikuwa hajitambui kwa kilio, kwani alikuwa anagalagala chini kama mtoto mdogo!
Mwanae analilia huku na yeye analia kule, kukawa kati ya mama na mtoto hakuna wakumnyamazisha mwenzie, tafrani moja kwa moja!
Masudi alikuwa haamini macho yake kwa kitu kilichotokea, kwani rafiki yake ameshaachiliwa huru na mahakama,sasa anakamatwa tena kwa kosa gani?!
Eshe akajizoazoa pale chini akamwambia shemeji yake Masudi;
"Shemeji kama simu yako ina pesa tafadhali naiomba ili nimpigie simu Inspekta Jamila."
Masudi akampa simu yake iliyokuwa na pesa ya kuweza kuongea na Eshe akampigia simu Inspekta Jamila huku akiwa analia kwa kwikwi.
Inspekta Jamila aliipokea ile simu ,Eshe alijitambulisha kwake na kumpa tukio lililotokea muda mfupi uliopita.
majibu aliyoyapata kutoka kwa yule askari wa kike yalimshangaza. Kwani Inspekta Jamila alimjibu kwa mkato kwamba.
"MBWA HAFI MAJI, AKIUONA UFUKWE." Kisha akamtaka aende ofisini kwake anamsubiri!
*******
Mwaduga Dingo alipelekwa kituo cha polisi cha kati, akaingizwa ndani huku akiwa ametaharuki kwa kiasi kikubwa, akiwa haamini na haelewi kipi kilichomsibu! Akawauliza wale askari waliomkamata.
"Mnanikamata kwa kosa lipi, wakati kesi mlionibambikizia, nimeshaachiwa huru?!"
Wale askari wakamwambia.
"Hapa hatuna shitaka na wewe, ila tumetumwa tukukamate na sisi tumetekeleza amri, hivyo subiri mpaka tupate maelekezo mengine!"
Mwaduga alichoka choko kwa kauli ile ya wale wana usalama, alichofanya ni kumuachia mungu, akapiga moyo konde akangoja kitakachotokea ili akabiliane nacho.
Dakika ishirini baadae aliingia Afande Kubuta na kumchukua Mwaduga.
Kitu kilichompa tofauti Mwaduga, ni kwamba askari huyu alimtesa sana siku alipokuwa anamuhoji ili amtajie wahalifu aliodhaniwa kuwa ni wenzie, ila sasa anamchukua kama rafiki yake!
Alitoka nae nje ya kituo kisha akapandishwa ndani ya gari ileile iliyokwenda kumchukua Dokta Masawe, Toyota Soluna yenye vioo vya kiza.{Tinted}
Huku akiwa anapulizwa na kiyoyozi ndani ya gari ile, Mwaduga alipelekwa ofisini kwa Inspekta Jamila, bila ya kufungwa pingu mikononi!
Alipofika katika ofisi ile Mwaduga alishangaa kumkuta mkewe na mtoto wake, rafiki yake Masudi na mkewe wakiwa na Inspekta Jamila wote kwa pamoja wakiwa wanapata vinywaji vya soda huku nyuso zao zikiwa zimekunjuka, zenye bashasha na tabasamu tele!
Na bila yakujifahamu, Mwaduga nae alijikuta akitabasamu.
"Pole sana Mwaduga, Karibu tena uraiani na sahau yaliyopita kwani, yaliyopita si ndwele, tugange yaliyopo, na yajayo."
Maneno hayo alikuwa anayasema Afande Kubuta, huku akimfungulia soda Mwaduga!
Kitendo kile kilikuwa kimepangwa na Inspekta Jamila ili Mwaduga asiweke chuki kwa Afande Kubuta katika yale yaliotokea siku za nyuma.
Mwaduga alitingisha kichwa kwa kukubali yale anayoambiwa huku akiipokea chupa yenye soda akasema;
"Kidonda kinapopona, lisalialo ni kovu
Kila unapoliona, ijapo liwe chakavu
Kumbukumbu huja tena, hata kama yakivivu
Yoye nimeyasamehe, ila sitoyasahau!"
Mwaduga aliposema maneno haya akamkumbatia Afande Kubuta, kisha akamkumbatia Inspekta Jamila, alipomkumbatia mkewe na mwanae, machozi ya furaha, yakachukua nafasi yake.
Mwisho akamkumbatia Masudi na mkewe, wote kwa pamoja akawaambia.
"Ndugu zangu nashukuru, kwa kuwa nasi pamoja
Kwani mlijikusuru, mkaacha yenye tija
Atawalipa ghafuru, moja kwa kumi na moja
Sina kubwa la kuwapa, zaidi ya shukurani."
Alipokwisha kuwashukuru wote kwa pamoja akambeba mwanae akakaa nae kitini, na Inspekta Jamila akamwambia Mwaduga.
"Kwanza pole kwa kizaazaa ulichokipata leo mahakamani, ila halikuwa jambo la bahati mbaya hata kidogo, bali ni mpango wetu jeshi la polisi kwa sababu ya usalama wako ilibidi tufanye vile! Kwani tuna hakika kuwa vyombo vya habari vingetangaza kuwa umeachiwa huru, ni dhahiri maisha yako yangekuwa katika hatihati, kwani wale majambazi wangesikia au kuona kupitia vyombo hivyo wangefanya Ima fa ima wakahakikisha wanakudhuru, au kukuondosha duniani ili usije kuwatambua, ikitokezea kuitwa kufanya hivyo!
Kwani kutoka sasa vyombo vya habari bila shaka vitatangaza kwamba umechiwa huru na kukamatwa tena!
Ingawa najua kwamba utajiuliza kuwa si bado watu watakuona ukiwa nyumbani kwako na labda kazini kwako pale Kituo cha Taxi cha magomeni usalama?!
Hilo tumejipanga nalo na tutakupa mikakati nini cha kufanya, pia wapo watu ambao tutataka uwatambue na baada ya hapo utaambiwa kitakachoendelea."
Inspekta Jamila akawageukia Masudi na mkewe, nao akawapa mikakati, mambo ya kuzingatia kwa kipindi hiki.
Baada ya hapo Masudi na mkewe wakaaga na kuondoka wakimuacha Mwaduga na Familia yake na wale askari wawili.
Huku nyuma Mwaduga alipewa mikakati ya jeshi la polisi linavyotaka afanye katika kipindi hiki.
Inspekta Jamila alizitoa zile picha alizokuwa amezichukua kwa njia ya video pale Friends Coner Hotel akaziweka mbele ya macho ya mwaduga Dingo, kisha akamwambia.
"Kuna yeyote unaemtambua katika picha hizi?"
Mwaduga alizitazama zile picha kwa makini, na wakati huohuo Inspekta Jamila na Afande Kubuta, wao walikuwa wakimtazama usoni Mwaduga.
"Hapa nawakumbuka hawa jamaa wawili."
Mwaduga alisema vile huku, akionyeshea kidole zile picha alizozikumbuka.
"Unawakumbukaje hawa jamaa, uliwahi kukutana nao wapi?"
Afande Kubuta alimtupia swali la haraka Mwaduga.
"Hawa jamaa, hakika ndiyo walionikodi siku ile kule Sinza, na huyu bwana huyu, ndiyo alienambia kuwa wanazo elfu tatu, niwapeleke kwa Macheni. Tena huyu bwana anaongea kwa kithethe huyu."
Mwaduga kama mtu aliepagawa, alikuwa ana hasira na wale watu kwelikweli.
"Na huyo mwengine?"
Afande Kubuta alimrudisha Mwaduga katika utambuzi, kwani tayari alikuwa keshapandwa na hasira.
"Huyu mwingine, alikuwa amepanda nyuma namkumbuka pia, tena huyu jamaa mwepesi kweli, kwani ndiye alieshuka mwanzo pale kwa macheni. Huku gari ikiwa bado haijasimama sawasawa!"
Mwaduga Dingo alikuwa anaichambua picha ya Jeradi Mwaipopo.
Baada ya utambuzi ule, Mwaduga Dingo pamoja na familia yake, walihamishiwa nje ya mji kwa muda, mpaka itakavyoamriwa vinginevyo, huku gharama za chakula, malazi na matibabu ikibidi, jeshi la polisi limechukua jukumu hilo!
*******
Siku ya Alhamisi saa nne ya asubuhi, ofisini kwa "IGP" kulikuwa na kikao cha dharula kujadili namna kesi ile ilipofikia, na inavyo endelea.
Miongoni mwa waliokuwemo katika kikao kile ni "IGP" mwenyewe, Kamanda wa kanda maalum, Kamanda wa mkoa wa kipolisi wa kinondoni, Mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini "DCI", Inspekta Jamila na Afande Kubuta.
Kikao kile kilikaliwa kiasi ya saa nzima wakubwa wale walitoa uzoefu wao, kwa vijana wao ilimradi mambo yaende sawa.
Mikakati ikakamilika mipango ikawekwa ili ndani ya wiki moja waweze kumaliza swala lile ili washughulike na mambo mengine!
"IGP" alikifunga kikao kile huku akiwa na matumaini makubwa kwa jinsi vijana wake wanavyochapa kazi kwa mwendo kasi.
Ruhusa ilitolewa na kila mmoja akarudi katika eneo lake la kazi.
Inspekta Jamila akiwa na Afande Kubuta wakiwa ofisini kwao, mara aliingia Mke wa Dokta Masawe na akataka kuongea na Afande Kubuta.
Yule Mwanamke jeuri wa Kichaga, tofauti na siku alipokuwa nyumbani kwake, wakati Afande kubuta akiwa na maaskari wenzake walipokwenda kwa minajili yakumkamata Dokta Masawe, leo alikuwa mpole na mwenye heshima kubwa!
Afande Kubuta na Inspekta Jamila walitazamana kisha, Afande Kubuta akamkaribisha mwanamke yule.
Baada ya kuketi akamuuliza.
"Nikusaidie nini Mrs Masawe?"
Mke wa Dokta Masawe akasema.
"Aksante nimekaribia, nimepigiwa simu na Mume wangu akiwa kituo cha polisi cha kati, na kuniambia kwamba amekamatwa, hivyo akanielekeza mahali hapa kwenu ili tuje kuongea ili tuyamalize!"
Maaskari wale wawili wakatazamana tena na safari hii akajibu Inspekta Jamila.
"Ndiyo mumeo amekamatwa jana kwa makosa ya mauaji, na kula njama kwa kushirikiana na majambazi katika kufanya uhalifu nchini, hivyo tumemkamata na baada ya kumuhoji mumeo amekiri shutuma hizo, hivyo ni kweli yupo kituo cha kati, baada ya kuwatia mbaroni washirika wenzake, itabidi wakasimame mahakamani, kujibu mashitaka."
Mke wa Dokta Masawe katika kitu alichosisitiziwa na mumewe, katika simu aliyoomba kwa askari pale kituoni, na akiongea katika lugha ya kichaga pekee ni kwamba,
Swala lile ahakikishe linaishia polisi, kwani kwa ushahidi uliopo akipanda mahakamani, hanusuriki na kifungo cha maisha, au kunyongwa kabisa hadi kufa!
Mke wa Dokta Masawe kwa majibu aliyoyapata kutoka kwa yule Askari wa kike yalimtisha na kumkatisha tamaa sana, hivyo akawaambia askari wale.
"Ndugu zangu naomba msaada wenu, yaliyotokea ndiyo yashatokea, hivyo nipo tayari kujisaidia naomba na nyie mnisaidie!"
Kwa mara ya tatu askari wale walitazamana katika siku ile, ikiwa kama hawaelewi alichokikusudia mke wa Dokta Masawe, wote kwa kauli moja wakasema.
"Tukusaidieje?!"
Na mke wa Dokta Masawe akasema huku akifungua mkoba wake.
"Nimekuja na Milioni mbili, naomba mchukue ili mnisaidie kulimaliza jambo hili likiwa polisi. Baada ya mume wangu kutoka tutawapa pesa nyingine!"
Mke wa Dokta Masawe alisema maneno yale na kutoa bulungutu la Fedha akaliweka juu ya meza ile, huku akiwatizama wale maaskari usoni mmoja baada ya mwingine.
Kilichotokea Mke wa Dokta Masawe hakukitegemea kabisa katika mawazo yake kama kingeweza kutokea!
Inspekta Jamila aliangaliwa na Afande Kubuta usoni, na Inspekta Jamila akakilaza kichwa chake kidogo pembeni ikiwa ni ishara ya kuruhusu jambo fulani kutendeka.
*******


**Vipi tena! ITAENDELEA


Jagarld Jullie Z Sangomwile Khantwe Mr Rocky Gunda66 Himidini VAN HEIST BPM ABUBAKAR SHEKAU NYIROmamsapkhan born again pagan princetx Ennie mcubic jonnie_vincy slim5 MAVUNO mp anold amoneyazan
 
Popote ulipo, jongea ram huku
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom