RIWAYA: Anga ya Washenzi na Gilbert Evarist Mushi

Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu Wa Nne
Sehemu ya 01
Lakini mita mia moja kutoka pale ilipopaki gari ya Daniel alisimama Elton Tonny ambaye ni mpambe wa Makamu wa rais. Elton Tonny alikuwa akilitazama gari la Daniel hadi lilipotoweka mbele ya macho yake. Upesi akakamata simu yake na kupiga namba fulani..

"Kila kitu kipo sawa huku. Kaeni tayari. Anakuja" Elton Tonny alisema na kurejesha simu mfukoni.
_____________
Daniel Mwaseba akiwa ndani ya gari aliuingiza mkono mmoja mfukoni na kuitoa simu yake, ni baada ya kusikia mtetemo mfupi wa kuashiria ujumbe kuingia. Akiwa makini na kuendesha gari, alitoa nywila katika simu yake na kuufungua ujumbe ule.

"Festus amezinduka."
Ulikuwa ni ujumbe mfupi kutoka kwa Gilbert Mwaitika. Akaamua kumpigia Gilbert. Simu ikaita kwa sekunde nne na kisha kupokelewa.

"Niambie Daniel" sauti ya Gilbert ikasikika ikisema simuni.

"Usiniambie Festus ameamka" Daniel akasema.
Wakati akiongea na simu, macho yake yakauona mteremko ukiambatana na kona kali mbele. Mita mia mbele ulikatiza mto mkubwa unaotoa maji yake kutoka kilele cha Mlima Kilimanjaro. Mto huo unajulikana kama mto Isiye ndio chanzo kikuu cha maji katika mto Pangani unaopita mkoani Tanga na kumwaga maji yake katika bahari ya Hindi.
Hali ilikuwa ni ya utulivu sana barabarani, hakukuwa na gari la ziada ama mtu akikatisha eneo la karibu. Daniel Mwaseba aliutoa mguu wake wa kulia kutoka kwenye kinyonya mafuta na kuupeleka katika sehemu ya kukanyaga breki ili aweze kuendana na mteremko ule mkali. Matairi ya gari yalianza kuisugua lami kwa mwendo wa taratibu na gari ilitii na kuanza kupungua mwendo. Lakini katika kupungua mwendo ulizuka mlio wa ajabu, mlio ambao ulishabihiana kwa kiasi kikubwa na mlio wa saa. Aliifungua droo ndogo iliyopo kwenye dashbodi ya gari na kuitoa saa yake, Lakini mlio anaousikia haukuwa ukitoka katika saa ile.

"Gilbert hebu subiri nitakupigia. Kuna kitu kinanichanganya hapa" Daniel Mwaseba alisema na kukata simu. Akaiweka mfukoni na kukanyaga breki tena na kupelekea gari kutembea kwa mwendo mdogo zaidi, akaisogeza gari yake hadi kando ya barabara ili aweze kuubaini mlio ule unatokea wapi.
Baada ya kupaki gari ile, Daniel Mwaseba alitega sikio lake kwa sekunde nane ndipo alipobaini mlio ule haukuwa ukisikika ndani ya gari, bali katika uvungu wa gari. Akafungua mlango wa gari na kutoka ili kwenda kutazama nje, alipofika akainama chini kidogo na kuchungulia...
Loooh!!! Aliona bomu limetegwa pembeni ya waya wa breki. Akajua bila shaka muda ule alipoikaribia kona iliyoambatana na mteremko akaikanyaga breki basi ilipelekea kulitegua bomu hilo kwani bomu hilo lilitegwa kuendana na mfumo wa breki ya gari. Hata hivyo asingeweza kulitegua bomu lile kwa kuwa alishachelewa, wakati anagundua bomu hilo, aliona sehemu yenye namba zinazojihesabu mithili ya saa zikionyesha zilibakia sekunde tano tu kabla ya bomu kulipuka.
Sekunde Tano zilikuwa ni nyingi sana kwa Daniel Mwaseba pindi awapo katika hatari, lakini leo hii zilikuwa ni chache sana, uchache huo ulitokana na ule mshangao uliomkumba baada ya kubaini kwamba lile ni bomu. Mshangao ule ukameza sekunde mbili, sekunde tatu zilizobakia Daniel Mwaseba aligeuka kwa kasi na kuanza kuzipiga hatua ndefu kukimbia...
Hakumalizia hatua ya pili, Mlipuko mkubwa ulitokea na kulisambaratisha gari lile huku yeye akirushwa kuelekea juu na kurushiwa umbali wa hatua kama Tano kutoka pale ulipotokea mlipuko. Pembeni ya barabara ile kulikuwa na mtaro mrefu sana uliojengwa kwa kuelekezwa katika Mto Isiye. Daniel Mwaseba aliporushwa kutokana na mlipuko ule alidondokea ndani ya mtaro ule na kubiringika mithili ya tairi hadi katika kingo za mto Isiye.

Dakika moja baada ya kutokea mlipuko ule ilifika Lori la kubebea mchanga na kupaki jirani kabisa na pale ulipotokea mlipuko. Punde vijana wapatao saba waliovalia tisheti nyeusi zenye nembo ya Fuvu la Kichwa wakateremka wakiwa na madumu makubwa yenye maji pamoja na mtungi mkubwa wa kuzima moto (Fire Extinguisher) na kuusogelea moto ule, mmoja wao alianza kuuzima moto kwa kutumia mtungi ule, baada ya moto kuzima wanaume wale walioshikilia madumu yenye maji walianza kumwaga maji sehemu ile na kukusanya vipande vya mabaki ya gari ya Daniel Mwaseba na kuvipakia ndani ya Lori. Baada ya kuhakikisha hakuna baki lolote lililosalia vijana watano walipanda lori lile na kuondoka. Vijana wawili waliobakia waliteremka na mtaro ule taratibu wakijisogeza mahali alipodondokea Daniel Mwaseba. Na mmoja kati ya wanaume hao alikuwa ni Henry.
Henry baada ya kuuona mwili ule alishtuka sana.

"Vipi, unamfahamu? Naona umeshtuka baada ya kumwona" mwanaume aliyeambatana nae akamuuliza Henry

"Aa.. amna, hata simfahamu ndio kwanza namwona leo. Kwani vipi?" Henry akajitetea akijaribu kujiweka sawa.

"Kumbe tuliyetumwa kumchukua ni Daniel Mwaseba! Daaah! Kama ningejua ni yeye ningemtaarifu mapema. Sijui nifanyaje hapa na wanaweza kunigundua kama nafahamiana nae" Henry alikuwa anawaza peke yake. Alikumbuka usiku wa jana kabla Daniel Mwaseba na wenzake hawajaachana naye alipatiwa karatasi yenye namba ya simu

"Chukua namba zangu. Ukipata chochote tutafahamishana." aliyakumbuka maneno haya, aliambiwa na Daniel usiku kabla ya kurudishwa na gari.

"Unawaza nini? Hebu tumwinue tunasubiriwa juu" Henry alishtuliwa na mwenzake kutoka kwenye dimbwi la mawazo. Bila kuchelewa wakashirikiana kuunyanyua mwili huo na kurejea nao barabarani, walipofika barabarani walikuta Noah Nyeusi imepaki pembezoni mwa barabara ikiwasubiri. Bila kuchelewa wakauingiza mwili wa Daniel Mwaseba ndani ya buti, wakaingia ndani ya Noah ile na kuondoka nayo.
-----------------------

Gilbert Mwaitika, Elizabeth Neville, Mwanasheria Mlevi pamoja na mwanadada aitwaye Cara walikuwa wakimsubiri Daniel Mwaseba kwa hamu kubwa. Hii ilikuwa ni baada ya David kuufungua mdomo wake punde tu baada ya kuzinduka. Wote walihamia nyumbani kwa Dokta Yusha baada ya kuitwa na Gilbert Mwaitika.
David hakuficha kitu, aliwaeleza jinsi alivyoitwa na mpambe wa Mheshimiwa Eliud Sumbi siku moja kabla ya ziara ya rais kufanyika. David aliwaeleza jinsi alivyokutanishwa na mheshimiwa Eliud Sumbi na kupatiwa mpango wa kubadili helikopta.

Siku ile ilikuwa hivi...
Baada ya David kuonana na mheshimiwa Eliud Sumbi, Siku hiyo walizungumza kwa takribani nusu saa na baada ya kuukubali mpango wa mheshimiwa Eliud, David alipatiwa dawa ya usingizi na Elton Tonny.

"Dawa hii utaipulizia kesho ndani ya Helikopta yenu nusu saa kabla ya kuingia. Baada ya hapo, muda ukifika wa kuirusha helikopta angani hakikisha wenzako ndio wanaanza kuingia ndani. Wakishaingia na kuvuta pumzi haitawachukua muda, watadondoka chini kama maembe machanga yaliyozidiwa na upepo" Elton Tonny alisema

"Watakufa?" David aliuliza baada ya kupatiwa dawa hiyo

"Hapana. Watapata usingizi mzito ambao hauamshiki hadi masaa thelathini na sita yapite. Wewe usiingie ndani hadi zipite tena dakika kumi na tano. Baada ya hapo utaingia, nawe utasinzia lakini ni kwa masaa manne tu ndipo utarejewa na fahamu. Ukisharejewa na fahamu utajifanya kutoa ripoti huelewi ni kitu gani kinaendelea. Na wakati huo sisi tutakuwa tumeshaimaliza kazi yetu. Kuhusu Helikopta ondoa shaka maana wakati huo tutairusha helikopta ya kufanana na yenu ili iwe rahisi kwa kazi yetu kukamilika"
David alipotaka kujua ni kazi gani aliambiwa atulie hadi itakapokamilika ndipo atajuzwa.

Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, wote wakaridhika na maelezo ya David, japokuwa walimwonea sana huruma kwani tayari alikuwa ni msaliti.

TUKUTANE TENA KESHO SAA 12 JIONI.

NOTE: Kama utauhitaji msimu huu wa nne utaupata jwa gharama ndogo tu ya Tshs 1000 tu. Lipia kwenda M pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie. Wale wengine tutaendelea kuisoma hapahapa kila ninapopata nafasi ya kuiweka.
Msimu wa Tano ndio msimu wa mwisho wa Riwaya hii, utaanza kupatikana kesho mchana kwa Tshs 700 tu
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu Wa Nne
Sehemu ya 01
Lakini mita mia moja kutoka pale ilipopaki gari ya Daniel alisimama Elton Tonny ambaye ni mpambe wa Makamu wa rais. Elton Tonny alikuwa akilitazama gari la Daniel hadi lilipotoweka mbele ya macho yake. Upesi akakamata simu yake na kupiga namba fulani..

"Kila kitu kipo sawa huku. Kaeni tayari. Anakuja" Elton Tonny alisema na kurejesha simu mfukoni.
_____________
Daniel Mwaseba akiwa ndani ya gari aliuingiza mkono mmoja mfukoni na kuitoa simu yake, ni baada ya kusikia mtetemo mfupi wa kuashiria ujumbe kuingia. Akiwa makini na kuendesha gari, alitoa nywila katika simu yake na kuufungua ujumbe ule.

"Festus amezinduka."
Ulikuwa ni ujumbe mfupi kutoka kwa Gilbert Mwaitika. Akaamua kumpigia Gilbert. Simu ikaita kwa sekunde nne na kisha kupokelewa.

"Niambie Daniel" sauti ya Gilbert ikasikika ikisema simuni.

"Usiniambie Festus ameamka" Daniel akasema.
Wakati akiongea na simu, macho yake yakauona mteremko ukiambatana na kona kali mbele. Mita mia mbele ulikatiza mto mkubwa unaotoa maji yake kutoka kilele cha Mlima Kilimanjaro. Mto huo unajulikana kama mto Isiye ndio chanzo kikuu cha maji katika mto Pangani unaopita mkoani Tanga na kumwaga maji yake katika bahari ya Hindi.
Hali ilikuwa ni ya utulivu sana barabarani, hakukuwa na gari la ziada ama mtu akikatisha eneo la karibu. Daniel Mwaseba aliutoa mguu wake wa kulia kutoka kwenye kinyonya mafuta na kuupeleka katika sehemu ya kukanyaga breki ili aweze kuendana na mteremko ule mkali. Matairi ya gari yalianza kuisugua lami kwa mwendo wa taratibu na gari ilitii na kuanza kupungua mwendo. Lakini katika kupungua mwendo ulizuka mlio wa ajabu, mlio ambao ulishabihiana kwa kiasi kikubwa na mlio wa saa. Aliifungua droo ndogo iliyopo kwenye dashbodi ya gari na kuitoa saa yake, Lakini mlio anaousikia haukuwa ukitoka katika saa ile.

"Gilbert hebu subiri nitakupigia. Kuna kitu kinanichanganya hapa" Daniel Mwaseba alisema na kukata simu. Akaiweka mfukoni na kukanyaga breki tena na kupelekea gari kutembea kwa mwendo mdogo zaidi, akaisogeza gari yake hadi kando ya barabara ili aweze kuubaini mlio ule unatokea wapi.
Baada ya kupaki gari ile, Daniel Mwaseba alitega sikio lake kwa sekunde nane ndipo alipobaini mlio ule haukuwa ukisikika ndani ya gari, bali katika uvungu wa gari. Akafungua mlango wa gari na kutoka ili kwenda kutazama nje, alipofika akainama chini kidogo na kuchungulia...
Loooh!!! Aliona bomu limetegwa pembeni ya waya wa breki. Akajua bila shaka muda ule alipoikaribia kona iliyoambatana na mteremko akaikanyaga breki basi ilipelekea kulitegua bomu hilo kwani bomu hilo lilitegwa kuendana na mfumo wa breki ya gari. Hata hivyo asingeweza kulitegua bomu lile kwa kuwa alishachelewa, wakati anagundua bomu hilo, aliona sehemu yenye namba zinazojihesabu mithili ya saa zikionyesha zilibakia sekunde tano tu kabla ya bomu kulipuka.
Sekunde Tano zilikuwa ni nyingi sana kwa Daniel Mwaseba pindi awapo katika hatari, lakini leo hii zilikuwa ni chache sana, uchache huo ulitokana na ule mshangao uliomkumba baada ya kubaini kwamba lile ni bomu. Mshangao ule ukameza sekunde mbili, sekunde tatu zilizobakia Daniel Mwaseba aligeuka kwa kasi na kuanza kuzipiga hatua ndefu kukimbia...
Hakumalizia hatua ya pili, Mlipuko mkubwa ulitokea na kulisambaratisha gari lile huku yeye akirushwa kuelekea juu na kurushiwa umbali wa hatua kama Tano kutoka pale ulipotokea mlipuko. Pembeni ya barabara ile kulikuwa na mtaro mrefu sana uliojengwa kwa kuelekezwa katika Mto Isiye. Daniel Mwaseba aliporushwa kutokana na mlipuko ule alidondokea ndani ya mtaro ule na kubiringika mithili ya tairi hadi katika kingo za mto Isiye.

Dakika moja baada ya kutokea mlipuko ule ilifika Lori la kubebea mchanga na kupaki jirani kabisa na pale ulipotokea mlipuko. Punde vijana wapatao saba waliovalia tisheti nyeusi zenye nembo ya Fuvu la Kichwa wakateremka wakiwa na madumu makubwa yenye maji pamoja na mtungi mkubwa wa kuzima moto (Fire Extinguisher) na kuusogelea moto ule, mmoja wao alianza kuuzima moto kwa kutumia mtungi ule, baada ya moto kuzima wanaume wale walioshikilia madumu yenye maji walianza kumwaga maji sehemu ile na kukusanya vipande vya mabaki ya gari ya Daniel Mwaseba na kuvipakia ndani ya Lori. Baada ya kuhakikisha hakuna baki lolote lililosalia vijana watano walipanda lori lile na kuondoka. Vijana wawili waliobakia waliteremka na mtaro ule taratibu wakijisogeza mahali alipodondokea Daniel Mwaseba. Na mmoja kati ya wanaume hao alikuwa ni Henry.
Henry baada ya kuuona mwili ule alishtuka sana.

"Vipi, unamfahamu? Naona umeshtuka baada ya kumwona" mwanaume aliyeambatana nae akamuuliza Henry

"Aa.. amna, hata simfahamu ndio kwanza namwona leo. Kwani vipi?" Henry akajitetea akijaribu kujiweka sawa.

"Kumbe tuliyetumwa kumchukua ni Daniel Mwaseba! Daaah! Kama ningejua ni yeye ningemtaarifu mapema. Sijui nifanyaje hapa na wanaweza kunigundua kama nafahamiana nae" Henry alikuwa anawaza peke yake. Alikumbuka usiku wa jana kabla Daniel Mwaseba na wenzake hawajaachana naye alipatiwa karatasi yenye namba ya simu

"Chukua namba zangu. Ukipata chochote tutafahamishana." aliyakumbuka maneno haya, aliambiwa na Daniel usiku kabla ya kurudishwa na gari.

"Unawaza nini? Hebu tumwinue tunasubiriwa juu" Henry alishtuliwa na mwenzake kutoka kwenye dimbwi la mawazo. Bila kuchelewa wakashirikiana kuunyanyua mwili huo na kurejea nao barabarani, walipofika barabarani walikuta Noah Nyeusi imepaki pembezoni mwa barabara ikiwasubiri. Bila kuchelewa wakauingiza mwili wa Daniel Mwaseba ndani ya buti, wakaingia ndani ya Noah ile na kuondoka nayo.
-----------------------

Gilbert Mwaitika, Elizabeth Neville, Mwanasheria Mlevi pamoja na mwanadada aitwaye Cara walikuwa wakimsubiri Daniel Mwaseba kwa hamu kubwa. Hii ilikuwa ni baada ya David kuufungua mdomo wake punde tu baada ya kuzinduka. Wote walihamia nyumbani kwa Dokta Yusha baada ya kuitwa na Gilbert Mwaitika.
David hakuficha kitu, aliwaeleza jinsi alivyoitwa na mpambe wa Mheshimiwa Eliud Sumbi siku moja kabla ya ziara ya rais kufanyika. David aliwaeleza jinsi alivyokutanishwa na mheshimiwa Eliud Sumbi na kupatiwa mpango wa kubadili helikopta.

Siku ile ilikuwa hivi...
Baada ya David kuonana na mheshimiwa Eliud Sumbi, Siku hiyo walizungumza kwa takribani nusu saa na baada ya kuukubali mpango wa mheshimiwa Eliud, David alipatiwa dawa ya usingizi na Elton Tonny.

"Dawa hii utaipulizia kesho ndani ya Helikopta yenu nusu saa kabla ya kuingia. Baada ya hapo, muda ukifika wa kuirusha helikopta angani hakikisha wenzako ndio wanaanza kuingia ndani. Wakishaingia na kuvuta pumzi haitawachukua muda, watadondoka chini kama maembe machanga yaliyozidiwa na upepo" Elton Tonny alisema

"Watakufa?" David aliuliza baada ya kupatiwa dawa hiyo

"Hapana. Watapata usingizi mzito ambao hauamshiki hadi masaa thelathini na sita yapite. Wewe usiingie ndani hadi zipite tena dakika kumi na tano. Baada ya hapo utaingia, nawe utasinzia lakini ni kwa masaa manne tu ndipo utarejewa na fahamu. Ukisharejewa na fahamu utajifanya kutoa ripoti huelewi ni kitu gani kinaendelea. Na wakati huo sisi tutakuwa tumeshaimaliza kazi yetu. Kuhusu Helikopta ondoa shaka maana wakati huo tutairusha helikopta ya kufanana na yenu ili iwe rahisi kwa kazi yetu kukamilika"
David alipotaka kujua ni kazi gani aliambiwa atulie hadi itakapokamilika ndipo atajuzwa.

Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, wote wakaridhika na maelezo ya David, japokuwa walimwonea sana huruma kwani tayari alikuwa ni msaliti.

TUKUTANE TENA KESHO SAA 12 JIONI.

NOTE: Kama utauhitaji msimu huu wa nne utaupata jwa gharama ndogo tu ya Tshs 1000 tu. Lipia kwenda M pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie. Wale wengine tutaendelea kuisoma hapahapa kila ninapopata nafasi ya kuiweka.
Msimu wa Tano ndio msimu wa mwisho wa Riwaya hii, utaanza kupatikana kesho mchana kwa Tshs 700 tu
Kazi nzuri sana
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu Wa Nne
Sehemu ya 02

Ni dakika takribani arobaini sasa zimepita tangu Daniel Mwaseba ashambuliwe na kuchukuliwa na watu wa Mheshimiwa Eliud Sumbi. Ndani ya viunga vya stesheni ya treni mjini Moshi pilikapilika za hapa na pale zilikuwa zikiendelea. Watu walikuwa ni wengi kutokana na treni ya abiria kuwa na safari ya kuelekea Jijini Dar es Salaam siku hii. Abiria wengi walishaingia ndani ya mabehewa ya treni tayari kwa kuanza safari. Ilisubiriwa tu ifike saa kumi na moja na nusu jioni ili safari ianze.
Katika behewa lenye namba T0065 ambalo lilikuwa ni behewa la pili kutoka mwisho alionekana Henry akiingia ndani. Upande wa ndani mwa behewa hilo kulikuwa na kitanda kimoja pamoja ba viti 12. Viti vinne vilikaliwa na watu wanne akiwemo Elton Tonny aliyeonekana kuwa bize na simu muda wote. Juu ya kitanda kulikuwa na mwili uliotundikiwa dripu. Na mwili huo ulikuwa ni wa Daniel Mwaseba aliyekuwa hoi bila utambuzi. Pembeni yake alisimama Mzee wa makamo aliyevalia koti jeupe huku macho yake yakibebelea miwani iliyoendana sawia na taaluma yake ya udaktari. Mzee huyu anaitwa Dokta Kalita, na ndiye mwenye jukumu la kumwangalia Daniel Mwaseba.

"Dokta jitahidi sana uwezavyo kuhakikisha huyu jamaa anakuwa salama. Anahitajika akiwa mwenye afya tele" Yalikuwa ni maneno ya Henry akimwambia Dokta Kalita punde tu baada ya kuingia ndani.

"Amepoteza damu nyingi sana kutokana na jeraha alilopata mguuni. Inahitajika damu ya haraka kijana wangu." Dokta Kalita alisema huku akiandika andika juu ya fomu aliyoishikilia mkononi.
Henry akakisogelea kiti alichokalia Elton Tonny. Akamwelezea kile alichosema Dokta Yusha.

"Bado dakika ngapi Treni kuanza safari?" Elton Tonny akauliza huku akizidi kuchezea simu yake kwa vidole.

"Zimesalia dakika arobaini na sita tu. Safari inataraji kuanza saa kumi na moja na nusu." Henry akasema huku macho yake yakitazama kitanda alicholalia Daniel Mwaseba.

"Hospitali ya rufaa ya Mawenzi haipo mbali na hapa. Pale wana bank ya damu salama, hivyo mwambie huyo dokta akuelekeze ni kundi gani la damu linahitajika" akasema Elton Tonny
Henry akafanya kama alivyoelekezwa, akaelekea Mawenzi na baada ya muda mfupi akarejea na mfuko mmoja wa damu. Bila kuchelewa Dokta Kalita akaitoa dripu ya maji iliyokuwa ikimwongezea Daniel Mwaseba maji katika mwili wake kupitia mshipa. Basi akawekewa damu na zoezi la kumpatia huduma ya kitabibu likatamatika ndani ya dakika ishirini na sita.
Zikiwa zimesalia dakika kumi, kipaza sauti kilichofungwa juu ya jukwaa la kupumzikia abiria kilitoa ukelele kuwahimiza abiria wawe tayari kwani zimesalia dakika kumi tu kufika saa kumi na moja na nusu jioni ili safari ianze. Basi waliokuwa nje wakaharakisha kuingia ndani ya treni na walioko ndani wakajiweka sawa katika viti vyao tayari kwa Safari. Wakati huohuo ndani ya behewa la pili kutoka mwisho, alipolazwa Daniel Mwaseba, Elton Tonny alikuwa akiagana na Henry. Elton alimkabidhi Henry jukumu la kuhakikisha Daniel Mwaseba anafikishwa salama kunako kambi yao kubwa iliyopo Tanga.

"Nakuamini sana Henry, sitarajii uzembe wowote kutoka kwako. Utaongozana na Vijana hawa watatu pamoja na huyu Dokta. Kila kitu kuhusiana na Dokta huyu nimeshamaliza, ni yeye tu kuhakikisha Daniel Mwaseba anazinduka ndipo yeye aweze kuondoka. Zingatia kile tulichoongea muda ule. Nikutakie safari njema Henry." Taratibu Elton akausukuma mlango wa behewa na kuufungua kisha kushuka.

"Ndugu Abiria. Sasa ni saa kumi na moja na nusu jioni. Naomba kila abiria aweze kuketi vizuri na kufunga mkanda wake tayari kwa kuanza safari yetu. Niwatakie nyote Safari njema" sauti nyororo ya kike ikasikika kupitia spika ndogo zilizofungwa ndani ya mabehewa ya treni.
"Nitafanya kila liwezekanalo ili Daniel asifike kambini" Henry akajisemea. Na taratibu viberenge vya treni vikaanza kuisugia reli na kuifanya treni ianze kushika njia.

Jua limeanza kupungua nguvu yake kuashiria kwamba siku inaelekea ukingoni. Mshale mdogo wa saa ya ukutani uligota kwenye sita, mshale mkubwa nao ukaing'ang'ania nambari kumi na mbili katika saa ileile. Ilikuwa ni saa kumi na mbili kamili jioni. Ni nusu saa tangu treni ya abiria itoke mjini Moshi. Muda huu treni hiyo ilikuwa ndani ya hifadhi ya taifa ya Mkomanzi iliyoko Same. Hali ilikuwa ni tulivu mno kwa upande wa nje, hii ni kutokana na pori lisilo na makazi ya wanadamu.
Henry alikuwa akiwaza peke yake huku akikitazama kwa makini kitanda alicholazwa Daniel Mwaseba. Pembeni ya kitanda alimwona Dokta Kalita akiwa ameketi pembeni. Mkononi mwake alibebelea kitabu kidogo cha riwaya kiitwacho PARADISO BREAK (Kuvunjika kwa Paradiso) kilichoandikwa na Mwandishi kijana aitwaye Gilbert Evarist Mushi. Dokta Kalita alikuwa bize kukisoma kitabu hicho na ni dhahiri alishazama kwenye ulimwengu wa simulizi kwani kitabu hicho kilionekana kumteka sana. Vijana wanne walioachwa pamoja na Henry walikuwa bize wakicheza mchezo wa Karata.
Henry akasimama na kusogelea dirisha, akachungulia upande wa nje, akatazama na saa yake mkononi, ilikuwa ni saa kumi na mbili na dakika tano. Kichwani alikuwa na wazo moja, wazo la kuwaangamiza wenzake kisha yeye aondoke na Daniel pamoja na Dokta Kalita. Na namna pekee ya kuondoka ni kutenganisha behewa lao na behewa la mbele yao ili treni iweze kuwaacha aweze kupata urahisi wa kuondoka kwani ingemuwia ugumu kuondoka na Daniel wakati safari ikiendelea. Lakini kikwazo kilionekana kipo katika behewa la mwisho, behewa ambalo limebeba askari wanaohusika na ulinzi wa treni hiyo kuanzia mwanzo wa safari hadi mwisho wa safari. Henry aliumiza sana kichwa ili apate namna ya kutoka na Daniel Mwaseba ndani ya treni, lakini hakupata njia. Mwishowe aliamua kusubiri yatokee maajabu labda angepata njia.

Ilikuwa ni saa tatu Usiku. Meza kubwa ilikuwa katikati yao ikisheheni mafaili, tarakishi mpakato zipatazo mbili pamoja na simu zao. Elizabeth Neville akiwa na Cara, Gilbert Mwaitika pamoja na Mwanasheria Mlevi walikuwa kwenye maongezi huku nyuso zao zikipendezeshwa na tabasamu. Wote walikuwa na furaha, ni baada ya Ochewa Owechi kufungua mdomo wake na kuzungumza kila kitu bila kuficha. Ochewa Owechi ama tukipenda tumwite Festus alifunguka kila kitu kuanzia utata juu ya kifo chake huko nchini Kenya hadi mpango wa kumuua Waziri wa Ulinzi Dr Edward Bavu. Festus hakuishia hapo, alieleza pia mpango wa kuuwawa kwa Rais Mark mara baada ya mpango wa kumuua Dr Edward Bavu kukamilika. Hakika maelezo yake yalimshangaza kila mtu, na kilichobakia sasa ni kuwasilisha ripoti kwa Chifu Abdallah Ntenga ila tu walivuta subira kumsubiri Daniel arejee.
Aliyefanikisha zoezi la kumhoji Festus hadi akaweza kuzungumza na kueleza kila kitu alikuwa ni Songelael Ntenga maarufu kama Mwanasheria Mlevi.

"Daah! Yaani hadi siamini, kama naota vile. Unajua Ochewa Owechi alikuwa hana tofauti kabisa na mimi yule wa miaka minne iliyopita!" Elizabeth Neville alisema walipokuwa wameketi pamoja kwa chakula.

"Kwani wewe wa miaka mitano nyuma ulikuwaje?" Cara alizungumza akiwa na shauku ya kusikiliza. Alikiweka kijiko chake cha chakula mezani ili aweze kumsikiliza Elizabeth anachomaanisha.

"Miaka mitano nyuma nilikuwa jasusi wa kutisha sana, nakumbuka Serikali ya nchi ya Cuba ilinituma kuja Tanzania kwa ajili ya kuiba nyaraka fulani hivi za siri." Elizabeth Neville alianza kuwasimulia..

ITAENDELEA TENA

Msimu wa nne unapatikana kwa Tshs 1000 tu. Msimu wa Tano unapatikana kwa Tshs 700 tu.
Ukilipia Tshs 1,500 utaupata msimu wa nne na tano. Lipa kwenda M pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu Wa Nne
Sehemu ya 03

"Kwani wewe wa miaka mitano nyuma ulikuwaje?" Cara alizungumza akiwa na shauku ya kusikiliza. Alikiweka kijiko chake cha chakula mezani ili aweze kumsikiliza Elizabeth anachomaanisha.

"Miaka mitano nyuma nilikuwa jasusi wa kutisha sana, nakumbuka Serikali ya nchi ya Cuba ilinituma kuja Tanzania kwa ajili ya kuiba nyaraka fulani hivi za siri. Tena nilifanikisha kuziiba na nilikuwa katika mpango wa kurejea Nchini Cuba lakini kwa bahati mbaya nilijikuta mikononi mwa kikundi cha watu fulani ambao hawakuwa upande wa serikali ya Tanzania. Nakumbuka Daniel Mwaseba na kina Songelael walikuwa wananitafuta sana ili nizirejeshe hizo Nyaraka, mbali na wao kunisaka pia kuna tajiri mmoja aitwaye Lucas alikuwa akinisaka kwa udi na uvumba ili aniue. Kulikuwa na vikundi vitatu tofauti vilivyokuwa vikinihitaji mimi. Viwili vikinihitaji niwapatie nyaraka huku kimoja kikinihitaji kiweze kuniua. Nadhani Songelael Ntenga unakumbuka huo mkasa" Elizabeth Neville alieleza huku akimtazama Mwanasheria Mlevi

"Nakumbuka sana bibiye. Ilikuwa ni moja kati ya misheni ngumu sana kwangu. Lakini mwishowe zile nyaraka ulizirejesha nyumbani kwa beby wako Daniel" Mwanasheria Mlevi alisema kisha kuachia cheko la kilevi. Wote kwa pamoja wakacheka kisha wakatulia na kumtazama Elizabeth Neville ili aendelee kuwasimulia.

"Sasa majamaa walinitesa sana kwa kila namna. Ilikuwa ni kama nipo kuzimu nyakati zile. Lakini sikuwahi hata kukohoa, nilikuwa nikiwatazama tu na kuigiza bubu mbele yao. Huyu Ochewa tunayemshikilia sasa amefanya nikumbuke mambo ya nyuma. Lakini huyu si kama mimi kwa asilimia zote kwa sababu amekata tamaa mwishowe kakubali kuzungumza. Mimi sikuwahi kukata tamaa japo nilishikiliwa kwa zaidi ya wiki tatu." Elizabeth Neville alieleza kwa upole. Kila mtu aliguswa na simulizi aliyoitoa. Ilisisimua sana na kuleta simanzi kwa wakati mmoja. .

"Pole sana kwa yale yaliyokukuta. Kumbe ndiye wewe uliziiba nyaraka za 001?. Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa bado polisi wa kawaida, sikuwa mwanajeshi kama hivi sasa. Nilisikia juu ya sakata hilo ambalo lilikuja kupelekea mkuu wetu asimamishwe, lakini baadae alikuja kurejeshwa." Gilbert Mwaitika alisema kwa hisia.

"Leo wewe na Daniel Mwaseba ni mume na mke, inapendeza sana jamani. Yaani mume Askari na jasusi na mke pia ni askari jasusi" Cara alisema kisha kukafwatiwa na cheko. Kila mtu akacheka na kuendelea kula.
Wakiwa katikati ya kula na baadhi ya stori zikiendelea, simu ya Elizabeth Neville iliita. Baada ya kuitazama alipokea haraka.

"Naam Dokta. Niambie" Elizabeth Neville alisema. Alikuwa ni Dokta Yusha.

"Leo nimechelewa sana kutoka kazini. Natumaini huko mnaendelea vizuri. Wagonjwa wetu wanaendeleaje?"

"Hakika ni jambo jema. Festus ameeleza kila kitu yaani. Tunawasubiri wewe na Daniel tujue kifuatacho" Elizabeth Neville akasema

"Kwani Daniel hajafika? Nimempigia hapa hapatikani" Dokta Yusha aliuliza.

"Bado hajarejea. Sisi tulijua labda upo naye. Hebu ngoja nami nimtafute tena sasa hivi.." Elizabeth alikata na kuitafuta namba ya Daniel.

"Mh!" aliachia mguno hafifu baada ya kusikia sauti ya mhudumu ikimwambia namba ya Daniel haikuwa ikipatikana kwa wakati huo. Alijaribu kupiga tena na tena, lakini haikupatikana. Elizabeth Neville aliikumbuka namba ya siri ambayo Daniel Mwaseba huitumia mara kadhaa katika kazi maalum. Aliipiga namba ile lakini nayo haikuwa hewani, zote zilikuwa hazipatikani.

"Daniel simu zake hazipatikani ghafla tu, sijui nini shida" Ukumbi mzima ulimtazama Elizabeth Neville kwa mshangao.

"Labda mtandao unasumbua, hebu jaribu tena. Au ngoja mimi nijaribu kumpigia na simu yangu" Cara alifwata simu yake na kumpigia Daniel. Majibu yalikuwa ni yaleyale.
"Au itakuwa ni mtandao? Au simu yake imezima chaji" Cara alitoa wazo

"Hahaha! Simu ya Daniel inazimaga kisa chaji kweli? Simu yake hukaa na chaji kwa siku nne, na leo ni siku ya pili tangu aitoe kwenye chaji. Pia kuhusu mtandao kusumbua sitaki kuamini kwa sababu mji wa Moshi ni moja kati ya miji inayoongoza kwa kuwa na minara ya kutosha inayowezesha mawasiliano kushika vizuri" Songelael Ntenga maarufu kama Mwanasheria Mlevi alisema huku akiiandika namba ya dharura ya Daniel ambayo hupenda kuitumia mara kadhaa. Aliipiga lakini majibu nayo yalikuwa ni yaleyale.

"Labda tumsubiri kwa nusu saa lingine kisha tutaona ni jinsi gani tutafanya kama hajarejea bado." Elizabeth Neville alisema. Wote wakakubaliana naye, stori zikashika hatamu hadi ilipotimia Saa tatu na nusu usiku.

Tarakishi ya Cara ilipiga kelele kuashiria kuna mtu anapiga. Haraka akaisogelea na kutazama.

"Sio Yeye" Cara alisema kwa unyonge. Kila mtu alidhani ni Daniel anapiga.
"Ni yule mdada kutoka idara ya Usalama nchini Kenya anapiga." Cara aliongezea.

"Hebu msikilize anasemaje" Gilbert Mwaitika akasema. Na Cara akapokea.

"Hello, habari za muda? Nimeshafanya kazi ile uliyoniomba, punde kuna barua pepe itaingia natuma hapa, ni ripoti ya kiuchunguzi juu ya kifo cha Festus Jabir Cosmas." sauti laini ya kike ilizungumza na maongezi kutamatika. Hapohapo mlio wa jumbe fupi kuingia ulisikika. Ilikuwa ni Barua Pepe iliyobeba maelezo ya kina kuhusiana na historia ya Festus kuanzia kuzaliwa, masomo, kazi hadi kifo chake. Cara na dada huyo wakakubaliana kufanya siri kwanza kuhusiana na taarifa ya Festus kuwa hai kwani ingezua tafrani kwenye idara ya usalama nchini Kenya.

"Hii si kawaida kwa Daniel jamani. Au wenzangu mnaonaje?" Cara aliwageukia wenzake na kusema baada ya kuachana na tarakishi yake.
Elizabeth Neville alijaribu kumpigia tena lakini bado simu ya Daniel Mwaseba haikuwa hewani. Walihisi kuna tatizo limemkumba Daniel na walipaswa kufanya kitu. Baada ya kushauriana kwa muda mfupi walikubaliana kuelekea hospitali ya KCMC wampitie Dokta Yusha ambaye anajua ni wapi Daniel Mwaseba alielekea. Cara na Gilbert walibaki, huku Mwanasheria Mlevi na Elizabeth Neville wakielekea hospitali ya KCMC.
ITAENDELEA

Huu ni Msimu wa nne wa Anga ya Washenzi. Unapatikana kwa Tshs 1000 tu. Msimu wa tano ambao ni wa mwisho nao unapatikana kwa Tshs 600 tu. Lipa kwenda TigoPesa namba 0678824073 au Mpesa namba 0765824715 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie.
Ikiitaka riwaya hii yote hadi mwisho njoo inbox nikupe utaratibu.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu Wa Nne
Sehemu ya 05

"Mimi sikuwepo. Mawazoo ndio aliyefanya" alijitetea kijana huyo.

"Mawazoo ni nani? Na alifanya nini huyo Mawazoo?" Elizabeth Neville aliuliza.

"Nyumbani kwao si mbali na hapa, nitakuonyesha na atakueleza yeye. Haki ya Mungu mimi sikuwepo, yeye alikuja kunielezea tu ndio nikaja hapa." alisema kijana yule kwa hofu kubwa.

"Sawa, twende kwa huyo Mawazoo. Ila chondechonde usinidanganye maana utazua tafrani na hakika jela nitakupeleka" Elizabeth Neville alionya. Alitoa simu yake na kumpigia Mwanasheria
"Mwanasheria kuna kitu nimepata huku, kama hujapata chochote huko kama vipi njoo huku"

"Huyu bibi kanieleza jambo. Bila shaka kuna mchezo ulifanyika katika gari ya Daniel japo sina hakika sana. Nakuja maana nimeshamaliza maongezi naye" Mwanasheria alijibu

"Haya wahi nakusubiri" Elizabeth alisihi na kukata simu.

Baada ya dakika moja Mwanasheria alifika na kueleza alichokipata.
"Kwahiyo huyo bibi alimwona mtu akiingia katika uvungu wa gari ya Daniel baada tu ya yeye kutoka!" Elizabeth alisema kwa mshangao

"Ndio nashindwa kuelewa huyo mtu alikuwa ni fundi aliyeagizwa na Daniel ama lah!" Mwanasheria alidokeza

"Kwahiyo huyo bibi bado anakunywa?" Elizabeth Neville akauliza

"Ndio hivyo. Kweli Wachaga na pombe ni damdam. Vuta picha alikuwepo tangu ujio wa Daniel hadi sasa" Mwanasheria akasema

"Na bado hajalewa. Hii noma sana. Ngoja huyu kijana atupeleke kwa huyo Mawazoo, bila shaka tutapata kitu" Elizabeth Neville alisema na kumtaka kijana yule awapeleke huko.
Dakika tatu tu zilitosha kuwafikisha mbele ya kijumba kidogo kilichoezekwa kwa makuti. Mwanga hafifu wa sola ulikuwa ukiangaza karibu na mlangoni. Kijumba hicho ndipo makazi ya Mawazoo kwa mujibu wa maelezo aliyotoa kijana yule. Mbele ya mlango walisimama watu watatu. Elizabeth Neville, Mwanasheria pamoja na kijana huyo.

"Atakuwa kweli? Jaribu kumwita" Elizabeth Neville alimgeukia kijana aliyewaleta pale.

"Atakuwa amelala, mlango unaonekana haujafungwa" alijibu kijana.
"Mawazoo... Mawazoo vipi rafiki yangu umelala?" kijana alipaza sauti yake. Utulivu ulikuwa ni mkubwa sana. Sauti ya mwenyeji haikusikika wala mchakacho wowote kutokea ndani.

"Wewe ni mwenyeji. Ingia" Mwanasheria Mlevi alimgeukia kijana yule na kumwambia. Kijana alitii na kuusogelea mlango. Alipougusa kidogo ulifunguka wenyewe, hali iliyoashiria haukuwa umefungwa kama siku nyingine. Mawazoo pindi alalapo ama atokapo ilikuwa ni lazima aufunge mlango wake. Lakini leo upo wazi na haijulikani kama kalala ama katoka.

"Ah! Labda leo ana usingizi mzuri sana hadi kupitiwa. Si kwa mkwanja ule alionionyesha aisee" Kijana alijisemea na kuzama ndani. Mwangaza wa taa ya sola ulitosha kuonyesha madhari ya chumba kile.

"Mamaaaaaaaa!" Kijana alitoka ndani huku akiachia yowe. Mkono imara wa Mwanasheria Mlevi ulimdaka.

"Kuna nini huko ndani?" Mwanasheria aliuliza huku mkono wake mmoja ukiichomoa bastola yake kutoka kwenye kiuno chake. Elizabeth Neville naye alifanya hivyohivyo kwa kuchomoa pia bastola ndogo.

"Damu. Damu" Kijana alisema akitetemeka kwa hofu. Kwa ujasiri Elizabeth Neville alipiga teke mlango na kuzama ndani.
Macho ya Mwanasheria pamoja na Elizabeth yakatua juu ya kitanda kilicholaliwa na Mawazoo akiwa amelala hapo, amefumba macho, na uhai ukiwa mbali naye sana! Damu zilitapakaa kuanzia kitandani hadi chini huku shingo yake ikionyesha alama ya mkato uliotokana na kitu chenye ncha kali. Wote walikosa cha kufanya.
'Paaah' Ulisikika mlio ufananao na mlio wa bastola. Sekunde hiyohiyo kikafwatia kishindo cha mtu au kitu kuanguka chini. Ni yule kijana aliyewaleta kina Elizabeth katika nyumba ya Mawazoo alikuwa tayari chini akijaribu kuutetea uhai wake uliokuwa ukilazimisha kumtoka kutokana na risasi ya kichwa. Risasi ilitoka upande wa mbele ya nyumba, na kwa kuwa kijana huyo alikuwa akitazama ndani, basi risasi hiyo ilimchapa katika kisogo na kutokeza mbele.

"Wamemuua, wamemuua...! Elizabeth akasema huku akijaribu kujificha.

"Ooooh shit. Halafu hatukumuuliza hata jina lake. Bonge la mistake hili." Mwanasheria akasema. Mkononi tayari alishaikamata bastola yake ndogo tayari kwa lolote.
Mara ikasikika kelele ya mtu akipiga yowe upande wa nje, dakika moja mbele wanakijiji zaidi ya kumi wenye hasira wakaizunguka nyumba ya Mawazoo wakiwa na zana za jadi kuwakabili wezi walioko ndani kwa Mawazoo.

"Mara hii tushakuwa wezi, ama kweli siku ya kufa nyani miti yote huteleza." Mwanasheria akasema kwa sauti ya chini iliyosikiwa na Elizabeth Neville.
Wakakubaliana watafute namna ya kutoka ndani kabla kibao hakijawageukia. Ndani ya sekunde 40 Mwanasheria Mlevi alikuwa nje, lakini upande wa pili wa nyumba ile.

" Hawa huhuuuuuu! Wanakimbiaaaaa"
Ilisikika kelele kubwa upande wa pili wa nyumba ya Mawazoo, wanakijiji wote wakakimbilia upande huo ilipotokea sauti.

"Wale kule njooniii"
Ikasikika sauti nyingine tena mbele yao kama hatua tano kutoka pale walipofikia. Wakahimizana kuwahi huku kila mtu akijiapiza kutoa kichapo kikali kwa wezi hao pindi watakapotiwa nguvuni. Naam, wakajongea mbele na mbele zaidi, lakini hawakusikia wala kupata chochote. Waliambulia patupu.
Lakini waswahili wanasema sikuzote mkono mtupu haulambwi. Inawezekanaje sasa kundi hili kubwa la wanakijiji mikono yao ikalambika ilihali hawajaambulia wezi hao? Wakabaki wakitazamana wenyewe kwa wenyewe.

"Hivi aliyekuwa anaita njooni huku ni yupi kati yetu?" Mmoja wao akauliza. Huyu alikuwa ni Mama mtu mzima. Mkononi alibebelea mwiko wa chakula. Aliamini ile ingekuwa ni silaha tosha kwake katika kukabiliana na wezi hao"

"Hapa tumepigwa ngumi za uso jamani. Tumepotezwa maboya. Turudi kule tulipotoka" Mwanaume mmoja kijana akaropoka kwa sauti ya juu. Wote wakaanza kuwahi kuelekea nyumbani kwa Mawazoo. Kwa marehemu Mawazoo.
_____________
Henry alishtuka kutoka usingizini, ilikuwa yapata saa sita kasoro usiku. Alikuwa ameketi juu ya kiti na kukiegemeza kichwa chake katika ukuta wa behewa. Treni ilikuwa ikizidi kuchanja mbuga. Akanyanyuka na kuangaza kila kona ndani ya behewa. Uzuri ni kwamba kulikuwa na mwanga wa taa uliomwezesha kuona kila kitu. Juu ya kitanda kama kawaida alilala Daniel Mwaseba akiwa bado hajitambui. Pembeni ni Dokta Kalita akiwa naye anakoroma. Wale vijana wanne wanaonekana wamevilaza vichwa vyao juu ya meza waliyokuwa wakichezea karata. Wote walionekana kuelemewa kwa usingizi.

"This is time' (Huu ni muda)" Henry akajisemea na kuelekea katika mlango wa kuingilia behewa la mwisho. Alijua kabisa behewa la mwisho huwa wanakuwa walinzi wa Treni wanaohakikisha usalama katika safari. Akaushika mlango na kuusukuma taratibu huku akiwaza baadhi ya mambo...

"Mheshimiwa aliniambia nihakikishe nampata David na nimmalize kabla ya saa sita mchana leo. Lakini hivi sasa inaelekea saa sita usiku na hajachukua hatua yoyote juu yangu, Halafu kirahisi tu napewa jukumu la kumsafirisha Daniel na kumpeleka kambini, mahali ambapo wengi hatupajui na ni ngumu kupajua. Napata wasiwasi" Aliwaza. Akamaliza kuufungua mlango ule, lakini alichokiona ndani ya behewa la Mwisho kilimtisha sana. Alirudi nyuma hatua moja huku akitetemeka kwa woga.

"Nimekwisha" Henry alisema huku lipsi zake zikichezacheza.

Nini kitaendelea? Henry ameona nini? Usikose sehemu ijayo hapahapa Simulizi Za Gilbert.
Ofa yetu bado inaendelea. Msimu wa nne na wa tano unapatikana kwa malipo ya Tshs 1500 tu. Kama umeshasoma wa nne basi lipia Tshs 700 kwa msimu wa Tano. Nambari ya Malipo ni M Pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
ANGA YA WASHENZI

Akamaliza kuufungua mlango ule, lakini alichokiona ndani ya behewa la Mwisho kilimtisha sana. Alirudi nyuma hatua moja huku akitetemeka kwa woga.

"Nimekwisha" Henry alisema huku lipsi zake zikichezacheza.

Henry ameona nini? Kwa nini aseme amekwisha? Hii ni Anga ya Washenzi kumbuka, na ni msimu wa nne huu.
Pata msimu wa nne na wa tano kwa ofa ya Tshs 1500 tu. Lipa kwenda M pesa namba 0765824715 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie. Wengine tusubiri tena kesho

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
ANGA YA WASHENZI

Akamaliza kuufungua mlango ule, lakini alichokiona ndani ya behewa la Mwisho kilimtisha sana. Alirudi nyuma hatua moja huku akitetemeka kwa woga.

"Nimekwisha" Henry alisema huku lipsi zake zikichezacheza.

Henry ameona nini? Kwa nini aseme amekwisha? Hii ni Anga ya Washenzi kumbuka, na ni msimu wa nne huu.
Pata msimu wa nne na wa tano kwa ofa ya Tshs 1500 tu. Lipa kwenda M pesa namba 0765824715 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie. Wengine tusubiri tena kesho

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
Mkuu me naona ni bora uache kupost kabisa ili wataotaka kununua wanunue,sasa hii ndo nini umeweka mfyuu
 
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.

Msimu Wa Nne
Sehemu ya 06

"This is time' (Huu ni muda)" Henry akajisemea na kuelekea katika mlango wa kuingilia behewa la mwisho. Alijua kabisa behewa la mwisho huwa wanakuwa walinzi wa Treni wanaohakikisha usalama katika safari. Akaushika mlango na kuusukuma taratibu huku akiwaza baadhi ya mambo...

"Mheshimiwa aliniambia nihakikishe nampata David na nimmalize kabla ya saa sita mchana leo. Lakini hivi sasa inaelekea saa sita usiku na hajachukua hatua yoyote juu yangu, Halafu kirahisi tu napewa jukumu la kumsafirisha Daniel na kumpeleka kambini, mahali ambapo wengi hatupajui na ni ngumu kupajua. Napata wasiwasi" Aliwaza. Akamaliza kuufungua mlango ule, lakini alichokiona ndani ya behewa la Mwisho kilimtisha sana. Alirudi nyuma hatua moja huku akitetemeka kwa woga.

"Nimekwisha" Henry alisema huku lipsi zake zikichezacheza.

Henry hakuwa na ujanja wowote ule baada ya kukutana uso kwa uso na Elton Tonny katika behewa la mwisho. Aligundua kumbe alishagundulika kwamba hakuwa miongoni mwao, isitoshe pia kitendo cha yeye kupewa jukumu la kusafirisha Daniel Mwaseba ilikuwa ni mtego na kipimo cha uaminifu kwake. Dhamira yake ya kutaka kumtorosha Daniel ilishagundulika.

"Hapa ni kuruka dirishani na kujitupa nje" Akawaza na kugeuka haraka. Lakini ndipo mwili wake ulipokosa nguvu kwa kile alichokiona. Wale vijana wanne waliokuwa wamelaza vichwa vyao juu ya meza walikuwa wameshikilia kila mmoja bastola na kumwelekezea yeye. Hapohapo mlango wa behewa lao ukafunguka na Elton Tonny kuingia.

"Henry mdogo wangu nilikuamini sana, ni kina nani hao wamekurubuni kiasi hiki? Umesahau ya kuwa una mtoto ambaye uhai wake upo mikononi mwako wewe? Maskini Jerry anakwenda kuaga dunia kisha baba yake anafuatia." Elton akasema huku akichomoa remote ndogo ya kuminya kuruhusu kifaa alichowekewa Jerry huko alipo kiweze kufanya kazi yake.

"Hapanaaaaaaaa" Henry alisema kwa nguvu baada ya kumwona Elton Tonny akiminya ile remote. Kwa ghadhabu akamkimbilia Elton huku mikono yake ikitetemeka kwa hasira, lakini hakumaliza hatua tatu baada ya risasi mbili kukita katika mgongo wake na yeye kuanguka chini. Na hapohapo safari ya Henry katika ulimwengu huu ulio na watu wengi wabaya ikafikia tamati. Ilitamatishwa na kifo palepale.
Lakini kwa upande wa Elton Tonny kuna jambo lilimshangaza sana. Haikuwa kawaida kwake kubonyeza rimoti kisha mwanga mwekundu uache kuwaka. Leo hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwake kuona hili. Baada ya kubofya kitufe cha remote hakuona mwanga mwekundu wala wa njano. Mwekundu uliashiria mlipuko huku wa njano ukiashiria bidhaa ya mauaji (Kill plug) ipo nje ya mwili wa binadamu. Haraka akashika simu yake na kuwasiliana na mtu fulani, akaelekeza jambo na kukata simu.
Baada ya dakika tano kupita simu yake iliita, akaipokea na kuiweka sikioni.

"Hallo Boss! Taarifa kutoka shuleni kwao zinasema mtoto huyo alichukuliwa saa nne asubuhi na Dada mmoja aliyejitambulisha kama shangazi wa Henry." Sauti simuni ikasema

"Haraka tuma watu nyumbani kwake, mke wake na huyo mtoto nawahitaji wakiwa maiti. Nitakaporudi kesho nizikute maiti zao" alisema kwa jazba na kukata simu. Kelele hiyo ikamkurupua Dokta Kalita kutoka usingizini. Akaanza kuogopa baada ya kuona mwili wa Henry ukiwa chini umetulia.

"Usiogope Mzee wangu. Usalama upo wa kutosha, ni mvamizi tu aliyetaka kutushambulia tumejaribu kumdhibiti" akasema Elton Tonny.

"Mmeua mnasema mmejaribu kumdhibiti? Hii nchi ina vijana wa hovy...." kabla hajamaliza sentesi yake Elton akamkurupua kwa sauti ya juu baada ya kuita
"Dokta!" Dokta Kalits akamtazama kwa hofu akijaribu kumeza mate.

"Anaendeleaje huyu?" Elton Tonny akauliza huku akikilaza kiganja cha mkono wake juu ya paji la uso wa Daniel Mwaseba.

"Anahitaji tu muda wa kutosha kupumzika. Hadi saa nne asubuhi kesho atakuwa amerejewa na fahamu" Dokta alijibu. Baada ya hapo Elton Tonny akachakata ujumbe mfupi na kuutuma mahali huku akitabasamu, akawaamuru vijana wake kusafisha pale chini, na bila kuchelewa mwili wa Elton Tonny ukatupiwa nje kwa kupitia dirishani, na hakika ingekuwa ni vigumu kwa mwili wake kupatikana kwani eneo hilo halikuwa na dalili yoyote ya makazi ya watu, ilikuwa ni katikati ya miti mirefu iliyofungamana. Kushoto na kulia kulikuwa na safu za milima.
************
'Turudi Masaa kumi na nne nyuma'
Ni saa nne na Robo asubuhi katika shule ya Mawenzi mjini Moshi. Inaingia gari aina ya Harrier Hybrid nyeusi na kupaki kwenye maegesho ya shuleni hapo. Anashuka Cara akiwa amevalia miwani nyeusi machoni, chini amevalia suruali ya pink yenye kubana vyema umbo lake, juu amevalia tisheti nyeupe yenye maandishi makubwa ya neno 'Sure Girl'. Chini amevalia raba nyeupe na kicgwani amevalia kofia kubwa ya mviringo maalum kwa kujikinga na jua. Kofia hii ilikuwa imesukwa na mkeka. Taratibu Cara anahakikisha amefunga mlango wa gari kwa funguo, anazipiga hatua upesi upesi hadi katika jengo moja lililoandikwa 'Taaluma'. Bila shaka ni ofisi ya mwalimu wa taaluma anaelekea. Anagonga mlango na kuruhusiwa kuingia. Na hapohapo kengele ya wanafunzi kuingia darasani inalia mara tatu.

"Ingia" Sauti ya mwalimu wa taaluma inasikika ikimtaka aingie ndani. Naye anatii na kuingia ndani. Anasalimiana na mwalimu huyo na kueleza dhamira ya kufika hapo.

"Naitwa Nusrat, ni shangazi wa Jerry, dada yake na Henry. Nilitaarifiwa na baba yake Jerry kufika kumjulia hali mwanae kwani leo hajisikii vizuri, ikiwezekana niende naye hospitali." Cara alidanganya jina lake. Hakuwa akiitwa Nusrat kama alivyojitambulisha, pia hakuwa shangazi wa Jerry wala dada wa Henry. Zilikuwa ni njama, zenye nia ya kuondoka na Jerry.

"Asubuhi aliletwa na mama yake hapa, na akasema baba yake atakuja kumsalimu mchana. Lakini baba yake alikuja saa mbili hivi, akasema kweli Jerry hayupo sawa hivyo atarejea baadae au kumtuma shangazi yake. Kumbe ndiye wewe? Karibu sana Nusrat" Mwalimu akasema huku akiutoa mkono wake na kumpatia. Wakapeana mikono ya salamu, na baada ya hapo mwalimu akaomba radhi na kutoka nje, akamwita mwanafunzi mmoja na kuteta nae, kisha akarejea ndani. Baada ya dakika mmoja Jerry akafika ofisini hapo akiwa hana furaha. Ni mtoto wa darasa la pili hivyo bado ni mtoto mdogo. Cara akamchangamkia kwa kumnyanyua na kumbeba, akaweka upesi kiganja chake cha mkono usoni kwa Jerry

"Looh! Ndio mwili unachemka hivi Jerry wangu! Pole sana baba angu, umeshakunywa uji?" Cara akasema huku akionyesha uso wa kujali.
Jerry akatingisha kichwa juu na chini kuashiria tayari amekunywa.
Jerry anakumbuka majira ya saa mbili asubuhi wakati yupo darasani aliitwa nje na mwalimu. Na kumbe muda huo ni baba yake alifika na kuomba kuonana naye. Anakumbuka baba yake alimwambia leo anataka waende kuogelea, hivyo aonyeshe sura ya huzuni kuwa anaumwa ili baadae aje kuchukuliwa.
"Jerry mwanangu, atafika shangazi kukuchukua itakapolia kengele mkiwa mapumziko. Ni mimi nitamtuma mwanangu. Atavaa suruali na pia atavaa kofia kubwa, sawa?"

"Sawa Baba"
Jerry alikuwa anakumbuka yote haya, hivyo alitaraji jambo hili kutokea.
"Jerry! Huyu ni nani?" Mwalimu akajaribu kumpima kama anamfahamu shangazi yake.

"Huyu ni Aunt yangu mwalimu" Jerry akasema huku akilaza kichwa chake katika kifua cha Cara. Moyo wa mwalimu ukasawajika na kumruhusu Cara kumchukua mtoto huyo.
Hivi ndivyo mtoto wa Henry alivyochukuliwa shuleni hapo.
________________

Elizabeth Neville alikuwa ndani ya gari waliyokuja nayo katika kijiji cha Uri. Zilishapita dakika mbili tangu waachane na Mwanasheria Mlevi katika kijumba cha Mawazoo.

"Huyu mwanaume hadi sasa hajafika tu? Au wamembananisha nini!" akawaza huku akishika mlango wa gari tayari kwa kuufungua aweze kushuka

"Nipo hapa, unakwenda wapi?" Sauti ya Mwanasheria ikasikika kutoka upande wake wa kushoto, nje ya gari. Alikuwa akihema kwa jasi kuashiria alikimbia sana.

"Uuuh.... Hawa washenzi wanakimbiza kama kuku yaani. Tuondoke tu hapa" Mwanasheria akasema.

"Tuondoke? Kilichotuleta tumekipata kwani? Nenda wewe." Elizabeth Neville akaweka mgomo.

"Hii itatusaidia. Tulipokubaliana mda ule nitoboe ukuta nitokee kwa nyuma kisha niwazuge wanakijiji wale basi niliokota hii waleti, na ni wazi inaonyesha ni ya muhusika wa yale mauaji, na ndiye atakayetupa mwangaza ni wapi alipo Daniel" Mwanasheria akasema na kumpatia Elizabeth Neville waleti ile. Baada ya Elizabeth Neville kuitazama na kukuta risasi tatu, kitambulisho pamoja na baadhi ya fedha aliamini kishingo upande. Wakapanda garini na kutimua.

Nini kitaendelea? Kama una Tshs 1000 tu leo basi unaweza kupata msimu wa nne na wa tano wa Riwaya yetu ya Anga ya Washenzi. Wahi ofa hii maana msimu wa tano hautopostiwa hapa facebook. Lipia Tshs 1000 kwenda M pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie.

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
Story haina mvuto alafu kama ka copy sehem flani flani na idea n hii hii ujasusi , kumbuka wayback since 2017 na kuendelea tulikua tunasoma ile ya SteveMollel alizochanganya (joana anaona kitu usiku) na ile (anga la washenzi) ..
Daaaah hatare sana boss maana anavyojikuta utadhani ndiyo maxeMello
 
Story haina mvuto alafu kama ka copy sehem flani flani na idea n hii hii ujasusi , kumbuka wayback since 2017 na kuendelea tulikua tunasoma ile ya SteveMollel alizochanganya (joana anaona kitu usiku) na ile (anga la washenzi) ..
Kwani ni story moja tu ndo ina jina la peke ake? Zipo nyingi tu. Anga ya Washenzi watakuja na wengine kuita story zao hvyo ba contect zitakuwa tofauti. Leta pointi

Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom