RITA eleweni jina la babu sio jina la ukoo

RITA eleweni jina la babu sio jina la ukoo

man dunga

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2013
Posts
3,726
Reaction score
6,581
Habari wote.

Wafanyakazi wa RITA mliomo humu eleweni na muwafahamishe pia na wenzenu kuwa jina la babu sio jina la ukoo. Mfano mimi naitwa John Julius Kipingo, cha kushangaza ukimuombea mtoto(mfano Peter) cheti cha kuzaliwa huko halmashauri kitakuja na majina ya Peter John Julius, ukiwauliza inakuaje mmeacha jina la mwisho ambalo kikawaida ndio jina la ukoo wanakuwa wabishi kuwa mtoto halimuhusu.

Jina la ukoo ni la kizazi na kizazi. Kama ni majina matatu basi ni jina la mtoto ,baba yake na la ukoo.Kama ni majina manne basi utaongeza na la babu yake ila huwezi ukaliacha jina la ukoo ukaweka la babu ndio likawa jina la mwisho(ukoo).
 
Habari wote.

Wafanyakazi wa RITA mliomo humu eleweni na muwafahamishe pia na wenzenu kuwa jina la babu sio jina la ukoo. Mfano mimi naitwa John Julius Kipingo, cha kushangaza ukimuombea mtoto(mfano Peter) cheti cha kuzaliwa huko halmashauri kitakuja na majina ya Peter John Julius, ukiwauliza inakuaje mmeacha jina la mwisho ambalo kikawaida ndio jina la ukoo wanakuwa wabishi kuwa mtoto halimuhusu.

Jina la ukoo ni la kizazi na kizazi. Kama ni majina matatu basi ni jina la mtoto ,baba yake na la ukoo.Kama ni majina manne basi utaongeza na la babu yake ila huwezi ukaliacha jina la ukoo ukaweka la babu ndio likawa jina la mwisho(ukoo).
Mbona wenzako tuna vyeti vya RITA ambavyo havina hiyo changamoto.
 
Mmh! Mkuu mbona majina ya mtoto unachagua mwenyewe mzazi utake yaweje.

Ndo mana kuna fomu ile unajaza na ndio wanayoifuata namna unataka majina ya mwanao yawe.

Kama mwanao anatumia majina matatu hilo la tatu unaliruka unaandika hilo na ukoo unalolitaka na wenyewe wanafuata vivyo hivyo.

Hapo si ajabu kukuta we mwenyewe ndo ulichemsha.
 
Kama ni majina matatu basi ni jina la mtoto ,baba yake na la ukoo.Kama ni majina manne basi utaongeza na la babu yake ila huwezi ukaliacha jina la ukoo ukaweka la babu ndio likawa jina la mwisho(ukoo).
Na ndio ipo hivyo miaka yote sasa hii imekuaje au waliambiwa waandike hivyo yaan waachane na jina la ukoo?
 
Mmh! Mkuu mbona majina ya mtoto unachagua mwenyewe mzazi utake yaweje.

Ndo mana kuna ile tangazo pamoja na fomu ile unajaza ukifika RITA na ndio wanayoifuata namna unataka majina ya mwanao yawe.

Kama mwanao anatumia majina matatu hilo la tatu unaliruka unaandika hilo na ukoo unalolitaka na wenyewe na wanafuata vivyo hivyo.

Au ulikuwa unataka mwanao awe na majina manne?
Yeah ndio inakua hivi miaka yote
 
mkiambiwa kwamba islamization of tanzagiza inaendelea muwe mnaelewa, jina la ukoo kurithishwa ni Christian, sasa wanabomoa "mfumo Kristo" na ndiyo maana wamefuta jina ukoo, kwa kifupi ukoo wako unapotea kwa maana watoto hawatarithi jina na jina la ukoo kupotea.

kwa muslims hakuna kitu kama jina la ukoo, jina la ukoo ni urithi tulioachiwa na Christianity ...
 
Habari wote.

Wafanyakazi wa RITA mliomo humu eleweni na muwafahamishe pia na wenzenu kuwa jina la babu sio jina la ukoo. Mfano mimi naitwa John Julius Kipingo, cha kushangaza ukimuombea mtoto(mfano Peter) cheti cha kuzaliwa huko halmashauri kitakuja na majina ya Peter John Julius, ukiwauliza inakuaje mmeacha jina la mwisho ambalo kikawaida ndio jina la ukoo wanakuwa wabishi kuwa mtoto halimuhusu.

Jina la ukoo ni la kizazi na kizazi. Kama ni majina matatu basi ni jina la mtoto ,baba yake na la ukoo.Kama ni majina manne basi utaongeza na la babu yake ila huwezi ukaliacha jina la ukoo ukaweka la babu ndio likawa jina la mwisho(ukoo).
ni uongoz wao tu kubadilisha huo mfumo!
 
Yeah ndio inakua hivi miaka yote
Hapo bila shaka mwenyewe ndo alichanganya madesa na ilivyo Wababa wengi huwa hamuhangaiki na hayo mambo unakuta siku anataka cheti cha mtoto aliagiza mtu ambaye alipofika kwenye kujaza ile fomu ye aliandika majina kwa namna yanavyofuatana na hilo la ukoo hata hakuhangaika nalo.
 
Zamani wakati nasoma nilijua jina la babu ndo la ukoo, Nimekuja kupata akili tayari mm peke angu ndo natumia jina la babu sio la Ukoo 😀

Sema sio mbaya, Mizimu yao itakua inashindwa kuni idendify.
 
Habari wote.

Wafanyakazi wa RITA mliomo humu eleweni na muwafahamishe pia na wenzenu kuwa jina la babu sio jina la ukoo. Mfano mimi naitwa John Julius Kipingo, cha kushangaza ukimuombea mtoto(mfano Peter) cheti cha kuzaliwa huko halmashauri kitakuja na majina ya Peter John Julius, ukiwauliza inakuaje mmeacha jina la mwisho ambalo kikawaida ndio jina la ukoo wanakuwa wabishi kuwa mtoto halimuhusu.

Jina la ukoo ni la kizazi na kizazi. Kama ni majina matatu basi ni jina la mtoto ,baba yake na la ukoo.Kama ni majina manne basi utaongeza na la babu yake ila huwezi ukaliacha jina la ukoo ukaweka la babu ndio likawa jina la mwisho(ukoo).
Kabila gani wewe?
 
Kwenye fomu kuna sehemu mbili tofauti, father's Name na Child's surname, ukijaza jina lako kamili upande wa baba, haimaanishi mfumo utahamisha jina lako la mwisho kwenda kwa mtoto moja kwa moja.

Lazima uandike jina la ukoo la mtoto husika, inaonekana wewe ulijaza majina yako matatu upande wa baba, kisha upande wa ukoo wa mtoto ukaandika jina lako la kwanza.
 
Nafikiri lengo lao au serikali ni kuwa na akina John Joseph Julius na Ally Muhammad Ahmad nchi nzima.

Huu ujinga huwezi ukuta Rwanda, DRC, Uganda, Uchina, Korea n.k.
 
Mmh! Mkuu mbona majina ya mtoto unachagua mwenyewe mzazi utake yaweje.

Ndo mana kuna fomu ile unajaza na ndio wanayoifuata namna unataka majina ya mwanao yawe.

Kama mwanao anatumia majina matatu hilo la tatu unaliruka unaandika hilo na ukoo unalolitaka na wenyewe wanafuata vivyo hivyo.

Hapo si ajabu kukuta we mwenyewe ndo ulichemsha.
Upo sahihi kabisa na kuna jamii ni nadra sana tena sana kukuta wanatumia majina ya ukoo na wengine hata majina ya babu zao walishaachana nayo..mfano mzuri ni huko kwa wahaya..unakuta mtoto anaitwa John Rugeiyamu Mathias au John Mathias Rugeiyamu, hapa unakuta jina la John na Rugeiyamu ni majina ya mtoto mwenyewe ambapo jina la Rugeiyamu alipewa punde tu baada ya kutoka tumboni kwa mama kuendana na nyakati alipozaliwa na Mathias ni jina la baba yake...au anaitwa John Mathias Rugeiyamu, hapa unakuta Mathias Rugeiyamu ni majina ya baba yake mwenyewe na hakuna jina la babu hapo au ukoo. Uhayani mara nyingi ukikuta mtoto anaitwa Anitha Kokushubila John basi hapo hakuna jina la babu wala ukoo na wao wanasema wanatumia Jina la Kwanza, La Kati na la mwisho ambalo wengi hilo la mwisho ndilo tunaita ukoo. Ingawa wao wana koo zao kabisa za kama Mushasha, Mukyaija,n.k na wanatambuana kabisa, wakiulizana wewe ni ukoo gani wanatajiana lakini ni nadra kukuta majina hayo ya ukoo/koo yapo kwenye vyeti. Mfano ni kwa Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka, huyu mama ukimuuliza anaweza kukwambia jina la ukoo tofauti na kinachosomeka kwenye majina yake.
 
NI heri ufuate huo mfumo wa ritha usilete ujuaji,Kuna baadhi ya kazi wako very sensitive kwenye interview zao itakuja kumgharimu mtoto ionekana kama taarifa zake za mchongo!
 
Habari wote.

Wafanyakazi wa RITA mliomo humu eleweni na muwafahamishe pia na wenzenu kuwa jina la babu sio jina la ukoo. Mfano mimi naitwa John Julius Kipingo, cha kushangaza ukimuombea mtoto(mfano Peter) cheti cha kuzaliwa huko halmashauri kitakuja na majina ya Peter John Julius, ukiwauliza inakuaje mmeacha jina la mwisho ambalo kikawaida ndio jina la ukoo wanakuwa wabishi kuwa mtoto halimuhusu.

Jina la ukoo ni la kizazi na kizazi. Kama ni majina matatu basi ni jina la mtoto ,baba yake na la ukoo.Kama ni majina manne basi utaongeza na la babu yake ila huwezi ukaliacha jina la ukoo ukaweka la babu ndio likawa jina la mwisho(ukoo).
Sahihi kabisa. Nilipambana nao sana. Wabishi.
Nilichogundua sasa. Wewe acha kutumia jina lako la 3 ambalo ni Julius,la babaako. Anza kutumia jina la ukoo. (Mfano wewe unaitwa John Julius Mwakyusa). Jiite Mwakyusa. Mke anapoenda kujiandikisha crinic hakikisha jina la baba aandike Mwakyusa John.
 
Back
Top Bottom