Risasi na uporaji muda huu hapa Ukonga

Risasi na uporaji muda huu hapa Ukonga

Gama

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
13,264
Reaction score
4,744
Muda mfupi uliopita katika barabara inayotoka Ukonga Mombasa kwenda Moshi bar, eneo la " kwa Temba" watu waliokuwa wakiendesha pikipiki wamevamia gari na kurusha risasi hewani kisha wakachukua kiasi kikubwa cha fedha iliyokuwa ndani ya gari.

Inasemekana kuwa meneja wa kituo cha mafuta cha Temba alikuwa akipeleka fedha kwenye kituo kikuu kilichopo Mzambarauni.

Hakuna majeruhi wala vifo
 
Hiv vyombo vya usalama vinafanya nin?,TISS si wanasemwa kumaliza ujambazi ulioshamiri,kipindi Rais jakaya anaingia madarakani,hasa mtandao wa ujambaz wa mabenk,wao pamoja polisi,wanashindwa kumaliza mtandao wa ujambazi wa bodaboda unaokua siku baada ya siku,au strategic mistake&delay? God willing we shall overcome n' truth to be revealed.
 
Ashukuru kapona nadhani siku nyingine atakumbuka kuomba ulinzi wa Askari,mzembe mwenzake kafa jana Mlimani City...
 
Ashukuru kapona nadhani siku nyingine atakumbuka kuomba ulinzi wa Askari,mzembe mwenzake kafa jana Mlimani City...

Si bure..., ni mawili either haujui unachoongea au unashirikiana na hawa majambazi
 
Hiv vyombo vya usalama vinafanya nin?,TISS si wanasemwa kumaliza ujambazi ulioshamiri,kipindi Rais jakaya anaingia madarakani,hasa mtandao wa ujambaz wa mabenk,wao pamoja polisi,wanashindwa kumaliza mtandao wa ujambazi wa bodaboda unaokua siku baada ya siku,au strategic mistake&delay? God willing we shall overcome n' truth to be revealed.

uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana..!
 
kila kitu shaghalabaghala tu!!
hii nchi leo unaweza ukalala njaa kesho ukaamka boss kwenye mabaa na pub!!!
 
Si bure..., ni mawili either haujui unachoongea au unashirikiana na hawa majambazi

Wewe unayejua unachoongea embu tuambie ingekuwa wewe ndio unatakiwa kupeleka hela kama hizo ungefanyaje?
 
Tanzania Mmmh Full Ujambazi !!! kutumia nguvu za silaha imekuwa kama vile kunywa maji ! au kusalimiana ...jamanii kila kukicha ..chamoto tunakisikia!
 
Wizi wowote ule wa fedha unahusisha kazi ya ndani yaani ni inside job.

Mkuu wewe kweli umeongea la maana na una uono mkubwa sana.
Utakuta mtu na akili zake timamu eti analaumu jeshi la polisi kwa hili.Sasa wao wafanye nini.

Issue ya wizi wa pesa kwa mtindo huu ni issue ya ndani,hakuna mtu anaejua kwamba gari hiyo au muda huo pesa inatoka.
Siku hizi watu wanataka utajiri wa haraka,kuna watu wapo tayari hata kuwachomea wazazi wao kwa majambazi ili wapate pesa.
Hili Suala hata mtoto mdogo anajua kwamba ni issue za ndani,na huu mchezo umekuwa ukifanyika sana.
Bado pia natoa ushauri kwamba siku zote jeshi la polisi linasema kwamba watu waombe msaada wakati wa kusafirisha pesa na pia kuna makampuni yaani Security Companies ambazo zinatoa huduma hii kwenye magari maalum na wakiwa na silaha.
Ubahili huu ndio matokeo yake haya.Na Pia wapitishe msako wao kwa wao.Ni Issue za kupiga hizi tena mfumo huu umekuwa sugu sana siku hizi.Wamelizwa wachina eee sasa hivi tunaanza sie kwa sie.
 
Muda mfupi uliopita katika barabara inayotoka Ukonga Mombasa kwenda Moshi bar, eneo la " kwa Temba" watu waliokuwa wakiendesha pikipiki wamevamia gari na kurusha risasi hewani kisha wakachukua kiasi kikubwa cha fedha iliyokuwa ndani ya gari.

Inasemekana kuwa meneja wa kituo cha mafuta cha Temba alikuwa akipeleka fedha kwenye kituo kikuu kilichopo Mzambarauni.

Hakuna majeruhi wala vifo

Noma!! kadoda11 Bulldog Geza Ulole
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom