Risasi na uporaji muda huu hapa Ukonga

Risasi na uporaji muda huu hapa Ukonga

Watu wengi wanabeba pesa hovyo sana. Tuamke,tuombe ulinzi.
 
Ujambazi hauishi kwa kukodi askari kutoa escorts usafirishaji wa pesa.
Simu, pochi zetu nani atatuescort? Majumbani mwetu je? Serikali kupitia vyombo vya Dola na kila mwananchi mwenye nia lazima washirikiane
 
Mkuu ngoja nikuulize swali, unadhani sahihi kwa Watanzania kuishi kwa uoga?

Mathalani watu wanaoporwa na vibaka pesa ndogo ndogo, je ni uzembe wa mtu anayeporwa?

Nilichokuwa nakisemea hapa ni kuhusu uzembe wa hawa watu ambao kila siku wana haswa kuomba ulinzi wa Polisi wakati wa kusafirisha pesa ila wao hawataki sijui ni ubahili au ni hawawaamini hapo askari wenyewe.

Kuhusu hilo lako huo bado ni uzembe wetu kwasababu hao vibaka tunaishia mitaani humu humu kwanini tusiwa-report kwenye viombo husika?na sio kutoa taarifa tu,hata kufatilia kama zimefanyiwa kazi,tunawalipa kwa kodi zetu still
 
Huyo meneja mshukiwa namba moja, anajua wahusika ndio maana hakuuwawa, maana kwenye deal za uhalifu kama hizi, huwa ni vigumu mtu kutoka salama.
 
Hapohapo jirani kulikuwa na polisi wa 'Tigo' wanachukua rushwa kutoka kwa madereva.
 
Samahani endapo nikiomba ulinzi wa Polisi natakiwa kumlipa?


||Tomorrow will say its a memory and we have enjoyed our lives for couple of days||

Ndio unatakiwa kumlipa mme wangu jamani hakumbuki kipindi kile naamisha hela niliwalipa ili nipate ulinzi.....lol.Please naomba leo uwahi kurudi mume wangu Rogie
 
Last edited by a moderator:
Kubwa jinga

Hujawaona makubwa jinga wenzako wamekufa mwingine kanusurika kisa ubahili wa kumpa askari 20 elfu awasindikize na vihela vyao?

Ukweli unauma muache ubahili mtakufa na vihela vyenu hivyo mnavyotembea navyo kwa mawazo
 
By Rapherl:
Ashukuru kapona nadhani siku nyingine atakumbuka kuomba ulinzi wa Askari,mzembe mwenzake kafa jana Mlimani City...

inapaswa ufanyiwe maombi ili upate ufahamu katika uyaongeayo...maana ni kama vile umefurahishwa na kilchotengana wala hujasikitishwa
 
samahan wakubwa ila swali langu ni,hao majambazi wanajuaje kama mtu ana hela flan?wamejuaje Jamaa wa mlimani cty alikua ana hela kama sio mtu aliechora dili?
Naamini wanaotugeuka ni watu wetu wa karbu tunaowaita marafiki,so watch out Guys
 
Kwa matukio yaliyotukia hivi karibuni nathubutu kusema TANZANIA SI SALAMA
 
Muda mfupi uliopita katika barabara inayotoka Ukonga Mombasa kwenda Moshi bar, eneo la " kwa Temba" watu waliokuwa wakiendesha pikipiki wamevamia gari na kurusha risasi hewani kisha wakachukua kiasi kikubwa cha fedha iliyokuwa ndani ya gari.

Inasemekana kuwa meneja wa kituo cha mafuta cha Temba alikuwa akipeleka fedha kwenye kituo kikuu kilichopo Mzambarauni.

Hakuna majeruhi wala vifo

huo mchongo
 
quote_icon.png
By Rapherl

Ashukuru kapona nadhani siku nyingine atakumbuka kuomba ulinzi wa Askari,mzembe mwenzake kafa jana Mlimani City...


Si bure..., ni mawili either haujui unachoongea au unashirikiana na hawa majambazi
KeyserSoze
unamaanisha nini mkuu?
maana ni kweli ukiwa umebeba pesa nyingi inatakiwa uombe support ya ulinzi either private ama public.
1.je unamaanisha kuwa hatuna maaskari wa ulinzi?
2. sehemu ya pili ya kushirikiana na majambazi ndo sijakuelewa kabisaa!
 
Polisi hawawezi kujua kama unasafirisha fedha. Ni jukumu lako kuwapa taarifa ili wakupe ulinzi. Watu waache kufanya mambo /vitu kwa mazoea

Usipende kuwaamini sana watu linapokuja suala la Pesa, hao Polisi wenyewe kama Pesa nyingi wanaweza kukufanyia mpango au wanaweza kukuua ili Pesa wachukue wao
 
Ashukuru kapona nadhani siku nyingine atakumbuka kuomba ulinzi wa Askari,mzembe mwenzake kafa jana Mlimani City...

Usipende kuwaamini sana watu linapokuja suala la Pesa, hao Polisi wenyewe kama Pesa nyingi wanaweza kukufanyia mpango au wanaweza kukuua ili Pesa wachukue wao
 
Usipende kuwaamini sana watu linapokuja suala la Pesa, hao Polisi wenyewe kama Pesa nyingi wanaweza kukufanyia mpango au wanaweza kukuua ili Pesa wachukue wao

mkuu inaonekana hauna imani kabisa na jeshi letu! unaweza tudokezea ni kwa nini?
 
mkuu inaonekana hauna imani kabisa na jeshi letu! unaweza tudokezea ni kwa nini?
Mkuu ikiwa polisi na majambazi wanakula njama kwenye kufanya ujambazi iweje tena hao hao niwaamini ninapokuwa na pesa nyingi?

Kuna matukio Mengi sana ambayo mapolisi wametiwa hatiani kutokana na kufanya ujambazi likiwemo tukio moja Mbeya ambalo lilishirikisha hadi askari magereza, na sijui kesi yao inaendeleaje hadi hivi sasa
 
Mkuu ikiwa polisi na majambazi wanakula njama kwenye kufanya ujambazi iweje tena hao hao niwaamini ninapokuwa na pesa nyingi?

Kuna matukio Mengi sana ambayo mapolisi wametiwa hatiani kutokana na kufanya ujambazi likiwemo tukio moja Mbeya ambalo lilishirikisha hadi askari magereza, na sijui kesi yao inaendeleaje hadi hivi sasa

Duh! kwa mpango huo sijui tuweke tumaini letu wapi?
Tunapokosa imani na vyombo vyetu vya dola sijui tutafanyaje?
Nahisi jamaa wanalipwa mshahara kiduchu ndo maana wanakuwa na vijitamaa vikubwa vikubwa!?
Ama wanaamua kutumia rungu walilopewa!?
Ama jamaa hawajafundwa vizuri juu ya somo la uzalendo!?
Ama jamaa elimu yao ni hafifu kwa hiyo wanaona dhuruma kwao ni sawa!?
Dah! kwa kweli sijielewi elewi!
Maana kuna wakati nilisikia mkuu wao sijui anaitwa nani? naye alihusika na uporaji na akakaa jela muda kadhaa.
Mh! hii ni fedheha kaka.
 
Back
Top Bottom