Ripoti ya Chande nahisi haitatoka!

Ripoti ya Chande nahisi haitatoka!

Sasa itakuwaje?. Tunasubir isomwe wazi Ili tuelekee kwenye mchakato wa kitabu cha kutuongoza kama nchi. Bila kusomwa tunatokaje tulipo? Wasione aibu ukitaka kupata mtoto lazima mvuliane nguo bana.
 
Ripoti inatoka Gwajima na Kitima wanaweza kutajwa kwenye ripoti
Tundu Lissu na CHADEMA watakosekana kwenye ripoti kama hiyo?

Lakini ukweli ni kwamba, hata kama ripoti ingetamka wazi kuhusu kilichochochea hayo ya Oktoba, na akatajwa Samia kwa ukaidi wake na uchu wa madaraka; hilo lisingebadili chochote wakati huu.

Samia na Genge lake wataendelea kama hakuna kilichotokea, na kuhimiza maridhiano wanayoyataka wao na siyo wanayoyataka waTanzania.

Hiyo ripoti haina faida yoyote kwa waTanzania, sanasana itakuwa ya manufaa kwa walioiunda tume ili iwasafishe.
 
Msipoteze muda kusubiri ripoti ya mchongo ya tume ya Chade haitatoka maana wameshidwa kudanganya wakati ukweli upo wazi!
Wanataka isubiriwe na kuongelewa ili kuipa uhalali.

Kuna watu wamefikia hatua ya kusema eti ripoti inatupia mzigo wa mauaji kwa serikali na Samia anagoma kuitoa mpaka ihaririwe kwanza.

Ni jambo la kushangaza sana watanzania wanaweza kuchezewa akili namna hii. Hivi kweli kweli kwa kuangalia wajumbe wa tume na walivypatikana watu wanategemea tume ya mchongo iseme kweli?

Subirini wengi wataanza kuweweseka tena jinsi ripoti ikavyokuwa na uongo wa mchana kweupe na kutoa mapendekezo ya kijinga.
 
Back
Top Bottom