Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,868
- 33,279
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mwalimu Mstaafu wa Kwaya Kuu Habari Njema Arusha Mjini Kati Ndugu John Lusungu Nusurupia Myavilwa.
Atakumbukwa kwa kazi ya kutunga na kufundisha nyimbo za Injili Kwaya mbalimbali nchini ikiwemo Kwaya ya Vijana Makorora Tanga miaka ya 1970+, baadaye akahamia Arusha ambako alitumikia kama Mwalimu wa Kwaya Kuu Arusha Mjini hadi kustaafu kwake miaka ya hivi karibuni,
Pamoja na kuimbia Kwaya Kuu Arusha pia alifundisha baadhi ya wanamuziki walioipigia na kuimbia kwaya mbalimbali nje na ndani ya KKKT, miongoni mwa kanda za miaka hiyo zenye utunzi wake akiwa Kwaya Kuu Habari Njema Arusha ni pamoja na;
Mungu Aiweke Roho yake Mahali Pema, mbele yetu wewe na nyuma yako ni sisi
Amin
Mwalimu John Lusungu Myavilwa aagwa rasmi 28.08.2022 mjini Arusha na kusafirishwa kwenda kupumzishwa kwao 29.08.2022 Ramadhani mjini, Njombe
Atakumbukwa kwa kazi ya kutunga na kufundisha nyimbo za Injili Kwaya mbalimbali nchini ikiwemo Kwaya ya Vijana Makorora Tanga miaka ya 1970+, baadaye akahamia Arusha ambako alitumikia kama Mwalimu wa Kwaya Kuu Arusha Mjini hadi kustaafu kwake miaka ya hivi karibuni,
Pamoja na kuimbia Kwaya Kuu Arusha pia alifundisha baadhi ya wanamuziki walioipigia na kuimbia kwaya mbalimbali nje na ndani ya KKKT, miongoni mwa kanda za miaka hiyo zenye utunzi wake akiwa Kwaya Kuu Habari Njema Arusha ni pamoja na;
- Nampenda Bwana Yesu
- Jibidishe
- Panda Mbegu Njema
- Nitakwenda Mbinguni kwenye raha njema
- Tutaimba Milele
- Wapendeni Adui Zenu
- Mko Tayari
- Sikiliza ni Sauti ya Mtu
- Njia ya Msalaba
- Mtafuteni Bwana
- Tumo Safarini
Mungu Aiweke Roho yake Mahali Pema, mbele yetu wewe na nyuma yako ni sisi
Amin
Mwalimu John Lusungu Myavilwa aagwa rasmi 28.08.2022 mjini Arusha na kusafirishwa kwenda kupumzishwa kwao 29.08.2022 Ramadhani mjini, Njombe