Ridhiwani Kikwete, thibitisha au kanusha

Nashangaa sana - hela za kuboresha huduma za afya hakuna, lakini za kuboresha maisha ya watoto wao - hizo zipo.
Iko siku ina kuja na siku ipo ambapo - Liwalo na Liwe - Litakuwa.
 
The good thing, amewekeza nchini. Personally sina shida na watu wa aina hii. Nawachukia wale wanahamisha hela na kwenda kuweka nje ya nchi badala ya kuziacha ziingie kwenye mzunguko hapa nchini na kuongeza uchumi.
 
Duuu kwenye thread kama hizi huwezi kumuona RIZ1,zomba wala Rejao huwezi kuwapata hapa, wataangalia tu hii thread, Dhaifu sana.
 
View attachment 57923Ridhiwani kikwete naomba uthibitishe au ukanushe umiliki wako wa jengo hili ndani ya Dodoma.Nitatoa nyaraka baada ya kusikia kauli.Naomba kuwasilisha.
NGOWILE, palasilote, asigwa, chilipamwao, MNAMBOWA, ngoshwe, Bangoo, Kizamani, MMASSI, Mwanaharakatihuru, paty, kiumbo, PPM, ngano, na wengine weengi mnaochangia mada hii, nina jambo moja la kusema.

Tofauti ya Ridhwani na sisi tusionacho ni moja, kwa nafasi yake ana uwezo wa kupata taarifa muhimu na miongozo ya jinsi ya kupata mitaji. Kwanza kwa kuwa mwanasheria na kutokana na uzoefu wake wa kushughulika na wateja, mara nyingi wanajua mbinu wanazotumia wateja wao katika kupata mitaji. Pili ni kwa baba yake kuwa raisi, hahitaji kusaidiwa na baba, kuwa mtoto inatosha. Hata wewe ungekuwa mtoto wa Rais, tabia ya wa- Tanzania wengi (ambayo tunatakiwa tuiache) ukiwa na nafasi kama hiyo ni kujikomba kwenda mbele. Wewe kama ni Mkurugenzi wa beni, na ukaambiwa Ridhwani anaomba apointment na wewe, unakurupuka na yeye anakuwa kipaumbele. Na utashare as much info as possible, just with expectation kuwa mtoto atanena jambozuri akiwa anakunywa chai nababa. So anapata access ya Mikopo (kwa njia halali bila shaka) na hili ndilo ninaloamini.
Ni wape mfano mmoja wa wahindi wanavyofanya. Ghorofa au uwanja unauzwa, anakwenda kwa mhusika na kunegotiate nae, wakishakubaliana unajua tena manunuzo ya nyumba ni mlolongo, so ukaguzi Ardhi, n.k. wakati huo anakwenda bank kuzungumza nao anawaeleza kuwa anataka kununua gorofa na kufanyia biashara. Anatumia pesa kiasi kuandika mchanganuo mzuri wa biashara. Mradi unapita, na mabenki hayataki kuchelewesha mkopo wakijiridhisha kwa ajili ya ushindani. Basi bank wanamlipa yule mhindi na mwenye nyumba anakwenda bank anadeposit na transfer inafanyika na bank kuchukua hati zote za nyumba kama dhamana (normaly ni kama 80% ya gharama zote, ingawa kuna taratibu nyingi tu wengine hutoa 100% ambayo ina masharti tofauti) na Mhindi anabaki na nyumba na anafanya biashara. So Bank ikifanya evaluation wakakuta thamani ni kubwa kuliko bei unayonunulia, wao wanakupa hiyo cash, inayobaki ni mtaji! Sanasana atakuwa ametumia pesa kuandaa mradi. Mnaionaje hii?
 
and he doesn't seem to slow down,.kibaha maili moja mbele kidogo ya TAMCO anashusha hoteli ya ghorofa,ni kama kula nyama ya mtu
 
View attachment 57923Ridhiwani kikwete naomba uthibitishe au ukanushe umiliki wako wa jengo hili ndani ya Dodoma.Nitatoa nyaraka baada ya kusikia kauli.Naomba kuwasilisha.


wabongo bana... kama anamiliki kihalali na kufuata taratibu zote .. kutakuwa na tatizo gani.. mbona wapo watanzania wakawaida wanamiliki vitu kama hivo..? au yoyote anyekuzidi ni ndio definition mpya ya fisadi ..?
 
View attachment 57923Ridhiwani kikwete naomba uthibitishe au ukanushe umiliki wako wa jengo hili ndani ya Dodoma.Nitatoa nyaraka baada ya kusikia kauli.Naomba kuwasilisha.

Wewe huoni kama hayo ni maendeleo wazawa wanajitahidi kujenga nchi yao, ingekuwa ya foreigner ungefurahi ya wazawa unapiga vita fitina. Riz1 hana nyumba hiyo wala yeye si mtumishi wa serikali kama amejenga ni jasho lake. Leteni mambo ya faida jamvini
 
Sasa athibitishe au akanushe nini? hivi wewe huwezi kujenga nyumba kama hiyo Tanzania hii, na mashamba yote aliyokuwachia bibi yako yanafanya nini?
 
Aliwahi kujisemea mzee wa watu marehemu Mlm JKN "Umasikini ni dhambi kwelikweli" na Mwalimu mwenzangu Dr Kopoka hapa Mlimani alisema siku moja "ukiwa tajiri na mwenzako ni masikini kupindukia, bado wewe ni masikini tu na hutakuwa salama kamwe"
 
Badala na wewe kutafuta vyako unakaa hapa JF kuleta unafiki, kama yake wewe inakuuma nini bana? We kama unataka gorofa la hivyo unaweza kulipata pia. Nenda Saudi Arabia tu. Utarudi na mihela kibao.
 
Nashangaa sana - hela za kuboresha huduma za afya hakuna, lakini za kuboresha maisha ya watoto wao - hizo zipo.
Iko siku ina kuja na siku ipo ambapo - Liwalo na Liwe - Litakuwa.

Viongozi wetu ni walafi na wenye tabia kama kupe ama kunguni! Iko siku watajificha kwenye calvat/mashimo na kujivisha baibui kama ilivyowatokea akina Ghaddafi ama Mubarak na familia zao.
 
Viongozi wetu ni walafi na wenye tabia kama kupe ama kunguni! Iko siku watajificha kwenye calvat/mashimo na kujivisha baibui kama ilivyowatokea akina Ghaddafi ama Mubarak na familia zao.

Hongera sana Rizwani unawekeza ndani ya nchi yetu. Hivyo unaleta maendeleo ndani ya nchi yetu. Wale wanaoiba fedha za wa TZ na kuziweka Uswisi hao ndo mafisadi wabaya. Wale wanoiba fedha na kuwekeza ndani ya nchi ni mafisadi wazuri. Hongera sana Rizwan endlea na uwekezaji huo ndani ya nchi. Vijana wanataka ajira.

Watu wanataka nyumba nzuri za kibiashara. Rizwan achana na kelele za milango hizo za walalahoi. Uraisi ni tasisi, hivyo kama ni mtoto wa raisi na un a akili sawasawa basi ni haki yako kutumia jina la ofisisi ya baba yako kunufaika nayo. Hicho ni kitu cha kawaida sana. Bali endlea kuwekeza ndani ya nchi yaetu.Amen!
 
hakuna mtu anapenda kuzaliwa na mwizi, nani atamwonea wivu mtoto wa kibaka hata kama kupitia huo ukibaka watakuwa matajiri. Au ndio Riz1 umejibu.
acha wivu kijana. Naona roho imekuuma sana jamaa kufanikiwa. Hela haiji kijiweni ndugu yangu. Badala ya kutoa puvu humu JF ni bora na wewe utafute mbinu za kujenga hata kachumba kamoja.
 
Nashangaa sana - hela za kuboresha huduma za afya hakuna, lakini za kuboresha maisha ya watoto wao - hizo zipo.
Iko siku ina kuja na siku ipo ambapo - Liwalo na Liwe - Litakuwa.

2015 Liwalo na liwe
 
Aliwahi kujisemea mzee wa watu marehemu Mlm JKN "Umasikini ni dhambi kwelikweli" na Mwalimu mwenzangu Dr Kopoka hapa Mlimani alisema siku moja "ukiwa tajiri na mwenzako ni masikini kupindukia, bado wewe ni masikini tu na hutakuwa salama kamwe"

Hii ndiyo Tanzania Profesa. Haina ubaya ku invest,ila sio kwa hela za walipa kodi na magumashi. Na hawa watoto wa viongozi sijui wanabiashara gani...
 
Muhimu hapa ni kwamba kapata utajiri huo kihalali?

Kama ni kihalali ana haki ya kumiliki hata magorofa yote ya Kariakoo. Lakini kama sio halali lazima tujiulize. Hapa sio kumwonea wivu bali tunataka uadilifu katika jamii yetu. Lakini pia mimi naomba wanajamii ambao mna mashaka na mali za mtu yeyote, awe mfanya biashara au mtumishi wa umma, mwende mahakamani kumtaka mhusika aje kuthibitisha umiliki wake halali wa mali anazotuhumiwa nazo. Kila mtanzania; mkulima. mfanyakazi, mfanya biashara, nk, anatakiwa kuwa na mali halali.

Tukiandika tu humu na kuacha haibadilishi chochote. Wizi utaendelea na kila uovu wa dhuluma na ufujaji wa mali za watanzania. Tutoke hapa tulipo, tuanze kuchukua hatua za kisheria sasa lkuwapeleka mahakamani wote ambao tunawatuhumu. Hata kwa vyama vya upinzani; haitoshi tu kuibua kashifa na kuacha.

Inabidi waende mahakamani ili wahusika waitwe kujieleza na kuthibitisha. Potelea mbali wakinunua hukumu lakini angalau kuna wengine watapata somo, na kuna watu wengine hawataweza kununua haki kama walivyozoea. Huko mahakamani nako kuna mahakimu na majaji wanataka uadilifu japo ni wachache.

Ipo siku HAKI YA KWELI itatendeka. Maana kuna haki inayopatikana mahakamani isiyo ya kweli, haki ya kufoji.
 
Back
Top Bottom