Ridhiwani Kikwete, thibitisha au kanusha

Ridhiwani Kikwete, thibitisha au kanusha

tuwekee humu na mali zako unazomiliki..sioni tatizo kama kuna uhalali..ni matumizi bora ya nafasi waliyopata..sali sana na wewe unaweza pata vyako..
 
acha wivu ulitaka na wewe uzaliwe na kikwete?
Suala sio kuzaliwa na Kikwete,kwani Marehemu Baba wa Taifa hakuzaa na hao wanawe umeshasikia wana uchafu kama huu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kijana si mwizi bali anatimia akili na nafasi aliyokuwa nayo. Pesa nyingi anspata bank baada ya kuwasilisha business plan za nguvu zinazoandikwa na wachumi waliobobea. Mtu mmojawao anayemwandikia budiness plan ni prof Lipumba.
 
My take Ridhiwan ni mtoto wa kiongozi mwenye akili, kama ni mjengo wake safi sana mwache afanye maisha kwa kutumia nafasi aliyonayo tatizo hapa wabongo walitaka kumuona Ridhi akiwa masikini na anatembea kwenye taxi asiemiliki hata nyumba nadhani hapo ndo mngelizika na ndo mngemuona ni kijana anaefaa. Maisha hayako hivyo mwenye akili ni yule atumiae nafasi yake vyema, wewe mwenyewe kuna nafasi ulipata kwa sababu labda baba yako alikua vyema kidogo kiuchumi kuliko mwenzako sasa iweje kwa Ridhi kutaka kumuona akiwa masikini na huku ni mtoto wa raisi.
 
Fanya kazi wewe acha mambo ya unafki na umbeya au unataka uwe nyumba ndogo nini
 
Badala na wewe kutafuta vyako unakaa hapa JF kuleta unafiki, kama yake wewe inakuuma nini bana? We kama unataka gorofa la hivyo unaweza kulipata pia. Nenda Saudi Arabia tu. Utarudi na mihela kibao.

hahahhaha Rizwani hili ndio jibu?
 



wabongo bana... kama anamiliki kihalali na kufuata taratibu zote .. kutakuwa na tatizo gani.. mbona wapo watanzania wakawaida wanamiliki vitu kama hivo..? au yoyote anyekuzidi ni ndio definition mpya ya fisadi ..?

Ndiyo fasion nw days ukiwekeza kama uko ktk system/politics utaitwa FISADI kama uko sekta binafsi utaitwa FREEMASON.
 
Hii ndiyo Tanzania Profesa. Haina ubaya ku invest,ila sio kwa hela za walipa kodi na magumashi. Na hawa watoto wa viongozi sijui wanabiashara gani...
Ndahani, nashawishika kuwa yawezekana wanatumia nafasi waliyonayo kupata mitaji kwa njia halali. Tofauti yake ni kuwa mimi na wewe tukienda bank kuomba mtaji, zengwe lake linaweza kuwa refu mpaka ufanikiwe, lakini Ridhwani dhamana yake ina faia mara dufu tu.

Pia Ridhwani anajua mbinu nyingi ambazo nyingine anaweza kuwa anatengenezewa kabisa ambazo ni halali kwa wanaojipendekeza na akapata mitaji. Sitashangaa kusikia anadaiwa madeni mengi.

Ila pia kingine mbacho hutokea kwa nchi nyingi za Afrika ni wawekezaji wetu wawe wazungu wawe wahindi, hupenda sana kutoa bahasha kwa familia za viongozi, na hizi wengi wa wanafamilia wameingia kwenye mtego, hope Ridhwani hajanasa.
 
tatizo la Watanzania wengi hawataki kufanya kazi wanapenda sana mtelemko, hata wewe ukijua kupanga mabo yako unaweza kuwa mwekezaji mzuri ndani ya nchi yako angalia ulaya matajiri wakubwa ni wakulima lkn kwetu kilimo ni kazi ya maskini tujifunze kujishughulisha kuliko kupiga porojo
 
Badala na wewe kutafuta vyako unakaa hapa JF kuleta unafiki, kama yake wewe inakuuma nini bana? We kama unataka gorofa la hivyo unaweza kulipata pia. Nenda Saudi Arabia tu. Utarudi na mihela kibao.

Kuna Nini Saudi Arabia? Nijuavyo Mimi Saudia Ni kitovu cha dini fulani. Vip wanagawa pesa au KUNA KITU HUWA WANAFANYA? Vipi na anayezungumziwa hapa naye pia alienda Huko?
 
profesa, umeongea sana lakini hoja ni kwamba yeye athibitishe kama ni mali zake... na hapo atangaze kama tunavyo tangaziwa mali halali za kin a bill gates. maana na kumbuka kipindi kile walipo mtuhumu alisema yeye ana mali chache na gari bovu aina ya camry sasa hayo yote ghafla ametoka wapi?
 
Hoja ya msingi ni kwamba anapata wapi fedha?je anakopeshwa na banayake au anakopa wapi.anaweza kuthibitisha pia chanzo chs utakiri wske mkubwa wa kasi alionao.ishu hapa ni kuwa mtoto wa Raisi halafu na utajiri wa ghafla. Maana tunakujua vizuri toka utoto wako bwana Riz
 
Waacheni wajenge huku huku Tanzania maana wakijenga mbali ikifika siku yakuwanyang'anya itakua shida! Waache wajenge zitakua zetu siku siyo nyingi! Watanzania tumeshawasoma wao wajione wajanja ila watafrai siku ikifika

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Sioni shida hapa, sema kama sio halali na ulete ushahidi kama ni ya kwake, msitumie software ya bongo zetu kupokea madudu. Je, wale waliopeleka Uswisi na huyu yupi mhalifu?

Huu ndio mfano dhahiri wa Moyo wa mkosaji, fanya bidii utatoka tu kijana
 
Badala na wewe kutafuta vyako unakaa hapa JF kuleta unafiki, kama yake wewe inakuuma nini bana? We kama unataka gorofa la hivyo unaweza kulipata pia. Nenda Saudi Arabia tu. Utarudi na mihela kibao.

Huku ni kutusi watu. Ina maana waendao hijja wote hurudi na maghorofa? Huyu Ridhiwani kwani ni Alhaji?
 
Back
Top Bottom