Serikali: Msitume nyaraka za Serikali kupitia makundi ya WhatsApp, ni marufuku

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,902
945

MHE. JANEJELLY NTATE AIBANA SERIKALI KUHUSU SHERIA YA KUTUMA NYARAKA ZA SERIKALI SEHEMU ISIYOHUSIKA HUSUSANI MAGROUP YA WHATSAPP

"Sasa hivi kuna utaratibu wa viongozi au maafisa kufungua group la WhatsApp na kutumiana nyaraka za kiserikali ndani ya group. Sheria ya TEHAMA mliyoitunga inazungumzia humo? Kama haimo na hairuhusiwi mnafanya nini ili sheria ijumuishe ili kuwaepusha wanaotumia huo mtandao wasije kupatwa na matatizo ya kuhukumiwa kwa kukutwa na nyaraka za Serikali sehemu zisizohusika?" - Mhe. Janejelly James Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, Mwakilishi wa Wafanyakazi Nchini anayetokea Mkoa wa Dar es Salaam

Swali hilo lilijibiwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete

MSITUME NYARAKA ‘WHATSAPP’ NI MARUFUKU

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema sheria inayosimamia nyaraka za Serikali inaelekeza kuwa mawasiliano ya Serikali yafanyike kwa njia ya barua na si vinginevyo.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2023-09-01 at 05.50.45.mp4
    36.9 MB
Akili itumike kuendana na zama hizi za teknolojia ya habari.
Tuna serikali mtandao, e- GA. Je ni kinyume Cha sheria?
Majibu marahisi kwa maswali magumu.
Kinachotakiwa ni utaratibu tu wa kutumia mtandao badala ya kusema barua.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom