Ridhiwani Kikwete ang'aka tena

Ridhiwani Kikwete ang'aka tena

huyu hata PAMPAS Azimfai mpe vile vitambaa vya kwetu kunja mara Nne ile khanga labda itamsaidia
 
kama kawa nipo pamoja na mtn na the finest angekaa kimya kama alivyo fanya `baba yake mkubwa mkapa` alikaa kimya na kashfa lake la kiwira ngoma imerudi kimya kimya imemsaidia sasa wewe Rz1 na mapete yako unatupotezea muda wa kuangalia mambo muhimu unapiga mikelele ambayo huna uwezo wa kuyatetea..sasa endelea uone ..omba Mungu mch.mtikila mpenda makesi asisonge mbele!!!!
 
Hili ni swali la leo kwenye kipindi chetu cha jf Noma

Baada ya waandishi wa habari kumuuliza bilionea mtoto kama akishindwa kumpeleka Mh Mbunge,Mwenyekiti, Wa chadema Dk Silaa na Mtikila akaomba ""jamani haya ni maisha yangu binafsi mbona mwanifwatailia naomba yaishe mniache"""

Kama mshiriki wa Jf Noma tunauliza swali je kijana huyu kuomba radhi aachwe ni kusoma nyakati kwenu wanachi na wana jF tutarudi studion baada ya habari
 
  • Thanks
Reactions: Ame
maumivu ya kichwa huanza polepole....jamaa kaona mbele moto bora apige u-turn ya nguvu arudi gambani kimyaaa!
 
Sasa Kama hayo ni mambo ya familia yake mbona alitoa siku saba aombwe msamaha sivyo atawapeleka mahakamani?,sasa anavyosema asifuatliwe inamaanisha nini?au anafikiri watu wamesahau.
Wito wangu kwa Slaa na Mtikila mpelekeni mahakamani huyo mtoto na sisi wananchi tupo nyuma yenu
 
Hii familia haina kawaida ya kufullfill promise,just like his dady,hawezi kufanya lolote huyo,wala hana mpya!!!!
 
kwanza GPA yake alipomaliza LLB ilikuwaje? Huyo dogo ni matope kichwani. Anasema hataki kufatiliwa na wanasiasa wakati naye ni mwanasiasa. Nina wasiwasi na uwezo wake wa kufikiri. Huyo si ndo aliharibu hata uchaguzi wa Yanga, achilia mbali kumfitini Masauni hadi kulazimika kujiuzulu, na si ndo alimfitini Bashe? Aende zake kule, tuna hasira naye ye hajui tu. Mwache aendelee kufuja kodi zetu tunamhesabia siku.
 
me hua nashangaa sana manake kama mtu ananjijua kua yupo safi wala hakuna hato sita hata kidogo
kwenda huko mahakamani.
sasa we utuhumiwe/uchafuliwe hivi, af unajijua kua upo safi kweli utakaa kimya.

we riz ni mwizi na ndo sababu unasita sna kwenda mahakamani.
 
me hua nashangaa sana manake kama mtu ananjijua kua yupo safi wala hakuna hato sita hata kidogo
kwenda huko mahakamani.
sasa we utuhumiwe/uchafuliwe hivi, af unajijua kua upo safi kweli utakaa kimya.

we riz ni mwizi na ndo sababu unasita sna kwenda mahakamani.
Ngoja broda,
Miaka mi4 iliyobaki si mbali...Sasa hivi watatumia kinga za Whitehouse, lakini ikiisha hiyo watajuta hawa!
Hawajifunzi kitu hawa kwa yanayotokea. Na wakiachia urais kazi ya kwanza iwe ni kuwanyang'anya Diplomatic passports zao ili wasiwe na pa kutokea!
 
Ndio imetoka hiyo! Wenzake walisema hivyo hivyo mwisho wakaingia mitini!
 
Kama hii issue inahusu maisha yake binafsi mboma alikurupuka kwenda kwenye vyombo vya habari kuwapa waliosema notisi ya siku saba? It doesn't make any sense to me.

Huu ndio utaratibu uliozoeleka hapa nchini a oneway traffic kibosile akijisikia anamshawasha wa kuonekana kwenye luninga anawaita wanahabari anatuliza kiu yake lakini akivurunda wakamfuata awahabarishe kulikoni wanazuiwa na secretary akipigiwa simu aidha apokei au anadai yuko kwenye kikao au anaeleza kuwa yeye sio msemaji
 
Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka


MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.
Hivi kweli wandugu wapenzi hii sio EPA No2???? Maana huyu Rais wetu alisema fedha za EPA wale wezi wamerudisha Tshs 70,000,000,000/= bilion sabini. Ikasemekana fedha hizo zimepelekwa TIB benki ya rasilimali ya taifa zote.Baadae tukasikia hizo fedha zimepelekwa kilimo kwanza na Mhs Rais Tshs 20,000,000,000/= Twenty billion. Sasa ebu tuulize swali hizo Fifty Billion zilizobaki zilikwenda wapi???????? Au bado zipo, na kama zipo ziko wapi na zinatumika kufanya nini????? Majibu tafadhari watu wa TIB au serikali na kilimo kwanza, Waziri mkuu au vipi???? Hizo ni fedha zetu lazima tujue vinginevyo ni EPA No2!!!!!!!
 
Nchi hii wamepita marais watatu kabla ya JK lakini hatukuwahi kuwasikia wala kuwaona watoto wao kwenye public. Tena wengi wao walikuwa wanyenyekevu sana. Inakuwaje huyo dogo asumbue vichwa vya watu kila siku? Au ndio ulimbukeni wa Kikwere?
 
Waaauhhh! Dogo jinga huyoo! Kumshtaki Mtikila na Dr Slaa ktk ni sawa na kupiga manati mzinga wa nyuki!!! Anaiga tabia za akina sunche!!!Kwa sababu ushahidi wa yeye kuwa bilionea anao basi na aende akashtaki huko mahakamani ili uma wa watz ushuhudie yaliyomo! asilete ubishololo!!!


Fabricandor fit faber!!!!(Kama kweli ni shujaa aony:bange::bange::bange:eshe umahiri wake!!)
 
Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka


MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.
Mchungaji Mtikila pamoja na Dr Slaa tafadhari anzeni na huyu kijana RIZ 1, apelekwe mahakamani aeleze alipataje hiyo mifedha. Kama alifikiri mahakama ni mchezo aone moto yeye ni lawyer atatokea mbele. Nia hasa ni kuzuia kwa muda malengo ya wizi wa mali za wananchi kama vile ni shamba la bibi!!!! Wengine watafuata baada ya kumaliza muda wao hapo Magogoni!!!!!!!
 
Back
Top Bottom