Ridhiwani Kikwete ang'aka tena

yani hata sichoki kustaajabu...; hii nchi haijawahi na haitakuja kua na vituko kama sasa

magogoni imekuwa abused vya kutosha awamu hii ya nne
 
NAAPA HANA MSHAURI !!!! Kama yeye na campani yake kutwa kucha anahangaika na totoz atashaurika saa ngapi huyo Riz 1??
 
Siku saba alizotoa kwa mbwembwe zimepita halafu anasema eti ni maisha yake!
 
My Advise: he better mind his own business na akaendelea ku build his asset colum na kukaa nyuma ya pazia kama mdau mmoja alivyo shauri
 
haka kajamaa kanatafuta sifa tu kwenye media...kwani nchi hii imekuwa na marais wangapi na watoto wao wakatulia bila kujitutumua bila sababu? He become and easy target of attacks from politicians because of his behaviours.
 
“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

hahhaaaaa, hapo kwenye red hapo, labda anataka awaendee kwa "Mtaalamu" but sijui mwaya
 
Huyo bwana mdogo kapotea, ndo maana wapo ktk mchakato wa kuachiana urais ili walindane sio? mhh 2015 ipo kazi
 
Mtoto huyu wa rais ni mcharuko hasa, sasa kamgusa simba sharubu. 7 days zimekatika kimyaaa naona wakubwa wamemfunika m.a.p.u.m.bu. Bora angekaa kimya tu. unajinyea then unaita media kukanusha bdae unasema kujinyea ni swala binafsi.
 
Huyu si ndo na yeye aliusika katika ule ufisadi wa mradi wa maralia?,
 
Aende tu mahakamani,
wamvue nguo hadharani.
Alidhani ni utani
kuanzisha vita jukwaani.
Kawatishia wenye ujuzi
kwa madaha na matanuzi,
Asielewe ni watambuzi,
wenye uelewa na ufafanuzi.
Sasa kapata kigugumizi,
anatoa kilio kama mwana wa mbuzi!
Aende tu mahakamani akavuliwe nguo hadharani!
 
nchi hii bwana ...sasa we Rizi ulikuwa unamtisha nani?wenzio ndo maana wanakaaga kimya...we mwizi halafu unaleta mdomo watakutoa nishai hawa we jishauwe tu kama umetiwa ndimu
 
hii movie naitamani sana;huyu dogo alijiharibia pale alipowaita waandishi wa habari na kuanza kutoa vitisho.Ni imani yangu kuwa mch.mtikila atafanya kweli kama alivyoahidi.
 
Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka


MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.

asante ndugu,chanzo cha habari??
 
asante ndugu,chanzo cha habari??
Kasome Tanzania Daima. Mie nilisema katika thread nyengine huyu hana ubavu wa kuwapeleka mahakamani akina Dr Slaa. Anapambana na mlima mkubwa asiouelewa nao ni nguvu ya umma. Nadhani amepata ushauri mzuri na kuwajulisha watanganyika kumbe na yeye ni Bilionea
 
Asante tupe chanzo cha habari.....

mbona mnapenda kuulizia vyanzo vya habari kwanini mtu hawezi yeye kama yeye kuwa chanzo cha habari? mbona hawo waandishi wanapata habari kupitia kwa mtu mmoja mmoja?" jadili mada achauvivu?
 
Back
Top Bottom