Richmond: Sitta anahusika pia?

Hizi information ni nzito jamani na zinahitaji kichwa kiwe kimetulia ndio uelewe haswa kilichotokea....naona kuna kamuelekeo kakusafishana kwenye hii ajenda na itafika hatua hoja muhimu itafunikwa na tutawasafisha wahusika....leo tuaanza kuona documents ambazo hazikwepo mwanzo na matokeo yake ni kubadili muelekeo wa suala hili na kupoint kidole upande mwingine....jamani watz sasa ni wakati wa kujadili mambo mengine ya maana yanayohusu nchi yetu na hili suala la richmond litolewwe uamuzi wa maramoja,linaweza kuja kuharibu amani ya nchi yetu....musituchanganye....
Angalia mawasiliano ya gile na sita wakati akiwa tic na muda richmond iliposajiliwa....hata ile redvco nayo kule texas imesajiliwa 2003....na hii barua hailezi kwamba wakati huo huyo bwana gile alikuwa anashughulikia richmond....jamani acheni kuchanganya watu na hoja zetu mnazotia sukari na chumvi kuwalambisha wananchi....msitupandishe hasira hata wale tunaowaamini tukawachukia na tukashinda kuleta maendeleo katika nchi yetu.....
 
Sitta anahusika si vitu vinajieleza hapo juu..hakuna ubishi wala kuomba kuongezewa ulinzi hapa.vita ni vita mraa
 
WAKATI tukielekea katika Mkutano wa 17 wa Bunge unaoanza keshokutwa Jumenne Oktoba 26, 2009, tujikumbushe yaliyojiri Mkutano wa Kumi na Saba miezi michache iloyopita haswa Agosti mosi, 2009 siku ambayo Kamati za bunge ziliwasilisha taarifa zao ikiwamo ile kamati ya Bunge ya Nishati na Madini. Kwa kuwa sasa gumzo ni Dk. Edward Hosea wa TAKUKURU, nimeweka msisitizo katika Azimio namba 20 la Bunge, ambalo kamati hiyo ilimsafisha Hosea, ili tuone kama watabadili msimamo wao ama watatoa maelezo?

Katika maelezo ya kamati yaliyosomwa na Shelukindo, walikubaliana na maelezo ya serikali kwamba hakukuwa na ukiukwaji wowote wa kisheria uliofanywa na TAKUKURU kwa kusema, "Mheshimiwa Spika Kamati inaridhika na taarifa hiyo."

Tuisome kwa makini taarifa hiyo tuone UADILIFU wa WABUNGE WETU.

Kwa heshima ya mdau mmoja hapa JF nimeambatanisha na barua ya Sitta kwenda kwa Gire (wakati akiwa TIC).

i870_SittatoGire.jpg

Hii fax ni forged na mtayarishaji ametoa photocopy ya heading, delivery report, signature n.k.

Hii ni mbinu ya mafisadi kutafuta kusafishwa.
 
Suala hapa ni kufuatilia maazimio ya Bunge, sio kuanza kuangalia report. maazimio ya Bunge ndio issue. Hizi ni juhudi nyingine za kudistract attention. Sasa mambo ya Fx ya 2001 wapi na wapi? kamam kumjua Gire mbona hata Ndesambulo alisema anamjua... hatudanganyiki tupo makini.. tusianze kuchanganyana hapa.. ni sawa na kina JK walivyoweka picha ya Salim wakati wa kampeni... kunjua ama kutokumjua Gire sio issue. issue ni Richmond kupewa mkataba kwa njia ya rushwa na kulipwa pesa bila kuleta umeme .. ni hapo tu . tusipoteze lengo
 
Yap ni kweli kabisa hii fax imekuwa forged..
Haiwezekani barua moja kichwa kikalalia upande mmoja kisha maelezo ya kati yakawa wima..Halafu tazama tarehe inasema 27 October, 2001.
Mafisadi jamani duh nimechoka!
 
WAKATI tukielekea katika Mkutano wa 17 wa Bunge unaoanza keshokutwa Jumenne Oktoba 26, 2009, tujikumbushe yaliyojiri Mkutano wa Kumi na Saba miezi michache iloyopita haswa Agosti mosi, 2009 siku ambayo Kamati za bunge ziliwasilisha taarifa zao ikiwamo ile kamati ya Bunge ya Nishati na Madini. Kwa kuwa sasa gumzo ni Dk. Edward Hosea wa TAKUKURU, nimeweka msisitizo katika Azimio namba 20 la Bunge, ambalo kamati hiyo ilimsafisha Hosea, ili tuone kama watabadili msimamo wao ama watatoa maelezo?

Katika maelezo ya kamati yaliyosomwa na Shelukindo, walikubaliana na maelezo ya serikali kwamba hakukuwa na ukiukwaji wowote wa kisheria uliofanywa na TAKUKURU kwa kusema, "Mheshimiwa Spika Kamati inaridhika na taarifa hiyo."

Tuisome kwa makini taarifa hiyo tuone UADILIFU wa WABUNGE WETU.

Kwa heshima ya mdau mmoja hapa JF nimeambatanisha na barua ya Sitta kwenda kwa Gire (wakati akiwa TIC).

i870_SittatoGire.jpg

Loo! Utashangaa jinsi jamaa atavyoruka kuwa saini katika barua hiyo siyo saini yake imegushiwa na mafisadi. Itakuwa story ile ile kama alivyomruka Katibu wa Bunge eti hakujua kuwa aliandika barua Takukuru kutaka iwachunguze wabunge kuhusu posho mbili na pia kama alivyomruka Waziri Mkuu kuwa barua aliyomuandikia kuhusu posho mbili kwa wabunge hajaipata mpaka leo..
 
Kama Fax ni forged basi tunaweza kuwaomba Tanzania Telecom wakatrace hiyo saa na muda huo kama kweli FAX ilitumwa Marekani ni SIMPO!!!!!

Ukweli utajulikana tu.
 
mimi nadhani mtoa hoja kaitoa vizuri sana na ushahidi kaambatanisha, sasa basi kwa mtu yoyote ambaye labda anaushahidi mwingine au ana ona labda kuna makosa yoyote kwenye fax ambayo yanaonekana kuwa ni Fax ya uongo ni bora akasema hapa na watu wengine wachambue labda aseme hiyo fax haina ref.no
 
• Yabainika aliwasiliana na mkurugenzi wake mwaka 2001

SAKATA la Kampuni yenye utata ya Richmond Development LCC iliyoshindwa kuleta jenereta za kuzalisha umeme wa dharura, linazidi kuchukua sura mpya kila kukicha, Tanzania Daima Jumatano imebaini.

Baada ya sakata hilo kulitikisa taifa kwa zaidi ya miaka miwili sasa na hata kufikia hatua ya kusababisha aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na mawaziri wengine wawili kujiuzulu Februari mwaka jana, sakata hilo sasa linaonekana kutaka kubadili mwelekeo na kuanza kumuandama Spika wa Bunge, Samuel Sitta.

Kubadilika sura kwa sakata hilo hivi sasa, kunatokana na kubainika kwa taarifa za
kuwapo kwa mawasiliano ya barua yenye malengo ya kutaka kuja kuwekeza kwa kampuni hiyo hapa nchini, yaliyokuwa yakifanywa kati ya mkurugenzi wake, Mohamed Gire na Sitta mwaka 2001, wakati huo akiwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC)!

Habari za kuaminika zinaeleza kuwa, kuvuja kwa taarifa hizi mpya ambazo tayari zimeshawekwa katika mtandao wa intaneti, kumepokewa kwa shangwe kubwa na kundi la majeruhi wa sakata la Richmond, ambao wanaiona hatua hii kuwa mwanzo wa ukweli halisi kuhusu sakata hilo, ambalo hatima yake ingali haijulikani hadi leo.

Kwa mujibu wa habari hizo,
mawasiliano hayo kati ya TIC na serikali kwa upande mmoja na kinara huyo wa Richmond anayeishi Marekani, yaliwahi kusababisha ujumbe wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye uliomjumuisha Sitta kwa wadhifa wake wa ukurugenzi wa taasisi yenye dhamana ya uwekezaji, kupata mualiko wa chakula cha mchana katika Jiji la Houston, Marekani katika kipindi cha kati ya mwaka 2001 na 2002.

Kuvuja kwa habari hizi, kwa mara ya kwanza kunathibitisha uvumi wa siku nyingi kwamba, Kampuni ya Richmond ilianza kupenya nchini hata kufikia hatua ya kufanya mawasiliano na viongozi wa juu wa serikali ya awamu ya tatu iliyokuwa ikiongozwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa, wakiwamo Sumaye na Sitta mapema mwaka 2001.

Maandishi yaliyoko katika ‘fax’ iliyoandikwa na kusainiwa na Sitta mwenyewe, Oktoba 27 mwaka 2001 kwenda kwa Gire, yanaonyesha kuwapo kwa mawasiliano ya kabla kati ya watu wawili hao, ambayo pia yalimhusisha ofisa wa tatu wa serikali anayetajwa kwa jina moja tu la Sela, mtu ambaye kumbukumbu zinaonyesha alikuwa ni mmoja wa wasaidizi wa karibu wa aliyekuwa Waziri Mkuu, Sumaye.

Katika ‘fax’ yake hiyo (ambayo imebandikwa ukurasa wa kwanza wa gazeti hili), Sitta anaonekana akimuelekeza Gire kuandaa barua ambayo itakuwa na maneno atakayochagua yeye mwenyewe, na akamwambia kuhusu kuwa na taarifa za mkurugenzi huyo wa Richmond kuwasiliana pia na Sela.

Hata hivyo, pamoja na Sitta kuonekana kuridhia uamuzi wa Sela kuendelea kulishughulikia suala wanalowasiliana na Gire kwa upande wake, bado
katika sehemu moja anamtaka mkurugenzi huyo wa Richmond kuhakikisha kuwa anampa taarifa kuhusu mawasiliano yao.

Ingawa haielezwi katika barua hiyo ni mradi gani hasa wa uwekezaji, mkurugenzi huyo alikuwa akitaka kuwekeza akipitia TIC.

Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, kabla ya kuonyesha dhamira ya kuwekeza katika umeme wa dharura, Richmond ilijaribu kuingia katika zabuni ya kufunga bomba la mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza wakati wa serikali ya awamu ya tatu.

Tanzania Daima Jumatano ilipowasiliana na Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Emmanuel ole Naiko ofisini kwake jijini Dar es Salaam na kumuonyesha nakala ya barua inayodaiwa kutumwa kwenda kwa Gire na iwapo walikuwa na nakala ya mawasiliano hayo, mbali ya kukiri kuitambua sahihi ya Sitta na namba ya simu inayoonekana kuwa ni ya kwao, alisema ni jambo gumu kusema haraka haraka iwapo kulikuwa na nakala hapo kwao.

‘‘
Ninachoweza kusema hapa ni kwamba, sijaziona taarifa hizi katika mtandao, ila sahihi ninayoiona hapa ni kweli ni ya Sitta, hata lugha iliyotumika inaonekana kuwa ni yake, kwani unajua alikuwa bosi wangu hapa kwa miaka mingi,” alisema Ole Naiko ambaye alilazimika kufanya kwanza mawasiliano na wasaidizi wake kadhaa kabla ya kuthibitisha kwamba hata namba ya ‘fax’ ilikuwa ni ya hapo ofisini.

Juhudi za gazeti hili kuwasiliana na Sitta mwenyewe na kupata maelezo yake kuhusu kuwapo kwa mawasiliano kati yake na mkurugenzi huyo wa Richmond hatimaye zilifanikiwa jana, baada ya kukwama kwa wiki nzima iliyopita.

Akizungumza kwa simu jana asubuhi,
Sitta alikiri kuwa na kumbukumbu za kuwahi kuwasiliana kwa njia ya fax na Gire na kwamba wakati huo mkurugenzi huyo wa Richmond alikuwa anakusudia kuwekeza katika bomba la mafuta akiwakilishwa na wakala wake aliyemtaja kwa jina moja tu la Muro.

Mbali ya hilo, Sitta alisema wakati huo ulikuwa ni wajibu wake kama mkurugenzi mtendaji wa TIC kufanya mazungumzo na watu mbalimbali waliokuwa wakionyesha nia ya kuja kuwekeza hapa nchini, akiwamo huyo Gire kwa nia njema na
si kwa malengo ya kifisadi.

‘‘Nakumbuka kuwasiliana naye...wakati ule alikuwa akijifanya akitaka kuwekeza katika bomba la mafuta na ‘agent’ wake alikuwa Mr. Muro...
Mazungumzo na mawasiliano yote tuliyafanya kwa nia njema kabisa ya uwekezaji,” alisema Sitta alipoulizwa iwapo ni kweli taarifa za kwenye mtandao wa intaneti na nakala ya barua yenye sahihi yake vilikuwa ni vyake.

Mbali ya hilo, Sitta alikiri pia kuwapo kwa mawasiliano hayo kati ya Gire na Ofisi ya Waziri Mkuu, wakati huo Sumaye, na kwamba alikuwa hana kumbukumbu sahihi iwapo kampuni aliyokuwa akitaka ije kuwekeza ilikuwa ni Richmond au nyingine.

‘‘Siwezi kukumbuka iwapo wakati huo huyo Gire alikuwa akitumia jina la Richmond au la. Unajua wakati huo kwa mwaka tulikuwa tukizungumza na makampuni ya uwekezaji hadi 500, hivyo si rahisi kukumbuka ‘details’ ndogo ndogo,” alisema Sitta.

Akiendelea alisema,
ni jambo lisiloingia akilini kwa maadui zake kutaka kuyatumia mawasiliano aliyoyafanya na Gire wakati huo, tena kwa nia njema, na kuyahusisha na ufisadi kwa sababu tu ya jambo baya alilokuja kulifanya miaka saba baadaye.

Sitta alikiri pia kwamba, wakati akiwa katika msafara wa Waziri Mkuu Sumaye (wakati huo) kwenye ziara yake ya Marekani,
Gire alikuwa miongoni mwa kikundi cha Watanzania 30 waliokwenda kuwapokea uwanja wa ndege wakati walipofika Houston.

Alisema wakiwa nchini humo kwa ziara ya kuhamasisha uwekezaji nchini,
Gire ambaye hivi sasa hawezi hata kumkumbuka kwa sura wakikutana, aliwaandalia chakula cha mchana kwa ajili ya Sumaye na ujumbe wake.

‘‘Tukiwa pale Houston, Gire nadhani alitu-offer (alituandalia) ujumbe wa Waziri Mkuu, ambao mimi nilikuwa miongoni mwao chakula, sikumbuki kama ni cha usiku au cha mchana... No kilikuwa ni chakula cha mchana. Na mazungumzo pale yalikuwa ni ya kawaida tu.
Ni makosa kuunganisha vitu vilivyofanywa kwa nia njema na ufisadi,” alisema Sitta.

Source:
Tanzania Daima
 
Kwani hapo kunatatizo? sioni kama hapo kuna tatizo lolote, yawezekana aliwasiliana na richmond yenyewe siyo hii uchwara ya tz
 
Mugongo Mugongo huko nyuma alisema hivi kuhusus huyu bwana:

1. Samuel Sitta – now, this is the epitome of hypocrisy. How can a man, with straight face, pose as a champion of virtues and ethics while his entire life is defined by unremarkable political achievements and countless allegations of abuse of office at TIC, in Bunge office and everywhere?

He has screwed up, and inserted himself as the main news item, in every major issue that has come before the Parliament. However, in this ongoing theatre, you have to give him credit for wrestling the Parliament from CCM's control and for using the Speakership to build his own little empire of patronage and clientelism.

At the moment, he is one of, if not THE, most powerful men in Tanzania . He coordinates his political mischief with Mr. Reginald Mengi, a tax-evading divorced showman with taste for younger women, to ensure that those scandalized in the Parliament get similar treatment in the media.


all of a sudden amekuwa hero wa the so called "WAPIGANAJI" ndio maana nikauliza kwenye ile thread nyingine hivi hawa wapiganaji wanataka kutufanya sisi wajinga au vipi?

I weje one minute wanasema CCM WOTE MAFISADI then on the next say wanasema kuwa Sitta ni mpiganaji mwenzao?
 
CCM, and upinzani for that matter hamna kitu. Kuna watu wanajitahidi tu.

To borrow from that famed Ghanaian novelist Ayi Kwei Armah, "The Beautiful Ones Are Not Yet Born".

Maybe all that we can shoot for is some genetic engineering. And frankly I am afraid of "Frankenstein;or, the Modern Prometheus"
 
Ya 2001 na moja ni sawa na ya 2005 au 2006 ? je Sitta alishiriki katikakutia saini huu mkataba wa richmonmd au ndio ile stlye ya mfaa maji anataka kushikilia hata unyasi
 
Tanzania Daima wanaleta habari za kipuuzi kweli siku hizi. Yaani hili gazeti limepoteza credibility kabisa. Mwandishi na mhariri wangekuwa makini wangeandika kwa kuweka uchambuzi wao wazi hasa ktk maeneo haya:-

(a) Mhe. Sitta aliwasiliana na Gire wa Kampuni ya Richmond Development LCC siyo ile kampuni ya kutunga ya Richmond Development iliyoingia mkataba na TANESCO 2006. Gire alikula dili na wakubwa akaamua kuandika jina linalofanana kidogo na kampuni yake ili wafanikishe wizi wao.

(b) Mhe. Sitta aliwasiliana na huyu jamaa mwaka 2001, wakati huo haikudhaniwa kabisa kwamba kutakuja kuwa na mradi wa umeme wa dharura huwa wa akina Lowasa.

(c) Richmond Development LCC chini ya Gire imekuwa ikiingia zabuni na Serikali huko nyuma mpaka ilipotimuliwa baada ya kushindwa kutekeleza mradi. Habari hizi siyo siri hata kwenye ripoti za Serikali zipo na kamati ya Mwakyembe iliziandika.

(d) Gire na Richmond Development LCC bila shaka ilikuwa akiwasiliana na viongozi mbali mbali kwani ilikuwa ni mzabuni wa Serikali. Kama itakuwa ni kuwajua wote waliowahi kuwasiliana na huyu jamaa watakuwa wengi tu but for what?

Huu ni ujinga mkubwa, tena ni aibu kutufanya watanzania wajinga kiasi hiki. Oosh ninachoka na hizi low fix.
 
Wanahabri mnachangia kuliharibu Taifa kwa kiasi kikubwa, Tanzania Daima mnaliharibu Taifa letu. Unajua ni kitu mbaya sana kujenga Taifa la wanaosema Nyeupe ni Nyeusi. Madhara ya ujinga na uongo huu utaambukizwa vizazi na vizazi, kwanini tusijifunze kuwa wakweli?

integrity of Tanzanians is questionable.
 
Back
Top Bottom