Revealing: TANESCO inaidai IPTL Tshs Bilioni 321...

Revealing: TANESCO inaidai IPTL Tshs Bilioni 321...

Ili uelewe kwamba ccm wamelaaniwa wabunge wa ccm watakuwa upande wa kutetea majambazi yaliyoiba fedha za watanzania. Lakini tunashukuru naomba wafadhili waendelee Na msimamo Wao Ili mambo yawe magumu tunyukane wenyewe kwa wenyewe huku nchini maana wananchi hatutakubali kukosa madawa,Huduma mbovu,barabara mbovu,elimu mbovu,ajira hakuna. Lazima tutawasha Moto labda wakimbie nchi pum.ba..vu
Hii ni hatari kama tutawachekea hawa jamaa ni wauwaji
 
Kuna mapimbi yanaitwa laki si pesa,msalani,lizaboni yaani hawa jamaa walikuwa wajitoa ufahamu juu ya fedha za escrow ki ukweli mimi na mashaka na uelewa wao au kama si uelewa basi walipewa kidogo ule mgawo wa escrow
 
Hivi inawezekanaje mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila alijua uchafu huu wa IPTL pasipo raisi kujua?

Kama raisi alijua,mbona alikaa kimya?Na kama raisi hakupewa taarifa,mpaka leo amechukua hatua gani kwa waliopaswa kumwarifu?

Kwa wenye kumbukumbu nzuri mtakumbuka kauli/ahadi ya JK kwa waandishi wa habari mwaka 2005 wakati anatangaza baraza lake la mawaziri kwa mara ya kwanza kuwa atatumia hata ushahidi wa kimazingira kuwawajibisha wateule wake na akatao mfano wa mtu kuwa na mali nyingi ndani ya muda mfupi tangu ateuliwe.

Sasa swali langu ni mbona imekuwa kinyume chake kabisa?

Hivi kweli tunahitaji kuendelea na katiba inayotoa kinga ya raisi kutoshitakiwa popote pale kwa makosa atayofanya akiwa madarakani na hata baada ya kustaafu?

Aliondoka Lowassa,sasa ni zamu ya Pinda.Vipi kiranja mkuu hagusiki?

Only in Tanzania!

Think twice mtanzania.


Mkuu hivi kweli hujuhi Uhusiano wa JK na IPTL ?
yani akiwa waziri wa Nishati na Madini na akiwa waziri wa fedha ?
 
ufisadi.jpg
 
IMG-20141117-WA0044.jpg

RIPOTI ya uchunguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), kuhusu kashfa ya kuchota fedha zaidi ya sh bilioni 200, kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow zilizohifadhiwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), umeanika madudu mazito yaliyofanywa na vigogo wa Serikali, Tanzania Daima limedokezwa.

Ingawa ripoti hiyo ambayo Tanzania Daima limebahatika kuiona, imekwepa kutaja majina ya vigogo hao na taasisi wanazotoka, lakini inaonyesha kuwa jumla ya fedha za Escrow ni sh bilioni 306 ambazo ni matokeo ya Shirika la Umeme nchini (Tanesco), kulipishwa tozo la uwekezaji zaidi ya kiwango kinachotakiwa kulipwa.

CAG katika ripoti hiyo, anasema Tanesco walipaswa kurejeshewa sh bilioni 321 zilizolipwa ziada kwa IPTL kati ya mwaka 2002 – 2012.

"Hivyo fedha za Escrow ni fedha za umma, yote ilipaswa kurudi Tanesco na shirika kuendelea kuwadai IPTL sh bilioni 15," alisema CAG.

Madudu mengine yaliyoibuliwa katika ripoti hiyo ni kwamba, kampuni ya PAP haikununua kihalali hisa 70% za kampuni ya Mechmar katika IPTL kwani zilizuiwa na Mahakama, hivyo hawana hati halisi za hisa na PAP ilifanya udanganyifu katika malipo ya kodi kwa kutoa nyaraka za uwongo na kuikosesha Serikali Mapato ya sh bilioni 8.7.

Inaeleza kuwa, kosa hili linahusu pia mamlaka ya TRA Ilala, ambao walihusika kufanya mauzo hayo.

Akaunti ya kampuni ya VIP Engineering and Management (VIPEM), ilifunguliwa na mmoja wa wabia wa IPTL, James Rugemalira, ambaye alikuwa akimiliki asilimia 30 ya IPTL huku kampuni ya Mechmar Bhd ya Malaysia ikiwa na hisa asilimia 70.

Kutokana na kiasi hicho cha hisa, Rugemalira amelipwa kiasi cha dola milioni 75 (Shilingi Bilioni 123), zikionyesha kwamba alilipwa kiasi cha dola milioni 7.5 (Shilingi bilioni 12.4) mwaka jana na kiasi kilichosalia alimaliziwa mwaka huu.

Kiasi hicho cha fedha kililipwa kwa Rugemalira na kampuni ya PAP inayomilikiwa na Harbinder Singh, ambaye kwa sasa ndiye mmiliki pekee wa IPTL baada ya kununua hisa za Mechmar na zile za VIP.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ambayo Gazeti hili imeinasa, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Gavana wa Banki Kuu (BoT), na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, walivunja sheria kwa kuelekeza kuwa kodi ya ongezeko la thamani kwenye tozo la uwekezaji isilipwe na kusababisha serikali kupoteza mapato ya sh bilioni 21.

"Waziri kwa kushirikiana na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, hawakufanya utafiti wa kini kuhusu uhalali wa umiliki wa kampuni ya IPTL. Katibu Mkuu alisaini kutoa fedha za Escrow bila kuhakikisha fedha za Tanesco zinarudi, hivyo kusababisha upotevu wa zaidi ya sh bilioni 321," inasema sehemu ya ripoti hiyo.

Kwa upande wa Tanesco, Mkurugenzi wa Shirika hilo na Bodi yake, hawakutimiza wajibu wao kwa kugeuza maamuzi yao (ama kwa kushinikizwa na Wizara au kwa rushwa), na kulikosesha shirika hilo zaidi ya sh bilioni 321.

Wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikaririwa bungeni kwamba fedha hizo sio za umma, ripoti hiyo inaonyesha kuwa ni za umma.

Mgogoro uliosababisha fedha kuwekwa katika akaunti hiyo ya Tegeta ya BoT, ulitokana na Tanesco kugoma kulipa gharama za uwekaji mitambo (Capacity Charge), kwa IPTL mwaka 2006 kwa vile ilibainika IPTL ilikuwa ikitoza gharama kubwa kuliko iliyopaswa.

Akaunti hiyo ya Tegeta, ilianzishwa kwa sababu ya kuhifadhi fedha zote zilizopaswa kulipwa na Tanesco hadi hapo mgogoro baina ya pande hizo mbili umalizike.

Hata hivyo, Septemba mwaka jana, serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, iliagiza BoT kulipa fedha hizo kwa kampuni ya PAP mara baada ya kuridhishwa na uamuzi wa Mahakama Kuu uliosema kwamba mgogoro baina ya wamiliki wa IPTL na Tanesco umemalizika na hivyo Benki Kuu haina sababu ya kuhifadhi fedha hizo tena.

Uamuzi huo wa kulipwa, ulizua upinzani mkali bungeni ambapo wabunge wawili wa kambi ya upinzani; Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe, walidai kuwa zoezi hilo limejaa ufisadi na Bunge liliazimia kwamba suala hili lifanyiwe uchunguzi wa kina na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), pamoja na ile ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Chanzo: Tanzania Daima | 17 Novemba, 2014
 
Ni bora nchi iingie vitani kwani baadae tutashikishana adabu kuliko kujifanya tuna amani ya woga inayotumiwa na wachache kufilisi nchi
 
tatizo la Watanzania ni upepo... tuna issue zaidi ya escrow, dawa ni kuzikomalia zote na sio moja tu
 
Ningebahatika kuwa rais wa Tanzania walau kwa wiki moja tu, kitu ambacho ningefanya ni kuhakikisha kuwa siku ya kwanza ya utawala wangu inatungwa Sheria ya kunyonga wanasiasa waliohujumu uchumi.

Siku ya pili napata orodha ya wahujumu uchumi sugu au mafisadi papa. Siku ya tatu wanafikishwa mahakamani. Siku ya nne kesi inasikilizwa, ushahidi unatolewa na watuhumiwa wanapewa dakika tano-tano tu za kujitetea kila mmoja. Siku ya tano hukumu zinatolewa. Siku ya sita wananyongwa hadharani. Siku ya Saba utawala wangu unaisha. Anaingia rais mwingine!
 
Watawala wamesha tujua watanzia ni kama wendawazimu vile hupati shida kuwa sahaulisha hii ngoma wiki ijayo tu upepo utakua umesha pita maisha yata endelea kama kawa.
 
hahaaaa waacheni tuu si ndo walivyozoea hivyo halafu utasikua kiongozi amejiuzulu na hukumu yake ndo imeishia hapi
 
Ningebahatika kuwa rais wa Tanzania walau kwa wiki moja tu, kitu ambacho ningefanya ni kuhakikisha kuwa siku ya kwanza ya utawala wangu inatungwa Sheria ya kunyonga wanasiasa waliohujumu uchumi.

Siku ya pili napata orodha ya wahujumu uchumi sugu au mafisadi papa. Siku ya tatu wanafikishwa mahakamani. Siku ya nne kesi inasikilizwa, ushahidi unatolewa na watuhumiwa wanapewa dakika tano-tano tu za kujitetea kila mmoja. Siku ya tano hukumu zinatolewa. Siku ya sita wananyongwa. Siku ya Saba utawala wangu unaisha. Anaingia rais mwingine!

Tunakuongezea wiki moja tena
 
Wapo wapuuzi hapa watakuja na kusema fedha sio za Umma.

Nakumbuka Mh Kangi Lugolo alipayuka bungeni na kusema fedha sio za umma.

AG nae akiwa bungeni alisema fedha sio za Umma.

hapa naamini AG awezi kupona.

Ngoja nimCC Mojawapo.
cc faizafox
 
Back
Top Bottom